Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #121
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA THERLATHINI NA MBILI: alisema Deus, kwa sauti yake tulivu, ambae alinekana kuzidi kujiamini, “unaweza kuithibitishia tume hicho unacho kisema kwamba ulikuwa ni mpango wa makusudi?” aliuliza mmoja wa jumbe wale, “ndiyo niliyanasa mawasiliano ya mmoja wa waasi akipewa maelekezo kuwa waondoke haraka, gun ship za UN na Special Force wapo njiani wanakuja eneo la tukio” alijibu Deus na mwisho akaomba kuwakilisha ushahidi. …….endelea….
Na jopo lile likaridhia ombi la Deus Nyati, ambae aliweka ushahidi wa simu aliyoiokota eneo la tukio, ambayo baada ya kuchunguzwa ikabainika kuwa kuna ushirika baina ya baadhi ya askari walikosa uaminifu toka jeshi la FARDC na kudi la waasi wa IFD NALU, katika mpango wa utekaji nyara.
Hakuhojiwa Deus peke yake ila walihojiwa baadhi ya watu waliohusika na safari ile kwa namna moja au nyingine, wakiwemo wale madoctor watatu pamoja na watu walioiratibu ile safari, ambapo ilionekana Deus alikuwa na kila sababu ya kutumia silaha kuokoa maafisa wenzake wa UN, na dawa ambazo zilikuwa zinasafarishwa kwaajili ya wakazi wa Ituli, hivyo kijana huyo mpole na mtaratibu akaonekana kuwa alichukuwa maamuzi sahihi yaliyopo ndani ya sheria.
Uamuzi wa mwisho uliochukuliwa, ni afisa habari wa UN upande wa MONUSCO, kuongea na vyombo ya habari huku pia wakihojiwa madoctor walio okolewa toka matekani ilikuweza kuondoa propagander za kwamba askari wa UN ameuwa raia wa Congo, “lilikuwa tukio la kuhusisha waasi waliotumia makombora mazito kulipua gari la jeshi la serikali, wakatuto kwenye gari huku wakipania kutufanyia vitu vibaya, bahati tulikuwa na askari makini mwenye uwezo wa hali ya juu, akapambana mpaka akatuokoa” alisema mmoja, kati ya wale madoctor.
Hilo lilisaidia kidogo kupunguza tuhuma juu ya kijana Deus, na hata baada ya week mbili kupita, tayari alikuwa amesha sahaulika modomoni mwa watu na wanaharakati wa mchongo, hata maandamano yalikoma kabisa.
Tukio hilo lilimkumbusha mbali sana Frank Nyati, yaani baba yake Deus, ambae licha ya kukubali na kufurahia uwezo mkubwa alio uonyesha kijana wake Deus, lakini pia alikumbuka jinsi serikali ya #mbogo_land ilivyomgeuka na kumwita muasi katika nchi yake, ambayo aliipigania na kuitumikia kwa uadilifu mkubwa.********
Naaam juma mosi moja, mida ya saa mbili za usiku, mtaa wa Jiwe la mwezi, jina hilo lilipatikana kutokana na vipande vya mawe ambavyo viliwai kupatikana miaka ya zaman kwa wingi eneo hilo, miaka ya 1844, wakianini kuwa ni vipande vilivyo meguka toka kwenye mwezi, kutokana na unga’aavu wake, mawe ambayo baadae waligundua kuwa ni madini aina ya Almasi, yaani Diamond ambayo yalikuwa na thamani kubwa sana, na ndiyo sehemu ambayo hapo zamani ilikuwa ndiyo makazi ya mwenye, yaani mfalme kabla ya kuamishia pale GOLDEN EMPIRE, ambako hipo mpaka sasa, historia inasema kuwa kabla hawajafahamu thamani ya madini hayo, walianza kwa kuyatumia kama mapambo kwenye kuta za nyumba zao za udongo zilizo kuwa zina jengwa wakati huo, hasa nyumba za viongozi.
Ila kwa sasa mtaa huu uliotawaliwa na nyumba kumi za kifahari, zenye kilakitu, licha ya kwamba nchi hii, miji yake na vitongoji na mitaa vyote kuwa na viunga vizuri, barabara za lami na zege, lakini mtaa huu ulikaribiana kabisa na makazi ya kiongozi wa nchi, ya GORDEN EMPIRE, au kama wenyewe walivyo zowea kuita, Golden House, ungesema ni kipande cha ardhi au mtaa, ulio nyofolewa huko ulaya, na kuja kupachikwa hapa Mbogo land.
Ndani ya Jumba moja kubwa la kifahali, kati ya yale kumi, yaliyopo mtaani hapo walionekana mfalme wa zamani, King Eric wa pili, akiwa na mfalme wa sasa, yaani King Elvis wa kwanza, kwenye ukumbi wa maongezi wanaongea jambo flani, huku wakishushia kahawa safi inayopatika nchini hapo, “Elvis kiukweli mimi kama mimi, nilikuwa madarakani kama kimvuri tu, babu yako Eugen ndie aliekuwa akiniongoza kwa kiasi kikubwa, ndio maana hata yeye alipozeeka, mimi nikaamua kukuachia madaraka, sababu sikuwa na uwezo wa kuongoza peke yangu, hivyo sielewi chochote na sina uzoefu wa maswala hayo, ambayo kwa kiasi kikubwa niliacha kwa wahusika kama vile mkuu wa usalama wa taifa, na waziri wa ulinzi” alieleza King Eric wa pili, ambae umri wake ulikuwa ni kama miaka hamsini sasa.
Elvis aliekuwa anamsikiliza baba yake, akukubaria na maelezo ya baba yake, “lakini baba lazima unaweza kuwa ulipata hata historia, kama kuna jambo kama hilo liliwahi kutokea na kama lilitokea lilileta madhara gani au sababu ilikuwa nini” alisema Elvis, ambae alikuwa amefanana sana na baba yake, “tatizo ni moja Elvis, sikuwa madadisi wa matukio ya nyuma zaidi nilifwatilia historia ya nchi kwa ujumla, lakini naweza kukushauri, kama una pata muda basi pitia kumbu kumbu zilizoandikwa na wafalme waliopita, unaweza kupata chochote ambacho kita kusaidia, kuliko kumsumbua babu yako Eugen” alisema King Eric.maneno ambayo King Elvis aliyaona kama hayakuwa na msaada kwake, maana licha ya kuwa na tabia ya kusoma kumbu kumbu za wafalme walipita, lakini hakuwahi kuona maandishi yanayofanana na vitu kama hivyo.
Baada ya maongezi yaliyochukuwa lisaa lizima, king Elvi akaaga na kundoka zake, huku akiaidi kwenda kusoma zaidi kumbu kumbu hizo, lakini hakuwa tayari kushirikisha wasaidizi wake, hasa wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa #mbogo_land, maana alisha fanya hivyo miezi michache iliyopita, na akiwataka kwenda kuongea na askari ili kufahamu kuna tatizo gani ambalo linawafanya askari kutoroka jeshi, na kitengo cha usalama wa nchi na kazi za siri.*******
Yap! turudi nchini DRC, week nne toka kushindikana kwa jaribio la utekaji nyara, wa madoctor watatu wa WHO, ambalo liliratibiwa na kikundi cha waasi wa IDFNALU, hali ilikuwa imesha tulia, na nikama vile watu walikuwa wamesha sahau kuhusu, tukio hilo, japo MONUSCO walichukuwa tahadhari zaidi kuhusu maafisa wake, hasa wanapokuwa kwenye majukumu na matembezi binafsi, huku Jeshi la ulinzi la Tanzania na raia wake, wakijivunia kuwa na askari mwenye uwezo mkubwa katika mapigano.
Deus akiwa bado yupo kule Mavivi mkoa wa ben, akidhania tayari yupo salama hasa baada ya kuonekana kuwa hakuwa na hatia, kwa shambulizi alilo lifanya aliendelea na maisha yake akifanya majukumu yake vizuri, tayri alisha pata malipo yake ya mwezi wakwanza, kati ya miezi 12 aliyotakiwa kukaa nchini Congo chini ya UN, akiwa anamiliki zaidi ya dollar elfu alobaini na tano, kwa kipindi hicho ilikuwa dollar moja ungebadiri kwa tsh 1800 mpaka 1870, ikiwa ni sawa na dollar 1500 kwa siku, kwamaana hiyo kijana wetu ndoto yake ya kumiliki BWM, ilikuwa inakaribia kutimia, sababu kwa fedha ile aliyokuwa nayo kwa ule mwezi mmoja, ilikaribia million 82 za kitanzania.
Ilimpa moyo Deus wa kukamilisha malengo yake, akiwa na uhakika kuwa atanunua gari analohitaji napengine kujenga nyumba kubwa na mzuri sana, hata kama atachukuwa uamuzi wa kuoa basi atakuwa sahihi, hivyo kijana wetu alitumia wakati wake kupanga mambo yake, huku muda mwingi akiendelea kuwasiliana na mwanamke aliemwita Pacha, ambao urafiki wao ulikuwa unazidi kuongezeka kila kukicha.
Ratiba mpya ya Deus kwa sasa ilikuwa ni kuwapeleka wakubwa wake mjini Ben, kwenye ofisi ya mayor (meya) wa mkoa wa Ben, ambako walikuwa wanavikao vya week mbili na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo, ambapo Deus kila alipowa shusha wakubwa wake hao, alienda kwenye ofisi ndogo ya MONUSCO pale Ben na kujaza mafuta, kisha kurudi kwenye ofisi za mayor, na kuegesha gari lake kisha kuanza kutumiana sms na Pacha wake, “hivi mchoraji wangu bishara unafanya saa ngapi, mbona muda mwingi nakuona online?” siku moja mschana ambae Deus alimwita Pacha alimwuliza Deus, wakati wanachati mida ya saa nne hivi, Deus akiwa amekaa ndani ya gari nje ya Jengo la mayor, “sindhani kama biashara inanizuwia kuchat na mtu anaenifanya nisikie baridi chini ya jua kali” aliandika Deus na kutuma, kisha akasubiria jibu.
Ilichukuwa dakika mbili jibu likarudi, ambalo lilikuwa ni vikaragosi kicheko, halafu ikifwatiwa na sms nyingine, “halafu na demu wako atakuwa na kazi gani?” aliuliza mschana ambae Deus alimtambua kama mwanafuzi wa chuo, huko mbeya Tanzania, “wala usiwe na shaka siku nikipata mchumba, kitu cha kwanza nita mweleza kuhusu urafiki wetu” alijibu Deus ambae kiukweli Hakuwa anafahamu hata sura ya mwanamke huyo.
Sekunde chache baadae ukaingia ujumbe wa kikaragosi mchashangao, ikifwatia sms nyingine, “kwahiyo una mwanamke hapo ulipo?” aliuliza pacha, “labda wewe Pacha wangu, ila zaidi ya hapo hata rafiki wa karamu wakike sina” sms hii ilipotumwa, haikuchukuwa hata dakika ikaja sms yenye karagosi kicheko, na kabla haijapoa ikafwaa sms nyingine, “mchoraji wangu tukifunga chuo nitakuja dar nikuone” ile sms ilimfanya Deus atabasamu kidogo, kisha akatulia sekunde kadhaa akitafuta jibu, maana licha ya kuwasiliana na mschana huy kwa muda mrefu, lakini hakudhania kama atatoa wazo kama hilo.
“usijari Pacha, tuombe wote tuwe dar” aliandika Deus, kisha akaituma kwenda kwa Pacha, ambae akutumia muda mrefu kujibu, “unamaana gani, tuombe wote tuwe dar, kwani utasafari?” aliuliza Pacha, hapo Deus akajibu haraka, “huwa situlii sehemu moja, kuna wakati huwa nasafari kwenda Songea kwa wazazi” aliandika Deus na kuituma kwenda kwa Pacha wake wakuzaliwa tarehe moja.*******
Naam siku mbili baadae, mida ya saa mbili asubuhi, Deus aliwashusha wakina Major Felix, nje ya jengo la ofisi za Mayor na kuondoa gari kueleka kwenye mafuta, ambapo ni pembezoni mwa barabara iendayo mavivi, kilomita sita toka kwenye ofisi za mayor, muda aliotumia kuweka mafuta haukuzidi hata dakika kumi, maana gari lilikuwa na mafuta kiasi, hivyo alikuwa kama anajazia tu, na alipo maliza kujazia akaondoa gari kurudi kule kwenye ofisi za mayor, lakini wakati anaikamata njia panda ya Panasonic hotel, akamwona mschaa mmoja mdogo wa miaka kama kumi na saba hivi akiwa amemshika mkono mama mtu mzima alieonekana kuwa katika hali ya uchovu wa mwili ni wazi alikuwa amezidiwa na homa.
Deus alitaka kuwapita lakini roho yake ikasita kidogo na kuamua kusimamisha gari, akidhania kuwa anaweza kutoa hata msaada wa Fedha kwa mschana yule mdogo ili zimsaidie usafiri, pengine ingekuwa bora kama kijana wetu angesikiliza wazo lake la kwanza la kuwaacha wale watu wawili asio wafahamu, unadhani nini kilimtokea kijana wetu, ambae sasa tunamwona akifanya kazi za mipango ya hatari, …..…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
Usiku mwema nyoteeees
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA THERLATHINI NA MBILI: alisema Deus, kwa sauti yake tulivu, ambae alinekana kuzidi kujiamini, “unaweza kuithibitishia tume hicho unacho kisema kwamba ulikuwa ni mpango wa makusudi?” aliuliza mmoja wa jumbe wale, “ndiyo niliyanasa mawasiliano ya mmoja wa waasi akipewa maelekezo kuwa waondoke haraka, gun ship za UN na Special Force wapo njiani wanakuja eneo la tukio” alijibu Deus na mwisho akaomba kuwakilisha ushahidi. …….endelea….
Na jopo lile likaridhia ombi la Deus Nyati, ambae aliweka ushahidi wa simu aliyoiokota eneo la tukio, ambayo baada ya kuchunguzwa ikabainika kuwa kuna ushirika baina ya baadhi ya askari walikosa uaminifu toka jeshi la FARDC na kudi la waasi wa IFD NALU, katika mpango wa utekaji nyara.
Hakuhojiwa Deus peke yake ila walihojiwa baadhi ya watu waliohusika na safari ile kwa namna moja au nyingine, wakiwemo wale madoctor watatu pamoja na watu walioiratibu ile safari, ambapo ilionekana Deus alikuwa na kila sababu ya kutumia silaha kuokoa maafisa wenzake wa UN, na dawa ambazo zilikuwa zinasafarishwa kwaajili ya wakazi wa Ituli, hivyo kijana huyo mpole na mtaratibu akaonekana kuwa alichukuwa maamuzi sahihi yaliyopo ndani ya sheria.
Uamuzi wa mwisho uliochukuliwa, ni afisa habari wa UN upande wa MONUSCO, kuongea na vyombo ya habari huku pia wakihojiwa madoctor walio okolewa toka matekani ilikuweza kuondoa propagander za kwamba askari wa UN ameuwa raia wa Congo, “lilikuwa tukio la kuhusisha waasi waliotumia makombora mazito kulipua gari la jeshi la serikali, wakatuto kwenye gari huku wakipania kutufanyia vitu vibaya, bahati tulikuwa na askari makini mwenye uwezo wa hali ya juu, akapambana mpaka akatuokoa” alisema mmoja, kati ya wale madoctor.
Hilo lilisaidia kidogo kupunguza tuhuma juu ya kijana Deus, na hata baada ya week mbili kupita, tayari alikuwa amesha sahaulika modomoni mwa watu na wanaharakati wa mchongo, hata maandamano yalikoma kabisa.
Tukio hilo lilimkumbusha mbali sana Frank Nyati, yaani baba yake Deus, ambae licha ya kukubali na kufurahia uwezo mkubwa alio uonyesha kijana wake Deus, lakini pia alikumbuka jinsi serikali ya #mbogo_land ilivyomgeuka na kumwita muasi katika nchi yake, ambayo aliipigania na kuitumikia kwa uadilifu mkubwa.********
Naaam juma mosi moja, mida ya saa mbili za usiku, mtaa wa Jiwe la mwezi, jina hilo lilipatikana kutokana na vipande vya mawe ambavyo viliwai kupatikana miaka ya zaman kwa wingi eneo hilo, miaka ya 1844, wakianini kuwa ni vipande vilivyo meguka toka kwenye mwezi, kutokana na unga’aavu wake, mawe ambayo baadae waligundua kuwa ni madini aina ya Almasi, yaani Diamond ambayo yalikuwa na thamani kubwa sana, na ndiyo sehemu ambayo hapo zamani ilikuwa ndiyo makazi ya mwenye, yaani mfalme kabla ya kuamishia pale GOLDEN EMPIRE, ambako hipo mpaka sasa, historia inasema kuwa kabla hawajafahamu thamani ya madini hayo, walianza kwa kuyatumia kama mapambo kwenye kuta za nyumba zao za udongo zilizo kuwa zina jengwa wakati huo, hasa nyumba za viongozi.
Ila kwa sasa mtaa huu uliotawaliwa na nyumba kumi za kifahari, zenye kilakitu, licha ya kwamba nchi hii, miji yake na vitongoji na mitaa vyote kuwa na viunga vizuri, barabara za lami na zege, lakini mtaa huu ulikaribiana kabisa na makazi ya kiongozi wa nchi, ya GORDEN EMPIRE, au kama wenyewe walivyo zowea kuita, Golden House, ungesema ni kipande cha ardhi au mtaa, ulio nyofolewa huko ulaya, na kuja kupachikwa hapa Mbogo land.
Ndani ya Jumba moja kubwa la kifahali, kati ya yale kumi, yaliyopo mtaani hapo walionekana mfalme wa zamani, King Eric wa pili, akiwa na mfalme wa sasa, yaani King Elvis wa kwanza, kwenye ukumbi wa maongezi wanaongea jambo flani, huku wakishushia kahawa safi inayopatika nchini hapo, “Elvis kiukweli mimi kama mimi, nilikuwa madarakani kama kimvuri tu, babu yako Eugen ndie aliekuwa akiniongoza kwa kiasi kikubwa, ndio maana hata yeye alipozeeka, mimi nikaamua kukuachia madaraka, sababu sikuwa na uwezo wa kuongoza peke yangu, hivyo sielewi chochote na sina uzoefu wa maswala hayo, ambayo kwa kiasi kikubwa niliacha kwa wahusika kama vile mkuu wa usalama wa taifa, na waziri wa ulinzi” alieleza King Eric wa pili, ambae umri wake ulikuwa ni kama miaka hamsini sasa.
Elvis aliekuwa anamsikiliza baba yake, akukubaria na maelezo ya baba yake, “lakini baba lazima unaweza kuwa ulipata hata historia, kama kuna jambo kama hilo liliwahi kutokea na kama lilitokea lilileta madhara gani au sababu ilikuwa nini” alisema Elvis, ambae alikuwa amefanana sana na baba yake, “tatizo ni moja Elvis, sikuwa madadisi wa matukio ya nyuma zaidi nilifwatilia historia ya nchi kwa ujumla, lakini naweza kukushauri, kama una pata muda basi pitia kumbu kumbu zilizoandikwa na wafalme waliopita, unaweza kupata chochote ambacho kita kusaidia, kuliko kumsumbua babu yako Eugen” alisema King Eric.maneno ambayo King Elvis aliyaona kama hayakuwa na msaada kwake, maana licha ya kuwa na tabia ya kusoma kumbu kumbu za wafalme walipita, lakini hakuwahi kuona maandishi yanayofanana na vitu kama hivyo.
Baada ya maongezi yaliyochukuwa lisaa lizima, king Elvi akaaga na kundoka zake, huku akiaidi kwenda kusoma zaidi kumbu kumbu hizo, lakini hakuwa tayari kushirikisha wasaidizi wake, hasa wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa #mbogo_land, maana alisha fanya hivyo miezi michache iliyopita, na akiwataka kwenda kuongea na askari ili kufahamu kuna tatizo gani ambalo linawafanya askari kutoroka jeshi, na kitengo cha usalama wa nchi na kazi za siri.*******
Yap! turudi nchini DRC, week nne toka kushindikana kwa jaribio la utekaji nyara, wa madoctor watatu wa WHO, ambalo liliratibiwa na kikundi cha waasi wa IDFNALU, hali ilikuwa imesha tulia, na nikama vile watu walikuwa wamesha sahau kuhusu, tukio hilo, japo MONUSCO walichukuwa tahadhari zaidi kuhusu maafisa wake, hasa wanapokuwa kwenye majukumu na matembezi binafsi, huku Jeshi la ulinzi la Tanzania na raia wake, wakijivunia kuwa na askari mwenye uwezo mkubwa katika mapigano.
Deus akiwa bado yupo kule Mavivi mkoa wa ben, akidhania tayari yupo salama hasa baada ya kuonekana kuwa hakuwa na hatia, kwa shambulizi alilo lifanya aliendelea na maisha yake akifanya majukumu yake vizuri, tayri alisha pata malipo yake ya mwezi wakwanza, kati ya miezi 12 aliyotakiwa kukaa nchini Congo chini ya UN, akiwa anamiliki zaidi ya dollar elfu alobaini na tano, kwa kipindi hicho ilikuwa dollar moja ungebadiri kwa tsh 1800 mpaka 1870, ikiwa ni sawa na dollar 1500 kwa siku, kwamaana hiyo kijana wetu ndoto yake ya kumiliki BWM, ilikuwa inakaribia kutimia, sababu kwa fedha ile aliyokuwa nayo kwa ule mwezi mmoja, ilikaribia million 82 za kitanzania.
Ilimpa moyo Deus wa kukamilisha malengo yake, akiwa na uhakika kuwa atanunua gari analohitaji napengine kujenga nyumba kubwa na mzuri sana, hata kama atachukuwa uamuzi wa kuoa basi atakuwa sahihi, hivyo kijana wetu alitumia wakati wake kupanga mambo yake, huku muda mwingi akiendelea kuwasiliana na mwanamke aliemwita Pacha, ambao urafiki wao ulikuwa unazidi kuongezeka kila kukicha.
Ratiba mpya ya Deus kwa sasa ilikuwa ni kuwapeleka wakubwa wake mjini Ben, kwenye ofisi ya mayor (meya) wa mkoa wa Ben, ambako walikuwa wanavikao vya week mbili na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo, ambapo Deus kila alipowa shusha wakubwa wake hao, alienda kwenye ofisi ndogo ya MONUSCO pale Ben na kujaza mafuta, kisha kurudi kwenye ofisi za mayor, na kuegesha gari lake kisha kuanza kutumiana sms na Pacha wake, “hivi mchoraji wangu bishara unafanya saa ngapi, mbona muda mwingi nakuona online?” siku moja mschana ambae Deus alimwita Pacha alimwuliza Deus, wakati wanachati mida ya saa nne hivi, Deus akiwa amekaa ndani ya gari nje ya Jengo la mayor, “sindhani kama biashara inanizuwia kuchat na mtu anaenifanya nisikie baridi chini ya jua kali” aliandika Deus na kutuma, kisha akasubiria jibu.
Ilichukuwa dakika mbili jibu likarudi, ambalo lilikuwa ni vikaragosi kicheko, halafu ikifwatiwa na sms nyingine, “halafu na demu wako atakuwa na kazi gani?” aliuliza mschana ambae Deus alimtambua kama mwanafuzi wa chuo, huko mbeya Tanzania, “wala usiwe na shaka siku nikipata mchumba, kitu cha kwanza nita mweleza kuhusu urafiki wetu” alijibu Deus ambae kiukweli Hakuwa anafahamu hata sura ya mwanamke huyo.
Sekunde chache baadae ukaingia ujumbe wa kikaragosi mchashangao, ikifwatia sms nyingine, “kwahiyo una mwanamke hapo ulipo?” aliuliza pacha, “labda wewe Pacha wangu, ila zaidi ya hapo hata rafiki wa karamu wakike sina” sms hii ilipotumwa, haikuchukuwa hata dakika ikaja sms yenye karagosi kicheko, na kabla haijapoa ikafwaa sms nyingine, “mchoraji wangu tukifunga chuo nitakuja dar nikuone” ile sms ilimfanya Deus atabasamu kidogo, kisha akatulia sekunde kadhaa akitafuta jibu, maana licha ya kuwasiliana na mschana huy kwa muda mrefu, lakini hakudhania kama atatoa wazo kama hilo.
“usijari Pacha, tuombe wote tuwe dar” aliandika Deus, kisha akaituma kwenda kwa Pacha, ambae akutumia muda mrefu kujibu, “unamaana gani, tuombe wote tuwe dar, kwani utasafari?” aliuliza Pacha, hapo Deus akajibu haraka, “huwa situlii sehemu moja, kuna wakati huwa nasafari kwenda Songea kwa wazazi” aliandika Deus na kuituma kwenda kwa Pacha wake wakuzaliwa tarehe moja.*******
Naam siku mbili baadae, mida ya saa mbili asubuhi, Deus aliwashusha wakina Major Felix, nje ya jengo la ofisi za Mayor na kuondoa gari kueleka kwenye mafuta, ambapo ni pembezoni mwa barabara iendayo mavivi, kilomita sita toka kwenye ofisi za mayor, muda aliotumia kuweka mafuta haukuzidi hata dakika kumi, maana gari lilikuwa na mafuta kiasi, hivyo alikuwa kama anajazia tu, na alipo maliza kujazia akaondoa gari kurudi kule kwenye ofisi za mayor, lakini wakati anaikamata njia panda ya Panasonic hotel, akamwona mschaa mmoja mdogo wa miaka kama kumi na saba hivi akiwa amemshika mkono mama mtu mzima alieonekana kuwa katika hali ya uchovu wa mwili ni wazi alikuwa amezidiwa na homa.
Deus alitaka kuwapita lakini roho yake ikasita kidogo na kuamua kusimamisha gari, akidhania kuwa anaweza kutoa hata msaada wa Fedha kwa mschana yule mdogo ili zimsaidie usafiri, pengine ingekuwa bora kama kijana wetu angesikiliza wazo lake la kwanza la kuwaacha wale watu wawili asio wafahamu, unadhani nini kilimtokea kijana wetu, ambae sasa tunamwona akifanya kazi za mipango ya hatari, …..…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
Usiku mwema nyoteeees