Shukrani,Tahadhari na Rai yangu baada ya mchakato wa awali kura ya Maoni Rombo

Shukrani,Tahadhari na Rai yangu baada ya mchakato wa awali kura ya Maoni Rombo

Haaaa kashatoa tamko anasubiri maamuzi ya chama kuhusu kugonbea ubunge rombo zile ni kura za maoni tu.

So, anadhani kamanda Selasini atakatwa na wakuu na badala yake awekwe yeye? sidhani kama CHADEMA kuna upuuzi huo kama wafanyavyo CCM.
 
Ben is very smart..... kwa umri wake mfupi katika siasa za Tanzania unaweza kuona namna anavyojijenga bila papara.... very potential politician in near future..... chama mtengenezeni huyu..... msikwazwe na pressure ya kiu iliyo ndani yake.....taratibu tutafika.....
 
Mchakato wa awali wa kura za maoni Rombo katika kinyang’anyiro cha ubunge jimbo la Rombo umekamilika. Ingawa kura za awali zilizopigwa na wajumbe hazikutosha lakini ili mchakato huu ukamilike ni hadi kamati kuu itakapofanya maamuzi kwa kuwa ndicho chombo chenye jukumu hilo kikatiba. Sitapenda kuingia kwa undani kuhusu kasoro na mambo mengine kuhusu uchaguzi huu

Kwanza,Nampongeza sana Mbunge wa Zamani wa Rombo Mhe.Joseph Selasini kwa idadi ya kura alizopata. Ni jambo la kheri kuwa kabla na baada ya uchaguzi tumeendelea kuheshimiana kwa kuwa kila mmoja anamuhitaji mwingine katika kipindi hiki na sote tunatambua kuwa chama chetu ni kikubwa kuliko sisi. Maslahi ya Rombo na watu wake yatakuwa salama zaidi chini ya CHADEMA ambayo haina migawanyiko

Pili,Nawashukuru wagombea wenzangu kwa kunipigia kura nyingi katika kipengele cha Wagombea kupigiana kura.Niliongoza kwa kuwa Wagombea wote walinipigia kura akiwemo mbunge wa zamani.Kila mmoja wao alipiga kura ya kunipendekeza kuwa mgombea wa ubunge ikiwa wao hawatapitishwa na chama.Hii ni imani kubwa sana kwangu.Nina kila wajibu wa kuilinda imani hii walionionyesha

Tatu,Nawapongeza wajumbe wote walionipigia kura.Sikutumia fedha nyingi.Sikuwashawishi kwa fedha bali kwa hoja zangu.Nina deni la kuwalipa kwa imani hii kubwa walionionyesha.

Nne,Nawashukuru sana marafiki zangu walionipa sapoti kwahali na mali katika mapambano haya.Kuna kaka na Dada zangu wa JF walionisapoti kwa hali na Mali.Wakiridhia nitawataja katika pongezi zangu.Hakika sikuwahi kujisikia mwana-Familia wa JF kama kipindi hiki.

Nawashukuru sana wanahabari kwa kuwa mstari wa mbele na hasa vyombo vya habari vilivyogoma kutumika vibaya katika kipindi hiki.Kwa kuwa istilahi ya kiswahili ina upungufu mkubwa wa misamiati,nyote naomba mridhike kwa neno moja tu ninalowaambia ‘’ASANTENI”. Asanteni sana sana

Tano,Natoa Rai kwa wagombea wenzangu,viongozi na wanachama wadumishe utulivu katika kipindi hiki kuliko wakati mwingine wowote

Aidha,Ninasikitishwa na kulaani vikali kitendo cha baadhi ya makamanda kupandisha bendera za chama kingine baada ya kupata taarifa za matokeo ya uchaguzi.Naomba tuwe na subira kwani maamuzi ya kamati kuu bado.Rufaa na malalamiko yatafanyiwa kazi na chombo husika.Na tuwe tayari kwa maamuzi yoyote ya kamati kuu ya chama.
Tudumishe utulivu na nimetoa Rai kwa viongozi na wafuasi wa wagombea wenzangu tuwe na uvumilivu kwani uvumilivu ndio ukomavu wa kisiasa.

CHADEMA ni kikubwa kuliko sisi sote,Rombo ni Kubwa kuliko sisi sote

Mungu Ibariki CHADEMA,Mungu Ibariki Rombo Yetu

Aluta Continua,Victory Ascerta

Ben Saanane
Sasa Ben kwanini hujawalalamikia moderators kukuwekea heading isiyoendana na uzi wako wa kushukuru?
 

Tatu,Nawapongeza wajumbe wote walionipigia kura. Sikutumia fedha nyingi. Sikuwashawishi kwa fedha bali kwa hoja zangu.Nina deni la kuwalipa kwa imani hii kubwa walionionyesha.

Naomba tuwe na subira kwani maamuzi ya kamati kuu bado.Rufaa na malalamiko yatafanyiwa kazi na chombo husika.Na tuwe tayari kwa maamuzi yoyote ya kamati kuu ya chama.


Paragraph 1: Tafsiri yake ni kwamba umepata kura chache kwa sababu ulitumia fedha kidogo! Kwa maana nyingine unadai mwenzio alipata kura nyingi kwa sababu alitumia fedha nyingi.

Paragraph 2: Kama sijakosea rufaa itakuwa inatokana na maelezo yangu hapo juu! Tungoje matokeo lakini sioni dalili za wewe kupewa jimbo CDM, kamwe!
 
Kura si za siri! Sasa unajuaje kuwa ulipigiwa kura na flani? Au zilipigwa za wazi!
 
. Ben Saanane,

..kwa mtizamo wangu utakisaidia chama zaidi ukijikita ktk masuala ya UTAFITI na SERA.

..jaribu kukaa na wasomi kama Prof.Safari, Prof.Baregu, na wengine, kuwasaidia viongozi wakuu, pamoja na wabunge wetu.
 
Last edited by a moderator:
Ushauri wangu kwako ndugu yangu ben, watumikie wananchi wa rombo kupitia udiwani huku ukijijenga kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu ujao, sio lazima kuwatumikia kupitia ubunge. Aluta continue

Wakati akijijenga kwenye udiwani. Selasini anazidi kujijenga kwenye ubunge..teh teh teh
 
Ben is very smart..... kwa umri wake mfupi katika siasa za Tanzania unaweza kuona namna anavyojijenga bila papara.... very potential politician in near future..... chama mtengenezeni huyu..... msikwazwe na pressure ya kiu iliyo ndani yake.....taratibu tutafika.....
Kweli. . .. .sijui system ya kukuza watu huko ndani ikoje. . . . . Na sioni akiwa anatumika katika maeneo ambayo angeweza kuwa na manufaa zaid kwa chama huku naye akikua. . . . . natamani angewekwa kurugenzi ya mafunzo anoe vijana. . . .Uwezo wa kujenga hoja na kujiamini nadhani huko angeweza kutumia uwezo wake vizuri sana naye angekomaa zaidi. . . .
 
. Ben Saanane,
..kwa mtizamo wangu utakisaidia chama zaidi ukijikita ktk masuala ya UTAFITI na SERA.
..jaribu kukaa na wasomi kama Prof.Safari, Prof.Baregu, na wengine, kuwasaidia viongozi wakuu, pamoja na wabunge wetu.

Kwani yeye anachagua pa kukaa au viongozi ndio wanatakiwa kuona uwezo wa vijana na CV zao ili wawapangie majukumu stahiki???!

Ukitoa siasa na utashi binafsi Ben Saanane sio mtu wa jukwaani, ukisoma hoja na maandiko yake huyu ni mtendaji zaidi kuliko siasa za majukwaani. . . . . . Sijui think tanks wa CHADEMA wanamuangaliaje
 
Last edited by a moderator:
Ukiacha Akunay, hakuna mbunge mwingine hadi sasa wa CDM aliyeangushwa katika kura za maoni. Hii inatoa picha fulani beyond Rombo. Kwa maoni yangu ni kuwa nchi nzima, wananchi wanaounga mkono CDM, wanaiunga kwa sababu wanatamani kuiondoa CCM. Hivyo katika majimbo yanayowakilishwa na CDM unaweza kuona kabisa wanaCHADEMA wanaona kama mbunge ndiye kamanda yao katika movement dhidi ya serikali... Kama ni vita basi mbunge anatazamwa kama kamanda wa kikosi aliyeko mbele kabisa.

Wananchi hawajali sana juu ya utendaji wa mbunge kwenye mambo ya maendeleo jimboni maana wanatambua kuwa kizingiti kikubwa ni serikali kuu, ya CCM.

Naamini itakuwa ngumu kidogo, au itahitaji strategy tofauti sana kuwashawishi wanaCHADEMA kuwa "kamanda tuliye naye sasa sio sahihi"...
 
Duh umekatwa mara nyingi wewe kijana tafuta kazi nyingine ufanye

kinachonishangaza kwa vijana wenzangu hasa wanaojiita wasomi kila mmoja kawa muoga wa maisha na kufikiri kias kwamba kila mmoja anadhan lazima awe kiongoz wa siasa-mim sipingi kuwa wana siasa napinga kuwalazimisha wananchi wawadhani kuwa ninyi ndio suluhu ya matatizo yao-kama lengo ni kuikomboa jamii kwann sasa msitumie elimu na weled wenu kuanzisha projects zitakazosaidia jamii na kutengeneza ajira? kwann mnadhadhalika kwa kutumikia matakwa ya akili zenu wakat uwezo huo hamna-Ben Saa 8 nakushaur fanya shughuli nyingine hizo kura ndio kauli ya wana Rombo kwako. utajidhalilisha wewe na Chama chako sasa umeanza kuutangazia umma wa Tz kuwa CDM wala sio kimbilio kwamba rushwa ni nje nje sasa km mnatoa rushwa mtaweza kweli kuisimamia Serikali-achen hizo baaana fanyeni kaz
 
kinachonishangaza kwa vijana wenzangu hasa wanaojiita wasomi kila mmoja kawa muoga wa maisha na kufikiri kias kwamba kila mmoja anadhan lazima awe kiongoz wa siasa-mim sipingi kuwa wana siasa napinga kuwalazimisha wananchi wawadhani kuwa ninyi ndio suluhu ya matatizo yao-kama lengo ni kuikomboa jamii kwann sasa msitumie elimu na weled wenu kuanzisha projects zitakazosaidia jamii na kutengeneza ajira? kwann mnadhadhalika kwa kutumikia matakwa ya akili zenu wakat uwezo huo hamna-Ben Saa 8 nakushaur fanya shughuli nyingine hizo kura ndio kauli ya wana Rombo kwako. utajidhalilisha wewe na Chama chako sasa umeanza kuutangazia umma wa Tz kuwa CDM wala sio kimbilio kwamba rushwa ni nje nje sasa km mnatoa rushwa mtaweza kweli kuisimamia Serikali-achen hizo baaana fanyeni kaz

Wazo la kufanyiwa kazi. . . .
 
Kura si za siri! Sasa unajuaje kuwa ulipigiwa kura na flani? Au zilipigwa za wazi!

Wagombea walikua watano. Nilipata kura zote tano.Kwa hiyo Wagombea wote walinipigia kura

Huo ulikua uchaguzi mwingine tofauti na wa wajumbe wa Mkutano Mkuu Wa Wilaya
 
Hongera.

Umeonyesha ukomavu kisiasa.

Hata hivyo, sehemu moja katika maandiko yako (hoja ya Tatu) umeandika "Sikutumia fedha nyingi...".

Maana yake nini:

1. Ulitumia fedha, ila aliyeshinda alitumia fedha nyingi kushawishi wapiga kura?

2.Ungetumia fedha nyingi, zingeweza kukupatia ushindi?

Mwisho, bado kijana. Siasa za Tanzania bado zinakuhitaji. Unanafasi. Huu uwe mwanzo, kuwa na subira utafanikiwa...
 
Wagombea walikua watano. Nilipata kura zote tano.Kwa hiyo Wagombea wote walinipigia kura

Huo ulikua uchaguzi mwingine tofauti na wa wajumbe wa Mkutano Mkuu Wa Wilaya

Sawa,Jipange pange twenty twenty.
 
Back
Top Bottom