Simulizi: Nini maana ya mapenzi

Simulizi: Nini maana ya mapenzi

SEHEMU YA 161


Kulipokucha alienda ofisini kama kawaida ila alikuwa akijitahidi kutoka kwa muda ambao Bahati hamkuti nje, yani alikuwa anajitahidi kumkwepa Bahati kwa vyovyote vile kwani aliona kuwa Bahati si mwanaume wake maana hata tena namna ya kufanya ndugu wa Bahati wasimchukie.
Siku hiyo wakati anatoka ofisini na anakaribia na kwao, simu yake ikaita kwa namba ngeni kabisa, akajiuliza kuwa ni nani ila akapokea,
“Erica”
“Ndio, mimi ni Erica”
“Siamini masikio yangu, naongea na Erica kweli?”
“Ndio, kwani wewe nani?”
“Mimi ni Babuu”
“Babuu? Kumbe upo?”
“Nipo ndio Erica, siamini kama leo nimekupata hewani. Uko wapi saizi?”
“Naelekea nyumbani”
“Naomba nipajue nyumbani kwenu, walau nije nikusalimie”
Basi Erica akamuelekeza Babuu nyumbani kwao, na muda mchache tu baada ya Erica kufika kwao Babuu nae alikuwa amefika, na Babuu alipomuona Erica alimkumbatia kwa furaha sana,
“Siamini kama nimekuona Erica, nimekusaka wewe mwanamke dah! Umejua kuutesa moyo wangu Erica”
“Ila mimi nina mwanaume mwingine”
“Shiiiii sijakuuliza habari za kuwa na mwanaume Erica, ila nimefurahi kukuona naomba uwe unaniruhusu kuja kukuona maana moyo wangu utakuwa na amani. Erica, wewe ni msichana wangu wa kwanza, na mimi ni mvulana wako wa kwanza. Siwezi kukutoa kwenye akili yangu Erica, yani kwenye mawazo yangu unatembea wewe tu”
“Ni kweli usemayo Babuu ila mimi sio kama Erica Yule wa mwanzo, nimebadilika sana siku hizi”
“Haijalishi Erica, kubadilika kwako hakuwezi kufuta kumbukumbu zako kwangu. Erica haijalishi ni kitu gani kilitokea kati yetu ila bado upo moyoni mwanagu, haijalishi upo kwenye mahusiano na nani ila moyoni mwangu bado unaishi”
Erica alimuangalia Babuu ambaye alionekana kuwa na maneno matamu kama aliyokuwa nayo mwanzo, kisha Babuu alimuuliza Erica kuwa anafanya nini kwa kipindi hiko.
“Niko field, na kesho ndio siku ya mwisho maana karibia tutafungua chuo na ndio utakuwa mwaka wangu wa mwisho”
“Field upo sehemu gani?”
Erica akamuelekeza, Babuu akamuomba kuwa kesho akitoka waonane ili angalau amsindikize hadi hapo kwao, Erica alimuitikia kisha akamuaga na kuingia ndani kwao.
Alipokuwa ndani alimuwaza sana Babuu, akakumbuka siku ya kwanza kuonana na Babuu jinsi akili yake ilivyoruka, alikuwa binti mbichi kipindi hiko hata nyumbani kwao haruhusiwi kutoka ila kwasasa kawa gumegume, kashatoa mimba mbili yani thamani yake imebaki machoni pa watu tu ila kiukweli imepungua, hata akashangaa kwa Babuu kuendelea kumwambia maneno ya upendo kuwa bado anampenda sana. Kiukweli siku hiyo, hadi alilala alikuwa bado akimuwaza Babuu ingawa hakujua kama angeweza kumfikiria namna hiyo.
 
SEHEMU YA 162

Siku iliyofuata alijiandaa na kwenda ofisini ila ilikuwa ndio siku yake ya mwisho kwa mafunzo, alikuwa akifurahia mwenyewe kwani tangu amekuwa pale kazini hajawahi kukorofishana na mtu yeyote. Alipofika ofisini, shemeji yake alimuita kwa furaha sana,
“Leo ni siku ya mwisho kuwa hapa ofisini Erica, ila ningependa tule chakula cha jioni pamoja”
“Hakuna tatizo shemeji, wapi hapo?”
“Kuna hoteli Fulani hivi, wanapika chakula kizuri sana”
“Nitajie shemeji”
James akamtajia na kumwambia kuwa akitoka ofisini ajiandae, basi Erica akakaa kwenye meza yake na kukumbuka kuwa Babuu alimuomba aende ampitie ofisini siku hiyo, ikabidid amtumie ujumbe kuwa ataenda kwenye chakula cha jioni na shemeji yake kisha akamtajia hoteli watakayokuwepo, Babuu alipiga simu ya Erica na kuanza kuongea nae huku akimuuliza vizuri kuhusu hapo mahali atakapokuwepo,
“Erica, mimi nitakuja hata hapo hotelini hata nikikaa mbali tu nikakuona nitaridhika”
“Ila usijali, huyu ni shemeji yangu atanirudisha mwenyewe nyumbani”
“Ndio Erica ila nitakuja tu”
“Khaa wewe nae mbishi, kwaheri”
Erica akakata simu na kuendelea kuweka mambo yake sawa.
Jioni ilipofika shemeji yake alimshtua mpaka kwenye hiyo hotel, walishuka kwenye gari na kuingia hotelini kisha wakakaa bustanini, huku kwa mbali ukisikika mziki laini na kisha kuletewa vinywaji na chakula ila kile kinywaji Erica alipokunywa tu alianza kujihisi kizunguzungu hatari kama mtu aliyekunywa pombe balaa, James akainuka na kwenda kuongea na muhudumu,
“Naomba kile chakula utubebee utupelekee chumbani kule nilipokodi maana mpenzi wangu hawezi kula hapo amelewa”
Wakati James anarudi ili amchukue Erica, alishangaa kuona Erica akikokotwa na kijana mwingine wakitoka nje ya ile hoteli.
 
SEHEMU YA 163


Jioni ilipofika shemeji yake alimshtua mpaka kwenye hiyo hotel, walishuka kwenye gari na kuingia hotelini kisha wakakaa bustanini, huku kwa mbali ukisikika mziki laini na kisha kuletewa vinywaji na chakula ila kile kinywaji Erica alipokunywa tu alianza kujihisi kizunguzungu hatari kama mtu aliyekunywa pombe balaa, James akainuka na kwenda kuongea na muhudumu,
“Naomba kile chakula utubebee utupelekee chumbani kule nilipokodi maana mpenzi wangu hawezi kula hapo amelewa”
Wakati James anarudi ili amchukue Erica, alishangaa kuona Erica akikokotwa na kijana mwingine wakitoka nje ya ile hoteli.
James alipigwa na bumbuwazi kuwa Yule kijana ni nani na kwanini kamchukua Erica, akaanza kumfata kwa nyuma ila alipofika nje alimuona Yule kijana akimpakiza Erica kwenye bajaji kisha kuondoka na ile bajaji, bado James alikuwa na bumbuwazi, akaenda akapanda gari yake ili kufata ile bajaji, ila alipofika barabara kuu tu ile bajaji ilimpoteza kabisa yani hakuelewa ilipoenda, kile kitendo kilimfanya ajilaumu kwanza, muda wake, pesa yake kila kitu chake alichofanya kwa siku hiyo ilikuwa ni bure kabisa.
Kuna muhudumu wa ile hoteli alipewa madawa ya kulevya na James ili aweke kwenye kinywaji cha Erica, naye alitimiza wajibu wake, James alijilaumu sana kuwa ni bora angemkokota na kwenda nae chumbani kuliko kubembwa na mtu asiyejulikana. Kwa muda huo hata hakuelewa kuwa aende wapi kumtafuta Erica, akajaribu kupiga simu ya Erica ila iliita sana bila ya kupokelewa hadi kukatika, alipiga tena na tena ila simu yake haikupokelewa na mara ya mwisho wakati anajaribu namba ya Erica haikupatikana na kuhisi kuwa simu ya Erica imezima, yani hapo ndio akili yake ilichanganyikiwa kabisa. Akapata wazo kuwa aende nyumbani kwao akamuulizie kwanza kwani hata kurudi pale hotelini hakutamani ukizingatia mambo yake hayajawa alivyotaka, halafu akawaza kuwa kama Erica akiwahi nyumbani basi atamsemea sifa mbaya yeye, kwahiyo akaona bora yeye awahi nyumbani kwakina Erica.

 
SEHEMU YA 164


James alifika nyumbani kwakina Erica na kugonga, kisha mama mkwe wake akamfungulia mlango na kumkaribisha, James akamsalimia na kumuuliza,
“Erica kashafika nyumbani?”
“Bado hajafika, hata namshangaa leo kachelewa chelewa halafu hajaniambia kama atachelewa”
“Samahani mama ila utaona kama namfatilia binti yako, ila Yule ni kama mdogo wangu ndiomana namfatilia kwa lengo zuri tu”
“Hakuna tatizo mwanangu, tena unavyomfatilia ndio vizuri, sasa atakuwa wapi?”
“Unajua leo ni siku yake ya mwisho kufanya mafunzo pale ofisini, sasa nikaongea nae vizuri kuwa anisubiri nimalize kazi zangu nimrudishe nyumbani. Nikiwa sina habari najua ananisubiri, nikashangaa tu kuna mtu kaja kunitonya kuwa njoo umuone shemeji yako, nikatoka nikamuona Erica kashikiliwa na mwanaume halafu akionekana kuwa amelewa kisha akapanda bajaji na Yule mwanaume na kuondoka. Yani….”
“Subiri, subiri kwanza. Erica anakunywa pombe? Jamani Mungu wangu, yani binti yangu mimi anakunywa pombe? Eeeh Mungu, nimekukosea wapi mimi? Binti yangu kawa mlevi?”
Mama Erica machozi yalikuwa yakimlenga lenga kwani kwa binti zake wote hakuna hata mmoja aliyepata sifa ya kunywa pombe, kwahiyo kuambiwa swala la Erica alilewa lilimshtua sana, akamuuliza tena,
“Kwahiyo akaenda wapi na huyo mwanaume?”
“Sijui mama, nimejaribu kuwafatilia lakini wamenipotea, nikampigia simu Erica kwakweli kaniambia vitu vya kunitia simanzi sana”
“Vitu gani baba?”
“Erica kaniambia, acahana na mimi, usinifatilie huna undugu na mimi. Nikamwambia naenda kuwaambia ndugu zako mambo haya, akasema tena usithubutu kusema maana ukisema nitakusingizia kuwa ulitaka kunibaka. Kwakweli mama hiyo kauli imeniuma sana”
“Jamani huyu Erica kapatwa na shetani gani mwanangu jamani? Yani akusingizie wewe kubaka? Erica jamani, mbona hana fadhila mwanangu! Yani kumsaidia kote huko aseme maneno ya ujinga kama hayo? Ngoja aje hapa nyumbani, nashukuru kwa taarifa mwanangu ingawa zimenichanganya haswaa”
“Pole mama, ila Erica nampenda kama mdogo wangu. Sikutaka aharibikiwe maana yupo kwenye ofisi yangu na ni mimi mtasema sikumuangalia vizuri, ila Erica alinishushua mbele ya dada yake kuwa nisimfatilie maisha yake, mwanaume yoyote anayetaka kuwa nae ni yeye. Maana mwanzoni kulikuwa na kimwanaume kimoja kinakuja kumchukua akitoka kazini, namuhurumia Erica mama!”
“Na wewe kwanini hukuja kuniambia siku zote hizo mpaka maji yamemwagika?”
“Mama, siku zote Erica ananiambia nisiseme chochote, yani siamini kuwa ndio mtoto Yule mdogo wa kipindi kile ndio kawa hivi”
“Hizi habari zimenichanganya kabisa yani sielewi, narudia maneno kama kichaaa, sielewi”
James akaaga na kuondoka, mamake Erica alikuwa na mawazo sana huku machozi ya hasira yakimjaa kuwa binti yake kaanza lini ulevi na zaidi ya yote tabia ya kuanza kuzunguka na wanaume,
“Erica leo utanieleza kwakweli, sijalea mtoto mlevi mimi, sijalea mtoto malaya mimi, sijalea mtoto muongo mimi. Hiyo tabia umeitoa wapi Erica, yani mtu anayekusaidia eti unataka umtungie stori kuwa alitaka kukubaka! Erica huna hata uso wa aibu!”
Alikuwa na huzuni sana na hasira kwani katika mabinti zake wote hakuwahi kumtegemea Erica kuwa binti wa tabia zisizofaa.
Mama Erica alikaa macho hadi usiku sana ila bado Erica hakurudi hadi aliamua kwenda kulala kuwa akirudi atagonga mlango kwani mpaka usiku sana Erica hakurudi.
 
SEHEMU YA 165



Kulipokucha huyu mama alizidi kupatwa na hasira kwani bado Erica hakurudi nyumbani, akili yake ikakosa uelekeo kabisa maana kila alipopiga simu ya Erica haikupatikana, akaamua kwenda kwa mwanae Bite maana alishachanganyikiwa.
“Mumeo hajakueleza kuhusu mambo ya Erica?”
“Kaniambia juu juu na nimeshangaa kwakweli, vipi karudi?”
“Bado hajarudi nyumbani jamani mtoto huyu ananitaka nini mimi?”
Ikabidi Bite amueleze mama yake kuhusu kijana anayekuwaga na erica na jinsi hata walivyomkataza na mumewe alivyowajibu,
“Alisema yeye ni msichana mkubwa na tumuache na maisha yake, kwakweli mama niliumia sana maana Erica ni mdogo wangu natakiwa kuwa nae makini ila akasema tuachane nae kabisa”
“Hapa nimechanganyikiwa, huyu mtoto sijui atakuwa wapi”
Mama akaamua kupiga simu kwa Mage ambaye alipopata ile taarifa ilibidi aende kwa Bite pia ili wajadiliane, walijaribu kupiga simu ya Erica haikupatikana na hapo ikawa ni hofu kubwa sana kwao kuwa ni kitu gani kilichompata ndugu yao.
“Sasa huyo mwanaume hamjui anapoishi jamani?”
“Hatujui mama, ila Yule kijana ndio anatokaga sana na Erica yani tumefanya mambo ambayo hata haiwezekani kukwambia mama, huyu Erica huyu loh!”
Mage akaamua kumpigia simu Derick ili kujaribu kumuuliza alipo Erica labda alijua ila Derick alijibu kuwa hajui popote alipo Erica,
“Kwani imekuwaje hadi Erica apotee?”
“Inavyosemekana alikuwa amelewa sana na akaondoka na huyo mwanaume hadi muda huu hakuna anayejua Erica yuko wapi jamani, na ubaya zaidi hata simu zake hapokei”
“Ila dada mngepunguza presha tu, Erica ni binti mkubwa na hawezi kupotea kirahisi hivyo, atapatikana tu hata msiwe na mashaka”
“Derick tumechanganyikiwa, Erica ni mtu mzima kweli ila yupo chini ya wazazi angetakiwa kusema sehemu alipo, au hata angeongea kwenye simu ingekuwa afadhali kidogo kuliko hivi, hewani hatumpati na hatujui alipo”
“Ila cha kuwashauri tu ni kuwa muwe wapole jamani, nina uhakika Erica atarudi akiwa salama salimini”
Ila Derick nae alishangazwa nah ii taarifa kuwa Erica alikuwa amelewa maana kwa ajuavyo Erica hanywi pombe, akawaza kuwa labda amenza kunywa pombe. Ila kitendo cha familia ya Erica kumuulizia Erica kwa Derick hawakujua tu kuwa ni swala ambalo lingezua utata mkubwa sana pindi Erica atakaporudi maana Derick sio mtu wa kunyamaza.
Walikaa pale na kujadiliana ila hawakupata shuluhisho, James nae alirudi mapema kujifanya anasaidia swala la kupotea kwa Erica, ila akashauri warudi nyumbani tu ili kuangalia kama Erica amerudi, basi waliondoka James, Mage na mama yao. James alifanya vile ili kuwaondoa tu pale nyumbani kwake.

 
SEHEMU YA 166

Kufika nyumbani wakamkuta Bahati getini kumbe nae alikuwa akimsubiria Erica baada ya kumkosa hewani kabisa kwa siku kadhaa mfululizo maana Erica alibadilisha laini ya simu, kwahiyo alihisi akifika nyumbani kwao itakuwa rahisi kumuona. James alipomuona Bahati akamwambia mama mkwe wake,
“Eeeh mama, kijana mwenyewe ndio Yule pale anayesumbua akili ya Erica”
“Khaaa si muuza samaki huyu!”
Mama Erica alimfata Bahati kwa hasira sana, na kumkunja kisha James akasogea na kumpiga vibao kadhaa kisha akasema kuwa wasimsikilize chochote kwani huyo ndio mtuhumiwa namba moja, walimpandisha kwenye gari ya James na kwenda nae kituo cha polisi. Kwakweli Bahati alikuwa akishangaa tu, maana hata hakuelewa kuwa imekuwaje kuwaje yeye kushikwa kama mwizi kiasi kile maana hata hakujua kama Erica alipotea.
Walivyofika kituoni, James alishuka na Bahati na kuwaambia wale wamsubirie kwenye gari, James alienda na Bahati kwa mapolisi, na aliimuita polisi mmoja pembeni na kumpa kitu kidogo ili amshikishe adabu Bahati, na Yule polisi pale pale alianza kumshurutisha Bahati.
Kisha James akarudi kwenye gari na kuwaambia wale kuwa Erica atapatikana tu, akaenda kuwarudisha nyumbani, kisha akaondoka.
Mage nae alikaa kidogo tu na kumuaga mama yao, kwani kuna mahali alitakiwa aende,
“Mama naomba uniruhusu tu”
“Sawa, ila hapa sina hata hamu ya kula”
“Ila mama jaribu hata kunywa juisi tu, twende ninavyoondoka uchukue juisi dukani. Badae nitarudi”
Mama Erica alikubali na kwenda na Mage dukani ila kiukweli alikuwa na mawazo sana.

Erica alishtuka kichwa chake kikiwa kizito sana kiasi kwamba hakuna alichoelewa kimetendeka juu yake, akaangaza macho huku na huku akagundua yupo kwenye chumba asichokijua kwani hayakuwa mazingira ya nyumbani kwao, akiwa anashangaa shangaa akamuona Babuu akiingia kwenye kile chumba,
“Ooooh Erica, umezinduka asante Mungu”
Erica alikuwa akishangaa tu na kumuuliza Babuu,
“Kwani imekuwaje? Hapa wapi? Nafanya nini hapa?”
“Erica, hapa ni nyumbani kwangu”
“Nyumbani kwako! Nimekuja kufanya nini hapa?”
“Usiwe na jazba erica, nisikilize kwanza nikwambie”
“Haya niambie”
Aliongea huku akionekana kuchukizwa sana kupelekwa pale,
“Erica, jana nilifika kwenye ile hoteli mliyopanga kwenda na shemeji yako kabla hata ya muda wenu na hadi mnaingia pale nawaona. Sasa shemeji yako alienda kuagiza vinywaji sijui na chakula, nilimuona akiongea na kijana mmoja na kumpa pesa, ilibidi nifatilie ili nijue ni kutu gani. Yule kijana nilimuona akibeba vinywaji ambapo kimoja wapo ilikuwa ni juisi kwenye glasi ila nilimuona akitia kitu kwenye ile juisi, nikafatilia kuona ni nini kinaendelea. Pale mlipokaa vikaletwa vinywaji na chakula, ukaanza kunywa ile juisi ila taratibu ulionekana kuregea hadi kulaza kichwa chako kwenye meza, nikamuona Yule shemeji yako ameinuka. Sikutaka kujua ameenda kufanya nini ila nilichohisi ni kuwa ana lengo baya na wewe, ikabidi nianze kukukokota pale ili nikutoa eneo lile. Tulifika nje nikakodi bajaji tukaanza kuondoka ila shemeji yako akawa anatufata nyuma ikabidi nimwambie Yule dereva bajaji atupitishe njia za panya na tukampoteza mwelekeo Yule shemeji yako. Nilitaka nikupeleke kwenu ila nikakumbuka kuwa mama yako ni mlokole na hatopendezewa kukuona kwenye hali kama ya ulevi, yani Erica ulikuwa kama mtu aliyekuwa pombe saana, ikabidi nikulete hata nyumbani kwangu. Erica hakuna chochote nilichofanya kwako, siwezi kufanya jambo lolote bila ridhaa yako, furaha yangu mimi ni kuona ukizinduka tu”
Erica alijaribu kufikiria na kukumbuka vizuri, akakumbuka pale alipokunywa kinywaji na kuzidiwa na kizunguzungu basi ila mengine hakuyakumbuka ila alitambua kwamba shemeji yake alikuwa na lengo baya kwake,
“Yani Yule shemeji yangu jamani, kweli alitaka kunibaka loh! Asante kwa kuniokoa Babuu, nashukuru sana. Saa ngapi saa hizi?”
“Ni saa sita mchana hii yani hadi nilikuwa na mashaka nikasema usipozinduka nikupeleke hospitali ila nilikuwa nahofia kuwa nitaenda kujielezea nini”
“Mungu wangu, mama atakuwa na wasiwasi balaa, naomba niende nyumbani”
“Hakuna shida, nitakusindikiza ila ngoja unywe kahawa kwanza”
Babuu alimmiminia Erica kahawa na kumpa anywe ili angalau aweke kichwa vizuri,
“Na simu yako iliita sana jana ila nilipoangalia jina niliona Shemeji james, na alikuwa akipiga sana kwahiyo nikaamua kuizima. Samahani kwa hilo kama litakukwaza”
“Hata usijali Babuu, cha msingi umeniokoa toka kwenye mikono ya lile shetani. Yani mtu anatembea na dada yangu, bado haridhiki anataka kunibaka na mimi loh! Sijui wanaume mmeumbwaje!”
“Sio wote bhana Erica, hiyo ni tabia ya mtu hata kuna wanawake wengine wenye tabia hizo”
“Hapana, wanaume nyie sio watu kabisa mna tamaa sana”
“Erica, kumbuka na mimi ni mwanaume pia ila umelala hapa bila kujitambua na sijakufanya chochote. Tumetofautiana wanaume, na hiyo ni tabia ya mtu tu. Huyo shemeji yake itakuwa ndio tabia yake hiyo”
“Sawa ila kwa muda huu nahitaji kumuona mama yangu tu maana najua atakuwa na mawazo sana”
Baada ya hapo Babuu alimsaidia kujiweka sawa Erica kwani bado kichwa chake hakikuwa vizuri. Kisha wakatoka nje na kukodi bajaji ya kuwapeleka nyumbani kwakina Erica.
 
SEHEMU YA 167


Walifika nyumbani kwakina Erica, Babuu alitaka aingie nae ndani ila Erica alimzuia,
“Hapana Babuu, nenda tu. Sitapenda mama aone nimefika nikiwa nimeongozana na mwanaume, nashukuru sana kwa msaada wako”
“Haya Erica, ila kumbuka upatapo jambo lolote juwa yupo Babuu bega kwa bega na wewe kukusaidia. Siwezi kuacha kukupenda Erica”
Babuu alisogea na kumkumbatia Erica, kisha akambusu na kumuaga halafu Erica akaingia ndani kwao.
Kumbe mama Erica alikuwa ametoka dukani kwahiyo kile kitendo cha Babuu kumkumbatia Erica na kumbusu alikishuhudia vilivyo, alipatwa na hasira sana yani alijikuta hata alichonunua amekitupa, huku akijaribu kuwakimbilia ila Babuu nae alishapanda kwenye ile bajaji na iliondoka.
Mama Erica alifika na kuingia ndani kwa gadhabu sana na kuita,
“Erica, wewe Erica, hebu njoo hapa”
Erica alitoka chumbani na kwenda sebleni maana alitaka kujiandaa akaoge, mamake alimshika na kuanza kumpiga,
“Umefanya usiku wote nishindwe kulala, kumbe umeenda kufanya umalaya wako”
Huyo mama alimpiga sana Erica bila hata kusikiliza kuwa Erica ana jambo gani la kueleza maana hakumuuliza na wala hakumpa nafasi ajieleze ila yeye alimpiga tu, hadi Erica alizimia.
Baada ya kuzimia alihamaki,
“Mungu wangu, mwanangu! Erica mwanangu jamani, mwanangu Erica!”
Erica alikuwa kimya kabisa na kufanya mamake achanganyikiwe.


Huyu mama alimpiga sana Erica bila hata kusikiliza kuwa Erica ana jambo gani la kueleza maana hakumuuliza na wala hakumpa nafasi ajieleze ila yeye alimpiga tu, hadi Erica alizimia.
Baada ya kuzimia alihamaki,
“Mungu wangu, mwanangu! Erica mwanangu jamani, mwanangu Erica!”
Erica alikuwa kimya kabisa na kufanya mamake achanganyikiwe.
Alishindwa hata aanzie wapi na aishie wapi, akachukua simu yake na kumpigia Mage kumpa taarifa kuwa Erica amerudi na kuzimia kwahiyo awahi na usafiri wampeleke hospitali, kwa bahati Mage hakuwa amefika mbali sana kwahiyo alirudi nyumbani akiwa kwenye bajaji, alishuka kisha kusaidiana na mama yao kumbeba Erica na kumpakia kwenye bajaji kwaajili ya kumpeleka hospitali.
Wakiwa kwenye bajaji Mage alimuuliza mama yake,
“Kwani imekuwaje mama?”
“Usiniulize habari hizo Mage, ngoja kwanza tukamuhudumie hospitali”
Walifika hospiatali na kupokelewa ambapo moja kwa moja Erica alikimbizwa kwa daktari. Kwakweli mama yao alikuwa amechanganyikiwa sana, hata hakujua ni nini afanye kwa wakati huo. Mage akapata wazo la kumpigia simu shemeji yake kwani alijua hapo hospitali lazima kutakuwa na maswala ya pesa, kwahiyo mtu wa kuwasaidia kwa haraka ni shemeji yake James,
“Shemeji tupo hapa hospitali tumemleta Erica amezidiwa yani hata hatuelewi”
“Imekuwaje kwani?”
“Sijui shemeji”
“Basi nakuja”
Mage alikata simu huku akiendelea kumpa moyo mama yake kuwa Erica atakuwa sawa kabisa.
Baada ya muda kidogo Erica alitolewa kwa daktari na kupelekwa wodini, kisha wakataka kwenda kumuona ila daktari aliwazuia kwa muda na kuwaita pembeni,
“Msijali amezinduka na atakuwa sawa kabisa”
“Ooooh asante Mungu jamani mwanangu dah!”
“Usijali mama, ila tulia kuna mambo nataka nikuulize”
“Niulize tu”
“Kwani mwanao mara ya mwisho alikuwa wapi? Ameangukia wapi?”
“Ameangukia nyumbani, ila mara ya mwisho sijui alikuwa wapi”
“Inaonekana mwanao alitumia madawa ya kulevya”
Mage na mama yake walishtuka sana na kumuuliza daktari kwa mshangao,
“Madawa ya kulevya?”
“Ndio, sasa sielewi alitumia kwa ridhaa yake au imekuwaje ila inaonekana ametumia madawa ya kulevya tena mengi, halafu alipigwa maana ana alama”
Wakati akiendelea kuwaelezea alifika James eneo lile na kuingilia kusikiliza yale mazungumzo, kitendo kile cha kusikia kuwa Erica alitumia madawa ya kulevya kilifanya amvute dokta pembeni ili aongee nae cha kuwaambia wale ndugu wa Erica na sio habari za madawa tena.


 
SEHEMU YA 168


Kwenye mida ya saa mbili usiku, Erica aliruhusiwa kurudi nyumbani kwahiyo walirudi nae, kwakweli Erica alikuwa kimya tu huku akimuangalia shemeji yake akiwaendesha kuwarudisha nyumbani, alikuwa na chuki nae kwakweli na laiti angejua shemeji yake alichosema kwao basi hasira zingemzidi maradufu.
Walifika nyumbani na kumuacha akapumzike, kwani alionyesha kutokutaka kuongea jambo lolote ukizingatia mwili wake ulikuwa na maumivu maumivu ya kupigwa na mama yake.
Alienda kuoga na kukaa kitandani huku akijiuliza sana,
“Hivi kosa langu nini lakini? Kwanini mimi? Sielewi, yani nataka kubakwa nafanyiwa kitu cha kikatili kama kuwekewa madawa kwenye kinywaji change, ila narudi nyumbani mama anashindwa nata kuniuliza anafikia tu kunipiga jamani hii ni haki kweli? Kwanini nafanyiwa hivi lakini? Kichwa chote bado kinaniuma”
Aliamua kujilaza tu kwani hata akiendelea kujiuliza ni kuendelea kujiumiza kichwa tu.
Kulipokucha mama yake alienda kumuamsha na kumuomba akanywe chai,
“Nakuomba uje kunywa chai mwanangu”
“Sawa mama”
Erica aliinuka na kwenda kuoga kwanza kisha akaenda kunywa chai, na alipomaliza sasa alienda kukaa na mama yake ili ajue ni kwanini mama yake alichukua jukumu la kumpiga tu,
“Mama, mbona jana ulinipiga tu bila kuuliza ilikuwaje!”
“Mwanangu, kwanza nisamehe bure ila mimi ni mzazi na nina umia sana pindi nikisikia kuwa mwanangu kaanza tabia mbaya. Ngoja nikuulize tu kidogo, umeanza lini kunywa pombe mwanangu?”
“Hapana mama, mimi sio mlevi”
“Unajua mwanzoni daktari alisema kuwa inaonyesha ulitumia madawa ya kulevya ila badae alikuja kusema kumbe sio madawa ni pombe kali. Mwanangu umeanza lini kunywa pombe? Kumbuka nimekulea katika maadili ya dini, na siku zote nakufundisha kuwa pombe ni mbaya. Umeanza lini kunywa pombe? Niambie ukweli mimi ni mama yako”
“Hapana mama, situmii pombe mimi”
“Niambie ukweli Erica, mimi ni mama yako. Ukinificha mimi utamwambia nani tena? Halafu Yule mwanaume muuza samaki uliniambia anakuleteaga samaki kumbe ni mwanaume wako!”
“Kheee mama, nani kakwambia kuwa ni mwanaume wangu?”
“Erica na hilo unanificha kweli?”
“Sikufichi mama ila nashangaa aliyekupa hizo taarifa”
Ilibidi mama Erica, amuelezee Erica jinsi walivyomkuta Bahati pale mlangoni na jinsi James alivyosema hadi kumpeleka polisi,
“Kheee mama, kwahiyo kijana wa watu mmempeleka polisi!”
“Ndio, kama mtu kaenda kunifichia binti yangu kwanini nisimpeleke polisi!”
“Jamani mama, hausiki na kupotea kwangu huyo. Ni nani aliyetoa wazo hilo la kumpeleka Bahati polisi? Ni James eeeh!”
“Kheee wewe mtoto huna adabu yani James unamuita James badala, umuite shemeji yako!”
Erica aliinuka na kwenda chumbani kwake, akachukua simu yake ilikuwa bado imezimwa, akaiwasha na baada ya muda akampigia simu shemeji yake,
“Erica mrembo, unaendeleaje?”
“Mbwa wewe, usiniulize chochote. Kwanini umemuweka Bahati polisi? Eeh! Sasa naenda huko polisi, halafu nasema ujangili uliotaka kunifanyia”
“Sasa polisi unaenda kufanya nini?”
“Naenda ili wamuachie Bahati”
“Acha kunichekesha Erica, unafikiri huyo Bahati anaweza kuachiwa kwa njia ya jazba kama usemayo wewe? Hiyo sio njia ya kuachiwa huyo Bahati, hivi unajuaga mimi ni mtoto eeeh! Nina akili kukuzidi na huwa nafanya vitu kwa akili, unatakiwa kuwa mpole niombe kwa adabu kuwa nimtoe Bahati na sio kwa kunikaripia”
Erica alinyamaza kwa muda na alikuwa na hasira sana na huyu shemeji yake, ila kwavile alitaka Bahati atoke ikabidi awe mpole tu, kwani kiukweli nay eye ni muoga wa polisi balaa,
“Basi shemeji nakuomba umtoe Bahati”
“Sawa, nitamtoa ila kwa sharti moja yani ukilivunja namrudisha tena rumande”
“Naomba lisiwe sharti gumu”
“Hata sio gumu, naomba usiseme chochote kuhusu mimi”
Erica alimuitikia shemeji yake kwa shingo upande na shemeji yake aliahidi kumtoa Bahati, kiukweli roho ilimuuma sana Erica kwani shemeji yake ndio muhusika halafu anawekwa ndani mtu hata asiyehusika. Alikata simu huku akiwa na kinyongo sana kwenye moyo wake, alikaa kule kule chumbani akiwa na mawazo ila mama yake akamuita tena na kumwambia,
“Erica, hutakiwi kukaa na mawazo kwakweli, ujue mamako nipi. Niambie nini kinakusibu?”
“Hakuna kitu mama”
“Haya, basi niambie sasa ilikuwaje juzi mpaka kunirudia nyumbani jana?”
“Mama, hata mimi sina kumbukumbu”
“Huna kumbukumbu kivipi? Erica ujue nimekuona na mwanaume aliyekurudisha mkibusiana kwenye geti langu bila hata ya aibu? Kwakweli Erica ningekuwa mzazi mwingine yani ningekufukuza kabisa. Yani wewe nakuona na mwanaume halkafu unasema huna kumbukumbu kweli!”
“Hivi mama hata nikikwambia ukweli utaniamini?”
“Niambie tu ukweli, kama huyo mwanaume anakupenda sana basi akuoe uone jinsi ndoa vilivyo na uchakae hadi ukumbuke chakula ulichokuwa unakula hapa nyumbani. Unataka kunificha nini kwa mfano? Wakati shemeji yako aliona kila kitu ukiwa umelewa na kuondoka na mwanaume. Erica naongea kwa uchungu hivi aaargh sitaki hata kuongelea tena, ni kichefuchefu tu kukuangalia”
Mama yake Erica aliinuka zake, Erica aliwaza sana akaona ni vyema kumwambia mama yake ukweli ila alitaka tu kusikia kuwa Bahati ameshatoka ndio amwambie ukweli mama yake kwani kauli ya kusema kuwa alionekana amelewa na kuondoka na mwanaume ilimuumiza sana.
 
SEHEMU YA 169



Erica aliingia chumbani kwake, na kukuta simu yake kuna mtu alipiga kisha akakuta ujumbe,
“Erica mpenzi wangu una nini lakini? Hewani hupatikani, unafanya niwe na mawazo mwenzio jamani, unajua huku ni usiku muda huu ila hadi sasa sijalala, usingizi hauji kabisa sababu yako, Erica basi ingia fecebook kidogo tuongee mpenzi wangu”
Ikabidi Erica aiwashe na ile simu yake nyingine na kuingia kwenye mtandao, ni kweli alikuta jumbe kadhaa za Rahim hadi zilimtia simanzi kwakweli na kuona ni jinsi gani Rahim alimpenda, alijisikia fahari sana kupendwa na Rahim na kujiona ni msichana mwenye bahati sana kati ya wenye bahati ulimwenguni.
Aliwasiliana nae kwa bashasha sana na kumwambia kuwa anakaribia kufungua chuo, basi Rahim akamuahidi kumtumia pesa nyingine itakayokuwa ikimsaidia pindi atakapofungua chuo, Erica alifurahi sana na kuona kweli mwanaume kapata, akawasiliana nae sana mpaka usiku ulifika kwa upande wa Erica na kwa upande wa Rahim ilikuwa kumekucha, alimwambia
“Erica, kwa hakika leo nimekesha”
“Pole Rahim, sasa si utasinzia leo kwenye mambo yako”
“Hapana siendi popote leo, ngoja nilale tu. Nadhani ile hela nitakutumia kesho”
“Asante mpenzi wangu”
Erica aliagana na Rahim huku akiwa na tabasamu kubwa sana usoni mwake, alikaa akimuwaza sana Rahim kisha kuinuka na kwenda kufanya maandalizi ya kula chakula cha usiku na kulala maana hakuwa na kazi nyingine ya ziada ya kufanya kwa wakati huo, yani toka sakata la juzi basi mama yake amekuwa akifanya kila kazi mwenyewe na wala hakupoteza muda wa kumuita ita mtoto wake kwani aligundua ni mengi sana anamficha.
Erica alienda jikoni na kuangalia chakula ambapo alikuta mama yake ameshapika, ila akaona chakula cha siku hiyo hataweza kukila mpaka apate soda maana ilikuwa ni ndizi nay eye alipenda kula ndizi huku akinywa soda, kwahiyo akaenda kuchukua hela ili aende dukani kununua soda.
Wakati ametoka nje akitaka kwenda dukani, alishangaa kuona mtu amejikunyata pale nje ya geti lao, akashtuka sana na kumshtua Yule mtu kuwa ni nani, alishangaa sana kuona mtu huyo ni Bahati,
“Kheee Bahati!”
Bahati aliinuka na kumkumbatia Erica,
“Jamani Erica wangu, nafurahi kukuona”
“Unafanya nini hapa!”
“Erica nimeruhusiwa muda si mrefu kutoka selo, ila nikasema iendi nyumbani nitakuja hapahapa nje ya nyumba yenu labda Mungu asikie kilio change nikuone. Nimeteseka Erica, nimepigwa Erica bila ya kosa lolote, siwezi kukutenda chochote kibaya ila nikashangaa nikipigwa eti nilitaka kukubaka kwakweli imeniuma sana”
“Sikuelewi Bahati”
“Nielewe tu Erica, kwani hukujua kama jana nilikuja hapa kwenu na mkasa huo wa kupelekwa selo kunikuta?”
“Hebu nieleze vizuri”
Bahati akamueleza ilivyokuwa jana yake hadi yeye kupelekwa selo, kwakweli Erica alishangaa sana kile kitendo cha kuambiwa kuwa James alimpiga kwanza Bahati na kumpeleka polisi,
“Jamani huyu James ananitaka nini mimi jamani! Pole Bahati ila naomba uende kwenu”
“Nitaenda Erica, ila niambie kwanza ilikuwaje hadi simu zako hazipatikani, na nyumbani kwenu kunihisi mimi vibaya ilikuwaje?”
“Bahati naomba uende kwenu, maana sitaki matatizo zaidi”
“Matatizo gani?”
“Wewe nenda kwenu tu, na wakikuuliza ulikuwa wapi utasemaje?”
“Nitajua cha kusema”
“Ila naomba usiseme kama ni mimi ndiye nimesababisha umefungwa, kwenu wataniua”
“Sikuelewi Erica, una maana gani?”
Erica hakuona umuhimu wa kumficha ilibidi amwambie ukweli kuhusu nyumbani kwao walichomtenda siku ile aliyoenda kuangalia mabwawa ya samaki, kwakweli Bahati aliumia zaidi baada ya kuambiwa vile kuwa kwao walimshambulia Erica, kwa jinsi alivyochukia alitamani hata aruke kwenda kwao. Ila alimsindikiza kwanza Erica dukani akanunue soda na kurudi kwao kisha yeye akaondoka kwenda kwao.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 170


Erica alirudi ndani kwao na kula, kisha alipomaliza alikaa na mama yake kumueleza maana muda huo aliamua kumueleza siku hiyo kuhusu shemeji yake,
“Mama, naomba saizi nikwambie ukweli kilichotokea kwangu juzi”
“Haya niambie”
“Mama, shemeji alienda na mimi hotelini kupata chakula cha jioni, nikaletewa kinywaji baada ya kunywa nikahisi kizunguzungu na kutokujielewa kabisa, alikuja tu mtu kuninyanyua na kuniondoa eneo lile kiukweli hata sikuelewa. Sasa nilipozinduka ndio Yule mtu akaniambia ukweli, mama shemeji alitaka kunibaka”
“Kheeee nilikaa kimya nikisubiria hiyo kauli yako ya kusema alitaka kukubaka, hivi Erica huna aibu kabisa! Yani James anavyotusaidia kwenye nyumba hii, ni kitu gani ambacho James hatusaidii? Leo hii ndio atake kukubaka kweli? James amekujua wewe hata kujitoa tongotongo huwezi halafu leo hii useme James alitaka kukubaka! Erica una matatizo gani wewe mwanangu?”
“Mama, kwani James kakupa nini wewe? Kama ameweza kutembea na msichana wa kazi hadi kumpa mimba, ndio ashindwe kunibaka mimi! Hebu mambo mengine uwe unafikiria mama yangu, nimeamua kukwambia ukweli, ukiukubali haya na ukiukataa haya, ila Yule James sitaki tena msaada wake, sio mtu mzuri kwangu Yule. Anataka kunibaka, hata kama unamuamini vipi ila ndio hivyo alitaka kunibaka”
Erica aliinuka na kwenda chumbani maana hakutaka mama yake amuelewe au asimuelewa ila yeye alitaka kusema ukweli na ndivyo alivyofanya.
Alitaka kulala ila kabla hajalala alipigiwa simu na Babuu akiulizwa hali yake na kumjibu kuwa yupo salama,
“Vipi naweza kukuona kesho”
“Mmmh nitaangalia kama nitakuwa na muda”
“Jamani Erica, basi hata nije kwenu nikuone”
“Nitakwambia basi, ila usipende kunipigia pigia sana simu usiku mimi ni mchumba wa mtu”
“Ila Erica kwani huyo mume unaishi nae jamani! Najua upo kwenu ndiomana nimekupigia”
Basi akaongea ongea nae kidogo pale na kulala, ila ikiwa ni saa kumi alfajiri alisikia kama mlio wa simu yake, akaangalia na kukuta ni Rahim alimtafuta, akajua lazima atakuwepo facebook akaamua kuingia kwenye simu yake,
“Tayari nishakutumia Erica, nimekutumia milioni mbili”
Yani Erica hadi usingizi ulikata maana alijua hela ya matumizi angemtumia ndogo tu ila kuona kamtumia hela nyingi alijikuta hadi akiamka vizuri na kuendelea kusoma jumbe zingine za Rahim huku akimjibu na kumshukuru. Kwa upande mwingine alianza kupanga matumizi kwa ile hela aliyotumiwa, alikuwa tu akijisemea
“Ila mimi sinaga matumizi ya hela nyingi hivi. Yani laity Rahim angejua kama maisha yangu ni ya kawaida kabisa hata asingehangaika kunitumia hela nyingi hivi”
Aliongea ongea pale na Rahim kwa njia ya ujumbe huku akipanga kuwa kesho yake ndio aende akatoe zile pesa.

Kulipokucha aliamka saa nne asubuhi kwasababu toka ile saa kumi alikuwa akitumia tu facebook mpaka saa moja asubuhi, sasa alilala tena na kuamka saa nne. Alimkuta mama yake sebleni na kumsalimia kisha mama yake akamwambia,
“Mmmmh hii tabia ya kuamka saa nne hapana mwanangu, haifai kwa mtoto wa kike”
“Samahani mama, ni leo tu”
“Ni leo tu wapi wakati ndio tabia yako siku hizi hiyo, hata sijui chuo unasomaje”
Alimkanya kanya pale ila baada ya hapo tu Erica alijiandaa na kutoka.
Moja kwa moja alienda benki ambayo ingekuwa rahisi kwake kutoa zile pesa, alipokuwa nje alipigiwa simu na Babuu akiulizwa mahali alipo, sababu hakuwa na mashaka yoyote na Babuu alimtajia tu alipo kisha akakata simu na kuingia benki ila muda kidogo Babuu alimtumia ujumbe,
“Unajua mimi muda huu hata sipo mbali na hapo uliposema, nakuja nitakusubiri nje nipo na mamdogo”
“Sasa mamako mdogo wa nini?”
“Niliwahi kumwambia kuwa kuna msichana mmoja niliwahi kumpenda sana, ndio leo nimekutana nae kanisikia nikiongea nawe kwenye simu kapenda akuone”
“Mmmh! Haya sawa, utanisubiri basi”
Erica alifanya zile harakati zake za kutoa pesa na kuweka katika pochi yake kisha akatoka, na alishasahau wazo la kuonana na Babuu kabisa kwani alipochukua zile hela akili yake ilikuwa ikiwaza hela tu.
Akawa anaondoka, mbele kidogo Babuu alimuita,
“Erica, Erica, Erica”
Erica akageuka nyuma na kumuangalia Babuu akamuona kwa mbali kuna mwanamke kasimama nae, alipomuangalia mwanamke Yule vizuri aligundua ni Mrs.Peter yaani mama yake Rahim.

 
SEHEMU YA 171


Erica alifanya zile harakati zake za kutoa pesa na kuweka katika pochi yake kisha akatoka, na alishasahau wazo la kuonana na Babuu kabisa kwani alipochukua zile hela akili yake ilikuwa ikiwaza hela tu.
Akawa anaondoka, mbele kidogo Babuu alimuita,
“Erica, Erica, Erica”
Erica akageuka nyuma na kumuangalia Babuu akamuona kwa mbali kuna mwanamke kasimama nae, alipomuangalia mwanamke Yule vizuri aligundua ni Mrs.Peter yaani mama yake Rahim.
Erica alishtuka kidogo na akili ya haraka haraka ikacheza kuwa Yule ndio mamake mdogo na Babuu kwahiyo kuna undugu flani upo kati ya Babuu na Rahim, hakutaka kupoteza muda kwakweli maana aliisikia bodaboda ikipitakaribu yake aligeuka na kuisimamisha akapanda na kuondoka bila kujali Babuu alimuita kwa kiasi gani, kwani hakutaka kuanza kuulizana tena maswali na Yule mama halafu alihisi Yule mama hajamuona vizuri kwahiyo alishukuru ile bodaboda kupita karibu yake, yani ni alimuelekeza tu kwao kisha Yule wa boda boda akampeleka.
Erica alifika kwao na kuingia ndani akamkuta mama yake akiendelea na ile kazi yake ya kushona, akamsalimia mama yake kisha baada ya salamu alimuuliza mama yake,
“Mama unataka hela?”
“Hivi kuna mtu asiyetaka hela mwanangu? Katika dunia hii, kuna mtu asiyependa hela? Nataka ndio”
Erica akaingia kwanza chumbani kwake, halafu akamchomolea mama yake laki tano na kumpelekea, mama yake alihamaki sana,
“Erica, hela zote hizi?”
“Ndio mama, kwani kuna tatizo gani?”
“Isije kuwa ndio posa napewa kwa mtindo wa tofauti!”
“Hapana mama sio posa, ila kuna mwanaume ananitongoza ndio kanipa hela hizo”
“Kheee mwanangu jamani, una bahati sana. Huyo mwanaume mlete nyumbani haraka umtambulishe. Nitawapa baraka zote”
Erica akacheka na kusema,
“Mama na wewe”
“Sio mama na wewe, mwanaume wa kukupa hela zote hizi ni wa kumshikilia tena umshikilie haswaaa, ungemleta tu nyumbani nimtambue”
“Nitamleta mama, ila kwasasa hayupo nchini. Akirudi tu namleta”
“Wow, Erica sikujua kama una akili kiasi hiko, yani umetafuta mwanaume wa maana kiasi hiko! Erica mwanangu nakupa Baraka zote kwa huyo mwanaume”
Erica alitabasamu sana na kwenda chumbani huku akimuwaza mama yake pia kuwa anaona pesa mbele tu na kama angemuonyesha zote ambazo Rahim alikuwa anatuma ingekuwaje. Erica alitulia chumbani kwake akiwaza vitu vingi sana, hakuwa na matumizi mengi ya pesa kama wanawake wengine kwahiyo ile pesa kwake ilikuwa ni nyingi sana.
Alichukua simu yake na kukuta amepigiwa sana na Babuu, kisha akaamua kumpigia,
“Erica mbona umenikimbia? Umefanya nionekane mjinga kwa mamdogo”
“Sikutaka tu kukwambia ukweli ila sikutaka kuonana na ndugu yako yoyote”
“Kwani kuna tatizo gani Erica, maana hata Yule mamdogo ameuliza kuwa kwanini ulikimbia”
“Kwani aliniona wakati naondoka?”
“Amekuona ndio wakati ile bodaboda uliyopanda ikiondoka, akaniuliza kuwa wewe ni Erica gani?”
“Ukamjibuje?”
“Sikumjibu chochote sababu hakufahamu”
“Babuu sikia, mimi hukuniandaa kabla zaidi ya kuniandikia ujumbe tu kuwa upo na mamako mdogo, kiukweli sikujiandaa kukutana na mtu mwingine yeyote asiyenizoea. Nisamehe kwa hilo”
“Poa. Usijali Erica”
Alikata simu kwani alianza kuwaza namna ya kumkwepa Babuu kwani aligundua kuwa Babuu ana undugu na Rahim yani ni mtoto wa mamkubwa na mdogo na hawezi kumuacha Rahim kwasababu ya Babuu kwahiyo alitafuta njia tu za kumkwepa Babuu.
Alitulia ila jioni yake alisikia mtu akigonga geti lao, akatoka na kukuta ni Bahati, akamuuliza kwa mshangao,
“Bahati tena! Umekuja kufanya nini sasa?”
“Erica sikujua yote ambayo ndugu zangu wamekutendea, Erica bora hata ndugu zangu wote wanitenge lakini sio wewe. Nakupenda sana”
“Ila mimi sikupendi”
“Erica najua unasema kwa hasira tu, nakupenda sana. Wewe ndio mke wangu, ndoto zangu zote ni kuwa na wewe. Nakupenda Erica wangu”
“Hivi Bahati nifanye kitu gani ili uamini kwamba sikutaki tena? Sijawahi kukupenda Bahati na sitokupenda kamwe, yupo mwanaume mwingine nimpendaye”
“Ndiyo huyo Erick au?”
“Sio Erick ila yupo mwingine nimpendaye, tafadhali bahati endelea na mambo yako tu”
“Kama hunitaki Erica ujue nipo tayari nifie hapa mlangoni kwenu”
Erica alimuacha pale mlangoni na kuingia zake ndani.
 
SEHEMU YA 172

Erica alikaa ndani kwao kwa muda sana ila akafikiria akili za Bahati akaona kuwa hawezi kuondoka pale, na kiukweli hakupenda kuona Bahati akiteseka sababu yake, akaamua kutoka nje na ilikuwa saa nne usiku lakini alimkuta Bahati pale pale nje, kwa bahati siku hiyo mamake alikuwa ndani tu kwahiyo angetoka toka nje angemuona Bahati.
Alimkuta pale ikabidi aongee nae kwa utaratibu,
“Bahati jamani, unajua sipendi kuona ukipata shida au kuhangaika”
“Ila mimi nahangaika sababu yako Erica, nakupenda sana”
“Sikia nikwambie kitu, kama wanipenda sana naomba huu muda unaopoteza hapa utulie ufanye biashara zako. Kwa hakika ukitoka kimaisha itakuwa rahisi kuwa na mimi”
“Ila Erica, mimi nahangaika kwenye shughuli zangu sababu yako ila wewe kama hunitaki tena shughuli zangu zina maana gani! Sioni umuhimu wa shughuli zangu ikiwa hunitaki tena”
“Kwahiyo nikikutaka ndio utakuwa busy na shughuli zako?”
“Nitafanya shughuli zangu kwa raha sababu najua upo”
“Sasa Bahati jamani, fanya shughuli zako kwaajili ya watoto wako na sio mimi”
“Hao watoto nitapata nikiwa na wewe Erica, nakuomba Erica uwe na mimi”
“Sikia basi masharti yangu, ukifata haya masharti ndio nitakuwa na wewe”
“Niambie hayo masharti Erica”
“Nataka uwe busy na biashara, unanipigia simu hovyo hovyo ndiomana nilizima simu yangu. Sitaki unipigie simu hovyo hovyo, nyumbani kwetu unapajua ila sio sababu yaw ewe kuja kila unapojisikia. Nakuomba Bahati, tafuta maisha kwanza ndio iwe rahisi kwa mimi kuwa na wewe, ukiendelea hivi kuhangaika hangaika kwa hakika hakuna kitu utakachokuwa unafanya, yani utapoteza hela tu bila matunda yoyote. Tafuta maisha kwanza”
“Sawa Erica, ila basi naomba niwe naongea nawe hata kwenye simu kidogo itakuwa afadhari kuliko hivi Erica. Usinione hivi ila nawaza maisha yetu sana tu, hapa nataka nikiingiza faida ya kutosha kwenye ile biashara yetu, nianzishe biashara nyingine ambapo ukimaliza chuo wakati unasubiria ajira utakuwa unaendelea nayo”
“Yani wewe una mawazo ya biashara tu”
“Ndio nina mawazo ya biashara ila hela tu ndio inakuwa shida kwangu ila nina uhakika hizi biashara nikizikazania haswaaa yani maisha yatakuwa mazuri tu. Maisha yetu yatabadilika Erica, siwezi chezea hela zile ulizonipa lazima zizae matunda na ipo siku nitakufanyia kitu ambacho huwezi kukifikiria kuwa naweza kufanya ila nitakufanyia kitu kikubwa sana Erica”
Erica alimwambia asubiri kidogo na kuingia ndani, Bahati hakujua ni kitru gani ambacho Erica anaenda kufanya ila alimsubiria tu.
Muda kidogo Erica alirudi na kumwambia,
“Sasa, nataka uwe busy na biashara, si umesema kuna biashara unataka kunianzishia na mimi ili nikimaliza chuo nihangaike nayo. Sasa mimi harakati za kuanzisha biashara kwasasa sina ila hela ninayo, nakupa hela hii ukafanye hiyo biashara”
“Lakini Erica sijasema kuwa nataka pesa”
“Nakuomba upokee hela hii Bahati, nina maana yangu halafu naomba usiwe unanifatilia sana. Nahitaji kuwa huru sio kugandwa gandwa na mwanaume kila ninapokuwa hadi nashindwa kupumua ndiomana sikutaki”
“Ila hapana Erica siitaki hiyo hela”
“Kama hii hela huitaki basi, usinifatilie tena na mimi na wewe basi”
Ilibidi Bahati awe mpole na kupokea ile hela kwa Erica huku akiahidi kufata masharti yake maana anaogopa kweli kuambiwa hatakwi na Erica, kisha Erica alimwambia akodi bodaboda aondoke,
“Ila bado kitu kimoja Erica”
“Kitu gani hicho?”
“Naomba namba yako ya simu nyingine”
“Bahati, kwetu unapajua, kwa dadangu unapajua, chuo ninachosoma unakijua unataka nini tena? Namba ya simu sikupi hadi ujirekebishe tabia yako, sitaki unitafute mara kwa mara yani kuanzia leo hapa kwetu uwe unakuja mara moja kwa mwezi”
“Dah Erica kwanini lakini unanifanyia hivyo?”
“Siku ukiendelea na kununua gari ninalopenda mimi ndio nitakuruhusu uje kwetu mara kwa mara, ila kwasasa kafanye kazi”
“Dah! Erica unanitesa lakini?”
“Ukitaka kupatana na mimi fanya kile ninachosema, fanya kazi kwa bidii maana sioni fahari niseme kuwa mpenzi wangu ni mvuvi. Tafadhali jiimalishe na ubadilishe aina ya kazi. Kwaheri”
Bahati ilibidi akubali kila kitu maana alihisi pengine akiendelea kuongea labda Erica atabadilisha mawazo tena na kumtimua kabisa, alipigia simu bodaboda kisha ikafika akapanda na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 173


Erica alirudi ndani, yani hata alikuwa hajutii kitendo cha kutoa hela kwa Bahati kwani yeye aliwaza kuwa pengine baada ya Bahati kupata zile hela angemkimbia hata alishangaa kuona bado Bahati akimng’ang’ania.
Basi alienda kulala tu muda huo, ila kwa upande wa Bahati alikuwa na hisia kubwa sana kuwa Erica anampenda sana sababu si rahisi kwa mtu asiyekupenda kukupa pesa kama Erica anavyofanya kwa Bahati, aliiangalia vizuri ile hela aliyopewa na Erica ilikuwa ni milioni moja na alipanga kufanya kitu cha maana zaidi ili siku atakayoonana tena na Erica amuonyeshe kitu kizuri alichokifanya, muda mwingi Bahati aliutumia akimfikiria Erica ila tofauti kwenye kichwa cha Erica maana kwa kipindi hiko hakuweza kutumia hata sekunde tu kumuwaza Bahati ila alifanya vitu ili Bahati aismfatilie tena wakati huo huo hakutaka kumuumiza.
Mawasiliano ya Erica na Rahim yalipamba moto na hakutaka Babuu ajue chochote kwani aliwaza kama Babuu angejua basi angemuharibia.
Erica alifungua chuo na kwenda chuoni kama kawaida akitokea kwao kwani toka yale maswala ya yeye kusifika kwa jina baya chuoni hakutaka tena kuishi hosteli.
Alikuwa akienda chuo na kurudi kwao huku akiwasiliana na Rahim tu kwa kipindi hiko hata Babuu alipompigia simu alimwambia kuwa yupo busy sana na masomo yake kiasi kwamba hawezi kuonana na mtu yeyote.

Siku hiyo Mage alienda nyumbani kwao kuzungumza na mama yao, muda huo Erica alikuwa chumbani kwahiyo alisikia kila kitu ambacho dadake aliongea na mama yao. Mama Erica alimsimulia Mage vile alivyoambiwa na Erica kuwa James alitaka kumbaka,
“Hivi unaamini hilo jambo Mage?”
“Mama, Erica ni ndugu yetu sisi tusimuamini halafu tumuamini James inakuja kweli? Kumbuka James kampa mimba msichana wa kazi tena mama sijakwambia lingine, kumbe kuna msichana pale mtaani kazaa na James nimezipata hizo habari ila sijataka kumwambia mdogo wangu atachanganyikiwa”
“Kheee kumbe yule mwanaume ndio ana akili fupi kiasi hicho?”
“Ndio hivyo mama ila usipaniki wala nini, halafu hiyo habari ya James kutaka kumbaka Erica naomba ibaki kuwa siri yetu na isifike kwa Bite, ana mtoto mdogo kwasasa atachanganyikiwa”
Mama yao alikubaliana nae na kumwita Erica ambapo waliongea nae kuwa habari ile ifanywe kuwa ni siri kati yao.
“Hakuna shida, nimesema ukweli ili nisiendelee kusingiziwa kwenye mambo ambayo sijayafanya”
“Sawa, ila Erica nataka niongee mara moja na wewe tu”
Ilibidi muda wa kuondoka dada yake amsindikize na aweze kuongea nae,
“Nasikia Erica ulikuwa na mahusiano na Derick kabla ya kujua ni ndugu yako”
“Hapana dada, nani kakwambia?”
“Usibishe Erica, nataka nikusaidie unajua kutembea na ndugu ni laana tena laana kubwa sana tu, nataka nikusaidie mdogo wangu”
“Sijawahi kuwa na mahusiano nae”
“Basi ilimradi umekataa siwezi kukulazimisha”
Basi Erica aliagana na dada yake na kuondoka, aliwaza sana kuwa siri ya kutembea na Derick nani kaitoa, akawaza tena kuwa pengine ni Derick mwenyewe ila amewezaje wakati ni aibu kwa wote wawili, ila kwa upande wake aliona ni vyema kumkatalia dada yake kuwa hajawahi kuwa na mahusiano na Derick kabla.
 
SEHEMU YA 174


Kipindi hiki chuoni hakuwa na makubwa sana kwani wale waliokuwa wakimtisha wote walishamaliza chuo yani Tumaini na Dora walishamaliza kwahiyo alibaki na watu wachache tu, hata Derick alikuwa kashamaliza na walikuwa wakijiandaa kwaajili ya kwenda kwenye mahafali.
Ilikuwa kesho yake ndio siku ya mahafali na Erica alipanga siku hiyo ya kesho asifike kabisa chuoni, ila akakutana na Fetty,
“Erica umepotea sana”
“Fetty kumbe upo!! Nilijua ni mmoja kati ya waliomaliza chuo”
“Nipo ndio, ila pole nasikia kipindi cha likizo ulipata matatizo”
“Matatizo gani tena?”
“Si nasikia ulitekwa”
Akakumbuka kuwa dada yake alimwambia kwamba kupotea kwake aliulizwa na Derick kwahiyo kwa vyovyote vile ni Erick ndio kasema habari hiyo ila aliamua kuikana pale kwa Fetty kwani alijua habari bila kuikana ndio inazidi kutembea na kukuchafulia jina, kisha Fetty akamuuliza tena,
“Vipi kesho umeandaa zawadi gani za kuwapa watu wako wa karibu?”
“Hapana kesho siji”
“Kwanini?”
“Sina mtu yeyote wa karibu, sitakuja kesho”
“Ila ungekuja Erica, ungepata uzoefu wa mahafali yako mwakani”
“Fetty, mahafali yangu mwakani itakuwa ya kipekee kwahiyo sina haja ya kupata ujuzi”
Kisha akamuaga Fetty ila lile swala la kusema kuwa mahafali yake mwakani yatakuwa ya kipekee lilimuingia vizuri sana Fetty kwenye akili yake, ila alimuangalia tu Erica muda mwingine alimuona kama ni msichana mwenye malingo sana.
Erica aliondoka na kurudi kwao, usiku wa siku hiyo aliwasiliana sana na Rahim,
“Nataka kuja nchini Erica”
“Wow, nitafurahi sana”
“Ila sitasema nyumbani kama nimekuja nataka iwe siri ya mimi na wewe. Nyumbani nitaenda tu ila sitaki wajue kama narudi siku ipi”
“Karibu sana Rahim, itakuwa ni lini hiyo?”
“Nahisi baada ya miezi mitatu au mine”
“Ukija kipindi nimefunga chuo itakuwa vizuri sana”
“Basi utaniambia tarehe za kufunga chuo, ila nitakutumia pesa kidogo ya maandalizi ya kunipokea”
“Nitakwambia”
“Ila ungependa nikuletee zawadi gani?”
“Yoyote tu Rahim”
“Sema bhana”
“Basi niletee cheni, heleni na saa”
“Aaah sawa, nitakuletea na nimefurahi umetaja zawadi uitakayo”
Erica aliwasiliana kwa furaha sana na Rahim na alijiwekea asilimia mia moja kuwa Rahim ndio mume wake moja kwa moja kwani kitendo tu cha kutaka kurudi kwaajili yake ni kitendo cha tofauti, alilala akiwa na furaha sana.

Siku hiyo alitafutwa sana kwenye simu na Babuu ikabidi apokee ili asikie kuwa anataka kuongea nae nini,
“Nahitaji kuonana na wewe Erica”
“Njoo nyumbani kwetu”
Kwa kipindi hiko Erica hakutaka kuonana na mtu mbali na nyumbani kwao kwa kuhofia usalama wake, pia alikuwa akijilinda kwaajili ya mpenzi wake Rahim.
Babuu alifika nyumbani kwao na kumpigia simu ambapo Erica alitoka nje kwenda kuzungumza nae,
“Erica jana nilienda chuoni kwenu kwenye mahafali”
“Ulienda kufanya nini?”
“Na nilijua utakuwepo kumbe wala haupo, kuna ndugu yangu amemaliza chuo ndio nilikuwa pale kwenye mahafali yako. ILa nilikutana na Yule rafiki yako Dora dah habari aliyonipa sikuielewa”
Kwa muda huo Erica hakutaka kufahamu ni ndugu gani wa Babuu alikuwa kwenye mahafali ila alitamani kujua kuhusu habari alizopewa ni zile zile za siku zote au ni habari gani, akamuuliza na kumsikiliza kwa makini kuwa ni habari gani, akashangaa babuu akimpa zile habari ambazo zilizagaa chuo kuhusu yeye.
“Hizo habari ni za uongo Babuu”
“Hata mimi sijaziamini ila Erica, ningependa usafishe jina lako”
“Sasa nitalisafishaje na wenyewe washaamini hivyo?”
“Nilihusu nikusaidie kulisafisha”
“Kivipi? Hebu niambie utalisafishaje”
“Subiri utaona ila nitasafisha jina lako na hautokuwa tena na sifa mbaya”
“Haya nashukuru”
Aliongea ongea nae pale na kuagana nae, kisha yeye kurudi ndani kwao. Hakutaka kujua Babuu atatumia njia gani kusafisha jina lake kwani hata jina lake kuchafuliwa bado haikuwa tatizo sana kwake kwani aliamini kwasasa yupo mwanaume ampendaye na mwenye vigezo vyote.
 
SEHEMU YA 175



Kitendo cha Babuu kusema kuwa anataka kusafisha jina la Erica kwenye kile chuo kilifanya Babuu awe karibu sana na Erica huku akiwasiliana nae mara kwa mara bila kumwambia kuwa ni njia gani atazitumia kulisafisha jina lake.
Erica alipoona anakaribia kufunga chuo, alimtaarifu Rahim nae alimwambia tarehe atakayoenda kisha akamtumia pesa, alimtumia milioni moja kwaajili ya maandalizi ya kwenda kumpokea.
“Erica naomba unitafutie hoteli ya kufikia maana sitaki kufika nyumbani moja kwa moja, shida yangu nikuone wewe kwanza”
“Sawa Rahim nitafanya hivyo”
Siku ambayo Rahim alikuwa anafika, Erica aliaga kwao kuwa anaenda chuo mara moja kumbe alikuwa na yake ya kumpokea Rahim.
Aliondoka kwao na kwenda kutafuta kabisa hoteli ambayo Rahim angefikia kwasababu alishaambiwa kuwa atafute kabisa hoteli ya kufikia Rahim. Alipokodi mahali akaondoka na kwenda uwanja wa ndege sasa kwa lengo la kumpokea Rahim, wakati yupo ametulia akimsubiri Rahim akapigiwa simu na Babuu,
“Erica kuna mahali nakuona halafu nina shida na wewe”
“Shida gani?”
“Tuonane kwanza Erica, nina shida na wewe”
“Babuu jamani, tutaongea siku nyingine”
“Unajua nakuona, upo uwanja wa ndege”
Erica akaona ameonekana kweli, ikabidi tu amwambie amfate ili aongee nae, muda kidogo Babuu alifika, kwahiyo hakuwa mbali na pale kwakweli Erica alihisi kama akili inamruka vile kwani kabla hajaongea na Babuu, alipokea ujumbe toka kwa Rahim,
“Erica, hii ni namba yangu ya hapa, nishaingia nchini upo upande gani mpenzi wangu?”
Alihisi kuchanganyikiwa kabisa maana pale alisimama na Babuu halafu Babuu ana undugu na Rahim.

Erica akaona ameonekana kweli, ikabidi tu amwambie amfate ili aongee nae, muda kidogo Babuu alifika, kwahiyo hakuwa mbali na pale kwakweli Erica alihisi kama akili inamruka vile kwani kabla hajaongea na Babuu, alipokea ujumbe toka kwa Rahim,
“Erica, hii ni namba yangu ya hapa, nishaingia nchini upo upande gani mpenzi wangu?”
Alihisi kuchanganyikiwa kabisa maana pale alisimama na Babuu halafu Babuu ana undugu na Rahim.
Akili ikamcheza pale na kumwambia Babuu amsubirie pale kwani yeye anaenda uwani, Babuu alikubali na Erica akaondoka.
Simu yake ilikuwa ikiita sana na alikuwa akipigiwa simu na Rahim, sababu alikuwa kachanganyikiwa hata kupokea hakuweza, alitafuta gari ya kukodi na kupanda huku dereva akimuuliza kuwa anaenda wapi ila hata kumjibu hakumjibu kwani akili yake ilishapotea kabisa.
Muda kidogo akapokea ujumbe mwingine toka kwa Rahim,
“Mpenzi nimekutana na ndugu yangu ambaye sikutegemea kukutana nae kabisa kwa muda huu, uko wapi nikutambulishe tu maana nimemwambia asiseme popote nipo na shemeji yake”
Erica alisoma ule ujumbe na kuhisi akili kumruka kabisa.
Akili ikamcheza tena muda ule ule na kumwambia Yule dereva wa ile gari asogee yale mazingira ambayo Rahim na Babuu wamesimama, alipokuwa anawaona vizuri alimwambia dereva asimamishe kwanza gari kisha akachukua simu yake na kumpigia Babuu,
“Hellow Babuu nina shida huku uwani nakuomba mara moja”
“Ila kuna ndugu yangu nimekutana nae hapa, kuna mtu tunamsubiria au nije nae?”
“Usitake kunikera Babuu, nilishakwambia maswala ya kunijia na watu, wewe unajua nimekutwa na nini huku hadi uje na ndugu yako? Njoo mara moja bhana”
“Haya nakuja”
Babuu alionekana kumuaga Rahim na kuondoka, muda ule ule Erica hakutaka kupoteza muda alimwambia dereva asogeze lile gari hadi alipo Rahim, halafu akazima simu yake na kushuka ili kumshtua Rahim, kwakweli Rahim alifurahi sana na Erica hakutaka kupoteza nae muda kwani alipanda nae kwenye lile gari na kuondoka kuelekea hotelini ambako aliambiwa na Rahim kuwa amkodie hoteli. Muda wote huo Erica alikuwa amezima simu yake kwani hakutaka Babuu ampate hewani kabisa kwa muda huo.
 
Back
Top Bottom