Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Mh mbona siku nyingi zinapiga? singanojr Kama Kuna kulipia tuambie wengine tupo tayari kupata huu mwendelezo na si kusubiri kama hivi
 
SEHEMU YA 276.

Zilipita takribani siku sita na sasa ilikuwa ni siku ya ijumaa tena, katika siku zote hizo hakuna kilichotokea kwa Edna wala kwa Roma Zaidi ya Maisha ya kawaida waliokuwa nayo wanandoa hao kila siku.

Jambo moja kubwa tu ni kwmaba Edna alikuwa kwenye mawazo na hio yote ni baada ya jumapili iliopita Kwenda kituo cha yatima kwa minajili ya kumuona Lanlan , lakini jambo la kushangaza ni kwamba hakuweza kumpata kabisa na hata alipoenda sehemu ambayo wanaishi , nyumba ilikuwa imefungwa na hilo lilimuongezea huzuni mrembo huyo kwani alikuwa amemkumbuka sana mtoto huyo.

Siku hii ya Ijumaa ilimbidi Roma Kwenda kwenye kampuni mpya ambayo imefunguliwa na mke wake Edna na hii yote ni mara baada ya kupigiwa simu na Daudi kwamba mwekezaji Rose Situ anataka kuonana na boss mwenyewe kwa ajili ya mazungumzo ya kibiashara, hivyo Roma hakuona shida ya Kwenda kuonana na Rose ambaye ndio mwekezaji , alijua Rose alikuwa akitumia nafasi hio kutaka kumuona hivyo aliona ni sawa tu Kwenda kwani hata yeye amemiss.

Kwasababu alikuwa akiishi Osterbay , alitumia dakika ishirini mpaka theratini kuendesha gari mpaka kwenye jengo la kampuni.

Roma aliingiza gari baada ya kufika na kuliegesha na kisha alitembea na kuingia kwenye Lift ndani ya jengo hili la Ghorofa na kubonyeza kitufe namba kumi na tisa na ndani ya dakika chache tu alikuwa juu kabisa ya Floor ambayo ndio kampuni ya Vexto Media ilikuwa na makao yake hapo.

Mrembo Rose alievaa akapendeza alionekana kuketi eneo la mapokezi akiongea na Wendy , alikuwa mrembo haswa na mavazi aliochagua kuja nayo siku hio yalimpendezesha mno na hakuna mtu yoyote anaweza kugundua kuwa mwanamke huyo ni muuzaji madawa ya kulevya kwani haiba yake iliwakilisha upole, Roma alitabasamu kumuona Rose na kabla hajamfikia sauti ya Daudi ilimwita kwa nyuma yake.

“Director, you are here, Miss Rose waited for a long time."”Aliongea Daudi kwa furaha na Roma alitabasamu na kutingisha kichwa huku akimkonyeza Rose ambaye aliishia kutabasamu.

Roma aliwapa ishara kwa ajili ya kuongozana wote mpaka kwenye ofisi yake ikiwemo Rose na ndani ya sekunde kadhaa waliingia ndani ya ofisi hii na Roma alienda kuketi kwenye kiti chake cha kibosi na kumfanya Rose kuridhika na mwonekano wa mpenzi wake.

“Boss tulikuwa tukijaribu kumuelezea Miss Rose kuhusu mipango tuliokuwa nayo juu ya kampuni yetu , lakini pia shindano la kuibua vipaji ambalo tunakwenda kuanza nalo na ameridhishwa sana na wazo letu”

“Tumezungumza na kuamua shindano hili tulipe jina la Kizazi Nyota ,linaonekana halijakaa vizuri ila tumeamua kufanya haraka ili kuanza matangazo juu ya shindano hili”Aliongea Daudi na Roma alitingisha kichwa kukubaliana nae.

“Sina maoni yoyote nakubaliana na kila mlichopanga , kama kuna lingine la ziada inabidi mniambie , Mpango wenu kwa sasa ni upi?”Aliuliza Roma

“Kwasaabu taratibu za shindano hili hazina utofauti sana na za Bongo Star Search, tumeona turahisishe kwa kutumia namna wanavyoendesha mashindano yao, kilichobaki kwasasa ni namna ya kuchagua majaji ambao watasimamia shindano zima”Aliongea Wendy na Roma alifikiria kidogo.

“Okey ni vigezo gani ambavyo mnaona vinafaa kwa ajili ya majaji?”

“Ili mtu kuwa jaji lazima awe na umaarufu wa kutosha , mwonekano wake kwa jamii , lakini pia lazima atambulike kimataifa kwani shindano hili linakwenda kutoa watu wenye vipaji ambao watakwenda kufadhiliwa na kampuni yetu hivyo lazima tuwe makini kwenye kuchagua majaji , lakini hata hivyo Director umesema unajua namna ya kufanya shindano hili liwe maarufu hivyo tumeona tukuachie upande wa majaji”

“Okey sina sana ujuzi na maswala ya burudani , ila nina rafiki yangu ambaye ypo kwenye mambo ya burudani na ni msanii mzuri wa kimataifa , kama nilivyosema shindano hili nataka lipate umaarufu hivyo naamini kama tutamtumia watu wengi watalifatilia na kupata umaarufu”Aliongea Roma na kufanya Wendy , Daudi na Rose kushanga na Roma akatabasamu.

“Director tunaweza kumfahamu mtu unayemzungumzia?”Aliuliza Daudi na Roma alitingisha kichwa na kusema ndio na kuwapa ishara kuja nyuma ya meza yake na baada ya wote kuja aliingia kwenye mtandao wa Istagram na kisha alitype jina la Christine Stewart na akaunti yake ilitokea.

“Director usiniambie huyu ndio mtu ambaye unapanga kuwa jaji , itakuwa nni ngumu kumpata , lakini pia atahitaji malipo makubwa”Aliongea Wendy na Roma akatabasamu.

“Ni nani huyu kwanza hata simfahamu?”Aliongea Rose haikueleweka ni kweli hamfahamu au lah lakini macho yake yalidhihirisha kwamba hamfahamu huyo mwanamke mrembo aliekuwa akionekana kwa picha.

“Miss Rose naona hauangaliagi Muvi ,,Christine Stewart ni Hollywood Star mwenye mvuto mkubwa duniani kote , ameshinda tuzo mbalimbali kama vile ya Oscar , Grammy na tuzo ya mwimbaji bora wa karne , inasemekana ana umri wa miaka 26 na pia ana akili nyingi sana za kibiashara , duniani kote wanaume wengi wanahusudu urembo wake na kutamani siku moja kupata nafasi ya kulala nae hata mara moja”Aliopngea Daudi na kumfanya Wendy amfinye aliona anaongea sana , lakini kwa Roma ilionekana ni kawaida tu kwani Daudi alionekana ni moja ya shabiki wa Christine hivyo ni kawaida kwa mtu kumsifia mtu anayempenda kwa kupitiliza.

“Kwahio Daudi huyu anafaa kuwa Jaji au hafai, kuhusu Gharama hata msijali , kama nilivyokwisha kusema huyu ni rafiki yangu mkubwa na anaweza akawa jaji wetu bure kabisa”Aliongea Roma na kufanya Hata Wendy aone Roma anatania , alikuwa akimjua Christine hawezi kuja Tanzania kupoteza muda kisa ya kuwa jaji , lakini pia alikuwa ni mtu mkubwa sana katika ulimwengu wa burudani , hivyo Roma kuwa na urafiki na mwanamke mrembo kama huyo aliona anawapiga Kamba.

“Anafaa sana Director kama tungekuwa na uwezo wa kumpata , lakini huyu mrembo ni levo nyingine kwetu hivyo nashauri kama tutaangalia wasanii wa hapa hapa Tanzania kama Diamond au Alikiba”Aliongea Wendy na Roma hakujali sana , kwanza alienda upande wa direct Message(DM) kuangalia kama yupo online na alijikuta akitabasamu baada ya kuona mrembo huyo nyota wa dunia yupo online kwenye mtandano huo.

Roma kwakutmia akaunti yake ya jina lake la Roma , aliandika ujumbe wa meseji wa salamu Kwenda kwa Christine huku Rose, Daudi na Wendy wakimshangaa Roma , waliona Roma ni mtu mwenye vituko sana , lakini dharau zao ziliisha mara baada ya kuona Christine anapiga Vidio Call, na Roma alipokea na kumfanya Daudi na Wendy kutoa macho baada ya kuona sura ya mrembo Christine , ni kama hawakuwa wakiamini hivi kama ni yeye kweli.

“Christine nadhani sijakusumbua najua upande huo ni usiku?”Aliongea Roma kwa kingereza.

“Roma ijapokuwa sijapenda simu yako ya muda huu , lakini niamini mimi haijawahi hata siku moja ukatoa taarifa ya eneo ulipo” Baada ya Daudi kusikia maneno hayo alijikuta akishangaa Zaidi baada ya kusikia Christine akitaja jina halisi la Roma.

“Nadhani napaswa kueleza shida yangu haraka haraka nikuache upumzike , sasa hivi nimekuwa Director wa kampuni kwenye maswala ya burudani na wewe ni gwiji kwenye idara hii, nimepanga kuanzisha mashindano ya kusaka vipaji na bado sina jaji ambaye anaweza kufanya shindano la kampuni yangu kuwa maarufu , hivyo naona wewe unafaa kabisa”Aliongea Roma kwa kingereza cha kimarekani kabisa.

“Hahaha.. Roma sijui nini kimekukuta huko Tanzania ila nimefurahi kusikia kama umekuwa Director wa kampuni”Aliongea Christine mrembo kwa mapozi na kumfanya hata Rose kuanza kushikwa na wivu kwani alihisi huenda Roma na Christine ni wapenzi na akiangalia Christine amemzidi sana urembo.

“Kwahio nichukulie haya maneno yako kama jibu ni ndio?”Aliuliza Roma huku akitabasamu kawaida , licha ya kwamba mtu aliekuwa akiongea nae alikuwa mtu mzito lakini alionekana kawaida kabisa na ni kama walikuwa wakifahamiana sana.

“I can participate. I originally planned to give myself a good holiday this year, but I can't do every contest, so other judges will do the most work”Aliongea Christine akimaanisha kwamba atashiriki kama jaji lakini sio kwa mashindano yote , kwani alikuwa akipanga kufanya mwaka huo kuwa wa mapumziko , hivyo kazi nyingine zitafanywa na majaji wengine.

“Miss Christine usiwe na wasiwasi kabisa , sisi tunakuhitaji siku moja tu ya fainali na hatutakusumbua tena , karibu sana Tanzania na asante kwa kukubali ombi letu”Aliongea Daudi kwa shauku kubwa baada ya kusikia Christine yupo tayari kuja Tanzania kwa ajili ya kuwa jajii.

“Huyu ni msaidizi wangu , anafahamika kwa jina la Daudi , atazungumza na wewe juu ya kazi yote utakapofika hapa Tanzania , mimi nimetumia sura yangu tu ili ukubali ombi la kuja Tanzania”Aliongea Roma na kumfanya Christine kutabasamu kivivu na kuachama akiashria kwamba anataka kulala

“I understand, my contact information, you know, I am sleepy now, good night, Roma”

“Goodniht”Aliongea Roma na palepale video Call ilikatwa na Daudi na Wendy walijikuta wakianza kupiga makofi kwa furaha , waliamini kwa kupitia Christine umaarufu wake basi hata wao watakuwa maarufu sana na pia kampuni yao kujulikana ndani ya muda mfupi.

Roma aliwaandikia Email ya Christine Daudi na Wendy kwa ajili ya kuwasiliana na management yake na kisha wakatoka ndani ya ofisi hio wakimuacha Roma na Rose.

“Nini tatizo Rose?”Aliongea Roma baada ya kuona Rose anamwangalia Roma kwa macho yasio ya kawaida.

“Huyu mwanamke mremo uliekuwa unaongea nae , niambie ukweli na yeye ni mpenzi wako?”

“Babe Rose huyu ni rafiki yang tu , ni kweli ni mrembo lakini sina mahusiano nae kabisa huo ndio ukweli ni rafiki yangu wa karibu sana”Aliongea Roma.

“Ulishindwa vipi kulala na mrembo kama huyo ulipokuwa nje ya nchi kama ni rafiki yako , ilihali wanaume wengi wanatamani hio nafasi?”

“Haha.. ni kweli lakini mimi sina njaa ya kila mwanamke, au naonekana kuwa na njaa ya wanawake?”Aliongea Roma na Rose alibetua mdomo na kushindwa kujibu swali na Roma alimsogelea na kisha kumbusu.

Baada ya taratibu za Rose kusaini mkataba wa uwekezaji wa pesa zake ndani ya kampuni ya Roma , aliaga kwa ajili ya kuondoka , lakini Roma hakutaka kabisa kumwacha mrembo huyo kuondoka peke yake na aliamua kumsindikiza.

“Rose mpenzi sijawahi kukununulia zawadi yoyote , leo nataka nikakufanyie Shopping”Aliongea Roma na Rose tabasamu lilimtoka ni kweli Roma hakuwahi kumpa zawaidi na pia hakuwahi kujali juu ya hilo , lakini kwasababu Roma alikumbuka mwenyewe juu ya hilo alijikuta akifurahi kweli na kuona Roma anampenda.

Roma aliendesha gari mpaka mlimani City sehemu ambayo aliona inafaa kwa ajili ya kumfanyia shopping mchepuko wake Rose , hakuwa na wasiwasi kabisa baada ya kuegesha gari na alikuwa amependezana na Rose kiasi cha kupelekea hata waliokuwa ndani ya eneo hilo kuwaonea wivu , kwa jinsi walivyokuwa wakionekana hakuna mtu ambaye anaweza kusema Roma ana mke na yupo kazini akipambana , Roma alionekana kujiachia mbele ya Rose na kumfanya mrembo huyo kutabasamu.

Roma aliingia kwenye duka la nguo za kike ndani ya duka kubwa lililopo hapa mlimani duka la Singa fashion Wear, walianza kuchagua mavazi mbalimbali na kila Rose aichopenda Roma alitoa maelekezo kwa muhudumu ndani ya duka hilo kukichukua na kuhifadhi kwa ajili ya Kwenda kujaribisha , na iliwachukua takribani lisaa mpaka kumaliza na hapo ndipo Roma a Rose walipohamia upande wa duka la viatu vya kike na kuanza kumchagulia Rose.

“Nimekipenda hiki babe ni kiatu kinachotamba sana mjini kwa sasa”Aliongea Rose na kukichukua na kujongea mpaka kwenye sofa kwa ajili ya kujaribu , hakutaka kujaribu hapo hapo kwani nguo aliokuwa amevaa ni fupi na kama angeinama basi wanaume waliokuwa nyuma yake wangeona vyote vya siri.

“Leta nikusaidie kukuvalisha”Aliongea Roma na kuchukua viatu vile kwenye mikono ya Rose na kisha alichuchumaa kwa ajili ya kumvalisha tukio ambalo lilifanya wanawake waliokuwa hapo ndani kuona wivu jinsi Rose anavyojaliwa na mpenzi wake.

Wakati Roma akiwa bize kumvalisha Roma , mara macho ya watu yaligeuka upade mwingine baada ya mwanamke mrembo kuingia ndani ya eneo hilo la Mlimani City kwenye duka hilo hilo la viatu.

“Miss karibu sana”Aliongea muhudumu wa duka hilo na kumfanya hata Roma kugeuka na hio yote ni mara baada ya kuhisi pafumu ya bei mbaya anayoifahamu , moyo wake ulipiga kite na kugeuka nyuma na hapo ndipo macho yake yalipogongana na mke wake Edna na hakuelewa Edna alikuwa akifanya nini muda huo ndani ya maduka hayo kwani aliamini muda huo angekuwa kazini.

Kwa upande wa Edna hivyojivyo hakuamini kama mwanaume aliekuwa mbele yake anaemvalisha mwanamke mrembo kiatu ni yule mume wake ambaye alikuwa akiamini muda huo alikuwa kazini akiendelea na majukumu yake.















SEHEMU YA 277

Haikueleweka Edna alikuwa ndani ya eneo hilo la Mlimani City kwa ajili ya kufanya nini, alimwangalia Roma aliekuwa anamvalisha Rose kiatu kwa sekunde kadhaa na kisha alisonga mbele pasipo ya kuongea neno , ni kama alimpuuza Roma.

Upande wa Rose mwenyewe hakuwahi kuonana kabisa na Edna na kwa na siku hio ndio kwa mara ya kwanza anaonana nae na alihusudu urembo aliokuwa nao mwanamke wa Roma na alijiambia hakuwa akiingia kwa chochote kwa mke mkubwa , lakini licha ya mke mkubwa kuwa mrembo lakini aliogopeshwa mno na macho yake.

“Roma nadhani hatukupaswa kuja hapa , nimekuwa na bahati mbaya sana na mke wako kwa siku ya kwanza”Aliongea Rose lakini Roma aliishia tabasamu na kumalizia kumvisha Rose kiatu mpaka akamaliza.

“Babe Rose naona umependeza sana”Aliongea Roma huku akimwangalia Rose kwa tabasamu , lakini Rose alishindwa kumuelewa kabisa Roma , kwani yeye anazungumza swala la mke wake lakini yeye analipotezea.

“Rose najua una wasiwasi na mke wangu , ila hilo lisikuumize kichwa unapaswa kuwa na amani , mimi ndio nimekuleta hapa na huna makosa yoyote , mimi nitatafuta namna ya kuyamaliza na Edna”Aliongea Roma na Rose alitabasamu , kwanza mpaka hapo alishukuru kwa kitendo cha Roma kutokumuacha na kumkiimbilia mke wake , kwake swala hilo aliona ni kama heshima ambayo Roma amempa hivyo aliishia kutabasamu.

Upande wa Edna haikueleweka alikuwa amekuja kuchukua nini , lakini ndani ya dakika kadhaa alikuwa akitoka na bahati nzuri hakuweza kuwaona Rose na Roma tena kwani washasogea upande mwingine na tofauti ya sehemu aliowaona , hivyo aliona akaushe na kurudi, alionekana kuwa kauzu kweli , licha ya kwamba jambo ambalo amelishuhudia lilimuumiza lakini alijiambia kwamba anapaswa kuvumilia kwani hakujua namna ya kumdhibiti Roma , hivyo aliona ajue mambo yake.

Edna baada ya kurudi ofisini kwake alikaa kwenye kiti chake na kisha kuvuta pumzi nyingi na kisha alichukua mkoba wake alioingia nao na alitoa kasha la plastiki ambalo linatumika kuhifadhia nyaraka na kisha alitoa bahasha iliokuwa ndani ya kasha hilo na alifungua ndani yake na kutoa baadhi ya karatasi na kuanza kuzisoma moja baada ya nyingine kwa umakini mkubwa, takribani dakika kama ishirini hivi alitumia kusoma karatasi hizo na alijikuta akifikiria kitu na hapo hapo alitoa simu yake na kutafuta jina la Athena.

“Amiri kuna kazi mpya nataka kuwapa muifatilie kwanzia sasa”Aliongea Edna kwa sauti yake kavu.

“Ndio boss nakusikiliza”

“Nataka mfuatilie kwanini Serikali ilivunja mkataba wa ujenzi wa jengo la Bima ya Taifa na Vexto Construction mwaka 2014 ilihali jengo hili lilikuwa kwenye hatua za mwisho za ujenzi”

“Sawa boss , kuna taarifa nyingine ya ziada ambayo inaweza kutupa mwanga?”Aliuliza Amiri aliekuwa akiongea kwa simu na Edna aliinua karatasi zilizokuwa kwenye meza na kisha kuziangalia.

“Mnaweza kuanza kuchunguza kampuni ya INNOVA na MAYA juu ya uhusikaji wao katika hili, nahitaji pia maelezo kwanini jengo lilichukua miaka mingi kumalizika ilihali lilikuwa kwenye hatua za mwisho wakati Vexto wanavunja mkataba”

“Sawa boss nitalifanyia kazi kwanzia sasa”

“Swala hili lifanyike kwa siri sana na kwa weledi mkubwa”

“Sawa boss” Na simu palepale ilikatwa. Na mlango ulifunguliwa na akaingia Monica katibu wake.

“Boss kuna mgeni mapokezi anahitaji kuonana na wewe kwa shida binafsi”Aliongea Monica kwa heshima na kumfanya Edna ashangae kwani hajazoea kuonana na watu wenye shida binafsi muda wa kazi.

“Amejitambulisha kwa jina gani?”

“Desmond Jeremy”Aliongea Monica na Edna alijikuta akishangaa , alikuwa akimjua Desmond , lakini hakujua kwanini amekuja mpaka kwenye kampuni yake.

“Mwambie sipokei wageni wenye shida binafsi muda wa kazi”

“Sawa boss”Aliitikia Monica na kutoka.

Siku hio Desmond ni kama alifanya makusudi kabisa , kwanza kabisa alfika ndani ya eneo hilo la kampuni na gari aina ya Roll Royce ya mwaka 2022 , gari ambayo inaaaminikuka kuwa na thamani ya shilingi bilioni mbili za kitanzania , kitu cha pili ni kama alivunja kabati kwani alikuwa amependeza kweli kuliko isivyokuwa kawaida na cha ajabu Zaidi alikuwa amebeba ua zuri siku hio na alitoka nalo kwenye gari na kufanya kila mtu kuona ua hilo zuri alilobeba.

Kampuni ya Edna ilikuwa inaongoza kuwa na wafanyakazi wa kike , hivyo kitendo kile kilivutia sana wanawake hao na kujiuliza HB huyo alikuwa hapo ndani kwa ajili ya nani, kila mmoja mwanamke mrembo alitamani awe kwenye nafasi ya kupewa ua ambalo limeshikiliwa na Desmond.

“Samahani kaka nikusaidie nini?”Aliuliza mtu wa mapokezi chini kabisa ya jengo hili na kumfanya Desmond kutabasamu.

“Nipo hapa kwa ajili ya kumuona Edna Adebayo”Aliongea Desmind kwa kujiamini na kumfanya hata mhudumu kushangaa na mpaka hapo aliamini huenda Desmond ndio mpenzi wa boss wake Edna , mwanamke mrembo sana ambaye siku zote kila mmoja ya mfanyakazi alitamani kujua mwanaume anaetoka nae kimapenzi na kwa muonekano wa Desmond aliamini wanaendana kabisa , kwanza mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa na pesa , pili alikuwa na mvuto mkubwa sana kiasi ambacho hata yeye angejitoa kwa usiku mmoja kwa mwanaume huyo kama angemtaka, mwanadada wa mapokezi licha ya kwmaba mwanaume aliekuwa mbele yake hakuwa akimfahhamu vizuri , lakini pia licha ya kuvutia kwake hakutaka kabisa kuvunja taratibu za kampuni kwa ajili yake na alitanguliza taaluma yake.

“Kaka samahani , unamiadi nae?”

“Sina miadi nae , lakini kama utamwambia Desmond mume wake mtarajiwa yupo hapa ataniruhusu kumuona”Aliongea Desmond na kuzidi kumpagawsiha mno mwanadada wa mapokezi na baada ya kuona mwanaume huyo ni mwenye kujiamini na haonyeshi ishara yoyote ya kuwa mgonjwa wa akili , ilibidi afanye hima kuwasiliana na katibu Muhtasi wa Edna ili kujaribu kuuliza

“Hello Monica , kuna mgeni wa boss anafahamika kwa jina la Desmond hapa mapokezi”Aliongea mwanadada huyo kwa Kiswahili safi.

“Anashida gani na boss?, Binafsi au kikazi?”Aliuliza Monica na Mwanadada yule alimwangalia Desmond na kuona kabisa huyo mwanaume yupo kwa shida binafsi.

“Binafsi”

“Okey! Subiri niwasiliane nitakupatia jibu”Aliongea Monica na ndani ya dakika chache simu ya mapokezi iliita na akapokea.

“Mwambie boss hapokei watu binafsi muda wa kazi”Aliongea Monica na kisha kukata simu na mwanadada wa mapokezi alimwangalia Desmond kwa namna ya huruma.

“Boss amesema hapokei watu kwa shida binafsi”Aliongea mwanadada wa mapokezi na kumfanya Desmond kutoa tabasamu la uchungu.

“Usijali mrembo , mke wangu namfahamu ni mchapa kazi na asubuhi niligombana nae , nitamsubiri hapa mpaka atakapotoka”Aliongea Desmond.

“By the way kuna huyu mfanyakazi anafamika kwa jina la Roma Ramoni , yupo hapa kazini?”Aliulizia Desmond na mwandada yule alifikiria.

“Mr Roma ni Director wa Vexto Media na hafanyi kazi hapa makao makuu”Aliongea na Desmond alitabasamu na kisha alijongea mpaka eneo la Kantini kwa ajili ya kumsubiria Edna , alijiambia pasipo ya kumuona Edna haondoki siku hio.

Ukweli ni kwamba alikuwa akijiamini mno kwasababu moja , kwanza alikuwa akijua wafanyakazi wa Vexto karibia wote hawakufahamu Roma na Edna ni mume na mke na jambo hili lilimfurahisha sana yaani, na alijikuta akiamini maneno ya rafiki yake Elvice juu ya Roma kutopendwa na Edna na wameoana kwa sababu maalumu ambayo hawakuwa wakiijua , hivyo maneno hayo kwake yalikuwa yakitosaha kabisa na kumpa motisha ya kuendeleza mapambano ya kumpata Edna.

Edna siku hio hakutoka kabisa hata kula chakula cha mchana , alionekana kuwa bize sana na hata Monica alimpomkumbusha kuhusu chakula alimwagiza amletee Karanga na juisi ya matunda aina ya Apple.

“Desmond!”Aliita CEO msaidizi wa Edna bwana Ernest Komwe baada ya kumuona Desmond.

“Hahaha… Komwe ni wewe , siamini amini”Aliongea Desmond kwa bashasha na wakakumbatiana.

Muda huu ErnestKomwe alionekana ndio anashuka kwa ajili ya chakula cha mchana na ndio alibahatika kuonana na Desmond ambaye alijipa kazi ya kumsubiria Edna.

Walisalimiana na walionekana walikuwa wakifahamiana kitambo sana kwani walikumbushiana baadhi ya mambo ya chuo.

Desmond alijikuta akishangaa na kufurahi kwa wakati mmoja baada ya kugudnua Komwe ni Naibu Mkurugenzi wa kampuni ya Vexto.

“Unafanya nini hapa Desmond?”Aliulizia Komwe huku akiangalia ua lililokuwa kwenye meza.

“Nipo kwenye harakati”Aliongea na kumfanya Komwe kucheka sana.

“Kama zilezile za siku zote?”

“Unakumbukumbu wewe .. hahaha”

“Haha.. ni pisi gani imekutoa Rwanda mpaka hapa Tanzania?”

“Boss Wenu”aliongea Desmond na kumfanya Komwe kushangaa mno.

“Mh! Kazi unayo kijana wangu”

“Kwanini?”

“Yule mwanamke ni kauzu hatari , nikwambie tu licha ya mimi kuwa msaidizi wake lakini nimeongea nae maongezi binafsi mara chache sana , muda wote yuko bize na kazi , siamini kama unaweza kumpata na jambo kubwa nasikia ana mume”Aliongea Komwe kwa sauti ya chini kwani wafanyakazi washaanza kujaa kwa ajili ya kupata chakula.

“Haha… kama ana mume basi mimi ndio nitakuwa mume wake”

“Haha.. si kweli rafiki yangu , Roma Ramoni ndio mume wake, taarifa zote ninazo”Aliongea Komwe na kumfanya Demsond kutabasamu.

“Unaonekana kuwa jasusi wa kujitegemea?”

“Haha.. kawaida sana, Desmond huwezi kumpata Edna , licha ya kwamba nazielewa swaga zako lakini pale jiachie tu, frequency za yule mrembo ili uendane nae itabidi ufe ufufuke au upate maono hahaha..”Aliongea Komwe kama mtu anaemkatisha tamaa , lakini Desmond hakujali kwanza aliamini Komwe hakuwa akimjua vyema Edna, kwake mrembo Edna ashawahi kumpenda na akalijua hilo , hivyo alijiambia ni rahisi sana kumpata kuliko wengine wanavyofikiria.

“Nadhani hupaswi kusubiria hapa rafiki yangu , kama kweli unataka kumzawaida hilo Ua basi kasubiri kwenye eneo la maegesho kwani anashuka na Lift yake binafsi mpaka maegeshoni kwake”Aliongea Komwe na kumfanya Desmond kushukuru.

Saa kumi kamili Edna akiingia eneo la maegeso ya magari kwa ajili ya Kwenda nyumbani alijikuta akishangaa baada ya kumuona mwanaume kaegamia gari yake , baada ya kumwangalia vizuri aligundua ni Desmond na alishangazwa imekuwaje walinzi wakamruhusu kuingia eneo la kwenye maegesho yake binafsi.
 
SEHEMU YA 278

Edna ambaye hakumhofia Desmond alisogea kwa hatua za taratibu lakini za kupendeza mpaka akalikaribia gari lake na pasipo ya kutaka kuongea lolote alifungua gari lake kwa ajili ya kuingia.

“Edna..!!”Aliita Desmond na kumfanya Edna ashangae baada ya kugundua Desmond kapiga magoti chini.

“Unafanya nini Desmond?”

“Nipo hapa kwa kukuomba msamaha Edna kwa kilichotokea siku ile mpaka ukakasirika , hayakuwa makusudi yangu bali ni hisia ndio zilinifanya kuwa vile”Aliongea Desmond na kumfanya Edna kukumbuka siku ambayo Demsond alilazimisha kumkiss.

“Kama limekuleta hilo basi jua kwamba halipo kwenye kichwa changu hivyo simama na uende kwa amani”Aliongea Edna na kisha aliweka mkoba wake kwenye gari.

“Edna kama ni kweli umenisamehe , basi naomba uchukue hili ua kama ishara ya kunisamehe”Aliongea Goodman akiwa amepiga magoti vile vile na kumfanya Edna kukosa utulivu na alishukuru eneo hilo lilikuwa likitumika kuegesha magari ya wafanyakazi wakubwa tu wa kampuni , la sivyo ingemletea shida.

Edna baada ya kufikiria kwa dakika kadhaa , alifanya maamuzi ya kuchukua ua hilo kutoka kwa Desmond ili kuonyesha ishara ya kwamba amesameheana nae , ili wawe na amani.

“Desmond nishakwambia tayari kwamba nimeolewa na uache matendo yako ambayo hayana maana kwangu tena , kwa heri”Aliongea Edna na Desmond alitabasamu na kisha akatingisha kichwa kuashiria kuwa anakubaliana nae.

Edna alitoa gari yake taratibu na kupotea kwenye macho yake na kujikuta akisimama na kushika kiuno.

“Edna nisipokuvua nguo ya ndani labda sio mimi Desmond , kwasasasa ndoto zangu zote ni kukuvua nguo na nitahakikisha hilo nalitimiza kwa namna yoyote ile , hakuna sababu ambayo itanifanya kughairisha matamanio yangu”Aliongea Desmond.

“Mzee wa harakati usifikirie sana haha.., nimekusaidia kuchukua kapicha kako ukiwa umepiga magoti”Ilisikika sauti upande wa nyuma na kumfanya Desmond kugeuka na kukutana na sura ya Komwe.

“Mshenzi wewe kwahio ulikuwa ukinipeleleza?”

“Umekosea mwanaharakati , mimi narejea home na gari yangu ile pale”Aliongea Komwe na kumfanya Desmond atabasamu na kumwambia amuonyeshe hio picha.

“Sio mbaya una akili muda mwingine , kama vipi nirushie hio picha kwenye watsapp yangu inanifaa kwa matumizi ya baadae”Aliongea Desmond huku akiangalia pucha ya Edna akiwa ameshikilia ua alilompa kama zawadi huku yeye akiwa amepiga magoti.

Baada ya Desmond kiongea hivyo aligeuka na kutoka eneo hilo la maegesho kwa ajili ya kutafuta gari lake na hio ni baada ya kumtajia Komwe namba yake ya Watsapp.

Komwe baada ya kuingia kwenye gari lake aina ya Range , alifungua upande wa watsapp na kutafuta jina la Bosss na kisha alienda mpaka upande wa kupandisha picha(Upload) na kuselect picha ya Desmond na Edna na kisha akaituma kwa mtu mwenye jina la boss na ndani ya dakika chache vijivema vya Blue vilionekana na hakujibiwa Zaidi ya kupigiwa na mtu aliekuwa anamwita Boss.

“Komwe sijakuingiza ndani ya kampuni ya Vexto kwa ajili ya kufuatilia mambo ya kijinga’Ilisikika sauti ya mwanamke upande wa pili ikimfokea.

“Nisamehe Boss , lakini swala hili niliona ni vyema kama utalifahamu kwani unajua fika mahusiano ya Edna na Desmond”

“Kwahio kama kuna mahusiano wewe inakuhusu nini, mimi sina shida yoyote kama Edna na Kaka yake watatiana , ninachotaka ni mipango yangu kukamilika na ndio maana upo ndani ya kampuni kama CEO msaidizi, sijui unanielewa?”

“Ndio boss nimekuelewa”

“Nieleze maendeleo ya kazi”

“Kila kitu kinaenda sawa boss, nimeweza kutega vinasa sauti ndani ya ofisi ya Edna na sasa natafuta nyaraka muhimu”

“Good endelea kufanya kazi yako kwa siri kubwa , ukifeli jua ndoto zako haziwezi kutimia kwa namna yoyote ile na utaendelea kuishi masikini Maisha yako yote, ninachohitaji kwa namna yoyote ni hizo nyaraka , zikipatikana hizo Edna hatakuwa tena na uhalali wa kumiliki kampuni ya Vexto kisheria”

“Naelewa Boss”

“Fanya kinachokuhusu , achana na mtoto wangu Desmond , kama amempenda Edna sina kipingamizi na nitamsaidia kumpata kama ndio kitu kitakacho mpa furaha”Komwe alishangaa mno na kisha akatikia ndio na kisha simu ilikatwa.

“Dammit , Huyu mwanamke ni shetani sijapata ona , inabidi nifanye kinachonihusu la sivyo anaweza kuniondoa duniani muda wowote”Aliwaza Komwe na kutafuta namba ya Desmond na kutuma zile picha.

Edna ile anafika Sellasie Road alitupa nje lile ua na kuendelea na safari yake ya kurudi nyumbani.

*******

Saa kumi kamili ndio muda ambao Roma alirudi nyumbani , huku kwenye kichwa chake akifikiria namna ya kuyajenga na mke wake Edna , tukio lililotokea asubuhi aliamini lingewafanya wawili hao kuwa katika mgogoro jambo ambalo hakuwa akitaka litokee.

Ukweli ni kwamba Roma hakuwa na mpango wowote kabisa wa kiuachana na mwanamke wake yoyote yule , alijiambia ni labda wanawake ndio waanze wao kumuacha , lakini kama wataendelea kumpenda basi atajitahidi kwa uwezo wake wote kuwafanyia kile kilichopo ndani ya uwezo wake , kuhusu mke wake Edna aliamini kwamba yeye hana maamuzi yoyote ya kufanya na ni juu ya Edna mwenyewe kukubaliana kwamba mume wake yeye ana wanawake nje na anapaswa kuwakubali hivyo hivyo na kuendana nao vizuri , jamaa huyu alitamani kwamba Siku moja michepuko yake yote ipatane na mke wake na kuishi Maisha ya amani kabisa kama mfalme Sulemani wa kwenye biblia.

Kuhusu mawazo hayo alijikuta akijicheka mwenyewe kwani swala hilo lilikuwa ni gumu sana kutekelezeka na litategemea maamuzi ya Edna.

Roma aliona gari ya mke wake na kuridhika baada ya kuona yupo nyumbani, aliingia sebuleni a kukutana Zogo la Sophia na Bi Wema ambao walikuwa wakibishana kuhusu maswala ya Tamthilia , Yezi kwa upande wake yeye alikuwa tayari ni mwanachuo wa UDSM na ni yeye aliempeleka siku ya jumatatu kwa ajili ya kufanya usaili.

Roma alisalimiana na Bi Wema na Sophia na kisha alijongea juu ghorofani na Kwenda kusimama kwenye chumba cha mke wake Edna na kisha akagonga kwa dakika kadhaa pasipo mlango kufunguliwa na alijaribu kusukuma na kukuta mlango umefungwa kwa ndani na akaamini mke wake atakuwa amelala na kuanza kuondoka , lakini kabla hajapiga hatua ya pili mlango ulifunguliwa na Edna alieonekana kuvaa vazi la kulalia , vazi ambalo kama ni mwanaume mwenye uchu basi ungeteseka sana kwa kumuona mrembo huyo , Edna mwenye macho ya usingizi alimwangalia Roma kwa macho ya kawaida, macho yasio na hasira wala furaha.

“Babe Wife umeshindaje?”Alisalimia Roma.

“Safi”Aliitikia Edna na Roma alitabasamu na kisha kumwagalia Edna aliekuwa anavutia kwenye macho yake na palepale alifanya mamuziya kumsogelea Edna kwa ajili ya kumkumbatia na kumbusu , lakini aliishia kubusu mlango kwani Edna aliufunga tena kwa funguo kabisa kwa ndani na Roma alitabasamu kwa uchungu na kisha alitembea mpaka kwenye chumba chaka na kuingia ndani kwa ajili ya mapumziko.

******

Upande mwingine ndani ya maabara , ambayo Yan Buwen anafanyia kazi , bwana huyu alionekana kuwa ni mwenye hasira kweli na hio ni mara baada ya kupima damu ya Denisi na kukuta haikuwa na chembechembe zoazote za damu ya Roma , Yan Buwen mpango wake ulikuwa ni kupata damu ya Roma ambayo ilikuwa na mfumo wa DNA za tofauti na binadamu wa kawaida , ili kupitia damu hio aweze kufanya ‘Cloning’.

Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba mpango wa Yan Buwen ni kupata damu ya Roma ili aweze kutengeneza kiumbe kinachofanana na Roma kwa asilimia mia moja na akifanikiwa hilo atumie jiwe la kimungu kukipa kiumbe hiko nguvu ya kupambana na Roma.

Yaani alitaka Roma apambane na sura yake mwenyewe na teknolojia hio ya kuzalisha kiumbe kinachofanana yaani kopi inaitwa Human Cloning.

Sasa mpango wake huo ulishindikana kabisa kwani matibabu ambayo alipatiwa Denisi yalikuwa ya tofauti kabisa na kile alichotarajia, yeye aliamini Roma angetumai damu yake katika mwili wa Denisi , lakini kwa jinsi damu ya Denisi ilivyokuwa ikionekana katika vifaa vyake aliona kabisa Roma hakutumia damu kumponya Denisi na hili lilimshangaza Zaidi.

Ukweli ni kwamba Denisi alikuwa amekwisha kupona kabisa na alikuwa akiendelea na kazi zake kama kawaida , lakini licha ya yale ambayo yamemkuta hakuwa ametulia kabisa na wala ndoto yake ya kumuua Roma haikuwa imeisha kabisa na ndio maana alimtafuta tena Yan Buwen.

Sasa asichokijua Denisi ni kwamba Yan Buwen alikuwa akimtumia tu ili kukamilisha mipango yake ya kuweza kutmia jiwe la kimungu katika miili ya binadamu, hata kumtuma Denisi Kwenda kumshambulia Roma ilikuwa ni sehemu ya mipango yake na Denisi yeye kwakua alikuwa akimwamini Yan Buwen kama mwanasayansi, aliamini Yan Buwen ni rafiki yake na wanasaidiana kupambana na adui wa aina mmoja yaani Roma Ramoni.

Sasa siku ambayo Denisi alikutana na Yan Buwen kwenye hoteli ya Serena ndio alitumia wasaa huo kuchukua kiasi cha damu ya Denisi kwa ajili ya Kwenda kupima na sio kwamba Yan buwen aliomba hio damu kwa Denisi , la hasha, Denisi mwenyewe kumtafuta Yan Buwen na kutaka kujua kama anaweza kupata tena uwezo wake na Yan Buwen ndio alimpa maelekezo kwamba ni mpaka akapime damu yake na hapo ndio zoezi la Yan Buwen kuchukua damu ya Denisi likafanikiwa.

“This is real Strange , I underestimated him and I screwed up but nothing to worry, I am genius Yan Buwen, man of many options , plan A failed, Plan B failed let activate Plan C”

“Hii inashangaza , nilimdharau na nilifanya makosa , lakini sina wasiwasi , mimi ndio jiniasi Yan Buwen mwanaume mwenye chaguzi nyingi , Mpango namba A umefeli , mpango namba B umefeli , ngoja nianzishe mpango namba C”Aliongea Yan Buwen huku akiweka tabasamu lake la kifedhuli na kisha alitoka kwenye maabara hii ya kisasa kabisa , maabara ambayo ilikuwa ikitumiwa na Profesa Shelukindo lakini pia maabara ambayo imejengwa na raisi wa Marekani mheshimiwa Barrack Mabo.

Yan Buwen baada ya kutoka kwenye maabara hio moja kwa moja alimpigia simu mheshimiwa Kigombola kuhitaji kuonana nae na mhesimiwa alimpa taarifa kuwa yupo nyumbani na anaweza Kwenda na Yan Buwen hakujali sana , aliingia kwenye gari yake na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa mheshimiwa Kigombola.

Saa kumi na moja kamili siku hii ya Ijumaa ndio Yan Buwen alifika nyumbani kwa mheshimiwa Kigombola na alipokelewa kwa bashasha na mheshimiwa.

“Nieleze Mr Yan Buwen , ni jambo gani ambalo unataka kuzungumza tena na mimi, kwa nilivyosikia ni kwmaba Denisi yupo hai mpaka sasa , ikimaanisa kwamba mpango umefeli”

“Ni kweli mheshimiwa mpango A umefeli lakini pia mpango B ulifeli”Aliongea na kumfanya mheshimiwa kushangaa kidogo.

“Kulikuwa na mpango B?”Aliuliza.

“Ndio mpango B ulikuwepo”Aliongea Yan Buwena na kuanza kumuelezea mheshimiwa Kigombola namna ambavyo alitaka mpango B uende.

“Kwahio mpango wako B ulikuwa ni kutaka kupata Damu ya Roma?”

“Ndio mheshimiwa Mstaafu , nataka damu ya Roma kwa namna yoyote ile na huo ndio mpango wa sasa na lazima ufanikiwe”

“Kwanini unataka damu ya Roma? Ni mpango ngani upo nao tena?”

“Nahitaji kumtegeneza Hades mwingine”Aliongea huku akitabasamu kifedhuli na kumfanya mheshimiwa kushangaa , kumbuka mheshimiwa Kigombola alikuwa mwana siasa tu na hakuwa na uelewa mkubwa sana juu ya maswala ya kisayansi , hivyo swala la kutegenezwa Roma mwingine aliona ni jambo ambalo haliwezekani labda Mungu aingilie kati.

“Kigombola hupaswi kushangaa, ukiwa na ushirikiano na mwanasayansi kama mimi basi jihehasabie upo hatua moja nyuma kuitwa Mungu”Aliongea Yan Buwen na kumfanya mheshimiwa kukunja ne.

“Sawa Mr Yan , lakini hili swala linawezekanaje?”

“Human Cloning technology Mr Kigombola”

“Ndio nini?”
 
SEHEMU YA 279

“Human Cloning ni aina ya sayansi ambayo inatumia DNA za mwili kutengeneza kopi halisi ya mtu husika kwa njia ya ‘Somatic cell nuclear transfer’ and Pluripontent stem cell induction”Aliongea Yan Buwen na kumfanya Kigombola asielewe chochote.

“Okey Mr Yan kama kweli swala unalozungumzia linawezekana , je ni mpango gani ambao unao baada ya kumpata Roma mwingine?”

“Hahaha… kama nilivyosema Mheshimiwa mstaafu , mpango wangu ni kama mpango wako, wote tunataka kumuangamiza Roma na kwa uwezo aliokuwa nao haliwezekani kwa sasa labda mpaka nitakapoweza kugundua teknolojia kubwa Zaidi kupitia tafiti za Profesa Shelukindo , ninachokifanya ni kumfanya Roma kupambana na sura yake mwenyewe , nitamtegeneza Roma mwingine ambaye anauwezo kama wake na hapo ndipo mpango wangu utaweza kufanikiwa kwa asilimia mia moja”

Mheshimiwa Kigombola alijikuta akishangaa mno na alianza kuanza kumuogopa Yan buwen , kwani swala ambalo anamwambia muda huo ni swala zito kabisa , hakuweza kujua kama ulimwengu ulikuwa umepiga hatua kubwa namma hio katika maswala ya kisayansi.

“Mheshimiwa nataka unisaidie katika mpango wangu C wa kuhakikisha napata damu ya Hades”aliongea na kumfanya Mheshimiwa kumwangalia.

“Kivipi?”

“Nataka kumtumia Neema Luwazo kwenye mpango C”Aliongea Yan Buwen na kumfanya Kigombola kutoa macho.

“Neema Luwazo , unamfahamu vipi Neema?”Aliongea na Yan Buwen alitabasamu kifedhuli.

“Namjua Neema kama moja ya mwanamke wako , lakini pia mwanamke ambaye hivi karibuni umepokonywa na bwana Roma Ramoni, kabla sijaja Tanzania nilikuwa na taarifa za kutosha ,Mheshimiwa usinichukulie poa mimi ni taaisisi kama ilivyokwako”Aliongea Yqan Buwenna kumfanya Mheshimiwa kuvuta pumzi.

“Unataka kumtumia vipi Neema?”

“Mpango ni mwepesi sana na kwa kupitia Neema hakuna ambacho kinaweza kushindikana” aliongea Yan Buwen na kisha alitoa simu yake kubwa na kisha Kwenda upande wa picha na kumpatia mheshimiwa Kigombola

“Huyu..!!!”Mheshimiwa alijikuta akivuta pumzi na kuzishuha na kumwangalia Yan buwen machoni.

“Najua mahusiano ya Neema na huyu mtu na nitahitaji uhusikaji wako katika hili”Aliongea na kumfanya mheshimiwa kufikiria.

“Nipe mpango ndio nitaamua”Aliongea na Yan Buwen alimpa ishara mheshimiwa ya kumsogelea na kuanza kumuelezea kila kitu kwa sauti ya chini kabisa na mpaka anamaliza mheshimiwa jasho lilianza kumtoka.

“Mh! Huyu Yan Buwen ni uzao wa shetani kamili”Aliwaza uku akifuta jasho na kitambaa huku mwili ukimsisimka kwa maneno alioambiwa. Ila Yan Buwen alikuwa akitabasamu kifedhuli na alionekana kujiamini kwa asilimia kubwa.

“Upo tayari mheshimiwa?”

“Nipo tayari”Aliongea na kumfanya yan buwen kutabasamu.

*********

Upande mwingine ndani ya maabara ilioko ndani ya bara la Antarctica anaonekana mrembo Naira akiingia ndani ya chumba maalumu ambacho kinahifadhia makabati ya kuhifadhia miili kwa teknolojia ya Cryosleep.

Mrembo huyu ambaye alikuwa amevalia mavazi ya kitabibu , alionekana kuwa na wasiwasi mwingi mara baada ya kuingia ndani ya chumba hiki, baada ya kufika katikati, mwanga wa rangi ya ‘Aqua’ ulimulika chumba kizima na kumfanya kuona masanduku yote matatu ambayo yapo ndani ya hiko chumba.

Alipita kila sanduku pasipo kufungua na kusoma maandishi yaliokuwa juu ya masanduku hayo , sanduku la kwanza lilisomeka jina la Hades na ndani yake kulikuwa na mwili, sanduku la pili lilikuwa la Seventeen na ndani yake kulikuwa na mwili , sanduku la tatu kulikuwa na jina la ‘Gaia’ lakini ndani yake hakukuwa na mwili , mwanadada huyu alisimama kwenye sanduku hili na kujiuliza kwanini kuna jina juu ya hilo sanduku lakini ndani yake hakukuwa na mwili kama masanduku mengine.

Wakati akiendelea kushangaa na kujiuliza maswali , mara mlango wa chumba hiki cha teknolojia ya Cryosleep ulisukumwa na alionekana mwanamke mrembo Athena alievalia mavazi ya kawaida , gauni rangi nyeupe lililomfikia magotini huku akiwa hajavaa chochote kwenye miguu yake na mkononi ameshikilia glass mbili za wine.

Naira aligeuka na kumwangalia Athena na kisha alitabasamu na kugeuza macho yake kwenye sanduku ambalo halina mwili ndani yake, ukweli ni kwamba Naira licha ya kwamba yupo hapo ndani kwa Zaidi ya miaka sasa , hakuwahi kupewa maelezo juu ya baadhi ya masanduku na taarifa alizokuwa nazo ni za kwenye sanduku la Seventeen tu , kwani alikuwa akifahamu kwamba Athena alikuwa na mpango wa kutumia mwili wa Seventeen hapo baadae kama ilivyokuwa tabia yake mwili wake ukizeeka hufanya ‘Transmigration’

Athena alitabasamu na kisha alimsogelea Naira na kisha akamkabidhi Glass iliojaa wine.

“Nimekuona ukikodolea sana sanduku hili ambalo halina mwili bali lina jina juu yake?”Aliuliza Athena na Naira alitingisha kichwa kuashiria kwamba ni kweli na Athena alitabasamu na kisha akazunguka upande wa pili wa sanduku hili linalotoa mwanga wa taa nyekundu kwa namna ya kubipu na kisha akamwangalia Naira usoni .

“Gaia was our GreatGrandmother, Mother of our Planet”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa, ukweli ni kwamba mrembo Naira tokea amfahamu Athena alikuwa ashaifahamu historia yote ya miungu ya kigiriki, hivyo mshangao wake haukuwa kwenye maneno ya Athena bali kwaninni Athena alikuwa ametenga jina la Gaia kati ya masanduku matatu.

“Kwaninni umetenga Sanduku lake ilihali mwili wake haupo?”Aliuliza Naira.

“Swali zuri Naira , Nimetengwa sanduku lake kwasababu nahitaji kurudisha uhai wake”Aliongea na kumfanya Naira kuzidi kushangaa na kutoelewa.

“How!!”

“How many Godstones do we have , until now?”

“We do have ten Godstones here”

“Na moja lingine analo Yan Buwen kukamilisha idadi ya madjiwe kumi”Alimalizia Athan ana Naira alitingisa kichwa.

“Katika majiwe yote kumi na mbili moja ndio muhimu sana kangu na kwa misheni yangu kwasababu sio jiwe tu ambalo ndani yake kuna nguvu ya Ant-matter ,bali ndani yake kuna roho ya Gaia”

“I don’t understand Athena”

“Yes you do….”Aliongea na kisha akavuta pumzi.

“Ijapokuwa kwasasa umefanikiwa kujua namna ya kuweza kuitumia nguvu iliopo kwenye Godstone haimaanishi kwamba mafanikio hayo yana maana kwangu , jambo moja ambalo litanifanya kuhisi mafanikio ni pale nitakapo pata jiwe la mwisho ambalo tulilipoteza , jiwe hili ndio pekee ambalo litaweza kunipa nguvu mimi ya kutawala roho za ndugu zangu lakini pia kujenga koneksheni na Roho zilizomezwa na binadamu”Aliongea kwa sauti yake ndogo inayovutia.

“Kwahio unamaanisha roho ya Gaia ipo ndani ya Godstone na kupitia roho hio ndio itakuwezesha kuwa na nguvu ya kuongoza miungu mingine , namaanisha ndugu zako?”

“Ndio, na sio kwa ndugu zangu tu ambao nilikuja nao hapa duniani bali hata kwa binadamu, nitaweza kuziendesha akili zao na wataweza kufikiria kama ninavyofikiria mimi na kufanya ninachotaka wafanye”Naira hakushangaa sana kwani mpaka muda huo alikuwa anajua mipango ya Athena , mipango ya kutawala dunia na kuanzisha dini moja tu ambayo binadamu wote wataweza kuabudu na ili aweze hilo ndio huo mpango wa kutaka kuzitawala akili za binadamu.

“How about Hades, He is related to you, Why in Cryosleep?”

“Hades kazi yake ilishaisha zamani tokea siku ambayo aliweza kumtambua binadamu mwenye vinasaba vya damu tofauti na binadamu, matokeo ya Seventeen na Roma Ramoni , Hades aliamini ni mpango wake lakini asichokijua ni kwamba alikuwa akifanya yote kwenye mtego niliomuwekea”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa.

“Hades anaamini mpango LADO ulifanikiwa kwasababu yake, lakini ambacho hakuwa akikifahamu ni kwamba nilimuwekea mtego ili kunisaidia kufanikisha mpango LADO, I used his brain to achieve what I want and all his plan was my goals and I am only one who understand what is turning point”

“Turning Point?”

“Yes!, like reverse point”

“What do you mean?”Athena alitabasamu.

“Ni rahisi sana Naira kuelewa , jaribu kujichhukulia mfano wewe mwenyewe , najua upo hapa kunisaidia juu ya mpango wangu lakini najua kwenye moyo wako haujawahi kuwa mkweli kwenye kunisapoti na unafikiria wakati ukiwa sahihi uharibu kila nilichokiandaa kwa miaka mingi hio ndio ‘Turning Point’, unakwenda kugueza kila kitu nilichokitengeneza ili kuniadhibu mimi mwenyewe na hivyo ndio nilikifanya kwa Hades”aliongea Athena kwa sauti kavu kidogo na kumfanya Naira kuanza kujawa na woga.

“Sijawahi kufikiria hivyo Athena , I have been of pure heart toward your goals”Aliongea kwa wasiwasi na kumsogelea Athena karibu kwa namna ya kubembeleza

“Naira wewe ni binadamu na asili yenu ni usaliti kwasababu moja tu Mungu aliwapendelea kwa kuwapa uhuru wa kuchagua…”Aliongea lakini Athena alijikuta akiishia njiani mara baada ya Naira kupeleka mkono sehemu za siri za Athena , na kwasababu alikuwa amevalia kigauni chepesi kilichomfikia magotini mkono uligusa sehemu husika na alimfanya Athena kufumba macho.

“Naira…Aisiii….” Aliongea na Naira hakumpa nafasi kabisa Athena alichokifanya ni kupeleka mdomo wake kwenye mdomo wa Athena na kilichofautia ni kudendeka huku Athena akizidi kujawa na hisia , kitendo kilichokuwa kikifanyika ni cha kifirauni.

Dakika chache mbele walihamia eneo ambalo wanatumia kama ‘living Room’ na walianza kufanya matendo ya kishoga kwa takribani nusu saa nzima na walionekana wote kwa Pamoja kuwa katika ulimwengu mwingine kabisa.

“Niambie kwenye sayari yenu ushawahi kuwa na mahusiano na mwanaume?”Aliuliza Naira aliemlaza Athena chini yake, yaani hapa kilichoonekana ni kwamba Athena ndio tuseme ni mwanamke na Naira ndio mwanaume.

“Have you heard about Utopia?”Aliuliza Athena akimwambia kwamba ashawahi kusikia neno Utopia.

“Ndio nimsikia neno Utopia kutoka kwenye kitabu cha Sir Thomas More”

“Ulishakisoma?”Aliuliza na Naira alitingisha kichwa na kusema Hapana.

“Jina la sayari yetu ni Utopia”Aliongea na kumfanya Naira kushangaa mpaka kuacha kufanya alichokuwa akifanya na kumruhusu Athena kuketi kwenye sofa.

“You mean perfect world?”

“Unamaanisha ulimwengu mkamilifu?”

“Yes our world was very perfect”Aliongea na kumfanya Naira kuwa na maswali bado.

“But how possible , the world to be perfect , people differ in many ways, the only word ‘Nature’ can not make the world to be perfect”

“Lakini inawezekana vipi ulimwengu kuwa mkamilifu , watu wana tofautiana kwa mambo mengi na neno ‘Asiri’ lenyewe haliwezi kuufanya ulimwengu kuwa mkamilifu”

“Sio kweli neno ‘Perfect’ mara nyingi halisimami katika wingi bali katika umoja, hio ndio namna ambavyo tuliweza kutafsiri neno Perfect, We all felt perfection in our own ways”

Aliongea Athena kwa kusema kwamba kwenye dunia yao kulikuwa na usawa katika njanja zote kwanzia maswala ya kiuchumi , kisiasa mpaka ya kijamii , binadamu wanaheshimiwa kwa chaguzi zao wenyewe na kulikuwa na sheria inayomlinda kila mmoja kutokana na uchaguzi wake , kwa mfano yeye alikuwa ni shoga huko kwenye dunia yake na alikuwa akiheshimiwa kutokana na uchaguzi wake jambo ambalo ni tofauti sana kwa hapa duniani kwani neno ‘ushoga’ ni chukizo kwa misimamo ya kidini , jambo ambalo anataka kulibadilisha na kuufanya ulimwengu kuwa ‘Modern Utopia’ anasema kwamba kwao mwanzoni dunia yao haikuwa ikiendana na jina Utopia , lakini maendeleo yao na namna walivyoweza kupevuka kiakili ndio walivyoweza kutokuamini katika Mungu asieonekana bali yule Mungu anaeonekana.

“So your goals is to make human abandon invicible God and follow Vicible God?”

“Kwahio malengo yako ni kumfanya binadamu amuache Mungu asieonekana na kumfuata yule anaeonekana”Alitingisha kichwa kukubali.

“Lakini hujanijibu swali langu bado la mwanzo”

“Sijawahi kuwa na mahusiano na jinsia tofauti kwenye sayari yetu na hakuna binadamu ambaye ashawahi kunitenga juu ya hilo kwani wote tuliacha kuamini katika Mungu asieonekana na kuamini katika Mungu anaeonekana, Mungu ambaye alililifanya neno Utopia kuwa katika Umoja na sio Wingi , nataka kumfanya binadamu hapa duniani kwa nafsi yake kuhisi anaishi Maisha yenye ukamilifu ndani yake , ukamilifu ambao utaanzia nafsini na kusambaa sayari nzima na malengo yangu juu ya Modern Utopia yatakamilika, I will be God who satisfy human physicaly and spiritually”Aliongea kwa Kingereza.

Yaani kwa maana nyepesi ni kwamba mpango wake ni kuwafanya binadamu kuacha kumuamini Mungu ambaye yupo katika Imani na waamini Mungu anaeonekana , Mungu ambaye ataweza kukidhi kila hitaji la binadamu , yaani kwa mfano kama kinachompa furaha mtu ni kuwa Shoga basi anaruhusa na mengineyo mengi ambayo binadamu wanayatamani kuyafanya lakini wanaogopa kutokana na kwamba Mungu haruhusu n ani Dhambi.

Mnisamehe kama nimetumia maneno makali , najaribu kuhakikisha simulizi inaeleweka.

Mpango wa Hades wa kumtengeneza Roma kumpiga Athena unaonekana kama ulikuwa mtego wa Athena mwenyewe , kama ni kweli inamaana Hades hakuchukua tahadhari mapema nah io Turning point anayozungumzia Athena ni ipi.

Kuwa na amani simulizi itafika mwisho hii na mwisho wake utaupenda na utajifunza vingi.
 
SEHEMU YA 280.

Ni siku ya pili yaani siku ya jumamosi ilipita na sasa ilikuwa ni siku ya jumapili , Blandina mama yake Roma baada ya kuhisi hali isio ya kawaida kati ya Edna na mke wake Edna aliona awashauri Kwenda wote kwa pamoja kituo chake cha kulelea yatima kutembelea Watoto , huku akitumia kisingizio kwamba Roma anakwenda kumuwakilisha yeye .

Edna ambaye mwanzoni hakupenda wazo hilo alikubaliana na mama mkwe wake , kwani pia sababu yake ilikuwa na mashiko na pia aliona nia halisi ya Blandina kutaka kusuluhisha migogoro yao , hivyo alikubaliana kuongozana na Roma.

Ukweli ni kwamba Edna alikuwa amemchunia kwa asilimia mia moja Roma , tukio la Rose kuvishwa kiatu ilihali Roma hakuwahi kumfanyia hivyo lilimtekenya sana na yeye kama mke alihisi wivu, ile akili yake ya mwanzo kwamba Roma ameoana nae kimkataba ilikuwa ishaanza kupotea kabisa na alitamani sana Roma kutambua nafasi yake kama mke wake na kuacha mambo ya ajabu ya kuwa na wanawake wengi lakini hata hivyo yeye sio mtu wa kulalamika , aliona adhabu pekee kwa Roma ni kumchunia na kutoongea nae kabisa na kujali mambo yake.

Na ni kweli, adhabu yake ilikwa ikifanya kazi vizuri sana kwa Roma , kwani Roma siku yote ya jumapili alitafuta visababu vya kutaka kuongea na Edna , lakini alishindwa kabisa kuongea nae na kuishia kusikia uchungu moyoni , Edna hakumpa hata nafasi ya kutamka neno kwani Edna akishapata chakula atakimbilia chumbani kwake na hata Sebuleni hakupenda kukaa kabisa.

Sasa siku hio kidogo alimshukuru mama yake kumtengenezea nafasi ya Kwenda nae mpaka Kiwangwa, aliona hio ndio nafasi pekee ya kuyajenga na mke wake , lakini licha ya hivyo hakujua ni kwa namna ipi anaweza kumlainisha Edna ambaye alikuwa kama barafu.

“Roma mwanangu sijui umemfanya nini Edna , ila tumia siku ya leo nzima kuhakikisha unamfanya Edna anarudi katika hali ya kawaida , mkeo akitabasamu ni baraka kwa upande wako na usimfanye anune”Hayo ndiomaneno ambayo Blandina alimuasa Roma kabla hawajatoka kuianza safari. na Roma aliitikia kwa kichwa kuonyesha kwamba atalifanyia kazi swala hilo.

Uhusiano wa Blandina na Roma ulionekana kuanza kukomaa na hata lile gepu la miaka mingi lilionekana kuanza kupungua na Roma ashaanza kabisa kumkubali mama yake na yote hayo ni juhudi ambazo Blandina alikuwa akionyesha kwa upande wa Roma , lakini pia ile hali yake ya kujutia kwa makosa yake alioyafanya ,ilimfanya Roma kumuonea huruma mama yake.

Alichotegemea Roma kilikuwa ni tofauti kabisa kwani Edna baada ya kukaa kwenye gari alifumba macho na kuegamia kiti na kulala na kumfanya Roma ashindwe kumuongelesha , alijua yote hio ni janja ya Edna kutotaka kuongea nae.

Ukweli ni kwmaba licha ya Roma kutafuta njia ya kurudisha hali ya Edna kuwa ya kawaida na aache kumnunia lakini kwa upande wake hakuwa na mpango wa kumwambia samahani , aliona neno hilo sio sahihi kabisa kulisema na lingemfanya kuonekana dhaifu , lakini hata hivyo halina maana , neno samahani maana yake ni kwamba sirudii kosa , hivyo yeye akisema hivyo na akirudia hakutakuwa na maana tena.

Dakika kadhaa mbele walikuwa wakiingia kituo cha kulelea Yatima na walipokelewa vizuri na Mama Issa na alifurahi pia kumuona Roma kaja na Edna ndani ya kituo hiko.

“Mama Issa vipi kuhusu Lanlan hajaja kabisa hapa?”Aliuliza Edna na kumfanya Mama issa kumwangalia Edna na kutabasamu.

“Unaonekana kumpenda sana yule mtoto Edna?”Aliongea na Edna aliitikia kwa kichwa.

“Walikuwepo hapa muda si mrefu na mlezi wake”Aliongea Mama Issa na kumfanya Edna kujawa na shauku na furaha.

“Kweli , wako wapi?”

“Edna punguza presha muite kwanza Roma?”Aliongea Mama Issa na kumfanya Edna kugeuka kumwangalia Roma aliekuwa akiongea na watoto na haikueleweka alikuwa akiwaambia nini lakini walionekana kusikiliza kwa umakini.

“Romaa..!!”Aliita Edna kivivu na Roma aliekuwa bize alimwangalia.

“Mama Issa anataka kuongea na sisi”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa , hakuelewa ni jambo fani la Ghafla ambalo mama Issa anataka kuongea nao.

Roma aliwaacha Watoto na kisha alisimama na kumfuata Edna mpaka sehemu ambayo imejengwa kwa ajili ya mapumziko na baada Mama Issa kuona wanandoa hao wamemfikia ilibidi anyanyuke na kuwapa ishara kwamba wamfuate Kwenda ofisini kwake.

Edna alishangaa ni jambo gani ambalo Mama Issa anataka kuongea nao , lakini hakujali sana na waliongozana mpaka ndani ya ofisi.

“Edna nimeongea jana juu ya Maisha yenu kwa ujumla wewe na mumeo..”Aliongea na kisha akaacha na kuwaangalia ni kama alikuwa akiwasoma usoni mapokeo yao na kweli Edna alishangazwa na maneno ya Mama Issa kwani swala la ndoa yake na Roma ni la kifamilia Zaidi.

“Mama Issa unataka kusema nini?”

“Msijisikie vibaya nimeongea na Blandina kwa makusudi maalumu kwani kuna jambo muhimu sana nahitaji leo kuongea na nyie , Roma mama yako hajakuambia nadhani kama nilikuhitaji leo hapa kituoni Pamoja na Edna?”Roma alitingisha kichwa kuashiria ni kweli na Mama Issa alitabasamu.

“Edna nadhani ulishakutana na Master Chi?”

“Master Chi! Mbona simfahamu”

“Namaanisha babu yake Lanlan”

“Ooh! Kumbe anafahamika kama Master Chi , ndio nimekutana nae”Aliongea Edna na kumfanya Roma kukumkumbuka Lanlan.

“Master Chi amekubali uishi na Lanlan kwa muda”Aliongea Mama Issa na kumfanya Edna atoe macho ya mshangao na furaha juu yake.

“Kweli Mama Issa?”Aliongea Edna akishindwa kuificha furaha yake mpaka kumshangaza Roma.

“Ndio maana nikazungumza kuhusu swala la ndoa yenu kwanza, Master Chi alisema upo tayari kumlea Lanlan lakini ameonekana kuwa na wasiwasi”

“Kumlea!!”Aliuliza Roma kwa mshangao kwani hakuwahi kumsikia Edna akiwa na mpango wa kumlea mtoto na hakuelewa kinachomaanishwa na Edna aligundua hilo.

“Mr Roma inaonekana Edna hajakuambia kilichotokea alivyokutana na Master Chi, nimebahatika kufahamiana na Mastar Chi wiki hii lakini amekuwa mchangamfu mno na mtu wa maneno ya moja kwa moja ,alinieleza Edna alikuchagua wewe zidi ya Lanlan”Aliongea Mama Issa na kumfanya Roma kumwangalia Edna hakuelewa vizuri swala la kuchaguliwa na ilibidi Mama Isaa kuongea kila kitu na kumfanya Roma kuelewa sasa na kushangaa huku akimwangalia Edna , hakujua kama Edna siku ile alifanya maamuzi ya aina hio , alijikuta akitabasamu baada ya kugundua Edna alikuwa tayari kumchagua zidi ya Lanlan , lilikuwa jambo kubwa kwake mpaka hapo.

Edna ukweli aliona aibu hakupenda siri hio ijulikane lakini alishindwa kumzuia kabisa Mama Issa kuongea , lakini pia aliamini kama atamzuia Mama issa asiongee basi angeshindwa kupata muafaka wake wa kuishi na Lanlan.

“Edna haina haja ya kuona aibu kumpenda mumeo “Aliongea mama Issa na kumfanya Edna kuona aibu za kike.

“Mama Issa nadhani uende sasa moja kwa moja kwenye swala zima la Lanlan”aliongea Roma maana hakupenda sana maongezi ya kisiasa.

“Okey Mr Roma ni hivi , babu yake Lanlan yaani Master Chi ameridhizia muishi na Lanlan kwa muda wa siku ishirini na tisa, kama atatokea ndani ya siku hizo ishirini na tisa kutoka kwenye safari yake basi atamchukua Lanlan na kama hatotokea ndani ya siku hizo ishirini na tisa basi inabidi mumlee Lanlan kama mtoto wenu wa kumzaa”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa lakini upande wa Edna kufurahi.

“Mimi sikubaliani na swala hili”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwagalia kwa mshangao lakini Mama Issa alionekana kutulia.

“Kama mwanaume ndio una haki ya kukataa , hili swala hamjakaa mkalizungumza kama wanandoa na ndio maana Master Chi alipitia kwangu kabla ya kuja kwenu moja kwa moja, nitawapa muda mjadiliane kama mtafikia maamuzi ya kutotaka kumlea Lanlan basi kituo hiki kitamlea na kumpa huduma zote stahiki akiwa chini ya mlezi wake Qiang Xi, Roma swala hili nimezungumza na Mama yako na amesema anawaachia maamuzi nyie wenyewe”Aliongea.

Roma aliamini kama atakubali Edna amlelee Lanlan inamaanisha kwamba anaweza asimpe kabisa kitumbua na asingeweza kupata mtoto wake halali wadamu yake , hivyo swala la kulelea ilihali wana uwezo wa kuzaa aliona ni la ajabu.

“Nitawaacha muongee”Aliongea Mama Issa na kisha alisimama na kutoka kwenye ofisi hio ili kuwapa nafasi Roma na Edna wajadiliane kuhusu mustakabali wa Lanlan kama watamlea katika siku hizo ishirini tisa zikiisha kama babu yake Lanlan hatorudi au Lanlan alelewe na kituo.

“Wife kuna haja gani ya kulea wakati una uwezo wa kuzaa watoto wako?”Aliuliza Roma mara baada ya Mama Issa kutoka.

“Lanlan hana mama na baba yake hajulikani mpaka sasa , nimetokea kumpenda sana na moyo wangu unaniambia hana tofauti kabisa na mtoto wangu na nipo tayari kumlea”Aliongea Edna kwa sauti ya chini , alionekana kuwa mpole.

Moja ya sheria ya kituo cha Son and Daughter Orphanage katika kumlea mtoto ni mpaka kuwe na uthibitisho wa ndoa ndio utaruhusiwa kumchukua mtoto na hayo yalionekana kuwa malengo ya Master Chi ambaye ni babu yake Lanlan , alitaka Mama Issa alisimamie hilo na hata swala la Edna kuulizwa kama yupo tayari kumuacha Roma na kumchukua Lanlan ulionekana kuwa mtihani wa Master Chi kwa Edna na alifaulu , Master huyo alijiambia hawezi kumuachia Lanlan akarudi kwenye mikono ya baba yake ilihali bado hana familia ya kueleweka sasa haikueleweka hayo ndio masharti ya Seventeen au Lah, lakini kila alichokifanya ni kwa ajili ya kuchukua tahadhari.

“Wife unakumbuka kwamba tumeoana kwa mkataba na ni siku therathini tu zimebaki mpaka mkataba wetu kuisha?”Aliuliza Roma na kumfanya Edna kuukumbuka mkataba , ukweli hakuhesabu siku na alivyofikiria aliona ni kweli ni miezi mitano sasa imatimia tokea waanze kuishi Pamoja.

“Kabla ya kufikiria kule lazima tuanze kufikiria mahusiano yetu kwanza”

“Unaongea kama mtu ambaye ushafanya maamuzi tayari”Aliongea Edna.

“Unamaanisha niin kuhusu maamuzi , mimi nimeweka tatizo tulilokuwa nalo wazi , mkataba wa ndoa unatufunga labda kama tayari ushaamua kuishi na mimi milele”

“Najua ni kweli mkataba unatufunga , ninachotaka kujua ni msimamo wako , Roma hujawahi kuwa siriasis na mimi hata kidogo na juu ya haya yote unaonekana ulikuwa ukihesabu siku zilizobaki za mkataba na ndio maana nasema unaonekana kufanya maamuzi tayari”Aliongea Edna huku akikaza sauti.

“Edna unamaanisha nini sijawahi kuwa siriasi na wewe, au ni kwasababu ya tukio la Ijumaa?”

“Sio tukio la Ijumaa tu Roma , unaelewa kila kitu , tumeenda Ufaransa ukaahdii utaniambia kila kitu unachokifanya na matokeo yake hukuniambia chochote na nikajikuta nipo baharini baada ya kutekwa na Goodman , vipi kuhusu Nasra kumpeleka ukweni kujitambulisha , tukio la Ijumaa je , unataka nitafsiri vipi?, Babu yake Lanlan alivyoniambia nichague kati ya Lanlan na wewe nilikuchagua na sikufikiria juu ya siku zilizobaki za ndoa yetu , lakini leo hii limekuja swala la mimi kutaka kumlea Lanlan umeweka wazi zimebaki siku therathini , unataka nikutafsiri vipi?, ndio maana nasema una maamuzi yako tayari kichwani”Aliongea Edna na kumfanya Roma aanze kufikiria makosa yake , ni kweli alikuwa na mpango wa kumpeleka Nasra ukweni kujitambulisha swala ambalo hajamueleza Edna , siku walioenda Ufaransa alipanga mpango na miungu wenzake na hakumtaarifu Edna na mwisho wa siku akajikuta akiwa baharini, swala la Rose juzi aliona yote hayo Edna ana haki ya kulalamika , lakini swala la Edna la kusema ameshafanya maamuzi kichwani aliona ni kama anaonewa kwani kwanza hakuwahi kufikiria kumuacha.

“Edna sijawahi kufikiria kukuacha hata siku moja na hilo neno la kwamba nimeshafanya maamuzi unatakiwa kulifuta kwenye kichwa chako , swala ambalo tunazungumza hapa ni swala la Lanlan, ni kweli nina mpango wa kumsindikiza Nasra na lazima nitimize ahadi yangu kwake kama mwanaume wake, nina wanawake wengine ambao pia nina paswa kuwajibika kwao , lakini swala la kusema sijawahi kuwa siriasi na wewe litoe kwenye kichwa chako”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie na mpaka hapo mrembo huyu ni kama alikuwa akisikiliza msimamo wa Roma.

Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba Roma alikuwa akimwambia kwamba hana mpango wa kuachana na michepuko yake kwa namna yoyote ile lakini alipata ahueni kidogo baada ya kuona Roma pia hana mpango wa kumuacha.

“Roma wewe ni mbinafsi na unatamaa sana..”

“Wife mimi ndio nina tamaa na pia ni mbinafsi na ndio maana ninachoeleza hapa ni msimamo wangu na unapaswa kunielewa , sina mpango wa kumuacha mwanamke yoyote ambaye nishajihusha nae kimapenzi lakini pia sina mpango wa kukuacha na kumpa mtu mwingine cheo cha kuwa mke wangu”Aliongea Roma yaani alichoongea kwake ni kama sheria na kilitoka moyoni kabisa, Edna baada ya kusikia maneno hayo alijikuta akifumba macho na kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa wakti mmoja alionekana alikuwa akifanya maamuzi.

“Basi tufanye dili”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa ila alitaka kusikia Edna aataka kufanya na yeye dili gani.
ITAENDELEA , SIMULIZI NDEFU I HIGHLY RECOMMEND UNITAFUTE WATSAPP 0687151346
 
Edna bhana! Alitegemea mwamba ramon akomae miez sita bila kuweka kisu alani? Si kitakamata kutu au kuziba kabisa?
 
Edina anawakilisha kundi la wanawake wapumbavuu wanaoishi na wanaume zao ila wanawakomoa Kwa kuwanyim vitumbua wakidhani wanawakomoa kumbe wanajikomoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weekend hii Mkuu Tubariki na episode kadhaa, Ukifanya hivyo tutakupa Edna upachike mwanzi uvune ulanzi.
 
Weekend hii Mkuu Tubariki na episode kadhaa, Ukifanya hivyo tutakupa Edna upachike mwanzi uvune ulanzi.
Kijana wa masta...uko huku? Yeah weekend inakuwa ndefu sana bila ma episode ya mkuu SinganoJr. Mkuu Singano wabariki wana wape mashavu...hadith tamu sana, elimu ya dunia na sayansi, mapenzi...kila kitu kipo...Hongera sana Singanojr.
 
Back
Top Bottom