Simba ndiyo timu ya Tanzania iliyofanyiwa vurugu na magumashi mara nyingi katika mashindano ya CAF

Simba ndiyo timu ya Tanzania iliyofanyiwa vurugu na magumashi mara nyingi katika mashindano ya CAF

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Kuna timu inajitapa eti imehusika kuleta uhuru wa Tanzania ila haijawahi kuvuja jasho na kucheza katika mazingira magumu ambayo unaweza hata kuwaza kama baada ya mechi utabaki na uhai wako. Simba ndiyo timu pekee Tanzania ambayo imepitia mazingira hayo mara nyingi kuliko timu yoyote ile.

Tuanzie miaka ya 70, Simba ilifanyiwa vurugu nchini Misri, kipa wake akanyang'anywa gloves ikatolewa katika mazingira ya kutatanisha sana. Kama sikosei hii ilikuwa hatua ya nusu fainali (nikosolewe kama nimekosea).

Kuna ile mechi ya Sudan miaka ya 90 Simba vs El Mereikh. Simba walifanyiwa vurugu mbaya sana uwanjani, wakapigwa mawe sana tu.

Tunakuja mechi ya jana, Simba vs Al Ahly Tripoli. Hivi unadhani Simba wangepata goli pale hali ingekuwaje? Unadhani hili halikuwa vichwani mwa wachezaji? Unafuu pekee kiusalama jana ulikuwa kukubali kufungwa ila wachezaji wakakomaa, hafungwi mtu hapa!

Naomba Simba ianze kupewa heshima inayostahili nchi hii, tafadhali.
 
Dk 90 ....bila shoot on target [emoji32][emoji32]

Hio timu Bora mudi silete mbeya iwe inalima mpunga

Makolo ni laana Kwa taifa[emoji3063]
1726467386954.jpg
 
Kuna timu inajitapa eti imehusika kuleta uhuru wa Tanzania ila haijawahi kuvuja jasho na kucheza katika mazingira magumu ambayo unaweza hata kuwaza kama baada ya mechi utabaki na uhai wako. Simba ndiyo timu pekee Tanzania ambayo imepitia mazingira hayo mara nyingi kuliko timu yoyote ile.

Tuanzie miaka ya 70, Simba ilifanyiwa vurugu nchini Misri, kipa wake akanyang'anywa gloves ikatolewa katika mazingira ya kutatanisha sana. Kama sikosei hii ilikuwa hatua ya nusu fainali (nikosolewe kama nimekosea).

Kuna ile mechi ya Sudan miaka ya 90 Simba vs El Mereikh. Simba walifanyiwa vurugu mbaya sana uwanjani, wakapigwa mawe sana tu.

Tunakuja mechi ya jana, Simba vs Al Ahly Tripoli. Hivi unadhani Simba wangepata goli pale hali ingekuwaje? Unadhani hili halikuwa vichwani mwa wachezaji? Unafuu pekee kiusalama jana ulikuwa kukubali kufungwa ila wachezaji wakakomaa, hafungwi mtu hapa!

Naomba Simba ianze kupewa heshima inayostahili nchi hii, tafadhali.
poleni...tatizo mmezidi uchawi
 
poleni...tatizo mmezidi uchawi
Kama kuna viashiria vya uchawi katika ile mechi basi ungewashutumu zaidi wale Al Ahly maana mipira ilikuwa inawapita wachezaji wa Simba katika mazingira ya kutatanisha
 
Back
Top Bottom