Siasa zinaamua pia mpira: Kipindi cha Rais wa Pwani / Zanzibar GSM huwa anachapisha pesa, Timu anayoidhamini itaendelea kutawala hadi 2030

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Kwa mpunga anaoingiza kwenye biashara kwa sasa pesa zinatiririka mithiri ya mashine ya kutoa copy.

Kipindi cha Kikwete mambo kwa GSM yalikuwa poa sana japo hakuwa kaingia kwenye mpira.

Kipindi cha Magu hali ilikuwa ngumu sana, hapa nakumbuka alikuwa anasumbuliwa hata na kina Makonda

Rais wa sasa nae ni kama marudio ya style ya uongozi wa Kikwete, GSM imerudi kwa kishindo hakuna kifani, Pesa anazovuna ni nyingi mno, biashara zinatapika pesa

Kwa hali hii navyoona ni mpaka 2030 mwendo ni huu huu maana mpira ni pesa na hizo pesa GSM anazichapisha!! kabla ya 2027 Yanga itakuwa inalipa wachezaji mishahara ya milioni 50,

Anguko zito linakuja 2031.
 
Kelele tu hizi

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo Rais anayetokea Pwani pamoja na huyu mama wa sasa ukimjulisha na huyo GSM ndiyo waliosababisha timu nyingine kama simba, Azam kukosa ubingwa wa ligi kuu! Kuingia hatua ya nusu fainali kombe la shirikisho! Kuisababishia simba kuishia hatua ya robo fainali!!

Ni huyo Rais wa Pwani na huyu wa ukimjulisha na GSM ndiyo walio washinikiza kusajili wachezaji wa kukoteza!! Ni miezi michache tu iliyopita Yanga hii hii mlikuwa mkiikejeli kwa kushindwa kumlipa Fei Toto mshahara mkubwa!

Shida iko wapi vilabu vyetu vikifikia hiyo hatua ya kuwalipa wachezaji wao milioni 50! Tena kwa mwezi!! Vipi wale wachezaji wanaolipwa Pounds 500,000/= kwa wiki!!

Kwa hali hii basi hata zile milioni 5 za motisha kwa kila goli wangepewa Yanga tu.

All in all, haya ni mateso yanayotakana na mafanikio ya Yanga ndani ya hii miaka miwili. Hakuna sababu nyingine kwa mtu mzima na akili zake, kujitoa ufahamu kiasi hiki.

Na mtateseka sana kudadek zenu! Mtatafuta kila aina ya visingizio, na mwisho wa siku mtagundua chanzo cha matatizo yote, ni nyinyi wenyewe na ubabaishaji wenu.
 
sasa ndo utafute timu ya kushangilia mpk 2030 timu yako iwe inateseka tu sio poa
 
Huko mbali sana

Ebu relax,

Just enjoy the moment
 
Aahaaa
 
Thibitisha kwamba GSM amechukua jukumu la Central Bank ku print pesa
 
Duh kwahyo makolo hawatachukua kombe hadi 2030
 
Na nyie chapisheni hizo pesa, labda mtaacha kutolewa kiume.
 
Kwa Jina la Yesu tunakataa anguko.

Shindwa pepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…