akiwa muislam au mkristo kwetu sio shida sababu ni sehem ya historia yetu sisi watanganyika....tatizo mnaona dini Fulani ni muhimu kuliko maisha ya watu Fulani kwa ntindo huu tusahau maendeleo
Aisee,popote ninapo ninapo msoma Mohammed Said,kuna kitu kinapungua ndani yangu
Na ndio waliokomesha biashara ya utumwa iliyokithiri kipindi cha uislamuLusungo,
Wakoloni ndiyo waliokuja kuupa nguvu Ukristo wakishirikiana na Wamishionari.
Mkuu Remote kwa hiyo na wewe ile "One Ten" umeipanda sana kwenda Ipamba na njia panda?Mikate ya Lyalamo kwa masista na miwa ya Msukanzi?Ulanzi wa mto Lupalama na manesi wa Ipamba umehusika nao sana eee?Karibu tujadiliane na tuelimishane,kwa kweli mimi nimekuwa mwanafunzi mzuri tu wa Mohamed Said japo kuna maeneo huwa tunatofautiana...Asante mkuu barafu nipo napata vitu.. Pamoja na kusoma kwangu Tosamaganga kuna vingine sikuvijua
uko sahihi:Sikushangai nnajuwa wewe ni katika wale mliojazwa ujinga kuwa TANU iliasisiwa na Nyerere. Ukiusoma ukweli kutoka kwa Alama Mohamed Said roho inakuuma na unapungukiwa na la kusema, kwani ukweli ukidhihiri uongo hujitenga.
na ndio pia walio wachukua babu zetu utumwani kwa kuwapeleka mauritius na reunion katika mashamba ya miwa,na pia seychelles na comoros...waliiua biashara ya utumwa baada ya kuona mashine zina tija zaidi kuliko mitulinga ya watumwaNa ndio waliokomesha biashara ya utumwa iliyokithiri kipindi cha uislamu
babuzo gani hao?Ina matter sana tena sana kujuwa historia na kwanini ni Waislam tu walioipigania hii nchi kwa hali na mali.
Jee, hutaki kuelezwa kama babuzo walikuwa wasaliti?
barafu na huku uliwahi kuishi?duuuView attachment 331564
Mkuu BansenBurner na lusungo hii picha sasa ndio inathibitisha kuwa umisionari huko Iringa ulikuja baadae sana baada ya Uislamu kutamalaki.
Picha hii ni Parokia ya Tosamaganga yenye historia kama nilivyoeleza hapo juu,na nyumba hiyo nyeupe ndio ilikuwa ya mwanzo iliyojengwa kwa ajili ya Mafrateli Wazalendo(yaani weusi,Frateli ni kijana anayelelewa kuja kuwa Padre) na ilijingwa miaka ya mwanzo ya 1900 mpaka sasa ipo.Kushoto kwake ni Kanisa Kuu la Tosamaganga ambalo ndio yalikuwa makao makuu ya Jimbo la Iringa kabla ya kuhamishiwa Kihesa Iringa Mjini.
Huo mnara pembeni ulijengwa mwaka 1997 kwa ajili ya kumbukumbu ya Mapadre Wazungu na Waswahili(Wazalendo) tokea kazi ya umisionari ianze jimboni Iringa.Mpaka sasa Tosamaganga ni kati ya Parokia chache za Jimbo la Iringa zinazoendelea kukaliwa na Wamisionari wa Consolata wa kutoka Italia,parokia nyingine zinaendelea kuongozwa na mapadre waafrika wa Jimbo hilo.Hivyo Mzee Mohamed Said yupo sahihi katika uchambuzi wake,mimi kama mkristo mkatoliki ninakubaliana na uchambuzi wake kuhusu eneo hili.
Namuomba na FaizaFoxy maeneo ya kukubaliana na ukweli awe anakubali kama wenzake
Lusungo,
Wakoloni ndiyo waliokuja kuupa nguvu Ukristo wakishirikiana na Wamishionari.
watanzania watu waajabu sana hasa wewe,,wacha kuaibisha wenzako kwa uharaka uvivu usio na tija,,sadlymbona kuna maandishi ya kiarabu ?
watanzania watu waajabu sana hasa wewe,,wacha kuaibisha wenzako kwa uharaka uvivu usio na tija,,sadly
Asante sana mkuu na heshima kwako, hii ndio maana halisi ya historia. Nini, kwanii na lini? . Sio ushabiki tu usiokuwa na maana watu wanaoleta hapa. Kuna thread kama unaona huna mchango lazima ukae kimya ujifunze na sio kushabikia tu.Tatizo watu uvutana sana kwenye majadiliano na hasa linapoingizwa suala la dini.
Issue ya Mtwa Mkwawa kuwa muislamu nafikiri sio la kujadili hapa kwa facts zifuatazo:
1: waarabu "uislamu" waliingia east africa coast kuanzia karne ya 8 wakati Wazungu "ukristo" wameingia karne ya 16,rejea Wareno.
2: tofauti ya malengo waliyojia,nitafafanua
Waarab-lengo lao kuu ni biashara na kueneza uislamu.
Wazungu-lengo lao kuu lilikuwa ni kutafuta malighafi kutokana na industrial revolution huko europe,at first walikuwa na little information about africa "dark continent" na hapa ndo wale agents of colonialism wanapojitokeza na pia kueneza ukristo.
3: Waarabu walishirikiana vizuri sana na machifu akiwemo Mkwawa "slaves wengi waliuzwa na machifu wao kwa waarabu" tofauti na Wazungu na hasa wajeruman na ndo maana ilikuwa rahisi kwa waafrika kushirikiana na waarabu kuliko wazungu.
Sasa ebu tuangalie facts kumuhusu chief Mkwawa:-
1: alikuwa mfuasi wa dini za jadi "kama alivyo tu mshana jr"
2: baadae alisilimu na kuwa muislamu na kupewa jina la Abdallah.
...kwenye suala la kusilimu,mpwa wake aliyeitwa "Mpangile wa Ngindo msala sasi sinagopi" alimuonya kuwa ni hatari kwake maana alilazimika kuacha kuzitumia dawa za asili ambazo "wazee" waliamini ndo siri ya ushindi ya jeshi lao lililoitwa "Vanyamapelela"
3: dies at 43yrs of age.
4: he was womaniser, kuthibitisha hili tafuta jina la asili la mkwawa utajua. Lakini baada ya kusilimu alibaki na wake wa4 tu na wengine wakawa masulia wake.
5: he was slave trader.rejea ugomvi wake na chief Merere wa Usangu.
Hitimisho:
Suala la waislamu kuwa front line kupigana na wazungu "ukristo" sio ajabu kwa sbb zifuatazo:-
1: conflict of interest-Wazungu walikuwa wanakuja kuharibu maslahi yao,rejea abolision of slave trade.
2: puppet leaders-machief karibia wote waliwekwa kutetea maslahi ya Waarabu "uislamu"
Naomba niishie hapa,ikibidi kurudi nitarudi.
hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaHistoria ya Tanganyika naona kuna watu waliamua kuifuta kwa makusudi na kwa faida zao maana hata vita ya maji-maji namna tulivyojifunza shule na uhalisia ni tofauti
na ndiyo walioanzisha biashara ya utumwa( waingereza)Na ndio waliokomesha biashara ya utumwa iliyokithiri kipindi cha uislamu
Waarabu ndio walianzishana ndiyo walioanzisha biashara ya utumwa( waingereza)
HAPANA, labda wasomaji wengine watusaidie kuhusu hili sualaWaarabu ndio walianzisha