Sijaona andiko la Uislamu linalokataza kula mbele ya mtu aliyefunga

Sijaona andiko la Uislamu linalokataza kula mbele ya mtu aliyefunga

Usichanganye mambo mnamu!
Naam ngoja nikusome zaidi nione wapi nimechanganya mambo.
Kula ni jambo la halali kidini iwe hadharani au kwa siri lakini kwa mwezi wa ramadhani linakuwa ni halali kwa mwenye dharura.
naam haswaa.
iyo wala haina shida na ni sheria inayowahusu waislamu pekee
Naam naam hakika.
Kwa sababu serikali ina jukumu la kuhakikisha watu wake wanakuwa huru katika kutekeleza ibada zao
Naam hakika ndugu yangu ndivyo ilivyo.
ndipo kwa Zanzibar wakaamua kupiga marufuku watu wote kula hadharani muda wa kati ya alfajiri na magharibi bila kujali mlaji ni
Hapa ndipo shida inapoanzia,na nitakujibu katika nyanja mbili.

1.KiDINI : unapokuwa umefunga alafu mtu akala unamuona basi ELEWA kwamba mtu huyo hakunyimi uhuru wa wewe kuendelea na ibada hiyoo ya kufunga,huo ufahamu haupo katika uisilamu ni madai ya kijinga ya baadhi ya watu wasioelewa mambo.

Ni kama mtu anayefanya ibada ya kusali aseme kwamba ananyimwa uhuru na mtu ambaye amemuona anapita na pikipiki wala hasali,haimake sense

2.KiSHERIA ZA NCHI : wataalamu kadhaa wa sheria wamwfafanua kwamba sheria ama katiba ya zanzibar haijataja jambo hilo kwamba ni kosa,na ndio maana watu wanaohukumiwa wanahukumiwa kwa makosa mengine kama vile ukorofi na uzururaji na sio kula hadharani mchana.

Mmoja ya wanasheria hao ni wakili maarufu zanzibar Ndugu kijogoo alifafanua hivyo,na kama wewe unaona kuna sheria iliyotaja wazi kosa hilo ilete hapa.
Ndiyo maana nikasema HIZO NI SHERIA ZA SERIKALI KATIKA KUWARAHISISHIA WATU WAKE KUTEKELEZA IBADA YAO
Kwanza serikali haijaweka bado hiyo sheria unaposema ni sheria unakuwa unakosea na ndio maana ukienda mahakamani ukaomba data za watu waliohukumiwa kwa kosa la kula mchana wa ramadhani huwezi kukuta hiyo kitu.

Pili andiko langu limelenga KUBAINISHA KWAMBA DINI HAIJAKATAZA MTU ASIYEFUNGA KULA MBELE YA MTU ALIYEFUNGA,hivyo huku unakozunguka kote mkuu ni kwenda kimyume na maudhui yangu.
Kama unamaanisha hakuna dalili ya kuzuia kwa yule asiye muislamu basi ni kweli hakuna lakini jibu nilishatoa hilo hapo juu kwenye herufi kubwa.
Jawabu lako sio la kweli kama nilivyotangulia kusema na sababu ni tatu nakuwekea.

1.hakuna sheria iliyitaja kosa hilo.
2.jambo hilo ni kuingilia uhuru wa wengine kwa sababu kula ni jambo lenye kufaa.
3.jawabu lako limeenda kinyume na maudhui yangu yaani umetoka nje ya reli.
Kama unasema kumaanisha waislamu basi ndugu utakuwa unapotea au umekwishapotea
Muisilamu ambaye hafungi bila udhuru wowote bila shaka anafanya makosa sio sawa na Allah ndio atamhukumu kwa kosa hilo,

Muisilamu ambaye hafungi bila sababu akila mbele ya mwenzie aliyefunga jua tu kwmaba atakuwa makosani kwa sababu hajafunga na sio kuwa makosani eti kwa sababu tu anakula mbele ya mtu aliyefunga.
Wanazuoni wote wanaona kuwa mtu muislamu asiye funga basi ikifika muda anataka kula asile hadharani
Unaposema wote bado unakanganya mambo kwa sababu neno wote ni pana sana kwani hatujui unakusudia wote wa kishia ?
Wote wa kisunni ?
Wote wa kiibadhi ?
Wote wa ki shaairah ?
Wote wa kiahmadiyyah ?

Hivyo basi kauli yako ya wanazuoni wote bado haina mashiko kwa sababu wote unayoisema haipo.
Hekima yao ni moja tu katika hili nayo ni kuepusha mikanganyiko,
Hakuna mkanganyiko wowote,huo sio mkanganyiko wa uhalisia bali ni sababu iliyotengenezwa tu ili katazo hilo lipite.

Mtu ambaye hajafunga akila mchana haleti mkanganyiko kwa wasiokuwa waisilamu bali ataleta mkanganyiko kwa waisilamu WASIOJIELEWA kwa sababu waisilamu wasiojielewa wao hawajui kwamba kuna watu kwao kula ni ruksa mchana wa ramadhani.
sintofahamu na dhana mbaya kwa wasioelewa vizuri dini.
Hekima hii ni feki kwa sababu ipo kinyume na malengo waliyoyakusudia.

Kitendo cha kulazimisha watu wasile hadharani ndio kunaleta dhana mbaya pamoja na sintofahamu kwa wasiokuwa waisilamu.
Na moja ya dhana mbaya zinazoletwa na katazo hili ni kudhani kwamba uisilamu ni dini isiyotoa uhuru kwa wasiokuwa waisilamu na pili watu wasioelewa uisilamu hudhani kwamba uisilamu unalazimisha watu kufanya ambbayo kwao sio wajibu,

Hivyo hekima hiyo iliyokusudiwa inakuwa kinyume chake na sio kama unavyotuaminisha hapa na jambo hilo liko wazi.
Imagine mama aliye kwenye siku zake ale hadharani unafikiri mtoto wake wa miaka 7-9 atamuelewaje?
Suala la malezi baina yako na mwanao haliingilii uhuru wa watu wengine,watu wengine hawalazimiki kufuata yale unayomfundusha mwanao.

Hata ukiwa unamfundisha mwanao kusali unatakiwa na wewe mzazi ama baba ukasali naye msikitini.
I
Lakini kitendo cha wewe na mwanao kwenda msikitini hakitofanya uwalazimishe wasiokuwa waisilamu nao waende msikitini au wajifungie majumbani eti kisa unamfundisha mwanao kusali,

hiyo ni sababu dhaifu mkuu kwa sababu watu wengine wana uhuru wao ambao hauwezi kuvunjwa kwa kigezo tu kwamba unamfundisha mwanao.
Au chukulia unafakamia hotelini je huoni yule asiye mwislamu atautafsiri uislamu vibaya pamoja na waislamu wenyewe na mwisho hata kukata tamaa na uislamu kabisa
Atautafsiri uisilamu vibaya endapo mtamlazimishe asile mchana mpaka ajifiche wakati yeye halazimiki kwa lolote juu ya mfungo huu.
Inawezekana sijaeleweka kabisa
Umeeleweka ila haujakubalika hoja zako ndio msana mimi mtoa uzi nakujibu nukta baada ya nukta.
lakini kwa ufupi ni kwamba huyu bwana mleta uzi anapinga ijitihad za wanawazuoni.
Jitihada za wanazuoni hazina nafasi katika Dini ya Allah ambayo imekamilika,wanachuoni hawana nafasi ys kuharamisha jambo ambalo Allah kanyamazia hakubainisha uharamu wake.

Rejea hadithi ya mtume ambayo mtume alifikia kusema...

".. وسكت عن أشياء رحمة لكم فلا تبحثوا عنها
.."Mungu amenyamazia baadhi ya mambo ili iwe rahma kwenu,basi msichunguzechunguze.."

Wanachuoni hawatakiwi kuharamisha mambo ambayo Allah ameyanyamazia kwani Allah hakuona ?
Au uisilamu haukukamilika ndio maana tunahitaji jitihada za wanazuoni ?

Tumuulize tu mbona akioga mtoni nguo anaziweka mbele yake ili azione vizuri je, aya na hadithi inayoelekeza hivyo kaipata wapi?
Asili kila ambacho hakikutajwa uharamu wake basi ni halali.

Hivyo maadamu sikuharamishiwa kuweka nguo mbele yangu basi ni halali kwangu kuweka.

Elewa hiyo kanuni kwamba vitu vyote kwa asili ni halali,pale inapokuja dalili ya kuharamisha ndio kinakuwa haramu.


Hivyo usiniulize kwa nini naendesha gari wapi limetajwa kwamba uendeshe katika hadithi , jawabu langu ni rahisi kwamba hakuna aya au hadithi imeharamisha jambo hilo ndio maana tunachagua cha kufanya.

Elewa hii kanuni "الأصل في الأشياء الإباحة

Asili katika vitu ni kujuzu kufanyika kwake endapo haijsjs dalili ya kuharamisha.
 
Leo ss Ni ijumaa kuu ilanimeona wagogo wengi wanakula nyama bila wasiwasi
Kutokula Nyama Siku ya Ijumaa Kuu Ni Amri Ya 2 katika Amri za Kanisa Moja Takatifu Katoliki La Mitume.

Miongoni mwa wagogo Kuna Wakristo wasio wakatoliki, Kuna Wapagani wengine kama waislamu na wote wasiomuabudu Mungu Baba Mwana na Roho Mtakatifu.

Hivyo Kuona wagogo wanakula nyama si tabu .. yawezekana no wagogo Wapagani.
 
Tukiwa tuna masiku kadhaa tokea mfungo uanze nimejaribu kukutana na changamoto kadhaa kwa baadhi ya watu wakikereka na watu wanaokula mbele yao huku wakiwa hawajafunga.

My take
Sijaona andiko linaloashiria kuonesha kwamba ni vibaya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Dhambi ipo kwa mtu ambaye anatakiwa afunge na hajafunga na wala hana sababu ya msingi.

dhambi hiyo itakuwa ni kwa sababu hajafunga na wala sio dhambi kwa sababu ya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Na wala sijaona andiko linalomlazimisha mfungaji ati achukie kitendo cha mtu kula mbele yake.
DarCity atakubishia
 
Ni sheria za nchi husika
Kula, Kutafuna, Kunywa maji kwenye mazoezi, au kula mchana hadharani wakati wa Ramadhani ni uhalifu katika nchi za kiarabu UAE.

Wakati wa Ramadhani, hairuhusiwi kula, kunywa au kuvuta hadharani nyakati za mchana

Adhabu kwa mtu anayeonekana kukiuka sheria inaweza kuwa kifungo cha hadi mwezi mmoja, au faini ya Dirham 2,000.
Kaomba kufahamu andiko nakazia
 
Tukiwa tuna masiku kadhaa tokea mfungo uanze nimejaribu kukutana na changamoto kadhaa kwa baadhi ya watu wakikereka na watu wanaokula mbele yao huku wakiwa hawajafunga.

My take
Sijaona andiko linaloashiria kuonesha kwamba ni vibaya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Dhambi ipo kwa mtu ambaye anatakiwa afunge na hajafunga na wala hana sababu ya msingi.

dhambi hiyo itakuwa ni kwa sababu hajafunga na wala sio dhambi kwa sababu ya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Na wala sijaona andiko linalomlazimisha mfungaji ati achukie kitendo cha mtu kula mbele yake.
Wewe
Tukiwa tuna masiku kadhaa tokea mfungo uanze nimejaribu kukutana na changamoto kadhaa kwa baadhi ya watu wakikereka na watu wanaokula mbele yao huku wakiwa hawajafunga.

My take
Sijaona andiko linaloashiria kuonesha kwamba ni vibaya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Dhambi ipo kwa mtu ambaye anatakiwa afunge na hajafunga na wala hana sababu ya msingi.

dhambi hiyo itakuwa ni kwa sababu hajafunga na wala sio dhambi kwa sababu ya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Na wala sijaona andiko linalomlazimisha mfungaji ati achukie kitendo cha mtu kula mbele yake.
Wandanganye wavivu wa kusoma kama wewe eti andiko halijaonekana. Sio kila ambacho hujaona kuwa maana yake hakipo. Saa nyingine hujaona kwa sababu wewe ni kipofu au huoni vizuri. Nini maana ya kuamrisha mema na kukataza mabaya . Ikiwa Allaah kuamrisha watu wasile mchana wa Ramadhani yule anayekula mchana kfanya jambo baya. Na mtume صلى الله عليه وسلم anasema " Mwenye kuona jambo baya na alizuie kwa mkono wake, na Kama hawezi alikataze kwa ulimi wake , na kama hawezi na alichukie kwa moto wake".
Kwa ujumla mimi nasema Zanzibar ina taratibu zake ambazo ni nje ya mambo ya muungano na lazima ziheshimiwe.
 
Tukiwa tuna masiku kadhaa tokea mfungo uanze nimejaribu kukutana na changamoto kadhaa kwa baadhi ya watu wakikereka na watu wanaokula mbele yao huku wakiwa hawajafunga.

My take
Sijaona andiko linaloashiria kuonesha kwamba ni vibaya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Dhambi ipo kwa mtu ambaye anatakiwa afunge na hajafunga na wala hana sababu ya msingi.

dhambi hiyo itakuwa ni kwa sababu hajafunga na wala sio dhambi kwa sababu ya kula mbele ya mtu aliyefunga.

Na wala sijaona andiko linalomlazimisha mfungaji ati achukie kitendo cha mtu kula mbele yake.
Wewe
Andiko langu linahusu uisilamu na sio nchi fulani.

Ujumbe wangu ni kuwa sijaona katazo la uisilamu wenyewe likisema kwamba ni dhambi kula mbele ya mtu aliyefunga.

Elewa ninaposema uisilamu,sijataja nchi.

Kama kuna Nchi inakataza ijue tu keamba inakataza kwa utashi wake na sio sheria ya Dini inasema hivyo
Wewe maandiko ya uislamu huyajui kwa sababu wewe si muislamu au hujui chochote kuhusu Sheria za uislamu. Natamani ningekutana na wewe ana kwa ana nikuonyeshe vitabu vingi tu vinavyoonyesha usahihi wa hicho wanachokifanya wazenji. Ila kwa kukusaidia ni kwamba katika misingi muhimu sana ya uislamu ni swala la kuamrisha mema na kukataza mabaya. Moja ya mambo mema ni kufunga mchana wa Ramadhani, na Moja ya mambo mabaya ni kula mchana wa Ramadhani bila dharura ya kisheria na kwa utaratibu wa kisheria. Mimi nikushauri tu ukasome biblia tu na misali ya waumini na katekasimu takatifu, habari za maandiko ya Sheria na kanuni za uislamu unajitia ujuaji wakati huna ujualo!.
 
Wewe

Wewe maandiko ya uislamu huyajui kwa sababu wewe si muislamu au hujui chochote kuhusu Sheria za uislamu. Natamani ningekutana na wewe ana kwa ana nikuonyeshe vitabu vingi tu vinavyoonyesha usahihi wa hicho wanachokifanya wazenji. Ila kwa kukusaidia ni kwamba katika misingi muhimu sana ya uislamu ni swala la kuamrisha mema na kukataza mabaya. Moja ya mambo mema ni kufunga mchana wa Ramadhani, na Moja ya mambo mabaya ni kula mchana wa Ramadhani bila dharura ya kisheria na kwa utaratibu wa kisheria. Mimi nikushauri tu ukasome biblia tu na misali ya waumini na katekasimu takatifu, habari za maandiko ya Sheria na kanuni za uislamu unajitia ujuaji wakati huna ujualo!.
Huyu Qadiani kazi yake ni kupinga kila waislamu wana chofanya ili waonekane mbele ya wa ukuristu kwamba uislamu ni wa hovyo wa Ahmadiyya/Qadiani ndo sahihi, tatizo lao kuu hao maqadiani hawasomi madrasa wana kalilishwa vipande vipande Quran, na waheshimu hadeeth au Sunnah za mtume, kwa ufupi sio waislamu ni makaafiri wspinga Uislamu.
 
Um
Ni kweli na ndio maana hata mimi sijawapangia nini wafanye,au nimewapangia wapi ?

Sasa kitendo cha wao kuingiza pombe hakituzuii sisi kusema pombe haifai katika uisilamu.

Wao acha waingize pombe ila na sisi tutaendelea kuhubiri kwamba uisilamu umekataza pombe.

Wao acha waendelee kuzuia watu mambo kadhaa katika ramadhani ila na sisi haituzuii kusema kwamba uisilamu haujakataza hayo.

Hivyo basi uhuru wa watu kujipangia mambo yao hautufanyi sisi tusibainishe uhalisia wa uisilamu
Esahau pepo ya ala kuna pombe sasa unajizuia nini wakati ukifa utaenda kukutana nazo,dini ni upuuzi sana ni ugonjwa wa akili mbaya zaidi wagonjwa hawajui kama ni wagonjwa
 
Wewe

Wewe maandiko ya uislamu huyajui kwa sababu wewe si muislamu au hujui chochote kuhusu Sheria za uislamu. Natamani ningekutana na wewe ana kwa ana nikuonyeshe vitabu vingi tu vinavyoonyesha usahihi wa hicho wanachokifanya wazenji. Ila kwa kukusaidia ni kwamba katika misingi muhimu sana ya uislamu ni swala la kuamrisha mema na kukataza mabaya. Moja ya mambo mema ni kufunga mchana wa Ramadhani, na Moja ya mambo mabaya ni kula mchana wa Ramadhani bila dharura ya kisheria na kwa utaratibu wa kisheria. Mimi nikushauri tu ukasome biblia tu na misali ya waumini na katekasimu takatifu, habari za maandiko ya Sheria na kanuni za uislamu unajitia ujuaji wakati huna ujualo!.
Kwahiyo mmeruhusiwa mkifunga muanze msako kutafuta na kunusa wapi wanapika na kula mchana?upuuzi mtupu imani ni hiyari na hiyari ya shinda utumwa,ndiomana mu watumwa hadi uvumilivu unawashinda na kuamua kujilipua uislamu ni dini ya hovyo sana ,wafuasi wake ni kama wachanganyikiwa ni mazombi wasio jitambua.
 
Naam ngoja nikusome zaidi nione wapi nimechanganya mambo.

naam haswaa.

Naam naam hakika.

Naam hakika ndugu yangu ndivyo ilivyo.

Hapa ndipo shida inapoanzia,na nitakujibu katika nyanja mbili.

1.KiDINI : unapokuwa umefunga alafu mtu akala unamuona basi ELEWA kwamba mtu huyo hakunyimi uhuru wa wewe kuendelea na ibada hiyoo ya kufunga,huo ufahamu haupo katika uisilamu ni madai ya kijinga ya baadhi ya watu wasioelewa mambo.

Ni kama mtu anayefanya ibada ya kusali aseme kwamba ananyimwa uhuru na mtu ambaye amemuona anapita na pikipiki wala hasali,haimake sense

2.KiSHERIA ZA NCHI : wataalamu kadhaa wa sheria wamwfafanua kwamba sheria ama katiba ya zanzibar haijataja jambo hilo kwamba ni kosa,na ndio maana watu wanaohukumiwa wanahukumiwa kwa makosa mengine kama vile ukorofi na uzururaji na sio kula hadharani mchana.

Mmoja ya wanasheria hao ni wakili maarufu zanzibar Ndugu kijogoo alifafanua hivyo,na kama wewe unaona kuna sheria iliyotaja wazi kosa hilo ilete hapa.

Kwanza serikali haijaweka bado hiyo sheria unaposema ni sheria unakuwa unakosea na ndio maana ukienda mahakamani ukaomba data za watu waliohukumiwa kwa kosa la kula mchana wa ramadhani huwezi kukuta hiyo kitu.

Pili andiko langu limelenga KUBAINISHA KWAMBA DINI HAIJAKATAZA MTU ASIYEFUNGA KULA MBELE YA MTU ALIYEFUNGA,hivyo huku unakozunguka kote mkuu ni kwenda kimyume na maudhui yangu.

Jawabu lako sio la kweli kama nilivyotangulia kusema na sababu ni tatu nakuwekea.

1.hakuna sheria iliyitaja kosa hilo.
2.jambo hilo ni kuingilia uhuru wa wengine kwa sababu kula ni jambo lenye kufaa.
3.jawabu lako limeenda kinyume na maudhui yangu yaani umetoka nje ya reli.

Muisilamu ambaye hafungi bila udhuru wowote bila shaka anafanya makosa sio sawa na Allah ndio atamhukumu kwa kosa hilo,

Muisilamu ambaye hafungi bila sababu akila mbele ya mwenzie aliyefunga jua tu kwmaba atakuwa makosani kwa sababu hajafunga na sio kuwa makosani eti kwa sababu tu anakula mbele ya mtu aliyefunga.

Unaposema wote bado unakanganya mambo kwa sababu neno wote ni pana sana kwani hatujui unakusudia wote wa kishia ?
Wote wa kisunni ?
Wote wa kiibadhi ?
Wote wa ki shaairah ?
Wote wa kiahmadiyyah ?

Hivyo basi kauli yako ya wanazuoni wote bado haina mashiko kwa sababu wote unayoisema haipo.

Hakuna mkanganyiko wowote,huo sio mkanganyiko wa uhalisia bali ni sababu iliyotengenezwa tu ili katazo hilo lipite.

Mtu ambaye hajafunga akila mchana haleti mkanganyiko kwa wasiokuwa waisilamu bali ataleta mkanganyiko kwa waisilamu WASIOJIELEWA kwa sababu waisilamu wasiojielewa wao hawajui kwamba kuna watu kwao kula ni ruksa mchana wa ramadhani.

Hekima hii ni feki kwa sababu ipo kinyume na malengo waliyoyakusudia.

Kitendo cha kulazimisha watu wasile hadharani ndio kunaleta dhana mbaya pamoja na sintofahamu kwa wasiokuwa waisilamu.
Na moja ya dhana mbaya zinazoletwa na katazo hili ni kudhani kwamba uisilamu ni dini isiyotoa uhuru kwa wasiokuwa waisilamu na pili watu wasioelewa uisilamu hudhani kwamba uisilamu unalazimisha watu kufanya ambbayo kwao sio wajibu,

Hivyo hekima hiyo iliyokusudiwa inakuwa kinyume chake na sio kama unavyotuaminisha hapa na jambo hilo liko wazi.

Suala la malezi baina yako na mwanao haliingilii uhuru wa watu wengine,watu wengine hawalazimiki kufuata yale unayomfundusha mwanao.

Hata ukiwa unamfundisha mwanao kusali unatakiwa na wewe mzazi ama baba ukasali naye msikitini.
I
Lakini kitendo cha wewe na mwanao kwenda msikitini hakitofanya uwalazimishe wasiokuwa waisilamu nao waende msikitini au wajifungie majumbani eti kisa unamfundisha mwanao kusali,

hiyo ni sababu dhaifu mkuu kwa sababu watu wengine wana uhuru wao ambao hauwezi kuvunjwa kwa kigezo tu kwamba unamfundisha mwanao.

Atautafsiri uisilamu vibaya endapo mtamlazimishe asile mchana mpaka ajifiche wakati yeye halazimiki kwa lolote juu ya mfungo huu.

Umeeleweka ila haujakubalika hoja zako ndio msana mimi mtoa uzi nakujibu nukta baada ya nukta.

Jitihada za wanazuoni hazina nafasi katika Dini ya Allah ambayo imekamilika,wanachuoni hawana nafasi ys kuharamisha jambo ambalo Allah kanyamazia hakubainisha uharamu wake.

Rejea hadithi ya mtume ambayo mtume alifikia kusema...

".. وسكت عن أشياء رحمة لكم فلا تبحثوا عنها
.."Mungu amenyamazia baadhi ya mambo ili iwe rahma kwenu,basi msichunguzechunguze.."

Wanachuoni hawatakiwi kuharamisha mambo ambayo Allah ameyanyamazia kwani Allah hakuona ?
Au uisilamu haukukamilika ndio maana tunahitaji jitihada za wanazuoni ?


Asili kila ambacho hakikutajwa uharamu wake basi ni halali.

Hivyo maadamu sikuharamishiwa kuweka nguo mbele yangu basi ni halali kwangu kuweka.

Elewa hiyo kanuni kwamba vitu vyote kwa asili ni halali,pale inapokuja dalili ya kuharamisha ndio kinakuwa haramu.


Hivyo usiniulize kwa nini naendesha gari wapi limetajwa kwamba uendeshe katika hadithi , jawabu langu ni rahisi kwamba hakuna aya au hadithi imeharamisha jambo hilo ndio maana tunachagua cha kufanya.

Elewa hii kanuni "الأصل في الأشياء الإباحة

Asili katika vitu ni kujuzu kufanyika kwake endapo haijsjs dalili ya kuharamisha.
Sawa, ubarikiwe sana kiongozi!
 
Hivi ninyi mna ubongo kweli ? Hata amri za KUFUNGA hoteli mchana ni za hovyo kabisa. Mungu gani huyu mnayemwabudu?
Mungu anaelazimisha kumuabudu kwa Mitutu Mabomu Sime Majambia Mijeledi Kufungwa Jela na Mashinikizo mengine huyo sio Mungu.
 
Hivi Hawa wanzanzibari mbona wanajikuta wao ndo watu Bora Sana kuliko wengine? Binafsi sioni Kama ni sahihi kukataza watu wasile hadharani eti kwa kuwa ni mfungo ilhali kula ni hitaji la msingi la binadam na si hanasa.
Nnachojua Mimi wanzanzibari ni washamba na limbukeni wa dini, na hata hao wanaotetea unyanyasaji wa namna hiyo kwa wasio kuwa waislam hata huo uislam wenyew hawaujui zaid ya kukalili Quran kuliko kuielewa, nje na hapo Mimi naona wanachokifanya ni zaid ya utoto na kutojielewa.
 
Wandanganye wavivu wa kusoma kama wewe
Haya ngoja tuone nani ni mvivu,ni bora niwe mvivu wa kusoma kuliko kuwa mvivu wa kuelewa.
eti andiko halijaonekana.
Sijaona,huwenda lipo kama unavyoashiria ila mimi sijaona kwa kweli,kama wewe unalo andiko ambalo ni khaaswa. limekuja kukemea jambo hilo utuwekee.

Usije ukanijia na andiko ambalo ni la ujumla (aaamu) kwa sababu maandiko ha ujumla yapo mengi yakiashiria kutokataza jambo hilo.
Sio kila ambacho hujaona kuwa maana yake hakipo
Na pia vipo ambavyo sijaviona na havipo kweli.
Saa nyingine hujaona kwa sababu wewe ni kipofu au huoni vizuri.
Na saa nyingine sioni kwa sababu ni kweli havipo.
Nini maana ya kuamrisha mema na kukataza mabaya
Hii ni dalili aaamu (العام) yaani unatumia dalili ya ujumla badala ya kutuletea dalili maalumu (الخاص) iliyokuja kuharamisha jambo hilo kwa kulitaja haswa kwani Mungu hasahau.

Kwa sababu uisilamu umebainisha kwamba "HAKUNA KULAZIMISHANA KWENYE DINI"

Nini maana ya kuamrisha mema na kukataza mabaya
Nami nikuulize nini maana ya HAKUNA KULAZIMISHANA KWENYE DINI ?

nini maana ya "ALLAH HAJAKUKATAZENI KUISHI KWA WEMA NA WALE AMBAO HAWAWAPIGENI VITA ?"

unadhani wema ni kumkataza asile mchana kama kawaida yake mpska akajifiche uchochoroni,huo ndio wema ?


Ikiwa Allaah kuamrisha watu wasile mchana wa Ramadhani yule anayekula mchana kfanya jambo baya.
Allah ameamrisha watu wasali muda ukifika,je WEWE HUWA UNAWAFUNGIA NDANI WASIOKUWA WAISILAMU WASITEMBEE MUDA WA SALA ?

AMA UNAWAINGIZA MSIKITINI KWA LAZIMA WASIOKUWA WAISILAMU MUDA AMBAO WAISILAMU WANASALI ?

Je ULIPATA KUSIKIA MTUME KAWAFANYIA HIVYO WASIOKUWA WAISILAMU MUDA WA SALA UKIFIKA ?


Mwenye kuona jambo baya na alizuie kwa mkono wake, na Kama hawezi alikataze kwa ulimi wake , na kama hawezi na alichukie kwa moto wake".
Mtume hakuwalazimisha wasiokuwa waisilamu kusali katika misikiti,na kutokusali ni jambo baya,je Mtume hakukataza mabaya ambayo aliyaona ya wasiokuwa waisilamu kuacha kusali ?
Kwa ujumla mimi nasema Zanzibar ina taratibu zake ambazo ni nje ya mambo ya muungano na lazima ziheshimiwe.
Mimi nimesema sijaona kwende uisilamu na wala sijasema kwamba sijaona zanzibar,habari ya zanzibar umeiweks wewe,mimi nimegusia kwanza katika uisilamu.,hao wa zanizibar watajua wenyewe.
 
Huyu Qadian
Haya ni madai hewa tu ambayo hayaathiri chochote kwangu.
kazi yake ni kupinga kila waislamu wana chofanya
Kama wewe kazi yako ni kusapoti kila waisilamu wanachofanya mpaka wakifanya ushoga unasapoti sawa.

Kama wewe unasapoti kila wanachofanya waisilamu mpaka wakilawiti watoto katika madrasa sawa.

Kama wewe kazi yako ni kusapoti kila wanachofanya waisilamu mpaka wakiwa wanazini na kutiana mimba sawa.

Mimi huo sio uisilamu wangu,mimi ni muisilamu nninayeangalia uisilamu umesema nini kwa hakika juu ya jambo hilo,kama utaniona kafiri ama kadiani ni sawa tu kwa sababu ninachojali ni je Allah atanionaje.
kwa ufupi sio waislamu ni makaafiri
Nyie ndio waisilamu mnaotegemewa kuusogeza mbele uisislamu kwa kuwakufurisha wale ambao mnatofautiana nao mitazamo ?😆.

Kufanya takfiir kwa muisilamu ni katika madhambi ambayo mtume anasema kama mtu hana ukafiri uliomrembea basi unakurudia wewe.

Allah ndie mjuzi
 
Ni sheria za nchi husika
Kula, Kutafuna, Kunywa maji kwenye mazoezi, au kula mchana hadharani wakati wa Ramadhani ni uhalifu katika nchi za kiarabu UAE.

Wakati wa Ramadhani, hairuhusiwi kula, kunywa au kuvuta hadharani nyakati za mchana

Adhabu kwa mtu anayeonekana kukiuka sheria inaweza kuwa kifungo cha hadi mwezi mmoja, au faini ya Dirham 2,000.
Nilivyomuelewa mtoa mada ni andiko kutoka kwenye Quran siyo katazo la binadamu.

Kama quran ni maneno ya Allah kwa nini inapingwa kwenye eneo hilo ambalo haijasema chochote?.
 
Back
Top Bottom