Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Ok hiki ninachoandika ni off topic.

Kuna jamaa aliripoti shule, bishoo si mchezo. Kuna jamaa akawa anamuonea onea tu akimkuta anakula anachukua chakula, anachukua madaftari yake. Halafu anamwambia kama unaweza si upigane? Ishu ilienda kama mwezi.

Maji yakikata kuna kama kijito cha maji ndiyo hua tunayafuata, basi yule bishoo akavaa traki raba na fulana akamkuta mshkaji yupo na sisi akamwambia twende mtoni. Jamaa akajibu kwa dharau "Unataka nikakuf.ire?" mshkaji akajibu hapana nataka tukapigane, Ila tuwe wawili tu atakayerudi shule hapa ndiyo mshindi, jamaa akakubali wakaenda.

Dakika 10 nyingi tunamuona bishoo anarudi. Akatuambia kamchukueni jamaa, tumefika kule yule jamaa kila unapomgusa analia akafuatwa na gari la shule gari lenyewe wipers hazifanyi kazi na ukungu umeshakuja ikabidi mmoja akae kwenye boneti awe anafuta futa na mwendo uwe wa kobe.

Baada ya kupona akatuambia "Yaani sijaambulia hata ngumi moja, huyo jamaa hafai" kumbe yule bishoo ni mshindi wa Judo ngazi ya mkoa huko mkoani kwao. Halafu ikatokea wakawa marafiki vibaya mno.
Mmmhhhh we jmaa kwa kamba me skuwezi aiseee
 
Ile shule siisahau kwanza tokea utoto nilikua sipendi maharagwe... Nilivyofika kwenye ule mji nilikaa kwa rafiki wa familia yetu kama wiki nikawa naenda kuisoma shule.... Siku natinga shule nikakuta ni ugali maharagwe tena ya mawese yasiyoiva nikawa nashangaa mbona kila vessel ni la njano.... Tulikula mawese ile shule sisahau...

Ila kuna jamaa yangu alinifurahisha sana... Siku amefika shule jioni wakamshushia katikati ya mabweni... Watu wakaanza kupiga makelele asulubiweeeee jamaa akadaka tax akarudi alipotoka...
 
Dah mwe msinukumbushe IFUNDA TECH form one mimi Suku ya kwanza tu Master P na Chichi (viongozi wa bweni) waktukabidhi viunga vya maua kuvitunza vilowe kila siku asubuhi na jioni.. Kula shida foleni kama ya kwenda mbinguni, Uonezi, Maticha wakax, Baridi Kali blanket nilfua once in whole those four years, na mengine Mengi... Heshima kwako IFUNDA TECH
 
Ilikuwa form V, baada ya orientation, tunes za kujuana. Wengi tulishapewa majina ya rafiki wa rafiki ambae anakuja shule ile.

Dining siku ya kwanza mdada mmoja akimwaga magarage kisa alimkuta mende ndani ya bakuli. Kwakuwa bado tulikuwa na makula kula kuna waliomtengenezea orange squash na marie biscuits.

Baada ya miezi miwili pale shule, mdada alikuwa hodari wa kutoa mende kwa kijiko na kuendelea na menu.
Hahahaha thanks for sharing[emoji23]
Mimi mara ya kwanza kukanyaga boarding school ya serikali ilikua form 5 ikafika muda wa kula jioni tukaenda nikitegemea ugali kama naoujua mimi.kufika nakuta ugali fulani hvi una harufu na muonekano mbaya na maharage hayajaungwa hata yale sijui tu yalikuaje.sikula ile siku nikalala njaa.baada ya siku chache shule ilinishinda
 
Kuna shule inaitwa Mwakavuta (wenyeji wanaiita Mwakauta) nikavuta siku za kuripoti kwa kua nilitaka nitoke nyumbani baada ya valentine day.

Nafika siku hiyo ni jumapili siku ya wali. Nikala kidogo nikaugawa, naenda kuosha sahani ghafla ukungu umetanda kiasi hauwezi kuona hatua mbili mbele.
Nikasimama pale pale kwa zaidi ya dakika 45 ili ukungu upite nisije nikapotea nikaingia msituni. Sehemu yenye baridi kali kama haujavaa viatu au ni vyepesi vidole vya miguuni unaanza kuhisi vinachomwa chomwa na sindano. Nahisi ni dalili za kua frostbitten.

Ukungu unamalizikia vidole vikawa vinaonyesha kama damu imevilia. Tumelala bwenini nakutana na watu kutoka Chunya, Kilimanjaro, Moshi, Kigoma, Mafinga n.k. na wote wanasema baridi la pale si mchezo.

Asubuhi naamka. Njia za shule zote zina theluji, boksa niliyoiacha jana kwenye kamba imeganda kwa barafu.

Nikaanza kupima pros na cons.
-Kwanza walimu walituambia watoto wa O Level wote wana ngoma, kumbe na wale watoto waliambiwa sisi wote tuna ngoma. Ingawa wakinga siyo wabanaji lakini hilo doa litachukua muda wangu.

-Shule haina mabinti wazuri, hao waliopo wavuna mbao na wanakijiji wote mnawagombea.

-Unaweza kua na hela lakini hakuna cha kununua.

-Umbali mpaka wilayani ni 22KM na gari ni moja likipita limepita ama utembee, nilitembea aisee nilikoma, kila sehem ya mwili iliuma. Nilienda kupiga PPS hadi PPS zinatoka ndo nagundua kuna makamasi yalikua yananitoka. Sijui mpiga picha alidhani urembo.

-Rate ya kupiga puchu ikawa juu.

-Walimu wawili wa masomo yangu walikua wanakukaririsha kitu cha kitabuni hawakichambui wala nini halafu ni unasomewa sasa akiwa anasoma unagundua na yeye kuna vitu anavijua hapo. Mmoja alienda Mbeya akakaa zaidi ya mwezi huku somo limesimama.

-Chakula kibaya sijapata kujua. Kuna wadudu hua wanaranda randa kwenye balbu ukiwaua wanatoa harufu mbaya, sasa wale unawakuta kwenye maharage wapo kibao. Wali ikawa ndiyo luxury food, ugali unaula kidogo, asubuhi unanywea uji, makande, unakula kidogo asubuhi unanywea uji.
Wali ulisababisha watu wapigane, kulikua kuna paper two sasa form six wanajihisi wao ndiyo wanatakiwa kuanza, jamaa wa form five akafosi kingi ebwana washkaji wawili akaanza kumpiga.
Ila baadaye na yeye aliwatafuta mmoja mmoja na wakamheshimu.

Nilifeli kwa mengi.
MAKETESTAN BULL ON GWAH 😀😀😀😀😀
 
Waliniibia yeboyebo zangu nilizosafiri nazo kutoka mkoa.
Just imagine ndo nafika tu bwenini nikaleta usafi ule wa kihome home si nikavua mayeboyebo yangu ili ningie Dom, loooh wana wakapita nazo,nilikuja kuziona nipo form two term ya pil[emoji23].
Machalii wa Shaban Robert 06 Mzumbe Secondary tuheshimiane mazee.
 
Wale wazee wa Ndanda boy shule safi siku nimeripoti tumelala vizuri saa kumi na moja naskia kiongozi mmoja anapayuka form five amkaaaaaa!!! Huku akiimba wimbo wa blood (the game ft Damian Marley) basi huu wimbo lazima niwe nao kila kwenye music devices zangu!!!
 
Niliingia boarding form five:
Maisha ya boarding nilishayajua coz nikiwa o level weekend naenda kulala mashuleni kwa washkaji zangu!! So sikuwa na ugeni na misosi wala tabia.

Nilipokelewa na watemi wa form three, sura yangu tu wakajua huyu mwenyewe! Ilibidi wawe wananilia timing 🤣🤣🤣😃

Nilianza na intro! Usiku mnene nimelala kitandani ndoo na mazaga mengine nimeweka pembeni ya kitanda! Madogo wanatest zari kuniibia wanavizia wakijua nimelala, wanashtuka nawaambia oyaaah! Rudisha ndoo!

Kesho yake ikawa story shule nzima jamaa halali! Ukigusa ndoo yake au chochote anakutoa mbio! Ikawa ni mchezo na hakuna siku nilifeli, walichemka!

Wakanibananisha bwenini siku moja usiku sina hili wala lile! Nashtuka madogo kama kumi hivi wa form three na two wamenizunguka wanadai wananipa kipigo najitia msela sana hata kama nipo five!!

Niliruka ghafla toka kitandani nikatua kwenye mabega ya yule mbabe zaidi! Wakiwa wamehamaki mbabe wao kaanguka chini nikawahi switch ya taa nikazima kukawa giza totoro!! Nilitoa mkanda niliwadunda isivyo kawaida kuniona hawanioni wanashtukia vichapo mbaya zaidi mlango walifunga wenyewe kufungua hawawezi!! Walikula kichapo heavy sana!

Baada ya vilio kuzidi mle bwenini walinzi wakaja kuvunja mlango! Kuna niliokuwa nimewapasua na bakoli ya mkanda ikabidi wakatibiwe! Kesho yake waalimu hawanielewi na hawaamini kichapo nilichotoa, nikaambiwa rudi home kalete mzazi!!

Nilipoondoka sikurudi tena, na shule nikajihamisha mwenyewe kwenda shule yenye hostel badala ya boarding, dingi alikuja kujua baadae sana shule ninayosoma tena mkoa mwingine! akanyoosha mikono!!
 
Back
Top Bottom