Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,699
- Thread starter
- #281
167
Almasi Dilunga
Saa 12:25 alfajiri…
ILIKUWA Jumamosi tulivu mno na hali ya hewa ilikuwa ya ubaridi kidogo, angani wingu zito la mvua lilikuwa likijitengeneza taratibu na hivyo kuashiria kuwa mvua ilikuwa mbioni kunyesha. Ndege angani walikuwa wanashindana kuimba na kuruka huku na kule kwenye vilele vya miti. Na kwenye mapaa na vibanda majogoo pia yalishindana kuwika.
Ni mwezi mmoja na nusu ulikuwa umepita tangu tutoke Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma na kurudi Kilosa. Mtoto Mariam alikuwa amepata nafuu na alikuwa akiendelea vizuri baada ya kuongezewa damu na kisha kupewa dawa ambazo tuliambiwa tuwe tukimpa kila wiki.
Alfajiri hiyo nilikuwa nafanya mazoezi ya kukimbia mbio za taratibu yaani jogging, pembezoni mwa reli ya kisasa inayotoka Morogoro kuelekea Dodoma. Nilikuwa nimevaa jezi ya Manchester United na raba nyepesi nyeusi miguuni.
Ilikuwa ni kawaida yangu kudamka alfajiri na mapema kila siku na kufanya mazoezi ya mwili ikiwemo ya kukimbia umbali wa kilomita zisizopungua tano.
Mbio zangu ziliishia kwenye kijumba chetu kilichojengwa kwa tofali za kuchoma, katika eneo la Kichangani, mojawapo ya mitaa maarufu ya Mji wa Kilosa. Hiki ni kijumba ambacho nilikijenga kwa nguvu zangu katika miezi miwili tu kutokana na kufanya kazi kwa bidii.
Kila mtu pale mtaani, eneo la Kichangani, alinipenda sana kwa sababu ya upole wangu na pia sikuwa na makuu hata chembe, niliishi vizuri na watu hasa majirani zetu.
Saa 2:30 asubuhi ilinikuta nikiwa nimeketi sebuleni nikiwa nasikiliza kipindi cha uchambuzi wa habari mbalimbali za michezo kwenye redio yangu ndogo ya kutumia betri, ni wakati huo ambao Zainabu aliingia ndani akiwa amebeba ndoo ya maji kichwani na mkononi alishikilia mfuko mdogo mweusi.
Alipoingia tu aliuachia ule mfuko mweusi ukaangukia chini karibu na miguu yake na kisha yaliitua ile ndoo, akajinyoosha huku akipumua kwa nguvu, halafu akatumia upande wa khanga aliyojifunga kujifuta jasho usoni.
Kisha aliliendea kabati dogo la vyombo lililokuwepo pale sebuleni, akalifungua na kuchukua kiberiti kilichokuwa nyuma ya jagi la sukari na kutoka nacho nje.
Baada ya dakika zipatazo kumi Zainabu aliingia tena ndani na kuniambia kuwa amepeleka maji ya kuoga bafuni. Niliinuka, nikavua nguo za mazoezi nilizovaa na kujifunga khanga kisha nikaelekea bafuni wakati Zainabu akipasha moto kiporo cha wali jikoni.
Huko bafuni nilijimwagia maji na kupiga mswaki, na dakika kumi baadaye nilitoka nikiwa nimechangamka kweli kweli. Kweli maji ni tiba kwani sasa nilikuwa najisikia safi zaidi. Nilipoingia ndani Zainabu alikuwa anaandaa meza, nikapitiliza moja kwa moja chumbani ambako nilivaa suruali nyeusi ya kadeti, singlendi nyeupe na shati jeupe lenye mistari myeusi.
Kisha nikatoka sebuleni na kumkuta Zainabu akiwa ameshaandaa kifungua kinywa; chai na kiporo cha wali na maharage yaliyoungwa na nazi. Kilikuwa chakula kitamu sana nilichoamini kingeisindikiza vizuri Jumamosi ile tulivu mno.
Nilipomaliza kunywa chai nilimwambia Zainabu kuwa nakwenda kumjulia hali rafiki yangu Almasi kwa kuwa siku iliyokuwa imetangulia nilimwacha akiwa na majeraha.
Kabla sijaondoka nilitandaza mikono yangu huku nikimtazama Zainabu kwa uso uliochanua kwa tabasamu. hii ilikuwa kawaida yangu kumkumbatia Zainabu na kisha kumbusu kwenye paji la uso wake kabla sijaondoka. Zainabu alinitazama kwa sekunde chache, tukawa tunatazamana. Kisha naye akatandaza mikono yake. Tukakumbatiana.
Tulibaki tumekumbatiana kwa kitambo fulani tukiwa kimya. Yaani hakuna aliyesema chochote ingawa nilihisi kuwa mioyo yetu ilikuwa inawasiliana. Mikono yake kaizungusha shingoni kwangu, mikono yangu nimeizungusha kiunoni kwake. Zainabu alionekana kujiachia mikononi kwangu… ile kifua chake kilivyokua kinanichoma, niliweza kusikia sauti ya mapigo yake ya moyo.
Pasipo kutarajia Zainabu alinishika kichwa changu akakiinamisha kumwelekea kisha aliniletea mdomo wake na kuuzamisha ulimi wake kinywani mwangu. Ndimi zetu zikakamatana vilivyo huku pumzi nyepesi ikipita puani. Mikono yangu chakaramu ikaanza kusafiri taratibu hadi kifuani kwake na hapo nikaanza kuyatomasa matiti yake taratibu kwa ufundi wa hali ya juu.
Zainabu aliachia sauti hafifu ya mguno wa mahaba kama mtu aliyekuwa amepagawa na wazimu wa mapenzi. Macho yake malegevu yalitaka kufumba lakini yaliishia katikati ya mboni zake na hivyo kumfanya aonekane kama aliyelewa.
Kisha ncha ya ulimi wangu ilifanya ziara kwenye tundu la sikio lake na hapo nikasikia tena sauti hafifu ya mguno wa mahaba kutoka kwa Zainabu sambamba na mapigo ya moyo wake kuanza kwenda mbio. Sasa Zainabu hakuweza tena kuvumilia badala yake kwa papara akaanza kunivua shati langu. Mara akaonekana kusita baada ya kuhisi kulikuwa na mtu mwingine aliyeingilia faragha yetu.
Wote tuligeuza shingo zetu haraka kutazama upande tuliohisi kulikuwa na mtu, tukamwona mtoto Mariam akiwa amesimama kando huku akitutazama kwa udadisi. Tukatazama.
“Lakini… kwani lazima leo uende kwa Almasi! Si unaweza kwenda hata siku nyingine?” Zainabu aliniuliza kwa sauti ya puani huku akiwa bado amenikumbatia. Alikuwa akinitazama kwa namna ambayo ilionesha utayari wake.
“Kwani sijakwambia kwamba Almasi yupo matatizoni? Ni mimi pekee ninayeweza kumsaidia,” nilimwambia Zainabu huku nikimtazama machoni. Kisha nikaongeza, “Kuna mambo hayapo sawa na maisha yake, hivyo siwezi kumwacha peke yake.”
Ni kweli. Almasi alikuwa rafiki yangu mkubwa. Tulielewana sana, pengine kwa kuwa wote tulikuwa na uwezo mkubwa kiakili na upeo wa kujua mambo ingawa niliamini Almasi alikuwa ni zaidi ya mtu wa kawaida, alikuwa genius.
Almasi alikuwa kichwa ile mbaya, yaani alikuwa ana akili sana na mwenye kujua mambo mengi mno. Alikuwa hivyo kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu, tatizo lake kubwa lilikuwa kuvuta sana bangi na misimamo yake. Bila hivyo bila shaka angekuwa anafundisha chuo kikuu na pengine angeshaukwaa uprofesa.
Hata hivyo, kwa upande wangu sikujua kuhusu kiwango cha elimu yangu kwa kuwa sikuwa nakumbuka chochote kilichotokea nyuma. Hata hivyo niliamini kuwa nayajua mengi kwa kuwa nilikuwa na tabia ya kumpa kila mtu nafasi ya kuwa mwalimu wangu. Kila mtu alinifunza kwa yale aliyoyafahamu na niliheshimu kauli na mawazo ya wote kwa uzito sawa. Hata hivyo, uelewa wa mambo ulibaki kuwa juu yangu mwenyewe.
Kukutana kwetu kulikuwa kwa bahati tu. Ilitokea tu mwezi mmoja uliokuwa umepita, siku moja baada ya kuachishwa kazi kwenye kampuni ya Yapi Merkezi iliyoshughulika na mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Morogoro hadi Makutupora Dodoma, nilikuwa na mawazo mengi nikiwa sijui nini nifanye.
Japo nilijitahidi kuonekana nipo sawa na kwamba sikujali kusimamishwa kazi lakini ukweli siku hiyo sikuwa sawa kihisia na hivyo jioni ya siku hiyo niliamua kutoka nifanye matembezi. Niliamua niende mbali na makazi ya watu, sehemu tulivu zaidi ili nikatafakari hatma yangu.
Ilikuwa majira ya saa kumi na mbili na ushee jioni, jua lilikuwa limekwisha anza kuzama na kiza kikianza kuchukua nafasi yake, anga la rangi nyekundu lilikuwa likinywea katika ukungu na nyota hafifu zilikuwa zinaanza kujitokeza moja baada ya nyingine, na kwa mbali, upande wa Magharibi, wekundu ulikuwa ukififia na kiza kikianza kuchomoza taratibu.
Muda huo nilikuwa nimerudi kutoka kuonana na Jerome baada ya lile Sakata la mchana wa siku hiyo. Nilikuwa nimemfuata nyumbani kwake baada ya saa za kazi, nilipanga kukutana naye uso kwa uso ili nimweleze kile nilichokusudia.
Endelea...