Siku nimebaki mimi na kipa tu na ghafla mpira ukugeuka sufuria la hela ndipo nilipoamini uchawi upo!

Siku nimebaki mimi na kipa tu na ghafla mpira ukugeuka sufuria la hela ndipo nilipoamini uchawi upo!

Haaaahaaa a.. Umenikumbusha nikiwa nacheza ligi daraja la tatu mkoa wa dodoma .. Tulikutana na walugaluga fulani kutoka Mlali huko.
.. Halftime tulikula 4 BILA.. Kumbe kuna mganga wao nje akienda chooni tu hapo karibu na uwanja akitoka tu.. Uku chuma kinaingia.... Tulisanuliwa hatukuamini.. Ikabidi viongozi wamuangalie second half.. Kweli akaingia chooni.. Alivotoka mda sio mrefu tupigwa la 5..wakaamini..ikabidi jamaa azuiwe kjingia chooni na wahuni... Game hii tulikula 5-0.
Longolesa...hao jamaa ni htr sana.
 
Hivi huko EPL hawatumii uchawi!

Kuna mwamba alikuwa rafiki yangu tulikuwa tunapiga mishe pahala. Sasa moja ya vyanzo vyake vya mapato ilikuwa kukodiwa kupiga ball. Kuna siku kakodiwa kakubali fresh kabisa na nikam-escort hadi ground.

Maajabu nikaona jamaa kachomoa dakika za mwisho kabisa kabla ya game kuanza.
Nikamuuliza kwa nini! anasema hao wachezaji wa timu wanataka wacheze bila kinga yoyote, kwamba yeye kashachoka kulogwa, mkimkodi lazima muwe na kinga kwenye timu yenu.
 
Uchawi kwenye boli upo
FnZL0paWQAI5zJl.jpeg
 
Kitambo sana niliamini uchawi upo.

Nilikuwa nachezea timu moja ya daraja la tatu kule Temeke. Ile siku nilitanguliziwa mpira nikawatoka mabeki wa timu ya Yombo Makangarawe, nikampiga chenga kipa ambaye alikuwa ameshatoka golini, gafla mbele yangu sikuliona goli nilichofanya niliamua kupiga tu mpira mbele yangu.

Cha ajabu niliona mashabiki wanashangilia goli wakati mimi mwenyewe sikuliona goli mbele yangu.
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
Nakumbuka huu siku
 
Siku hiyo bwana tulikuwa na game na timu ya mtaa mwingine walikuwa wahasimu haswa, kila game walikuwa wanatupiga siku hiyo tukasema ngoja tuende kwa sangoma ingawa binafsi sikwenda ila masharti tuliyopewa ni kujipaka mafuta ya nguruwe 🐷 siku ya game, tulijitokeza mafuta balaa wote tunanukia haswa iwe ulikuwa muislam ilikuwa lazima upate, hata hivyo pamoja na mafuta yetu tuliambulia kichapo cha bao 2 bila
 
Kuna game sikumbuki ni African sports ya Tanga na timu gani sijui wakati jamaa anapiga shuti golini watu wameanza kushangilia goli mara ghafla Mpira unapasuka kabla ya kuingia golini.
 
Kama ni hivyo basi nimeacha kumlaumu Bangala kwa kukosa ile penati mpaka tukarnda kuokota mpira Chamazi
 
Kuna mechi Moja ya Simba na Yanga Mwanzoni mwa miaka ya 90 pale shamba labibi mchezaji wa Yanga Rajabu Rashid alijikuta akiokota mpira ndani ya ene la 18 la timu yake.
Hata haileweki kilimkuta Nini, Mwamuzi akaamuru ipigwe Penalty kuelekea Yanga goli la kaskazini ya uwanja.
Penalty ilienda kupigwa na mchezaji na mpiga penalty mashuhuri wa Simba Hamis Tobias Gaga.
Gaga akapiga Penalty mpira ukagonga Mwamba ukarudi uwanjani Yanga waka okoa Ile hatari langoni mwao.
Ile mechi Simba walifungwa 3-1 Kwa Magoli ya Makumbi Juma, Tomas Kipese na Sanifu Lazaro
Hii ndio taarifa iliyokaa mkao na yenye kueleweka...hakuna mbambamba.
 
Dah kumamake wallah umenikumbusha ndondo za kaliua asee

kulikua na shekhe anaitwa shekhe seif alikua bingwa sana kwenye haya mambo...

kuna wakati hata Simba waliwahi mtumia huyu mzee

mpira wa bongo bila uchawi hutoboiii...
 
Kombe la uzinduzi wa Wilaya ya Mvomero mwaka 2001 uwanja wa shule ya Msingi Mvomero. Timu za ndondo maarufu za Wilaya ya Mvomero kama Gheto boys na Asec za kijiji cha Mvomero, Wami Magereza, Timu za Dakawa na Turiani. Fainally ni Gheto na Asec.

Hii Asec ilikuwa chini ya waarabu waliokuwa vizuri kiuchumi pale Mvomero na walikodi wachezaji wa ligi kuu na walikuja na coaster imejaa wachezaji wa ligi kuu nadhani zamani ilikuwa inaitwa ligi daraja la kwanza kama sikosei toka Dar kama Kipanya Malapa mzee wa ndondo, masamaki geofrey (marehemu), kipa Chachalamuya "Madusi" Ally Yusuph"Tigana" na wengine toka Dar. Refa ni Mwalimu Liyapiyapi toka Lusanga Sekondari akosqidiwa na Mgambo maarufu anaitwa "Ombopa". Game imewalalia Gheto boys iliyokuwa chini ya vijana wa kijiji cha Mvomero Rama Lundenga, Siwaseme (Fundi wa Mpira) na Abu Ramadhani "Amokachi" (alikuja chezeaga Yanga huyu jamaa) na Salumu wa "ghetto". Ikabidi viobgozi wa gheto wawasiliane na Babu alikuwa kijiji cha mvomero kitongoji cha "Dibamba". Hahaaa Mtaalamu akasema ngoja, ushindi ni wenu msiwe na shaka. Jamaa akachukua gobore lake na kulipiga juu. Pepo likawaingia wachezaji wa Asec na kuanza vurugu dhidi ya refa na wao kwa wao. Game ikaisha kwa vurugu na gheto akawa bingwa. Hii mechi ndio chanzo cha Pengo kwenye meno ya Kipanya Malapa.

Huyu mtaalamu alitumiwa tena na Mtibwa mechi moja na simba pale Manungu ile mechi Mtibwa alifungwa ila Golikipa wa Simba Mwameja alimpiga refa from nowhere kwani babu yule ndio alikuwa anayatuma mapepo na kuwaingia wapinzani na kuamza kuleta vurugu bila chanzo

Kombe la uzinduzi wa Wilaya ya Mvomero mwaka 2001 uwanja wa shule ya Msingi Mvomero. Timu za ndondo maarufu za Wilaya ya Mvomero kama Gheto boys na Asec za kijiji cha Mvomero, Wami Magereza, Timu za Dakawa na Turiani. Fainally ni Gheto na Asec.
Hii Asec ilikuwa chini ya waarabu wa Mvomero na walikodi wachezaji wa ligi kuu na walikuja na coaster imejaa wachezaji wa ligi kuu akina Kipanya Malapa mzee wa ndondo, masamaki geofrey (marehemu), kipa Chachalamuya "Madusi" Ally Yusuph"Tigana" na wengine toka Dar. Refa ni Mwalimu Liyapiyapi toka Lusanga Sekondari akosaidiwa na Mgambo maarufu anaitwa "Ombopa". Game imewalalia Gheto boys iliyokuwa chini ya vijana wa kijiji cha Mvomero Rama Lundenga, Siwaseme (Fundi wa Mpira), Abu Ramadhani "Amokachi" (alikuja chezeaga Yanga huyu jamaa) na Salumu wa "ghetto". Ikabidi viongozi wa gheto wawasiliane na Babu alikuwa kijiji cha mvomero kitongoji cha "Dibamba". Hahaaa Mtaalamu akasema ngoja, ushindi ni wenu msiwe na shaka. Jamaa akachukua gobore lake na kulipiga juu. Pepo likawaingia wachezaji wa Asec na kuanza vurugu dhidi ya refa na wao kwa wao. Game ikaisha kwa vurugu na gheto akawa bingwa. Hii mechi ndio chanzo cha Pengo kwenye meno ya Kipanya Malapa.
Huyu mtaalamu alitumiwa tena na Mtibwa mechi moja na simba pale Manungu ile mechi Mtibwa alifungwa ila Golikipa wa Simba Mwameja alimpiga refa from nowhere kwani babu yule ndio alikuwa anayatuma mapepo na kuwaingia wapinzani na kuanza kuleta vurugu bila chanzo na Mtibwa akapewa point za mezani.
Noma hio mzee nawapata vizur hao gheto man from turian
 
Back
Top Bottom