Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Litro na moneytalk kula na kuliwa kwenye anga za ushushushu ni kama uji na mgonjwa. Hata huyo Rehema mnayemuonea huruma kama afisa kipenyo akiwa kazini kuna mazingira ya kazi yatamlazimisha kuliwa ili kupata taarifa mzee baba akijua wala hatakuwa na nongwa.

Hivyo kaeni kwa kutulia[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] acheni makasiriko

By the way, Bishop Hiluka tuletee mambo weekend isijekuwa ndefu[emoji2][emoji2][emoji2]

Sent from my SM-T555 using JamiiForums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]nimekupata ndugu yake na jason
 
taharuki..jpg

324

Mwafaka…



Saa 6:15 mchana…

KULISHAKUCHA muda mrefu na sasa ilikuwa nusu siku, jua likiwa utosini. Hadi muda huu sisi watatu hatukuwa tumeambua japo lepe la usingizi. Tulikesha na kulipombazuka tulijiweka fiti kwa mazoezi mepesi kisha tukaketi kikao kifupi na kupeana majukumu ya siku hiyo kabla hatujaingia kazini kutimiza majukumu yetu, japokuwa penzi zito la Pamela lilinifanya niwe hoi kwa uchovu.

Pamoja na uchovu huo lilikuwa limeamsha ari mpya nafsini mwangu, kupitia mahaba mazito aliyonipa Pamela. Kitu fulani kilikuwa kimeanza kujengeka moyoni mwangu.

Kumbukumbu za penzi motomoto tulilopeana kule bafuni nyumbani kwa Luteni Lister zilikuwa zinapita kichwani kwangu, nikakumbuka jinsi nilivyoingia bafuni na kumkuta Pamela akiwa amesimama katikati ya chumba cha maliwato ya jumuia akiwa ametoa nguo zake na kubakiwa na bikini na sidiria tu. Sikujua kama nia yake ilikuwa kujimwagia maji au vipi! Nilimkuta akiwa ameelekeza uso wake upande wa ukutani akiugeuzia mlango mgongo.

Nilipoingia Pamela alionekana kushtuka na kugeuza shingo yake kutazama nyuma, macho yake legevu kwa sababu ya pombe na pia kwa kuwa yalikuwa yakipambana na usingizi, yalinitazama kwa tuo kama mtu ambaye hakuamini alichokuwa akikiona pale.

Kwa muda nilibaki nimesimama huku nikilitathmini umbo lake zuri kuanzia chini miguuni hadi kichwani kwake. Na hapo Pamela akageuka mzima mzima kunikabili.

Sasa hisia zangu zilianza kuwa taabani hasa pale macho yangu yalipoanza kufanya ziara katika kifua chake, nikaziona chuchu zake laini zilizosimama kwa utulivu juu ya matiti yake yaliyofichwa kwenye sidiria. Kisha macho yangu yakashuka taratibu hadi kwenye tumbo lake dogo na kukiona kitovu laini chenye kishimo kidogo.

Macho yangu yakaendelea na ziara na yalipofika kiunoni nikaiona nyonga yake laini yenye mifupa miteke iliyopakana na mzigo imara wa makalio ya ukubwa wa wastani yaliyotuama vyema na nilipoyashusha zaidi nikaiona minofu ya mapaja yake makubwa yaliyokaza kutokana na mazoezi ya kila siku. Macho yangu yalipovutwa kutazama katikati ya mapaja yakasababisha mshumaa wangu uliokuwa umesimama dede kuanza kuuma kutokana na misuli yake kukaza.

Wakati nikiwa katika hali ile ya mduwao, Pamela akaamua kuvunja ukimya. “Jason!” aliniita kwa sauti tulivu ya chini huku akishusha pumzi ndefu.

“Unasemaje, Pamela!” niliitika huku nikimtazama moja kwa moja machoni.

“Umefuata nini huku bafuni?” Pamela aliniuliza huku akinitazama usoni kwa macho yake legevu.

Sikumjibu na badala yake nilimsogelea taratibu na kumshika kiuno chake chembamba kiasi chenye mifupa miteke na kuanza kukiminya minya kiasi na kuziamsha taratibu hisia zake. Kisha nikamuegemeza ukutani na kumbana kwa ukaribu zaidi, na hapo ndimi zetu zikakutana. Baada ya hapo nilichoweza kusikia ilikuwa ni sauti nyepesi ya pumzi yake zikipenya kwenye tundu za pua yake sambamba na miguno ya mahaba. Hata hivyo kuna muda alitaka kuleta pingamizi lakini hakufanikiwa kwa kuwa nilimdhibiti.

Nilipotaka kumvua bikini akanizuia, “Usiwe na haraka babu wee, acha nikuoneshe mambo, si umelilia mwenyewe!” Pamela alisema kisha akaangua kicheko na kunisukumia sakafuni, nikakaa chini huku nikihema kwa nguvu kama simba aliyemkimbiza swala na kumkosa.

Pamela akanisogelea na kunigeuzia makalio yake kisha akaja juu yangu na kupiga magoti, akakaa kama mtoto anayetambaa. Taratibu akaanza kucheza kuendana na muziki uliosikika kwa mbali toka kwenye redio ya Luteni Lister iliyokuwa sebuleni. Kwa hali hiyo akawa ananipagawisha kwa makalio yake yenye ukubwa wa wastani aliyokuwa akiyachezesha kwa nyuma na kuyafanya yawe yanatetemeka tetemeka.

Nikaona kama alikuwa ananizingua, nikamsukumia mbele na kusimama kisha nikamshika kiuno chake na kuanza kukiminya minya tena kabla sijaivuta ile bikini na kuichana kisha nikaitupia kando. Akabaki mtupu. Hakukubali, kama mtu aliyepandwa na wazimu wa mapenzi alianza kunivua nguo zangu na kuzitupilia mbali kisha akanishika mkono na kuniongoza taratibu hadi kwenye bomba la mvua, akalifungua na maji yakaanza kutumwagikia na kuzidisha kaubaridi kalikotufanya tukumbatiane kwa nguvu.

Nikajiuliza kwa nini nilikuwa namchelewesha? Nikamwinamisha ili nianze kuchimba dhahabu kwenye mgodi lakini yeye akawahi kuinuka na kunitaka nilale chali chini sakafuni, nikalala bila kuwa na hiana yoyote japokuwa pale sakafuni kulikuwa na maji. Kisha Pamela akaja juu na kuushika mshumaa wangu uliosimama dede japokuwa haukuwa na miguu, akaukalia taratibu na kuuzamisha kwenye mgodi. Joto kali la mgodi wake likanipagawisha na kunifanya nihisi kupaa angani huku nikihisi raha isiyo kifani.

Huku mikono yake akiwa ameikita kifuani kwangu akaanza kukichezesha kiuno chake kama pangaboi huku akiupeleka mshumaa wangu katika zile pande kuu nne za dunia pasipo kujali kama angeutengua au kuuvunja.

Niligundua kuwa Pamela alikuwa mwanafunzi aliyehitimu vizuri katika darasa la mahaba na kwa kweli alifanikiwa kunisahaulisha kwa muda juu ya mikasa yote niliyopitia tangu nilipoanza harakati za upelelezi juu ya tukio la kigaidi kwenye jengo la Alpha Mall. Ilikuwa starehe ya kipekee ambayo nilikuwa sijaipata tangu Rehema alipoondoka kwenda Tabora.

Kama nyati mwenye hasira kali nilimnyanyua Pamela na kumpigisha magoti kama mtoto anayetambaa, nikamshikilia kiuno chake huku nami nikiwa nimepiga magoti na kuufikia vizuri mgodi wake, nikaanza kuchimba nikimpelekea moto usio wa kitoto. Muda wote wakati nachimba na kupekecha Pamela alikuwa akitoa vilio na vicheko vya raha na kunifanya niongeze kasi ya mashambulizi katika mgodi wake.

Hadi tunaamua kuachana, wakati tayari kulishaanza kupambazuka, tulikuwa tumekwisha enda ngwe mbili za pambano kali lililotawaliwa na rafu na ubabe wa kila aina. Kisha tukaoga kwa pamoja kuondoa uchovu na kwenda kufanya mazoezi.

Kwa namna moja au nyingine Pamela alikuwa ameuteka moyo wangu na sasa nilianza kuona ugumu wa kufanya kazi nikiwa karibu naye kwa kuchelea kuharibu kazi. Alikuwa amezitendea vyema hisia zangu na raha tuliyopeana ilitufanya siku hii tusitazamane usoni. Muda mwingi macho ya Pamela yalikuwa yakinitazama kiwiziwizi

_____

Wakati mawazo haya yakipita kichwani kwangu ilikuwa imeshatimia saa sita na robo mchana na tulikuwa tumekaa kwenye viti ofisini kwa mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, mzee Rajabu Kaunda, kwa kikao kifupi cha kupashana habari za huko tulikotoka. Ni katika kikao hiki ndipo tulipopata habari za ile code ngumu, ‘G2603H70=RM’, iliyotushinda kuifungua.

“Wataalamu wa Code wameniambia kuwa wamefanikiwa kufumbua code hii japokuwa imewachukua muda mwingi kucheza nayo,” mkurugenzi mkuu alisema huku akimpatia Luteni Lister karatasi iliyokuwa imekunjwa vizuri ikiwa na maelezo yake. Luteni Lister aliipokea ile karatasi kisha akaifungua na kuanza kusoma kwa sauti.

“Hii herufi ‘G’ inasimama badala ya neno ‘Go’. Nambari ‘2603’ ni namba ya bikoni ya kiwanja ambacho kipo Mbezi Beach, hii ‘H’ inasimama badala ya neno ‘House’ huku nambari ‘70’ ikimaanisha namba ya nyumba hiyo, na tulipofuatilia tumegundua kuwa nyumba namba 70 ambayo ipo kwenye bikoni namba 2603 huko Mbezi Beach mmiliki wake ni bilionea maarufu wa Tanzania ambaye kwa sasa makazi yake yapo nchini Afrika Kusini, Rashid Mrutu, mume wa Ummi Mrutu, ndiyo maana ya zile herufi mbili za mwisho, RM…” Luteni Lister alisoma kwa sauti majibu ya lile fumbo. Halafu akaongeza.

Endelea...
 
taharuki..jpg

325

“Pia inasemwa kuwa, mfanyabiashara huyo ambaye kwa sasa ametengana na mkewe aliijenga nyumba hii kwa siri sana kiasi kwamba hata mkewe Ummi Mrutu hakufahamu kama mumewe alimiliki nyumba hii, na aliitumia kwa mambo binafsi ya siri sana! Kwa nini hakutaka mkewe ajue? Hakuna aliye na majibu…”

“Siri ndani ya nyumba ya Rashid Mrutu! Hapa kuna kitu, naomba mniamini… hii code imefungua kila kitu kuhusu upelelezi wetu juu ya kifo cha mama Ummi Mrutu!” nilisema kwa kujiamini. Kisha nikaongeza, “Hata hili suala la wanausalama kuniwinda kila mahali ili waniue ni kwa kuwa wana hofu ninaweza kunusa taarifa hizi, kwani wanashirikiana kwa karibu sana na mtandano huu hatari na ushahidi tayari tunao kuwa wanalipwa mamilioni ya fedha kuvujisha siri za serikali na za kiusalama kwa mtandao huu.”

“Unadhani huyu mfanyabiashara Rashid Mrutu anaweza kuwa ndiye aliyeidhinisha mamilioni ya fedha kwa wanausalama kupitia akaunti ya Kangaroo Group?” mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa aliniuliza huku akinikazia macho.

“Sidhani, nina uhakika! Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata kule Alpha Commercial Bank, fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya Kangaroo Group zimetokea kwenye benki mama iliyopo nchini Afrika Kusini, na sasa tunaambiwa kuna siri ya hatari ndani ya nyumba ya Rashid Mrutu ambaye baada ya kutofautiana na mkewe akahamishia makazi yake nchini Afrika Kusini! Hamuoni kama hapa kuna uhusiano fulani kati ya mambo haya?” nilisema kwa kujiamini kisha nikaongeza.

“Waziri Ummi Mrutu aliaminika kuwa mtu mwadilifu sana asiyeweza kumvumilia mtu yeyote asiye mwadilifu, na zipo taarifa kuwa mumewe alikuwa na makando kando kibao akiwa pia mmoja wa ma-tycoon wakubwa wa mihadarati duniani ndiyo maana wakatengana. Upo uwezekano kuwa waziri alikuwa anatishia mustakabali wa biashara zake ndiyo sababu akaamua kummaliza.”

Maneno yangu yaliwafanya watu wote mle ofisini kwa mkurugenzi mkuu wanitazame kwa mshangao mkubwa. Kwa namna fulani walistaajabia wepesi wa akili yangu katika kuhusisha mambo. Niliamini kabisa kuwa hayo ndiyo yalikuwa majibu ya fumbo lile gumu lililotushinda kulifumbua.

Na hapo Pamela akasema, na kwa mara ya kwanza tangu kulipokucha, alinitazama usoni, “Kwa maana hiyo, mwandishi wa ujumbe huu alikusudia kukufikishia taarifa za kukutaka uende Mbezi Beach kwenye nyumba nambari 70 iliyopo kwenye bikoni nambari 2603 ambayo ni mali ya Rashid Mrutu… huko kuna siri kubwa ambayo huenda ndiyo imesababisha kifo cha waziri, hili ni jambo moja… na la pili kuna hatari ofisini, hatujui ni ipi na katika ofisi ipi, yako binafsi au Idarani kwenye Taasisi za SPACE!”

Sasa kila kitu kilianza kuwa wazi, ulikuwa ni ukweli mchungu kuwa baadhi ya wanausalama wenzetu walikuwa mawakala wa mtandao huu hatari na walikuwa wakilipwa fedha nyingi.

Hata hivyo tulijikuta tukiwa na maswali lukuki; Ni nani aliyeuleta ule ujumbe nyumbani kwangu? Na ilikuwaje baadaye usiku akaonekana akiwa na Daniella ambaye tuliamini alikuwa mmoja wa wanausalama waliopo kwenye mtandao huu hatari, na ushahidi ulijionesha pale alipofanya jaribio la kutaka kutuua kwa bomu lililotegwa kwenye gari letu?

Nilipoanza kujiuliza ni nani ambaye angeweza kuwa ameuleta ule ujumbe nyumbani kwangu mara nikamkumbuka Sajenti Mambo. Nikakumbuka jinsi alivyotuokoa na kifo cha bomu lililotegwa kwenye gari kule benki. Na hapo ile picha ya mtu niliyemwona nyumbani kwangu usiku akiwa amevaa koti refu na kofia pana ya pama iliyoficha uso wake akiwa na Daniella kisha wakaondoka na gari aina ya Lexus ikajifunua. Sasa nilikuwa na uhakika kuwa mtu huyo alikuwa Sajenti Mambo!

Nikaamua kuwashirikisha maofisa wenzangu kuhusu hisia zangu, na wote tukakubaliana kumtafuta Sajenti Mambo ili tupate majibu ya maswali yetu, kwani ilionesha Sajenti Mambo aliyafahamu mengi kuhusiana na tukio lile la kigaidi.

“Kumbukeni kuwa Sajenti Mambo ni mmoja wa maofisa waliopo kwenye payroll list ya kulipwa mamilioni ya fedha toka akaunti ya Kangaroo, lakini mimi kwa sasa simwangalii kama mshukiwa bali kama shahidi anayeweza kutupatia majibu ya maswali yetu na mwanga zaidi kuhusiana na kazi hii,” nilisema na kushusha pumzi. Kabla sijaendelea Luteni Lister akaingilia.

“Nakubaliana na wewe, Jason. Tukimpata Sajenti Mambo tutakuwa tumepata mwanga wa nini kinaendelea. Nadhani tusipoteze muda zaidi, inatakiwa tuingie kazini sasa kumtafuta Sajenti Mambo kwa kutumia vyanzo vyote vya taarifa… tumpate kabla ya jioni ya leo,” Luteni Lister alisisitiza.

Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa alibetua kichwa chake kuafiki kisha akanyanyua kikonyo cha simu iliyokuwa mezani pake na kupiga namba fulani halafu akaiweka sikioni. “Victor, nakuhitaji haraka ofisini kwangu,” alisema na kukata simu kisha akairudisha mahala pake.

“Msemayo vijana nakubaliana nayo a hundred percent, Sajenti Mambo ni mtu muhimu sana kwenye kesi hii,” mkurugenzi mkuu wa Idara aliunga mkono hoja. “Lakini pia tunatakiwa kwenda mbele zaidi ili kubaini hii akaunti ya Kangaroo inamilikiwa na nani, na nani aliyezituma fedha zote hizi toka huko Afrika Kusini.”

Nilitaka kusema neno lakini kabla sijasema lolote mlango wa ofisi ya mkurugenzi mkuu ukagongwa mara moja na kufunguliwa, wote tukageuka kutazama mlangoni na kumwona ofisa mmoja, mwanamume mwenye umri wa takriban miaka arobaini akaingia ndani. mara moja nikatambua kuwa huyo ndiye Victor.

Victor alitusalimia kisha akasimama mbele ya mkurugenzi mkuu wa Idara kwa unyenyekevu mkubwa.

“Victor, fanya kila unaloweza nipate taarifa za akaunti hii ya Kangaroo iliyopo Afrika Kusini kabla ya jioni ya leo,” mkurugenzi mkuu wa Idara alimwamuru Victor akimwonesha karatasi ya taarifa za fedha za akaunti ya Kangaroo. “Nataka kujua kampuni hii imeanzishwa lini na wapi, nani hasa mwenye kampuni hii, na kila unachoweza kupata. Tumia njia zote unazoweza kupata taarifa. Sawa?”

“Sawa, mkuu,” Victor alijibu kwa unyenyekevu huku akiipokea ile karatasi na kuitazama mara moja tu kisha akayarudisha macho yake kwa mkurugenzi mkuu wa Idara. Kisha akapiga saluti na kuondoka.

Muda huo huo simu yangu ilianza kuita, nikaitazama na kuona namba ngeni. Bila kusita nikaipokea na kuiweka sikioni. “Hallo!”

“Jason!” sauti ya kiume upande wa pili wa simu iliita kwa wasiwasi.

“Ndiyo. Nani mwenzangu?” niliuliza kwa sauti tulivu huku nikikunja sura yangu.

“Albert Mambo hapa…” yule mtu upande wa pili wa simu alisema na kunifanya nishtuke kidogo kwani sikutegemea kumpata Sajenti Mambo kirahisi hivyo.

“Sajenti Mambo?” niliuliza kwa mashaka kidogo katika kutaka kupata uhakika. Watu wote mle ofisini kwa mkurugenzi mkuu wa Idara waliposikia nikilitaja jina la Sajenti Mambo wakawa na shauku ya kutaka kusikiliza. Nikaweka sauti kubwa (loud speaker) ili kila mmmoja aupate ujumbe moja kwa moja.

“Ndiyo, ndugu yangu. Kama hutojali naomba tukutane jioni ya leo kwa maongezi maana mambo hayako sawa kabisa katika nchi hii. Kama mimi na wewe hatutaweza kuwa wazalendo na nchi yetu tusitegemee mtu toka nje aje aipende nchi hii,” Sajenti Mambo alisema kwa huzuni na kushusha pumzi.

“Tutaonana vipi sasa?” niliuliza kwa shauku.

“Nitakujulisha baadaye wapi na muda gani tuonane, ila naomba iwe siri sana na uje peke yako maana kuna usaliti mwingi sana sasa hivi kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama,” Sajenti Mambo alisema.

“Kwa hiyo… ni wewe uliyeuleta ule ujumbe nyumbani kwangu?” nilimuuliza kwa shauku.

“Ndiyo. Naamini umeuelewa na kuufanyia kazi!” Sajenti Mambo alisema.

“Nimeuelewa ila bado kuna mambo yananitatiza kidogo…” nilisema.

“Usijali, tutaongea baadaye, nitakujulisha kila kitu. Kwa kifupi hali si shwari kabisa, kuna mambo makubwa yanaendelea chini ya zulia,” Sajenti Mambo alisema na kukata simu. Sauti yake ilionesha wasiwasi mkubwa.

Dah! Baada ya simu kukatwa ukimya ukatawala kwa muda ndani ya ile ofisi kisha mkurugenzi mkuu akavunja ukimya, “Kwa sasa Mambo ndiye ‘sosi’ wetu mkubwa, naomba tusiipoteze nafasi hii. Namfahamu vizuri, ni mzuri sana kwenye kuchambua taarifa na upembuzi wake wa mambo ni wa kiwango cha juu.”

Tulibaki kimya tukijaribu kutafakari. Mkurugenzi mkuu akaongea jambo ambalo siku zote nilikuwa na shaka nalo, “Labda niwamegee siri, Mambo ni mmoja kati ya maofisa wa Usalama wa Taifa waliopenyezwa kwenye Jeshi la Polisi, hivyo mtaona ni kwa namna gani anaweza kuwa mtu muhimu kwetu.”

* * *

Endelea kufuatilia...
 
taharuki..jpg

326

Saa 9:59 alasiri…

Anga lilikuwa limetandaza wingu zito lililolifunika jua la alasiri utadhani nalo lilikuwa linajumuika na waombolezaji kwenye maziko ya mwanamama Ummi Mrutu ambaye mwili wake ulikuwa unazikwa kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, baada ya kukabidhiwa kwa familia kufuatia uchunguzi wa mwili wake kukamilika.

Kutokana na namna mwili wa marehemu ulivyokuwa umeharibika ulikuwa ukizikwa kwa shida sana, kwani kilichokuwa kikizikwa kilikuwa ni mabaki yaliyopatikana ya mwili wake.

Ilikuwa ni jioni nyingine tena na ulinzi ulikuwa mkali sana katika eneo lote la makaburi ya Kinondoni na maeneo ya jirani. Kulikuwa na watu wengi mno mfano wa utitiri, kadamnasi ya watu waliokuwa wamekusanyika vikundi vikundi, nyuso zao zikiwa zimegubikwa na majonzi na huzuni.

Alasiri hii ilikuwa imechukua sura mpya. Baadhi ya shughuli nchini hususan katika jiji la Dar es Salaam zilikuwa zimesimama kabisa ili kupisha tukio lile la heshima na la kizalendo liweze kufanyika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwepo makaburini akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wengine wa serikali na wa kisiasa wakiwemo mawaziri, makatibu wakuu wa wizara, wakurugenzi wa idara na taasisi mbalimbali, makamanda wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa ngazi mbalimbali wa kiserikali na wa vyama vya siasa bila kujali tofauti zao, na bila kusahau wananchi wa kawaida. Wote hawa walikuwa katika nyuso za masikitiko.

Wengi walivaa vitambaa vyeusi mikononi mwao kuashiria kuwa hawakuwa katika hali ya furaha bali walikuwa katika hali ya tanzia na huzuni wakiwa tayari kuuhifadhi mwili wa mpendwa wao, Waziri wa Mambo ya Ndani, Ummi Mrutu, aliyepoteza maisha yake wakati akiendelea kulitumikia taifa kwa uadilifu mkubwa. Kila mmoja alikuwa ameumia kwa namna yake.

Ndiyo. Waliumia kwa sababu yule waziri mashuhuri kabisa, waziri mpambanaji wa kweli ambaye hakuwahi kukata tamaa katika mapambano dhidi ya uovu, aliyewajali wanyonge na kuamini kuwa siku moja Watanzania wote wangeishi kwa umoja na furaha, yule kamanda asiyekuwa na gwanda wala nyota begani alikuwa ametoweka kama moshi angani.

Yule shujaa wa mapambano asiyeogopa kufa wala asiyemhofu yeyote lakini magaidi wakautoa uhai wake. Alikufa akiwa anapambana, hakuwahi kupumzika kamwe. Wangeweza kusema amekufa kishujaa, wangeweza kumwita shujaa lakini hii haikupunguza uchungu wa kifo chake. Alikuwa amekufa!

Pia kulikuwa na ndugu wafiwa, jamaa na marafiki ambao walionekana kushindwa kujizuia na kumwaga machozi, hawa walikuwa wamevaa fulana nyeupe zenye picha ya mwanamama Ummi Mrutu kifuani.

Mimi pia nilikuwepo hapo makaburini alasiri hiyo nikiwa sina wasiwasi kabisa kwa sababu niliamini kuwa ulinzi wa kutosha ulikuwepo. Mwili ulikuwa mchovu kwa kukosa usingizi na pia mahaba mazito kutoka kwa Pamela, lakini sikuwa na namna yoyote ya kukwepa majukumu yangu. Pamela hakuwepo kwa sababu wanawake hawakuruhusiwa kuwepo makaburini, lakini Luteni Lister pia alikuwepo lakini akiwa katika eneo tofauti na lengo letu lilikuwa moja tu, kufuatilia nyendo za watu waliokuwa wametajwa kwenye ile orodha tuliyoichukua kule benki.

Wakati wote nilikuwa nimeshika mkononi kamera yangu kubwa ya kiuandishi wa habari aina ya Canon EOS R yenye lenzi kubwa iliyoniwezesha kuona mbali na nilikuwa napiga picha. Niliamua kuitumia kamera hii baada ya ile nyingine kubwa zaidi aina ya Lumix SFX-20 kupata hitilafu ndogo kutokana na mtikisiko wa bomu kule Makumbusho.

Nikiwa miongoni mwa waandishi wa habari, nilikuwa napiga picha kila tukio nililodhani lingekuwa muhimu kwenye upelelezi wetu. Eneo lile la makaburini lilikuwa limejaa makachero wa Usalama wa Taifa walioonekana kutanda kila kona katika hali ya kuhakikisha kuwa itifaki ya ulinzi na usalama inazingatiwa vizuri eneo lote.

Baadhi ya makachero hao walifahamu vyema kuwa sikuwa pale kama mwandishi wa habari bali kwa majukumu yangu kama ofisa kificho wa Usalama wa Taifa.

Niliwatazama makachero hao. ‘Askari ni askari tu, avae magwanda asivae,’ niliwaza kila nilipoona hali ya makachero hao wakati wakitimiza majukumu yao. Japo walijitahidi kutojionesha, kana kwamba hawakuwa katika majukumu ya ulinzi, lakini sikushindwa kusoma hali ya kukosa utulivu mioyoni mwao na ramani ya misukosuko katika nyuso zao.

Muda mwingi mikono yao ilichopoka na kupelekwa mifukoni kuzipapasa bastola zao; miguu yao ikicheza cheza kwa namna ya ukosefu wa utulivu mioyoni mwao. Mara kwa mara waliyatupa macho yao huku na kule katika namna ya kutafuta kitu ambacho kingeonekana kutishia amani na usalama wa eneo lile.

Nikiwa nimejichanganya katikati ya kundi la waandishi wa habari, nilikuwa makini sana kufuatilia mambo yaliyokuwa yakiendelea eneo lile nikitaka kufahamu vizuri kila kitu kilichokuwa kikiendelea hapo. Kila mara niliyatembeza macho yangu huku na kule nikizichunguza nyuso za watu mbalimbali waliofika eneo lile huku nikitarajia kuziona nyuso za watu fulani ambao majina yao yalitajwa kwenye orodha ya mgawo wa mabilioni ya fedha.

Wakati nilipokuwa nikiyatembeza macho yangu kuwatazama watu waliokuwepo eneo lile nikagundua kuwa kulikuwepo na nyuso mbili za watu zilizokuwa na hali isiyo ya kawaida, zilikuwa nyuso zenye furaha sana kana kwamba ule msiba haukuwa na maana yoyote kwao. Nilizitilia shaka nyuso hizo kisha nikawasiliana na Luteni Lister kwa kutumia njia yetu ya mawasiliano ambayo isingeweza kuingiliwa na yeyote, nikamweleza juu ya shaka yangu.

Baada ya mwili kuingizwa kaburini na kuzikwa, shekhe alitoa mawaidha kwa wafiwa kuwa wastahamilivu, na kwamba Ummi Imani Uledi alikuwa ameshakunywa kifo chake kutoka kwenye kikombe cha umauti, ambacho kila mmoja hapa duniani aliahidiwa kunyweshwa baada ya muda fulani.

Kisha shekhe huyo alimalizia halafu akaomba dua ndefu kwa lugha ya Kiarabu na mwishoni watu waliitikia dua. Baada ya hapo akaruhusu watu kutawanyika kwa maelezo kuwa wanafamilia walikuwa wamesema kusingekuwa na matanga nyumbani kwao.

Kwa kuwa wingu zito la mvua lilikuwa limetanda angani hivyo mara tu viongizi wa kitaifa walipoondoka na watu kutambua kuwa mazishi yale yalikuwa yamefika tamati wakaanza kutawanyika haraka kuikwepa mvua ile kubwa iliyokuwa ikijiandaa kunyesha.

* * *

Itaendelea...
 
Dah!😖 Wamechukua umeme wao na nilisahau kuichaji laptop yangu, ina chini ya 25%. Ukirudi mapema nitatupia zingine, vinginevyo tuombeane uzima...
 
View attachment 2161351

(Kutoka kwa mwandishi wa stori za kusisimua zilizowahi kuchapishwa hapa JF za Taxi; Kizungumkuti!; Laiti Ningejua!; Hekaheka!; Hadi Lini! na nyinginezo)

Na Bishop Hiluka

0685 666964 | bjhiluka@yahoo.com



Kijasho Jepesi


Saa 12:15 asubuhi…

WALA sikujua kitu gani kilikuwa kimeukatisha ghafla usingizi wangu! Niliyafumbua macho yangu taratibu nikayatembeza mle chumbani kuangalia huku na kule, nikakutana na ukungu wa kiza chepesi machoni. Hali ile ikanifanya niyatulize vizuri mawazo yangu huku nikijaribu kufikiria pale nilikuwa wapi.

Hata hivyo, sikulipata jibu la haraka na hivyo niliamua kupeleka mikono yangu huku na kule nikijaribu kupapasa pale nilipokuwa nimelala. Sikuchukua muda kugundua kuwa nilikuwa nimelala juu ya kitanda chenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa.

Kitanda kilikuwa kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita kilichokuwa katikati ya chumba kikubwa. Kwa kufanya vile taratibu fahamu zangu zikaanza kurejewa na uhai.

Niliweza kugundua kuwa nilikuwa nimelala kitandani chumbani kwangu ila sikuweza kukumbuka haraka muda huo ulikuwa ni wa saa ngapi, ingawa hisia zangu ziliniambia kuwa tayari kulikuwa kumeanza kupambazuka kutokana na kusikia sauti za majogoo waliokuwa wakishindana kuwika kwenye mabanda.

Pia niliweza kusikia, kwa mbali, sauti za ndege angani walioshindana kuimba nyimbo nzuri na kuruka huku na kule kwenye vilele vya miti mikubwa iliyokuwa nje ya ile nyumba na kandokando ya barabara ya mtaa ule wa Ng’ambo mjini Tabora, eneo la jirani kabisa na uwanja wa mpira wa Ali Hassan Mwinyi.

Nilikuwa nimelala peke yangu pale kitandani na nilipojichunguza nikagundua kuwa nilikuwa nimejifunika shuka lakini sikuwa nimevaa nguo yoyote mwilini mwangu hali iliyonistaajabisha sana! Sikuwa na kawaida ya kulala bila nguo hata kama ingekuwa ni wakati wa joto kali kiasi gani, bado nisingeweza kulala bila nguo.

Haraka nikataka niamke na kuketi pale kitandani lakini hilo halikufanikiwa kwani kichwa changu kilikuwa kizito mithili ya mtu aliyekuwa ametwishwa kiroba cha mchanga, hali hiyo ilinifanya niyafunge macho yangu taratibu na kuendelea kujilaza.

Nikiwa bado nimelala pale kitandani mawazo yalianza kupita kichwani kwangu mfano wa filamu, nilijaribu kukumbuka nilirudi vipi usiku pale nyumbani na nilikuwa na nani. Mara ikanijia picha ya usiku wa kuamkia siku hiyo. Nikakumbuka kuwa nilikuwa katika eneo la Chemchem mtaa wa Baruti mpaka majira ya saa saba za usiku.

Usiku huo nilikunywa pombe nyingi na kula nyama choma, na kama isingekuwa ushawishi wa rafiki yangu Majaliwa Nzilwa, haki ya nani nisingetia mdomoni pombe siku hiyo.

Majaliwa Nzilwa, jamaa fulani mfupi na mcheshi sana ambaye tulipenda kutaniana muda wote, alikuwa rafiki yangu wa muda mrefu tangu tukisoma katika Shule ya Msingi Gongoni iliyopo katika Manispaa ya Tabora.

Ukaribu wetu uliwafanya wengi kudhani tulikuwa ndugu kwa kuwa muda mwingi tulipenda kuwa pamoja hasa kila nilipotoka kazini, na licha ya urafiki wetu, Majaliwa pia alikuwa mshauri wangu mkubwa katika mambo yangu mbalimbali.

Hayo niliyakumbuka vema, na si akili ya pombe, picha ilikuwa inapita kichwani kwangu kama niliyekuwa naangalia filamu. Nilikumbuka kuwa Majaliwa alininunulia chupa kubwa ya pombe kali aina ya Grant’s Whisky nikaanza kugida kama maji, kisha alimwagiza Masawe mchoma nyama atuchomee ubavu mzima wa mbuzi. Baadaye tena alinunua chupa kubwa ya K Vant na chupa kadhaa za Savannah.

Usiku huo nilikunywa sana kwa kuwa sikuwa sawa kisaikolojia, nilikuwa nimevurugwa kwelikweli! Nilikumbuka pia kwamba baadaye Majaliwa alinitambulisha kwa msichana fulani hivi mwenye asili ya Kiarabu, aliitwa Rahma. Alikuwa msichana mzuri kwa sura na umbo, akiwa na macho mazuri yaliyojawa na haya alikuwa amevaa gauni fupi lililoishia juu kidogo ya magoti yake la rangi ya bluu lenye vidotidoti vyeupe vinavyong’aa.

Alikuwa mrefu na kifua chake kilibeba maziwa ya ukubwa wa wastani huku kiuno chake chembamba kikiwa kimebeba nyonga pana kiasi. Nywele zake zilikuwa nyingi ndefu nyeusi na zilikuwa zimeipendezesha sura yake ya kitoto. Nilikumbuka vyema kuwa Rahma alijitambulisha kwangu kwamba alikuwa mgeni pale Tabora na alitokea Singida. Hivyo tu!

Ni hivyo tu ndivyo nilivyovikumbuka kuwa vilitokea usiku huo, hakuna kingine isipokuwa kuwa na rafiki yangu Majaliwa eneo la Chemchem, kuja kwa huyo mwanamke wa Kiarabu aliyeitwa Rahma, tukala na kunywa, basi! Nilipojaribu kukumbuka mambo mengine kichwa changu kiligoma kabisa kuyakumbuka!

Nikiwa bado nipo kitandani, macho yangu bado nimeyafunga, nilihisi kuchoka mno na mawenge ya usingizi. Si hayo tu, bali pia uvivu ulinijaa na tumboni mwangu njaa ilikuwa inakereza mfano wa seremala aliyekuwa akiranda mbao. Vyote kwa pamoja vilikuwa vinanipa hali ya kutaka kuendelea kubadili uchago.

Akilini, niliutaka utulivu kwa gharama yoyote ile, japo nipate kukimalizia kipande cha usingizi kilichobakia, wala sikujua kingekwisha saa ngapi. Nilichotaka ni kulala tu mpaka pale ambapo mwili wangu ungeniruhusu kuamka. Niliuhisi uzito wa kichwa changu na nilikuwa nina mawenge ya usingizi, ukichanganya na uvivu uliokuwa umesababishwa na mning’inio mkali wa pombe nilizokunywa, vilinipa hali ya kutaka kuendelea kuuchapa usingizi.

Nilipanga nilale na nikiamka niende nikapate supu ya kongoro na chapatti kwa Mama Kashindye, aliyeishi upande wa pili wa barabara ya mtaa huo na baada ya hapo ndiyo nimtafute Majaliwa, huenda yeye angekuwa ana kumbukumbu nzuri ya kilichotokea usiku kuliko mimi.

Nilijiambia kuwa kwa muda huo sikupaswa kuumiza sana kichwa changu kwa hayo mambo ya usiku, sikufikiria kama yalikuwa na umuhimu wowote kwa muda huo, pindi nikiamka ningejua cha kufanya. Hivyo nilijigeuza kuelekea upande mwingine wa kitanda na kuendelea kulala. Sikujali sauti za kukera za majogoo waliokuwa wanashindana kuwika kwenye mabanda na juu ya mapaa. Nilijisemea kuwa kwa sababu nilikuwa nimeanza likizo basi wacha nilale mpaka usingizi ukate kabisa.

Jitihada zangu za kuutafuta usingizi zilikatishwa kikatili na sauti kali ya kitu mfano wa kengele iliyoanza kulia chumbani kwangu, sauti ile iligeuka kuwa kero kubwa masikioni mwangu. Niliposikiliza vizuri nikagundua kuwa ilikuwa ni simu yangu ya mkononi iliyokuwa sehemu fulani mle ndani. Nikawaza kuwa hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kunipigia simu muda ule wa alfajiri zaidi ya mpuuzi mmoja tu, Majaliwa! Kwani Majaliwa na mimi tulipenda sana kutaniana na Majaliwa aliongoza kunikera. Kila nilipokasirika yeye aliona raha sana, na ili kukabiliana na hali hiyo ilibidi nimzowee.

Sikuwa na namna yoyote ya kufanya kwani sauti ya simu ilizidi kuniletea kero kubwa masikioni mwangu, na pia nilitambua kuwa kama mpigaji wa simu hiyo, kwa muda huo, angekuwa Majaliwa au mtu mwingine yeyote basi kungekuwa na tatizo na angeendelea kupiga hadi nipokee, hivyo nililitupa pembeni shuka nililojifunika, kisha kwa msaada wa swichi iliyokuwa kando ya kitanda changu nikawasha taa ya mle chumbani huku akili yangu ikiwa imeanza kupoteza utulivu.

Na hapo nikaziona nguo zangu zikiwa zimetupwa tupwa ovyo sakafuni mle chumbani, si hivyo tu niliona pia kifaa fulani kimoja kidogo cha kujipima virusi vya ukimwi ambacho kinauzwa kwenye maduka ya dawa na ki-sindano kidogo cha kutobolea ili kutoa damu. Vifaa hivyo vilikuwa vimetumika.

Kingine nilichokiona pale sakafuni ilikuwa ni mtapakao wa shanga za rangi mbalimbali zivaliwazo na wanawake kiunoni. Jambo hilo likanitia hofu kubwa huku mapigo ya moyo wangu yakianza kunienda mbio isivyo kawaida.

Itaendelea...
Ohooooooo
 
Back
Top Bottom