Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,710
- 9,063
Wakuu salamu kwenu. Siku nyingi sijaandika ila leo nitauliza swali dogo tu.
CHADEMA wanasema hawajapeleka majina NEC lakini wabunge wameapishwa juzi. Baada ya uapisho na CHADEMA kupitia kwa Katibu Mkuu kuwakana wabunge wale sijasikia kituo cha redio, televisheni au gazeti zikiwahoji wahusika upande wa NEC na Bunge.
Hivi kweli tuna vyombo ya habari?
cc Mshana Jr Mwanahabari Huru Pascal Mayalla na wengine nisaidieni mawazo
Waandishi wanaogopa sana yale yalomkuta Azory Gwanda wa Mwananchi na Mwaibalile wa CH-10