Siasa zimezidi The Law School of Tanzania. Hiki chuo kimulikwe!

Sheria ndogo yao ihusuyo mitihani na rufaa, sheria ndogo namba 15 inasema kuwa mwanafunzi anaweza kufanya uhakiki wa maksi alizopata, tafsiri ni kuwa ataoneshwa booklet na kuona maksi zake ila wapi bwana, hakuna aliyewahi kupewa na ni wakali balaa ukiomba booklet. Wanafunzi hawataki kufaulishwa bali wanataka kuona usahishaji ni wa haki na matokeo ni ya haki au la. Kifungu ni hicho hapo 15(7)
 

Attachments

  • Screenshot_2022-10-08-17-30-04-642_com.google.android.apps.docs.jpg
    115.7 KB · Views: 12
yeah kuhusu ubora wa Mawakili wa Law school ni kweli, wengi wao wamelalamikiwa kutokuwa competent Compared to Mawakili wa bar kina Lissu,Mwakyembe etc
 
yeah kuhusu ubora wa Mawakili wa Law school ni kweli, wengi wao wamelalamikiwa kutokuwa competent Compared to Mawakili wa bar kina Lissu,Mwakyembe etc
Mkuu hali ilivyo pale LST ni kama kama huwa wanakata mstari kuwa hawa waonekane wamefaulu na hawa waonekane wamefeli. Sasa katika hiyo katakata ndio wanafunzi wenye mapenzi na sheria na wenye kuijua sheria wanaachwa halafu wasio na weledi wanatoboa, mahakamani ndio wanaonekana sasa wakiwa hafifu. Ila kungekuwa na usahishaji wa haki, basi hata hao wa LST wangekuwa ni competent tu kama wale wa bar exam, yaani wanaofaulu ingekuwa ni kwa haki na wanaofeli vivyo hivyo
 

Ndo maana tunasema mawakili watarajiwa muende mahakamani kutetea haki hiyo, sasa ninyi wasomi wa degree mna ogopa nini kutetea haki yenu mpeleke kesi iamuliwe na mahakama kuu au mahakama ya juu kabisa Mahakama ya Rufaa .
 

Ilibidi kukupa muda wa kutosha kama alivyoshauri Infantry Soldier ili kuweza kusikia kutokea kwa walalamikiwa.

Hizi ni lugha zilizozoeleka sana pale LST kutokea kwa walimu:

"Kingine sio kila mtu lazima awe Wakili, mbona hampigii kelele NBAA na watu pia wanafeli sana."

NB: Hata MUCHS enzi hizo walikuwa wakisema haikuwa lazima kwa kila mtu kuwa daktari tiba, hadi zama zilipobadilika.

Haipo shaka kuwa utakuwa umetokea kuyatetea yanayolalamikiwa.

Hata hivyo umeshindwa kusema lolote kuhusiana na tuhuma za rushwa, kwamba mwala kwa urefu wa kamba zenu.

Pana mjumbe Black jew anasema mtu akiwa na 5m/- atatoka first sitting hata kama ni kilaza.

Umejikita kuhalalisha Ph.D holders kufeli LST kana kwamba wao huwa hawakupita wala kufaulu LLB.

Unadai kuna uduni wa elimu kwenye vyuo vikuu (bila shaka isipokuwa LST). Hata hivyo kigezo cha kuingia LST ni LLB na walimu wanaofundisha LLB ni hao hao wanaofundisha LST. Iweje uduni huo wa elimu kuwa vyuo vikuu peke yake ambako wanafunzi wanafaulu?

Nikirejea kwenye utata wa matokeo ya LST. Kuna alama dash (-) isiyojulikana nI kufaulu, kufeli, grade au ni marks ngapi?

Ni vipi kuwepo kwa alama za marks zisizojikana kwa watahiniwa kwenye matokeo rasmi?

Vipi kupata alama dash (-) kwenye somo moja umefaulu na kupata alama hiyo kwenye somo jingine kuwa umefeli (conditions zote kwenye columns zikiwa sawa)?

Vipi wanafunzi wawili somo hilo Hilo wote wana dash (-) mmoja kafaulu na mwingine kafeli?

Usiri huu kwenye utahini ni kwa manufaa ya nani?
 
Ndo maana tunasema mawakili watarajiwa muende mahakamani kutetea haki hiyo, sasa ninyi wasomi wa degree mna ogopa nini kutetea haki yenu mpeleke kesi iamuliwe na mahakama kuu au mahakama ya juu kabisa Mahakama ya Rufaa .

Mkuu hii nchi ni ngumu sana. Ndiyo maana waungwana wanadiriki kusema tumerogwa na aliyeturoga kesha kufa.

Alikuwapo bwana mmoja alifungua kesi dhidi ya TLS. Tatizo ni kukosa wa kumwuunga mkono hadharani. Watu wanaogopa kuchuma majanga na kula na wa kwao.

Matokeo alitishiwa maisha, nyuma ya vitisho watuhumiwa ni walimu wa LST.

Itambulike hiki chuo kuna ma billioni ya shilingi wanayovuna walimu hawa. Watakuacha salama in isolation?

Fikiria ada ni zaidi 1,570,000/- kwa mwanafunzi inayolipwa yote si kwa instalment. Hii achilia mbali vitabu vya figisu, vitambulisho, sheria, na mazagazaga mengine. Intake moja Ina wanafunzi kama 700.

700 x 1,570,00 = 1,099,000,000/-

Kwa mwaka Kuna intakes 2.

Anahatarisha je mtu kitita hicho chote akiwa in isolation.

Watanzania ni muhimu tutambue umuhimu wa kujitokeza kuwaunga mkono hadharani wanaojitokeza kupambana na ma mafioso ya namna hii bila kujali yalipo.
 
Wanaojiita mawakili wasomi wenyewe wamekimbilia kwenye siasa na ni zao la hapo, so ni kaliba yake
 

Mkuu umeandika kwa uchungu sana kuyaweka bayana yanayowasibu wanafunzi kwenye chuo hiki ambacho kilipaswa kuwa cha mfano.

Inatia kinyaa kuwa awaye yote anaweza kutetea uozo huu uliofanywa kuwa ni mazoea yaliyokubalika



Kwa hakika hiizi nchi bila ya kusimama na kujitoa mhanga hali itaendelea kuwa mbaya zaidi kwa kina sisi tusiokuwa na majina.

Familia hizi zinajinyima mno kupeleka watoto shule.

"Kweli mwalimu anasema si lazima kila mtu kwa wakili ki fedhuli fedhuli tu?"

Utahini huu uliogubikwa na usiri huu unakubalika namna gani?

Ajabu na kweli bwana BALENSIAGA na wenzake hawauoni uvumilivu wa jamii, wanafunzi na wazazi wa wanafunzi hawa, labda hadi meza ipinduke.

Kwamba kuna undugunization, kujuana, nk? Kwamba una u bin unao fanana na majaji au vigogo wa serikali ndipo nyota yako itang'ara? Nani asiyeyajua hayo?

Kwa hakika wasidhani haya yataendelea milele.
 

Hawa jamaa ni wapuusi tu. Hii inaitwa character assassination. Nani anashindwa kum character assasinate nani akipewa fursa na uwezo?

Haya si ndiyo ya jiwe na kuwafurusha wataalamu majukwaani?
 
Wanaojiita mawakili wasomi wenyewe wamekimbilia kwenye siasa na ni zao la hapo, so ni kaliba yake

Tatizo kubwa ni ubinafsi uliopitiliza. Watu hukaa kimya wakiona haki za wengine zikikiukwa kama haziwahusu wao leo.

Ukipiga kelele kuhusu watuhumiwa kuuwawa na polisi tegemea kusikia ukiitwa panya road. Ya kwamba wanaouwawa na wakajipambanie wenyewe.

Tumekuwa kama mazuzu tu.
 

Je lini mtaweza mawakili watarajiwa wa Tanzania kutetea haki ya kufanya kazi ya uwakili katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kufaulu mitihani ya nchi wanachama wa EAC, mfano ya Kenya

Practising in Kenya​

In general, foreign lawyers are not allowed to practise in Kenya unless they have been admitted as an advocate in the country.
Only citizens of Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda or Tanzania who have the required qualifications may be admitted as an advocate.

Foreign law firms cannot establish their own offices in Kenya. They can only operate in the country through an alliance with a Kenyan law firm. Several international law firms have taken this approach.
 
--Kuhusu Rushwa sijui, labda ueleze linafanyika vipi, mimi sijasoma hicho chuo ila nna mdogo wangu alisoma hapo labda nikamuulize Rushwa kivipi
-halafu si kweli kuwa Walimu wa LLBni walewale wa LST, Kwa hiyo Walimu wa LLB TUMAINI,Rucu,saut,mzumbe ndio wale wale wa LST?Hapana sijui
-
 

Hii si ndiyo ile inaitwa kuruka kimanga sasa?

Kwamba wewe uliyoyaandika hapa ni kutokea kwa taarifa ulizozipata kwa nduguyo aliyesoma hapo?

Yaani detailed course descriptions za LST. Lugha ulizotumia (typical)zile zile za pale LST. Visingizio vile vile vya pale LST kufunika mass failures za wanafunzi na kuhalalisha utahini uliogubikwa na usiri mkubwa usiokuwa na afya.

Kwani wewe ulikuwa na interest gani mkuu kujinasibu na u LST kiasi cha kujikita kutetea yanayolalamikiwa chuoni hapo? Kwamba wewe siyo mnufaika wa lolote kweli, ila mpita njia tu?

Kwamba ungependa tukuelewe hivyo?

Zingatia haya hapa chini siyo ya pedestrian fulani Kariakoo:







Labda uhakiki na nduguyo:

1. Prof. Majamba ni mwalimu sheria UDSM.
2. Mr. Chuwa ni mwalimu sheria Tumaini.
3. Nk, nk.

Kwamba walimu TLS ni wale wale LLB hakuwezi kupotoshwa kwa tafsiri zako finyu unazojaribu kuziweka hapa. Kumbuka mada hii inahusu athari kubwa sana kwa watu kiasi cha awaye yote kujaribu kuifanyia siasa itakuwa ni kutojitendea haki yeye mwenyewe.

Kwani kwenye hiyo isiyopungua 1bn/-inayolipwa in advance na wanafunzi kwa cohort, huyo nduguyo nayo hakuwahi kukwambia mgawanyo unaowafikia walimu huwa ni kiasi gani?

Kwamba rushwa hujaisikia hapo? Kwa mazingira haya na lugha hizi? Akuamini nani?



Rushwa aina gani inaweza kukosekana hapo?

Ama kwa hakika, ya nini serikali kujikita kupambana na panya road mitaani wakati wengine wabaya zaidi wako hapa?

Ikumbukwe panya road wa TLS anazalisha panya road zaidi mitaani. Kwani pesa zinazopotea bure kwenye hii kufelishana zisigetumika kuinua wanafamilia wengine kuwaepusha na u panya road?

Ama kwa hakika hii nchi ni ngumu kweli kweli.
 
-nilishakwambia sina interest zaidi ya huyo mdogo wangu ambaye alikuwa anasoma hapo na alikuwa na supp kadhaa
-kuhusu mgao wa hiyo bilioni 1 kwa kweli sijui kabisa mkuu
-naona umeweka takwimu za matokeo, unadhani hapo first sitting walitakiwa wawe angalau wangapi?, discontinue wangapi? na supp wangapi?
-kuhusu rushwa hata mimi nimekuwa nikisikia tena mara nyingi tu, hoja ni kwamba hao 26 wa fest sitting watakuwa wamepata kwa rushwa au?
-Vipi kuhusu hoja ya kwamba kuna mitihani huwa inatungwa ni migumu kupita kiasi,i.E iko juu na uwezo wa mwanafunzi?/
-halafu kuna hoja ya kwamba ndugu ni Walimu hiyo ni kweli, nimeuliza nikaambiwa kuwa kuna ndugu wapo hapo wanafundisha.
 
Mkuu yaonekana umejipanga kuitetea LST ukitokea gizani. Labda kama unadhani tunalazimika kuandika malalamiko haya kwa bahati mbaya.

Huna lolote la kusema kuhusiana na utahini? Zingatia kinacholalamikiwa ni utahini wala si kingine.

NIsiache kukumbusha ule usemi pendwa ya kuwa:

"The way to hell is paved with good intentions."

Kwanini haya ya kuwaandaa wanasheria kwa vitendo yasifanyike chini ya vyuo vikuu husika wanakosoma kama inavyokuwa kwa interns wale wa medicine?

Kwa nini vyuo viruhisiwe kufundisha wanasheria wasioweza kufanya kazi popote?

Mwanafunzi a pass first class chuo kikuu lakini a DISCO law school kwenye magnitude hii?



Halafu wewe usimame kidedea kutetea uozo huu? Kwamba wewe unaona ni sawa?

Hivi nitakuwa niko mbali na ukweli nikidhani kuwa wewe bagamoyo ni mmoja wa wale wahusika wakuu mlioifikisha TLS kwenye haya ya siasa hapa tulipo?
 
HATA MATOKEO YAO HAYA YALIYOTOKA JUMATANO YANA WALAKINI INABIDI WARUDIE KUYASAHIHISHA MAANA KUNA WATU WAMEFELISHWA MAKUSUDI

Naunga mkono hoja. Hapa kuna pass mark dash (-). Hiyo haijulikani ni kufaulu, kufeli, grade gani au ni marks ngapi.

Somo moja mtu anapata dash kafaulu na somo jingine dash kafeli.

Watu wawili somo hilo wana pass mark dash, mmoja kafeli mwingine kafaulu.

Kwa uhalali upi?
 
Familia hizi zinajinyima mno kupeleka watoto shule.
Watu wanahangaika kusomesha wanafunzi miaka 4 ya chuo kikuu LLB na mwaka mmoja huko LST halafu ada zao zinatupwa kwa elimu ya kijana kuishia hapo LST kwa kukwamisha kimakusudi na walimu wa taasisi hiyo, wanaendelea kunyonya ada za wanafunzi kwa kuwadiskosha makusudi, wanaendelea kuneemeka kwa ada za supplementary ambapo kila component hulipiwa Tshs. 30,000/= yaani kwa somo moja tu, LST huweza kuingiza zaidi ya milioni 11 kwa siku moja (masaa 3) tu, sasa kwa masomo karibu 10 wanaingiza kiasi gani? Na hapo ni somo, ukisema uchambue kwa component maana yake somo moja lina component 3, kwa hiyo mtu analipa elfu 90 kwa somo zima, sasa kwa wanafunzi 400 waliosupp hawa LST wanapata kiasi gani? Na hizi ada ndio chanzo chao kikuu cha mapato kwa mujibu wa Fact and Figures report ya 2018/2019 iliyotolewa nao LST, inapatikana hapa Facts and Figures 2019
Sasa kwa nini isiaminiwe kuwa wanafelisha sana wanafunzi ili LST wapate mapato kupitia ada za masomo na supplementary??

Kwani kwenye hiyo isiyopungua 1bn/-inayolipwa in advance na wanafunzi kwa cohort, huyo nduguyo nayo hakuwahi kukwambia mgawanyo unaowafikia walimu huwa ni kiasi gani?
Mkuu, hii taasisi ni ya kifisadi kabisa na kama ulivyoeleza madhara ya ufelishaji wao hovyo wanafunzi ni makubwa kwani sio kwa watu binafsi tu bali kwa Taifa zima, unapozalisha majobless wenye taaluma, hasara ni kwa Taifa, cha ajabu Mkaguzi Mkuu wa Serikali hajawahi kutoa ripoti ya ukaguzi kwa hii taasisi inayojiita ya serikali huku kihalisia ni ya watu binafsi wachache.

Hebu angalia hapa, kwa mujibu wa Fact and Figures yao ya 2019, inaonesha LST walikuwa na watumishi 52, huku walimu wakiwa ni 11 na 41 wakiwa ni wasio walimu (utawala). Sasa hawa watumishi wanalipwa mishahara kwa mwaka kiasi cha Tshs. 1,321,523,820.97 ambapo kwa mwezi ni kiasi cha Tshs. 2,117,826.64 (flat rate) kwa kila mwalimu. Fedha hii haitoki serikalini bali ni katika ada za wanafunzi, hapo fedha za supplementary, statement za matokeo, rufaa nk hazijaoneshwa hesabu yake zinatumika vipi. Na ni kwa nini kama chuo ni cha serikali, mishahara ya walimu itokane na ada za wanafunzi na sio kapu kuu la serikali?? Hamuoni kuwa kufanya ada kama chanzo cha mapato ya kulipa mishahara ni mwanya wa wazi wa kutengeneza 'vipindi' ili mishahara ipatikane?? Ni wazi wanafunzi wanafelishwa ili warudie kusoma na mishahara ipatikane kupitia ada zao. Tunaomba Serikali hii hii ingilie kati, uchunguzi ufanyike kwenye matokeo ya wanafunzi na tuhuma za rushwa. Hali ni mbaya, kweli mwalimu anaharibu future ya mwanafunzi kwa sababu tu apate mshahara?? Kweli

Hiyo fact and figures ni kama inavyojieleza hapa kwenye kielelezo.
 

Attachments

  • Screenshot_2022-10-09-09-21-32-668_com.google.android.apps.docs.jpg
    97.3 KB · Views: 10
  • Screenshot_2022-10-09-09-22-06-373_com.google.android.apps.docs.jpg
    56.5 KB · Views: 5
  • Screenshot_2022-10-09-09-20-36-568_com.google.android.apps.docs.jpg
    74.2 KB · Views: 8
Hata ujibuji wa mitihani, unaku mwenzako anasema alijibu namna hii, na wewe unakuta ulijibu namna ileile ila sasa yeye amefaulu na wewe umefeli, ukiomba uoneshwe booklet yako namna ilivyosahishwa, ni vita hawakubali kukupa na wanakujibu kwa kejeli kuwa uliwahi kuona wapi chuo kikuu wanapewa booklet kuonesha usahishaji?? Hapo wanasahau kuwa bylaw yao wenyewe inaruhusu jambo hilo na pia wanasahau kuwa LST sio chuo kikuu..

Wanataka watu waje kuua walimu kwa hasira humo maofisini ndio wajifunze
 

Jitihada zako za kuchomoa betri zinaonekana. Umesahau kuwa ni wewe ulisema tuhuma za rushwa huzijui. Kumbe na wewe umekuwa ukizisikia? Hukuwa umeonyesha Hilo awali.

Kwamba kuna mitihani migumu inatungwa kuliko uwezo wa wanafunzi? Hii ni hoja yako mpya kabisa kuwahi kuisikia. Umeipata wapi wewe hoja hii? Kumbuka nimejaribu kuainisha wazi wazi tatizo na hata ufumbuzi wake.

"Pana tatizo la utahini. Ufumbuzi pande tatu ziwe tofauti. Yaani mtahiniwa, mtunga mtihani na msahihishaji. Mtunga mtihani asiwe msahishaji na asiwe mwalimu husika wa somo. Kama ilivyo kwa shule za msingi na secondary ambako masomo na mitihani ni kwa mujibu wa syllabus."

Kwamba takwimu zilipaswa kuwa je?

Haupo mtihani ambao matokeo yake hayafuati formula ya normal distribution na yakawa halali:



Kwa utaratibu huu takwimu zingekuwa hivi:



Ambako idadi ya DISCO ingekuwa takribani sawa na idadi ya walio perform with distinction au first class.

Mfano angalau ingekuwa hivi:

Wenye distinction au first class 3
DISCO 4
supp 26
Pass 600

Ni aibu kuwa malengo mazuri yaliyokuwapo ya kuwa na TLS yamegeuzwa siasa na sasa chuo ni kijiwe cha ndugu waliojiapiza kuwafelisha wahitimu waliofaulu vyuo vikuu kwa starehe zao.

Kwa uhalali upi? Au kwa ugumu upi wa sheria?
 

Inasikitisha sana. Nchi imegeuzwa kuwa shamba la bibi.

Kuleta mabadiliko kwenye mafyongo kama haya inawezekana. Siyo rahisi lakini pia siyo impossible.

Watanzania tumekuwa watu wakulalamika bila kuchukua hatua kwa vitendo. Vyama vya siasa navyo ndivyo hivi visivyoweza kuziona fursa za kupigania haki. Nao wamebakia kulalama tu.

Imeachwa kuwa kupigania haki ni sawa na kujichumia majanga na kula na wa kwenu.

"Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe."

Ni heri kufukuzwa chuo ukipigania haki ya kufaulu au kufeli kwa halali, kuliko kusubiria kufelishwa ukiwa ada umelipa, vitabu vyao umenunua nk na kunyanyaswa juu.

Erythrocyte hatuna cha kufanya kwenye kadhia kama hizi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…