Elections 2015 Siku tano za kampeni: Chokochoko za CCM, serikali yake na vyombo vya ulinzi

Elections 2015 Siku tano za kampeni: Chokochoko za CCM, serikali yake na vyombo vya ulinzi

Chadema imeshauzwa. Kuna kila dalili kuwa mnunuzi wa Chadema anataka kuibadilisha iwe kikundi cha sanaa...

uchaguzi mkuu umeshachafuliwa tayari. kuna kila dalili ccm imepania kuvuruga uchaguzi huu kwa kutumia vyombo vya dola kama polis na hata mamlaka za mitaa. huko mbele ya safari tusitafute mchawi..
 
Habari za jioni ndugu watanzania wenzangu..!

Salam salamu ndugu mheshiniwa Rais.

Sitaki nimwambie mtu yeyote yule ila maoni na mtazamo wangu uende moja kwa moja kwa rais wa nchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mh. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mh. Rais kama kweli ni rais mwenye dhamana ya kuongoza nchi hii kwa mjibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania unalo jukumu la kuwaongoza wananchi wa taifa hili bila misingi ya ubaguzi au upendeleo wa aina yeyote.

Vitendo tunavyoshuhudia katika mwanzo wa kampeni za uchaguzi haviashirii amani wala aina yeyote ya umoja wa kitaifa ambao tumekuwa nao kwa muda miaka zaidi ya hamsini.

Kunyimwa uhuru wa kidemocrasia itakuwa ni moja ya makosa makubwa yatakayorigharimu taifa hili lenye tunu ya amani tuliyorithishwa na mzee wetu hayati baba wa tiafa mwl.j.nyerere.

Kitendo cha kuwanyima upinzani uhuru wa kufanya mikutano sehemu za umma kama viwanja vya taifa, jangwani, kuzuia mikusanyiko ya siasa, kukmata watu, kupiga watu mabomu hakiwezi kuiweka nchi yetu katika hali ya kuitunza tunu ya amani nchini. Na pia kinapelekea kuligawa taifa katika vipande vipande.

Ukiwa kiongozi wa nchi na mwenye dhamana ya kila mtanzania kuwa huru, salama na haki za kiraia ujue unayo dhamana ya kuhusika na kila madhara yatakayo mpata mtu yeyote na taifa kwa ujumla.

Tatizo la haya yote ni hofu ya mabadiriko hasa ya uongozi kwa serikali na chama tawala ila nikukumbushe mh. Rais chukua muda kujifunza kwa baba wa taifa mwaka 1992 juu ya vyama vingi ambapo maoni ya wengi yalionesha kutokukubali vyama vingi. Ila busara ya mzee nyerere nakuona nguvu ya mabadiriko ambayo katika zama zote hajawahi kushindwa alimua kukubali vyama vingi.

Mabadiriko yanayoonekana kuwatia hofu watawala kwa maana ya rais na taasisi ya za chini ya ofisi ya rais wanaamini yamachagizwa na vyama vya upinzani hili ni kosa la kwanza kwa kipngozi makini huitaji kutumia njia za kisayansi kujua kinachochagiza mabadiriko. Nitataja chache hapa chini:-

Wananchi kukata tamaa na maisha hasa kufuatia hali duni za maisha na kutokuwepo mipango thabiti ya kuwakwamua kwa adui huyu namba moja UMASIKINI.

Kingine tabia ya jamiii kubadirika na wakati kufuatia maendeleo ya sayansi na technology uwepo wa mawasiliano ambapo sasa mtu anaweza kujifunza mambo mbalimbali kote duniani kunapelekea mahitaji ya jamiii kimabadiriko kuongezeka na watu hawaoni serikali ikibadirika kuwapatia mahitaji yao mfano utasikia serikali ikijiringanisha na MKOLONI huku ikisahau watu wanajipima na nchi zinazoebdelea.

Mwisho niombe kwa viongozi wenye dhamana ya nchii hii kwa kuanza na RAIS, JESHI, MAHAKAMA na USALAMA WA TAIFA na taasisi nyingine ndogo ndogo za kisekta zenye dhamama katika uchaguzi huu mkuu kuwa sawa maana bila haki au matumizi yeyote ya nguvu kupoka haki ya kidemocrasia hayayaacha taifa hili likiwa salama. Viongozi wenye dhamana hasa wastaafu waache watumizi ya lugha za kuudhi na kebehi kama alivyofanya mzee MZEE MKAPA.

Mwisho nikukumbushe mh. Urejee na kuifanyia kazi kauli yako SOTE TUNAJENGA NYUMBA MOJA (TANZANIA) KWANINI TUGOMBANIE FITO. na busara ile ile ya uliyo waambia wanaccm dodoma kuwa CHAMA KWANZA MTU BADAE itumike pia hapa TAIFA KWANZA (TANZANIA) ALAFU CHAMA(CCM) BADAE. iwapo ccm ikishindwa Tanzania itabaki ile ile na UKAWA au vyama vingine vikishindwa Tanzania itakuwepo vilevile.

mkuu unaponda maji kwenye kinu. kikwete yupii? labda mwingine..
 
Sheria ya vyama intaka vyama vipewe muda -pawe na mgawanyo sawa kipindi cha kampeni kwa vyama na wagombea , NEC inawajibika kuona vyama vinatendewa haki, msajiliwa vyama na mabalozi wanapaswa kufahamishwa panapokuwa hakuna haki, UKAWA mkiwa legelege hakuna kitakachoendele lazima mshupae liwalo na liwe

hao wote uliowataja ni maccm kwa mlango wa uani.
 
Tatizo lenu UKAWA mnafikiria mambo ni rahisi tu kwamba mpite mnadanganya watu kuwa mnataka kuwaletea mabadiliko wakati hamuwezi halafu serikali iwaache tu mfanye mnavyotaka. Haiwezekani.

Mkuu kwa miaka 50 ccm imewaongopea Babu ,baba ila mie nataka niongopewe na ukawa ila we we endelea kuongopewa pamoja na kizazi chako "nakataa kutoka moyoni kuongopewa na ccm""
 
Wananchi wamepandwa na hasira sana,

Kila kona ukipita mazungumzo ni hayohayo,kwamba ukawa wameanza kufanyiwa hila na fitina mapemaa,hii ni hofu za chama dola.Enyi chama dola kwenye vikao vyenu iwe vya siri au vya wazi kuhusu nia yenu ya umwagaji damu katika nchii hii ya Tanzania,mshindwe katika jina la Yesu kristo wa Nazareti aliye hai.

Katika madhabahu zenu zote mnazodaiwa damu iwe za Albino au za ajali ambazo mmeshindwa kutimiza na kutaka kusababisha mauaji ya Kimbari mshindwe katika jina la Yesu.

Damu ya Yesu inenayo mema inene kinyume na mabaya yote katika ardhi hii ya Tanzania inayolia sababu ya damu zisizo na hatia.

Ee Mungu baba kwa yeyote aliye wahi kumwaga damu ya mtanzania kwa hila, kwa mauaji ya albino na ajali za namna nyingine yeyote,na kwa wenye nia ya kumwaga damu kwenye nchii hiii.

Tunakuomba Yehova Mungu mkuu,damu hiyo iwe juu ya vichwa vyao wenyewe,pamoja na familia zao kama ilivyotokea katika nyumba ya Sauli.Kwa wanaoandaa mashimo ya kuzika watanzania ee Mungu tunakuomba kwenye mashimo hayo waingie wenyewe.

Amen
 
Wameshajua kuwa hawatashinda huu uchaguzi ndo maana wameanza chuki mapema sana,na wamejipanga hata kufanya mauaji ya halaiki ili waendelee kutawala,Mungu atasimama upande wa wanyonge na kuwatetea shetani ccm atashindwa kwa damu ya Yesu kristo mwana wa Mungu aliye hai.
 
Kweli hii vituko Tanzania...

Lowassa wewe ndio Rais..

Keep cool, wapelekeeee wapelekeee
washakubali, is just a matter of time..

Kilichobaki SASA, wanataka Lowassa asitembee hata ardhini au majini... wanshindwa tu kusema, LOWASSA KAA HOME USITOKE... ni hilo tu linashindikana... maana NGUVU YA UMMA, ITAGEUZA DOLA NA UMMA KUCHUKUA NCHI yao ikifika huko...

So, wanavyozidi kumzibia Lowassa, umma unaona, na kumpenda zaidi..

Ukiangalia kwa makini, ktk kampeni za Magufuli, WATU WOTE WANAOHUDHURIA WAMEKATA TAMAA KABISAAAAAAA... CHEKI NYUSO ZAO... even you can read their minds.. hawana imani na CCM, wameichoka.. CCM washaona hawana lao tena..


So sasa imebakia tu SUMATRA imzuie Lowassa, hapo UMMA, utaamua sasa...!!
 
Nadhani Watakao pata Hasara Kubwa wegi wao Ni Watawala Waliotutawala kwa Miaka 50; Wanaweza Kujutia Baadae Kwani Tunaishi Nao Huku Huku Mtaani.
 
Ccm ni kama binti jeuri aliyemletea jeuri shangingi wa mtaa unajua kilichotokea ?
usilog out nikupe kisanga hicho
 
Nasikia hata TRCA wana mpango wa kumkataza kutumia simu.

Hata Lowassa akikaa nyumbani tu, wizara ya ardhi itatoa tamko kumpiga marufuku kukaa kwenye ardhi yake..!!
Tamko litasema...

'...Wizara ya ardhi na makazi imepiga marufuku kwa wagombea wote wa urais kukaa nyumbani maana wanaweza kusababisha uvunjifu wa amani'.
'...Wagomea wote wa urais hawaruhusiwi kukaa kwenye ardhi inayosimaniwa na wizara ila kwa kibali maalum kutoka wizarani makao makuu...'
 
Ccm ni kama binti jeuri aliyemletea jeuri shangingi wa mtaa unajua kilichotokea ?
usilog out nikupe kisanga hicho

Nikilog out si nitakiona hicho kisanga kama guest user? We kilete tu.
 
**they just create their own beautfull bombs""
---->>>mkandamizo utakapokuwa mkubwa kupitiliza,ni lazima utatafuta njia ya kutokea na hapo hilo ndilo boom!<<<-------
 
Mamlaka ya hali ya hewa inaweza kuja na kituko kingine.

Kutokana na kuwepo na joto kubwa katika bahari ya Mediteranian ambayo itasababisha mvua za El Nino wagombea uRais watatakiwa kuomba kibali Mamlaka ya hali ya hewa kabla ya kufanya mikutano yao ili kuondoa uwezekano wa kutokea madhara yatakayosababishwa na mvua za El Nino.
 
Hata Lowassa akikaa nyumbani tu, wizara ya ardhi itatoa tamko kumpiga marufuku kukaa kwenye ardhi yake..!!
Tamko litasema...

'...Wizara ya ardhi na makazi imepiga marufuku kwa wagombea wote wa urais kukaa nyumbani maana wanaweza kusababisha uvunjifu wa amani'.
'...Wagomea wote wa urais hawaruhusiwi kukaa kwenye ardhi inayosimaniwa na wizara ila kwa kibali maalum kutoka wizarani makao makuu...'


Haaaaaa... CCM kwishaaaaa kabisaaaaaaaaaaaa....
 
Back
Top Bottom