Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #61
Musijar mzigo unakujaLikizo hii kaka.mwaga mzigo.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Musijar mzigo unakujaLikizo hii kaka.mwaga mzigo.
Kimoja cha mwisho 😅jaman eddy hata kimoja cha mwisho
Ndio jamanKimoja cha mwisho 😅
Bado shusha mzigo kaka.wakulaliaMushalala?
BadoooooMushalala?
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA ISHIRINI
MTUNZI : Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI NA TISA: lakini hakupata jibu, zaidi ya kuwaona wale wote watatu, wakimtazama kijana mdogo Deus, na wao wakamtazama, ‘eti dogo, mmetokaje ndani ya hii tren, tena mkwa hamja pata majeraha yoyote?” aliuliza yule mwanajeshi wa jeshi la ulinzi wenye cheo cha Canal, huku anamkazia macho Deus, ambae alikuwa tofauti na wale wengine, kwamaana akuonyesha dalili ya wasi wasi, wala taharuki ya ajali….…endelea….
“tuliruka tu, hakuna cha zaidi tulichotumia” alijibu Deus Frank, ambae kama ungemkuta pale usingedhania kama alikuwepo ndani ya ile tren, labda kule kuchafuka kwake ndio ungegundua kuwa alikuwa mmoja wa walionusulika toka kwenye ajali.
Kwa jibu hilo yule Kanali alievalia sare za kijeshi zile za kivita, alimtazama yule kijana toka juu mpaka chini, halafu akatazama Caroline, kabla hajawatazama wale wengine watatu, na kisha akarudisha macho yake tena usoni kijana Deus, “lakini wewe siyo mfanyakazi ndani ya hii tren?” aliuliza yule Kanali, huku anamkazia macho Deus, ambae alitabasamu kidogo, huku anakwepesha macho yake ya upole, “ndiyo mzee huyo na huyu mschana ni abilia waliokosa express, tukawapa lift, ila yeye ndie alietusaidia kuruka toka kwenye Tren” alisema yule dereva wa Tren kwa msisitizo, wakati huo tayari wanajeshi walioenda kusaka miili ya watu walioruka kule nyuma, walikuwa wanarudi huku wamebeba watu wawili pamoja na begi kubwa la mschana Caroline, naamini tutafahamu kwanini waliliacha.
Hapo wanajeshi wote pamoja na wale wa jeshi la ukoaji, wakamtazama Deus kwa mshangao, “kwa hiyo walioumia na kufa hukuwapa maelekezo, au hawakufata maelekezo yako, “aliuliza yule Kanal ambae kwenye shati lake, juu ya mfuko wa kifuani, upande wa kushoto kulikuwa na neno Tanzania, na upande wa kulia kulikuwa na neno JP KASUBA, huku mabegani mwake kukionekana nyota mbili chini ya ngao ya taifa, wengi huiita bibi na bwana, kushoto na kulia, “waliruka mapema, kabla hatuja elezana chakufanya” alisema Deus, kwa sauti yake tulivu.
Wakati maongezi yanaendelea, mara akaja askari wa jeshi la ulinzi, huku akiwa amevalia groves za kitabibu mikononi mwake, ilionyesha wazi kuwa ni muuguzi, alipofika alipiga salut na yule Kanali Kasuba akaitikia kwa salut, “afande tupo tayari kuondoka, kumwaisha yule majeruhi, amevuja damu nyingi sana” alisema yule askari mwenye alama ya yota mbili mabegani mwake, “ok! sawa wachukuwe na hawa wanne, huyu bado nina maongezi nae” alisema Kanal, pasipo kupepesa macho, huku anamtazama kijana Deus, kwa macho kama ya kutaka kubaki pamoja nae, na hapo mschana Caroline pia akamtazama Deus, ambae pia alikuwa anamtazama kwa macho ya tabasamu, “usijali mdogo wangu, tutaonana tu” alisema Deus kwa sauti tulivu, “usijari binti tangulia tu, yeye anakuja, tuaongea mambo ya kikazi” alisisitiza Kanali, safari hii kama vile anamwondoa wasi wasi Caroline, ambae alikubali kuongozana na yule askari pamoja na wale wafanyakazi wa TAZARA, mpaka kwenye gari la wagonjwa, ambako alilikuta begi lake.
Kanali Kasuba pamoja na askari wengine, wakiwa na Deus ambae pia alikuwa na begi lake dogo mgogoni, wakiwa wana wasindikiza kwa macho wakina Caroline, ambao walipolifikia gari, nikama walikuwa hawaamini kilicho watokea, kila mmoja kwa wakati wake aliweza kusimama na kugeuka kutazama kule alipokuwepo Deus, kisha kuingia kwenye gari.
Caroline yeye alivunja record, maana alipogeuka na kumazama Deus, akajikuta anapunga mkono, hata wakina Kasuba wasijuwe anapungiwa nani, “dogo punga mkono” alisema Kasuba akimlenga Deus, ambae alipunga mkono huku anatabasamu, na hapo kidogo Caroline akaachia kijitabasamu, kilicho ambana na simanzi, niwazi alihisi asingeweza kumwona tena kijana huyu, ambae amekuwa msaada mkubwa kwake, katika ajali hii.
Naam wakina Caroline waliingia garini, na gari likaondoka kuelekea mjini, na wakina Kasuba wakilisindikiza kwa macho mpaka lilipotoweka, “imeisha hiyo, niwazi umekuwa muhimu kwao, kiasi kwamba kila mmoja anahitaji muendelee kuwa wote mpaka mwisho wa safari yenu” alisema kanal Kasuba na wote wakacheka kidogo, huku Kasuba anamgeukia Deus, “dogo unaweza kutueleza ilikuwaje ukaweza kuwasaidia hao wote kutoka ndani ya tren?” aliuliza Kasuba, na wenzake wote wakatega masikio macho kumsikiliza kijana Deusi, ambae alianza kutoa maelezo mara moja.*******
Naaam ilikuwa hivi, baada ya kuwatuliza wale wafanyakazi wa TAZARA nao kuacha kila walicho kuwa wanakifanya na kumtazama Deus, huku Tren ikizidi kukaribia daraja, ndipo Deus, akamtazama yule dereva, “mzee kuna namna ya kupanda juu ya behewa?” aliuliza Deus, na yule dereva wa Tren akajibu haraka, “behewa hili hauwezi kupanda labda linalofwata, hilo lipowazi” Deus hakusubiri huyu mzee amalize kujibu, “twendeni haraka, kwenye hilo behewa tumekaribia daraja, alisema Deus, ambae kwa upande wake tayari alikuwa amesha vaa begi lake dogo mgongoni, maana ukiachilia nguo chache zilizo kuwepo, pia kulikuwa na vitu muhimu kwake, kama vile Fedha, vyeti vyake vya shule, na bastora ndogo, ya kisasa aina ya Walther P99, inayotumia risasi yenye mzingo wa mm 6, ambayo anaimiliki kinyume cha sheria, maana hakuwa na kibali cha kumiliki, japo siyo ya kufanyia maovu, hii alipewa na baba yake kwaajili tu, ya kuhakikisha anaitumia kukabiliana na lolote la unyang’anyi litakalo toke akiwa njiani na gari ambalo anaenda kulifwata.
Deus akamshika mkono Caroline ambae licha ya kuwaona wale wafanyakazi wa tren wanaelekea upande wa nyuma wa behewa lile fupi la wafanyakazi wa Tren, yeye alikuwa anamtazama Deus, “begi langu” alisema Caroline, na hapo Deus ambae licha ya kumshangaa mschana huyu kwa kukumbuka begi lake, katika hali ya hatari kama hii, lakini hakumsemesha chochote mschana huyu, zaidi ya kumwachia mkono, na kulishika lile begi kubwa na zito la mschana yule, kisha aka sogea mlangoni akafungua mlango na kulitupa lile begi, pasipo kuangalia lilipo dondokea, kisha akamfwata Caroline, na kumshika mkono kisha kuelekea kule ambako wengine walielekea, ambao sasa walikuwa wamesha fungua mlango na kutoka nje.
Nawalipotoka nje waliwakuta wale jamaa watatu wamesha panda juu ya behewa lenye mbao, na kumsubiri, Deus, ambae alimsaidia Caroline kupanda kwenye mbao za kwenye behewa, huku wale wengine wakimpokea kule juu, kisha Deus nae akapanda juu, ya behewa lile, wakati huo tayari kichwa cha Tren kilikuwa kimebakiza mita kama mia mbili na nusu kuingia darajani, daraja ambalo lilikuwa limesha sombwa na maji, jamani sikilizeni, kosa lolote litagharimu maisha yako au ulemavu wa kudumu, hivyo fanyeni kama niakavyo waeleza” alisema Deus huku anamshika mkono, Caroline, na kuanza kukimbia juu ya mbao, kurudi nyuma zaidi ya Tren, hata wale jamaa watatu pia wakakimbia kuwafwata, mpaka karibu na mwisho ambapo Deus alisimama, akiwa bado amemshika Caroline, nawao wakasimama.
“jamani hatuna muda wakupoteza, mtaruka juu kwa kuelekea nyuma pembeni kidogo ya usawa wa behewa, unapotuwa jilegeze kiasi, mme elewa?” alipiga kelele Deus, “ndiyo” japo walijibu kwa pamoja, lakini kiukweli zilikuwa sauti za chini, ambazo zilikosa matumaini, “haya kila mtu kwa wakati wake, kumbuka kosa moja unapoteza maisha” alisema Deus, na hapo watu hawa kama vile hawaja mwelewa Deus, wote wakamtazama, wakamtazama Deus kisha akamshika Caroline, na kunyanyua kama mtoto, kifuani kwake, kisha akapiga hatua tatu upande wa kulia wa behewa na kuruka juu, Caroline alijikuta akipiga ukelele mkubwa wa uoga, huku anafumba macho kwa uoga, huku akijikuta wakielea kwa sekunde kadhaa hewani, kabla hawaja tuwa chini na kwenye vidimbiwi vidogo vya maji pasipo kupata jeraha hata moja.
Na wale wengine lipoona hivyo, nao wakaruka kama alivyofanya Deus, japo walipata vimichubuko vidogo, wakati huo huo waliweza kuona kichwa cha tren kikiacha njia yake na kutumbukia mtoni, na mkia wake ukifwatia, “baada ya hapo ndio tuka rudi kwenda kuwaangalia wale walioruka mwanzo, pamoja na begi la yule mschana, ambalo tulilikosa, likaja kuonwa na hawa askari” alisema Deus, akimaliza kumweleza Kanali Kasuba.
Ukweli simulizi ilikuwa ni yakusisimua, siyo tu kwa Kanal Kasuba, ila pia kwa wengine wote waliokuwa wanasikiliza, “kijana kwanini unaficha utambulisho wako?” aliuliza Kanali Kasuba, huku anamtazama Deus machoni, lakini Deus ambae alikuwa anamtazama Kasuba, alionekana kutoa macho ya mshangao.
Naweza kuona kitamburisho chako?” aliuliza kanal huku anamtazama Deus, huku amenyoosha mkono tayari kupokea kitambulisho….…..#NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa jamii forums
Ongeza mkuuMushalala
InaendeleaImeisha kumbe