Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,699
- Thread starter
- #981
341
Yuko wapi!
Saa 12:53 asubuhi…
NILIINGIA ofisini kwa mkuu wangu wa kikosi maalumu kilichoshughulika na operesheni hatari (SOG), Kanali Othman Mjaka, dakika saba kabla ya saa moja, muda ambao nilitakiwa kufika hapo, nikitokea Julius Nyerere International Airport. Kwa haraka niliyokuwa nayo sikuweza hata kupita nyumbani kwangu Upanga ili nijimwagie maji na kubadilisha nguo kwani nilikuwa nimechafuka sana.
Ofisi ya Kanali Othman Mjaka ilikuwa nzuri sana na pana ikiwa na mazingira nadhifu na yaliyovutia kwa mpangilio wa samani za kisasa za ofisini, ilikuwa na zulia zito jekundu sakafuni na meza ndefu ya ofisini yenye viti ishirini. Viti kumi upande wa kushoto na viti vingine kumi upande wa kulia.
Mle ndani ya ofisi kulikuwa na ukimya mzito ulionifanya nisikie sauti ya hatua zangu mwenyewe wakati nilipokuwa nikitembea kukatisha katikati ya kile chumba nikielekea kule mbele kwenye meza alikokuwa ameketi Kanali Mjaka.
Aiwa katika umri wa miaka 52, Mkuu huyo wa SOG alikuwa ameketi kwa utulivu kwenye kiti chake kikubwa cha kiofisi cha ngozi halisi cha kuzunguka na chenye magurudumu madogo, nyuma ya meza yake kubwa ya ofisini mwisho wa ofisi ile upande wa kulia. Uso wake ulikuwa umesawajika kidogo ila macho yake yalikuwa makini kupitia taarifa fulani kwenye kishkwambi chake alichokuwa amekishika mkononi pasipo kuniangalia pamoja na kuwa alitambua kuwa nilikuwa nimeingia ndani ya ofisi yake.
Kanali Mjaka alikuwa mfupi na mnene kiasi, mweupe sana mwenye ule weupe wa kichotara akiwa mchanganyiko wa damu ya Kishirazi na Kiarabu. Kwa kuwa alitokea Pemba hivyo wengi walipenda kumwita Kanali Mpemba.
Sura yake ilikuwa ya mviringo iliyoonesha utulivu, na macho yake yalikuwa makubwa yenye uchovu lakini yaliyojaa kiburi na yenye kila dalili ya kuonya. Asubuhi ile alikuwa amevaa suti ghali ya kijivu ya single button, brand ya Piacenza kutoka Italy na miwani mikubwa myeupe ya macho.
Kanali Mjaka alikuwa ameipata nafasi ya kuongoza kikosi hiki maalumu cha siri cha kushughulika na operesheni hatari kutokana na umahili wake kwenye operesheni za kijasusi, alikuwa ofisa nguli, mwenye elimu na uzoefu wa hali ya juu katika kazi za kijasusi.
Licha ya kushiriki katika operesheni lukuki ndani ya nchi pia alikuwa amefanya kazi katika nchi kadhaa za Ulaya na Mashariki ya Kati, na kukamilisha malengo ya Idara ya Ujasusi kwa ufanisi mkubwa. Hadi muda huu Kanali Mjaka alikuwa na takriban miaka therathini katika Idara ya Usalama wa Taifa, na muda huo ulimwezesha kujenga rekodi ya utendaji bora kulinganisha na umri wa kati aliokuwa nao.
Nilipofika mbele ya meza yake nilisimama kwa ukakamavu huku nikimtazama kwa wasiwasi kidogo, kwa namna alivyokuwa nilihisi kabisa kuwa mambo hayakuwa shwari hata kidogo. Nilimsalimia kwa adabu huku nikiendelea kumtazama usoni kwa wasiwasi kidogo.
Hakuhangaika kuniangalia wala kunijibu na badala yake aliniashiria kwa mkono kuwa nivute kiti niketi halafu yeye akaendelea kutazama katika kile kishkwambi chake pasipo hata kunitazama, huku uso wake ukiwa umesawajika kidogo na mawazo yake yakionesha kuwa mbali na kile chumba. Sikushangaa hata kidogo kwa tabia ile kwani mara nyingi huyu mkuu wetu alikuwa haitikii salamu na sisi tulikwisha mzoea.
Kwa takriban dakika kumi Kanali Mjaka aliendelea kuzama kwenye taarifa alizozisoma kwenye kile kishkwambi chake pasipo kunitazama au hata kunieleza chochote jambo lililoniacha njia panda. Kwa jinsi ukimya ulivyokuwa umetawala mle ofisini nilitambua kuwa hali ile haikutokana na uzito wa taarifa aliyokuwa akiipitia kwenye kile kishkwambi bali ilitokana tu na dharau zake. “Wana tabu sana hawa watu wafupi!” Niliwaza.
Nikiri kuwa sikuwa nikimchukia kabisa huyu Mpemba, badala yake nilimu-admire sana kutokana na rekodi yake iliyotukuka ya utendaji kazi wake ndani ya Idara ya Ujasusi. Hata hivyo hiyo haikuondoa ukweli kuwa Kanali Mjaka alikuwa mmoja kati ya watu waliojisikia sana na waliokuwa na dharau nyingi katika hii dunia! Pengine ni kwa sababu ya nafasi yake ndani ya Idara ya Ujasusi, rekodi yake na usomi wake.
Baada ya dakika zile kumi za ukimya mzito ndani ya ile ofisi nilianza kukosa uvumilivu na fundo la chuki lilianza kunikaba kooni, nikiwa bado njia panda mara mlango wa ofisi ile ukagongwa mara moja na mgongaji huyo akaufungua na kuingia pasipo kusubiri kukaribishwa, kwani hata kama angegonga mara mia moja asingejibiwa. Nikageuza shingo yangu kutazama kule mlangoni na hapo nikamwona mwanadada mmoja mrefu na mweupe mwenye haiba ya kuvutia akiingia.
Sura yake ilikuwa ndefu na macho makubwa ya kike halafu malegevu. Pua yake ilikuwa ndefu na mdomo wake ulikuwa na kingo pana na alikuwa na vishimo vidogo mashavuni mwake. Nywele zake nyeusi ndefu na laini alikuwa amezifunga kwa nyuma na alikuwa amevaa fulana nyepesi nyeupe iliyoyaficha vyema matiti yake imara yenye ukubwa wa wastani na juu yake alikuwa amevaa suti, shati na suruali, ya kitambaa very expensive cha dengrizi ya rangi ya bluu mpauko brand ya Brunello Cucinelli.
Kiuno chake kilikuwa chembamba kiasi chenye misuli imara kikiwa kimeizuia suruali yake na miguuni alikuwa amevaa buti ngumu nyeusi za ngozi. Mgongoni alikuwa amebeba begi dogo jeusi la safari, ambalo bila shaka lilikuwa na vifaa vyake vyote muhimu kwa kazi za kijasusi.
Kwa sekunde chache macho yangu yalikataa kabisa kuamini kuwa taswira ya mrembo yule aliyeingia iliyokuwa mbele ya macho yangu ilimwakilisha ofisa usalama aliyekuwa na mbinu na ujuzi wa hali ya juu katika kazi za kijasusi na komando wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania… Luteni Daniella Palangyo.
Asubuhi hii Daniella alikuwa katika mwonekano wa kupendeza ulioanza kuichanganya akili yangu na kuamsha hisia fulani zisizoelezeka mwilini mwangu. Mtikisiko wa umbo lake refu na zuri la kike wakati akizitupa hatua zake kama mlimbwende aliyekuwa kwenye jukwaa la kugombe taji la dunia, akija pale nilipoketi ulizidisha hisia zangu na hamu ya kutaka kubanjuka naye, ili nione kama uzuri ule ulikuwa hadi ndani au nje tu. Maana isijekuwa uzuri wa mkakasi ndani gome la mti!
“Daniella!” nilijikuta nikimwita kwa mshangao uliochanganyika na furaha na kusahau kabisa, kwa muda, kama nilikuwa nimechukizwa na tabia ya Kanali Mjaka.
“Jason!” Daniella naye aliniita kwa mshangao huku akiharakisha kuja pale nilipoketi na kunikumbatia kwa furaha. Tukakumbatiana.
Endelea...