Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #221
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA HAMSINI NA TATU
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI: Walikuwa wamechoka haswaa, walitulia dakika kadhaa wakihema kwa kumaliza mbio ndefu, kabla hawajashtuliwa na simu ya mezani toka mapokezi, ambayo ilipokelewa na Neela mwenyewe, ikiulizia kama wapo tayari kuletewa chakula, jambo lililo kubaliwa na Neela kwamba chakula kiletwe..endelea….
Baada ya hapo wakaingia bafuni kumalizia kuoga, kisha wakaenda kutulia pale kwenye kibaraza cha nje wakisubiri chakula kilicholetwa mara moja na wao kuendelea kula mpaka sisi tulipowakuta wakiwa hapa wakiendelea kuonek
ana aibu kwa kile walichokifanya kule ndani.******
Naam twendeni #Mbogo_land, moja kwa moja Golden House, ambapo tuna muona waziri wa ulinzi bwana Chitopelah akitoka nje ya jengo hilo ni wazi alikuwa amesha maliza kikao na mfalme, na moja kwa moja akaelekea kwenye maegesho ya magari ya wageni VVIP, ambao wengiwao ni mawaziri.
Lakini wakati anakaribia gari lake, simu yake ikaanza kuita akaitoa mfukoni na kuitazama, alipoona jina la mpigaji akatazama kushoto na kulia, aliporidhika kwamba alicho kitazama kipo katika hali inayo mruhusu kupokea simu akaipokea na kuiweka sikioni, “niambie Kadumya, kuna taarifa yoyote” aliuliza Chitopelah kwa sauti ya chini huku anaendelea kutembea kulifikia gari alililo likusudia, “ndiyo boss, tayari vijana wameshakabidhi mzigo, dhahabu kilo hamsini, kama ulivyoagiza shambulio la kwanza ni kilomita nne kabla ya kuingia Ndanda, itatengenezwa ajari, kisha vijana watachukuwa box na kuondoka nalo, bwana Tshen hatofahamu kama tumechukuwa sisi ataamini kuwa mzigo umeibiwa baada ya ajari” ilisikika sauti upande wapili wa simu, “mpango mzuri, tunachojari sisi ni kwamba, tayari ameshaweka fedha kwenye account yetu ya siri, itasaidia kuwapatia posho vijana, ila tuna jambo la kuongea jioni ya leo, naona mfalme ameanza kutia mashaka juu ya utoro wa askari” alisema Chitopela kwa sauti ya chini.
“vipi kuhusu mpango wapili wa kurudisha mzigo” aliuliza Kadumya, “ufanyike kama tulivyopanga, wasiliana na vijana wa dar es salaam, wahakikishe mzigo haupandi ndege, kisha wakati wanahangaika kutafuta njia nyingine ya kusafirisha, waupore na kuurudisha mikononi mwetu, maana tukiupoteza itakuwa vigumu kupata mzigo kama huo, kwa sasa uthibiti ni mkubwa sana wa madini toka hapa nchini” alisema Chitopela, ambae tayari alisha lifikia gari alilokuwa analifuata na kukata simu, kisha akaingia ndani ya gari lile kisha gari likaondoka, wakipisana na gari moja aina ya land lover Puma, lenye rangi ya kijani, lenye namba 2008MLA 6202 , mali ya jeshi la #mboogo_land, ambalo lilikuwa linaingia pale Golden House huku ndani likiwa na watu watatu waliovalia nguo za kijeshi maalumu kwaajili ya vita, yaani vazi la vita, kama wazungu wanavyoita combati dress, huku mmoja kati yao aliekaa seat ya mbele kushoto, akionekana kuwa na cheo cha major general, na kwenye ukosi wake (kola), vikionekana vialama vyekundu, alionekana kuwa ndie mkubwa wao.
Naam gari liliingia kwenye maegesho ya VVIP, nakusimama pale pale lilipotoka gari la waziri wa ulinzi, Dickson Chitopelah, kisha akashuka yule major gen, ambae kwa muonekano ni mtu ambae alijaaliwa umbo na mwonekno wa kijeshi, ukiachilia misuri ya mikono iliyoonekana vyema baada ya kukunja shati lake la kombati, pia alikuwa mrefu mwenye kifua kipana, mweusi alie valia miwani meusi ya jua na kofia nyeusi kichwani mwake, ikiwa ni ishara ya askari wa kikosi cha mizinga mikubwa, mfano Tank yani vifaru mizinga mikubwa kama vile D 30 na mingineyo, pia BM -12 Grad, ikiwa ni silaha toka Urusi, yenyewe inayoitwa Boyevaya Machina, na pia hutumiwa na askari wapelelezi wa kivita, Amoured Reccenasence.
Ambae alianza kutembea kwa mwendo wa haraka kuelekea kwenye lango la kuingilia kwenye jengo ilikuwa la kipekee lenye ofisi za mfalme, ndani ya makazi ya mfalme Elvis wa kwanza, huku akionekana kupendeza kwa nembo ya dhahabu, iliyoonyesha picha ya mwewe, ikimaanisha ni kiumbe ambacho hufanya uchunguzi mkali kwenye mawindo yake kabla ya kufanya uvamizi, lilokaa juu ya mfuko wa kulia wa shati lake chini ya jina lake, lililoonyesha kuwa alikuwa ni AR kwa maana ya kwamba Amour Racce.
Huyu anaitwa Major Gen Sixmond Mbedo, mkuu wa kitego cha upelelezi kivita, ambae siyo tu kukubalika kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kupanga na kufanikisha uchunguzi wa ndani na nje ya nchi, pia alikuwa na Elimu kubwa sana ya fani hiyo ya uchunguzi wa kivita, kiasi kuaminiwa na king Elvis, hata kupewa kibari cha kuingia kwa mfalme mara kwa mara anapokuwa na taarifa muhimu.
Dakika tano baadae tayari major Gen Sixmund, alikuwa amesha ruhusiwa kuingia ndani ya ofisi kubwa ya mfalme Elvis wa kwanza, aliemkuta anamsubiri, baada ya kupewa taarifa na watu wa mapokezi na baada ya salamu zote za heshima, ndipo major Gen Sixmund akaeleza kilicho mleta “mtukufu mfalme, hii ni taarifa nyeti sana,
toka kwa wachunguzi wa mipakani na maeneo ya jirani” alisema Gen Sixmund, kwa kituo, “endelea, nakusikiliza Gen” alisema mfalme Elvis kwa sauti tulivu, “mfalme, wachunguzi wetu wamegundua uwepo wasiri wa kundi la Uhuru kwa Umwagaji Damu, yaani UMD, kikundi ambacho kilidhaniwa kimesha tokomezwa mwaka 1992, na lengo lao ni kufanya mapinduzi ya serikali yako tukufu” alisema Gen Sixmund, akionyesha kuhuzunishwana taarifa zile alizo zileta.
Kama Six alihuzunishwa na taarifa aliyoileta yeye mwenyewe basi ilikuwaje kwa mfalme Elvis, imekuwaje hilo kundi likarudi tena hata baada ya operation kubwa iliyofanyika miaka hiyo ya tisini?” aliuliza king Elvis kwa mshtuko mkubwa sana, “mtukufu mfalme, kundi hilo lililoanzishwa mwanzoni mwa miaka ya tisini, na kutoweka ghafla mwaka 1992, lilizusha wimbi kubwa la usaliti ndani ya serikali ya mfalme Eugen, ndipo serikali ikitumia kitengo cha MLSA, ilianzisha msako mkali wa wasaliti wote waliojificha serikalini, na kuwaangamiza kwa siri wao na familia zao” ,alieleza Gen Sixmund, kabla king Elvis hajamkatiza, “Gen, ni kwanini familia zao zilihusishwa na nani alitoa wazo hilo?” aliuliza King Elvis, ambae alionekana kusikitishwa na kitendo kile.
Hapo Gen Sixmund akaeleza kilicho tokea, “mtukufu mfalme, ukweli jambo hilo lilimshangaza kila mmoja, hata baadhi ya mataifa makubwa yalilipigia kelele swala hilo, lakini mfalme alikanusha vibaya na kuzuia waangalizi wakijeshi, japo wengi tunaamini kuwa mpango ule uliokuwa chini ya bwana Chitopela ulisaidia, lakini bado wakosoaji walisema kuwa wengi waliuwawa kimakosa na mbaya zaidi walikuwa ni viungi muhimu serikalini” alieleza Sixmund, “sasa Gen, ushauri wako ni upi” na kikundi hicho kipo wapi?” aliuliza mfalme, kwa maana unapotoa report unatakiwa kutoa ushauri.
Hapo Sixmund akatulia kidogo na kujiweka sawa, kwa maana alitakiwa atoe ushauri ambao ungekuwa na faida kubwa kwa mfalme na serikali yake, “mtukufu mfalme, bado kikundi hakijulikani, kipo sehemu gani, kwa maana hizi ni taarifa za awali, lakini sehemu ambayo wanakaa na kuratibu mambo yao inasemekana ni dar es salaam Tanzania, ambako ndio makazi ya viongozi wao, ushauri wangu mtukufu mfalme ni kwamba, nitateuwa mtu ambae anaweza kusimamia kikundi kidogo cha jeshi cha uchunguzi toka ndani ya jeshi letu la ulinzi, kitengo cha AR, ambacho kitachunguza kwa siri, mienendo na mipango ya UMD, ili tujuwe namna ya kuwadhibiti” alisema Sixmund, “sawa kibari kimetolewa, teuwa kikundi na msimamizi, lete bajeti yako, kwaajili ya kikundi, nahitaji taarifa za mara kwa mara kujuwa kila kinachoendelea” alisema mfalme Elvis, kabla ya kuagana na Sixmund, ambae aliondoka zake na kwenda kuandaa kikundi hicho cha siri, ndani ya kitengo chake cha AR.*******
Kampala Uganda, Hotel Ajun Serasie, wakati Neela na Deus wanaendelea kula, huku Neela akionekana wazi kuzidi kujawa na hisia za mapenzi, mara ghafla Neela akasogeza mkono wake na kuushika mkono wa Deus, kisha akamtazama kwa macho tulivu yenye hisia kali za mapenzi, “Deus nilidhania hii inaweza kuwa ishara ya neno asante, maana mwili wangu huwa siutoi kwaajili ya burudani kwa mtu, niliutoa mara chache kwa mwanaume aliesema atakuwa mume wangu, ni kutoka Tanzania, nilikutana nae wakati nasoma chuo pale muhimbili, akakosa uvumulivu na kunisaliti ndio maana nilikuchukia siku ya kwanza tulipokutana, niliona kuwa wanaume toka Tanzania sio waaminifu, nikaamua kukupa kama asante kwa kuniokoa toka kwenye mikono ya wale majambazi washenzi, lakini nimegundua kuwa, nilichokipata kwako ni zaidi ya kile nilichokupatia, hakika bado nina deni kwako” alisema Neela na kumfanya.
Deus alitabasamu kidogo, kisha akaongea kwa sauti tulivu iliyojaa mahaba, “hapo mwanzo sikuwahi kujaribu mapenzi, ila nimeshangazwa na kile nilichokiona kwako, sikutegemea kama mapenzi ni matamu hivi, umekuwa mwalimu wangu mzuri sana” alisema Deus, huku tabasamu likiendelea kutawala usoni mwake, “wewe umenifanya niyafanye yote ulio yaona, japo niliwahi kushiriki mapenzi, lakini Deus, leo ndio nimefanya mapenzi kiukweli, yaani kamavile kulikuwa na mwalimu pembeni yetu, yaani kama mwanaume wangu wa zamani angepata kuniona wakati ule, angeshangaa sana” alisema Neela huku uso wake ukijawa na tabasamu lililojaa aibu ya kike na kumalizia kwa kicheko cha chini, huku anakwepesha macho yake yasitazamane na macho ya Deus.
Wakati wanaongea hili na lile, mara simu ya Neela ikaanza kuita, wote wakaitazaa na kuona jina la mpigaji likiwa limeandikwa BABA, Neela akaipokea haraka na kuiweka sikioni, kisha akaanza kuongea kwa lugha ambayo Deus hakuielewa, mpaka walipomaliza na kukata simu, “alikuwa baba yangu, yupo na mama wanaondoka Ethiopia sasa kwa ndege binafsi, wanakuja kukuona mwanaume ulieyakoa maisha yangu, nilikuambia mwanzo kuna watu wanahitaji kukuona” alisema Neela, kitu ambacho kilimshangaza sana, Deus, “kwanini lakini mbona ni kitu cha kawaida tu, kwanini wazazi wako wanakuja toka Ethiopia?” aliuliza kwa mshangao Deus na kumfanya Neela acheke kiogo, kisha kuanza kumueleza jambo alisilolijuwa kuhusu yeye na familia yake.*******
Naam Gari aina ya BMW lilioekana likikatiza kwenye barabara ya tunduru masasi, kuelekea upande wa mashariki, yaani kwenye mji wa masasi uliopo mkoa wa mtwara kwa speed kari sana ya kilomita mia moja themanini kwa saa, na sasa lilikuwa limebakiza kilomita chache sana kuingia masasi mjini.
Ndani ya gari hilo anaonekana mtu mmoja tu, ambae ndie dereva, tena ni mschana mrembo, mwenye umri kati ya miaka 24 au 25 hakika ingekushangaza sana, kwa mschana mdogo kama huyu kuendesha gari kwa speed kama hii, gari lilikuwa la kisasa, ambalo lina mambo mengi sana, ukiachia seat zake kuwa nzuri zenye kustarehesha msafiri, pia screen dogo ya video kila seat, huku dash board yake yenye mambo mengi sana, ikizidi kueleza kuwa iligari aina BMW 7, sio la kawaida, kuanzia speed yake ya mwisho kuwa 280, pia vitufe vingi vya kuongozea gari, pamoja na kioo kiogo chenye ramani ya sehemu anayoenda ikionyesha kilomita na hali ya hewa.
Naam wakati mschana huyo mrembo wa sura na umbo alikuwa anapunguza mwendo kuingia mjini masasi mara simu yake ikaita, nae akabiofya kitufe flani kwenye dash board ya gari lake la kisasa, sehemu ya kioo cha video ndogo pale mbele, ambapo kuna jina la mpigaji wasimu lilionekana limeandikwa Boss Atshen na kuanza kuongea. “naam boss, ndio naingia masasi sasa” alisema yule mschana, mrembo, ambae hata sauti yake ni nzuri, “sikia Sheba, ramani inaonyesha mbele yako kuna njia panda, barabara tatu za lami, mbele kulia na hiyo unayotoka, na moja ya kushoto ni ya vumbi, ifuate hiyo sina uhakika na hawa washenzi, wanaweza kubadili mchezo muda wowote” ilisikika sauti toka kwenye ile screen na ile kutazama vizuri tayari alikuwa anaivuka ile njia panda, hivyo akapunguza mwendo zaidi na kuingia kwenye kituo cha mafuta kilichopo pembezo mwa njia panda, upane wa kushoto mtu yeyote angejuwa kuwa gari hili linaingia kuweka mafuta, lakini haikuwa hivyo, lilipitiliza moja kwa moja mpaka njia ya kutokea na kuingia kwenye ile barabara aliyo elekezwa. ..…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
SEHEMU YA HAMSINI NA TATU
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI: Walikuwa wamechoka haswaa, walitulia dakika kadhaa wakihema kwa kumaliza mbio ndefu, kabla hawajashtuliwa na simu ya mezani toka mapokezi, ambayo ilipokelewa na Neela mwenyewe, ikiulizia kama wapo tayari kuletewa chakula, jambo lililo kubaliwa na Neela kwamba chakula kiletwe..endelea….
Baada ya hapo wakaingia bafuni kumalizia kuoga, kisha wakaenda kutulia pale kwenye kibaraza cha nje wakisubiri chakula kilicholetwa mara moja na wao kuendelea kula mpaka sisi tulipowakuta wakiwa hapa wakiendelea kuonek
ana aibu kwa kile walichokifanya kule ndani.******
Naam twendeni #Mbogo_land, moja kwa moja Golden House, ambapo tuna muona waziri wa ulinzi bwana Chitopelah akitoka nje ya jengo hilo ni wazi alikuwa amesha maliza kikao na mfalme, na moja kwa moja akaelekea kwenye maegesho ya magari ya wageni VVIP, ambao wengiwao ni mawaziri.
Lakini wakati anakaribia gari lake, simu yake ikaanza kuita akaitoa mfukoni na kuitazama, alipoona jina la mpigaji akatazama kushoto na kulia, aliporidhika kwamba alicho kitazama kipo katika hali inayo mruhusu kupokea simu akaipokea na kuiweka sikioni, “niambie Kadumya, kuna taarifa yoyote” aliuliza Chitopelah kwa sauti ya chini huku anaendelea kutembea kulifikia gari alililo likusudia, “ndiyo boss, tayari vijana wameshakabidhi mzigo, dhahabu kilo hamsini, kama ulivyoagiza shambulio la kwanza ni kilomita nne kabla ya kuingia Ndanda, itatengenezwa ajari, kisha vijana watachukuwa box na kuondoka nalo, bwana Tshen hatofahamu kama tumechukuwa sisi ataamini kuwa mzigo umeibiwa baada ya ajari” ilisikika sauti upande wapili wa simu, “mpango mzuri, tunachojari sisi ni kwamba, tayari ameshaweka fedha kwenye account yetu ya siri, itasaidia kuwapatia posho vijana, ila tuna jambo la kuongea jioni ya leo, naona mfalme ameanza kutia mashaka juu ya utoro wa askari” alisema Chitopela kwa sauti ya chini.
“vipi kuhusu mpango wapili wa kurudisha mzigo” aliuliza Kadumya, “ufanyike kama tulivyopanga, wasiliana na vijana wa dar es salaam, wahakikishe mzigo haupandi ndege, kisha wakati wanahangaika kutafuta njia nyingine ya kusafirisha, waupore na kuurudisha mikononi mwetu, maana tukiupoteza itakuwa vigumu kupata mzigo kama huo, kwa sasa uthibiti ni mkubwa sana wa madini toka hapa nchini” alisema Chitopela, ambae tayari alisha lifikia gari alilokuwa analifuata na kukata simu, kisha akaingia ndani ya gari lile kisha gari likaondoka, wakipisana na gari moja aina ya land lover Puma, lenye rangi ya kijani, lenye namba 2008MLA 6202 , mali ya jeshi la #mboogo_land, ambalo lilikuwa linaingia pale Golden House huku ndani likiwa na watu watatu waliovalia nguo za kijeshi maalumu kwaajili ya vita, yaani vazi la vita, kama wazungu wanavyoita combati dress, huku mmoja kati yao aliekaa seat ya mbele kushoto, akionekana kuwa na cheo cha major general, na kwenye ukosi wake (kola), vikionekana vialama vyekundu, alionekana kuwa ndie mkubwa wao.
Naam gari liliingia kwenye maegesho ya VVIP, nakusimama pale pale lilipotoka gari la waziri wa ulinzi, Dickson Chitopelah, kisha akashuka yule major gen, ambae kwa muonekano ni mtu ambae alijaaliwa umbo na mwonekno wa kijeshi, ukiachilia misuri ya mikono iliyoonekana vyema baada ya kukunja shati lake la kombati, pia alikuwa mrefu mwenye kifua kipana, mweusi alie valia miwani meusi ya jua na kofia nyeusi kichwani mwake, ikiwa ni ishara ya askari wa kikosi cha mizinga mikubwa, mfano Tank yani vifaru mizinga mikubwa kama vile D 30 na mingineyo, pia BM -12 Grad, ikiwa ni silaha toka Urusi, yenyewe inayoitwa Boyevaya Machina, na pia hutumiwa na askari wapelelezi wa kivita, Amoured Reccenasence.
Ambae alianza kutembea kwa mwendo wa haraka kuelekea kwenye lango la kuingilia kwenye jengo ilikuwa la kipekee lenye ofisi za mfalme, ndani ya makazi ya mfalme Elvis wa kwanza, huku akionekana kupendeza kwa nembo ya dhahabu, iliyoonyesha picha ya mwewe, ikimaanisha ni kiumbe ambacho hufanya uchunguzi mkali kwenye mawindo yake kabla ya kufanya uvamizi, lilokaa juu ya mfuko wa kulia wa shati lake chini ya jina lake, lililoonyesha kuwa alikuwa ni AR kwa maana ya kwamba Amour Racce.
Huyu anaitwa Major Gen Sixmond Mbedo, mkuu wa kitego cha upelelezi kivita, ambae siyo tu kukubalika kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kupanga na kufanikisha uchunguzi wa ndani na nje ya nchi, pia alikuwa na Elimu kubwa sana ya fani hiyo ya uchunguzi wa kivita, kiasi kuaminiwa na king Elvis, hata kupewa kibari cha kuingia kwa mfalme mara kwa mara anapokuwa na taarifa muhimu.
Dakika tano baadae tayari major Gen Sixmund, alikuwa amesha ruhusiwa kuingia ndani ya ofisi kubwa ya mfalme Elvis wa kwanza, aliemkuta anamsubiri, baada ya kupewa taarifa na watu wa mapokezi na baada ya salamu zote za heshima, ndipo major Gen Sixmund akaeleza kilicho mleta “mtukufu mfalme, hii ni taarifa nyeti sana,
toka kwa wachunguzi wa mipakani na maeneo ya jirani” alisema Gen Sixmund, kwa kituo, “endelea, nakusikiliza Gen” alisema mfalme Elvis kwa sauti tulivu, “mfalme, wachunguzi wetu wamegundua uwepo wasiri wa kundi la Uhuru kwa Umwagaji Damu, yaani UMD, kikundi ambacho kilidhaniwa kimesha tokomezwa mwaka 1992, na lengo lao ni kufanya mapinduzi ya serikali yako tukufu” alisema Gen Sixmund, akionyesha kuhuzunishwana taarifa zile alizo zileta.
Kama Six alihuzunishwa na taarifa aliyoileta yeye mwenyewe basi ilikuwaje kwa mfalme Elvis, imekuwaje hilo kundi likarudi tena hata baada ya operation kubwa iliyofanyika miaka hiyo ya tisini?” aliuliza king Elvis kwa mshtuko mkubwa sana, “mtukufu mfalme, kundi hilo lililoanzishwa mwanzoni mwa miaka ya tisini, na kutoweka ghafla mwaka 1992, lilizusha wimbi kubwa la usaliti ndani ya serikali ya mfalme Eugen, ndipo serikali ikitumia kitengo cha MLSA, ilianzisha msako mkali wa wasaliti wote waliojificha serikalini, na kuwaangamiza kwa siri wao na familia zao” ,alieleza Gen Sixmund, kabla king Elvis hajamkatiza, “Gen, ni kwanini familia zao zilihusishwa na nani alitoa wazo hilo?” aliuliza King Elvis, ambae alionekana kusikitishwa na kitendo kile.
Hapo Gen Sixmund akaeleza kilicho tokea, “mtukufu mfalme, ukweli jambo hilo lilimshangaza kila mmoja, hata baadhi ya mataifa makubwa yalilipigia kelele swala hilo, lakini mfalme alikanusha vibaya na kuzuia waangalizi wakijeshi, japo wengi tunaamini kuwa mpango ule uliokuwa chini ya bwana Chitopela ulisaidia, lakini bado wakosoaji walisema kuwa wengi waliuwawa kimakosa na mbaya zaidi walikuwa ni viungi muhimu serikalini” alieleza Sixmund, “sasa Gen, ushauri wako ni upi” na kikundi hicho kipo wapi?” aliuliza mfalme, kwa maana unapotoa report unatakiwa kutoa ushauri.
Hapo Sixmund akatulia kidogo na kujiweka sawa, kwa maana alitakiwa atoe ushauri ambao ungekuwa na faida kubwa kwa mfalme na serikali yake, “mtukufu mfalme, bado kikundi hakijulikani, kipo sehemu gani, kwa maana hizi ni taarifa za awali, lakini sehemu ambayo wanakaa na kuratibu mambo yao inasemekana ni dar es salaam Tanzania, ambako ndio makazi ya viongozi wao, ushauri wangu mtukufu mfalme ni kwamba, nitateuwa mtu ambae anaweza kusimamia kikundi kidogo cha jeshi cha uchunguzi toka ndani ya jeshi letu la ulinzi, kitengo cha AR, ambacho kitachunguza kwa siri, mienendo na mipango ya UMD, ili tujuwe namna ya kuwadhibiti” alisema Sixmund, “sawa kibari kimetolewa, teuwa kikundi na msimamizi, lete bajeti yako, kwaajili ya kikundi, nahitaji taarifa za mara kwa mara kujuwa kila kinachoendelea” alisema mfalme Elvis, kabla ya kuagana na Sixmund, ambae aliondoka zake na kwenda kuandaa kikundi hicho cha siri, ndani ya kitengo chake cha AR.*******
Kampala Uganda, Hotel Ajun Serasie, wakati Neela na Deus wanaendelea kula, huku Neela akionekana wazi kuzidi kujawa na hisia za mapenzi, mara ghafla Neela akasogeza mkono wake na kuushika mkono wa Deus, kisha akamtazama kwa macho tulivu yenye hisia kali za mapenzi, “Deus nilidhania hii inaweza kuwa ishara ya neno asante, maana mwili wangu huwa siutoi kwaajili ya burudani kwa mtu, niliutoa mara chache kwa mwanaume aliesema atakuwa mume wangu, ni kutoka Tanzania, nilikutana nae wakati nasoma chuo pale muhimbili, akakosa uvumulivu na kunisaliti ndio maana nilikuchukia siku ya kwanza tulipokutana, niliona kuwa wanaume toka Tanzania sio waaminifu, nikaamua kukupa kama asante kwa kuniokoa toka kwenye mikono ya wale majambazi washenzi, lakini nimegundua kuwa, nilichokipata kwako ni zaidi ya kile nilichokupatia, hakika bado nina deni kwako” alisema Neela na kumfanya.
Deus alitabasamu kidogo, kisha akaongea kwa sauti tulivu iliyojaa mahaba, “hapo mwanzo sikuwahi kujaribu mapenzi, ila nimeshangazwa na kile nilichokiona kwako, sikutegemea kama mapenzi ni matamu hivi, umekuwa mwalimu wangu mzuri sana” alisema Deus, huku tabasamu likiendelea kutawala usoni mwake, “wewe umenifanya niyafanye yote ulio yaona, japo niliwahi kushiriki mapenzi, lakini Deus, leo ndio nimefanya mapenzi kiukweli, yaani kamavile kulikuwa na mwalimu pembeni yetu, yaani kama mwanaume wangu wa zamani angepata kuniona wakati ule, angeshangaa sana” alisema Neela huku uso wake ukijawa na tabasamu lililojaa aibu ya kike na kumalizia kwa kicheko cha chini, huku anakwepesha macho yake yasitazamane na macho ya Deus.
Wakati wanaongea hili na lile, mara simu ya Neela ikaanza kuita, wote wakaitazaa na kuona jina la mpigaji likiwa limeandikwa BABA, Neela akaipokea haraka na kuiweka sikioni, kisha akaanza kuongea kwa lugha ambayo Deus hakuielewa, mpaka walipomaliza na kukata simu, “alikuwa baba yangu, yupo na mama wanaondoka Ethiopia sasa kwa ndege binafsi, wanakuja kukuona mwanaume ulieyakoa maisha yangu, nilikuambia mwanzo kuna watu wanahitaji kukuona” alisema Neela, kitu ambacho kilimshangaza sana, Deus, “kwanini lakini mbona ni kitu cha kawaida tu, kwanini wazazi wako wanakuja toka Ethiopia?” aliuliza kwa mshangao Deus na kumfanya Neela acheke kiogo, kisha kuanza kumueleza jambo alisilolijuwa kuhusu yeye na familia yake.*******
Naam Gari aina ya BMW lilioekana likikatiza kwenye barabara ya tunduru masasi, kuelekea upande wa mashariki, yaani kwenye mji wa masasi uliopo mkoa wa mtwara kwa speed kari sana ya kilomita mia moja themanini kwa saa, na sasa lilikuwa limebakiza kilomita chache sana kuingia masasi mjini.
Ndani ya gari hilo anaonekana mtu mmoja tu, ambae ndie dereva, tena ni mschana mrembo, mwenye umri kati ya miaka 24 au 25 hakika ingekushangaza sana, kwa mschana mdogo kama huyu kuendesha gari kwa speed kama hii, gari lilikuwa la kisasa, ambalo lina mambo mengi sana, ukiachia seat zake kuwa nzuri zenye kustarehesha msafiri, pia screen dogo ya video kila seat, huku dash board yake yenye mambo mengi sana, ikizidi kueleza kuwa iligari aina BMW 7, sio la kawaida, kuanzia speed yake ya mwisho kuwa 280, pia vitufe vingi vya kuongozea gari, pamoja na kioo kiogo chenye ramani ya sehemu anayoenda ikionyesha kilomita na hali ya hewa.
Naam wakati mschana huyo mrembo wa sura na umbo alikuwa anapunguza mwendo kuingia mjini masasi mara simu yake ikaita, nae akabiofya kitufe flani kwenye dash board ya gari lake la kisasa, sehemu ya kioo cha video ndogo pale mbele, ambapo kuna jina la mpigaji wasimu lilionekana limeandikwa Boss Atshen na kuanza kuongea. “naam boss, ndio naingia masasi sasa” alisema yule mschana, mrembo, ambae hata sauti yake ni nzuri, “sikia Sheba, ramani inaonyesha mbele yako kuna njia panda, barabara tatu za lami, mbele kulia na hiyo unayotoka, na moja ya kushoto ni ya vumbi, ifuate hiyo sina uhakika na hawa washenzi, wanaweza kubadili mchezo muda wowote” ilisikika sauti toka kwenye ile screen na ile kutazama vizuri tayari alikuwa anaivuka ile njia panda, hivyo akapunguza mwendo zaidi na kuingia kwenye kituo cha mafuta kilichopo pembezo mwa njia panda, upane wa kushoto mtu yeyote angejuwa kuwa gari hili linaingia kuweka mafuta, lakini haikuwa hivyo, lilipitiliza moja kwa moja mpaka njia ya kutokea na kuingia kwenye ile barabara aliyo elekezwa. ..…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums