Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Narudi
 
Ok
 
Aisee togo wewe ni bonge la kiazi
 
Sehemu ya 29


ILIPOISHIA:

Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.

SASA ENDELEA…

“Mambo Togo?”

“Safi, karibu,” nilisema huku nikitazama huku nakule. Yule ndugu yangu alikuwa amesimama pembeni akikutazama kwa zamuzamu.

“Samahani nina maongezi kidogo na wewe,” alisema. Kwa hali niliyokuwa nayo, nilikuwa nikifikiria jambo moja tu kutokakwake, mapenzi.

“Nisubiri kwa kule mbele,” nilimuelekeza huku harakaharaka nikitoka na kuelekea bafuni. Nilijimwagia maji ya baridi kwa wingi ili angalau nitulie kisha nikarudi chumbani na kuvaa nguo.

Nilijitazama tena kwenye kioo, bado nilikuwa na alama za kuvilia damu usoni lakini sikujali, akili yangu ilikuwa ikihitaji kitu kimoja tu kwa wakati huo. Nilitoka kimyakimya bila kumuaga mtu yeyote mpaka nje.

Nikamfuata yule ndugu yangu na kumwambia kwamba iwe siri yetu nitampa zawadi, nikamsisitiza kwamba asimwambie mtu yeyote. Alikubali, nikamshukuru nakumfuata yule msichana ambaye alionesha kuwa na shauku kubwa ya kuonana na mimi.

Tulitoka mpaka nje kabisa, sehemu ambayo mtu yeyote aliyekuwa ndani asingeweza kutuona, akanikumbatia kwa nguvu na kunibusu shingoni. Nilijikuta nikisisimka mno, nikawa nachekacheka tu mwenyewe.

Aliniambia kuna mahali anataka rtwende pamoja kwa sababu alikuwa na jambo muhimu lililokuwa likimsumbua ndani ya moyo wake. Nilimuuliza amepata wapi ujasiri wa kuingia mpaka kule ndani? Akaniambia ilikuwa ni muhimu sana kuonana na mimi na ndiyo maana hakujali chochote.

“Huwa unakunywa pombe?” aliniuliza, nikatingisha kichwa kumkatalia. Licha ya kujaribu mara kadhaa kunywa pombe za kienyeji tukiwa Chunya, kiukweli kichwa changu kilikuwa kibovu sana, kiufupi sikuwa na uwezo wa kuhimili pombe. Akacheka sana huku mara kwa mara akinipigapiga begani.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Chagua sehemu ambayo unadhani inaweza kufaa kwa mazungumzo ya mimi na wewe, twende beach, Mlimani City au tutafute ‘lodge’ yoyote nzuri,” aliniuliza l;akini kati ya sehemu zote alizozitaja, ni moja tu ndiyo niliyokuwa naelewa, beach. Sikuwa najua Mlimani City ndiyo wapi na kupoje wala sikuwa najua huko ‘lodge’ ni wapi na kuna nini cha muhimu. Waliosema ushamba mzigo, hawakukosea.

Ilibidi nimuulize ili anipe ufafanuzi, akacheka sana, akaniambia Mlimani City ni kituo maalum cha kibiashara, mahali ambapo kuna maduka makubwa, mabenki, migahawa ya kisasa ya sehemu mbalimbali za starehe. Akaniambia pia kuwa neno lodge ni la Kiingereza lakini linamaanisha nyumba ya kulala wageni. Nikashtuka!

“Unamaanisha gesti?”

“Ndiyo?” alinijibu huku akinitazama kwa macho yake mazuri, ikabidi nijifanye sitaki nataka kwa sababu kule kwetu kulikuwa na stori kwamba watu wanaoingia gesti wakati hawapo safarini ni wale wahuni walioshindikana. Nikamwambia kwamba Mlimani City atanipeleka siku nyingine, akanitazama tena usoni na kuachia tabasamu pana.

Japo jibu langu halikuwa la moja kwa moja, nadhani alinielewa haraka nilikuwa namaanisha nini. Tuliingia kwenye Bajaj, nikageuka huku na kule na nilipohakikisha hakuna aliyeniona, nilimpa ishara kwamba tuondoke.

Kwa makusudi kabisa, aliniegamia kimahaba huku mara kwa mara akiendelea kuniangushia mabusu ya hapa na pale. Yaani kama angekuwa anajua kilichokuwa ndani ya kichwa changu, kamwe asingethubutu kumwagia petroli kwenye moto.

Hatukwenda mbali sana, Bajaj ikaingia kwenye jengo moja la kisasa, getini likiwa na maandishi yaliyosomeka Sideview Hotel, tukashuka kwenye Bajaj, nikawa nashangaashangaa huku na kule, alinishika mkono bila hata wasiwasi, tukaingia mpaka ndani ambapo alimfuata dada wa mapokezi na kuanza kuzungumza naye.

Alimwambia anahitaji chumba kwa siku nzima mpaka kesho yake. Nilishangaa kwa nini anataka tukae mpaka kesho yake wakati anajua mimi ni mgeni na nilikuwa chini ya wazazi wangu. Hata hivyo, sikutaka kumhoji chochote mpaka nipate nilichokuwa nakitaka.

Alitoa pochi yake na kuhesabu fedha, akampa yule mhudumu, akatoka na funguo na kwenda kutuonesha chumba chenyewe. Kilikuwa chumba kizuri mno, yaani pengine kuliko vyumba vya kwenye majumba ya watu wengi sana. Picha niliyokuwa nimeijenga kichwani mwangu mwanzoni, nilitegemea chumba kitakuwa kama vile vya gesti za kijiji, kitanda kidogo chenye kunguni na kilicholegea, godoro chafu na jembamba sambamba na mashuka makuukuu.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Kitanda kilikuwa kikubwa, juu yake kikiwa kimetandikwa kwa mashuka meupe na mito mikubwa mizuri, chini kikiwa kimepigwa marumaru safi nyeupe, huku taa zenye mwanga fulani mzuri zikizidi kuyapendezesha mandhari ya chumba hicho, nikawa nashangaashangaa.

Sikuwa na habari kwamba mwenzangu bila hata kuzungumza kile alichosema tunataka kuzungumza, ameshaanza kufaanya kazi nyingine. Alikuwa tayari ameshavua blauzi yake na kubaki na bra, akawa anahaha kufungua suruali yake iliyokuwa imembanana kulichora vilivyo umbo lake. Nilijikuta nikitetemeka mwenyewe, hata sijui ni kwa nini, nikampa mgongo.

“Togo! Mimi mwenzio na…ku..pe…” alishindwa kumalizia alichotaka kukisema, akagusanisha mdomo wake na wangu huku mikono yake ikiwa imenibana kisawasawa kwenye kifua chake kilichosheheni. Kwa kuwa rahma alikuwa amenipa ‘twisheni’ ya mambo hayo, na mimi sikutaka kubaki nyuma, nilimpa ushirikiano, tukawa tunaelea kwenye ulimwengu tofauti kabisa.

Ile halai niliyokuwa naisikia mwanzo, safari hii ilizidi mno, yaani nikawa naona kama nachelewa. Tofauti na Rahma, huyu yeye hakuwa na aibu kabisa na kila alichokuwa anakifanya, alikuwa akifanya kwa kujiamini. Akaninyonyoa manyoya yote kama kuku aliyechinjwa huku na yeye akifanya hivyohivyo, muda mfupi baadaye, tukawa ‘saresare’ maua.

“Togoo!” aliniita kwa mshtuko huku akiwa amepigwa na butwaa iliyochanganyikana na furaha.

“Kumbe upo hivi,” alisema huku akinitazama kwa macho yake kama anasikia usingizi, sikuelewa kauli yake hiyo ilikuwa ikimaanisha nini, lakini aliendelea kunimwagia sifa lukuki kwamba siku ya kwanza aliponiona tu aligundua kwamba nina sifa za kipekee ambazo wanaume wengine hawana.

Sikutilia sana maanani kile alichokuwa anakisema, akili yangu ilikuwa ikiwaza jambo moja tu. Muda mfupi baadaye, tuliianza safari huku mimi nikiwa ndiyo kiongozi wa msafara. Unajua kama una kiu kali ya maji, hata ukipewa jagi zima unaweza kulifakamia lote mpaka liishe. Hicho ndicho kilichotokea kwangu.

Ghafla nilishangaa akianza kugeuza macho na kutupatupa mikono na miguu kama mtu anayetaka kukata roho, haraka nikashuka chini na kuanza kumtingisha kwa nguvu huku nikishindwa hata namna ya kumuita maana kiukweli sikuwa nalijua jina lake.

Kadiri nilivyokuwa namtingisha ndivyo alivyozidi kulegea, mara akatulia huku macho yake yakiwa yamegeuka na kutazama upande wa juu. Nilijaribu kusikiliza mapigo ya moyo wake lakini hayakuwa yakipiga na hakuwa akipumua.

“Mungu wangu,” nilisema huku nikianza kutafuta nguo zangu, harakaharaka nikavaa huku kijasho chembamba kikinitoka, nikawa najiuliza nini cha kufanya maana tayari ulishakuwa msala. Hakuna ambaye angeamini kwamba msichana huyo amekufa mwenyewe, wangejua kwamba nimemuua, nilijikuta nikitetemeka mno.

Akili niliyoipata, ilikuwa ni kuondoka haraka hotelini hapo bila mtu yeyote kujua. Nilichukua shuka na kumfunika kisha nikafungua mlango. Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu, nilitoka na kuurudishia mlango, harakaharaka nikawa natembea kuelekea nje.

Kwa bahati nzuri, nilipofika pale mapokezi, yule dada hakuwepo, nikatoka kimyakimya mpaka nje, nikaelekea lilipo geti kubwa huku nikijitahidi kuvaa tabasamu la uongo ili walinzi wa hoteli hiyo wasishtukie chochote.

“Aroo! We kijana… Aroo wewe,” nilisikia sauti ya mlinzi wa nje ya geti la hoteli hiyo akiniita, moyo ukalipuka paah!

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya thelathini______30





ILIPOISHIA:

Kwa bahati nzuri, nilipofika pale mapokezi, yule dada hakuwepo, nikatoka kimyakimya mpaka nje, nikaelekea lilipo geti kubwa huku nikijitahidi kuvaa tabasamu la uongo ili walinzi wa hoteli hiyo wasishtukie chochote.

“Aroo! We kijana… Aroo wewe,” nilisikia sauti ya mlinzi wa nje ya geti la hoteli hiyo akiniita, moyo ukalipuka paah!

SASA ENDELEA…

“Unaenda wapi?”

“Naenda dukani afande.”

“Mwenzako umemuacha wapi?”

“Yupo ndani, narudi sasa hivi, naenda kununua kinga.”

“Mbona kama una wasiwasi?” alisema yule mlinzi huku akinisogelea. Licha ya kujaribu kucheza na akili zake, ni kama alishashtukia jambo kwa jinsi nilivyokuwa na hofu. Mtu kukufia chumbani, usifanye mchezo.

Hata kama ulikuwa jasiri vipi, lazima uchanganyikiwe. Hicho ndicho kilichonitokea. Hofu ilishindwa kujificha kwenye macho yangu, nikawa nakwepesha macho kwa sababu niliamini yule mlinzi kwa jinsi alivyonishupalia, angeweza kugundua kitu. Nilitamani kufanya kitu lakini sikuwa na uwezo, harufu ya jela ikaanza kunukia.

“Mkazie macho usoni,” ile sauti ya ajabu ya baba, ilisikika masikioni mwangu, nikageuka huku na kule lakini baba hakuwepo eneo hilo. Kwa kuwa mara zote ilikuwa ikinisaidia, nilifanya kama nilivyoelezwa.

Nilimkazia macho yule mlinzi, na yeye akanitazama. Ghafla nikashangaa anakuwa mpole ghafla, mwanzo alikuwa amekunja sura lakini ghafla alitabasamu. Niliendelea kumkazia macho.

‘Haya nenda, unajua siku hizi kumekuwa na matukio ya ajabu sana kwenye hizi nyumba za kulala wageni kwa hiyo lazima tuwe makini,” alisema huku akichekacheka, akageuka na kurudi getini. Sikuamini kilichotokea.

Kwa tafsiri nyepesi, baba alikuwa anaona kila kinachoendelea kwa sababu asingeweza kuniambia maneno yale tena katika muda muafaka kabisa. Hofu yangu ilikuwa ni je, anajua nilichokifanya kule gesti? Mara kwa mara alikuwa akinikanya lakini kwa ubishi wangu nikaona kama ananibania nisifaidi.

Sikuwa nalijua Jiji la Dar es Salaam wala sikuwa najua ramani ya kunifikisha nyumbani, kitu pekee nilichokumbuka, ni barabara ile tuliyojua, nikawa natembea harakaharaka huku nikitamani kama ningekuwa na uwezo ningepaa kabisa na kutoweka eneo hilo.

Nilinyoosha na barabara na nilipofika mbali, nilianza kukimbia, hofu kubwa ikiwa imetanda kwenye moyo wangu. Kwa bahati mbaya zaidi, sikuwa nakumbuka sehemu ambayo tulikatia kona na kutokezea kwenye barabara hiyo, nikajikuta nikipoteza uelekeo, nikawa nazunguka huku na kule, kijasho chembamba kikinitoka.

Sikuwa na fedha mfukoni kwamba ningezitumia kukodi bodaboda na kuwaelekeza nyumbani. Nikiwa naendelea kuumiza kichwa, hatimaye nilipata akili mpya. Pale nyumbani, kwa nje kulikuwa na kituo cha madereva wa Bajaj na nimewahi kusikia kwamba wenyewe wana umoja wao na wanajiita City Boys wakimaanisha watoto wa mjini.

Kuna Bajaj ilikuwa ikija mbele yangu, nikaipiga mkono, ikapunguza mwendo na hatimaye ikasimama. Nilimfuata dereva na ikabidi niwe mkweli kwake, nikamwambia kwamba nimepotea na ramani pekee iliyopo kichwani mwangu, ni kituo cha Bajaj cha City Boys.

Alicheka kisha akaniambia niingie kwenye Bajaj yake, nikamtahadharisha kwamba sikuwa na fedha, akaniambia atanisaidia.

“Wewe si unakaa pale kwa akina Rahma, mbona mimi nakujua,” alisema yule kijana kwa uchangamfu, nikamshukuru Mungu wangu na kuelewa kwa nini alicheka nilipomueleza kwamba nimepotea.

‘Mimi nakusaidia lakini na wewe nataka unisaidie jambo, unajua mi nampenda sana yule dada Rahma ila naogopa kumwambia ukweli maana muda wote yupo ‘sirias’, nataka unisaidie kufikisha ujumbe, mwambie Zedi dereva teksi, ukifanikisha ntakuwa nakuja kukuchukua nakutembeza viwanja mbalimbali na Bajaj, hata ukitaka pesa ntakuwa nakutoa,” aliniambia yule dereva Bajaj.

Kwa kuwa nilikuwa na shida kwa wakati huo, nilimkubalia kila alichokuwa anakisema. Hakuwa akijua kwamba mimi ndiye mmiliki wa Rahma. Kumbe sikuwa mbali sana na nyumbani, muda mfupi baadaye tukawa tumeshafika, akanishusha getini na kunisisitiza kuhusu ombi lake, nikazidi kumdanganya kwamba asiwe na wasiwasi.

Niliposhuka niliingia moja kwa moja ndani huku bado hofu kubwa ikiwa imetanda kwenye moyo wangu.

“Ulikuwa wapi?” mama aliniuliza kwa ukali mara tu nilipofika sebuleni. Nikakosa cha kujibu kwa muda, nikawa najiumauma, baadaye nikamwambia kwamba kuna rafiki yangu nilikuwa nimemsindikiza.

“Rafiki? Rafiki gani? Una rafiki hapa mjini wewe?” mama alinihoji huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya masihara. Ilibidi ninyamaze kimya, nikataka nipitilize kwenda chumbani lakini aliniambia nataakiwa kukaa nao hapohapo sebuleni kwa sababu ninapopewa muda wa kuwa huru nashindwa kuutumia uhuru wangu vizuri.

Huo ulikuwa mtihani mkubwa sana kwangu, ikabidi nimwambie mama kwamba bado sijisikii vizuri, akaniambia nitakapotoka tena bila ruhusa yake au bila kuaga, atanisemea kwa baba aninyooshe. Nilifurahi kwa sababu aliniruhusu niende chumbani kwangu.

Nilipoingia tu, nilijifungia kwa ndani, nikakaa kwenye ukingo wa kitanda na kujiinamia, maswali mengi yakiendelea kupita ndani ya kichwa changu. Sikuwa najua nini itakuwa hatima yangu endapo ukweli utafahamika. Hata hivyo, kwa upande mwingine, nilianza kujiuliza mimi kosa langu ni nini kwa sababu, yeye ndiye aliyenifuata hadi nyumbani na ndugu yangu alikuwa shahidi.

Yeye ndiye aliyenishawishi twende kwenye nyumba ya kulala wageni na hata tulipofika, alionesha wazi kwamba alikuwa akinihitaji na kwa vile na mimi nilikuwa kwenye hali mbaya, tulijikuta tukiangua dhambini.

Nilijaribu kujiuliza kwamba labda kuna kitu kisicho cha kawaida nilimfanyia mpaka yakatokea ya kutokea lakini sikukumbuka chochote. Bado niliendelea kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.

Nikiwa nimejifungia chumbani, mara nilianza kusikia kelele sebuleni, ndugu zangu wakawa wananiita nikaangalie. Ilibidi nitoke na kwenda mpaka sebuleni. Habari za dharura au Breaking News kama wengi walivyozoea kuita, zilikuwa zikioneshwa runingani moja kwa moja kutoka eneo la tukio.

Zilikuwa ni habari za samaki hatari aina ya papa kuvamia kwenye ufukwe wa bahari ya Hindi na kusababisha vifo vya watu kadhaa, wakiwemo wavuvi na wengine waliokuwa wakiogelea ufukweni huku wengine kadhaa wakijeruhiwa. Nilijikuta moyo wangu ukilipuka kuliko kawaida.

Kilichonishtua ni kwamba, mazingira ya tukio lile, yalikuwa sawa kabisa na kile kilichonitokea nilipoenda ufukweni na Rahma.

Habari zilieleza kwamba wavuvi walaikuwa kwenye boti yao wakivuta nyavu lakini ghafla, samaki huyo aliwashambulia kwa kuvunjavunja boti yao na kuanza kuwala, mmoja baada ya mwingine, hali iliyosababisah maji ya bahari yageuke rangi na kuwa mekundu.

Yaani kilekile nilichokieleza na kila mmoja kuniona kama mwendawazimu, ndicho kilichokuwa kimetokea, taarifa ya habari iliendelea kueleza kwamba polisi na vikosi vya uokoaji, wamefika eneo la tukio na wanahangaika kupambana na samaki huyo mkubwa.

Baada ya habari hiyo kuisha, watu wote pale sebuleni walinigeukia na kunitazama kwa mshangao uliochanganyikana na hofu. Tukiwa bado tunatazamana, mara baba aliingia getini akiwa ameongozana na baba yake Rahma na askari watatu waliokuwa na silaha. Nikajua mwisho wangu umefika, nilishindwa cha kufanya, nikabaki nimesimama palepale, nikitetemeka kuliko kawaida.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 31



ILIPOISHIA:

Nikiwa bado naendelea kumtazama kwa jicho baya, mara nilishtuka kusikia vishindo viwili vikubwa juu ya bati, kama vile nilivyokuwa navisikia usiku uliopita, moyo wangu ukapatwa na mshtuko mkubwa mno. Mara nilisikia vishindo vingine vitatu mfululizo, nikawa nimepigwa na butwaa huku macho yangu yote yakiwa juu.

SASA ENDELEA…

Kwa jinsi vishindo hivyo vilivyokuwa vikisikika, ilikuwa ni kama kuna watu wanaruka kutoka angani na kudondokea juu ya bati kwani vilikuwa vizito mno. Safari hii nilitaka kuwa makini kushuhudia je, kile ninachokisikia mimi, kila mtu anasikia hivyohivyo maana nilishahisi kuna kitu hakipo sawa kwangu lakini baba hataki kuniambia ukweli.

Baada ya vishindo vile vya kama watu au vitu kutua juu ya bati, mara vilianza kusikika vishindo vya mtu akitembea juu ya bati.

Unajua haya matukio kama hujawahi kutokewa nayo, huwezi kuelewa ile hofu unayokuwa nayo lakini kiukweli, ni bora tu uwe unasikia lakini yasikutokee. Hakuna hofu inayotesa kama hofu ya matukio kama haya yanapokutokea, hasa usiku kama huo.

Nilijikuta nywele zikisisimka vibaya mno, mapigo ya moyo yakawa yananienda kwa kasi maana sikujua safari hii wanakuja kwa mtindo gani. Vishindo viliendelea kusikika kisha kikasikika kishindo kingine ambacho kwa makadirio yangu ya haraka, kilikuwa ni kwenye sakafu ya mle mahabusu.

Nilishindwa kuelewa, inawezekanaje usikie mtu anatembea juu ya bati, tena kwa nje halafu muda mfupi baadaye umsikie akirukia na kudondokea kwa ndani, tena jirani kabisa na pale ulipo! Inatisha sana.

“Humu ndani kuna wanga eeh! Mbona nywele zinanisisimka? Sasa ole wake mtu aniguse,” mmoja kati ya wale mahabusu tuliokuwa nao mle ndani, aliyekuwa amekaa kwenye kona nyingine, alisikika akiongea kilevilevi, akawa anaporomosha matusi mazitomazito.

Kitendo kile kilinifanya niamini kwamba hatimaye sasa sikuwa peke yangu ambaye nilikuwa nikishuhudia mchezo uliokuwa ukiendelea. Niliamini hivyo kwa sababu kwenye kona aliyokuwa amekaa yule mahabusu ambaye alikuwa akiendelea kutukana, ndiko ambapo makadirio yangu yalinionesha kwamba yule mtu aliyekuwa akitembea juu ya bati alidondokea palepale.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Matusi aliyokuwa akitukana, yalisababisha mahabusu wengine ambao bado hawakuwa wamelala, waanze kucheka kwa nguvu na kumtania kwamba amelewa lakini kelele zote zilizimika ghafla bila mtu yeyote kutoa amri, ikatokea tu kwamba watu wote wapo kimya.

Katika ukimya huo, ulisikika msonyo mkali ambao japokuwa wale mahabusu wengine waliamini kwamba umetolewa na yule mahabusu aliyekuwa akitoa matusi mazito kwa wale aliowaita wanga, mimi nililitazama tukio hilo katika sura nyingine tofauti.

Haikuwa mara ya kwanza kusikia msonyo wa namna hiyo ingawa safari hii ulionekana kutoka kwa mtu tofauti ambaye sijawahi kuisikia sauti yake. Unajua kuna watu wamezaliwa wakiwa na uwezo fulani wa kipekee, sijui niuiteje lakini kwa kifupi mtu anakuwa na uwezo wa kufikiri na kuyaona mambo kwa utofauti na wengine.

Yaani kuna baadhi ya watu, nyie wengine wote mnaweza kuamini kwa mfano ajali iliyotokea barabarani imesababishwa na uzembe wa dereva kukimbia kwa mwendo kasi akiwa hajafunga mkanda, lakini mtu mwingine hapohapo akalitazama tukio na kutoa jibu tofauti kabisa ambalo pengine halikutegemewa.

Baba amewahi kunifundisha kwamba japokuwa watu wa namna hii huwa wanachekwa au kuzomewa na kuonekana wanaishi kwenye ulimwengu wa ndoto, lakini wao ndiyo huwa sahihi kwa sababu wanautazama ulimwengu kwa jicho tofauti na watu wengine wote.

Ndicho kilichotokea mle mahabusu, wakati watu wote wakilichukulia tukio la yule mahabusu kudai kule ndani kuna wachawi kisha akaanza kuporomosha matusi, wengi walimuona kama mlevi tu lakini mimi nilimtazama kwa jicho tofauti.

Hata uliposikika ule msonyo na watu kuanza kumtuhumu kwamba anawavurugia usingizi wao, mimi nilikuwa nikiamini kwamba hakuutoa yeye na alichokuwa akikisema kwamba mle ndani kulikuwa na wanga, ulikuwa ni ukweli mtupu.

“Sikilizeni, sikilizeni,” alisema yule mahabusu, kwa msaada wa mwanga hafifu uliokuwa ukipenya kutokea nje, nilimuona akiinua kichwa chake juu kutazama darini, lakini kelele za mahabusu wengine zikamfanya ashindwe kusikia alichokuwa akitaka kukisikia.

“Au naye ana nguvu kama mimi?” nilijiuliza kwa sababu wakati akiwataka watu wote watulie ili wasikie, ni kweli juu ya bati kuna mtu alikuwa akitembea kwa vishindo kabisa kisha naye akasikika akidondokea ndani ya ile mahabusu.

*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Baada ya hapo, vilianza kusikika vishindo vya watu wakirukia mle mahabusu mfululizo, nikawa natetemeka nikiwa sijui nini kitatokea maana kama unavyojua, milango ya mahabusu huwa muda wote imefungwa na haiwezekani ikafunguliwa kwa muda ule. Nilichokuwa nakiomba, ni wachawi hao wasije wakawa wamekuja kwa shari kama ilivyotokea kwangu na safari hii, nilijifunza kuufyata mkia, sikutaka kuzungumza chochote zaidi ya kuzidi kukodoa macho yangu gizani kama nitaona kitu chochote.

Nilishangaa mfuko wa suruali yangu ukianza kutetemeka kama ndani kulikuwa na kitu ‘kinacho-vaibreti’, sikukumbuka kama niliweka kitu chochote mfukoni na hata kama ni simu, wala sikuwa nikimiliki baada ya baba kunipokonya ile niliyopewa na yule dada ambaye ndiye aliyesababisha muda huo nikawa nyuma ya nondo.

Kwa hofu kubwa niliingiza mkono mfukoni huku nikiwa bado nimekodoa macho, nikagundua kwamba kulikuwa na kitu kwenye mfuko wangu ambacho sikuwa najua ni kitu gani.

Mbaya zaidi, sikujua ni nani aliyekiweka kwenye mfuko wa nguo yangu kwa sababu wakati naingizwa na wale askari, waliniambia pale kaunta nitoe kitu chochote nilichokuwa nacho mfukoni na wala sikuhitaji kujisachi kwa sababu nilikuwa najua sina chochote.

Cha ajabu, nilipokigusa kitu hicho tu, kiliacha kutetemeka lakini yote tisa, kumi ni kwamba nilianza kuona vitu vya ajabu mno. Japokuwa mle ndani kulikuwa na giza, niliweza kuwaona watu wote vizuri, mpaka sura zao utafikiri ilikuwa mchana, ila tofauti yake ni kwamba hakukuwa na mwanga wenye uangavu kama wa mchana bali ulifanana kwa mbali na nuru ya mbalamwezi.

Kwa wale tuliokulia vijijini nadhani wanaelewa vizuri usiku wa mbalamwezi unavyokuwa, yaani unaweza kusema ni mchana kabisa kwani vitu vyote vinaonekana japo siyo vizuri kama vile nilivyokuwa naona mimi.

Nilianza kuwatazama mahabusu wenzangu mmoja baada ya mwingine maana kama unavyojua, niliingizwa giza likiwa limeshaingia na kwa sababu mle ndani hakukuwa na taa, watu pekee niliowaona vizuri ni wale waliokuwa jirani na mimi.

Cha ajabu, wakati nikiendelea kuwatazama mahabusu hao ambao wengi walishaanza kusinzia kutokana na uchovu, niligundua kwamba kulikuwa na watu wengine wasio wa kawaida mle ndani, nao wakiwa wamejichanganya na mahabusu lakini tofauti yao ilikuwa moja.

Karibu wote walikuwa na macho mekundu sana na walikuwa wakinitazama kama wanaosubiri kuona nitafanya nini lakini kubwa, wote walikuwa watupu kabisa. Nilipopiga jicho harakaharaka na kujaribu kuwahesabu, walikuwa kama saba hivi, tena wengine wawili walikuwa ni wanawake na kama unavyojua mahabusu huwa hawachanganywi wanawake na wanaume.

Wote waliacha kila walichokuwa wanakifanya, wakawa wananitazama kwa macho makali. Sikuelewa nini hasa kimetokea, wakati nikiendelea kuwatazama vizuri kwa mara ya pili, kuna jambo moja lilinishtua mno mpaka nikajikuta nimetoa mkono mfukoni, giza likarudi kama lilivyokuwa mwanzo.

Je, nini kitafuatia?
 
Baba kuingia ndani ya geti akiwa na mapolisi waliobeba bunduki na watu kutembea juu ya paa wapi na wali boss wangu.
Umechanganya madini.
 
Hicho kidevice cha mfukoni ni unyama mwaisa [emoji38][emoji38][emoji38]
 
We jamaa mbona una roho mbaya hata kunitag mwanangu? Poa ntakuja kuishi hapa
 
Naweka kambi hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…