Simba Sports Club achaneni na nia yenu ya kumfukuza kocha wetu Patrick Aussems kwani tutakuja kujuta na kulia akiondoka

Simba Sports Club achaneni na nia yenu ya kumfukuza kocha wetu Patrick Aussems kwani tutakuja kujuta na kulia akiondoka

Huyo Aussems mwenyewe amekuja kwa 10 per cent, haiingii akilini unamwacha Leschante na Masoud Jouma unamleta kocha ambae hata kufanya sub ni issue.

Ulipomtaja huyo Masoud Djuma Irambona ndiyo nimekuona ' Mpuuzi ' kabisa na kumbe huijui Simba SC na yaliyokuwa yakiendelea kati ya Wachezaji wa Simba SC na huyo Kocha wako ambayo kwa bahati mbaya siyo ya Kimaadili kwa Mimi kuweza Kuyaanika hapa ila Watu wa Mpira na Watoto wa Mjini tunayajua na ndiyo maana tulipiga Kelele zetu ili aondolewe mapema kabla hali haijawa mbaya na nashukuru Uongozi ulitusikia na ukaachana nae.
 
Lewing ni wa wapi

Anaitwa Patrick Leiwig ambaye alishawahi kuwa Kocha Wetu na baadae tukaachana nae akaenda Stand United ya Shinyanga ambako huko nako alishindwa na kuamua Kuondoka Kwake kurudi Kwao. Ni Mzee na kwa taarifa za sasa zinasema kuwa hata Afya yake sasa siyo nzuri na amezidi Kudhoofu tu huko aliko. Alikuwa ni Kocha mwenye kupenda mno Kutumia Vijana na ndiyo huyu alifanya Wachezaji kama akina Said Ndemla, Jonas Mkude, Christopher Edward na wengineo Kuanza Kuaminiwa ndani ya Klabu.
 
Kumuondoa uchebe kwa sasa ni upopoma tuu. mo atakua anataka kuleta uleule uswahili

Na ndiyo maana nimemuonya na kuionya Simba SC mapema sana juu ya hili. Simba SC wakiachana na Kocha Aussems watajuta.
 
Hapa popoma umechemsha hao vijana uliowataja wamepita chini ya makocha zaidi ya watatu kabla Patrick Liewing hajaja simba.

Mathalan Mkude na Edward Christopher wlianza kupata nafasi ya kikosi cha kwanza chini ya Milovan Cirkovic.

Said Ndemla alipandishwa kikosi cha kwanza na Abdallah Kibadeni pamoja na Ramadhan Singano baadae akaja kuwa regular starter chini Goran Kuponovic.


Anaitwa Patrick Leiwig ambaye alishawahi kuwa Kocha Wetu na baadae tukaachana nae akaenda Stand United ya Shinyanga ambako huko nako alishindwa na kuamua Kuondoka Kwake kurudi Kwao. Ni Mzee na kwa taarifa za sasa zinasema kuwa hata Afya yake sasa siyo nzuri na amezidi Kudhoofu tu huko aliko. Alikuwa ni Kocha mwenye kupenda mno Kutumia Vijana na ndiyo huyu alifanya Wachezaji kama akina Said Ndemla, Jonas Mkude, Christopher Edward na wengineo Kuanza Kuaminiwa ndani ya Klabu.
 
Aondoke zake hana adabu. Anaondoka kwenda kutafuta timu nyingine kihunihuni. Atuachie timu yetu. Wanakuja wenye weledi zaidi. Simba tuna pesa za Mo. Mtu akilete ujinga tunatimua tu.
 
Timu inaongoza ligi. Imefungwa mechi moja imetoa sare mbili. Ligi ndio kwanza hata nusu ya msimu haijafika.

Kuna mishabiki inataka kufukuza kocha. Wakati huo shabiki huyo ni shabiki pia wa Chelsea ya pale Uingereza lakini husikii akimshikia bango Lampard aondolewe ukizingatia timu inashika nafasi ya nne. Anaamini msimu bado anaweza fanya vizuri zaidi.

Kuna Mbumbumbu nyingine hapo juu inasema haiwezekani Kocha unafungwa na timu moja(Kagera Sugar) nje ndani. Wakati huo anaona kawaida tu Barcelona kufungwa nje ndani na Levante tena kwa goli nyingi tu.

Halafu atokee mtu aniambie type hizi za mashabiki zinafikiri kwa kutumia kichwa na sio kiungo kingine ntamtia mkwenzi huo hatakuja nisahau.
 
Hapa popoma umechemsha hao vijana uliowataja wamepita chini ya makocha zaidi ya watatu kabla Patrick Liewing hajaja simba.

Mathalan Mkude na Edward Christopher wlianza kupata nafasi ya kikosi cha kwanza chini ya Milovan Cirkovic.

Said Ndemla alipandishwa kikosi cha kwanza na Abdallah Kibadeni pamoja na Ramadhan Singano baadae akaja kuwa regular starter chini Goran Kuponovic.

Duh kweli katika hili nimekuwa Popoma kwani ' nimekengeuka ' mno kwa Rekodi zangu. Suala la Patrick linanipa taabu Mkuu.
 
Kuna mdau anamtaka Lechantre arudi Simba. Kiukweli Lechantre ni kocha mzuri ila falsafa ya kudefend kama Mourinho inaondoa utamu wa mpira. Timu inamiliki mpira muda wote wa mchezo lakini ushindi unakuwa moja bila tu. Na tabia yake ya kupanga wachezaji kuanzia beki na mbili mpaka kiungo mshambuliaji wote wazuiaji inaondoa zile amsha amsha. Huyu kocha ndio alikuwa anampanga Kapombe namba nane.

Raha ya mpira ni zile amsha amsha za washambuliaji na mawinga kupiga kambi kwenye goli la timu pinzani sio unaangalia mpira kama unatazama drafti au bao
 
Nadhani na Mimi sitokuwa mbali Kuyaiga haya Maamuzi yako na nitabaki zangu tu Kushangilia Timu zangu pendwa za Liverpool, Barcelona, AC Milan, PSG, Borussia Dortmund, Kaizer Chiefs, Corinthians, River Plate na Makabi Haifa.
Siku wakikutana Liver na Barca utashabikia timu gani?
 
MO hawezi kukubali kulipa uchebu milioni 23 kwa mwezi wakati wametolewa klabu bingwa caf, lazima atimuliwe
 
Imethibitishwa na vyanzo vya ndani kuwa hata Kitambi anaondoka anakuja Matola.

Wenyewe wana sema mafanikio ya msimu uliopita ni viongozi siyo Kocha,ndiyo hapo ujiulize viongozi walichangia kwa namna gani?
 
Imethibitishwa na vyanzo vya ndani kuwa hata Kitambi anaondoka anakuja Matola.

Wenyewe wana sema mafanikio ya msimu uliopita ni viongozi siyo Kocha,ndiyo hapo ujiulize viongozi walichangia kwa namna gani?

Acha Kusema Vyanzo vya ndani na badala yake sema tu kwamba hii tetesi umeisikia katika ile ' Segment ' ya ' Chabo Chabo ' ya Sports Headquarters ya Efm ya leo.
 
Mi nilidhani tangu timu iwe chini ya Mo ukiritimba kama huu umeisha kumbe bado,,,,kama ni kweli wana au watamfukuza bwana mandevu utakua uamuzi wa kibumbavuuuu kwa klabu ya simba tangu huu mwaka uanze katika nchii kwenye mpira.
Nimezifuatilia sababu za baadhi ya Viongozi wa Simba SC na Mashabiki ' Wapuuzi ' wachache juu ya sababu zao kutaka Kocha Mkuu wa Simba SC Patrick Aussems aondoke na Kugundua kuwa zote ni za Kipopoma. Moja ya sababu ambayo hadi hivi sasa imeniacha hoi ni kwamba baadhi ya Viongozi hawamtaki Kocha Patrick Aussems kwakuwa huwa hataki Wachezaji wakae Kambini muda wote na badala yake huwa anataka Timu ikusanyike Siku mbili kabla ya Mechi.

Sasa kama Simba SC tumeshakubaliana Kuingia katika Mfumo wa Kisasa ni kwanini tena tunakuwa na Mawazo ya Kiswahili Kiswahili hivi? Hivi Vilabu vikubwa na vyenye Maendeleo makubwa duniani Wachezaji wao huwa wanashinda tu Kambini Msimu mzima wa Ligi kama wako Shule za ' Bodingi ' ambazo wengi wetu tumepita huko?

Maoni yangu kama GENTAMYCINE na naomba mnisikie Kiumakini kabisa ni kwamba kama kuna Kocha ambaye Simba SC tunaweza kuwa tumepata bahati ya kuwa nae basi ni huyu Patrick Aussems. Nina Wachezaji Waandamizi kabisa wa Simba SC na mwingine sasa anacheza nchi nyingine wote kila ninapozungumza nao wanasema hawajaona tatizo la Kocha Aussems hasa Kimbinu na Kiufundi na Kuondoka Kwake kutaiathiri Klabu kwa Kiasi kikubwa mno.

Sikatai Aussems kama Binadamu anaweza akawa na Matatizo ( Mapungufu ) yake ila tukisema tumfanyie ' Assessment ' hakuna Mtu ambaye anaujua vyema Mpira na amewahi pia Kuucheza anaweza kukubali Kocha Aussems afukuzwe Klabuni. Moja ya Sifa Kuu ya Kocha japo zipo nyingi ni Kocha kuwa na Upendo na Ukaribu hasa wa Kiurafiki na Wachezaji wake kwani hii husaidia Yeye kuweza Kupitisha Mafunzo yake Kiurahisi kabisa na akafanikiwa. Hili Kocha Aussems amefanikiwa nalo kwa 100% ndani ya Klabu ya Simba.

Hivi Kocha ambaye hadi hivi sasa ameifanya Simba SC iongoze Ligi, Timu inacheza vizuri na hata kama huwa inafungwa au inatoka Sare nayo ni sehemu ya Mchezo kwani Falsafa ya Mpira duniani kote inasema kuwa Mpira ni Mchezo wa Kushinda, Kufungwa na Kutoka Sare. Simba SC isifungwe au isitoke Sare yenyewe ni nani? Ni Timu ya Mungu? Kama ni sababu za Kiufundi Kocha Aussems hana tatizo ndani ya Simba SC ila kama Kocha Aussems anafukuzwa pengine kwakuwa hapendi Ujinga, Utoto na Upumbavu tena ule wa Kupangiwa Kikosi au wa kutoa 10% kwa baadhi ya Watu wa karibu wa Simba SC na Viongozi basi ni sawa afukuzwe tu na Mimi GENTAMYCINE nitapiga Goti kwa Mungu ili niiombee ' Laana ' Klabu yangu hii pendwa ya Simba SC.

Mwisho najua na nina uhakika kuwa ' Mwekezaji ' wa Simba SC ' Tajiri ' Mohammed Mo Dewji ni Mdau mzuri na mkubwa wa huu Mtandao wa JamiiForums, tunae hapa 24/7 japo huwa hakai muda mwingi kutokana na Ratiba zake lakini pia ni Mtu ambaye huwa anapenda Kunisoma GENTAMYCINE. Hivyo basi namwomba ( nakuomba ) Mohammed Dewji hebu na Wewe acha Kuingizwa katika huu ' Uswahili ' wa baadhi ya Viongozi wa Simba SC na Mashabiki ' Wapuuzi ' ambao wanakudanganya kuhusu Kocha Patrick Aussems na Wewe unawaamini na Kukubali kuwa atimuliwe.

Nina uhakika tena wa 100% kama Kocha Patrick Aussems atabaki Simba SC, akiaminiwa zaidi, akipewa Ushirikiano, Uweledi ukitawala ndani ya Uendeshaji wa Timu yetu ya Simba, akaongozewa Wachezaji Wawili au Watatu tu ( hasa Washambuliaji ), tukaachana na hawa Wabrazili wa ' Madili ' huku tukijitahidi Kuwarudisha akina James Kotei na Emanuel Okwi Simba SC itafanya vyema si tu katika Ligi Kuu yetu y VPL bali hata katika Mashindano ya Kimataifa ya Barani Afrika.

GENTAMYCINE nakataa na nasema Kocha Patrick Aussems asifukuzwe ndani ya Klabu yetu ya Simba kwani tutakuja Kujuta.
 
Alifanya hivyo baada ya kumuona ni effective zaidi kwenye defence na attack tofauti na Mkude na Mzamiru ambao wote ni defence midfielders.

Kapombe anafanya vitu viwili kwa usahihi uwanjani lateral movement na vertical movements

Anauwezo mkubwa kwenye battle za one against one kuliko Mzamiru.

Passing accuracy yake iko juu kuliko Mzamiru au Ndemla ambao ndiyo walikuwa viungo wajuu baada ya Kotei kurudishwa kucheza kama defender.

Anaweza kuwin aerial duels zaidi kuliko Mzamiru kulingana na height yake.

Lechantre was right.
Kuna mdau anamtaka Lechantre arudi Simba. Kiukweli Lechantre ni kocha mzuri ila falsafa ya kudefend kama Mourinho inaondoa utamu wa mpira. Timu inamiliki mpira muda wote wa mchezo lakini ushindi unakuwa moja bila tu. Na tabia yake ya kupanga wachezaji kuanzia beki na mbili mpaka kiungo mshambuliaji wote wazuiaji inaondoa zile amsha amsha. Huyu kocha ndio alikuwa anampanga Kapombe namba nane.

Raha ya mpira ni zile amsha amsha za washambuliaji na mawinga kupiga kambi kwenye goli la timu pinzani sio unaangalia mpira kama unatazama drafti au bao
 
Alifanya hivyo baada ya kumuona ni effective zaidi kwenye defence na attack tofauti na Mkude na Mzamiru ambao wote ni defence midfielders.

Kapombe anafanya vitu viwili kwa usahihi uwanjani lateral movement na vertical movements

Anauwezo mkubwa kwenye battle za one against one kuliko Mzamiru.

Passing accuracy yake iko juu kuliko Mzamiru au Ndemla ambao ndiyo walikuwa viungo wajuu baada ya Kotei kurudishwa kucheza kama defender.

Anaweza kuwin aerial duels zaidi kuliko Mzamiru kulingana na height yake.

Lechantre was right.

Mwalimu Kashasha ni Pacha wako kwa Kuzaliwa au ni Baba yako Mzazi hivyo Umerithi Uchambuzi wake au labda ni Yeye Mwenyewe?
 
Back
Top Bottom