Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Halafu kumbe portion 5 ulishatuma duh ndio nashangaa hapa naona portion 6 jf sijui wanakwama wapi kwenye notifications mara zinakuja mara haziji lol ngoja niue zote kwa mpigo Santo sana!!
Mbona nilikutag mrembo? Itakuwa notification ndio hazikuja
 
5th Portion:

.... Akili yangu faster ikaniambia, hapa nitakuwa nimeleta mchepuko wa Mshua home, ndio maana Mama kazimia alipouona. Nikajisemea,
Kipindi hayo yanaendelea, Mshua alikuwa anaongea na yule bi mkubwa niliyekuja kuja nae. Maongezi yao yalikuwa ya kawaida tu, lakini kila nikijaribu kumsoma Mshua kuona kama ana wasiwasi,

***** ****** ******** ******* *******

Maisha yaliendelea vizuri pale nyumbani, likizo ilivyo karibia kuisha, nikaondoka.

Siku zikaenda, hatimae masomo yakafikia tamati. Nilipofanikisha kumaliza chuo, kabla ya graduation, Mzee akawa ameniita home. Siku niliyofika, hatukuongea mambo mengi, ila baada ya siku 3 ndio akaniweka kikao. Tukaongea mengi sana kuhusu maisha. Mwisho wa siku akaniambia "Ukirudi tena mjini, kuna mtu nataka ukaonane nae". Nikamuuliza ni nani? Akajibu "usijali, nitakupa namba yake, na namna ya kumpata. Anaweza kukusaidia maisha yako baada ya chuo". Nikamuitikia sawa. Lakini kimoyo moyo sometime nilikuwa namind, maana kama kunipa namba yake ya simu na hizo taarifa zake, angeweza kunipa hata kwa njia ya simu nikiwa Dar.

Nilivyotaka kurudi Dar, alinipa ile namba ya huyo mtu, Kisha akaniambia mengine nitayapata nikishaongea nae, maana anatarajia simu yangu. Nikarudi zangu mjini.

Baada ya kama siku tatu tokea nMtu kama simu hapokei, ukienda kwake siutaishia getini?. Nikaamua kumpigia simu siku hiyo hiyo, ili kama kesho nitaenda, basi awe anautarajia ujio wangu. Nilivyopiga, simu ikaita kidogo, alaf ikakatwa. Akanitumia msg "Nipo kwenye ambae nilikuwa nae kwenye hayo mahusiano kwa wakati huo, kila nikimwambia issue ya kumtambulisha nyumbani, anasita sita. Kwamba tusubirie kidogo, mara tuzae
Analyse: "Nisubirie nini tena Mama? Hutaki kuitwa mkwe?"
Mama: "Nataka sana mwanangu, tena kati ya wanangu ambao natamani kushuhudia harusi yao ni wewe mwanangu"
Analyse: "Basi niruhusuni nimlete mumfahamu Mama"
Mama: "Kusema ukweli naogopa mwanangu. Naogopa sana sijui utaniletea mwanamke wa aina gani, maana kuna muda akili zako unazijua mwenyewe. Hata ile siku niliyopatwa na mshtuko, akili yangu iliniambia yule mwanamke uliyeongozana nae ndio umekuja kumtambulisha"

Nilichoka. Nikajikuta nimekaa kimya kwa muda, nisijue cha kusema. Kumbe ile ndio sababu ya Mama kupata mshtuko?. Yani familia zingine wakisikia watoto wao wanataka kuoa inakuwa furaha, kwa upande wangu naleta wasi wasi? Vijana wenzangu wakiongozana na wamama, wakawasaidia mizigo, wanaonekana vijana wa heshima, Mimi Mama yangu kuniona nimeongozana na mmama, kapatwa hadi namshtuko? ๐Ÿคฆ๐Ÿคฆ๐Ÿคฆ๐Ÿคฆ....

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Maza alidhani umemletea Mkwe lijishangazi๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚!!
 
6th Portion:

.... I was a bit disappointed. Tukaongea story zingine mbili tatu, alafu tukaagana. Niliendelea kulifikiria lile swala, mwisho wa siku nikadhamiria nijipange Kisha niende mpaka kijijini, walau nipate kuongea nao ana kwa ana, maana dhamira yangu ilikuwa thabiti. Tofauti na wao walivyohisi, Mimi sikuwa napanga kuoa shangazi, kuna binti nilikuwa nae kwenye mahusiano ambayo kwa kiasi fulani yalikuwa serious.

Wiki moja baadae, sister angu akawa ameniita niende kumtembelea Mwanza, lakini pia aweze kuniunganisha na mchongo fulani. Nilivyoenda akafanikisha kuniunganisha na ilo deal, japo halikuwa na muda mrefu, maana nilikaa kule takriban mwezi mmoja.

Kumbe ukiachana na huo mchongo, sister alikuwa na mission nyingine. Nyumbani, wazazi walimpa jukumu la kumfahamu mwanamke wangu, Kisha awape taarifa. Sister nae alichokosea, badala walau aniulize, akawa anapitia simu yangu kimya Kimya. Simu yangu haikuwa na password, fingerprint wala patterns, so ilikuwa rahisi kuaccess information.

Katika mapenzi kuna muda wapenzi huwa wanachatig ujinga ili kusogeza siku. Sasa kuna chatting fulani nilikuwa nachat na shangazi, kiutani utani nilimwambiaga "Yani wewe ningefanikiwa kukuoa, ningekuwa na raha sana", ilikuwa ni chatting za kupoteza muda tu, ila sister akaichukulia serious. Na kwenye gallery alikuta picha zake kadhaa, akajirushia Kisha akakausha, maana hakuwa na namna ya kuniambia, kwasababu info amezipata kwa njia isiyo halali.

Siku zikaenda, na ule mchongo ukafika tamati, nikarudi Dar. Sasa kuna siku yule shangazi alitaka nimpost kwenye status, baada ya kuvutana sana, nikaona isiwe case, nikawahide watu wote muhimu, Kisha nikampost nakuweka caption ya kawaida tu. Sasa kumbe sister alikuwa ameinstall Whatsapp mbili kwenye simu yake, na Mimi sikugundua. Akaiona ile status. Nashangaa kuona amereply "Mdogo wangu ndio maana hata uleje haunenepi, mzigo wote huo kweli?"

Ikabidi nijaribu kumkataa:

Analyse: "Huyo ni Mama wa rafiki yangu"
Sister: "Kwenda huko, niliona picha zenu kwenye simu yako, nikahisi ni yaliyopita, kumbe ndiyo yaliyopo?
Analyse: "Haipo hivyo dad... "
Sister: "Huyo ndio mwanamke unataka kumpeleka nyumbani bila aibu? Hivi akili zako zipoje lakini?"

Ikabidi nikaushie msg zake, akaamua kunipigia simu, alinisema sana siku hiyo, hadi nikahisi kizungu zungu. Nikaanza kujihisi sasa hapa nilipofikia pashakuwa pabaya, wanaonizunguka wote hawana utulivu wala amani, inabidi niachane na haya mambo sasa.

Hata lile wazo la kumpeleka yule binti home, ikabidi nilisimamishe kwa muda. Maana mazingira hayakuwa supportive tena, na Kwa jinsi ninavyomjua Mshua, panaweza pakatokea ngumi nikienda, alaf sikutaka tufikie huko.

Huyu manzi, kipindi namwambia nataka nikamtambulishe nyumbani, alikuwa anasita sita, mara aseme nivute subira kidogo, muda bado. Alivyosikia nimesitisha kumpeleka nyumbani, ukawa ugomvi sasa, maana akawa ana push sana nimpeleke, hadi nikawa najiuliza, hiyo subira aliyokuwa anasema niivute, imekatika au?.

Fast forward kidogo. Niliendelea kufanya mishe zangu za kuunga unga mjini, huku nikipata nafasi, nazungusha bahasha maofisini. Pale gheto nilipokuwa nimepanga, kuna Mzee fulan smart, amechomekea muda wote, ni mtu mzima, ila hana mvi hata moja, panki lake muda mwingi limepakwa super black, nae alikuwa amepanga pale. Sema tofauti yetu, Mimi nilikuwa nimepanga chumba kimoja, yeye alichukuwa vyumba viwili na sebule, maana alikuwa na familia.

Mzee sikuwa na mazoea nae sana, hata jina lake halisi nilikuwa silifahamu, nilizoea kusikia mkewe anamuita baba fulani (jina kapuni), au vijana wengi pale mtaani walipenda kumuita Mzee Dingi (na Mimi humu nitapenda kutumia ilo ilo jina la Mzee Dingi). Huyu Mzee kwa mtazamo wa nje, alikuwa na muonekano fulani wa kimamlaka, yani ukimuona tu kwa mara ya kwanza, unahisi atakuwa mtu mzito au yupo kitengo nyeti somewhere. So, kutokana na mambo yangu kuwa magumu, nikapata wazo la kuongea nae, pengine anaweza akaniunganishia mchongo wowote hapa mjini. Siku ya siku nikamkabili, ilikuwa siku ya jumapili, maana huwa anashindaga home tu.

Nilivyomuelezea shida yangu, kabla ya yote akaniuliza kwanini nimemfata yeye?. Nikamjibu nimejaribu tu, maana siwezi jua nani anaweza nisaidia, maana mjini Sina connection ya maana. Mzee Dingi akaniuliza elimu yangu na taaluma niliyonayo. Nikajielezea vizuri pale. Tukaongea mambo mengi, mwishowe akaniambia, kesho nivae vizuri, Kisha nimpigie simu anielekeze nitakapomkuta. Tukabadilishana namba za simu, nikarudi ghetto kwangu.

Kesho yake nikajiandaa vizuri, Kisha nikampigia simu anipe direction. Akanielekeza niende mpaka city center, maeneo ya Samora, kuna bustan fulani ipo opposite na NBC, nimsubirie pale. Nikabeba copy za vyeti vyangu kwenye bahasha, nikaanza safari ya kuelekea town. Nilivyofika, nikamjulisha, akaniambia nimsubirie atakuja. Nikatulia.

Nilikaa sana pale, karibia masaa mawili, Mzee hajatokea, wala hajanicheki. Sema sifa kubwa ya jobless ni uvumilivu, nikaendelea kuvumilia. Baada ya muda, pembeni yangu alikuja akakaa jamaa, ambae alionekana kama Yuko stressed hivi. Kila muda anapiga simu, na ukimuangalia vizuri kama anataka kulia. Sasa katika kupoteza time maana nilikuwa bored, nikajikuta namuuliza kilichomsibu. Jamaa ndio kunipa story kuwa huwa anafanya biashara ya mkaa, analeta na kuuza kwa jumla, kisha anarudi mkoani. Hii ilikuwa ni trip yake ya kwanza tokea aanze biashara kwa upande wa Dar, mzigo wote umekamatwa na maliasili maana pia alikuwa amebeba vitu ambavyo hakuwa na vibali navyo, So upo kituo cha polisi. Haelewi afanye nini, na wale waliomshika, wanataka mpunga mrefu ili aachiwe. Ndani ya muda ule mfupi, alijikuta tu ananiamini, tukawa tunaongea kama watu ambao tumefahamiana kwa muda mrefu.

Binafsi sikuwa na cha kumsaidia, nikabaki nampa pole na kumtia moyo tu. Ghafla Mzee Dingi akawa amefika, nikanyanyuka kumsalimia, alafu nikawa nasubiria anioneshe direction tunayoenda, ila yeye akawa amemakinika sana na yule jamaa niliyekuwa naongea nae. Akaniuliza "Huyu mwenzako ana Nini?". Nikashangaa kwann amemuita mwenzangu, ila sikujali sana, nikampa briefly tu.

Baada ya kuisikia story ya jamaa, pale pale Mzee Dingi akasema anafahamiana na mwanasheria ambae alishamsaidiaga rafiki yake kwenye mzozo na maliasili. Akamwambia yule jamaa aongozane na sisi wakati yeye anampigia simu mwanasheria. Kilichonishangaza, wakati tunaondoka, ile simu aliyopiga, ikaita kwa Mzee mwingine ambae alikuwa eneo lile lile anakunywa kahawa, sema kakaa benchi jingine. Yule jamaa wa mkaa hakuusoma mchezo, sijui ni stress au vipi.

Mzee Dingi aliongea huku simu kaiweka loudspeaker wote watatu tunasikia, mwisho wa siku mwanasheria akasema yupo maaneo ya stesheni,kuna mgahawa anapata chai, so tumfate pale. Tukaongozana Mimi, Mzee Dingi na jamaa wa mkaa. Stesheni kuna mgahawa upo unaface stand direct, ndio tukaingia hapo. Tukamkuta huyo mwanasheria, nilivyoiangalia ile sura, ni Mzee ambae tokea nilivyofika kwenye bustan pale Samora, nilimkuta, muda wote alikuwa anasoma gazeti, story kidogo huku anakunywa kahawa. Yani kiufupi hakuwa na haraka yoyote. Ila tulivyomkuta hapo kwenye mgahawa, akatwambia tuongee tunachotaka kuongea, hana zaidi ya dakika 15, anawahi mahakamani.

Kuna kengele Fulani ikalia kichwani mwangu. Zilipigwa sound za kutosha pale, sound nyingi sana. Mpaka ikafikia hatua, yule jamaa wa mkaa akahitajika kutoa laki 5 ili issue yake iwe solved siku ile ile. Jamaa wa mkaa akawa anajaribu kubargain yule mwanasheria feki akanyanyua briefcase yake akatishia kuondoka, Mzee Dingi akawahi kumtuliza kuwa amsaidie jamaa issue yake, jamaa nae kwa kuhofia kupoteza mtu wa kumsaidia, akakubali kutoa hiyo 500k. Pale pale akili ikaniambia, kuna mtu anatapeliwa muda sio mrefu.

Kati ya wote pale, yule jamaa wa mkaa, alionekana kuniamini Mimi kuliko wengine. Hata ile 500k waliyokubaliana atoe, akanitupia Mimi jicho fulani kama vile kuomba ushauri au kuuliza atoe au asitoe?. Kwa mazingira yalivyokuwa, nikajikuta nampa ishara atoe hela, asiwe na wasi wasi, ila nafsi ilikuwa inanisuta sana.

Wote wanne, tukatoka nje ya ule mgahawa, tukapanda gari ya yule mwanasheria, mpaka ATM, jamaa wa mkaa akatoa hela. Kisha tukarudi mpaka karibu na jengo la mamlaka ya bandari, kufika pale, yule mwanasheria na jamaa wa mkaa wakashuka na kuingia ndani, Nia ni kwenda kuandikishiana hela walizipeana, then ndio waende polisi. Baada ya dakika kama 15, yule mwanasheria akarudi peke yake, akazama kwenye gari haraka, Mzee Dingi akang'oa.

Akili yangu ikawa wazi, kuwa Mzee Dingi ni tapeli tu, yeye na mwenzie. Ikabidi nivunje ukimya ndani ya gari, kwamba kilichafanyika haikuwa haki. Hakuna aliyenijibu, Mzee Dingi akapaki gari kituo cha mnazi mmoja pale, then Mzee Dingi akawa ananiambia "Bahasha wanazunguka nazo vijana wanaotafuta kazi, wewe umeshapata kazi tayari, tafuta briefcase au begi la kubeba mkononi, kesho usije tena kazini na hiyo Bahasha". Nikamwangalia yule Mzee, hana hata chembe ya huruma au kujutia. Yule mwanasheria feki, akaniuliza "Kwani bwana mdogo unachotaka hasa ni nini?". Nikamjibu " Tumrudishie jamaa hela zake". Mzee Dingi akadakia "Sikia apostle, Ungetaka kumsaidia, ungemsaidia kipindi tupo pale mgahawani, acha kutia huruma wakati hela unaitaka"

Nikajikuta hasira zinazidi, hasa alivyoniita apostle, maana ilikuwa ni kama kebehi fulani hivi. Yule mwanasheria feki kwenye ile 500k, yeye akachukua 200k, Mzee Dingi akapewa 200k, alafu akachukua 100k na kunikabidhi Mimi,kisha akanipa na namba ya simu kwenye kikaratasi. Akaniambia "Hiyo ndio namba ya yule jamaa, hiyo 100k ndio mgao wako, mtafute umrudishie walau nusu hasara"

Nikabaki nimetoa macho tu.....
[emoji28][emoji28]
 
5th Portion:

.... Akili yangu faster ikaniambia, hapa nitakuwa nimeleta mchepuko wa Mshua home, ndio maana Mama kazimia alipouona. Nikajisemea, nishaharibu hapa, tena siku ya kwanza tu kuja.

Nikamkimbilia Mama pale chini. Yule bi mkubwa akawa anakuja taratibu, Mshua nae akawa ametoka ndani. Tukawa tunampa huduma ya kwanza, huku Mshua ananiuliza "Imekuwaje akawa hivi?. Nikamjibu kuwa sielewi, na kiukweli sikuwa naelewa. Baada ya kumpepea pepea huku Mshua akimnawisha kwa maji ya baridi kichwani, Mama fahamu zikawa zinarudi taratibu.

Kipindi hayo yanaendelea, Mshua alikuwa anaongea na yule bi mkubwa niliyekuja kuja nae. Maongezi yao yalikuwa ya kawaida tu, lakini kila nikijaribu kumsoma Mshua kuona kama ana wasiwasi, ila namuona yuko neutral tu. Mama nae fahamu zilivyorudi kabisa, akapewa na maji akanywa. Alivyoona Mshua na yule bi mkubwa wanaongea kama watu wanaofahamiana, nikaona na yeye kazidi kupata ahueni. Ikabidi viletwe viti hapo hapo nje, ili bi mkubwa aendelee kupata hewa safi. Mshua akatoa utambulisho pale, nikaona Mama kumbukumbu juu ya yule bi mkubwa zikawa zimemrudia, kumbe na yeye alikuwa anamfahamu.

Baada ya chakula cha pamoja, yule bi mkubwa akaomba kuondoka maana anaratiba zingine. Mzee akamsindikiza. Huku nyuma nilivyobaki na Mama, nikajaribu kumuuliza alikutwa na nini mpaka kuzimia? Akanijibu "Acha tu, cha muhimu niko sawa sasa". Jitihada zangu za kumbembeleza aniambie, zikagonga mwamba, ikabidi nisalimu Amri.

***** ****** ******** ******* *******

Maisha yaliendelea vizuri pale nyumbani, likizo ilivyo karibia kuisha, nikaondoka.

Siku zikaenda, hatimae masomo yakafikia tamati. Nilipofanikisha kumaliza chuo, kabla ya graduation, Mzee akawa ameniita home. Siku niliyofika, hatukuongea mambo mengi, ila baada ya siku 3 ndio akaniweka kikao. Tukaongea mengi sana kuhusu maisha. Mwisho wa siku akaniambia "Ukirudi tena mjini, kuna mtu nataka ukaonane nae". Nikamuuliza ni nani? Akajibu "usijali, nitakupa namba yake, na namna ya kumpata. Anaweza kukusaidia maisha yako baada ya chuo". Nikamuitikia sawa. Lakini kimoyo moyo sometime nilikuwa namind, maana kama kunipa namba yake ya simu na hizo taarifa zake, angeweza kunipa hata kwa njia ya simu nikiwa Dar.

Nilivyotaka kurudi Dar, alinipa ile namba ya huyo mtu, Kisha akaniambia mengine nitayapata nikishaongea nae, maana anatarajia simu yangu. Nikarudi zangu mjini.

Baada ya kama siku tatu tokea nifike mjini, nikampigia yule mtu. Akanitambua vizuri, Kisha baada ya mazungumzo machache, akasema atanitafuta, akitulia. Nilikaa wiki nzima, hakunicheki. Mshua kuna siku akaniuliza kama nilimtafuta yule mtu, nikamjibu "Ndio, ila alisema atanitafuta akitulia, ila amekuwa kimya". Mzee akaniambia mtafute tena.

Nikampigia tena, hakupokea. Kesho yake nikampigia tena, alivyopokea akaniuliza "Nani mwenzangu?", Ikabidi nijitambulishe upya, alivyonikumbuka, akasema alibanwa na shughuli alafu pia namba yangu hakuwa ameisave, ndio maana alishindwa kunitafuta. Nikamjibu aina shida Mzee. Akaniuliza "Siku gani unakuwa na muda?", Nikamjibu "Kila siku". Akacheka kidogo, alafu akasema atanipigia mwishoni mwa wiki, ili ikiwezekana tuonane.

Ilivyofika mwisho wa wiki, nikasahau makubaliano na yule Mzee, nikajikuta nimemualika mpenzi wangu gheto. Wakati tupo pale, Mzee akapiga simu. Ugomvi wangu mkubwa na huyu binti ilikuwaga simu, alikuwa hataki kabisa tutumie simu tukiwa pamoja, labda mpaka aondoke. Kwahiyo akijaga, simu tunaziweka silent, alaf zinakaa juu ya meza. Yule Mzee alipiga mara 3, zote sikuweza kuzisikia. Nilikuja kuziona zile missed calls jioni sana. Nilipojaribu kumpigia hakupokea. Nikatulia. Baada ya wiki, Mshua akanipigia simu kuuliza kama niliongea na yule mtu, ikabidi nimuelezee hali halisi ilivyo. Baada ya kunisikiliza mpaka mwisho, akaniambia "Tukimaliza kuongea na simu, jaribu kumtafuta tena". Ikabidi nimuulize Mshua, yule Mzee ni nani haswa? Na kwanini natakiwa kumcheki?

Mshua: "Huyo ni mtu wa huku kijijini kwetu, ni kama ndugu yetu. Anafahamiana na watu wengi huko mjini, anaweza kukusaidia"

Analyse: "Ila hapokei simu, alaf ni kama vile hataki huu ukaribu unaojaribu kuuweka"

Mshua: "Ila ni mtu anayeweza kukusaidia, ngoja nikuelekeze kwake, ili umfate kule"

Mshua akanielekeza, lakini sikuwa comfortable kabisa kwenda. Mtu kama simu hapokei, ukienda kwake siutaishia getini?. Nikaamua kumpigia simu siku hiyo hiyo, ili kama kesho nitaenda, basi awe anautarajia ujio wangu. Nilivyopiga, simu ikaita kidogo, alaf ikakatwa. Akanitumia msg "Nipo kwenye kikao, nitakupigia nikitoka. Nani mwenzangu?"

Ile msg ilinifanya nijisikie vibaya na huu undugu wa kufosi. Mzee kila siku ananiuliza Mimi nani?. Sikuijibu ile msg, nikajisemea, kama akinipigia baada ya hicho kikao, sawa. Asisipopiga, simtafuti tena. Yule Mzee hakupiga. Nikampotezea.

Nikaendelea na harakati zingine za utafutaji. Siku, wiki, miezi ikapita. Mshua hakuwahi niuliza tena kuhusu yule Mzee, na hata ilipokuwa tukiongea, hakuingizia ilo swala. Baada ya miaka kama miwili au mitatu kasoro, nikawa nimedhamiria swala la kwenda kumtambulisha mwanamke nyumbani, ili mambo yakienda sawa, siku zijazo nioe.

Na wazo ilo lilitokana na msukumo niliokuwa nao ndani yangu, maana nilikuwa nishaanza kuingiwa na uvivu usio wa kawaida. Kupika, kufua, usafi nk. Yani kiufupi kazi zote za ndani kwangu zilikuwa mzigo. Tatizo pekee nililokuwa nalo, mwanamke ambae nilikuwa nae kwenye hayo mahusiano kwa wakati huo, kila nikimwambia issue ya kumtambulisha nyumbani, anasita sita. Kwamba tusubirie kidogo, mara tuzae kwanza ajifunze malezi. Binafsi sikuwa na mpango wa kuzaa nae bila kuwa tumeoana, maana kama tukishindwana, sitaki nitakae kuja kumuoa nimpe lundo la watoto wasio wake. Baada ya kujadiliana nae kwa kina, mwisho wa siku tukawa tumekubaliana kuanza hizo process.

Nilivyofikisha hiyo taarifa nyumbani, kila mtu aliipokea neutral, hakuna aliyekuwa na shauku au furaha nayo. Mama akaniambia niendelee kujipanga kwanza kimaisha.

Analyse: "Ila Mama, maisha ndio haya haya, hakuna jipya, mambo mengine yatakaa sawa mbeleni"
Mama: "Ni sawa mwangu, pia nakuombea sana heri, ila huoni kama ungesubiria kidogo?"
Analyse: "Nisubirie nini tena Mama? Hutaki kuitwa mkwe?"
Mama: "Nataka sana mwanangu, tena kati ya wanangu ambao natamani kushuhudia harusi yao ni wewe mwanangu"
Analyse: "Basi niruhusuni nimlete mumfahamu Mama"
Mama: "Kusema ukweli naogopa mwanangu. Naogopa sana sijui utaniletea mwanamke wa aina gani, maana kuna muda akili zako unazijua mwenyewe. Hata ile siku niliyopatwa na mshtuko, akili yangu iliniambia yule mwanamke uliyeongozana nae ndio umekuja kumtambulisha"

Nilichoka. Nikajikuta nimekaa kimya kwa muda, nisijue cha kusema. Kumbe ile ndio sababu ya Mama kupata mshtuko?. Yani familia zingine wakisikia watoto wao wanataka kuoa inakuwa furaha, kwa upande wangu naleta wasi wasi? Vijana wenzangu wakiongozana na wamama, wakawasaidia mizigo, wanaonekana vijana wa heshima, Mimi Mama yangu kuniona nimeongozana na mmama, kapatwa hadi namshtuko? [emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751]....

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
We jamaa story yako ina chekesha Sana inaonekana ulikuwaga kiboko
 
Back
Top Bottom