Sikufukuzwa kazi Singida Fountain Gate, nilivunja mkataba kwa makubaliano

Sikufukuzwa kazi Singida Fountain Gate, nilivunja mkataba kwa makubaliano

Ni kweli.
Mbona unadanganya watu mchana kweupe? Timu gani ya nje itahitaji hizi porojo za uswahili-swahili zinazotumiwa na timu za Bongo. Timu zinazojielewa zinawekeza kwenye wachezaji na miundo mbinu siyo poroji porojo za kiswahili. Huu mtindo wa kutumia porojo unafanya kazi kwa nchi yenye akili-nyumbu tu.
 
Kuna wapenzi wakiachana huwa wanaanza kuvutana kwa mijadala,nani kamuacha mwenzie? Mie sijawahi kuona maana ya nani kamuacha mwenzake...ni kuachana tu.
 
Mbona unadanganya watu mchana kweupe? Timu gani ya nje itahitaji hizi porojo za uswahili-swahili zinazotumiwa na timu za Bongo. Timu zinazojielewa zinawekeza kwenye wachezaji na miundo mbinu siyo poroji porojo za kiswahili. Huu mtindo wa kutumia porojo unafanya kazi kwa nchi yenye akili-nyumbu tu.

Kila nchi na tamaduni zake. Hizi unazoita porojo ni taaluma za watu. Na kwa kiasi kikubwa zimechangia kukuza soka letu na kulipa umaarufu.

Watu kama wewe ni wale mnaojichukia na kuthamini vya watu wengine. Nadhani ni ugonjwa wa kisaikolojia. Tafuta tiba haraka mkuu.
 
Kila nchi na tamaduni zake. Hizi unazoita porojo ni taaluma za watu. Na kwa kiasi kikubwa zimechangia kukuza soka letu na kulipa umaarufu.

Watu kama wewe ni wale mnaojichukia na kuthamini vya watu wengine. Nadhani ni ugonjwa wa kisaikolojia. Tafuta tiba haraka mkuu.
Ndugu yangu. Nothing compensate hard work in life. Huwezi ku-compensate ufanyaji kazi kwa kutumia maneno. Unajua tatizo liko wapi? Kwenye nchi yetu ya Tanzania sasa hivi, culture ya ki-pwani pwani imetawala sana. Culture ya maneno mengi, culture ya kujigamba kwa mdomo yaani ni maneno 24/7. Ndiyo maana unaona watu wenye mdomo mdomo na maneno mengi wanaishi maisha mazuri sasa hivi kwa sababu wanatumika kupumbaza watu baada ya serikali ku-colapse kimfumo. Iwe timu, iwe nchi, kamwe haitajengwa kwa kutumia mdomo.
 
Watu wa Soka,

Umofia kwenu.

Nimekuwa nikipokea SMS nyingi na maswali kwenye mitandao ya kijamii kuhusu nini kimetokea kati yangu na Klabu ya Singida Fountain Gate ambayo nilikuwa naitumikia kama Msemaji na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano.

Kuweka rekodi sawa tu, sijafukuzwa kazi wala hapakuwahi kuwepo mgogoro wowote kati yangu na Klabu. Nimefanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kufikia maono ya klabu katika eneo la kuisemea, kujenga mahusiano chanya na kuiweka timu karibu na wadau.

Kilichotokea ni makubaliano tu ya kuvunja mkataba na tulifikia makubaliano hayo pande zote mbili. Hivyo nilipata baraka zote kutoka kwa uongozi wa klabu.

Kwa sasa nipo mbioni kusaini mkataba na klabu nyingine kubwa ambako naenda kutumia ujuzi na uzoefu nilioupata kama nilivyoeleza kwenye taarifa yangu kwa umma niliyoitoa tarehe 05/05/2024.

Asanteni.

View attachment 2996745
Taarifa hii ilitakiwa itolewe na mwajiri wako (huyo wa zamani), na sio wewe mwajiriwa. Vinginevyo itakuwa vigumu kuamini kama ulifukuzwa au mlivunja mkataba kwa makubaliano
 
Watu wa Soka,

Umofia kwenu.

Nimekuwa nikipokea SMS nyingi na maswali kwenye mitandao ya kijamii kuhusu nini kimetokea kati yangu na Klabu ya Singida Fountain Gate ambayo nilikuwa naitumikia kama Msemaji na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano.

Kuweka rekodi sawa tu, sijafukuzwa kazi wala hapakuwahi kuwepo mgogoro wowote kati yangu na Klabu. Nimefanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kufikia maono ya klabu katika eneo la kuisemea, kujenga mahusiano chanya na kuiweka timu karibu na wadau.

Kilichotokea ni makubaliano tu ya kuvunja mkataba na tulifikia makubaliano hayo pande zote mbili. Hivyo nilipata baraka zote kutoka kwa uongozi wa klabu.

Kwa sasa nipo mbioni kusaini mkataba na klabu nyingine kubwa ambako naenda kutumia ujuzi na uzoefu nilioupata kama nilivyoeleza kwenye taarifa yangu kwa umma niliyoitoa tarehe 05/05/2024.

Asanteni.

View attachment 2996745

Hata kama ulifukuzwa kazi mkuu, sio big deal.

Kupanda na kushuka ndio maisha
 
Watu wa Soka,

Umofia kwenu.

Nimekuwa nikipokea SMS nyingi na maswali kwenye mitandao ya kijamii kuhusu nini kimetokea kati yangu na Klabu ya Singida Fountain Gate ambayo nilikuwa naitumikia kama Msemaji na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano.

Kuweka rekodi sawa tu, sijafukuzwa kazi wala hapakuwahi kuwepo mgogoro wowote kati yangu na Klabu. Nimefanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kufikia maono ya klabu katika eneo la kuisemea, kujenga mahusiano chanya na kuiweka timu karibu na wadau.

Kilichotokea ni makubaliano tu ya kuvunja mkataba na tulifikia makubaliano hayo pande zote mbili. Hivyo nilipata baraka zote kutoka kwa uongozi wa klabu.

Kwa sasa nipo mbioni kusaini mkataba na klabu nyingine kubwa ambako naenda kutumia ujuzi na uzoefu nilioupata kama nilivyoeleza kwenye taarifa yangu kwa umma niliyoitoa tarehe 05/05/2024.

Asanteni.

View attachment 2996745
Karibu sana kwenye timu yetu Nguruwe FC!

Kwaheri Ahmed!
 
Back
Top Bottom