Siku Nilipoiona Simu Kwa Mara ya Kwanza Odeon Cinema 1955 au 1956 au Nyuma ya Hapo Kidogo Sijavuka Miaka 4

Siku Nilipoiona Simu Kwa Mara ya Kwanza Odeon Cinema 1955 au 1956 au Nyuma ya Hapo Kidogo Sijavuka Miaka 4

Ulikatazwa kwenu kuwa na ukaribu na watu wasiyo wa imani yako katika makuzi, au hukumbuki kuwahi kuwa na urafiki na mtu yoyote asiye wa imani yako? Inakuwaje kwa mtu ambaye umesoma shule za kanisa siyo chini ya mbili? Hiyo ya msafara wa Dada ws Malkia mtoto anaweza kuweka kwenye long term memory sababu ni tukio la kipekee kwa maana ya umati kukusanyika pembezoni mwa barabara, magari mengi na Mhusika Mkuu kuwa Mzungu wa kike. Naamini hata ingekuwa Ulaya enzi hizo watoto wa umri huo wengi wana kumbukimbu ya kumtupia macho kwa mara yao watu wenye ngozi nyeusi.
Kumbe Mzee amesoma katika shule za Kanisa?
 
SIKU NILIYOIONA SIMU KWA MARA YA KWANZA ODEON CINEMA 1955 AU 56 AU NYUMA YA HAPO KIDOGO SIJAVUKA UMRI WA MIAKA MINNE

Nakumbuka kama jana vile.

Nilikuwa mgonjwa na baba yangu mdogo Mzee Issa akanichukua kunipeleka hospitali.

Ilikuwa usiku lakini si usiku mkubwa kiasi cha saa moja hivi.

Nina hakika na hili kwa kuwa Mzee Issa kanibeba tunatoka nyumbani Mtaa wa Kipata (Sasa Kleist Sykes Street) kwa miguu na nawaona watu mtaani njia nzima hadi tunafika New Street tunavuka Mnazi Mmoja tunapita kushoto tunaelekea Sultan Street (Libya Street).

Hapa Mnazi Mmoja palikuja kujengwa Mnara wa Uhuru. Siku zile Mnazi MMoja ile ilikuwa uwanja mtupu hauina chochote ni mchanga mtupu.

Tunaingia Ring Street (Sasa Jamhuri Street) tunapita pembeni ya Odeon Cinema tunaingia mitaa ya Uhindini jirani na Msikiti wa Sunni kulikuwa na hospitali maarufu sana ya daktari wa Kihindi nakumbuka ingawa sina hakika jina lake lilikuwa kama Dr. Koya.

Mama zetu wakimsifia sana kwa kutibu watoto.

Hii hospital imedumu hapo kwa miaka mingi hadi mimi nimekuwa mtu mzima nikipita pale nikiiona.

Baada ya kutibiwa baba yangu mdogo Mzee Issa miaka ile alikuwa kijana akawa ananirudisha nyumbani.

Ndipo tulipopita tena Odeon Cinema tukaingia ndani kwenye call box (kibanda cha simu) kilichokuwa pale ndani.

Baba yangu alikuwa kazini akifanyakazi Telephone Exchange.
Jumba hili hadi leo lipo.

Mzee Issa akatia pesa kisha akapiga simu kuzungumza na baba yangu kumfahamisha kuwa kanipeleka hospitali na nimetibiwa.

Mzee Issa akanipa simu nimwamkie baba yangu.
Sikuweza kuzungumza.

Miaka mingi ikapita.

Siku moja nikamhadithia Mzee Issa habari hii.
Alishtuka.

Akawa kashangaa kisha akaniuliza, ''Mohamed unakumbuka habari hii?''

326990267_3458502591073338_625044799509994387_n.jpg

327556309_1913726512302146_4804005542629042379_n.jpg

327246206_488592410128550_2450343156164433652_n.jpg


Shikamoo Baba, Mungu akupe maisha marefu miaka 100+ inshallah iwe heri kabisa
 
Kumbe Mzee amesoma katika shule za Kanisa?
Azarel,
Naam nimeanza darasa la kwanza Lutheran Primary School Moshi mwaka wa 1958.

Hapakuwa na shule tukisoma ndani ya kanisa.

Niko kwenye simu nikiwa kwenye laptop nitakuwekea picha ya hilo kanisa In Shaa Allah.

Kisha nikasoma shule nyingine ya kanisa St. Joseph's Convent School Dar es Salaam.

Nitakuwekea picha.
 
Ulikatazwa kwenu kuwa na ukaribu na watu wasiyo wa imani yako katika makuzi, au hukumbuki kuwahi kuwa na urafiki na mtu yoyote asiye wa imani yako? Inakuwaje kwa mtu ambaye umesoma shule za kanisa siyo chini ya mbili? Hiyo ya msafara wa Dada ws Malkia mtoto anaweza kuweka kwenye long term memory sababu ni tukio la kipekee kwa maana ya umati kukusanyika pembezoni mwa barabara, magari mengi na Mhusika Mkuu kuwa Mzungu wa kike. Naamini hata ingekuwa Ulaya enzi hizo watoto wa umri huo wengi wana kumbukimbu ya kumtupia macho kwa mara yao watu wenye ngozi nyeusi.
Mbona una shari sana ndugu
 
Azarel,
Naam nimeanza darasa la kwanza Lutheran Primary School Moshi mwaka wa 1958.

Hapakuwa na shule tukisoma ndani ya kanisa.

Niko kwenye simu nikiwa kwenye laptop nitakuwekea picha ya hilo kanisa In Shaa Allah.

Kisha nikasoma shule nyingine ya kanisa St. Joseph's Convent School Dar es Salaam.

Nitakuwekea picha.
Nimefurahi.
 
Nimefurahi.
Azarel,

Hizo picha mbili ni sehemu hiyo niliyosimama moja ila ''angle'' tofauti.

276306905_1143203219760388_4213218925397671151_n.jpg

Lutheran Primary School Moshi picha hii nilipiga 1989
277295468_1143204003093643_5580320659638863921_n.jpg

Picha hii nimepiga 2021

1675916373838.jpeg

Waliosimama kulia wa kwanza ni mimi na aliyechutama chini yangu sasa ni Chief wa Siha Edward Jonathan Kidaha, Waliosimama wa kwanza kushoto ni Gulamabbas Jivraj huyu alikuwa na akili si za kawaida anafuatia jina lake Israel tukikaa desk moja baba yake alikuwa Balozi wa Israel Tanzania.

Anaefuatia ni Charles Mesquita sina la kusema kuhusu huyu. Alikuwa hasemi mkimya si kawaida kati yake yeye na Gulamabbas sijui nani alikuwa zaidi kwa mbongo.

Inataka muda kulueleza hili darasa.
Mwangalie Chief Kidaha anaefuatia ni Razia au Salma (twin sisters) ukimruka anaefuatia Asya Kharusi kisha Bhatia mwingine. Sikuweza kumtambua nani Razia nani Salma miaka minne tuliokuwa darasa moja kuanzia Form 1 D hadi tunamaliza Form IV. Hili darasa lilikuwa likiongoza kwa kila kitu hapo shule.​
 
Azarel,

Hizo picha mbili ni sehemu hiyo niliyosimama moja ila ''angle'' tofauti.

276306905_1143203219760388_4213218925397671151_n.jpg

Lutheran Primary School Moshi picha hii nilipiga 1989
277295468_1143204003093643_5580320659638863921_n.jpg

Picha hii nimepiga 2021

View attachment 2511114
Waliosimama kulia wa kwanza ni mimi na aliyechutama chini yangu sasa ni Chief wa Siha Edward Jonathan Kidaha, Waliosimama wa kwanza kushoto ni Gulamabbas Jivraj huyu alikuwa na akili si za kawaida anafuatia jina lake Israel tukikaa desk moja baba yake alikuwa Balozi wa Israel Tanzania.

Anaefuatia ni Charles Mesquita sina la kusema kuhusu huyu. Alikuwa hasemi mkimya si kawaida kati yake yeye na Gulamabbas sijui nani alikuwa zaidi kwa mbongo.

Inataka muda kulueleza hili darasa.
Mwangalie Chief Kidaha anaefuatia ni Razia au Salma (twin sisters) ukimruka anaefuatia Asya Kharusi kisha Bhatia mwingine. Sikuweza kumtambua nani Razia nani Salma miaka minne tuliokuwa darasa moja kuanzia Form 1 D hadi tunamaliza Form IV. Hili darasa lilikuwa likiongoza kwa kila kitu hapo shule.​
Kumbukumbu nzuri
 
SIKU NILIYOIONA SIMU KWA MARA YA KWANZA ODEON CINEMA 1955 AU 56 AU NYUMA YA HAPO KIDOGO SIJAVUKA UMRI WA MIAKA MINNE

Nakumbuka kama jana vile.

Nilikuwa mgonjwa na baba yangu mdogo Mzee Issa akanichukua kunipeleka hospitali.

Ilikuwa usiku lakini si usiku mkubwa kiasi cha saa moja hivi.

Nina hakika na hili kwa kuwa Mzee Issa kanibeba tunatoka nyumbani Mtaa wa Kipata (Sasa Kleist Sykes Street) kwa miguu na nawaona watu mtaani njia nzima hadi tunafika New Street tunavuka Mnazi Mmoja tunapita kushoto tunaelekea Sultan Street (Libya Street).

Hapa Mnazi Mmoja palikuja kujengwa Mnara wa Uhuru. Siku zile Mnazi MMoja ile ilikuwa uwanja mtupu hauina chochote ni mchanga mtupu.

Tunaingia Ring Street (Sasa Jamhuri Street) tunapita pembeni ya Odeon Cinema tunaingia mitaa ya Uhindini jirani na Msikiti wa Sunni kulikuwa na hospitali maarufu sana ya daktari wa Kihindi nakumbuka ingawa sina hakika jina lake lilikuwa kama Dr. Koya.

Mama zetu wakimsifia sana kwa kutibu watoto.

Hii hospital imedumu hapo kwa miaka mingi hadi mimi nimekuwa mtu mzima nikipita pale nikiiona.

Baada ya kutibiwa baba yangu mdogo Mzee Issa miaka ile alikuwa kijana akawa ananirudisha nyumbani.

Ndipo tulipopita tena Odeon Cinema tukaingia ndani kwenye call box (kibanda cha simu) kilichokuwa pale ndani.

Baba yangu alikuwa kazini akifanyakazi Telephone Exchange.
Jumba hili hadi leo lipo.

Mzee Issa akatia pesa kisha akapiga simu kuzungumza na baba yangu kumfahamisha kuwa kanipeleka hospitali na nimetibiwa.

Mzee Issa akanipa simu nimwamkie baba yangu.
Sikuweza kuzungumza.

Miaka mingi ikapita.

Siku moja nikamhadithia Mzee Issa habari hii.
Alishtuka.

Akawa kashangaa kisha akaniuliza, ''Mohamed unakumbuka habari hii?''

326990267_3458502591073338_625044799509994387_n.jpg

327556309_1913726512302146_4804005542629042379_n.jpg

327246206_488592410128550_2450343156164433652_n.jpg


Kwa hii picha nashawishika kusema "familia yako ilikuwa moja ya zile familia bora" kwa wakati huo. Familia chache zilikuwa na exposure ya kuweka kumbukumbu kwenye picha. Aisee, memory nzuri sana. Ingawa baba yako mdogo imebidi kumkumbusha.
 
Kwa hii picha nashawishika kusema "familia yako ilikuwa moja ya zile familia bora" kwa wakati huo. Familia chache zilikuwa na exposure ya kuweka kumbukumbu kwenye picha. Aisee, memory nzuri sana. Ingawa baba yako mdogo imebidi kumkumbusha.
Jay...
Familia ya kawaida tu ya Kariakoo.
Picha hii alinipiga Mohamed Shebe.

Mohamed Shebe alikuwa na studio yake mkabala wa nyumba aliyokuwa akikaa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed Mtaa wa Kipata na Livingstone.

Mohamed Shebe ndiye mpiga picha wa kwanza kupiga picha za harakati za TANU na kumpiga picha Nyerere mapambano ya kudai uhuru yalipoanza mwaka wa 1954.
 
Jay...
Familia ya kawaida tu ya Kariakoo.
Picha hii alinipiga Mohamed Shebe.

Mohamed Shebe alikuwa na studio yake mkabala wa nyumba aliyokuwa akikaa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed Mtaa wa Kipata na Livingstone.

Mohamed Shebe ndiye mpiga picha wa kwanza kupiga picha za harakati za TANU na kumpiga picha Nyerere mapambano ya kudai uhuru yalipoanza mwaka wa 1954.
Ahsante kwa maelezo. Ila ndio hivyo, sidhani kama zile nyumba zilizo na historia ya harakati za Uhuru bado zipo, naamini zilishavunjwa kupisha majengo ya kisasa.
 
Mzee sikukuu kafariki nadhan 2020 au 2019 nyumbani kwake Sinza. Mwanae ni rafki yangu sana..

Miaka ya 1990 nilipata kuishi mtaa Gerezani Kariakoo

Saigon ndio pahara pekee nilikuwa nawaona. Jakaya Kikwete.. Abubakary Mgumia marehemu. Mansor Margam marehemu. Ditopile Mzuzuri Marehemu. Ismail Rage. Na wengine wengi tu..
Yanga ilikuwa inapata tabu sana kwa Sigara ya Marehemu Mansoor Magram.
 
Ahsante kwa maelezo. Ila ndio hivyo, sidhani kama zile nyumba zilizo na historia ya harakati za Uhuru bado zipo, naamini zilishavunjwa kupisha majengo ya kisasa.
Jayjay,
Kuna kipindi kinaitwa Zumari nimefanya na Jaffar Mponda nilisimama nje ya nyumba ya Abdul Sykes Mtaa wa Stanley (Max Mbwana) na Sikukuu nyumba ambayo Julius Nyerere aliishi baada ya kuacha kazi ya ualimu 1955.

Nyumba hii haipo badala yake zimejengwa apartments na ofisi.

Nilisimama nje ya jengo hili nikaeleza historia ya Julius Nyerere alipofika hapo 1952 na yote yaliyopitika ndani ya nyumba ile, uchaguzi wa Arnautoglo 1953 hadi kuundwa kwa TANU 1954 na safari ya UNO 1955.

Tukaenda Mtaa wa Kipata (Kleist Sykes) na Sikukuu ilipokuwq nyumba ya Clement Mtamila mahali ulipofanyika mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU kujadili kujiuzulu kazi Nyerere.

Nyumba zote hizo hazipo.

311576246_1279377356142973_6883545766458833396_n.jpg

Nyumba ya Abdul Sykes ilivyo sasa
311583521_1279375842809791_4138275745224367550_n.jpg

Nyumba ya Abdul Sykes ilivyokuwa katika miaka ya 1980 baada ya ukarabati
Hii ndiyo ilikuwa nyumba aliyokaa Julius Nyerere mwaka wa 1955 baada ya kuacha kazi ya Ualimu
311611445_1279311499482892_4691662268709046487_n.jpg

Mbele ya nyumba ya Abdul Sykes nikifanya kipindi cha Nyerere Day 2022​
 
Back
Top Bottom