Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 71
Mama Angel akiwa katulia alipigiwa simu na wifi yake na kuanza kuongea nae,
“Kwakweli wifi asante sana, yani jana wale wageni wmaekula na kusifia balaa yani nimepata sifa hizo mke wangu hadi balaa”
Muda huu mumewe nae alirudi kwahiyo aliongozana nae chumbani huku akiongea na ile simu,
“Kwakweli kaka muache tu achanganyikiwe juu yako”
Basi mama Angel alikuwa akicheka hadi mumewe kutaka kujua akizungumza na nani, basi mama Angel alimpa mumewe ile simu kuwa nay eye aongee nae, basi mumewe alianza kuongea nae,
“Yani Erick jana bhana, niliondoka hapo na mkeo ili anisaidie kupika, uwiii vitu alivyopika huku jamani ni Mungu pekee anajua yani wageni wangu wamejilamba haswaa”
“Oooh huyo ndio mke wangu bhana”
“Ndiomana unampenda”
“Nampenda ndio ila sio sababu ya kupika tu hapana, hiyo kupika ni ziada ila ninampenda mke wangu kwasababu zangu mwenyewe”
Basi waliongea pale na kukata ile simu kisha baba Angel alimuangalia mkewe na kumwambia,
“Na mimi nataka unipikie hiko chakula ulichopika kwa Tumaini, sio nje huko mnaenda kuwapikia mapochopocho halafu ndani unasahau maana naona toka tuje na Vaileth basi kila siku kula chakula cha Vaileth tu, nimekumbuka chakula chako mke wangu”
“Basi kesho nitapika”
Wakaongea ongea na kuamua kulala pale.
Kesho yake wakati wakina Angel wameenda shuleni, basi mama yao aliamua kubaki nyumbani na muda huo alitaka kusaga juisi.
Akaenda jikoni na kukuta kidude cha kuchomeka kwenye soketi hakipo basi alimuuliza Vaileth nae akamjibu,
“Oooh hiko nilimuona nacho Erick, nadhani alienda nacho chumbani kwake”
“Aaaah huyu mtoto nae na vidude vya umeme jamani ni hatari’
Basi alitoka pale na moja kwa moja kuelekea chumbani kwa Erick, wakati akiangaza macho yake akaona barua mezani kwa Erick basi akaenda kuichukua na kuisoma, yani alishtuka sana kuona ni barua kutoa kwa Samir kwenda kwa Angel,
“Mmmh sasa inafanya nini humu chumbani kwa Erick jamani!!”
Basi akaisoma mara mbilimbili akakuta ujumbe wa chini ukisema,
“Kesho nitakuja kwenu Angel, nitasimama pembezoni mwa ukuta wenu naomba uje tu unikumbatie yani hiyo itakuwa ni furaha yangu, nakupenda sana Angel mpenzi wangu”
Huyu mama akapumua kidogo na kusema,
“Yani hiyo kesho si ndio leo? Jamani hawa watu wanataka kunifanyeje mimi? Kwanini wananifanyia hivi!!”
Basi mama Angel alitoka nje na kukaa mitaa ile ile ya nje ya nyumba yao huku akisubiri kwa hamu kama gari itapiga honi basi atajua kuwa Angel amefika na atakimbilia nje kabisa ili Angel asiende huop upande uliotajwa na Samir, na kweli alitoka pale nje mara kadhaa bila kumuona huyo Samir kwahiyo aliamua tu kungoja pale ndani ya geti, yani hakufanya chochote tena zaidi ya kungoja Angel arudi. Ila alipoona Erica na Erick wamerudi akaona ni vyema nay eye akitoka nje kabisa.
Mama Angel akiwa katulia alipigiwa simu na wifi yake na kuanza kuongea nae,
“Kwakweli wifi asante sana, yani jana wale wageni wmaekula na kusifia balaa yani nimepata sifa hizo mke wangu hadi balaa”
Muda huu mumewe nae alirudi kwahiyo aliongozana nae chumbani huku akiongea na ile simu,
“Kwakweli kaka muache tu achanganyikiwe juu yako”
Basi mama Angel alikuwa akicheka hadi mumewe kutaka kujua akizungumza na nani, basi mama Angel alimpa mumewe ile simu kuwa nay eye aongee nae, basi mumewe alianza kuongea nae,
“Yani Erick jana bhana, niliondoka hapo na mkeo ili anisaidie kupika, uwiii vitu alivyopika huku jamani ni Mungu pekee anajua yani wageni wangu wamejilamba haswaa”
“Oooh huyo ndio mke wangu bhana”
“Ndiomana unampenda”
“Nampenda ndio ila sio sababu ya kupika tu hapana, hiyo kupika ni ziada ila ninampenda mke wangu kwasababu zangu mwenyewe”
Basi waliongea pale na kukata ile simu kisha baba Angel alimuangalia mkewe na kumwambia,
“Na mimi nataka unipikie hiko chakula ulichopika kwa Tumaini, sio nje huko mnaenda kuwapikia mapochopocho halafu ndani unasahau maana naona toka tuje na Vaileth basi kila siku kula chakula cha Vaileth tu, nimekumbuka chakula chako mke wangu”
“Basi kesho nitapika”
Wakaongea ongea na kuamua kulala pale.
Kesho yake wakati wakina Angel wameenda shuleni, basi mama yao aliamua kubaki nyumbani na muda huo alitaka kusaga juisi.
Akaenda jikoni na kukuta kidude cha kuchomeka kwenye soketi hakipo basi alimuuliza Vaileth nae akamjibu,
“Oooh hiko nilimuona nacho Erick, nadhani alienda nacho chumbani kwake”
“Aaaah huyu mtoto nae na vidude vya umeme jamani ni hatari’
Basi alitoka pale na moja kwa moja kuelekea chumbani kwa Erick, wakati akiangaza macho yake akaona barua mezani kwa Erick basi akaenda kuichukua na kuisoma, yani alishtuka sana kuona ni barua kutoa kwa Samir kwenda kwa Angel,
“Mmmh sasa inafanya nini humu chumbani kwa Erick jamani!!”
Basi akaisoma mara mbilimbili akakuta ujumbe wa chini ukisema,
“Kesho nitakuja kwenu Angel, nitasimama pembezoni mwa ukuta wenu naomba uje tu unikumbatie yani hiyo itakuwa ni furaha yangu, nakupenda sana Angel mpenzi wangu”
Huyu mama akapumua kidogo na kusema,
“Yani hiyo kesho si ndio leo? Jamani hawa watu wanataka kunifanyeje mimi? Kwanini wananifanyia hivi!!”
Basi mama Angel alitoka nje na kukaa mitaa ile ile ya nje ya nyumba yao huku akisubiri kwa hamu kama gari itapiga honi basi atajua kuwa Angel amefika na atakimbilia nje kabisa ili Angel asiende huop upande uliotajwa na Samir, na kweli alitoka pale nje mara kadhaa bila kumuona huyo Samir kwahiyo aliamua tu kungoja pale ndani ya geti, yani hakufanya chochote tena zaidi ya kungoja Angel arudi. Ila alipoona Erica na Erick wamerudi akaona ni vyema nay eye akitoka nje kabisa.