Sijivunii wazazi wangu

Sijivunii wazazi wangu

Umefika fomu foo bado unataka wakubebe wawe wanatembea na wewe huko mjini.

Pambaneni huko na msisahau kuleta pesa kwa wazazi.
Wala hawastahili kuletewa hata senti moja au hata sumniii!!!![emoji23][emoji23]

Inatakiwa wavune walicho panda.let them reap what they sow....[emoji1]

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Robert Heriel ,kitendo cha kuwaita wazazi wa (ko, ke) wapumbavu kinakuweka kundi gani?

Wacha sisi tunaoiamini biblia tuonekane wajinga NARUDIA waheshimu wazazi wako!

kuna kisa kimoja NUHU alilewa mpaka akavua nguo, mwanae mmoja alimtazama akacheka akaenda kuwaambia wenzake! Wakachukua nguo wakamvalisha, walitembea kinyumenyume ili wasione utupu wa baba yao! Ingekuwa wewe Robert Heriel ungesema mzee wako ni mlevi kavua nguo

MTU akifanya upumbavu unataka aitwe Mwenye hekima?
Hizi dini zimefundisha Watu unafiki WA kiwango kikubwa Sana.

Yaani Mimi Kwa vile ni Baba nikifanya upumbavu unataka Watoto wangu wanione ninahekima?
Watoto wangu sitawafundisha unafiki.
Baba Yao nikizingua wajue nimezingua, na wewe na uwezo wa kuniambia Mzee hapo umepuyanga. Nami niombe Radhi ikiwa kweli nimekosea.

Sio hizo hadithi za kijinga jinga, zakinafiki, zakizamani, zakitumwa, zakufanya Watu miungu Watu.
 
Wenye wazazi wenye connection na hawajasaidiwa unawaambia nini..?
Haikuwa lazima wao kusaidiwa na wazazi wao...

Hapa mada imejikita kwenye malezi ya mtoto angali bado haja anza kujitegemea from 0-18 years hapa lazima mzazi awajibike ipasavyo ila sio akwepe majukumu yake kwenye hichi kipindi..

Baada ya 18 years sasa hapo mtoto hana cha kuwalaumu wazazi..ila kama hawakuwajibika kumlea hadi anafika 18 years mtoto anastahili kuwasema wazazi wake....

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Kwani usipowapa pesa zako watakufa?

Ujue na wanao watakuja kukufanya hivyo hivyo.
Na wao wala sihitaji baraka zao ili nifanikiwe maana walikuwa wazembe kwenye kulea na kutimiza majukumu yao kama wazazi...

Point ni kwamba wazazi wazembe wasitumie kigezo cha "uzazi" kama defence mechanism ya kujilinda na kuficha Uzembe wao....

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Hivi ni wote mna wazazi kama wangu? Au mliwahi kuwa na wazazi kama wangu?, Najua ambao hamuelewi nini nazungumzia hapa haiwezi kuwaingia akilini au pia mnaweza kuhisi labda sina akili timamu na wale ambao kwa bahati mbaya mlishapoteza wazazi wenu basi pia hii tungo haitowaingia akilini, ila aina ya maisha ninayoyaishi ndo yanafanya niandike tungo hii ngumu ambayo si rahisi kuisikia kwa watu.

Sorry kwa kusahau kuwasalimu, ila kwa leo nipo na bad mood naji-feel tu kutema hii sumu ili isiniue maana hii kitu inaniuma sana wakuu, Imagine unakuwa na wazazi ambao hawajawahi kukupa direction ya maisha, Connections, Hawajaaliwa kumiliki kiwanja au hata nyumba useme utarithi, Haya basi wangekupambania usome uwatoe kwenye hiyo hali. wapi, Haya basi hata shughuli ya kufanya basi iwe imetokana na connection zao. wapi, Haya basi hata ushauri nini cha kufanya au pita njia hii. wapi, Kiufupi baada ya kumaliza Kidato cha nne nikaja Dar habari ya wao na mimi iliishia palepale.... I'm sure hata matokeo yangu hawayajui, ila wao wanajua mimi nimefeli. Mimi kuamua kuwaacha nisiwasumbue masuala ya kunisomesha kwa kuwa niliona hali ya nyumbani sio basi wao akili zao zimesave kwamba nilifeli ila sivyo. Okay, tuseme ni ukweli nimefeli hebu niambie je, mwanao ikitokea ameshindwa kuendelea na masomo basi unamtelekeza akajuane na maisha yeye mwenyewe?

Dah! Asee inaniuma kinoma ni Dsm mwaka wa nne sasa, Mzee yupo Arusha mama yupo Iringa (Wao waliachana punde tu baada ya mimi kuzaliwa) Mimi ni mtoto wa pekee kwa baba ila mama tayari ana watoto wengine wawili huko alipo.... Simu zao zikiita kwangu basi najua ni vizinga tu, Baba aliwahi kuanzisha mradi wake huko Moshi akanishawishi nimtumie kahela fulani tuwekeze tufanye jambo litatulipa nikafanya ikaja ikalaga kwangu nikasemehe kwa kuwa ni mzazi, Baba yangu anaishi kwa wazazi wake yaani kwa bibi yangu mimi., Mama yangu anaishi Iringa amepangisha na hata baba wa watoto wawili aliokuwa nao pia walishaachana (sahivi ni single mother)

Dah wakuu kuna vitu navificha hapa sitaki visema kutoka kwa huyu baba yangu na mama yangu kuna maneno waliwahi kunitamkia kwa nyakati tofauti tofauti maana nilishajuza kwamba hawaishi pamoja, ila acha niseme tu, kwa sasa wao wanajua mimi napiga harakati zangu za hapa na pale kwahiyo kuna wakati nawakumbuka japo 10k kila mmoja, Sasa ikitokea labda imepita muda mrefu sijafanya hivyo kila mmoja wao huisi kwamba nampendelea mwingine na pengine labda ndo inapelekea nisitume hela kwa muda mrefu. Jambo hili huleta mgogoro wa vinyongo baina yangu mimi na mzazi atakaehisi hivyo, Ni wote tu sometimes ni mama sometimes baba me, hupambana kuwaelewesha kwamba sivyo wanavyofikiriana hadi huchoka.... Kuna siku mzee aligomba hadi akanikatia simu nikakopa 12k nikamtumie eti akapiga simu muda huohuo huku anacheka "Mwanangu wewe ndo umetumia hii asante sana" nikamjibi ndiyo kwa hasira nikamkatia simu.

Wote tunaamini wazazi wetu ndo wanatupenda kwa dhati ila mimi kwangu ni tofauti kwani nilishajithibitishia kabisa kwamba wazazi wangu wapo after money, hata simu zao zikiita muda huu najua tayari hapa napigwa kizinga.

Baba alishawahigi kunitamkia maneno haya "Mimi nahesabu sina mtoto bana, Mtu hata hunisaidii chochote hapo nikikuambia nitumie kalaki kamoja utasema huna, kwenda kule me sio baba yako" hiyo ilikuwa kwenye simu and i was in hard situation for sure imagine pa kulala penyewe palikuwa kwa mshikaji kanisitiri, ila baadae tulikuja tukamalizana mshua kiume tukaendelea kuishi kinafki. Mama nae aliwahi kuniambia maneno haya "Yaani mi nahesabugi nina watoto wawili tu, We mtoto gani unamsahau mama yako kiasi hiki? Yaani hujawahi hata kunitumia zaidi ya 30,000 acha nimuombee huyu mwanangu wa pili ndo naona atakuja kunitoa kwenye umasikini...." Huyu mtoto wa pili sahivi yupo form 5 na anasomeshwa na mashangazi zake wao upande wa ndugu zake wapo vizuri kiuchumi kiasi chake so, mama yupo proud na huyu wa pili.... Me hiyo kitu though inaniuma mimi kama first born ila me humuachia Mungu wangu kwani ndiye alieruhusu niishi haya maisha.

Kiufupi me najionaga kama nina laana hivi, Imagine unazaliwa nje ya ndoa alafu bado wazazi wanaachane tena punde tu after umezaliwa😁😁😁, Acha nicheke tu maana muonekano wangu jamani ndo unafanya nione kabisa kwamba familia yetu ni kama kuna mahali ilichezewa, Me muonekano wangu ni ambao unaonesha kabisa kwamba imetokea bahati mbaya tu me kuzaliwa kwenye aina hii ya familia, Me najipenda sana watu hudhani me ni mtoto wa geti kali, Huishia kuitwa majina kama Bishoo,Sharo, Wa kishua ila me hubaki tu kushangazwa na hayo majina laiti wangejua.

Anyways ambao wangependa kujua naishije hapa Dar ni kwamba naishi ki-mission zaidi, Me ni kijana ambae napenda uhakika sana sinywi pombe,sivuti bangi, sina hobby na ladies, Me ni mtu ambae kiufupi sina mambo mengi, Me ni kijana ambae Mungu angenijaalia wazazi ambao wanaelewa wajibu wao ningekuwa mbali mno, Fikiria nimelelewa na baba pekee... though alikuwa careless ila hadi namaliza 4m4 sijawahi kuingia kwenye mtindo mbovu wa maisha, Me nimekuja Dar mbali na wazazi sina hili wala lile and they didn't even care of me na still nimeweza kujitegemea, Hadi kuna wakati najiuliza usikute hii kitu ndo imefanya wakaona huyu kashajiweza tuachane nae. Maana me nikiwa 17 tuu washaanza kunipiga vizinga na nikaonesha kuvimudu japo kibishi.

Simu zao za kinafki husema kwamba "Mwanangu lini uje kunisalimia, miaka mingi hujaonana na na baba/mama yako hivi unajua najisikiaje huku nilipo fanya uje bana" hapo ni baada ya 10k kuingia kwenye cm ya mmoja wapo... Kimoyomoyo mimi hujosemea kwamba "Kama sio ninyi maisha yangu yasingekuwa ya taabu hivi, Acheni niwatumie kidogo changu hiki ili mjihisi nanyi mna mtoto" Ila kiukweli sijivunii wazazi wangu, Sasa jamani hata useme ukasalimie unaenda kulala wapi Baba hana nyumba yupo kwa bibi imagine kweli tuende wote tukarundikane kwa bibi mjukuu na baba yake kweli? au haya kwa mama, Kapanga room mbili mimi na midevu yangu nikaingie nikae kwenye bedroom ya mama sure?

Eeh Mungu wangu nisamehe kama nakosea ila acha niyatoe tu maana sina wa kunisikiliza nitakufa kwa maumivu haya niliyonayo, Sometimes inafikia nakufuru kuona ni bora mtu uwe hauna wazazi kuliko kuwa nao ambao wanachangia kukurudisha nyuma na kukuvunja moyo, Wazazi waliotangulia wenye ramani ila hawakuoneshi njia.

Mtu mnajua mmeshindwa kumhakikishia mwanenu maisha bora haya basi kaonesha anaweza kupambana basi muacheni still bado mnataka kumpa majukumu ya kuwazingatia ninyi sure?

Pole kwa magumu unayopitia. Ila inatakiwa ujue kuwa wazazi ni binadamu tu waliotangulia kuishi kabla yako, na wakakuzaa.

Hawana kingine cha ziada zaidi ya hicho.

Sasa na wewe umeshaishi-ishi duniani kwa hiyo umeshajionea kuwa kuishi kwingi sio lazima kuambatane na kufanikiwa kwingi. Umeshajionea wazee wengi maskini. Umeshajionea wala bata wa kutosha. N.k.

Wazazi ni binadamu wa kawaida tu ambao nao wanapambana na maisha. Kitendo cha wao kukuzaa wewe usidhani kwamba wao ni watu special sana tofauti na binadamu wengine. Mapambano yao inaelekea hayakufanikiwa sana ndo maana wapo kama walivyo.

Kuzaa ni kitu rahisi sana.

Mtu yeyote yule anaweza akatia mimba, na kubeba mimba. Mimba ni zao la starehe. Mimba haihitaji akili yoyote au jitihada yoyote. Inakuja tu kama magugu baada ya mvua. Kama ni kazi, basi kuzuia mimba ni kazi ngumu kuliko kubeba mimba. Angalau kuzuia mimba kunahitaji matumizi ya akili. Kunahitaji ukumbuke siku za hatari na kuchukua hatua mahsusi za kuepuka kukutana kimwili katika siku hizo.

Masuala ya Kuchezewa (Kurogwa) Achana Nayo Kabisa!

Angalia maisha ya watu wengi. Maskini ni wengi kuliko matajiri. Umaskini ni jambo la kawaida. Utajiri ndo jambo la kitofauti. Kwa hiyo kuanza kufikiria kuwa umerogwa ni akili ndogo hiyo. Inawezekana labda na wazazi wako waliishi kwa imani hizo za ushirikina ndo maana wameishia hapo walipoishia.

Ukiruhusu tu kuhusianisha changamoto zako za kimaisha na masuala ya kurogwa basi utayumba sana, na utatapeliwa sana na wajasiriamali wa imani kama vile akina Mwamposa na waganga wa kienyeji.

Jifunze kutumia akili. Mfano akili yako imekutuma kuwa kumiliki kiwanja ni jambo zuri, basi fanyia kazi hilo. Weka lengo la kumiliki kiwanja na uanze kudunduliza kununua hicho kiwanja popote pale kinakopatikana. Katika harakati ndo utafungua fursa zaidi za kufanikiwa. Hauhitaji kwenda mganga wala kununua mafuta ya upako ili kufanikisha malengo yako. Kuwa mkali tu na malengo yako. Kama hela unayoingiza ni ndogo, acha kabisa habari ya kuwatumia wazazi wako mpaka utakapofanikisha lengo lako la kumiliki ardhi. Wazazi wakikupigia kelele waambie unadunduliza kwa ajili ya kufanikisha malengo yako ya kiuchumi.

Usiruhusu kabisa imani za uchawi kichwani mwako, hata kama watu wangapi watakwambia nini. Maana watanzania kwa kuropoka tu hawajambo, lakini mwambie akupe ushahidi sasa.... utasikia tu "We kama huamini shauri yako, ila uchawi upo!"
 
Kuna watu wengi tumeshindwa kuelewa kuwa psychologically kuzungumza ni njia ya kupata relief, Kuna weng wamefanya action mbaya zaidi hata kuua au kujiua kwa kushindwa tu kuyaongelea yale yanayowasibu.
 
Mzazi wako ni mjinga ?
Mtu kuwa mzazi haifanyi ujinga wake kuisha Akilini na wala sio kigezo cha kuficha Uzembe wake

Kama mzazi ni mjinga ni mjinga tu.
haibadilishi uhalisia wa ujinga wake.

Unataka kutumia kigezo cha 'Uzazi" kama defence mechanism ya kutetea uzembe wa wazazi?




Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Pole kwa magumu unayopitia. Ila inatakiwa ujue kuwa wazazi ni binadamu tu waliotangulia kuishi kabla yako, na wakakuzaa.

Hawana kingine cha ziada zaidi ya hicho.

Sasa na wewe umeshaishi-ishi duniani kwa hiyo umeshajionea kuwa kuishi kwingi sio lazima kuambatane na kufanikiwa kwingi. Umeshajionea wazee wengi maskini. Umeshajionea wala bata wa kutosha. N.k.

Wazazi ni binadamu wa kawaida tu ambao nao wanapambana na maisha. Kitendo cha wao kukuzaa wewe usidhani kwamba wao ni watu special sana tofauti na binadamu wengine. Mapambano yao inaelekea hayakufanikiwa sana ndo maana wapo kama walivyo.

Kuzaa ni kitu rahisi sana.

Mtu yeyote yule anaweza akatia mimba, na kubeba mimba. Mimba ni zao la starehe. Mimba haihitaji akili yoyote au jitihada yoyote. Inakuja tu kama magugu baada ya mvua. Kama ni kazi, basi kuzuia mimba ni kazi ngumu kuliko kubeba mimba. Angalau kuzuia mimba kunahitaji matumizi ya akili. Kunahitaji ukumbuke siku za hatari na kuchukua hatua mahsusi za kuepuka kukutana kimwili katika siku hizo.

Masuala ya Kuchezewa (Kurogwa) Achana Nayo Kabisa!

Angalia maisha ya watu wengi. Maskini ni wengi kuliko matajiri. Umaskini ni jambo la kawaida. Utajiri ndo jambo la kitofauti. Kwa hiyo kuanza kufikiria kuwa umerogwa ni akili ndogo hiyo. Inawezekana labda na wazazi wako waliishi kwa imani hizo za ushirikina ndo maana wameishia hapo walipoishia.

Ukiruhusu tu kuhusianisha changamoto zako za kimaisha na masuala ya kurogwa basi utayumba sana, na utatapeliwa sana na wajasiriamali wa imani kama vile akina Mwamposa na waganga wa kienyeji.

Jifunze kutumia akili. Mfano akili yako imekutuma kuwa kumiliki kiwanja ni jambo zuri, basi fanyia kazi hilo. Weka lengo la kumiliki kiwanja na uanze kudunduliza kununua hicho kiwanja popote pale kinakopatikana. Katika harakati ndo utafungua fursa zaidi za kufanikiwa. Hauhitaji kwenda mganga wala kununua mafuta ya upako ili kufanikisha malengo yako. Kuwa mkali tu na malengo yako. Kama hela unayoingiza ni ndogo, acha kabisa habari ya kuwatumia wazazi wako mpaka utakapofanikisha lengo lako la kumiliki ardhi. Wazazi wakikupigia kelele waambie unadunduliza kwa ajili ya kufanikisha malengo yako ya kiuchumi.

Usiruhusu kabisa imani za uchawi kichwani mwako, hata kama watu wangapi watakwambia nini. Maana watanzania kwa kuropoka tu hawajambo, lakini mwambie akupe ushahidi sasa.... utasikia tu "We kama huamini shauri yako, ila uchawi upo!"
Ushauri makini kabisa huu...Umetema madini yote mkuu....[emoji817][emoji817][emoji817][emoji404]

Sio hawa wengine wanataka kutumia "uzazi" kama defence mechanism ya kuwatetea wazazi wajinga na wazembe...

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Pole sana Kwa kupitia hayo kwa kukosa maarifa ya wajibu wako kama mtoto kwa wazazi, endelea kuwapenda kama unavyowapenda ila Sasa tambua wajibu wako kama mtoto Ili uwe na amani ya moyo, wajibu wa mtoto kwa mzazi ni kumuheshimu na siyo kutunza mzazi wewe ulichokosea nikuanza kutunza wazazi wako ukiwa Bado mdogo, kulingana na jinsi ulivyoeleza baba na mama yako wanaishi tofauti pia bado hukupaswa kubeba majukumu ya kuwatunza maana jukumu la kutunza mke na watoto ni la baba Sasa baba yako alipaswa kujitunza yeye, mke wake na wewe mtoto na mama yako kama alihitaji matunzo basi alitakiwa kumuomba baba yako na siyo wewe.

Kwa vile umeshajitambua anza upya kutengeneza maisha yako na uchumi wako Ili uwe baba bora utakapo anzisha familia yako, Sasa basi watu wanaotakiwa kulelewa niwazee maana nguvu zao zimekwisha hawawezi kufanya kazi ndipo hapo wazee wenye watoto wao hulelewa na watoto ndo maana unaona Kila dini na serikali inasisitiza na kulazamisha baba atunze watoto wake kwa kuwajibika kuwaandalia maisha ya baadaye Ili waje wamsaidie uzeeni, hapo utaona matunzo ya mama yapo kwa mumewe na siyo mtoto ila baba akifariki mama anatakiwa kutunzwa na jamii kama mjane na watoto watatuzwa pia na serikali pamoja na jamii kama wajane ila baba hata akifiwa na mke bado anawajibu wa kufanya kazi Ili atunze familia mpaka uzee utapomfika ndo watoto wanachukua jukumu la kumlea, hivyo basi Fanya jukumu lako la kuwaheshimu wazazi na hayo yakuwapa vipato achana nayo mpaka muda wako wa kuwahudumia ufike.
 
Mie kwa mtazamo wangu naona mtoa mada .. sio kwamba analaumu wazazi au kutoheshimu wazazi.
Ni kwamba anatoa maumivu anayopitia kutoka kwa wazazi

wangapi n wazazi maskini lakini anakaa kwa upendo na mtoto mpaka mtoto anaona mzazi wangu pamoja na umaskini ila kanilea kwa upendo na anamwombea mwanae apate na anashukuru anachotumiwa.

Sasa wewe hujamlea mtoto kiupendo pia bado unajua kwa umri huu mwanangu angetakiwa kuwa shule ila kaamua apambane na maisha.. kwanini usimpe support kwa maneno ya upendo ,faraja na kumuombea apate zaidi.

Ila wanachofanya wazazi wa huyu kijana ni ubinafsi na kutojali ndo kinachoumiza zaidi sio umaskini...
Ifike muda mzazi utake responsibility ya matendo yako.

Haya huyo baba ye mbona hana msaada kwa mama yake ..mpaka analelewa na mzazi wake tena mzee..hamuoni kuwa ye ndo anamatatizo.

Kijana endelea kupambana.. saidia unapoweza usipoweza usijiumize.
Mwenyezi Mungu anajua dhamira yako kuliko sie binadamu.
Fact...[emoji817][emoji817][emoji817][emoji404]

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
NAWASHUKURU WOTE MNAOTOA MAONI YENU, KUNISHAURI, KUNIPA MOYO NA HATA WALE MNAOKOSOA PIA MAANA NAAMINI PIA HAKUNA MWENYE MAONI YENYE NIA MBAYA KWANGU KWANI YOTE YANA MATOKEO MAZURI KWA KUWA SIJAONA COMMENT YENYE LENGO BAYA HATA MOJA.... NAWASHUKURU SANA KWA MUDA WENU
 
Kaa utambue,
anayemsaidia mtu yeyete katika maisha , ni Mungu, mimi ninaendika hapa bila mzazi wangu alifungwa nikiwa darasa la 4. Alikuwa mfanyakazi na bosi kiaina. maisha yalibadilika kutoka kuchagua chakula hadi kukosa hata chakula kibaya cha kutosha.
lakini leo nachagua chakula tena. ni Mungu tu
 
Back
Top Bottom