DOKEZO Shule ya Kibaigwa Girls imekataa kumpokea Mtoto wangu sababu sijamaliza Hela za Michango

DOKEZO Shule ya Kibaigwa Girls imekataa kumpokea Mtoto wangu sababu sijamaliza Hela za Michango

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mkuu sio fagio tu,kumpeleka mtoto advance ili apokelewe vitu walivyoorodhesha at least uwe na laki nne ndio pesa ya chini kabisa
Uko sahihi.

Nilikabidhiwa mwanafunzi nimpeleke kwenye hiyo shule mbona nilikiona cha moto.

Mazagazaga yote kuanzia shopping, michango, vifaa zaidi ya laki 6 ilikufa.

Hapa bado nadaiwa Jembe walisema mwezi wa 12 apeleke, ngoja nisubiri kama watafuatilia ila najua ishaisha hivyo
 
Michango ya shule ya serikali inafika laki kweli? Najua ada ni elf 35 Kwa muhula!

Isije kua mleta mada kaenda chako ni chako(jokes)
 
Uko sahihi.

Nilikabidhiwa mwanafunzi nimpeleke kwenye hiyo shule mbona nilikiona cha moto.

Mazagazaga yote kuanzia shopping, michango, vifaa zaidi ya laki 6 ilikufa.

Hapa bado nadaiwa Jembe walisema mwezi wa 12 apeleke, ngoja nisubiri kama watafuatilia ila najua ishaisha hivyo
Laki sita unapeleka shule ya aina Gani hiyo! Isije kua unazungumzia uniform viatu godoro sijui uchafu Gani wa mwanafunzi
 
Heb share hivo vitu vinavyofika laki nne,
Wote tumesoma siku hizi, wew peleka michango mtoto apokelewe, kwa hio unataka vyoo vya mtoto wako visafishwe kwa fagio ya nani?
Jumla ya michango inayotakiwa kulipwa Bank na upeleke pay slip ni elfu 80.

Vifaa unapeleka ukiwa nacho mkononi kama Jembe, Kwanja, Ufagio wa Nje, Mopper, reki, Rimu, ndoo, Godoro, Neti n.k

Then inafuatia Shopping ndio inakula hela ndefu, kumbuka ni watoto wa kike.
 
Habari Watanzania,

Nawasalimu kwa jina la muungano..

Nina kero yangu haswa kwa shule za advance wanaopokea kidato cha tano Walimu wakuu wanachukua maamuzi ya kukataa kumpokea Mtoto ikiwa tu hajamaliza michango na vifaa vingine kama vile vya usafi ukiangalia umbali uliotoka na Mtoto ni mbali sana.

Mfano mimi mwanangu kapangiwa Kibaigwa Girls iliyopo Dodoma, Mwalimu mkuu na makamo Mkuu wa shule wamenigomea kumpokea Mtoto kisa nimelipia nusu ya pesa za michango na sijakamilisha vifaa vya usafi ukizingatia nimetokea mkoa wa Mtwara

Sijui cha kufanya, naomba waziri husika kufuatilia hili jambo, wazazi tunashindwa kuwapeleka shule mapema watoto kutokana na hizi changamoti.

Naomba kuwasilisha

🤝
Wamesikia. Na umeshajulikana
 
Jaman elimu bure ni ada tu !! Ila mahitaji ya mtoto ni wewe mwenyewe mzazi na CCM walivyo wajanja wakasema elimu bure , wazazi msibweteke kusomesha bado ni gharama aseee

Angalau kama una mtoto anaenda kidato cha tano andaa 500k umekosa sana 350k iwepo na kama huna hela weka mambo ya msingi mbele kwanza.
Mfano sare za shule (mashati) atumie alizomalizia kidato cha nne , suruali au sketi apate moja na ya kushindia !! Viatu Pair moja anaweza kuanzia !! Shoe polish ndogo counter book sio lazima aende na Quire 4 aende na ndogo ! Bananeni hivyo hivyo dogo akasome ! Huku akiondoka na wewe unacheki mazingira jinsi ya kumwinua !

Mnavyolalamika hivi dogo akienda ndo imeisha hiyo mtoto anaishi kwa tabu vibaya mno ! Hatukatai kukosa kupo ila ukishapata mtoto na mradi ulimtafuta ukiwa kwenye furaha zako huo ni wajibu sio hiyari tena!
-mzazi mtarajiwa 😂
 
Uko sahihi.

Nilikabidhiwa mwanafunzi nimpeleke kwenye hiyo shule mbona nilikiona cha moto.

Mazagazaga yote kuanzia shopping, michango, vifaa zaidi ya laki 6 ilikufa.

Hapa bado nadaiwa Jembe walisema mwezi wa 12 apeleke, ngoja nisubiri kama watafuatilia ila najua ishaisha hivyo
Ipo hivyo mkuu,yan inabidi kujipanga hasa sio ile elimu bure basi kila kitu atakuta huko shuleni ni tofauti mkuu
 
Kwa hiyo unataka mwanao afanye usafi bila vifaa? Ninyi wazazi mnataka serikali iwanunulie watoto wenu mpaka chupi? Changieni kidogo basi na ninyi ili watoto waishi vizuri shuleni. Kam unaona ni ghali kununua mafagio mpeleke private za katoliki
 
Elimu ya TZ ni rahisi sana, yani unaambiwa fagio tu nalo hutaki kupeleka unalalamika.Tuache ujinga
Nadhani kinacholeta mtanziko hapa ni serikali kuhubiri elimu bure mpaka form 6 halafu pia jamani kuna watanzania bado ni maskini lazima hii hoja ya mkuu ipewe mashiko
 
Mleta uzi sikutetei ila huyo mkuu wa shule kama ni dada mmoja hivi mfupi na amehamia HAPO mwaka juzi basi inawezekana malalamiko yako yana ukweli maana ana kashfa ya upigaji hata huko alikotoka ngoja niishie hapa mamlaka zake zitafwatilia.
Mkuu funguka.
 
Jumla ya michango inayotakiwa kulipwa Bank na upeleke pay slip ni elfu 80.

Vifaa unapeleka ukiwa nacho mkononi kama Jembe, Kwanja, Ufagio wa Nje, Mopper, reki, Rimu, ndoo, Godoro, Neti n.k

Then inafuatia Shopping ndio inakula hela ndefu, kumbuka ni watoto wa kike.
Hongera umetoa ufafanuzi vizuri, maana watu humu wanacomment kama wamekatwa vichwa,


Mtoto wa kike yupo na mahitaji mengi sana,,,,
 
Habari Watanzania,

Nawasalimu kwa jina la muungano..

Nina kero yangu haswa kwa shule za advance wanaopokea kidato cha tano Walimu wakuu wanachukua maamuzi ya kukataa kumpokea Mtoto ikiwa tu hajamaliza michango na vifaa vingine kama vile vya usafi ukiangalia umbali uliotoka na Mtoto ni mbali sana.

Mfano mimi mwanangu kapangiwa Kibaigwa Girls iliyopo Dodoma, Mwalimu mkuu na makamo Mkuu wa shule wamenigomea kumpokea Mtoto kisa nimelipia nusu ya pesa za michango na sijakamilisha vifaa vya usafi ukizingatia nimetokea mkoa wa Mtwara

Sijui cha kufanya, naomba waziri husika kufuatilia hili jambo, wazazi tunashindwa kuwapeleka shule mapema watoto kutokana na hizi changamoti.

Naomba kuwasilisha

🤝
Bro si ulipie tu uachane na hizo Mambo
 
Elimu ya TZ ni rahisi sana, yani unaambiwa fagio tu nalo hutaki kupeleka unalalamika.Tuache ujinga
Unajua nchi zilizoendelea na zenye elimu bora inayoendesha hii dunia, wanafunzi hawafuti hata vumbi katika viti vyako, wachilia kuleta fagio? Elimu (rahisi sana) ni nini kwa mtazamo wako?
 
Sasa wewe ukitetewa huoni na Wazazi wengine watapuuzia suala la kukamilisha ada wakitegemea kutetewa? Shule itaendeshwaje?

Kwanini hukuomba ukamilishe ada na kununua vifaa ndio uende?

Hukuwa na mawasiliano ya Mkuu wa shule na makamu wake?
Na muda unamsubiri yeye tu au huoni changamoto licha ya kueleza bayana umbali anakotoka hivyo kuna gharama nyingi tu mpaka afike shuleni? Kwa uchumi gani wa MTz wa kawaida?
 
Mlipie mwanao,hakuna kitu kizuri kisicho gharama...mbona Watanzania tumekua watu wa kunung'unika sana?huyo mkuu wa shule anafanya kazi kwa mujibu wa taratibu, ulitaka usilipe hiyo Elimu bora itapatikana vipi?kama umepitia mchakato wa Elimu kwa sasa Elimu ni rahisi mno kuliko miaka 2000 kurudi nyuma,...wale waliosoma hiyo miaka ya 2005 kurudi nyuma wanafahamu Wazazi na watoto walivyokua serious...hizo lawama mwanao akisikia utamfanya akate tamaa ya hiyo shule.
Uongozi wa shule umeshindwa kuweka utaratibu wa malipo kufanyika kwa awamu? Kwa nini wanakataa kumpokea mwanafunzi?
 
Japo umeniquote kipumbavu ngoja nikujibu tu kistaarabu,mchango wa shule aufiki hata laki 1,vitu anavyotakiwa mtoto kuripoti navyo ndio gharama,vitabu tu vinakaribia laki 2,uniform,nguo za kushindia,godoro,vitendea kazi n.k,japo ni jukumu la mzazi ila uwezo watu wametofautiana sioni haja kuanza kumbully huyo mzazi ambae mwanae amekataliwa kupokelewa
Vitabu ni hiyari acha kudanganya watu hapa....pumbav
 
Back
Top Bottom