Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

Wandugu kama mjuavyo wengi wetu tumesoma shule za st. Kayumba kwa hiyo Ngeli ni ishu kwetu. Basi kwa kuunga unga hivyo hivyo nikachaguliwa Chuo (UDSM) sasa kufika huko si ndo mambo ya Seminar za DS 101 natakiwa ni-present ilikuwa balaa usiku kabla ya seminar sikulala naogopa, kwenye seminar yenyewe sasa jasho lilinitoka mwili mzima balaa yaani naona nyota nyota tu daah! sitaki kukumbuka. Lakini namshukuru Mungu baada ya pale nilifanya bidii y kujifunza kwa kusoma zaidi vitabu vya kiingereza na kuongea na watu wasiojua kiswahili (hasa waganda, Wazambia & Waganda) Angalau sasa mambo si mabaya Ulimi si mzito tena kiviile!!! English aisee ni hatari jamani. SHIKAMOO KIINGEREZA

dah mkuu sitaki hata kusimulia
 
Dawa ya kiingereza ni kusoma vitabu vya ngeli kusoma magazeti ya kila siku kama unapata lakini kiboko yake soma magazeti kwenye internet hasa yanayoandikwa na wachapishaji wa UK, USA kama unakosa magazeti soma ya bongo na Kenya ngeli yao sifuri kidogo afadhali hata ya SA na Zimbabwe imetulia kidogo.
 
Kuna mmoja tukiwa form one wakati huo kulikuwa na 'no English no service' rule, siku hiyo jamaa alisahau daftari, mwalimu kafika kwa mwanafunzi aliyekuwa mbele ya huyo jamaa, akaulizwa where is your exercise book akajibu I forgot it home, sasa ilipofika za much yake hakujua yule jamaa wa mbele alisemaje, alipoulizwa akasema I dolilo. Class nzima ilipasukiwa na kicheko

Hahaaaahaah mbavu zangu mieeeeee! I dolido akimaanisha nini? Aiseeeeee nimecheka usiku huu
 
Nakumbuka jamaa yangu aliniambia kwenye miaka ya 1990 waliomba kazi ya udereva kwenye shirika fulani la kimataifa hapa nchini, nafasi waliyokuwa wanataka ni mbili tu. Wakaitwa watu 6 kwenye interview, sasa jamaa mmoja akaitwa wa kwanza, hakuchukua muda akatoka...akawaambia wenzake huko ndani ni kingereza kitupu na kuna wazungu, jamaa yangu akaitwa wa pili, sema yeye alikuwa anajua kujieleza kiasi, anasema alipotoka nje hakukuta mtu hata mmoja, ina maana wale madereva walitimua mbio baada ya kusikia ndani ni English kwa kwenda mbele. Hivyo jamaa yangu akapata kazi kiulani peke yake, kwani hata yule wa kwanza alishindwa kabisa kuongea kingereza. Jamaa yangu akafanya kazi kwa miezi sita wakaridhishwa na utendaji wake, wakampa kazi ya kutafuta madereva wanaojua kingereza waajiriwe...

Kujua kingereza kuna raha yake....
 
Wakati nipo A-level, kuna mwalimu mmoja wa O-level tulikuwa tunacheka sana parade siku akiwa zamu! Kuna siku akawa anawakataza wanafunzi wasipite shortcut ili kulinda mazingira akasema, "You, don't pass there, there is no method!" Watu wakashikilia mbavu zao!
 
mimi humu humu jf yalinikuta nilipost haraka haraka nilikuwa nawahi college kipindi cha kwanza nikakosea kichwa cha habari afu ndo nilikuwa member mgeni nimejiunga sina muda mrefu hawakunielekeza nafanyaje marekebisho ikabidi nile nao sahani moja hivyo hivyo lol sisahau ingawa wote wameshakuwa rafiki zangu ya kale yamepita, juzi juzi baada ya kum pm mode akanirekebishia maana title ukishapost huwezi kurekebisha mwenyewe hahaha walinikaanga acha kabisa
 
Katika presentation ya kudefend dissertation chuon, Inatakiwa kubadilisha sehemu ya research proposal kua past tense, then ndo uje kuendelea na Part ya Result and discusion. Hivyo watu wanaweka was, were za kutosha. Bas mdada ananza kuwasilisha pale, "Goodmorning, My name WAS xxxx"
Yani hata yeye hakuamini alichokisema.
 
Prof. Mlambiti huyoo na yellow book yake. Umenkumbusha mbalii

Siku moja tupo kwenye seminar ya koz moja inaitwa rural agricultural economy maarufu kama YELLOW BOOK kwa waliosoma SUA wataelewa, basi picha moja ilikua imebandikwa ukutani ikapulizwa upepo ikadondoka chini jamaa kule mbele akiwa na maiki alisema "what is that, ooh the picture drop down without becouse" basi tulicheka sana
 
Halafu wanaharakati wa kiswahili wanataka kiswahili kiwe lugha rasmi ya kufundishia kuanzia nursery schools hadi universities. Hiyo ikikubalika wale wa shule za kayumbe kizungu watakisikia kwenye tv.
 
kwi kwi kwi. Yawezekana kabisa

Katika presentation ya kudefend dissertation chuon, Inatakiwa kubadilisha sehemu ya research proposal kua past tense, then ndo uje kuendelea na Part ya Result and discusion. Hivyo watu wanaweka was, were za kutosha. Bas mdada ananza kuwasilisha pale, "Goodmorning, My name WAS xxxx"
Yani hata yeye hakuamini alichokisema.
 
Mkuu naona bado na leo umechapia sio neno ndio kujifunza huku ni ''disperse'' na sio ''dispace'' Mbavu sina


Mie nakumbuka form one Kantalamba,nimefika nikawa kiranja,basi nikashika zamu kuongoza assemble,tumeimba nyimbo zote,ikafika muda wa kuwatawanyisha nikasema "you may disappear" badala "you may dispace" basi ilikuwa gumzo. Ticha akaniita chemba kunielekeza umombo. Ha ha ha
 
Kipindi tupo O level, akaingia mwalimu wa zamu, akaagiza tujihesabu, ajue idad ya watoro, bas ghafla ikaanza One,Two,Three..... Kufika nyuma kimyaa, tunaanza tena, ikifika pale kimyaa, kumbe jamaa imewakutia namba 12,13,14,15 ilikua ni vita kuzitaja..! kwa usalama wote wakahamia mbele ili waanze na 0ne.. hizi si mteremko.
 
Jamaa aliniomba nimjazie scholarship flani hivi kwa sababu ya uzoefu lakini nikamtaka ajaze yeye kila kitu kwanza halafu mi ndo nipitie. Ebwana hicho kiingereza yaani hoi nikashangaa mhitimu wa shahada ya kwanza tena amesoma HGL. Nikajua hata ningerekebisha akiitwa kwenye interview atakwama tu basi kwa kumuonea aibu nikamweleza mtu mwingine akamwambia. Baada ya miezi jamaa ananipigia akinifahamishabkwamba ameanza english kozi!!!! Akina Kadeghe na Nyambari Nyangwine wametuharibia kabisa vitabu vya lugha bora waturudishie Musa and Neema kuna afadhali
 
hiz kura pia noma, kama kuna ticha mmoja wakati tupo o level walikuja wazungu kutoka marekani walileta vitabu, walimu wakawa wanajitambulisha paredi, maadam mmoja alisema 'my name is madaam sanga, am married by two childrens'

Hahaha
 
Back
Top Bottom