Siku Nilipoiona Simu Kwa Mara ya Kwanza Odeon Cinema 1955 au 1956 au Nyuma ya Hapo Kidogo Sijavuka Miaka 4

Siku Nilipoiona Simu Kwa Mara ya Kwanza Odeon Cinema 1955 au 1956 au Nyuma ya Hapo Kidogo Sijavuka Miaka 4

Njabu...
NImezaliwa Mtaa wa KIpata (Sasa Kleist Sykes).

Nikitoka nyumbani kwetu kuelekea Mnazi Mmoja nakata Mtaa wa Swahili kushotom kuna nyumba ya Hassan Machakaomo.

Hassan Machakaomo baba yake Machakaomo alikuwa Mzulu aliyekuja German Ostafrika na Sykes Mbuwane na akina Plantan.

Machakaomo alikuwa mmoja wa viongozi wa Young Africans mwaka wa 1948.

Nakuwekea picha ya viongozi wa Young Africans wakiwa na Abeid Amani Karume na Mtoro Rehani mwaka wa 1948.

Hassan Machakaomo ni huyo wa kwanza aliyekaa chini.
Mtafute Karume.

Nakatiza Mtaa wa Sikukuu kulia kwenye kona na Kipata kuna nyumba ya Clement Mohamed Mtamila aluyekuwa Secretary wa TAA President akiwa Mwalimu Thomas Plantan.

Uongozi huu ndiyo uliopinduliwana Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kwa msaada wa Schneider Abdillah Plantan wakaingia madarakani Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes Secretary 1950.

Baada ya hapo navuka Mtaa wa Livingstone kulia ndipo ilipokuwa studio ya Mohamed Sheba aliyepiga picha nyingi sana za siku za mwanzo za TANU na kumpiga picha Julius Nyerere.

Baadhi ya picha hizi zipo katika Maktaba yangu kwa hisani ya mwanae Mbaraka Shebe.

Sasa nafika mwisho wa Kipata kushoto kuna nyumba ya Sheikh Abdallah Simba Liwali wa Songea na rafiki ya babu yangu, Salum Abdallah.

Babu yangu kaishi nyumba hii hadi 1947 alipohamia Tabora.
Mkabala wa nyumba hii ni nyumba ya Kleist Sykes.

Naingia New Street (Sasa Lumumba Avenue).
Naijua Gerezani na wakazi wake.

Hii ndiyo ilikuwa dunia yangu.

Njabu...
Kushoto waliokaa Hassan Machakaomo, Selemani Mwinyimadi Chambuso, Mohamed ''Mabosti'' Sultan.

Huyu Hassan Machakaomo baba yake Mzee Machakaomo alikuwa Mzulu aliingia Tanganyika na Herman Von Wissman mwishoni mwa 1800 kama askari mamluki pamoja na akina Affande Plantan na Sykes na wakaishi jirani Mtaa wa Kipata.

Mohamed Sultan alipewa jina la ''Mabosti,'' kwa ajili ya unadhifu wake katika mavazi na mbwebwe zake za kijana mtanashati.

Mohamed Sultan alipata kuwa President wa Young Africans.

Waliokaa kwenye viti kushoto wa kwanza jina halikupatikana, Rajab Swedi, Khamis Shari, Abeid Amani Karume, Kondo Salum Kipwata, Mtaruke Mangara, aliofuatia jina halikupatikana.

Kondo Kipwata inaaminika ndiye Mwafrika wa kwanza Dar es Salaam kununua radio wakati utangazaji wa radio ulipoanza mwaka wa 1952.

Watu walikuwa wakikusanyika barazani kwake Ilala kumsikiliza Yahya Hussein wakati huo mtoto mdogo akisoma Qur'an kupitia Sauti ya Unguja.

Kondo Kipwata alikuja kuwa President wa Young Africans katika miaka ya 1960 tena kwa kulazimishwa na wanachama na wapenzi wa Yanga baada ya kuwa kila mechi wanafungwa na mahasimu wao Sunderland.

Kondo Kipwata alikuwa haendi kuangalia mpira wa Yanga na Sunderland akisikiliza nyumbani kwake kwenye radio.

Mjukuu wa Affande Plantan na mtoto wa Mwalimu Thomas Plantan, Bi. Maunda Plantan alikuwa mwanamke wa kwanza kutangaza Sauti ya Dar es Salaam tena alikuwa English Service.

Waliosimama Abdallah Mzee, Chonjo Mwinchande Digendo, Juma Ismail, Shaaban Bajuni, anaefuatia jina halikupatikana, Khamis Mjinga, Selemani Mohamed, Mtoro Rehani, Mangara Tabu Mangara na Ali Majaliwa.

Mangara Tabu alikuwa President wa Yanga katika miaka ya 1960 mwishoni hadi 1970 mwanzoni na katika uongozi wake Yanga ilifanya makubwa pamoja na kujenga club hiyo iliyopo Jangwani kwa msaada wa Karume.

Mwangalie Mangara Tabu na Karume utaelewa urafiki wao umetokea wapi.
 
Ulikatazwa kwenu kuwa na ukaribu na watu wasiyo wa imani yako katika makuzi, au hukumbuki kuwahi kuwa na urafiki na mtu yoyote asiye wa imani yako? Inakuwaje kwa mtu ambaye umesoma shule za kanisa siyo chini ya mbili? Hiyo ya msafara wa Dada ws Malkia mtoto anaweza kuweka kwenye long term memory sababu ni tukio la kipekee kwa maana ya umati kukusanyika pembezoni mwa barabara, magari mengi na Mhusika Mkuu kuwa Mzungu wa kike. Naamini hata ingekuwa Ulaya enzi hizo watoto wa umri huo wengi wana kumbukimbu ya kumtupia macho kwa mara yao watu wenye ngozi nyeusi.
Njabu...
Unataka kuwajua marafiki zangu udogoni?
Angalia picha hapo chini:

1675015364898.jpeg

Kulia waliosimama: Mohamed Said, Yusuf Zialor, Kleist Sykes, Bubby Bohari, Abdallah Tambaza, Waliochutama kulia: Abdul Mtemvu, Wendo Mwapachu na Kaisi 1968.
 
Maso...
Mimi nina miaka 70 Alhamdulilah.

Kuwa niko "active kiakili," labda maana sina hakika nikipenda kusoma na kuandika toka udogoni.

Nguvu ya kuukwea Kilimanjaro sina.

Labda kitu kimoja ni kuwa sijatumia tumbaku wala ulevi wa aina yeyote toka kuzaliwa.
Dah mzee mimi nina miaka 28 ila nimeanza kuvuta fegi, bangi na kunywa viroba tokea nina miaka 15 hivi nitafika 70 kweli mzee wangu?

Ila mzee Mohamed Said wewe ni tunu katika taifa hili huwa nafurahi sana nikiona uzi wako.
 
Wapi hapo kuna ushabiki wa kidini?
Twilu...
Tufahamiane.

Nahisi tunaingia katika mitihani baina yetu kukoseana adabu na kutishana pasi na sababu kwa kuwa hatujuani:

PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES

The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.

The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006

Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.

Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.

Uamuzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.

Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam.

Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam

Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigani Uhuru wa Tanganyika Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaaam

Watu Mashuhuri Katika Kuulingania Uislam Tanzania, Sheikh Ilunga, Ibn Hazm Media Centre 2018, Dar es Salaam

Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania, Ibn Hazm Media Centre, 2018, Dar es Salaam

The School Trip to Zanzibar, Africa Proper Education Network 2020, Dar es Salaam

Rajabu Ibrahim Kirama, Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam, Readit, 2020, Dar es Salaam

In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).

Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).

Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)

The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).

Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).

The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).

Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).

Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).

Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).

Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).

Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.

Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.

Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.

Awards: Several Awards

Visiting Scholar: (2011)

University of Iowa, Iowa City, USA

Northwestern University, Chicago, Illinois, USA

Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.

OTHER COUNTRIES VISITED

Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.


1675016309422.jpeg

Northwestern University, Evanston Chicago​
 
Sisi wafia dini ya islamia brain zetu haiziweki kwenye kumbukumbu jina lolote la mkristo.
mfia dini hakumbuki hata alivyokuwa anapewa mikate na siagi kanisani na mapocho pocho mengine.....ndo maana ulikuwa hakauki kwenye vibaraza vya kanisa.

Nao ndo wamemsomesha huoni akitoa airtime,ameamua kuwa selective muslim extremist.

kihoro kitakua babu mudi!
 
mfia dini hakumbuki hata alivyokuwa anapewa mikate na siagi kanisani na mapocho pocho mengine.....ndo maana ulikuwa hakauki kwenye vibaraza vya kanisa.

Nao ndo wamemsomesha huoni akitoa airtime,ameamua kuwa selective muslim extremist.

kihoro kitakua babu mudi!
Luku...
Sijakutusi wala kukukejeli.

Nakuomba nawe unipe heshima yangu.

La unaona hilo ni gumu kwako basi acha mjadala na mimi.

Siko hapa kutukanana.
 
Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.

Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.

Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.

Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.

View attachment 2497529
Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).

Saigon katika 2020s:
View attachment 2497531
Kulia: Marehemu Nusura Faraj, Manzi, Marehemu Abdulkarim Shah (BuljiI) chini kulia Shariff Pazi na Mshike.
Mzee sikukuu kafariki nadhan 2020 au 2019 nyumbani kwake Sinza. Mwanae ni rafki yangu sana..

Miaka ya 1990 nilipata kuishi mtaa Gerezani Kariakoo

Saigon ndio pahara pekee nilikuwa nawaona. Jakaya Kikwete.. Abubakary Mgumia marehemu. Mansor Margam marehemu. Ditopile Mzuzuri Marehemu. Ismail Rage. Na wengine wengi tu..
 
Mzee sikukuu kafariki nadhan 2020 au 2019 nyumbani kwake Sinza. Mwanae ni rafki yangu sana..

Miaka ya 1990 nilipata kuishi mtaa Gerezani Kariakoo

Saigon ndio pahara pekee nilikuwa nawaona. Jakaya Kikwete.. Abubakary Mgumia marehemu. Mansor Margam marehemu. Ditopile Mzuzuri Marehemu. Ismail Rage. Na wengine wengi tu..
Alex,
Nani kafariki?
 
Mokaze,
Alhamdulilah sikuwahi kunywa ulevi wala kuvuta sigara.

Wakati niko kazini mtihani wangu mkubwa ulikuwa katika party ambazo ilibidi nitayarishe.

Nilikuwa Idara ya Masoko na lazima wateja wetu tuwafanyie takrima tukiwa na mikutano mchana tunawapa lunch na pombe kidogo.

Ikiwa jioni dinner na pombe hadi wachoke wenyewe.

Sasa linapokuja suala la vinywaji nikitaabika sana.
Mimi ndiye nilikuwa paymaster.

Nakumbuka kisa kimoja wakubwa zangu wananiuliza, ''Mohamed mmeweka Safari Beer peke yake?''

Mimi nikamjibu ndiyo.

''Kwani hakuna bia za maana mbona mnatufedhehesha kwa wageni wetu?

Ndipo nilipojua kuwa beer zina daraja zake kutokana na brand mfano Castle, Amstel, Stella Artoir nk.

Hii beer ya Stella kwa mara yangu ya kwanza niliijua Alexandria, Misri.
Baadae nikaja kuiona imeletwa Dar es Salaam na ilikuwa maarufu sana.

Lakini Misri ulevi unauzwa kimya kimya hautangazwi na lazima ufike hoteli maalum si kama kila mahali utapata pombe.

Wakubwa zangu wakawa wanasema, ''Huyu Mswahili anajua wapi mambo haya.''

Lakini mara moja nikamtafuta Manager wa hotel nikamwambia afanye haraka sana alete beer zingine zenye majina.

Nikawa nimejifunza.
Mtihani.
Ni Stella Artois, nakumbuka Mzee alikuwa anakuja nazo kutoka Airport ya KLM (KIA) baadae hii kampuni ikaanza kutengeneza Plisner Beer ambayo watanganyika wanamudu bei
 
Muulize huyo Mzee, kule St Joseph shule ya Kanisa, katikati ya jiji, alikokuwa anasoma miaka mingi, hakufahamiana au kujenga urafiki na mtu yeyote asiye Muislamu? Hata Baniani?
He ll never mention one, They y'll Kafir to him

As a smarter dude, I knew his intention[emoji23]
 
Alipokuwa na miaka 4 kakumbuka hadi alipokatiza mtaa wa Kleist Sykes SIKU MOJA?!! Mitaa yote ya Kariakoo hadi kufika Odeon Cinema ya wakati huo kaicha.
• Kleist Sykes street

• Abdul Sykes & Dosa Aziz

End of an Old Tale...!!!
 
Back
Top Bottom