Siku nimebaki mimi na kipa tu na ghafla mpira ukugeuka sufuria la hela ndipo nilipoamini uchawi upo!

Siku nimebaki mimi na kipa tu na ghafla mpira ukugeuka sufuria la hela ndipo nilipoamini uchawi upo!

WhoWeBe

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
2,299
Reaction score
4,282
Nilikuwa naupiga mwingi kiasi, kabla sijazeeka.

Mtama, Lindi kilikuwa kituo changu cha kwanza cha kazi baada ya kuajiriwa. Kama kawaida ya ujana, nikajichanganya kitaa na kufahamika mitaa ile na vijiji vya jirani vyote kuhusu usakataji wangu wa kabumbu. Kule, kabumbu (ligi) linapigwa sana baada ya mavuno.

Siku moja nikapata 'dili' la kwenda kushiriki ligi fulani huko kijiji fulani vilivyopo juu huko Makonde Plateau kijiji fulani km unaelekea tandahimba. Huko nikakuta kuna vilabu viwili vyenye majina makubwa ya timu za epl; Chelsea na Aston villa😂😂😂😂. Mimi niliajiliwa na Chelsea (kwa makubaliano yetu).

Kufupisha habari, nilifanikiwa kwenda na timu hadi fainali. Siku ya fainali ilipofika ulipigwa mpira si wa kawaida. Ngoma ilikuwa ngumu mno hadi dakika za mwisho. Ghafla, dakika za lala salama, bila kurarajia nikajikura mimi na kipa tu. Watu wote walijua, kutokana na mambo yangu, kazi imeisha na kuanza kushangilia.

Ebwana eee, huwezi kuamini ile nataka kuachia shuti nashangaa sioni mpira na badala yake naona sufuria jeupee kubwa kiasi limejaa hela, nikashikwa na bumbuazi nisijue nifanye nini.

Mara akili ikaniambia 'Acha ujinga' okota hela hizo. Nikaokota. Nilipomaliza kuokota tu nasikia filimbi ya refa na hapo kila kitu kikarudi katika hali ya kawaida, yaani fahamu zangu zikarudi. Kwa mshangao wangu, nikajikuta nimeshikilia ule mpira na hivyo ikabidi upigwe kuelekea kwangu. Kila mmoja akabaki ananishangaa pasipo kuamini.

Mwishowe mechi tukapoteza na huo ndo ukawa mwisho wangu wa kushiriki habari za mpira. Nilikoma!
 
Bongo noma sana. Mimi nilipenyezewa assist Moja safi wakati wakati nakimbia kuelekea kwa kipa nageuka nyuma kujua beki anakujaje. Badala ya kuona beki namuona fisi ndo ananikimbiza kapanua mdomo kwa kunitafuna. Nilikimbia nikaacha mpira na kipa kumpita mpaka kwa mashabiki. Kufika kwa mashabiki simuoni fisi nikaacha mpira kabisa wa huko vijijini
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
Hapo ushirikina upo wapi mana wewe hukuwa refa wa mchezo. Leta uzoefu wako kama wenzio hapo juu.
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
Hatari sana
 
Haaaahaaa a.. Umenikumbusha nikiwa nacheza ligi daraja la tatu mkoa wa dodoma .. Tulikutana na walugaluga fulani kutoka Mlali huko.
.. Halftime tulikula 4 BILA.. Kumbe kuna mganga wao nje akienda chooni tu hapo karibu na uwanja akitoka tu.. Uku chuma kinaingia.... Tulisanuliwa hatukuamini.. Ikabidi viongozi wamuangalie second half.. Kweli akaingia chooni.. Alivotoka mda sio mrefu tupigwa la 5..wakaamini..ikabidi jamaa azuiwe kjingia chooni na wahuni... Game hii tulikula 5-0.
 
Mobutu alipeleka timu kombe la dunia na waganga kibao.

Nini kilitokea?
Ile ya mobotu ilikua comedy, ukiangalia documentary za fifa kipindi Hiko wachezaji wake hawajui hata Sheria za mpira, ikiwekwa faulo kuelekea langoni mwao refa akipiga filimbi linatoka beki lao kwenye ukuta linaenda butua mpira, yaani vurugu tupu.... Sasa hata kama we ndo mganga watu kama hao unawasaidia vipi
 
Ile ya mobotu ilikua comedy, ukiangalia documentary za fifa kipindi Hiko wachezaji wake hawajui hata Sheria za mpira, ikiwekwa faulo kuelekea langoni mwao refa akipiga filimbi linatoka beki lao kwenye ukuta linaenda butua mpira, yaani vurugu tupu.... Sasa hata kama we ndo mganga watu kama hao unawasaidia vipi
Sasa kile alichofanya yule beki si ndiyo ilibidi wafanye wapinzani baada ya kulogwa?
 
Kombe la uzinduzi wa Wilaya ya Mvomero mwaka 2001 uwanja wa shule ya Msingi Mvomero. Timu za ndondo maarufu za Wilaya ya Mvomero kama Gheto boys na Asec za kijiji cha Mvomero, Wami Magereza, Timu za Dakawa na Turiani. Fainally ni Gheto na Asec.

Hii Asec ilikuwa chini ya waarabu waliokuwa vizuri kiuchumi pale Mvomero na walikodi wachezaji wa ligi kuu na walikuja na coaster imejaa wachezaji wa ligi kuu nadhani zamani ilikuwa inaitwa ligi daraja la kwanza kama sikosei toka Dar kama Kipanya Malapa mzee wa ndondo, masamaki geofrey (marehemu), kipa Chachalamuya "Madusi" Ally Yusuph"Tigana" na wengine toka Dar. Refa ni Mwalimu Liyapiyapi toka Lusanga Sekondari akosqidiwa na Mgambo maarufu anaitwa "Ombopa". Game imewalalia Gheto boys iliyokuwa chini ya vijana wa kijiji cha Mvomero Rama Lundenga, Siwaseme (Fundi wa Mpira) na Abu Ramadhani "Amokachi" (alikuja chezeaga Yanga huyu jamaa) na Salumu wa "ghetto". Ikabidi viobgozi wa gheto wawasiliane na Babu alikuwa kijiji cha mvomero kitongoji cha "Dibamba". Hahaaa Mtaalamu akasema ngoja, ushindi ni wenu msiwe na shaka. Jamaa akachukua gobore lake na kulipiga juu. Pepo likawaingia wachezaji wa Asec na kuanza vurugu dhidi ya refa na wao kwa wao. Game ikaisha kwa vurugu na gheto akawa bingwa. Hii mechi ndio chanzo cha Pengo kwenye meno ya Kipanya Malapa.

Huyu mtaalamu alitumiwa tena na Mtibwa mechi moja na simba pale Manungu ile mechi Mtibwa alifungwa ila Golikipa wa Simba Mwameja alimpiga refa from nowhere kwani babu yule ndio alikuwa anayatuma mapepo na kuwaingia wapinzani na kuamza kuleta vurugu bila chanzo
Nilikuwa naupiga mwingi kiasi, kabla sijazeeka.

Mtama, Lindi kilikuwa kituo changu cha kwanza cha kazi baada ya kuajiriwa. Kama kawaida ya ujana, nikajichanganya kitaa na kufahamika mitaa ile na vijiji vya jirani vyote kuhusu usakataji wangu wa kabumbu. Kule, kabumbu (ligi) linapigwa sana baada ya mavuno.

Siku moja nikapata 'dili' la kwenda kushiriki ligi fulani huko kijiji fulani vilivyopo juu huko Makonde Plateau kijiji fulani km unaelekea tandahimba. Huko nikakuta kuna vilabu viwili vyenye majina makubwa ya timu za epl; Chelsea na Aston villa😂😂😂😂. Mimi niliajiliwa na Chelsea (kwa makubaliano yetu).

Kufupisha habari, nilifanikiwa kwenda na timu hadi fainali. Siku ya fainali ilipofika ulipigwa mpira si wa kawaida. Ngoma ilikuwa ngumu mno hadi dakika za mwisho. Ghafla, dakika za lala salama, bila kurarajia nikajikura mimi na kipa tu. Watu wote walijua, kutokana na mambo yangu, kazi imeisha na kuanza kushangilia.

Ebwana eee, huwezi kuamini ile nataka kuachia shuti nashangaa sioni mpira na badala yake naona sufuria jeupee kubwa kiasi limejaa hela, nikashikwa na bumbuazi nisijue nifanye nini.

Mara akili ikaniambia 'Acha ujinga' okota hela hizo. Nikaokota. Nilipomaliza kuokota tu nasikia filimbi ya refa na hapo kila kitu kikarudi katika hali ya kawaida, yaani fahamu zangu zikarudi. Kwa mshangao wangu, nikajikuta nimeshikilia ule mpira na hivyo ikabidi upigwe kuelekea kwangu. Kila mmoja akabaki ananishangaa pasipo kuamini.

Mwishowe mechi tukapoteza na huo ndo ukawa mwisho wangu wa kushiriki habari za mpira. Nilikoma!
Kombe la uzinduzi wa Wilaya ya Mvomero mwaka 2001 uwanja wa shule ya Msingi Mvomero. Timu za ndondo maarufu za Wilaya ya Mvomero kama Gheto boys na Asec za kijiji cha Mvomero, Wami Magereza, Timu za Dakawa na Turiani. Fainally ni Gheto na Asec.
Hii Asec ilikuwa chini ya waarabu wa Mvomero na walikodi wachezaji wa ligi kuu na walikuja na coaster imejaa wachezaji wa ligi kuu akina Kipanya Malapa mzee wa ndondo, masamaki geofrey (marehemu), kipa Chachalamuya "Madusi" Ally Yusuph"Tigana" na wengine toka Dar. Refa ni Mwalimu Liyapiyapi toka Lusanga Sekondari akosaidiwa na Mgambo maarufu anaitwa "Ombopa". Game imewalalia Gheto boys iliyokuwa chini ya vijana wa kijiji cha Mvomero Rama Lundenga, Siwaseme (Fundi wa Mpira), Abu Ramadhani "Amokachi" (alikuja chezeaga Yanga huyu jamaa) na Salumu wa "ghetto". Ikabidi viongozi wa gheto wawasiliane na Babu alikuwa kijiji cha mvomero kitongoji cha "Dibamba". Hahaaa Mtaalamu akasema ngoja, ushindi ni wenu msiwe na shaka. Jamaa akachukua gobore lake na kulipiga juu. Pepo likawaingia wachezaji wa Asec na kuanza vurugu dhidi ya refa na wao kwa wao. Game ikaisha kwa vurugu na gheto akawa bingwa. Hii mechi ndio chanzo cha Pengo kwenye meno ya Kipanya Malapa.
Huyu mtaalamu alitumiwa tena na Mtibwa mechi moja na simba pale Manungu ile mechi Mtibwa alifungwa ila Golikipa wa Simba Mwameja alimpiga refa from nowhere kwani babu yule ndio alikuwa anayatuma mapepo na kuwaingia wapinzani na kuanza kuleta vurugu bila chanzo na Mtibwa akapewa point za mezani.
 
Haaaahaaa a.. Umenikumbusha nikiwa nacheza ligi daraja la tatu mkoa wa dodoma .. Tulikutana na walugaluga fulani kutoka Mlali huko.
.. Halftime tulikula 4 BILA.. Kumbe kuna mganga wao nje akienda chooni tu hapo karibu na uwanja akitoka tu.. Uku chuma kinaingia.... Tulisanuliwa hatukuamini.. Ikabidi viongozi wamuangalie second half.. Kweli akaingia chooni.. Alivotoka mda sio mrefu tupigwa la 5..wakaamini..ikabidi jamaa azuiwe kjingia chooni na wahuni... Game hii tulikula 5-0.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]wakaguru wa mlali ni hatari mzeee.
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
Aisee..
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
redio
20230322_121857.jpg
 
Nilikuwa naupiga mwingi kiasi, kabla sijazeeka.

Mtama, Lindi kilikuwa kituo changu cha kwanza cha kazi baada ya kuajiriwa. Kama kawaida ya ujana, nikajichanganya kitaa na kufahamika mitaa ile na vijiji vya jirani vyote kuhusu usakataji wangu wa kabumbu. Kule, kabumbu (ligi) linapigwa sana baada ya mavuno.

Siku moja nikapata 'dili' la kwenda kushiriki ligi fulani huko kijiji fulani vilivyopo juu huko Makonde Plateau kijiji fulani km unaelekea tandahimba. Huko nikakuta kuna vilabu viwili vyenye majina makubwa ya timu za epl; Chelsea na Aston villa😂😂😂😂. Mimi niliajiliwa na Chelsea (kwa makubaliano yetu).

Kufupisha habari, nilifanikiwa kwenda na timu hadi fainali. Siku ya fainali ilipofika ulipigwa mpira si wa kawaida. Ngoma ilikuwa ngumu mno hadi dakika za mwisho. Ghafla, dakika za lala salama, bila kurarajia nikajikura mimi na kipa tu. Watu wote walijua, kutokana na mambo yangu, kazi imeisha na kuanza kushangilia.

Ebwana eee, huwezi kuamini ile nataka kuachia shuti nashangaa sioni mpira na badala yake naona sufuria jeupee kubwa kiasi limejaa hela, nikashikwa na bumbuazi nisijue nifanye nini.

Mara akili ikaniambia 'Acha ujinga' okota hela hizo. Nikaokota. Nilipomaliza kuokota tu nasikia filimbi ya refa na hapo kila kitu kikarudi katika hali ya kawaida, yaani fahamu zangu zikarudi. Kwa mshangao wangu, nikajikuta nimeshikilia ule mpira na hivyo ikabidi upigwe kuelekea kwangu. Kila mmoja akabaki ananishangaa pasipo kuamini.

Mwishowe mechi tukapoteza na huo ndo ukawa mwisho wangu wa kushiriki habari za mpira. Nilikoma!
🤣🤣 Hatarii
 
Back
Top Bottom