Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

kma ni suala la kuonyesha maburungutu ya fedha chunya,mkwajuni ,saza na tunduma mbona kawaida tu. Kurejeshewa chenji incase gari limetangulia pande za tukuyu kiwira ni kawaida. Changamoto inakuja uaminifu ni zero hapa kwenye jiji la makala plus panya road attacks
 
Mr.Dudumizi umehamia na kuwa balozi wa Amani wa Zambia,Ile habari ya nchi yako ni kisiwa cha amani imeishia wapi🥱
Habari ipi hiyo mkuu? Afu tofautisha amani na usalama. Hivi ni vitu viwili tofauti ndio maana hata maneno yake pia yako tofauti.

AMANI: Mfano naweza kusema Burundi sasa hivi ni nchi ya amani kwa maana hakuna vita.

USALAMA: Ila pia naweza kusema Burundi hakuna usalama, kwa maana watu wamekuwa wakiuwawa, kutekwa, kufungwa, kubambikiwa kesi, kuingiliwa usiku majumbani kwao, kuporwa barabarani, kupigwa hovyo nk.

Kwahiyo Tanzania ni nchi ya amani, ila kwa upande wa usalama tunalega lega kidogo. Sema jeshi letu la polisi limejitahidi kurudisha usalama kwa kiasi kikubwa baada kuyangamiza yale magenge ya panya road nk.
 
Tunduma burungutu unaweza kutembea nalo ukiwa maeneo ya mpakani pale border kwa sababu askari polisi na wa uhamiaji ni wengi sana maeneo yale. Ila ukitoka kidogo tu nje ya hapo. Watu watakusaula hadi nguo ya ndani wakuache kama ulivyozaliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…