Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
1/6 inaitwa SuduthiSi kweli mjomba, Theluthi kubwa kuliko Robo.
1/3 > 1/4... Ama 0.667 > 0.25 ukiiweka kwenye desimali.
Kama ulimaanisha 1/6 ama 1/8 moja wapo katika hizi inaitwa Sumuni. Sikumbuki vizuri ni ipi kati ya hizo mbili ndio huitwa Sumuni ila hizo ndio ndogo kuliko robo i.e 1/4.
Kwa kifupi tu thaman iliyo ndogo kuliko robo ni kuanzia yenye kigawo kikubwa kuliko 4 ambayo ni 5 na kuendelea tukiwa na maana ya 1/5, 1/6, 1/7 en so sooo ila sio zenye thaman ndogo kuliko 4 kama 3 na 2 napo tukiwa na maana ya 1/3 (theluthi), 1/2 (nusu).
Mkuu kumbe O-Level ulisoma seminary?Labda kwavile nilipita seminary [emoji28][emoji28][emoji28]
Bora uliogopea mbali Maana ungepigwa "Zongo"Yule nilitemana nae mazima mkuu [emoji28][emoji28]
hapa unaachiwa msala bila shaka,13th Portion:
... Sikuwa na kitu nilichoweza kufanya kwa wakati ule. Hata kama ningesema nimbembeleze, still isingefanya kazi, maana sijui dhamira yake halisi ni ipi.
Sikutaka hata kulala pale. Nikaamua kurudi gheto kwangu, PS4 yake nikamuacha nayo.
Njia nzima kichwa kimezongwa na mawazo hasa juu ya yale mazungumzo na yule Mzee. Kuna muda unaweza ukawa umezungukwa na watu wengi, alaf wasiwe na faida, na wale wachache wenye faida pia usiweze kuwatambua. Kutwa nalalamika maisha magumu, michongo hakuna, alaf watu wenye uwezo wa kunipa michongo ndio nawapotezea, Kisha nakumbatia wasio na umuhimu.
Usingizi ulinipaa kabisa. Niliwaza mengi sana, kiasi kwamba nikajikuta namtumia msg yule Mzee kuomba kuonana nae tena siku inayofuata. Sikutegemea anijibu muda ule ule, maana ilikuwa ni karibia saa nane kasoro. Niliendelea kuwaza mambo tofauti tofauti mpaka nilipopitiwa na usingizi.
***** ****** ****** ******
Asubuhi niliamshwa na mlio wa simu yangu, iliyokuwa ikiita. Kuiangalia nakuta Mshua ndio anapiga. Sijui kwanini, ila nilishtuka sana. Nikajikuta naogopa kuipokea ile simu, maana najiuliza anataka kuniambia nini?. Yule Mzee amemwambia kama tumeonana? Au nikipokea nitaweza kuongea na comfortable?. Ushawahi kufanya jambo fulani la aibu sana, alafu ukutane na mtu au watu wanaolifahamu, huwa unapoteza ule uchangamfu mbele yao. Hata katika story utakazopiga nao, wakicheka utahisi wanakucheka ile aibu yako. Hiyo hali ndio nilikuwa najihisi muda huo wakati Mshua anapiga. Kwa mara ya kwanza nikashindwa kupokea simu ya Mshua. Ikaita hadi ikakata.
Nikiwa bado nipo pale pale kitandani, simu ikaanza kuita tena. Nilishtuka kana kwamba nimepigwa shoti ya umeme. Nilishusha pumzi za amani baada ya kuona jina la mpigaji. Ni yule Mzee ndio alikuwa ananipigia. Niliipokea, tukaongea mambo kadhaa, ila akaniambia Kwa hiyo siku hatokuwa na nafasi, lakini pia hata siku zinazofata, bado angekuwa busy. Hivyo akashauri kama alivyoniambia jana, kuwa wik end ndio ratiba yake inakuwa wazi. Tukakubaliana niende tena kule kule shambani kwake, siku ya jumamosi.
Baada ya kukata simu, mawazo yakanirudia tena. Picha ikanijia, ni Kwa namna gani masaa 24 yanaweza kubadili kila kitu. Maana ni ndani ya masaa 24, kutoka kuwa mtu anayeongea na Baba yake kwa vicheko na bashasha, hadi kuanza kumuogopa.
Baada ya masaa kadhaa ya kujivuta vuta pale kitandani, nikaanza kutafakari siku yangu niipeleke vipi. Unajua tatizo la kuwa jobless, ni kwamba unakuwa na muda mwingi sana, ila vitu vya maana vya kufanya ndio hakuna.
Baada ya kuwaza sana, nikaona ngoja niende kule maeneo ya katikati ya jiji, nikamtafute Mzee Dingi. Jamaa alitembea na karibia million 15, huku pakiwa na karibia million 6 ya kina Kisauti, ambayo hakuitolea jasho kabisa. Mawazo yakaniambia nimtafute walau nipate mgao wangu, maana tayari nishatumikia adhabu.
Nikasogea hadi maeneo ya Samora, ila hakuwepo. Nikatembelea vijiwe vyake vyote ila nikaambulia patupu, sielewi nampatia wapi. Kwenye simu bado kaniblock. Nikafikiria kwenda kwa Shani, ila nikaona tutaenda kulumbana, alaf ugomvi uzidi kuwa mkubwa. Nikajaribu kumpigia yule mpenzi wangu, nikakuta bado kaniblock. Nikaamua kurudi zangu home.
** * ***
Zilipita kama siku mbili hivi, Mzee Dingi akanipigia simu.
Mzee Dingi: "Uko wapi Apostle?"
Analyse: "Nipo gheto, vipi?"
Mzee Dingi: "Najua bado una hasira, ila wanaume hatuwekagi vinyongo, njoo tufanye kazi"
Analyse: "Nyie fanyeni tu mtajirike, Mimi Sina mpango na hizo kazi zenu"
Mzee Dingi: "Dogo mambo hayaendi hivyo, hakuna tuzo kwa ajili ya watu wanaopata hela kwa shida. Kazi zipo nyingi, utapata hela, na utasahau habari ya ilo deni unalonidai"
Analyse: "Siwezi fanya kazi alaf nimfaidishe mtu mwingine, nyie fanyeni tu ambao mnawezana"
Mzee Dingi: "Ile ilitokea tu, kwasababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. Safari hii tutakuwa mguu kwa mguu apostle"
Nikajifikiria kwa muda kidogo, nafsi ikawa mguu nje mguu ndani, Sina mchongo town, bills nitazilipa vipi?
Nikamuuliza, "Kuna dili gani sasa hivi?"
Mzee Dingi: "Hayo sio mambo yakuongelea kwenye simu, kesho njoo ofisini tujadiliane kwa kina"
Analyse: "Sina nauli, kama hatuwezi kuongea kwenye simu, Mimi siji"
Hakunijibu kitu, akakata simu. Alafu baada ya kama dakika tatu, ikaingia elfu sabini kwenye tigopesa toka kwa Mzee Dingi, Kisha akaniandikia msg.
"Kesho fanya juu chini uje Apostle. Usiende makao makuu, njoo tawi la kinondoni"
Nikamjibu "Poa"
Unajua kupambana kunaumiza, ila kukata tamaa kunaumiza zaidi. Maana aliyekata tamaa hana dira, anaweza kujikuta anafanya mambo ambayo hakuwahi kutarajia. Story na yule Mzee zilinifanya nikajiona hopeless sana. Nikajikuta nimeridhia kwa moyo mmoja kujiunga na kina Mzee Dingi.
. ***** ***** ***** ******
Kesho yake nikatimba pande za Kino, nikakuta timu ya watu watatu, Mzee Dingi akafanya utambulisho. Nikajiunga nao rasmi.
Tulijadili mipango kadhaa, na tokea siku ile tukaanza kupiga dili kulingana na zinavyokuja. Siwezi elezea in details ni kwanma gani tulikuwa tunafanikisha hizo deals, ni watu gani tuliwapiga au hata kuyataja hayo madili, maana sio lengo la story lakini pia huwezi jua nani anasoma, nisijekuamsha hasira zilizolala.
Tulikuwa tunahama vijiwe kadiri tunavyopiga dili, ili kuepuka kukutana na wale tunaowapiga. Wengi tuliokuwa tunawapiga, michongo yote ilikuwa based on coincidences, ndio maana baada ya kuspend time sana na kina Mzee Dingi, I will never ever believe in coincidence, NEVER.
Baada ya kama miezi miwili au mitatu, Mzee Dingi akaniomba tukutane wawili tu, Mimi na yeye. Tulikutana baa maeneo ya buguruni.
Mzee Dingi: "Apostle kuna mtu anataka kukutana na wewe. Kuna dili limejitokeza"
Analyse: "Ni nani huyo? Na kwanini atake kukutana na Mimi?"atake
Mzee Dingi: "Huyu mtu shoo zake sio ndogo ndogo Apostle. Dili zake zote ni mikia ya kondoo"
Analyse: "Mikia ya kondoo kivipi?"
Mzee Dingi: "Huyu kwa mwaka akipiga dili nyingi ni nne, ila mkwanja unaopatikana hapo, unaweza kwenda likizo muda mrefu, tena kwa mtoto kama wewe, unaweza Kaa hata mwaka bila stress ya kipato, ni matumizi tu"
Analyse: "Duh anaitwa nani huyo Mzee?"
Mzee Dingi: "Jina lake la kazi tunamuita Kesho Yetu"
Analyse: "Kwanini sasa anataka kuonana na Mimi?"
Mzee Dingi: "Wewe fanya mpango kesho tuonane nae pale Kinondoni, kuna dili analeta, linahitaji watu kadhaa, na wewe ametaka uwepo"
Analyse: "Ananijua kwani?"
Mzee Dingi: " Ndio anakujua, ameona kazi kadhaa ulizoshiriki, uchangamfu na usharp wako ndio anautaka"
Nikaguna pale, ila mwisho wa siku tukakubaliana, kesho yake tukutane pale Kino...
***** ****** ****** *****
Kesho yake asubuhi na mapema nikatimba Kinondoni Manyanya. Nikamcheki Mzee Dingi, akanielekeza walipokuwa wamekaa. Yupo yeye, mwanasheria feki, na Mzee mwingine ambae ndio ilikuwa mara ya kwanza namuona, kwa jina la kazi alikuwa anafahamika kama Kidevu.
Kitu kingine nilichonote, hawa jamaa wote hakuna aliyekuwa anafahamika kwa jina lake halisi. Na hiyo ndio sababu ilifanya Mimi niwaache waendelee kuniita apostle. Na kingine hakuna aliyekuwa anajulikana anapokaa. Kiufupi, ingetokea mmoja akakamatwa, angeishia kutaja majina ya apostle, Mzee Dingi, Kidevu au Kesho Yetu. Akiambiwa akaoneshe wanapokaa hao watu, wangezunguka Dar nzima.
Baada ya utambulisho. Mchongo mzima ukawekwa mezani. Kulikuwa na mwalim mstaafu ametoka kuchukua mafao yake. Yule mwalim alikuwa anahitaji eneo kubwa kwa ajili ya mradi wake wa green house aliotaka kuuanzisha. Lakini pia, alikuwa anahitaji vifaa kwa ajili ya umwagiliaji, na kuchimbiwa kisima kwenye ilo eneo atakalo nunua. Sasa mpango ilikuwa apigwe kwenye eneo, alafu dili likisha kamilika, apigwe kwenye vifaa na uchimbaji.
Mzee Dingi yeye alitakiwa kucheza kama dalali wa eneo linalouzwa, mwanasheria feki na yule Mzee Kidevu, wao wawe majirani, Mimi nikaambiwa niwe kama afisa mtendaji au mwenyekiti wa kile Kijiji. Mzee Dingi ananiambia:
"Wewe apostle inabidi uwe mtendaji wa kile Kijiji. Unajua watendaji wengi ni vijana na wasomi. Ni rahisi yule Mama kuamini"
Nikabaki na mwangalia tu. Akaendelea
"Yule Mama tukishamaliza kuuziana nae kiwanja, itabidi hapo hapo wewe (Mimi) kama mtendaji umwambie unaweza kumsaidia kutafuta kampuni ya uchimbaji visima, na kuweka set up nzima ya kila kitu kwa ajili ya project yake".
"Yani inabidi tukimaliza tu kulipana hela za kiwanja, malipo ya hizo process zingine yafatie. Kuna watu tutakuunganisha nao ambao ndio utaendelea nao kwenye hiyo nngwe ya pili"
Wakati tunaendelea kuongea pale. Kuna Mzee mwingine akaja, yuko smart, kabeba begi muundo wa briefcase au zile za kubebea laptop. Yule Mzee sidhani kama kuna mhuri ambao hana. Kibriefcase chake Kiko full, mihuri, Karatasi, Calculator nk. Akatoa mihuri kadhaa akaiweka mezani. Eneo ambalo alitakiwa akauziwe yule mstaafu, lilikuwa vigwaza. Huyu Mzee smart aliyeongezeka, ndio Mzee Dingi akanitambulisha kwake kama 'Kesho Yetu'. Huyu ndio alikuwa mastermind wa huu mchongo wote, na ndiye aliyetakiwa kuact kama muuzaji wa eneo. Na Kwa mujibu wao, tulitarajia kati ya million 50 mpaka 70, kutegemeana na namna tutakavyofatisha maelekezo ya Mzee Kesho Yetu.
Kila kitu kikawekwa sawa, then yule mstaafu akapigiwa simu, na makubaliano yakafikiwa kuwa kesho akalione lile eneo.
Unajua sometime unaweza Sikia story mtu katapeliwa,alafu ukaanza kumcheka na kumuona mjinga, ila huyu Mzee Kesho Yetu alinibadilisha mtazamo wangu. Mtu akitapeliwa, usimlaumu sana, peleka sifa kwa yule aliyemtapeli. Watu wana mahesabu makali sana, jinsi huyu Mzee Kesho Yetu alivyokuwa anapanga mambo, accuracy yake ni almost 100%. Kinachotakiwa ni kufatisha maelekezo yake tu.
Na hata dili nyingi ndogo ndogo tulizokuwa tunafanya na kina Mzee Dingi, zilikuwa zinatoka kwake zikiwa na full deatils ya kuzipush. Yeye alikuwa anapewa percent fulani ya mgao, alikuwa hashiriki. Ukiona kashiriki, basi ilo dili liko very serious, na target sio chini ya million 50. Na hata hii deal nilidhani usharp na usmart wangu ndio ulifanya anielewe na kuniunganisha kama jinsi Mzee Dingi alivyoniambia, lakin kumbe alikuwa na sababu ya tofauti kabisa. Kitu ambacho sikuwahi kukifikiria kabisa, ila yeye kwa upande wake alishakifikiria miezi mingi iliyopita. Na jibu alilipata ni "Apostle". Nilikuwa funguo yake bila hata ya Mimi mwenyewe kujua.
Tulivyoagana, wakati wengine washaanza kuondoka, nikamsimamisha Mzee Dingi.
Analyse: "Mzee hii deal inahusisha sura ngeni nyingi, na pia hela yake ni ndefu, kuna kila dalili ya kudhurumiwa hapa"
Mzee Dingi: "Apostle unaongea nini wewe?. Hakuna wa kukudhurumu hapa"
Nikamsikiliza tu, lakini sikuwa na amani kabisa.
Tukaagana nikaamsha. Mida ya jioni jioni, Mzee Dingi akaniwekea laki mbili kwenye simu. Kisha akanipigia
Mzee Dingi: "Apostle najua utakuwa na uhitaji wa hela, chukua hiyo, piga ua kesho inabidi utokee"
Analyse: "Tunakutania wapi?"
Mzee Dingi: "Wewe na wale wengine mtatangulia asubuhi sana. Mimi nitakuja na yule mlengwa baadae."
Analyse: "Poa poa"
Mzee Dingi: "Maelezo ya ziada utayapata kule kule, hakikisha unakuwa smart sana, usisahau begi lako"
Analyse: "Sawa nimeelewa "
Alivyokata simu tu, Shani akanipigia
Shani: "Uko wapi we Mtu?"
Analyse: "Nipo gheto tu"
Shani: "Naona umenisusa tokea siku ile. Mimi nishakumiss"
Analyse: "Me nipo"
Shani: "Unaweza kuja kwangu muda huu? "
Analyse: "Poa nakuja"
Shani: "Ndio maana nakupenda, huwekagi vitu rohoni. Haya njoo nakusubiri"
Nikaenda kuoga, ili niende.. ..
Khakhakhaa..mshua anampenda mkewe kwamba tangu wakuzae wewe ndio umekua kivuruge wao!?11th Portion:
... Kabla sijamfata nje, nikahakikisha kwanza kama milango Iko wazi au kama kaacha kamfungia Bi Mkubwa kwa nje. Nilivyokuta Iko wazi, ndio nikamfata.
Tofauti na matarajio yangu, kule nje Mshua alikuwa mpole sana kuliko kawaida yake. Na alikuwa anaongea kama mtu ambae mawazo yake yapo mbali sana.
Mshua: "Hivi unajua Mimi na yako ndoa yetu inamuda gani?
Analyse: "Nahisi kama thelathin naaa hivi"
Mshua: "Unahisi sio?". Sasa sikiliza, nilianza mahusiano na Mama yako mwaka 75, ila nilikuja kufunga nae ndoa mwaka 82. Katika kipindi icho chote tulikuwa na furaha sana. Na hata baada ya kufunga ndoa furaha na upendo viliongezeka pia. Katika kipindi chote icho, ugomvi serious ambao ulishawahi kutokea kati yetu, ilikuwa ni mara moja, mengine ni ya kawaida tu"
Nikabaki namwangalia tu, bila kumkatisha. Akaendelea "Ila tokea umezaliwa wewe, ugomvi kati yetu imekuwa kitu cha Kawaida sana. Kwanza sasa hivi Mimi sio priority tena kwa mke wangu, hasa wewe ukiwepo hapa nyumbani"
Nikajikuta nataka kucheka, yani Mshua na umri ule bado analia wivu?. Akaniwahi "Cheka uone nini kitafatia". Nikajibana, ila yeye ndio akajikuta anacheka 😅😅.
Akaniambia sikia "Nakukumbusha kuwa wewe sio last born, na Safari hii ukiondoka hapa usirudi tena bila mke. Yani wewe yeyote tu njoo nae Mimi kama baba nitampokea". Nikabaki nimeshangaa, Mzee Vipi?
Akaendelea "Ili kulegeza bond ya wewe na Mama yako, inabidi na wewe uoe, swala la utamuoa nani, utajua mwenyewe"
"Pia kitu kingine cha muhimu, unamkumbuka yule Mzee niliyekupaga namba yake?". Nikamjibu ndio, "Ukifika mjini, safari hii fanya juu chini uonane nae". Nikamjibu hakuna shida nitafanya hivyo.
Tukaongea mambo mengine tofauti tofauti ya kiutafutaji. Wakati tunahitimisha, ili turudi ndani maana Bi Mkubwa alituita tukale, Mshua akanisisitiza tena "Ukijiona unataka kurudi huku bila mke, basi uishie center, nitakufata tuongelee huko huko, na hakuna kumwambia Mama yako kuwa unakuja. Ila ukijitoa akili ukaja mpaka huku kijijini bila mke, basi jua lazima nikuozeshe binti yeyote wa hapa kijijini, swala la kumpenda, utampenda mbele ya safari ukishamzoea. Na ni lazima uondoke nae". Kumbe Bi Mkubwa alikuwa kasimama dirishani, haya maongezi ya mwisho mwisho akayasikia, nae akatoka nje "Kumbe ndio maana mmekuja kujificha, hayo ndio maongezi yenyewe?. Kama wewe ulitafutiwa mke, hizo ni enzi zenu, sio zama hizi. Mwanangu hachaguliwi mke, mwanangu oa ukiwa tayari, na ukiwa na mwanamke utakayemtaka, wala hakuna presha."
Hii kauli ya Bi Mkubwa nikawa sijaielewa, anamaanisha Mshua alitafutiwa mke?. Sikutaka inipite, ikabidi niulize. "Kumbe Baba alitafutiwa mke?". Mama akataka kujibu, ila Mshua akamuwahi na kunijibu "Achana nae, hajui anachokiongea huyo.
Mama (akacheka kidogo): "Kwamba sijui ninachokiongea?. Kumbe wanao hawajui story yako? (Akacheka tena)"
Analyse: "Story gani hiyo?. Baba siumetoka kuniambia umejuana na Mama tokea miaka ya 70, ukamuoa miaka ya 80?. Kuna story tofauti na hiyo?". Mama akawa anacheka tu.
Mshua: "Kwani mtu akituma mshenga, hapo anakuwa katafutiwa mke?. Huyu mama ako haelewi mambo yanavyoenda". Akamalizia kwa kicheko.
Ila kila Bi Mkubwa alipokuwa anataka kuongea, Mshua anamcrash as if anazuia asiongee. Nikajaribu kum-probe Bi Mkubwa walau anipe hiyo story ila akaishia kucheka.
Mama: "Atakuambia mwenyewe huyo, ila Cha msingi oa mwanamke utakayemtaka wala asikulazimishe"
Mshua: "Si alikuja na yule rafiki yangu, nusura ufe kwa kihoro hapa ukijua ndio mka mwana 😅😅😅"
Bi Mkubwa akamkata jicho bila kusema kitu, alaf akanigeukia Mimi, "Sema na wewe usije kutuletea kizaa zaa kama cha yule wa kipindi kile"
Nikaishia kutabasam tu, Kisha tukaingia ndani kula.
******** ****** ******* ***** *******
Baada ya siku mbili nikaondoka pale nyumbani. Kufika town, ramani zote hazisomeki. Nikamcheki yule Mzee, baada ya kunitambua tukaongea mawili matatu. Akaulizia kuhusu afya yangu, then tukaweka appointment nikaonanae mwishoni mwa wiki. Akanielekeza maeno ya Kongowe, kuna sehemu unapanda milimani, Mlamleni kwa mbele mbele huko. Sikuwa nimewahi kufika maeneo yale, ila nikasema itabidi niende.
Ilivyofika siku tuliyokubaliana. Wakati nipo njiani, akanipigia simu. Baada ya salamu akaniuliza,
Mzee: "Vipi umeshaanza safari ya kuja huku?"
Analyse: "Ndio Mzee"
Mzee: "Ukifika Kongowe mwisho, subiria hapo, kuna kijana wangu yupo njiani nae anakuja huku. Yupo na gari, mtakuja wote"
Analyse: "Sawa Mzee"
Nikafika mpaka pale, nikasubiria. Muda kidogo napigiwa simu, baada ya kuongea nae ndio nikajua ni huyo kijana ninayetakiwa kwenda nae. Nikasogea hadi alipopaki gari, then safari ikaanza. Njiani no story, hadi tunafika.
Kufika, ni eneo fulani kubwa, pia lina uzio. Ila kwa ndani sehemu kubwa Iko wazi, kuna mabanda mengi ya mifugo na nyumba moja ya kuishi watu, ambayo imejitenga kiasi chake.
Tukapokelewa na mlinzi. Baada ya muda kidogo, yule Mzee ndio akaja. Tokea nimeanza kuwasiliana nae, kwa mara ya kwanza hiyo ndio siku tulikuwa tunaonana. Nilishtuka kumuona, japo hiyo siku ndio ilikuwa tunakutana ana kwa ana, ila sura yake haikuwa ngeni kwangu, ni mtu ambae sura yake iko very popular. Alishawahi kuhudumu nyazfa kadhaa kwenye serikali, awamu za nyuma kabla ya Ngosha.
Ni mtu ambae najua tunatokea nae mkoa mmoja, ila sikuwahi jua kama anafahamiana na Mshua. Na hata Mshua siku zote anavyoniambiaga nikaonane nae, hakuwahi niambia huyo mtu ni nani haswa.
Yule Mzee kaniambia nimsubirie amalizie kuangalia mifugo yake na kuweka mambo sawa, kisha tutaongea. Na kweli baada ya kama dakika 45, akaniambia tuongozane kuelekea kwenye ile nyumba iliyojitenga. Lakini kabla hatujaifikia, akabadili mawazo, akamuagiza mmoja wa vijana waliokuwepo pale atuletee vitu, then tukaenda kukaa chini ya mti.
Wakati tunaweka viti vizuri ili tukae, akaniambia
Mzee: "Mbona kama umeshangaa kuniona Mimi, ulitarajia kukutana na nani?
Analyse: "Hapana sio hivyo Mzee, ni vile sikutarajia kukutana na sura ninayoifahamu"
Mzee: "Haya niambie ushawahi kuiona wapi hii sura unayosema unaifahamu?"
Sikujibu kitu, nikaishia kutabasam tu kama namna ya kuzuga.
Mzee: "Inaonekana uko busy sana"
Analyse: "Hapana Mzee"
Mzee: "Kwanini hukunitafuta kipindi chote icho, mpaka ile juzi ulivyo nipigia?."
Nikakosa utetezi.
Akaendelea
Mzee: "Kipindi kile tunawasiliana kwa mara ya kwanza, ndio nilikuwa kwenye mchakato wa kustaaf. Kwasasa nimstaafu, nakujaga kupoteza muda na mifugo huku"
Analyse: "Ni jambo zuri, ukisema ukae tu, mwili utashambuliwa sana na maradhi"
Mzee: "Ni kweli, maana umri huu hakuna tena kash kash"
Tuliongea vitu kadhaa, ambavyo ni kama tulikuwa tunajenga msingi wa dhumuni lililofanya tuwe pale. Baada ya hizo story za hapa na pale kuisha, tukaenda kwenye dhumuni sasa. Maongezi ambayo mpaka leo natamani nisingeyasikia au kuyajua. Ni maongezi ambayo kila nikiyafikiria, huwa naishia kujifyonya mwenyewe.
Maongezi ambayo yalifanyika kwa masaa machache ila yamekuwa yakiniumiza kwa muda mrefu.
Kiufupi, ni maongezi ambayo yananifanya najilaumu kila iitwayo leo......
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Nina imani hii paragraph imetugusa wengi wetu humu na tumelichukua kama somo kama ilivyomtokea ndugu yetu Analyse . Mzee ametugusa wengi sana kwa hekima zake.Mmekuwa kama mbwa, anayeweza kwenda umbali mrefu sana kufata jike, ila siku akija mwizi nyumbani, atamfukuza mpaka hatua chache kutoka nyumbani, kisha atamuacha. Vya maana hamvipi uzito, ila visivyo na msingi mnavifanya kwa umakini"
sio kwa punch za mzee hizi lol!!
Familia ikipata emergency unaweza toa milioni 5 za ghafla??
📌📌📌📌📌📌📌📌📌📌📌📌📌
Nimeanza kusoma
[emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]“Naam jembe langu"