Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,699
- Thread starter
- #121
96
Bila ubishi nikainuka, tukakumbatiana na kuanza kucheza. Nilipomkumbatia tu nikahisi kama chaji za umeme zinapita mwilini mwangu pale kifua cha Jamila kilichobeba chuchu laini kilipogusana na kifua changu. Kadiri muziki ulivyokuwa ukienda ndivyo tulivyojikuta tukikumbatiana kwa nguvu zaidi. Muziki ulimalizika lakini bado tuliendelea kukumbatiana kwa nguvu.
Taratibu Jamila akaupeleka mkono wake wa kulia chini kidogo ya kiuno changu na kukutana na kitu kigumu kilichotuna. Taratibu na kwa ufundi akakishika kitu kile kilichotuna na kunifanya nianze kuhema kwa nguvu kisha nikampiga busu zito lililomfanya aweweseke.
Nikataka kulianzisha pale pale sebuleni lakini Jamila akanitaka tuelekee chumbani, na mara tu tulipoingia chumbani hatukuchelewa, kukawa na mpambano mkali wa mechi ya kukata na shoka huku safari hii nikiwa naipangua mitego ya Jamila aliyoniwekea kiasi kwamba katika mizunguko mitatu tuliyokwenda nilimwonea kupita maelezo na kwa kuwa nilikuwa ndiyo mchezeshaji mkubwa wa mechi Jamila alijikuta akimwagikwa na machozi, na sikujua kama yalikuwa ya furaha au karaha!
Kiukweli, pasipo kujali maumivu ya mguu wangu nilimpagawisha sana Jamila hadi ikafikia wakati alikuwa akizungumza maneno ambayo sikuweza kuyaelewa, na baadaye aliniomba apumzike kwani hali ilishakuwa mbaya. Na hadi kunakucha wote tulikuwa hoi. Hakuna aliyekuwa na hamu na mwenzake.
Ukimya mkali ulitawala kati yetu huku kila mmoja akiyasikilizia mapigo yake ya moyo yalivyokwenda. Jamila alijinyanyua taratibu na kulaza kichwa chake kiduani kwangu huku akinikumbatia, alikuwa analia kilio cha kwikwi, wasiwasi ukaanza kunivaa.
“Baby mbona unalia?” nilimuuliza kwa wasiwasi.
“Jason, nakupenda sana hadi nahisi kuchanganyikiwa, nahitaji uwe mume wangu halali wa ndoa,” Jamila alisema huku akijitahidi kuyazuia machozi yaliyozidi kumtoka.
“Hilo haliwezekani kwa sababu ya tofauti zetu za rangi na dini. Ndugu zako hawawezi kukubali uolewe na Mbantu kama mimi.”
“Nalijua hilo Jason, ila najua nitalimaliza vipi na lazima utanioa,” Jamila alisema na kunifanya niogope mno. Nilianza kujilaumu kukutana naye.
“Jamila!” niliita kwa wasiwasi.
“Mmh!”
“Kubali tu kuolewa na mume uliyetafutiwa na ndugu zako ili usije ukakosa radhi ya wazazi,” nilijaribu kumshawishi.
Jamila alikaa kimya kwa kitambo fulani akionekana kuzama kwenye lindi la mawazo, kisha akainua uso wake kuniangalia. Machozi yaliendelea kumtoka.
“Jason, naomba unisikilize, kuna kitu nataka nikwambie ila naomba usikasirike,” Jamila aliniambia kwa sauti ya kunong’ona.
“Niambie tu siwezi kukasirika,” nilisema huku mapigo ya moyo wangu yakienda mbio isivyo kawaida.
“Hutokasirika?” Jamila aliniuliza huku akiniangalia machoni.
“Ndiyo.”
“Nina mpango wa kutoroka kabla ya harusi, tafuta nchi nzuri twende tukaishi kama ni fedha ninazo za kutosha,” Jamila alisema huku akifuta machozi.
“Nadhani unajua kwetu tumezaliwa watatu, kaka yetu Selemani na sisi wa kike wawili. Dada yangu Salma kwa sasa yupo Uarabuni ameolewa. Kwa upande wa baba yangu wao walizaliwa wawili tu, yeye na kaka yake, baba yetu mkubwa…” Jamila alizungumza katika hali ya utulivu, muda huo alikuwa amenikumbatia huku akiendelea kulia.
“Baba mkubwa hakubahatika kupata mtoto na alikuwa na mali nyingi… alinipenda sana na kabla hajafariki aliacha wosia kuwa mimi ndiye mrithi wa mali hizo… kwa hiyo mimi ni tajiri ila kwa kweli siyafurahii maisha ya nyumbani kwetu, nimekuwa ni mtu wa kuchungwa chungwa kiasi kwamba ninakosa uhuru wa kufanya mambo yangu,” alisema huku akiendelea kutiririkwa na machozi.
“Basi usilie, baby,” nilimwambia kwa sauti tulivu, hata hivyo nilikuwa najilaumu kukutana na Jamila.
“Hapana Jason, ndugu zangu wananionea sana, hawanipi uhuru… na mbaya zaidi huyo mwanaume wanayetaka kuniozesha kiumri ni sawa na baba yangu.”
“Kwani ana umri gani?”
“Sijajua ila hata wewe ukimwona utashangaa! Kisa tu ni tajiri mkubwa na anamiliki visima vya mafuta!” Jamila alisema huku akizidi kunikumbatia na kulia.
“Jason!” Jamila aliniita kwa sauti ya kunong’ona.
“Mmh!”
“Naomba uniambie ukweli, unanipenda?” aliniuliza huku akiniangalia machoni.
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Nisikudanganye, mimi nina wivu sana na nipo tayari kupoteza fedha yangu ili kumkomesha yeyote atakayeingilia uhusiano wetu…”
“Kivipi? Si unajua kuwa nina mchumba na karibuni tutaoana?” nilimuuliza Jamila huku nikimtazama kwa umakini.
“Nitafanya kila linalowezekana umsahau…” Jamila alisema huku akiniangalia machoni na kuchia tabasamu.
“Usiniulize nitafanyaje kwani hiyo ni siri yangu ya moyo. Na ukiachana na Rehema, msichana mwingine yeyote atakayejitokeza atanitambua mimi ni nani? Naomba tu tusije tukalaumiana!”
Dah. mwili wote uliingiwa ganzi. Nilizidi kumwogopa Jamila. Nikatamani kumfukuza halafu nimwambie asije tena nyumbani kwangu. Wazo jingine likanijia kuwa akiondoka tu nihame pale na nikaishi kwenye nyumba nyingine au nimfuate Rehema huko wilayani Misungwi.
“Lakini Jamila, naomba usijaribu kufanya jambo lolote litakalomuumiza Rehema sitakuelewa kabisa,” nilimpa onyo huku nikiidhibiti hasira yangu. “Pia sidhani kama ndugu zako ni wajinga kukuchangulia mume, wanajua kuwa ndiye atakayekufaa…” nilijaribu kumsihi.
“Mambo ya kuchaguliana waume yamepitwa na wakati, nakuapia hakuna mwanaume atakayenioa ila wewe. Ikishindikana basi nitajua cha kufanya na sitataka kuolewa tena maishani mwangu. Wewe ndiyo mume wangu, wewe ndiyo mwanga wa maisha yangu.”
Maneno ya Jamila yalikuwa yamenitisha mno, kila nikimwangalia sikuona yakini kwenye macho yake. Asubuhi ile tulinyanyuka kiuvivuvivu tukaingia bafuni na kuoga, kisha nilibadilisha shuka na kutandika vizuri kitanda changu na wakati huo Jamila alikuwa anaandaa kifungua kinywa.
Ilikuwa siku mpya, siku ya Jumatatu na asubuhi ile tuliagana nikaenda kazini huku Jamila akielekea kwa shangazi yake kwa ajili ya safari ya Masumbwe.
Siku ile nilifanya kazi nikiwa na mawazo mengi na nusura mawazo hayo yaharibu ufanisi wangu wa kazi. Hatimaye nilipanga kubadili namba ya simu na kuihama ile nyumba niende nikajifiche Mwime kwenye nyumba niliyojenga ambayo hadi wakati huo haikuwa ikikaliwa na mtu.
Jioni ya siku ile baada ya kutoka kazini nilibadilisha namba ya simu na kuwajulisha watu wangu wachache akiwemo Rehema kisha nikapanga kwenda kwanza Nyasubi kumtafuta Asia kisha baadaye niangalie utaratibu wa kuhamisha vitu kupeleka Mwime. Nilishukia Chattle Restaurant kisha nikaanza kutembea taratibu nikiambaa ambaa kando kando ya barabara kuelekea eneo alilokuwa akiishi Asia. Mtaa ule haukuwa na msongamano mkubwa na hivvyo sikupata taabu wakati nikitembea.
Itaendelea...