Siku nikifanikiwa kuwa Rais wa Tanzania; Mafisadi na familia zao zinazoneemeka kwa ufisadi, wataula wa chuya

Siku nikifanikiwa kuwa Rais wa Tanzania; Mafisadi na familia zao zinazoneemeka kwa ufisadi, wataula wa chuya

Duh!

Mkuu 'DEU87', nimeisoma mada yako kwa uangalifu hadi nilipofikia nilipofikia, kabla ya kushindwa kufika mwisho wake.

Umechanganya mambo mengi mno, kiasi kwamba mengi yanagongana.

Kuna mambo mazuri sana, kama hiyo namba 2,....

Lakini niseme wazi, mada yako inaweza kuwa mwanzo wa uchambuzi makini ni yapi yanatakiwa yafanyike kuinusuru Tanzania na unajisi inaofanyiwa nyakati hizi..

Pengine nitapata fursa ya kurudi na kufanya uchambuzi wa aina hiyo niuonao kwa upande wangu.

Lakini inabidi nikwambie hivi: Hakuna Mungu atakayekusubiri ufanye uamzi. Usije ukamsingizia Mungu kwa kushindwa kwako kufanya juhudi kutimiza malengo unayojiwekea mwenyewe.
Hili tu pekee, limekwishaonyesha udhaifu upande wako, hata kabla kazi ya kuinusuru Tanzania hujaianza.

Sasa kumbuka, ukishapata nafasi hiyo unayodhani itakuwezesha kuirekebisha Tanzania, visingizio kibao vitakuwa vikiibuka mara kwa mara, na hapo hapo ukimsingizia Mungu kutoruhusu.

Natumaini utakuwa umenielewa maana yangu.

Mwisho niseme, naungana nawe katika kuililia Tanzania yetu.
Well said Mkuu, ndo maana nikaona kuliko kukaa na haya mawazo mwenyewe, ngoja niyaweke kwa wanajamvi ili palipo na mapungufu, waweze kunirekebisha. Nashukuru umekuwa miongoni mwa hao.
Ahsante sana ndugu Kalamu.
Tuko pamoja.
 
Utakapokuwa Rais ndio siku utagundua kuna mizizi imejichimbia na ni mikubwa haigusiki na una sehemu ndogo tu ya kucheza nayo, ukifanya tofauti unajikuta mgeni rasmi katika bara usilolijua.
So sad!
 
Deep state (not Votes) reserve the rights of winning presidence

Deep state haipigiwi Kura

Deep state can change president the way and when they wish

nazungumzia deep state ya Belarus sio ya Uzbekistan
My Deep state will be God..
 
Mzena ileeeeee itakulaki ndani ya wiki mbili
 
Katiba ya sasa hivi itanisaidia kuwashughulikia mafisadi kwa uhuru zaidi pasipo kuogopa kupelekwa Mahakamani hata baada ya kuachia ngazi.. Maana Katiba ya sasa inatoa kinga ya Mh. Rais kutoshitakiwa kwa yote aliyoyafanya kipindi akiwa madarakani..
Bila shaka umenielewa ndugu yangu
Unamaanisha KATIBA ikibaki ilivyo itakupa GAP?? au ikibadirishwa unahisi siku ukiwa rais ndoto zako zitakuwa zimeshatimizwa na katiba??
 
MAGUFULI MPYA ATAKUWA KAFUFUKA,TANZANIA INAHITAJI RAIS SHUPAVU,JASIRI,MZALENDO NA MWENYE UDHUBUTU,

NINAJUA UKIWA NA SIFA HIZO,UTAKUWA UMEJITOA MHANGA MAISHA YAKO,NA USIKUOGOPE KIFO,
 
Habari wana Jamvi wa Jamii Forums, salamu nyingi kwenu.
Napenda kuwahakikishia kwamba nawapenda sana.
Ama baada ya salamu hizo za upendo, naomba moja kwa moja nidondoke kwenye mada.
Kama vile tunavyofahamu kwamba Mungu anaweza kumfanya mtu yeyote, wa hali yoyote, wakati wowote, kuwa yeyote, vivyo hivyo na mimi nina amini kwamba siku moja, Mungu akinifanikisha kuwa Rais wa nchi yangu ya Tanzania, pamoja na kwamba kwa sasa si mwanasiasa na wala si mtu maarufu na wala sitoki kwenye familia maarufu au tajiri; nitafanya haya yafuatayo kwa ajili ya usitawi wa Taifa langu na kwa watu wake pia;

1. Nitabadilisha mnyama anayeliwakilisha Taifa letu toka kuwa Twiga hadi kuwa Tai. Lengo ni kubadilisha mentality ya Watanzania toka kuwa watu wenye maono ya muda mfupi na mwendo wa taratibu kuelekea kwenye maendeleo hadi kuwa watu wenye kasi kubwa na maono ya muda mrefu. Tai haliwi. Hivyo hiyo itasaidia pia kutuondolea dhana potofu kwamba ili ule lazima uliwe kwanza hadi kwenye dhana ya kwamba unaweza kula tu bila kuliwa hata kidogo.

2. Nitawajengea Watanzania kuwa na moyo wa kufanya mambo makubwa kwa vitendo.

3. Nitaifanya Tanzania kuwa moja kati ya Mataifa makubwa kabisa duniani kijeshi, kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia n.k.

4. Nitawaheshimisha na kuwaenzi ipasavyo viongozi wote waliolitumikia Taifa letu kwa Uzalendo Mkubwa kuanzia kwa Hayati Julius Nyerere hadi kwa Hayati John Pombe Joseph Magufuli. Hii itawajengea moyo wa uzalendo viongozi wengine kuanzia ngazi ya chini kabisa hadi ngazi ya juu kabisa.

5. Viongozi wote ambao kwa namna moja ama nyingine walichangia kuliingizia Taifa letu hasara kwa namna yoyote, wawe hai au wamekufa, lazima watafidia hiyo hasara waliyolisababishia Taifa. Hii itajumuisha kutaifisha mali ambazo warithi wao walizirithi ziwe ndani au nje ya nchi. Pia adhabu ya kifungo kwa wale watakaokuwa hai itahusika. Hii itakuwa onyo kwa viongozi wengine wa kipindi hicho na wale watakaofuatia kuliongoza Taifa letu, ili waweze kuliongoza kwa uzalendo na kujitoa muhanga pia kwa ajili ya nchi yetu.

6. Idara ya usalama wa Taifa itaimarishwa kuanzia ngazi ya familia hadi ngazi za juu kabisa.

7. Serikali itawajibika kuwatunza katika nyanja zote (mavazi, malazi, chakula, elimu, afya n.k), watoto wote wa mtaani, watoto yatima, wazee wasio na uwezo wa kujitunza n.k. Kila raia lazima apewe mahitaji yote ya msingi na nchi yake.

8. Tenda zote za Serikali, zitapewa taasisi za serikali kama vile SUMA JKT, MAGEREZA, JWTZ n.k.

9. Nitajitahidi kupunguza tofauti kati ya matajiri na maskini kwa kuhakikisha keki ya Taifa inagawiwa sawa kwa wananchi wote.

10. Nitaboresha Taasisi zote za Serikali zionekane bora kuliko Taasisi binafsi.

NOTE: Serikali yoyote inawajibika kuhakikisha watu wake wote wanapata mahitaji yao yote ya msingi ikiwemo chakula, mavazi, sehemu nzuri za kuishi, usafiri, huduma za Afya, usalama wao na mali zao, mawasiliano, burudani n.k. Pia ni majukumu ya serikali kuhakikisha raia wanafurahia maisha na kujivunia nchi yao. Ni fedheha kwa serikali kwa raia wengi kuilalamikia kila siku kwa kushindwa kufanya kulingana na matarajio yao.

Ombi langu kwa Mungu ni kwamba hii Katiba tuliyo nayo sasa, iendelee kuwepo hadi huo muda ili niweze kufanya hayo yote niliyoyataja hapo juu.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Afrika Mashariki, Mungu ibariki Tanzania nchi yangu, Mungu ibariki Jamii Forum na members wake wote, Mungu nibariki mimi na familia yangu pia,

AMINA.
Nb: wapinzani watakuita dikteta
 
Na wee ukingia lazima ukwibeee tu

Ujinufaishe wewe na uko wako

Ova
 
Mzena ileeeeee itakulaki ndani ya wiki mbili
Mmmh!
Kazi ipo.
Mbona hakuna sehemu yoyote nimetukana mtu?
Kwa nini wanitafute?
Hata hivyo haya si ni mawazo yangu na Katiba yetu inaruhusu uhuru wa raia kutoa maoni yake?
Kingine, kabla hawajanitafuta, wawatafute kwanza moderators wangu waliouruhusu huu uzi.
 
Amina nakuombea ufanikiwe.

Katika hilo, usione haya, Kupambana mpaka na Viongozi wasowaaminifu wanaolamba Asali walioko kwenye vyombo vyetu vya Ulinzi na usalama.
Riwaya....heka heka za mbowe mlamba asali na chupa ya konyagi
 
Back
Top Bottom