Shule ya English Medium imegoma kumuhamisha mwanangu. Hatiani kukosa mtihani wa darasa la nne

We unamwa kweli, Sijasema kila mwenye mume mzee, Nimemlenga yeye kutokana story yake inaonesha anapitia hizo changamoto kwa sababu ameamua kuwa singlemaza.
Soma tena comment niliyo quote na hicho ulichojibu hapa ndio utajua mm na ww nani anaumwa.
Hapo Kuna zaidi ya hiyo million 1 uliyoiona ww, naona unamchukulia mkuu wa wilaya kama nani sijui.
 
Wewe Lipa deni watoto wapewe PREM namba wahamishwe kwenye mfumo acha janja janja

Tena umekosea mpaka heading, kichwa cha uzi kilibidi kisomeke "mwalimu amenitapeli pesa niliyokuwa namtumia kulipa ada"
 
Unahisi baba atafanya nini, wakati kinachotakiwa ni deni kulipwa?
Baba angeweza kulimaliza hilo tatizo aidha kwa kuzungumza nao kwa kina au kutafuta njia nyingine.

Kwa maelezo ya huyu mama na uzoefu wangu katika malezi, hili jambo linatatulika.

Huyu mwanamke kashindwa kuzungumza na hao wenye shule ili kupata muafaka na matokeo yake kaja kulalamika mitandaoni.
 
Umefanya mambo KIENYEJI SANA, kiuhalisia haikwepeki fanya ufuatiliaji wa kwenda kwa BIBI kusanya nyaraka zote za malipo ya ADA ziwasilishe shule uone kama WANAZITAMBUA.

Kama hawazitambui nenda Polisi kamfungulie mashtaka huyo madame uliyekuwa UNALIPA ADA Kupitia kwake kienyeji.

Hakikisha unaoushahidi wa kutosha kuwa ulikuwa unamtumia hizo fedha kama ADA.

BIBI naye athibitishe alikuwa analetewa hizo risiti za ADA na huyo madame.

Hakuna huruma hakuna msaada zaidi ya kulipa ada ili upate huo UHAMISHO , vinginevyo nenda kwa mkuu wa shule muombe kwa dhamana kuwa utalipa hizo fedha kwa mpango mtakao pangiana.
 
Kwa hiyo Baba angewashawishi shule wafute deni?
 
Kwa hiyo Baba angewashawishi shule wafute deni?
Achana na kushawishi; kwanza hilo deni lisingekuwepo kabisa.

Ni baba gani angelipa ada ya shule kwa mwalimu wa somo badala ya kwenda ofisini?

Na hata kama angelipa ageenda kuulizia kama imefika.

Tazama hapa mwalimu aliacha kazi miezi 2 na bado huyu mama hana taarifa.

Maana yake baada ya kuachana na baba watoto ufuatiliaji wa watoto ulikuwa finyu kiasi kwamba bibi ndiye aliyeachiwa jukumu na ndiyo maana risiti zikapelekwa bibi.
 
Tatizo,limetokana na wewe mzazi,
kulipa ada kimakosa.
Nashauri,funga safari kashulighulikie
tatizo huko Mwanza.
Usipende sana kufanyiwa mambo yako,bila kuyasimamia.
 
Hapo la muhimu ni kwenda kwa Afisa Elimu wilaya wa shule ambayo unataka mwanao ahamie, ukijieleza vizuri atamwamisha kwenye mfumo haraka.
 
Tatizo la huyo dada has nothing to do with u-single mother!!! Yeye ni mzembe na sijui hata nimuweke kundi gani!!! Wewe miaka hii kweli unalipa ada kwa kumtumia mtu pesa!!! Huo ni ujinga sijui upumbavu hata sijui niiteje!!! Ma-single mother wako wengi tu na wanatunza familia zao na hawafanyi upuuzi kama huo.
 

Ajitafakari
 
Msiwe mnapeleka watoto wenu kwenye shule hizo za English Mediums ni ubabaishaji mtupu
Uliwaonya sana lakini hawakusikia
Mbona watoto wenyewe hawana maajabu yoyote huku Mitaani.
Yaani maskini badala ya kuongeza miradi analipia watoto English medium leo anaanza kulialia na kamilioni na la 6
 
Naamini una akili timamu.
Makosa ni ya kwako. Mshukuru sana Mwalimu mkuu kukulelea wanao bila kulipa ada. Hupaswi kabisa kuilaumu shule,ishukuru kwa dhati.

Yaani wewe karne hii unalipa ada kwa mtu. Unalipa ada bila joining instructions! Huu si ujinga bali ni upumbavu uliopindukia. Ada inalipwa kwenye akaunti ya shule yaani wewe hujui?
Je,ujuaji wako ndiyo uliosababisha ukavunja ndoa yenu?

Ushauri.
Kwanza lipa ada yao, ikishindikana pata msaada kwa Afisaelimu (w) Msingi. Hii nayo ikigoma muone REO.
Mtoto hawezi kuzuiwa kufanya mtihani. Anaweza kufanyia popote kwasababu ni haki yake!

Mwisho;
Uache ujuaji na kulalamika ovyo wakati makosa yote ni yako.
 
Hizi risiti hazina makosa. Ni za tuition. Ada hulipwa shuleni lakini hela ya tuition hulipwa kwa mwalimu husika
 
Nakuelewa sana mkuu.
watu tunasoma lakni kutatua changamoto ni kazi.

Pia tumesikiliza upande mmoja tu vipi upande wa pili wanasemaje? Unaweza kuta dada hajalipa ada kabisa, hili linakuwaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…