Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

22nd Portion (Portion Finale)


.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;

"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.

Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.

Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.

Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.

Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.

Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.

Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.

Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.

Nikatikisa kichwa tu kukubali.

Akaendelea:

"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.

Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.

Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"

Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.

Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"

Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya

Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"

Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."

Akaendelea;

"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"

Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"

Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"

Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"

Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"

Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"

Mshua: "Hawakujali kivipi?"

Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"

Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"

Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".

Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"

Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".

Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;

"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"

Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"

Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."

"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"

"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"

"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."

"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"

Analyse: "Ndio?"

Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"

Analyse: (Kimya).

Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"

Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"

Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"

Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."

Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".

Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"

Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."

Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"

Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".

Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.

Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:

Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"

Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"

Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"

Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)

Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza

"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"

Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?

Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"

Wote tukaishia kucheka tu.

Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"

Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"

Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"

Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"

Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"

Mama: "Sawa"

Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"

Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)

Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"

Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"

Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:

"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"

Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"

Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.

Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.

Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.



*******************************************

Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.

Wasalaam,

Analyse
Asante kk
 
22nd Portion (Portion Finale)


.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;

"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.

Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.

Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.

Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.

Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.

Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.

Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.

Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.

Nikatikisa kichwa tu kukubali.

Akaendelea:

"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.

Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.

Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"

Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.

Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"

Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya

Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"

Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."

Akaendelea;

"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"

Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"

Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"

Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"

Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"

Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"

Mshua: "Hawakujali kivipi?"

Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"

Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"

Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".

Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"

Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".

Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;

"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"

Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"

Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."

"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"

"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"

"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."

"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"

Analyse: "Ndio?"

Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"

Analyse: (Kimya).

Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"

Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"

Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"

Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."

Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".

Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"

Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."

Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"

Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".

Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.

Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:

Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"

Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"

Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"

Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)

Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza

"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"

Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?

Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"

Wote tukaishia kucheka tu.

Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"

Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"

Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"

Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"

Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"

Mama: "Sawa"

Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"

Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)

Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"

Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"

Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:

"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"

Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"

Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.

Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.

Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.



*******************************************

Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.

Wasalaam,

Analyse
@Analyse the genius [emoji119]

Hii ni zaidi ya elimu huu ni wosia uliojitosheleza super and brilliant. Asante sana kwa kuweka hii mada hapa mahali.

Uendelee kuishi sana mkuu Mungu akubariki na muweke Mungu mbele.
 
22nd Portion (Portion Finale)


.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;

"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.

Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.

Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.

Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.

Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.

Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.

Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.

Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.

Nikatikisa kichwa tu kukubali.

Akaendelea:

"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.

Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.

Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"

Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.

Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"

Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya

Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"

Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."

Akaendelea;

"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"

Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"

Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"

Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"

Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"

Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"

Mshua: "Hawakujali kivipi?"

Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"

Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"

Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".

Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"

Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".

Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;

"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"

Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"

Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."

"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"

"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"

"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."

"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"

Analyse: "Ndio?"

Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"

Analyse: (Kimya).

Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"

Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"

Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"

Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."

Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".

Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"

Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."

Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"

Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".

Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.

Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:

Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"

Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"

Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"

Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)

Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza

"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"

Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?

Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"

Wote tukaishia kucheka tu.

Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"

Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"

Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"

Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"

Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"

Mama: "Sawa"

Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"

Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)

Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"

Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"

Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:

"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"

Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"

Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.

Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.

Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.



*******************************************

Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.

Wasalaam,

Analyse
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake...
 
@Analyse the genius [emoji119]

Hii ni zaidi ya elimu huu ni wosia uliojitosheleza super and brilliant. Asante sana kwa kuweka hii mada hapa mahali.

Uendelee kuishi sana mkuu Mungu akubariki na muweke Mungu mbele.
Shukrani sana mkuu 🙏 🙏
 
Mzee Dingi na mstaafu sijawahi kabisa kuonana nao tena. Nilishawahi kukutana mara moja na Mzee Kidevu, sikutaka hata story nae, nikamkimbia tu.

Mzee Kesho Yetu nilikutana nae mara mbili, mara ya kwanza hatukuongea chochote, mara ya pili nilikuwa kwenye kikao cha harusi, akaja ili wajumbe wamuone, yeye ni MC
Hakika watu wanaishi kwa "Mishen-town"
Yaani, Dingi kakaba kila sekta !!
 
1st Portion:

Kama ilivyo kwa wazazi wengine, wazazi wangu pia walikuwa wanatamani sana kijana wao nisome shule. Kile kitendo cha kuishia njiani, kwa upande wao hakikuleta taswira nzuri. Pamoja na mengi yaliyokuwa yamejitokeza, Bado tamanio lao la kuona naenda shule liliendelea kuwepo. Kitendo cha kukaa nje ya mfumo wa elimu, nilijiona kama vile regular education ishanitupa mkono, sana sana nilikuwa nafikiria kama nitaenda kusoma, basi walau iwe mafunzo ya ufundi, sikutaka kukaa darasani tena.

Ila kwa upande wa wazazi, hasa Mshua, yeye alikuwa anatamani niendelee na advance, maana sikuwa nimefeli O level, na yeye hakushindwa kuniendeleza, ni ile kiburi cha kitoto ndio kilitibua mambo. Ilifikia hatua nikiwasiliana na mshua, pakitokea quarrel ya aina yoyote, lazima swala la elimu liingiziwe, hata kama mada aihusiani. At last niliamua ngoja nirudi shule tu. Nilivyowafikishia ile taarifa Mshua aliipokea neutral, haoneshi kama kafurahi au la. Ila alikubaliana nayo.

Tokea nimalize form 4, ulikuwa umepita muda kiasi, Mshua alipata tabu kunipatia usajili katika shule ya serikali. Nakumbuka Mshua alikuwa muda wote ni kuongea na simu tu, mara kapiga huku, mara kule, mara kaenda kukutana na mtu huyu au yule. Maana mfumo wa government ulikuwa unanikataa. Option ya kwenda shule za private ilikuwepo, ila sikuelewa kwanini Mshua alikuwa analazimisha nisome shule ya serikali. Alifosi sana anavyojua yeye, hatimae nikafanikiwa kupenyezwa kwenye shule ya serikali, japo nilianza kwa kuchelewa takriban miezi mitatu.

Binafsi nilikuwa sitaki kusoma nje ya Dar, wakati mshua yeye alikuwa anaamini, nikipata shule Dar sitosoma. Kwahiyo aliniwahi na kauli moja, kama sitokubali kwenda kwenye shule itakayopatikana, basi nitarudi kwenda kusomea kule kijijini walipo. Sikuwa na namna. Hatimae nikabahatika kusajiliwa katika shule iliyokuwa pale mkoani Tanga.

Changamoto na Mzee wangu Bado ikarudi pale pale, kwenye swala la combination. Mzee yeye anasema nisome zile za Arts, binafsi sikuwa na mpango nazo. Tena kuonesha Yuko serious, kabla ya kwenda rasmi shule, alininunulia vitabu kadhaa vya language na Kiswahili. Mshua yeye alikuwa anaamini kwavile napenda kusoma vitabu, basi njia sahihi kwangu ni Arts. Ila kwa upande wangu, kusoma vitabu ni hobby tu. Sikutaka kubisha, nikavipokea, nikaenda shule rasmi shule.

Kitu cha kwanza nilichofanya baada ya kupokelewa pale shuleni, ilikuwa ni kutaka kujua combi zinazotolewa pale. Palikuwa na PCB, PCM, CBG na HKL tu. Nikaanza mchakato wa kuomba kubadilishiwa combination . Baada ya kuzungushwa sana, mwishowe nikauvagaa mziki wa PCM. Nilivyompa taarifa mshua, kwa mara ya kwanza Mshua akanitukana, kisha akaniambia "Hivi unajua nimepoteza hela kiasi gani mpaka wewe umepata hiyo nafasi, au unadhani nina hela za kuchezea?". Kila nikijaribu kujitetea, ananicrash, mwisho wa siku akaniambia "Unatumia nguvu sana kutaka kuniletea aibu kwenye familia, sasa Sikia ukipata zero nisikuone tena hapa kwangu"

Tukaishiana hivyo.

****************

Nilipata tabu sana pale shuleni, sana yani. Ile miezi 3 ya mwanzo ilikuwa kama miaka mitatu. Kila walim wakitangaza kuna test, nakosa amani kabisa, maana kama sijawa wa mwisho, basi ni wapili kutokea mwisho. Kuna jamaa alikuwa anaitwa Athuman au Ochu, huyo ndiye tuliyekuwa tunapokezana nafasi mbili za mwisho, akidoji test ya namba, basi ujue mkiani nitakuwa Mimi. Hapo kipindi Mimi shule naiona kama gereza, kuna wadau wanafanya solving kwenye nekta ya form 6, na maswali yanawatii. Kuna jamaa mmoja nikamganda sana awe ananikatia mapindi, maana kidogo alikuwa njema. Alivyojua Sina topic yoyote ambayo nimeshasoma, alinishangaa sana, akaniambia "Dogo hii ni PCM, hatuji shule kichwa kichwa". Huyu jamaa ndio alikuja kunionesha mchikichini, na hapo ndio nilikutana na watu (walimu) ambao walinibadilisha kabisa, walioniondolea aibu na fedhea darasani (mmoja kwasasa ni marehemu, Mungu amlaze pema).

Nilipoingia form 6, nishakuwa mwenyeji sasa pale Tanga, hakuna ratiba ya baikoko ambayo nilikuwa siijui. Hakuna malaya wa Chichi na La Cassa ambae nilikuwa simjui. Wamama hao ndio usiseme, Ijumaa mpaka Jumapili nilikuwa sionekani kabisa maeno ya hostel. Na baadhi ya Jumatatu, nilikuwa naenda shule kutokea nyumbani kwa Mama Mariam.

Nilijikuta nahitaji sana hela, ili kuweza kukeep up na movements zangu. Nilikuwa na jamaa yangu mmoja wa karibu sana, yeye alikuwa ni mzawa wa kule kule, aliitwa Ochu. Jamaa alichoresha mchoro, tuibe mahindi kwenye store ya shule, walau yatupatie vihela kadhaa tukiyauza.

Lile deal lilienda vizuri, maana tulikuwa tunahamisha mahindi kidogo kidogo, then tunaenda kuyahifadhi kwa bi mkubwa ambae mumewe ndio tulipatana tumletee gunia moja. Bahati mbaya, yule Mama akajikuta raia mwema, akavujisha ile issue kwa Mwalim. Siku hiyo kama kawaida tumejaza mahindi kwenye mabegi tunapeleka kwa jamaa, tunakuta Mwalim anatusubiria. Akatulaza kituoni, then kesho yake kesi ikasomwa assembly.

Tukala stick mbele ya umati. Kisha tukapewa suspension ya miezi 3, tukirudi tuje na wazazi pamoja na hela ya fine.

Issue inaanza, ni mzazi gani nitamuita? Mama hawezi kuja, Mshua yuko mbali sana na pale, lakini hata ingekuwa karibu nisingeweza kumwambia ule ujinga. Kwa upande wa mwanangu Ochu, wiki kama 2 zilizopita alikuwa na msala home kwao, kwahiyo alikuwa kwenye kipindi cha tahadhari, so hakuweza kuwaambia home kwao, japo yeye ni mzawa wa pale. Mwisho wa siku tukaadhimia tuite wazazi wa kukodi, japo mwana yeye lile wazo hakuliafiki hata kidogo. Hostel za ile shule niliyokuwa nasoma, zilizopo nje ya shule, zilikuwa opposite na vijumba fulani vya mbao, vimechoka sana, walikuwa wanaviita Kijiji Cha 21 (kama sijakosea), sasa mwanangu Ochu ndio akaenda kuchukua Mzee mmoja pale, aende akaigize kama baba ake mdogo. Siku ambayo Ochu alienda na baba ake mdogo feki, na Mimi nilienda kwa dhumuni la kuomba niendelee na masomo, mzazi wangu yupo njiani anakuja. So wakati tumesima pale, Mwalim wa nidham akamuuliza yule baba mdogo feki wa Ochu amekuja pale kwa dhumuni la nani? Yule dingi akasema yeye amekuja kusikiliza kesi ya Ochu, Mimi hanifahamu.

Mwalim: "Mzee umekuja kwa ajili ya nani hapa? Au wote?"
Mzee : "Nimekuja kwa ajili ya huyu (akimnyooshea kidole Ochu"
Mwalim: "Mwanao anaitwa nani?
Mzee: "Ochu.... , Athuman"
Mwalim: "Athuman nani?"
Mzee : Akawa Kimya. Mwalim akarudia tena swali, ila Mzee kimya.
Mwalim: "Una uhusiano nae gani?"
Mzee: "Mtoto wa kaka angu"
Mwalim: "Huyo kaka ako anaitwa nani?"
Mzee: (kimya)
Mwalim (akamnyooshea Ochu kidole) : "Haya, wewe na baba ako, ondokeni mkaje na baba enu"

Kisha akanigeukia na Mimi, wewe pia ondoka, bila mzazi nisikuone hapa.
Nikatangulia Mimi kutoka, wakanifata kina Ochua, hao tukaenda nje ya shule. Hapo tayari nishaingia ubaridi, maana sioni namna naweza kumwambia mshua aje.

Baada ya kama wiki hivi ya kuzurura zurura pale mjini, nikaenda sehemu moja inaitwa Nguvu Mali, kule kulikuwa na jamaa yangu anasoma Galanosi. Nilivyomuelezea msala wangu, akasema atanikutanisha na jamaa mmoja hivi, mchaga, ambae alikuwa na biashara yake karibia na maeneo ya shuleni kwao. Huyo mchaga, alikuwa anatumiwa sana na wanafunzi wa Tanga Tech kwenye misala kama hiyo. Kwa ufupi alikuwa mbobezi (kwa maelezo aliyonipa jamaa yangu)

Basi alivyonikutanisha nae, ikabidi nimpange issue ilivyo, kwamba kuna kesi ya uongo na kweli nimepewa huko shuleni, akaniuliza maswali mawili matatu, pia nikamuelezea jinsi Ochu alivyoumbuka ofisini, yule jamaa akacheka tu. Akasema hayo mambo madogo, kesho kutwa ntakuja. Wakati nataka kuondoka, akaomba advance 10k, maana tulipatana 25k.


Endelea hapa: Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
dadapesa anzia hapa
 
22nd Portion (Portion Finale)


.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;

"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.

Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.

Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.

Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.

Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.

Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.

Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.

Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.

Nikatikisa kichwa tu kukubali.

Akaendelea:

"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.

Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.

Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"

Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.

Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"

Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya

Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"

Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."

Akaendelea;

"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"

Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"

Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"

Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"

Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"

Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"

Mshua: "Hawakujali kivipi?"

Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"

Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"

Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".

Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"

Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".

Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;

"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"

Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"

Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."

"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"

"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"

"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."

"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"

Analyse: "Ndio?"

Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"

Analyse: (Kimya).

Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"

Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"

Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"

Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."

Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".

Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"

Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."

Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"

Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".

Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.

Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:

Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"

Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"

Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"

Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)

Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza

"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"

Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?

Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"

Wote tukaishia kucheka tu.

Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"

Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"

Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"

Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"

Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"

Mama: "Sawa"

Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"

Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)

Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"

Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"

Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:

"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"

Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"

Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.

Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.

Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.



*******************************************

Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.

Wasalaam,

Analyse
Mshua wako Ni mwanafalsafa mtupu. Great mkuu, ukikutana naye au mkiwasiliana naomba umfikishie salamu zangu, mwambie tumeburudika na kuelimika vya kutosha kwa punch zake mwanzo msisho, nawe umekua msimuliaji mzuri Sana, una maandishi flani yasiyochosha hata kidogo, Mwenyezimungu wetu wa haki akubariki wewe na kizazi chako chote in Sha Allah
 
22nd Portion (Portion Finale)


.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;

"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.

Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.

Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.

Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.

Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.

Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.

Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.

Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.

Nikatikisa kichwa tu kukubali.

Akaendelea:

"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.

Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.

Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"

Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.

Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"

Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya

Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"

Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."

Akaendelea;

"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"

Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"

Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"

Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"

Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"

Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"

Mshua: "Hawakujali kivipi?"

Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"

Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"

Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".

Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"

Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".

Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;

"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"

Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"

Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."

"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"

"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"

"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."

"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"

Analyse: "Ndio?"

Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"

Analyse: (Kimya).

Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"

Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"

Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"

Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."

Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".

Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"

Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."

Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"

Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".

Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.

Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:

Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"

Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"

Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"

Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)

Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza

"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"

Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?

Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"

Wote tukaishia kucheka tu.

Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"

Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"

Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"

Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"

Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"

Mama: "Sawa"

Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"

Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)

Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"

Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"

Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:

"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"

Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"

Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.

Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.

Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.



*******************************************

Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.

Wasalaam,

Analyse
Yani hata sijui nisemeje..ila mkuu hongera sanaa kwa huu uzi..mimi ni mdada ila nimeyachukua mafunzo ya baba yako na nitayafanyia kazi..kuna sehemu nimescreen shot maana ni nondo za hatari ni motivational quotes za maana...
Thanx Analyse sichoki kusoma story zako since day one..maana zinaburudisha na kuelimisha
Endelea kuni tag kwa new posts kwani tag zako haziendi bure zinafanyiwa kazi 😆 😆 😆
 
Back
Top Bottom