Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #161
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA ALOBAINI
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA THERASINI NA TISA: maana ukiachilia polisi waliokuwepo pale na silaha zao pia kulikuwa na vijana wawili waliovalia kiraia, pamoja na piki piki yao mmoja ambae ni dereva akiwa amevaa kofia ngumu kichwani, huku mwingine akiwa amevalia suruali ya kitambaa viatu vyeusi na tishert aliyo ichomekea na mkononi akiwa ameshikilia kofia nyeusi ni wale wale ambao aliwaona siku ya tukio la Momadou, “kum…make, ni Kisonge, kumbe huyu mshenzi yupo pale MONUSCO kama mamluki” alijisemea Deus, huku anamtazama kijana yule wa kikongo aliekuwa anatoa maelekezo flani kwa polisi hawa wa serikali ya Congo. …..…..….endelea….
Deus hakutaka kujiuliza sana maana alisha rudi tena uchochoroni na kuaendelea kukimbia kuelekea upande ambao aliamini angeibukia moja kwa moja pale kwenye kituo cha mafuta cha MONUSCO, huku kwa mbali akisikia kelele na maongezi ya polisi serikali ya DRC waliokuwa wanaendelea kumsaka.
Deus ambae leo alikuwa amevalia nguo zake za kiraia anatoa simu yake na kuipiga namba ya Feix, ambayo inapokelewa mara moja, “hallow afande kuna msala huku” aliongea Deus kwa sauti ambayo hakika usingeamini kama alikuwa katika shida kubwa kama hii, ilikuwa ni sauti tulivu na ya taratibu, “kuna nini Deus?” aliuliza Felix kwa sauti iliyojawa na mshtuko mkubwa, “nimeingia kwenye mtego wa yule mfanya usafi, lakini nimefanikiwa kuwakimbia” alisema Deus ambae alikuwa katika mwendo mbwa yaani mbio, “ok! fanya unachoweza hakikisha unafika kambini ukiwa salama na gari liwe salama” alisema Felix na kukata simu, ni wazi alikuwa anaenda kufanya maandalizi ya ujio wa Deus ambae alikuwa anaamini kuwa akishalifikia gari basi lazima angefika kambini muda mfupi ujao.
Deus alikimbia kwa uharaka ndani ya chochoro ngeni za mtaa ule mpaka alipoibukia nyuma ya uzio mkubwa wa ukuta wa mawe, ambapo bila kuuliza alitambua kuwa alikuwa ameshalifikia eneo la kituo cha mafua cha MONUSCO.
Kwa tahadhari kubwa sana Deus aliiingia ndani ya uzio huo akitumia gate dogo kwa kuonyesha kitambulisho chake kwamba ni afisa wa UN, kijana wetu anafanikiwa kuingia mle ndani, ana elekea upade wa mbele wa majengo ya MONUSCO kule ambako aliacha gari lake anaona kuwa ni salama kwake analifwaa gari lake kwa haraka.
Alipolifikia na kuingia ndani ya gari akaliwasha na kuondoka kwa mwendo wa taratibu kulifwa lango la kutokea pale MONUSCO, usingedhania kuwa alikuwa katika matatizo makubwa, hata walinzi waliokuwepo pale getini walimfungulia bila shaka lolote.
Naam kijana wetu alipoingia barabarani, na kuikamata barabara ya mavivi akaongeza mwendo na kuanza kutembea kwa speed kali sana kuelekea upande wa kaskazini mwa mji wa ben, huku akiya over take magari mengine yaliyokuwa yanaelekea upande huo, huku kijana wetu akitafakari kitendo alichofanyiwa na kijana yule mkongo, yaani Kisonge, ambae kwa kumbu kumbu za Deus ni kwamba ukiachilia tukio la jaribio la utekaji nyara wa madoctorta, pia Deus alikuwa na uhakika kuwa huyu kijana wa kicongo, ambae amemwona leo kule panasonoc, ndie mtu aliemwona akipiga simu siku ile ya tukio la Momadou na ndie anaehusika kwa asilimia kubwa kuingizwa kwenye mtego.
Dakika saba baadae Deus alikuwa anaingia kwenye lango la eneo la MONUSCO, pale airport Mavivi ambako alimkuta major Felix na wale maafisa wengine, yaani Luten kanali na yule major mwingine, wakiwa wanamsubiri, nae akawasimulia kisa kizima kuanzia siku ya kwanza anakutana na Sonia na kumsaidia kumpeleka bibi yake hospital pamoja na kuwalipia mpaka kile kilichotokea leo hii, kupigiwa kelele za kwamba yeye ni mbakaji, “nenda katulie chumbani kwako” alisema luten kanal na Deus akaenda chumbani kwake na kujilaza kitandani, hofu ikiwa imetanda moyoni mwake, hata alipojaribu kuperuzi simu yake alishindwa hata kujibu sms za pacha wake, zaidi alianza kuwaza kile ambacho kitamtokea muda mchache ujao pengine kingevuruga kabisa malengo ya maisha yake.
Naam kwakifupi muda mfupi baadae, polisi walifika pale Mavivi wakimuhitaji askari toka Tanzania, Deus Frank Nyati anae tuhumiwa kwa ubakaji, iliwashangaza sana kusikia polisi wakitaja majina matatu ya kijana huyo wa kitanzania, ingekuwa vigumu sana kujitambulisha majina yote hayo kwa mschana anae sadikiwa kumbaka.
Polisi wale walihitaji kundoka na Deus, wampeleke kwenye mamlaka hiyo ya kiraia tayari kukabiliana na mashitaka yaliyokuwa yana mkabiri, hata hivyo MONUSCO ikishilikiana na wakina Major Felix, hawa kukubaliana na swala hilo na baada yake walihitaji kumpeleka wao wenyewe kituo cha polisi na walifanya hivyo, walimpeleka Deus kituo cha polisi wakiwa na ulinzi mkubwa wa jeshi la Tanzania na askari wa jeshi la Nepal, ambao ndio walikuwa na jukumu la Military Polisi yaani MP, pale MONUSCO.
Walifika kituo cha polisi, ambako walimkuta Sonia pia alikuwa analia muda wote kuugulia kubakwa na kijana wa kianzania kwa usimamizi wa major Felix, Deus aliandika maelezo yake pale kituo cha polisi ambao baaae walidai kuwa Deus akae mahabusu mpaka siku ya kwenda mahakamani, jambo ambalo lilipingwa vibaya na Felix, na kusema kuwa Deus ataenda kukaa katika mahabusu zilizopo chini ya UN.
Naam polisi wa Congo walikubariana na Felix, japo haikusaidia, maana Deus alichukuliwa na MP toka Nepal na kwenda kuifadhiwa kwenye maabusu yao, huku akinyang’anywa baadhi ya vitu vyake kama vile simu ya mkononi na viatu mkanda na vitu vingine ambavyo mfungwa hakuruhusiwa kuwa navyo.
Taarifa zilifika makao makuu ya MONUSCO, na wakaagiza kuwa kesi ya Deus iendeshwe katika mahakama ya kijeshi chini ya UN, na siyo mamlaka ya kiraia, siku tatu baadae kesi ikaanza kusikilizwa na shitaka likasomwa kwa mara ya kwanza katika mahakama ya kijeshi iliyoendeshwa kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za MONUSCO pale mavivi, Deus akisomewa kosa la ubakaji, kosa ambalo Deus alilikataa na kufanya mahakama ihailishe kesi mpaka siku inayofwata, huku ikiagizwa kufika kwa mashaidi siku inayofuata, wakati huo tayari taarifa zilikuwa zimesha fika nchini Tanzania katika makao makuu ya jeshi, hakika iliwasikitisha watu wengi sana waliomfahamu Deus, akiwepo kanal Kasuba japo wapo walioamini kuwa Deus amebaka kweli, siku ile ndiyo siku ambayo Deus aliweza kutumia simu yake kwa sekunde chache, hivyo aliwajulisha wazazi wake kile ambacho kilikuwa kimemtokea.
Ukweli mzee Frank Nyati hakuonyesha kushtuka, baada yake alicheka kidogo na kutoa tamko, “hayo ndiyo maisha mwanangu, kumbuka kuwa kila unapozidi kutenda wema ndivyo unavyo jiongezea maadui”.
Siku inayofuata Mashahidi walifika pale mavivi, wakiwepo polisi watatu, Sonia mwenyewe akiwa na bibi yake, wote wakiwa kama mashahidi, maana kesi kama hii katika mahakama ya kijeshi, haina mlalamikaji, unashitakiwa kutokana na vifungu vya sheria.
Upande wa mshatakiwa aliesindikizwa na MP, walikuwepo wakina major Felix, ambao walimsikiliza Deus akianza kuelezea jinsi ilivyokuwa pale alipokutana na mschana huyo na kumsaidia katika matibabu ya bibi yake na mwisho kuanza kumshawishi kingono, huku yeye Deus akikataa kushiriki tendo hilo, na hatimae Sonia kuamua kupiga kelele za kwamba anabakwa.
Baada ya maelezo hayo mwanasheria wa UN, aliekuwa upande wa mashitaka akamuuliza maswali kadhaa kijana wetu, ambae mengine aliyajibu vizuri na mengine alikwama, mfano kuna wakati alimwuliza hivi, “Deus Frank Nyati tayari uliambiwa mgonjwa ametoka hospital kwa maana amesha pona, sasa kwanini uliendelea kwenda nyumbani kwa Sonia au ulihitaji akulipe fadhila kwa msaada uliompatia?” hapo Deus akaanza kujitetea, “mheshimiwa, nililetewa taarifa na bwana Kisonge kuwa Sonia ameagiza niende haraka kwasababu bibi yake amezidiwa, hivyo anaitaji msaada wangu” alijibu Deus kwa sauti ile ile ambayo muda wote husikika kwa utulivu na upole, “umesema kuwa Sonia amekusingizia kubaka je unadhani ni kwanini mschana huyu amefanya hivyo?” aliuliza yule mwanasheria, “mpaka sasa siwezi kusema sababu ya yeye kufanya hivyo, inaweza kuwa alishawishiwa au alishawishika kutokana na tamaa zake” alijibu Deus wakati huo Sonia bibi yake na wale mashahidi wengine walikuwa wamekaa wanasikiliza kwa umakini mkubwa, Sonia uso ameuinamisha chini.
Maswali yakaendelea, “bwana Deus unataka kuiambia mahakama kuwa Sonia alikudanganya kuwa bibi yake ni Mgonjwa na kama ndiyo Sonia alikuwa na lengo gani?” aliuliza mwanasheria, “mheshimiwa nilidanganywa na lengo la kunidanganya, lilikuwa ni kuniingiza mtegoni” alijibu Deus ambae licha ya sauti yake kuwa ya upole lakini alionyesha kujiamini, nikuulize swali la mwisho, je huo msaada ulioutoa kwa familia ya Sonia ulikuwa chini ya mpango wa shirika gani, la UN, UNHCR, WHO, au?” hapo Deus akajikuta anatabasamu, “ni msaada binafsi mheshimiwa” alijibu Deus, “bwana Deus nadhani ulisoma vyema mkataba wa UN kwa MILROB! hivyo basi ulipokuwa unatoa msaada ulijuwa kuwa nikosa kufanya kazi nje ya mkataba wa UN?” aliuliza mwanasheria swali ambalo, Deus, hakuweza kulijibu. …..…..….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
SEHEMU YA ALOBAINI
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA THERASINI NA TISA: maana ukiachilia polisi waliokuwepo pale na silaha zao pia kulikuwa na vijana wawili waliovalia kiraia, pamoja na piki piki yao mmoja ambae ni dereva akiwa amevaa kofia ngumu kichwani, huku mwingine akiwa amevalia suruali ya kitambaa viatu vyeusi na tishert aliyo ichomekea na mkononi akiwa ameshikilia kofia nyeusi ni wale wale ambao aliwaona siku ya tukio la Momadou, “kum…make, ni Kisonge, kumbe huyu mshenzi yupo pale MONUSCO kama mamluki” alijisemea Deus, huku anamtazama kijana yule wa kikongo aliekuwa anatoa maelekezo flani kwa polisi hawa wa serikali ya Congo. …..…..….endelea….
Deus hakutaka kujiuliza sana maana alisha rudi tena uchochoroni na kuaendelea kukimbia kuelekea upande ambao aliamini angeibukia moja kwa moja pale kwenye kituo cha mafuta cha MONUSCO, huku kwa mbali akisikia kelele na maongezi ya polisi serikali ya DRC waliokuwa wanaendelea kumsaka.
Deus ambae leo alikuwa amevalia nguo zake za kiraia anatoa simu yake na kuipiga namba ya Feix, ambayo inapokelewa mara moja, “hallow afande kuna msala huku” aliongea Deus kwa sauti ambayo hakika usingeamini kama alikuwa katika shida kubwa kama hii, ilikuwa ni sauti tulivu na ya taratibu, “kuna nini Deus?” aliuliza Felix kwa sauti iliyojawa na mshtuko mkubwa, “nimeingia kwenye mtego wa yule mfanya usafi, lakini nimefanikiwa kuwakimbia” alisema Deus ambae alikuwa katika mwendo mbwa yaani mbio, “ok! fanya unachoweza hakikisha unafika kambini ukiwa salama na gari liwe salama” alisema Felix na kukata simu, ni wazi alikuwa anaenda kufanya maandalizi ya ujio wa Deus ambae alikuwa anaamini kuwa akishalifikia gari basi lazima angefika kambini muda mfupi ujao.
Deus alikimbia kwa uharaka ndani ya chochoro ngeni za mtaa ule mpaka alipoibukia nyuma ya uzio mkubwa wa ukuta wa mawe, ambapo bila kuuliza alitambua kuwa alikuwa ameshalifikia eneo la kituo cha mafua cha MONUSCO.
Kwa tahadhari kubwa sana Deus aliiingia ndani ya uzio huo akitumia gate dogo kwa kuonyesha kitambulisho chake kwamba ni afisa wa UN, kijana wetu anafanikiwa kuingia mle ndani, ana elekea upade wa mbele wa majengo ya MONUSCO kule ambako aliacha gari lake anaona kuwa ni salama kwake analifwaa gari lake kwa haraka.
Alipolifikia na kuingia ndani ya gari akaliwasha na kuondoka kwa mwendo wa taratibu kulifwa lango la kutokea pale MONUSCO, usingedhania kuwa alikuwa katika matatizo makubwa, hata walinzi waliokuwepo pale getini walimfungulia bila shaka lolote.
Naam kijana wetu alipoingia barabarani, na kuikamata barabara ya mavivi akaongeza mwendo na kuanza kutembea kwa speed kali sana kuelekea upande wa kaskazini mwa mji wa ben, huku akiya over take magari mengine yaliyokuwa yanaelekea upande huo, huku kijana wetu akitafakari kitendo alichofanyiwa na kijana yule mkongo, yaani Kisonge, ambae kwa kumbu kumbu za Deus ni kwamba ukiachilia tukio la jaribio la utekaji nyara wa madoctorta, pia Deus alikuwa na uhakika kuwa huyu kijana wa kicongo, ambae amemwona leo kule panasonoc, ndie mtu aliemwona akipiga simu siku ile ya tukio la Momadou na ndie anaehusika kwa asilimia kubwa kuingizwa kwenye mtego.
Dakika saba baadae Deus alikuwa anaingia kwenye lango la eneo la MONUSCO, pale airport Mavivi ambako alimkuta major Felix na wale maafisa wengine, yaani Luten kanali na yule major mwingine, wakiwa wanamsubiri, nae akawasimulia kisa kizima kuanzia siku ya kwanza anakutana na Sonia na kumsaidia kumpeleka bibi yake hospital pamoja na kuwalipia mpaka kile kilichotokea leo hii, kupigiwa kelele za kwamba yeye ni mbakaji, “nenda katulie chumbani kwako” alisema luten kanal na Deus akaenda chumbani kwake na kujilaza kitandani, hofu ikiwa imetanda moyoni mwake, hata alipojaribu kuperuzi simu yake alishindwa hata kujibu sms za pacha wake, zaidi alianza kuwaza kile ambacho kitamtokea muda mchache ujao pengine kingevuruga kabisa malengo ya maisha yake.
Naam kwakifupi muda mfupi baadae, polisi walifika pale Mavivi wakimuhitaji askari toka Tanzania, Deus Frank Nyati anae tuhumiwa kwa ubakaji, iliwashangaza sana kusikia polisi wakitaja majina matatu ya kijana huyo wa kitanzania, ingekuwa vigumu sana kujitambulisha majina yote hayo kwa mschana anae sadikiwa kumbaka.
Polisi wale walihitaji kundoka na Deus, wampeleke kwenye mamlaka hiyo ya kiraia tayari kukabiliana na mashitaka yaliyokuwa yana mkabiri, hata hivyo MONUSCO ikishilikiana na wakina Major Felix, hawa kukubaliana na swala hilo na baada yake walihitaji kumpeleka wao wenyewe kituo cha polisi na walifanya hivyo, walimpeleka Deus kituo cha polisi wakiwa na ulinzi mkubwa wa jeshi la Tanzania na askari wa jeshi la Nepal, ambao ndio walikuwa na jukumu la Military Polisi yaani MP, pale MONUSCO.
Walifika kituo cha polisi, ambako walimkuta Sonia pia alikuwa analia muda wote kuugulia kubakwa na kijana wa kianzania kwa usimamizi wa major Felix, Deus aliandika maelezo yake pale kituo cha polisi ambao baaae walidai kuwa Deus akae mahabusu mpaka siku ya kwenda mahakamani, jambo ambalo lilipingwa vibaya na Felix, na kusema kuwa Deus ataenda kukaa katika mahabusu zilizopo chini ya UN.
Naam polisi wa Congo walikubariana na Felix, japo haikusaidia, maana Deus alichukuliwa na MP toka Nepal na kwenda kuifadhiwa kwenye maabusu yao, huku akinyang’anywa baadhi ya vitu vyake kama vile simu ya mkononi na viatu mkanda na vitu vingine ambavyo mfungwa hakuruhusiwa kuwa navyo.
Taarifa zilifika makao makuu ya MONUSCO, na wakaagiza kuwa kesi ya Deus iendeshwe katika mahakama ya kijeshi chini ya UN, na siyo mamlaka ya kiraia, siku tatu baadae kesi ikaanza kusikilizwa na shitaka likasomwa kwa mara ya kwanza katika mahakama ya kijeshi iliyoendeshwa kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za MONUSCO pale mavivi, Deus akisomewa kosa la ubakaji, kosa ambalo Deus alilikataa na kufanya mahakama ihailishe kesi mpaka siku inayofwata, huku ikiagizwa kufika kwa mashaidi siku inayofuata, wakati huo tayari taarifa zilikuwa zimesha fika nchini Tanzania katika makao makuu ya jeshi, hakika iliwasikitisha watu wengi sana waliomfahamu Deus, akiwepo kanal Kasuba japo wapo walioamini kuwa Deus amebaka kweli, siku ile ndiyo siku ambayo Deus aliweza kutumia simu yake kwa sekunde chache, hivyo aliwajulisha wazazi wake kile ambacho kilikuwa kimemtokea.
Ukweli mzee Frank Nyati hakuonyesha kushtuka, baada yake alicheka kidogo na kutoa tamko, “hayo ndiyo maisha mwanangu, kumbuka kuwa kila unapozidi kutenda wema ndivyo unavyo jiongezea maadui”.
Siku inayofuata Mashahidi walifika pale mavivi, wakiwepo polisi watatu, Sonia mwenyewe akiwa na bibi yake, wote wakiwa kama mashahidi, maana kesi kama hii katika mahakama ya kijeshi, haina mlalamikaji, unashitakiwa kutokana na vifungu vya sheria.
Upande wa mshatakiwa aliesindikizwa na MP, walikuwepo wakina major Felix, ambao walimsikiliza Deus akianza kuelezea jinsi ilivyokuwa pale alipokutana na mschana huyo na kumsaidia katika matibabu ya bibi yake na mwisho kuanza kumshawishi kingono, huku yeye Deus akikataa kushiriki tendo hilo, na hatimae Sonia kuamua kupiga kelele za kwamba anabakwa.
Baada ya maelezo hayo mwanasheria wa UN, aliekuwa upande wa mashitaka akamuuliza maswali kadhaa kijana wetu, ambae mengine aliyajibu vizuri na mengine alikwama, mfano kuna wakati alimwuliza hivi, “Deus Frank Nyati tayari uliambiwa mgonjwa ametoka hospital kwa maana amesha pona, sasa kwanini uliendelea kwenda nyumbani kwa Sonia au ulihitaji akulipe fadhila kwa msaada uliompatia?” hapo Deus akaanza kujitetea, “mheshimiwa, nililetewa taarifa na bwana Kisonge kuwa Sonia ameagiza niende haraka kwasababu bibi yake amezidiwa, hivyo anaitaji msaada wangu” alijibu Deus kwa sauti ile ile ambayo muda wote husikika kwa utulivu na upole, “umesema kuwa Sonia amekusingizia kubaka je unadhani ni kwanini mschana huyu amefanya hivyo?” aliuliza yule mwanasheria, “mpaka sasa siwezi kusema sababu ya yeye kufanya hivyo, inaweza kuwa alishawishiwa au alishawishika kutokana na tamaa zake” alijibu Deus wakati huo Sonia bibi yake na wale mashahidi wengine walikuwa wamekaa wanasikiliza kwa umakini mkubwa, Sonia uso ameuinamisha chini.
Maswali yakaendelea, “bwana Deus unataka kuiambia mahakama kuwa Sonia alikudanganya kuwa bibi yake ni Mgonjwa na kama ndiyo Sonia alikuwa na lengo gani?” aliuliza mwanasheria, “mheshimiwa nilidanganywa na lengo la kunidanganya, lilikuwa ni kuniingiza mtegoni” alijibu Deus ambae licha ya sauti yake kuwa ya upole lakini alionyesha kujiamini, nikuulize swali la mwisho, je huo msaada ulioutoa kwa familia ya Sonia ulikuwa chini ya mpango wa shirika gani, la UN, UNHCR, WHO, au?” hapo Deus akajikuta anatabasamu, “ni msaada binafsi mheshimiwa” alijibu Deus, “bwana Deus nadhani ulisoma vyema mkataba wa UN kwa MILROB! hivyo basi ulipokuwa unatoa msaada ulijuwa kuwa nikosa kufanya kazi nje ya mkataba wa UN?” aliuliza mwanasheria swali ambalo, Deus, hakuweza kulijibu. …..…..….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums