Shukrani za Jamal Emil Malinzi kwa wana JF

Shukrani za Jamal Emil Malinzi kwa wana JF

Hongera sana kwa ushindi, fahamu kwamba cheo ni dhamana, ukifanya vizuri utapongezwa na kuchaguliwa tena kuongoza kwa mujibu wa katiba,
Fanya yote mazuri kuhakikisha taifa stars inashiriki fainali za kombe la dunia mwaka 2018 huko Urussi
 
Hongera kwa ushindi,

Mimi ni mmojawapo waliofurahia ushindi huu.

Sema chonde chonde ukafanye kazi , usifanyie kazi kwenye social media japo ni vizuri ku interact kwa kupata maoni, ushauri , mitazamo tofauti etc
 
Ndugu zangu nashukuru uchaguzi tumemaliza salama na mimi nimeshinda. Nichukue fursa hii kuwashukuru wapenzi na wadau wote wa mpira miguu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki kwenye mchakato.

Siku chache zijazo nitafungua thread hapa nikiomba maoni na mapendekezo yenu kuhusu ni jinsi gani tutaimarisha timu yetu ya Taifa kwa ajili ya AFCON qualifiers Novemba mwaka ujao.

Tafadhali jiandae kuchangia.

Malinzi


Hongera sana kwa ushindi;
1. Nakusihi usilikimbie jukwaa hili kwa sababu wewe mwenyewe kwa hiari yako umechagua kuingia kwenye public office; jukwaa hili litakuwa sambamba kukupongeza utakapofanya vizuri na kukupa ushauri wa hapa na pale lakini hatutasita kukukosoa pale utakapo-Bugi! hiyo ni ofisi ya umma sio kaya au kampuni yako binafsi.
2. Anza kazi kwa vision na mission pana zaidi ya Timu ya taifa na AFCON; Soka la Tanzania haliko vizuri! linahitaji a comprehensive overhaul; mikakati endelevu ya kuinua vipaji na uwekezaji mkubwa katika miundo mbinu ya soka; utawala na mafunzo
3. mchakato wa uchaguzi ulikuwa na machungu mengi; drop all kinds of hard feelings dhidi ya wadau wote unaohisi walikukwaza ili kujenga mshikamano na kukuwezesha kunufaika na ujuzi na uzoefu wa wadau wote. Wewe sasa ni rais wa wadau wote wa soka nchini sio wale tu waliokusaidia kuupata urais wa TFF.

4. Yabebe na kuyaendeleza yote mema yaliyofanywa na uongozi unaoondoka madarakani, lakini yaache au yaboreshe yale yote unayoona yalikuwa na dosari.


Jukwaa hili litakuwa msaada mkubwa sana katika uongozi wako; usilikimbie wala kulidharau

Best wishes Jamal.
 
Kwanza hongera sana

pili nisemw tu kazi iliyoko mbele yako ni kubwa mno

kiasi kwamba ukiiweza utakuwa shujaa na ukiishindwa jiandae kwa lawama na matusi tele..

tatu ni kuwa nimesikia unasema tuandae AFCON

KWANGU KUANDAA afcon NI GHARAMA KUBWA ZAIDI KULIKO TAIFA STARS KWENDA afcon..

Mwisho usikimbie tu JF
kuwa in touch na members wa humu watakupa ushauri kila unapohitaji
 
Hongera sana mkuu Jamal,

Binafsi ni mpenda mabadiliko ila pia huwa sina rafiki au adui wa kudumu....Hata hivyo unaweza kunifanya niendelee kukuamini kwa kutimiza ahadi zako. Na pia ukizidi kuonesha kuwa huna lengo jingine zaidi ya kututoa kwenywe hii aibu...ya kichwa cha mwendawazimu...!!

Ndugu yangu Jamal, unayo nafasi ya kuandika jina lako katika kitabu cha watu walioleta mapinduzi ya soka nchini Tanzania....Itumie hiyo nafasi na historia itakuwa na wewe vizazi hadi vizazi...


Nakutakia kila la heri na Mungu awe nawe...as long as you have no evil minds and intentions...
 
Kwanza hongera sana

pili nisemw tu kazi iliyoko mbele yako ni kubwa mno

kiasi kwamba ukiiweza utakuwa shujaa na ukiishindwa jiandae kwa lawama na matusi tele..

tatu ni kuwa nimesikia unasema tuandae AFCON

KWANGU KUANDAA afcon NI GHARAMA KUBWA ZAIDI KULIKO TAIFA STARS KWENDA afcon..

Mwisho usikimbie tu JF
kuwa in touch na members wa humu watakupa ushauri kila unapohitaji

Nakubaliana na wewe mkuu,

Starting with small things is more reassuring...

Hayo makubwa yatakuja baadaye.....

Asianze na mambo ya kufikirika kama waliotamani na kuota kwenda Brazil bila hata mchezaji mmoja wa maana...

Na kupitia na kutafakari dreams zake, baadhi yetu tutaanza kumsoma kama kweli ana tofauti team inayomaliza muda wake au ni wale wale..
 
kwani ni nani huyu

Nenda chitchat ni sherehe kubwa utamjuwa tu ni nani huyu.
Kongosho tayari ameshaclaim ufirst lady kwenye trip za Zurich kugonga cheers na Sepp Blatter.

Wewe endelea kushangaa tu Matola ni miongoni mwa wadau wa gesi Tanzania. Lakini mimi siyo bwana Machache.
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana manfesto yenu mjaribu kuyatimiza.
Zawadi kubwa ninayotarajia ni Kuiona Taifa stars wakicheza kombe la Africa na la Dunia kwa maandalizi yako mazuri 2018

Hongera sana.tuna hitaji mabadiliko kwenye soka.
 
Ndugu zangu nashukuru uchaguzi tumemaliza salama na mimi nimeshinda. Nichukue fursa hii kuwashukuru wapenzi na wadau wote wa mpira miguu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki kwenye mchakato.

Siku chache zijazo nitafungua thread hapa nikiomba maoni na mapendekezo yenu kuhusu ni jinsi gani tutaimarisha timu yetu ya Taifa kwa ajili ya AFCON qualifiers Novemba mwaka ujao.

Tafadhali jiandae kuchangia.

Malinzi

Hongerah mkuu Malinzi kwa hilo ni imani yangu kuwa maslahi mapana ya taifa hili ytalindwa na kuheshimia.
 
Watanzania bwana. Wanapenda kumaliza hasira za matatizo yao kwa watu wengine.

Msiposhirikishwa lawama. Mtu kawashirikisha bado lawama.

Kwa haya uliyoyaandika hapa nadhani hujasoma Ilani yake ya uchaguzi. Kwa sisi tunaofatilia tunajua ipo kwenye mitandao ya kijamii. Itafute uisome kabla ya kuja na hizo lawama.


Mwenye matatizo ni wewe usiyekubali kutofautiana mawazo!!!!!!

Wewe ni msemaji wake????!!!!

Verified user,rais wa TFF anaweza kujibu yeye,so tuliza mshono !!!!

Unaleta hadithi za ilani ya uchaguzi wakati tunaongelea work plan yake na.time frame!!!


Kama wewe ni mfuatiliaji na uliridhika na ilani thanx, una maanisha ya kufanya yapo tayari kwa mujibu wa ilani na hakuna haja ya kuongeza au???!!


Na ndio maana sikubali huo utaratibu wa maoni maana kuna kina nyie mtao pewa lift muanze na kupiga honi na kubadili CD.
 
Ndugu zangu nashukuru uchaguzi tumemaliza salama na mimi nimeshinda. Nichukue fursa hii kuwashukuru wapenzi na wadau wote wa mpira miguu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki kwenye mchakato.

Siku chache zijazo nitafungua thread hapa nikiomba maoni na mapendekezo yenu kuhusu ni jinsi gani tutaimarisha timu yetu ya Taifa kwa ajili ya AFCON qualifiers Novemba mwaka ujao.

Tafadhali jiandae kuchangia.

Malinzi

hongera sana mkuu jamal malinzi kwa kutimiza ndoto yako..😛oa
 
Ndugu zangu nashukuru uchaguzi tumemaliza salama na mimi nimeshinda. Nichukue fursa hii kuwashukuru wapenzi na wadau wote wa mpira miguu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki kwenye mchakato.

Siku chache zijazo nitafungua thread hapa nikiomba maoni na mapendekezo yenu kuhusu ni jinsi gani tutaimarisha timu yetu ya Taifa kwa ajili ya AFCON qualifiers Novemba mwaka ujao.

Tafadhali jiandae kuchangia.

Malinzi

Hongera sana bwana Malinzi wewe na timu yako. Nategemea mtakuja na mabadiliko mazuri na tutashirikiana vyema. Kuna vikwazo nimekuwa nikipata hapo TFF, nisingependa nikutane navyo. Niko tayari kushirikiana na timu yako mpya ili kuendeleza na kuleta mafanikio katika mpira wa Tanzania. Kusema ukweli, miaka minne ijayo tukishirikiana vyema, ramani ya mpira wa Tanzania itabadilika. Hiyo ni ahadi yangu kwa timu yako!
Kila la kheri!
 
Nashukuru naweza bado kwenda uwanja Taifa na kushabikia mpira wa tz. Naomba Marsh, kibadeni na mkwasa waje tff. Wambura (the future tff president) for katibu mkuu. Miaka yote ya Ndolanga niligoma kushabikia soka tz hadi alipokuja Maximo.
 
ahaahaaaaa miss u big my lovely sister !

Kwa Malinzi umeshachelewa Kongosho tayari amekaba mpaka penati vekesheni za Uswiss anazdhibiti mwenyewe.

Ni nafasi yako hii usisubili mpaka Matola amuuwe kuwa verified user muanze kugombea vile visima vya gesi.
 
Last edited by a moderator:
Kwa Malinzi umeshachelewa Kongosho tayari amekaba mpaka penati vekesheni za Uswiss anazdhibiti mwenyewe.

Ni nafasi yako hii usisubili mpaka Matola amuuwe kuwa verified user muanze kugombea vile visima vya gesi.
ahaaaa mi wala sitaki bana ..am taken!
 
Ndugu zangu nashukuru uchaguzi tumemaliza salama na mimi nimeshinda. Nichukue fursa hii kuwashukuru wapenzi na wadau wote wa mpira miguu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki kwenye mchakato.

Siku chache zijazo nitafungua thread hapa nikiomba maoni na mapendekezo yenu kuhusu ni jinsi gani tutaimarisha timu yetu ya Taifa kwa ajili ya AFCON qualifiers Novemba mwaka ujao.

Tafadhali jiandae kuchangia.

Malinzi
Mkuu nikupongeze kwa ushindi wako, lakini hapo niliposhade kwa rangi nyekundu kidogo pamanishtua, ungetumia wingi badala ya umoja ingefaa zaidi, ni imani yangu basi kwa shangwe zote hizi za members wengi humu utaleta mabadiliko katika soka letu, lihame kutoka soka ya magazeti hadi soka halisi ya uwanjani, porojo zimekua nyingi sana, utendaji ni sifuri, ni zaidi ya miaka 5o sasa tumekwenda Afcon mara moja tu, na simba na yanga hazina hata viwanja...upokeaji wa mapato viwanjani mfumo ni wa kizamani sana, ukatishaji wa tiketi bado wakizamani, ukaaji ndani ya uwanja hakuna utaratibu, uwazi wa mapato na matumizi, uchaguzi wa timu ya taifa , kwakweli TFF inahitajika mabadiliko makubwa sana kuliko inavyofikirika, nadhani unaweza rekebisha machache katika kipindi cha uongozi wako...si kazi rahisi lakini tunauhakika utajitahidi..basi tukutakie utendaji mwema ulio na uwazi pamoja na weledi ukizingatia uzalendo kwa taifa letu.
 
Back
Top Bottom