Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
71.
"hahahahaha ukitaka kuwaongoza watu vizuri wagawe makundi" aliongea mtu mmoja ambae alikuwa amevaa gwanda za jeshi na kucheka kwa nguvu huku akiwa anaangalia video zilizowaonyesha wale wenzake na marehemu Marko wakigombana.
"Unahis vipi baada kumuondoa Marko katika uso wa dunia" swali la kwanza alilokutana nalo kutoka kwa Christine baada kufika tu hoteli. "ah kawaida tu, mbona kuuwa kwangu ni jambo dogo sana" alijibu Alex na kuelekea chumbani kwake, alijitupa kitandani huku akiwaza na kuwazua inakuaje Allen James anakuwa hatari kiasi kile. Maana zile mbinu nazotumia si mchezo, kuweza kulenga mita zaidi ya 70 bila kutumia darubini. Mwisho aliona atapasuka kichwa tu ikiwa ataendelea kuwaza, aliamua kuinuka na uingia chooni kwa ajili ya kujifanyia usafi. Alimaliza na kurudi chumbani, alivaa nguo za kawaida na kutoka.
Chakula kilikuwa kimeshaletwa walikaa pamoja na kuanza kula huku wakiongea mambo mengi. "kesho tutaelekea Uingereza na tutaondoka hapa asubuhi" Aliongea christine, "sawa hakuna shida" Alex alijibu kwa sababu alishajua mapema kuwa wangeondoka Urusi. Baada ya kula kila mtu alikwenda chumbani kwake na kuupitisha usiku ambao kwa Alex ulikuwa ni mzuri sana hasa ukizingatia kuwa kuna mtu ambae anamthamini kama mtu na sio mashine tu ya kufanyia mauaji.
Siku ya pili mapema waliondoka na kuelekea uingereza, katila ndege walipata viti vya mbali mbali. Alex alikaa na mtu mmoaja ambae alikuwa akisoma gazeti hivo hakufanikiwa kumuona sura. "naona tunakwenda Uingereza" Aliongea yule mzee na kumafanya Alex kushtuka kwa maana sauti hiyo aliifahamu kama ilikuwa ya Allen. "Allen unafanya nini humu" Alex aliuliza kwa sauti ya chini, "si nasafri kama abiria wengine" Allen alijibu huku akiondoa gazeti. Alex karibu acheke kwa nguvu maana kwa jinsi alivyokuwa Allen ni shida, alikuwa amebandika ndevu nyngi pamoja na sharubu kitu ambacho kama hujawaho kukutana nae lazima usingemjua.
"sasa sikia tupange mikakati, kwanza walioiteketeza familia yako ndio waanze kuangamia halafu ao wengine watafuata" aliongea Allen, "ah sasa si nimeshaanza kuwaondoa" Alex alijibu kwa kujiamini. "acha ujinga wewe yule uliemuua jana hahusiki na vifo vya familia yako" Allen aliongea na ghafla sura ya Alex ilibadilika na kuwa kama ameanza kukasirika. "mi nimekwambia unatumiwa kufanikisha kazi za watu" Allen aliendelea kusukuma msumari wa moto katika kifua cha Alex. "mbona sielewe elewi" Alex aliongea huku akionekana kuwa amechanganyikiwa, "ndio lazima usielewe kwa sababu unachezewa mchezo mchafu" Allen alijibu.
"hahahahaha ukitaka kuwaongoza watu vizuri wagawe makundi" aliongea mtu mmoja ambae alikuwa amevaa gwanda za jeshi na kucheka kwa nguvu huku akiwa anaangalia video zilizowaonyesha wale wenzake na marehemu Marko wakigombana.
"Unahis vipi baada kumuondoa Marko katika uso wa dunia" swali la kwanza alilokutana nalo kutoka kwa Christine baada kufika tu hoteli. "ah kawaida tu, mbona kuuwa kwangu ni jambo dogo sana" alijibu Alex na kuelekea chumbani kwake, alijitupa kitandani huku akiwaza na kuwazua inakuaje Allen James anakuwa hatari kiasi kile. Maana zile mbinu nazotumia si mchezo, kuweza kulenga mita zaidi ya 70 bila kutumia darubini. Mwisho aliona atapasuka kichwa tu ikiwa ataendelea kuwaza, aliamua kuinuka na uingia chooni kwa ajili ya kujifanyia usafi. Alimaliza na kurudi chumbani, alivaa nguo za kawaida na kutoka.
Chakula kilikuwa kimeshaletwa walikaa pamoja na kuanza kula huku wakiongea mambo mengi. "kesho tutaelekea Uingereza na tutaondoka hapa asubuhi" Aliongea christine, "sawa hakuna shida" Alex alijibu kwa sababu alishajua mapema kuwa wangeondoka Urusi. Baada ya kula kila mtu alikwenda chumbani kwake na kuupitisha usiku ambao kwa Alex ulikuwa ni mzuri sana hasa ukizingatia kuwa kuna mtu ambae anamthamini kama mtu na sio mashine tu ya kufanyia mauaji.
Siku ya pili mapema waliondoka na kuelekea uingereza, katila ndege walipata viti vya mbali mbali. Alex alikaa na mtu mmoaja ambae alikuwa akisoma gazeti hivo hakufanikiwa kumuona sura. "naona tunakwenda Uingereza" Aliongea yule mzee na kumafanya Alex kushtuka kwa maana sauti hiyo aliifahamu kama ilikuwa ya Allen. "Allen unafanya nini humu" Alex aliuliza kwa sauti ya chini, "si nasafri kama abiria wengine" Allen alijibu huku akiondoa gazeti. Alex karibu acheke kwa nguvu maana kwa jinsi alivyokuwa Allen ni shida, alikuwa amebandika ndevu nyngi pamoja na sharubu kitu ambacho kama hujawaho kukutana nae lazima usingemjua.
"sasa sikia tupange mikakati, kwanza walioiteketeza familia yako ndio waanze kuangamia halafu ao wengine watafuata" aliongea Allen, "ah sasa si nimeshaanza kuwaondoa" Alex alijibu kwa kujiamini. "acha ujinga wewe yule uliemuua jana hahusiki na vifo vya familia yako" Allen aliongea na ghafla sura ya Alex ilibadilika na kuwa kama ameanza kukasirika. "mi nimekwambia unatumiwa kufanikisha kazi za watu" Allen aliendelea kusukuma msumari wa moto katika kifua cha Alex. "mbona sielewe elewi" Alex aliongea huku akionekana kuwa amechanganyikiwa, "ndio lazima usielewe kwa sababu unachezewa mchezo mchafu" Allen alijibu.