Shule ya English Medium imegoma kumuhamisha mwanangu. Hatiani kukosa mtihani wa darasa la nne

Shule ya English Medium imegoma kumuhamisha mwanangu. Hatiani kukosa mtihani wa darasa la nne

Ushauri kama wa mganga wa kienyeji huu. Amesha kwambia hana hiyo hela na mtoto wapo kwenye usajili wa watoto wa darasa la nne wewe unasema tena aende kulipa hela ambayo hana na ambayo anasema alishalipa hana deni? Huo muda wa kuhangaishana na polisi huoni kuwa deadline itapita na mtoto wake hatosajiliwa kufanya mtihani?
Wewe ni great thinker kweli?

Mtoa mada nakushauri fanya kama ifuatavyo.

1. Chukua RB nenda kamkamate huyo mwalimu ikiwezekana nenda kamtafutie hapo shuleni kwao na hao watu wa hapo shuleni wakuelekeze pa kumpata au kamata mwalimu mkuu weka ndani muunganishe na huyo madam.


2. Wakati hili linafanyika watwange barua ya kuwashitaki kwa kosa la kuzuia uhamisho wa mtoto wako kinyume na sheria ya ya Elimu ya Tanzania ambayo inasema mtoto asizuiwe kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na ada.


3. Wakati huo huo nenda mahakamani maombi hati ya dharula ( injunction order ) ambayo itawaamuru uongozi wa shule kumuhamisha mwanao wakati kesi ya Msingi inasubiri kusikilizwa.

4. At the same time shirikisha media kwa mfano jirekodi wewe pamoja na watoto wako ukielezea kuhusu suala lako huku mtoto akielezea namna anavyo athiriwa na suala lako. Utapata msaada wa haraka sana.

Usifadhaishwe na majibu ya hovyo ya baadhi ya wachangia mada humu. Hivyo ndivyo walivyo wasomi wa Tanzania. Wasomi wa Tanzania huwaga hawaandaliwi kusolve matatizo mapya huwa wanaandaliwa kukariri tu.
Tatzo huo mfumo wa kulipa ada kwa mtu binafsi ndo lilipo anzia, solution hapo ni shule ipate haki yake, huyo mwalimu pambana naye indivudual ila shule haihusiki
 
Kama nimeelewa vizuri ni kuwa wewe umetapeliwa na huyo mwalimu uliyekuwa unampa ada ya mtoto wako akakulipie. Inawezekana mwalimu hakulipa bank na alikuwa anakueletea risiti ambazo hazikutoka kwenye utaratibu halali.
Kwa upande mwingine shule iko sawa kabisa kudai ada yao maana pesa hawakupokea kupitia utaratibu uliowekwa.

Nashauri uende shuleni uko Mwanza ukazungumze na wahusika wa shule muone namna gani mnaweza kutatua tatizo hilo ili mtoto apate haki.

Daa...!!!! Ulifanya kosa sana mkuu.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Kweli mkuu, huo ushauri auzingatie inaweza kusaidia
 
Tatizo mnaona usingle maza kama fashion... Hao watoto watakusumbua lwenye malezi hadi uone umuhimu wa kujishusha na kuishi na mume.
 
Nakupa ushauri kwa ajili ya mustakabali wa mtoto wako na pia usimuathiri kisaikolojia mtoto. Pole sana. Umejieleza kwa kirefu lakini chanzo cha tatizo kinabaki kwako mwenyewe kuamini watu katika mambo ya pesa. Kwani kulikuwa na ugumu gani wa kuchukua namba za akaunti ya shule ukawa unalipa ukiwa huko huko Dar?

Ushauri wangu. Cha kwanza mpaka sasa kubali umepigwa. Tafuta hela sehemu yoyote hata kwa kukopa kama laki sita hivi halafu nenda shuleni hapo mguu kwa mguu ukawalilie wakupe namba za usajili ili mtoto asajiliwe kwanza. Hakika watakupa tu.

Usianze kusema mara oooh sina muda wa kwenda Mwanza wakati hii ni dharura na inatakiwa itatuliwe mapema kwa ajili ya mtoto wako.

Baada ya kupata namba za usajili, sasa anza kufuatilia kuhusu huyo mwalimu ingawa umbali nao utakusababisha ukose nguvu za kufuatilia. Hilo suala inabidi mshirikiane wewe na shule kufuatilia kwa sababu hapo tapeli ni madam na siyo shule. Inawezekana madam alikuwa anaiba hata risiti na mhuri anagonga anawapa watoto wako. Lakini kuiachia shule ikufuatilie suala lako wewe ukiwa Dar haiwezekani tu mana Watanzania tunajuana.
 
Wanasema hawatambui risiti hizo kwa sababu zimetoka kwa huyo mwalimu. Wanataka nilipe milioni moja na laki 2 ndio wamtoe mwanangu kwenye system wamuhamishie kwenye hii shule yake mpya
Hii issue itakuhangaisha sana mkuu kama vipi anzia kwa mkuu wa wilaya ikishindikana huko nenda kwa wazir wa elimu ama Dr Gwajima Nina uhakika huko watakusaidia

Ila huyo mwalimu binafsi ningemtia adabu kwa hicho alichokifanya.
 
Tatizo mnaona usingle maza kama fashion... Hao watoto watakusumbua lwenye malezi hadi uone umuhimu wa kujishusha na kuishi na mume.
Kwahiyo Kila mwenye mume watoto wake wanalelewa vyema sio? Acha kujisahulisha kama vile unaishi sayar ya mars.
 
Kwanini unataka kutupia lawama kwa hiyo shule ya English medium mzazi, hapa kinachoonekana ni wewe kutapeliwa na huyo mwalimu uliyemuamini. Omba tu hiyo shule wakisaidie kiungwana uwahamishe watoto wako ila wakikaza mzigo unaangukia kwako.

Ni jukumu lako kulipa ada shuleni sio kwa mwalimu wa shule.
 
Kwahiyo Kila mwenye mume watoto wake wanalelewa vyema sio? Acha kujisahulisha kama vile unaishi sayar ya mars.
We unamwa kweli, Sijasema kila mwenye mume mzee, Nimemlenga yeye kutokana story yake inaonesha anapitia hizo changamoto kwa sababu ameamua kuwa singlemaza.
 
Nakupa ushauri kwa ajili ya mustakabali wa mtoto wako na pia usimuathiri kisaikolojia mtoto. Pole sana. Umejieleza kwa kirefu lakini chanzo cha tatizo kinabaki kwako mwenyewe kuamini watu katika mambo ya pesa. Kwani kulikuwa na ugumu gani wa kuchukua namba za akaunti ya shule ukawa unalipa ukiwa huko huko Dar?

Ushauri wangu. Cha kwanza mpaka sasa kubali umepigwa. Tafuta hela sehemu yoyote hata kwa kukopa kama laki sita hivi halafu nenda shuleni hapo mguu kwa mguu ukawalilie wakupe namba za usajili ili mtoto asajiliwe kwanza. Hakika watakupa tu.

Usianze kusema mara oooh sina muda wa kwenda Mwanza wakati hii ni dharura na inatakiwa itatuliwe mapema kwa ajili ya mtoto wako.

Baada ya kupata namba za usajili, sasa anza kufuatilia kuhusu huyo mwalimu ingawa umbali nao utakusababisha ukose nguvu za kufuatilia. Hilo suala inabidi mshirikiane wewe na shule kufuatilia kwa sababu hapo tapeli ni madam na siyo shule. Inawezekana madam alikuwa anaiba hata risiti na mhuri anagonga anawapa watoto wako. Lakini kuiachia shule ikufuatilie suala lako wewe ukiwa Dar haiwezekani tu mana Watanzania tunajuana.
Nyongeza. Wala usinielewe vibaya ukadhani naijua hiyo shule, ila nataka mtoto wako akae sawa kwanza halafu mengine yatafuata mana umesema juzi juzi mtoto alikuwa analia anakuuliza itakuwaje.

Niulize. Kwani hiyo shule imekataa kumsajili huyo mtoto kufanya mtihani wa darasa la nne?

Ni kweli, sheria inakataza mwanafunzi kuzuiwa kufanya mtihani kwa sababu ya ada.

Sasa ifahamike, huyo mtoto hajahama bali anasomeka anasoma hiyo shule ya medium huko Mwanza.

Hivi mama mtoto ukiendelea kuleta ubishi kwamba haujatapeliwa na madam, halafu muda ukafika hiyo shule ikamsajili huko Mwanza na yeye anasoma za Kiswahili huko Dar utafanyaje? Sheria ipo wazi inasema asizuiwe kufanya mtihani.

Nenda kawalilie hiyo shule uwape hata hela kidogo, kubali hasara tu.

Huyo mkuu wa wilaya yeye atataka dhuluma kwa shule?
 
Mimi ni single mother umri wangu ni miaka 34. Kwa ufupi Nina watoto wawili wa kiume wa kwanza ana miaka tisa wa pili ana miaka saba. Huyu kwanza yupo darasa la 4 na wa pili yupo darasa la 3. Kilicho nifanya nilete ujumbe huu hapa Jamii Forums ni kitendo cha dhulma kinacho taka kufanywa na shule ya English Medium dhidi ya watoto wangu.

Ni hivi baada ya kuachana na baba wa watoto wangu niliwapeleka wanangu kwa bibi yao Mwanza.

Wakati nawapeleka Mwanza mkubwa alikuwa kafikisha umri wa kuingia darasa la kwanza na mdogo alikuwa na umri wa kuingia chekechea.

Walipo fika mwanza nikawapeleka kwenye shule moja ya English Medium. Mwalimu wa shule hiyo ambae alikuwa jirani yangu ndio alie nishawishi niwapeleke watoto wangu kwenye shule hiyo kwa sababu alisema walikuwa na utaratibu mzuri wa malipo na walikuwa wanachukua hata shilingi elfu hamsini kwa mwezi au themanini.

Niliona inanifaa kwa sababu iliendana na kipato changu. Baba wa watoto pia alikuwa ana toa sapoti ya ada. Kweli nilienda nikalipa hela watoto wakasajiliwa wanapewa na prem number wakaanza kusoma. Pesa nililipa kwa huyu mwalimu kwa sababu aliniambia pesa niwe nalipa kwake yeye anaziwasilisha kwa uongozi kwa sababu walikuwa wanapewa commission na shule kwa kila mwanafunzi watakae mpeleka shuleni. Sikuwa Mimi tu pia kuna baadhi ya wazazi walikuwa wanalipa kwa utaratibu huo. Niliwaacha watoto kwa bibi yao nikarudi zangu Dar kuendelea na shughuli zangu. Nikiwa naendelea na utaratibu huo huo wa kulipa kupitia kwa huyo mwalimu ambae alikuwa anawaandikia watoto risiti wanaziwasilisha kwa bibi yao. Wakati mwingine anasema alikuwa anawaandikia maelezo ya kawaida kwamba wamelipa ada na kwamba ataziwasilisha hela kwa uongozi kisha atapewa risiti na shule atawapatia watoto wazipeleke kwa bibi yao.

Fast forward mwaka jana mwezi wa saba wakati wa likizo nilipiga simu kwa huyo madam kwamba ninataka kuwahamisha watoto wangu kuwaleta Dar anisaidie kuongea na uongozi tupate prem numbers za watoto. Madam akaniambia analishughulikia but akaniambia kwa wakati huo wa likizo watoto wanatakiwa kuwa shuleni hivyo ninatakiwa kulipa shilingi elfu themanini ambayo kama ilivyo kuwa siku zote alitaka niilipe kupitia simu yake. Lakini Mimi nilimwambia Nina wachukua watoto waje Dar ili niwe nao kwa ukaribu zaidi. Akasema sawa atashughulikia suala la uhamisho. Siku iliyo fuata nikampigia sikumpata nikaona nimtume mdogo wangu aende kuchukua namba za mwalimu mkuu wa shule.

Nilipo ongea na mwalimu mkuu wa shule cha kushangaza akasema huyo madam sio mwalimu wa hapo kwa zaidi ya miezi miwili na kwamba amewaliza wazazi wengi ambao walikuwa wanampa pesa yeye. Nikauliza sasa kuhusu haki za watoto wangu vipi kwa sababu ninataka kuwahamisha ma huyo mwalimu alikuwa mwajiriwa wao wanatusaidia vipi sisi wazazi tulio muamini na kumlipa pesa zetu?

Pili nikamwambia atazame kama watoto wamesajiliwa kwa sababu nilimpa shilingi laki moja na elfu sitini kama gharama za usajili kwa kila mtoto.

Niliogopa sana nilihisi huenda hata hiyo shule yenyewe haina usajili.

Mkuu akasema wacha atazame kuhusu status ya wanafunzi hao pamoja na rekodi zao za ada.

Kuhusu status ya usajili akasema watoto wote wana prem numbers ingawa gharama za kuwasajili pia nilipigwa.

Kuhusu ada nikaambiwa nadaiwa shilingi milioni moja na laki 2 kwa sababu tangu watoto waanze kusoma kwenye shule hiyo hawajawahi lipa hata senti tano.

Nikajiuliza how comes mnasema watoto hawajawahi lipa hata senfi wakati hadi matokeo ya watoto yapo nyumbani.

Walifanya vipi mitihani bila kulipa hata senti 5?

Walipata vipi prem numbers kama hawajawahi kulipa hata senti tano?

Nilifadhaika sana na nilianza kukosa imani na hiyo shule kabisa.

Niliwaagiza watoto wangu Dar then nika watafutia shule ya kawaida ya kiswahili. Nili ichagua shule hii kwa sababu ipo karibu na mahali ninapo ishi lakini pili sina uwezo wa kulipa kwenye shule za English Medium kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha na uwezo wangu kifedha kushuka na sapoti ya baba watoto imekuwa ndogo.

Kingine nilikosa kabisa imani na shule za English Mediums hasa hizi zinazo Anza Anza zenye wanafunzi wachache. Bado nilikuwa na kidonda kibichi kutoka kwa shule hiyo waliyo soma watoto wangu.

Nilipata nafasi kwenye shule ya kiswahili huku nikipambana kuomba shule waliyo kuwa wanasoma wawahamishe wanangu kwenye mfumo wawatoe kwenye shule yao wawahamishie kwenye shule hii mpya. Lakini cha ajabu muda wote wamekuwa wakinipiga danadana wanadai niwalipe pesa ambayo kiufupi hawanidai.

Sasa hivi darasa la nne wapo kwenye usajili wa mitihani ya taifa huyu mwanangu jina lake bado linasoma kwenye shule aliyo toka.

Walimu wanasema asipo hamishwa ndani ya deadline maana yake ni kwamba atatakiwa kwenda kufanya mtihani kwenye shule ile ile ambayo ni ya kiingereza au atatakiwa kurudia shule na kama akirudia basi prem number yake itaendelea kusoma juu yani itaonekana yupo darasa la 5 wakati yupo darasa la 4 yani kiufupi ndoto za mwanangu kitaaluma ndio zinakuwa zimeishia hapo. Sasa Mimi naomba msaada wa mamlaka zinazo husika zinisaidie ili mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la 4 ambayo inataka kupokwa na wamiliki wa shule aliyo toka bila justification yoyote. Sheria na taratibu za elimu ya Tanzania zina kataza mtoto kunyimwa haki ya kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na fedha. Uongozi wa hiyo shule ya English Medium unataka kuvunja sheria hii kwa kumkosesha mwanangu haki yake ya kufanya mitihani ya darasa la nne kwa sababu ya deni hewa. Mtoto wangu ameshinda analia siku nzima ya leo anauliza sasa mama itakuwaje..

Naomba msaada tafadhali. Namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua ada zipo namba za mkurugenzi wa shule zipo namba za mkuu wa shule zipo na risiti zote ambazo zilikuwa zinaandikwa kwamba mwanangu amelipa ada pia zipo kwa bibi wa watoto. Nipo tayari kuziwasilisha risiti hizo mbele ya uongozi wa shule kama zikihitajika ila kwa sasa ninacho hitaji ni mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la nne.

Uwepo wa namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua hela zangu pamoja na as wazazi wengine utarahisisha kukamatwa kwa huyo mwalimu ili alipe hizo pesa alizo Chukua. Niliwaambia uongozi wa shule wanisaidie huyo mwalimu akamatwe lakini wamekuwa wanapiga danadana kana kwamba wana mkingia kifua au wana ogopa kuchafua taswira ya shule yao.

Naomba msaada pia huyu madamu akamatwealipe hizo hela alizo Kula lakini wakati zoezi la kumtafuta na kumuweka ndani huyu madamu linaendelea naomba watoto wangu wapewe haki yao ya uhamisho.

Serikali waki hitaji ni disclose taarifa za hiyo shule pamoja na majina ya huyo madam wanae sema amekimbia na hela pamoja na majina ya uongozi nipo tayari kufanya hivyo.

Yericko Nyerere

Mh.
Dkt. Gwajima D
Mtafute pia malisa GJ kwenye mitandao akusaidie kupaza sauti
 
Hii issue itakuhangaisha sana mkuu kama vipi anzia kwa mkuu wa wilaya ikishindikana huko nenda kwa wazir wa elimu ama Dr Gwajima Nina uhakika huko watakusaidia

Ila huyo mwalimu binafsi ningemtia adabu kwa hicho alichokifanya.
Kesi ya milioni moja kupelekana kwa mkuu wa wilaya ni upotevu wa muda tu hata Mkuu wa wilaya hatokubali kuhangaika na ujinga wa hivo, yeye akubali kala hasara amtafute huyo mwalimu haata kwa kumtrack kama mwizi wa simu japo kuwa nako ataliwa hela na polisi ila akimpata atamkanda vizuri mtuhumiwa wake
 
Mimi ni single mother umri wangu ni miaka 34. Kwa ufupi Nina watoto wawili wa kiume wa kwanza ana miaka tisa wa pili ana miaka saba. Huyu kwanza yupo darasa la 4 na wa pili yupo darasa la 3. Kilicho nifanya nilete ujumbe huu hapa Jamii Forums ni kitendo cha dhulma kinacho taka kufanywa na shule ya English Medium dhidi ya watoto wangu.

Ni hivi baada ya kuachana na baba wa watoto wangu niliwapeleka wanangu kwa bibi yao Mwanza.

Wakati nawapeleka Mwanza mkubwa alikuwa kafikisha umri wa kuingia darasa la kwanza na mdogo alikuwa na umri wa kuingia chekechea.

Walipo fika mwanza nikawapeleka kwenye shule moja ya English Medium. Mwalimu wa shule hiyo ambae alikuwa jirani yangu ndio alie nishawishi niwapeleke watoto wangu kwenye shule hiyo kwa sababu alisema walikuwa na utaratibu mzuri wa malipo na walikuwa wanachukua hata shilingi elfu hamsini kwa mwezi au themanini.

Niliona inanifaa kwa sababu iliendana na kipato changu. Baba wa watoto pia alikuwa ana toa sapoti ya ada. Kweli nilienda nikalipa hela watoto wakasajiliwa wanapewa na prem number wakaanza kusoma. Pesa nililipa kwa huyu mwalimu kwa sababu aliniambia pesa niwe nalipa kwake yeye anaziwasilisha kwa uongozi kwa sababu walikuwa wanapewa commission na shule kwa kila mwanafunzi watakae mpeleka shuleni. Sikuwa Mimi tu pia kuna baadhi ya wazazi walikuwa wanalipa kwa utaratibu huo. Niliwaacha watoto kwa bibi yao nikarudi zangu Dar kuendelea na shughuli zangu. Nikiwa naendelea na utaratibu huo huo wa kulipa kupitia kwa huyo mwalimu ambae alikuwa anawaandikia watoto risiti wanaziwasilisha kwa bibi yao. Wakati mwingine anasema alikuwa anawaandikia maelezo ya kawaida kwamba wamelipa ada na kwamba ataziwasilisha hela kwa uongozi kisha atapewa risiti na shule atawapatia watoto wazipeleke kwa bibi yao.

Fast forward mwaka jana mwezi wa saba wakati wa likizo nilipiga simu kwa huyo madam kwamba ninataka kuwahamisha watoto wangu kuwaleta Dar anisaidie kuongea na uongozi tupate prem numbers za watoto. Madam akaniambia analishughulikia but akaniambia kwa wakati huo wa likizo watoto wanatakiwa kuwa shuleni hivyo ninatakiwa kulipa shilingi elfu themanini ambayo kama ilivyo kuwa siku zote alitaka niilipe kupitia simu yake. Lakini Mimi nilimwambia Nina wachukua watoto waje Dar ili niwe nao kwa ukaribu zaidi. Akasema sawa atashughulikia suala la uhamisho. Siku iliyo fuata nikampigia sikumpata nikaona nimtume mdogo wangu aende kuchukua namba za mwalimu mkuu wa shule.

Nilipo ongea na mwalimu mkuu wa shule cha kushangaza akasema huyo madam sio mwalimu wa hapo kwa zaidi ya miezi miwili na kwamba amewaliza wazazi wengi ambao walikuwa wanampa pesa yeye. Nikauliza sasa kuhusu haki za watoto wangu vipi kwa sababu ninataka kuwahamisha ma huyo mwalimu alikuwa mwajiriwa wao wanatusaidia vipi sisi wazazi tulio muamini na kumlipa pesa zetu?

Pili nikamwambia atazame kama watoto wamesajiliwa kwa sababu nilimpa shilingi laki moja na elfu sitini kama gharama za usajili kwa kila mtoto.

Niliogopa sana nilihisi huenda hata hiyo shule yenyewe haina usajili.

Mkuu akasema wacha atazame kuhusu status ya wanafunzi hao pamoja na rekodi zao za ada.

Kuhusu status ya usajili akasema watoto wote wana prem numbers ingawa gharama za kuwasajili pia nilipigwa.

Kuhusu ada nikaambiwa nadaiwa shilingi milioni moja na laki 2 kwa sababu tangu watoto waanze kusoma kwenye shule hiyo hawajawahi lipa hata senti tano.

Nikajiuliza how comes mnasema watoto hawajawahi lipa hata senfi wakati hadi matokeo ya watoto yapo nyumbani.

Walifanya vipi mitihani bila kulipa hata senti 5?

Walipata vipi prem numbers kama hawajawahi kulipa hata senti tano?

Nilifadhaika sana na nilianza kukosa imani na hiyo shule kabisa.

Niliwaagiza watoto wangu Dar then nika watafutia shule ya kawaida ya kiswahili. Nili ichagua shule hii kwa sababu ipo karibu na mahali ninapo ishi lakini pili sina uwezo wa kulipa kwenye shule za English Medium kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha na uwezo wangu kifedha kushuka na sapoti ya baba watoto imekuwa ndogo.

Kingine nilikosa kabisa imani na shule za English Mediums hasa hizi zinazo Anza Anza zenye wanafunzi wachache. Bado nilikuwa na kidonda kibichi kutoka kwa shule hiyo waliyo soma watoto wangu.

Nilipata nafasi kwenye shule ya kiswahili huku nikipambana kuomba shule waliyo kuwa wanasoma wawahamishe wanangu kwenye mfumo wawatoe kwenye shule yao wawahamishie kwenye shule hii mpya. Lakini cha ajabu muda wote wamekuwa wakinipiga danadana wanadai niwalipe pesa ambayo kiufupi hawanidai.

Sasa hivi darasa la nne wapo kwenye usajili wa mitihani ya taifa huyu mwanangu jina lake bado linasoma kwenye shule aliyo toka.

Walimu wanasema asipo hamishwa ndani ya deadline maana yake ni kwamba atatakiwa kwenda kufanya mtihani kwenye shule ile ile ambayo ni ya kiingereza au atatakiwa kurudia shule na kama akirudia basi prem number yake itaendelea kusoma juu yani itaonekana yupo darasa la 5 wakati yupo darasa la 4 yani kiufupi ndoto za mwanangu kitaaluma ndio zinakuwa zimeishia hapo. Sasa Mimi naomba msaada wa mamlaka zinazo husika zinisaidie ili mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la 4 ambayo inataka kupokwa na wamiliki wa shule aliyo toka bila justification yoyote. Sheria na taratibu za elimu ya Tanzania zina kataza mtoto kunyimwa haki ya kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na fedha. Uongozi wa hiyo shule ya English Medium unataka kuvunja sheria hii kwa kumkosesha mwanangu haki yake ya kufanya mitihani ya darasa la nne kwa sababu ya deni hewa. Mtoto wangu ameshinda analia siku nzima ya leo anauliza sasa mama itakuwaje..

Naomba msaada tafadhali. Namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua ada zipo namba za mkurugenzi wa shule zipo namba za mkuu wa shule zipo na risiti zote ambazo zilikuwa zinaandikwa kwamba mwanangu amelipa ada pia zipo kwa bibi wa watoto. Nipo tayari kuziwasilisha risiti hizo mbele ya uongozi wa shule kama zikihitajika ila kwa sasa ninacho hitaji ni mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la nne.

Uwepo wa namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua hela zangu pamoja na as wazazi wengine utarahisisha kukamatwa kwa huyo mwalimu ili alipe hizo pesa alizo Chukua. Niliwaambia uongozi wa shule wanisaidie huyo mwalimu akamatwe lakini wamekuwa wanapiga danadana kana kwamba wana mkingia kifua au wana ogopa kuchafua taswira ya shule yao.

Naomba msaada pia huyu madamu akamatwealipe hizo hela alizo Kula lakini wakati zoezi la kumtafuta na kumuweka ndani huyu madamu linaendelea naomba watoto wangu wapewe haki yao ya uhamisho.

Serikali waki hitaji ni disclose taarifa za hiyo shule pamoja na majina ya huyo madam wanae sema amekimbia na hela pamoja na majina ya uongozi nipo tayari kufanya hivyo.

Yericko Nyerere

Mh.
Dkt. Gwajima D
Nenda karipot police huyo mkuu wa shule na mkurugenz wakamatwe wawekwe lockup halafu nenda kwenye dawati la jamii, jinsia wanawake na wazee watakusaidia
 
Nenda karipot police huyo mkuu wa shule na mkurugenz wakamatwe wawekwe lockup halafu nenda kwenye dawati la jamii, jinsia wanawake na wazee watakusaidia
Mnaingiza siasa kwenye logic,
Hapo kazingua mwenyewe, atafute hela alipenada kisha aanze kumtafuta mwalimu jirani yake,
Shule haikuhusika na chochote ni yeye ndio alileta huo ushost,
 
Ukiachana na hayo yote unayopitia,,Kwanza nikupe pole na pia jipe moyo Kwa kuwa kila mmoja anapitia changamoto zake tena nyingine NI kubwa kuliko hiyo yako,,umejaaliwa utashi kaa fikiri kwa kina tatua hiyo changamoto yako hilo ndilo la msingi Haswa kwenye maisha ni wewe kwanza kama ilivyo Kwa wengine NI wao Kwanza,,Nje ya Mada tunaweza wasiliana zaidi kama hutojali Mama wawili??
 
Ada inatakiwa ilipwe kwenye akaunti ya shule unampaje mwalimu tu fika. Hizo risiti zinatengenezwa, mihuri inafojiwa, signature zinafojiwa yaani kwa kifupi unaweza kuta hizo risiti ni fake japo zina nembo na kila kitu cha shule.
Uzembe ni wako Ada huwa hailipwi kienyeji enyeji kwa kumuamini mtu.
Naweza sema huo mzigo ni wako na umefanya kosa kubwa sana.

Pesa huwa inalipwa kwenye account ya shule tu! Hata kama ni mkuu wa shule kakuambia pesa uwe unamtumia ni Kosa kubwa sana usije rudia tena.
 
Pole Sana , Ila watz na wachangiaji ni Kama huwa hawana kitu kichawani MTU anaomba ushauri then wewe unamlaumu .


MTU akileta lalamiko lake tujikite katika kutatua tatizo na sio kulalamika.
 
Back
Top Bottom