SEHEMU YA 285
Ni muda wa mchana juu ya bahari , inaonekana meli kubwa ya kivita ikiambaa ambaa kwenye ‘International water”, upepo na mawimbi ndio kitu pekee kilichoweza kusikika Zaidi kuliko injini zilizokuwa zikiendesha meli hio
Juu kabisa ya meli wanaonekana wanajeshi takribani ishirini hivi wenye vyeo tofauti tofauti huku wakiwa wamesimama kwa namna ya wasiwasi sana wakimwangalia mwanaume kijana aliesimama mbele yao.
Kwa jinsi walivyokuwa wakionekana ni kama wanajeshi ambao wamekamatwa na adui na sasa walikuwa wakisubiria adhabu ya kifo.
Kijana aliekuwa mbele yao aliwaangalia kwa kuwakagua mmoja mmoja kwa macho ambayo yalikuwa hayaonyeshi kuwa na hasira au furaha , yaani alikuwa akionekana kama mtu ambaye akili yake ipo lakini haipo ndani ya hilo eneo , alikagua kila mmoja kwa rangi zao tofauti , aliangalia waafrika walikuwepo , alikagua wazungu waliokuwepo na akakagua waarabu waliokuwepo , wote waliovalia nguo za jeshi zinazofanana.
“Since you guys took the money from someone else to deal with my people you should have expected this to happen , so stop giving me the look , I will give you all the chance to kill me too”
“Kwasababu nyie watu mmelipwa pesa ili kuja kudili na watu wangu , mlipaswa kutegemea hili kutokea , achene kuniangalia kwa macho yenu , Nitawapa nafasi ya kuniua na mimi pia”Aliongea, na kwa jinsi alivyoongea ni Dhahiri kabisa kwamba watu waliokuwa mbele yake walikuwa wamemchokoza kwa kuua baadhi ya watu wake na alikuwa juu ya meli hio kwa ajili ya kulipiza kisasi , lakini pia haikuwa hivyo tu ilionekana ndani ya meli hio kulikuwa na mateka wengine ambao wote hao walikuwa ni baadhi ya watu wake na alitaka awaokoke , lakini aikuwa akitaka kuwapa nafasi wanajeshi hao wachokozi wajaribu kumuua na yeye pia.
“Ni baadhi ya wanajeshi wachache sana kutoka kikosi chetu ambao wamehusika na kuuwa watu wako , lakini kwanini mpango wako ni kuua watu wote waliopo kwenye hii meli , lakini sio hivyo tu umeua pia familia zetu makao makuu”Aliongea moja ya mwanajeshi ambaye alikuwa na cheo cha Kanali , alikuwa ni mtu mzima kama miaka hamsini hivi.
“Huna chochote wewe kitu pekee kinachokusumbua ni kiu yako ya kutaka kuua watu kwa sababu zako za kipumbavu , wewe ni muyama na hupaswi kuwa katikati ya binadamu”Aliongea jamaa mmoja kwa lugha ya kijerumani akimnanga kijana aliekuwa mbele yao , alionekana kujiamini mno licha ya kumuogopa mtoa hukumu.
“Tunajua kwamba ni kweli unauwezo usio kuwa wa kawaida , lakini kitendo chako cha kuuwa watu bila hatia ni ushetani na naapa kwa kifo changu mbele ya maji haya , yote unayoyafanya sasa hivi yatakurudia”Aliongea kwa hasira na kabla hajasubiria jibu alijirusha baharini bila ya kusubiri adhabu yake na kufanya wenzake kuanza kupatwa na hofu Zaidi.
“Nilichosema kwenu ni kutumia mikono yenu kuniua na sio kunitamkia maneno ya laana”Aliongea kwa sauti na palepale alipotea alipo kuwa amesimama na kila anapoibuka yupo mbele ya mwanajeshi na ni damu pekee ambazo zilikuwa zikiruka hewani huku wanajeshi wale wakitenganishwa vichwa vyao kwa upanga, na zoezi lake lilichukua dakika mbili tu alikamilisha kila kitu , damu zilisambaa kwenye maji yote ya karibu na kufanya hata rangi yake kubadilika na kuwa nyekundu , kilikuwa ni kitendo cha kikatili mno ambacho kijana huyo alikuwa akikifanya na hakujali , alichokifanya ni kuinama na kuchukua kichwa cha mwanaume ambaye alimjua kama Jenerali wa jeshi hilo na kisha alitumia mkono wake na kupasua jicho lililokuwa likimwangalia kwa namna ya kumlaani kwa kumchinja na kisha akakitupa baharini.
Baada ya kuona karidhika na kazi yake ya chinja chinja alitoa kitambaa kilichokuwa kwenye mfuko wake wa suruali yake na kisha akajifuta damu zilizomchafua usoni na akamalizia na upanga wake na ile anatupa kitambaa kile chini , mlango wa meli hio ya kivita ulifunguliwa na anaonekana mwanamke mwenye tumbo kubwa akitoka , alikuwa ni mwanamke mrembo sana , lakini urembo wake ulififia kutokana na wasiwasi na mshangao aliokuwa nao , alimwangalia mwanaume kijana aliekuwa mbele yake na kisha macho yake akayahamishia kwenye miili na vichwa vya watu vilivyokuwa vimesambaa juu ya meli hio ya kivita na kujikuta akiziba mdomo na kuanza kutoa machozi , lakini licha ya hivyo mwanaume aliekuwa mbele yake hakumuhurumia hata kidogo wala kiguswa na machozi yake , yeye alikuwa akiangalia upanga wake na kuukinga na jua upande wa makali yake na kujikuta akitabasamu , ni kama moyo wake umeridhika sana kwa kitendo alichokuwa amekifanuya.
“Thirteen don’t kill anymore , haven’t you killed enough people ?”Aliongea akimaanisha kwamba Thirteen hupaswi kuua tena , kwani watu uliowaua hawakutoshi?.Aliongea kwa kuweweseka.
“My Dear Seventeen its not that I haven’t killed enough of them , there seems to be peaple constantly looking to die”
“Kipenzi changu Seventeen sio kwamba sijaua watu wa kutosha bali kuna watu ambao muda wote wanakitafuta kifo”Aliongea pasipo ya kujali.
“Miaka minne nyuma baada ya kuua wanajeshi wote wa Zero na kuharibu kambi yao , uliniahidi mwenyewe kama hautokuwa mkatili tena na kuuwa watu bila sababu , lakini kwanini .. kwanini kila mtu unaona anastahili kifo , hawa watu hawajakuchokoza na ni baadhi yao tu , kwanini ukaua familia zao zote na wao pia ?”Aliongea huku akianza kulia kwa kwikwi , alikuwa mrembo sana kiasi kwamba hata kulia kwake kulikuwa kukikipendeza lakini kijana aliefahamika kwa jina la Thirteen alionekana kutojali kabisa , kwanza hakujali ahadi yake aliowekeana na mrembo aliekuwa mbele yake, pili hakujali hisia zake wakati anapofanya mauaji”
“Seventeen unakumbuka mara ya mwisho nilikuuliza kwanini unapanda kuvaa mavazi ya rangi ya bluu mara zote na ulivyonijibu?”Aliouliza Thirteen lakini Seventeen hakumjibu Zaidi ya kuendelea kulia.
“You told me that when you were dressed in a blue clean looking shirt, you1`d feel a sense of achievement when blood got on your shirt”
“Uliniambia mwenyewe kwamba unapenda kuvaa vazi la bluu safi ili pale damu ya mtu inapokurukia kwenye nguo zako safi basi utajisikia mtu uliekamilisha jambo kubwa”
“Hayo mambo niliongea zamani , sasa hivi sitamani kabisa kuua binadamu mwenzangu napenda kuishi Maisha ya amani”Alionea Seventeen ambaye tumbo lake la ujauzito lilionekana wazi.
“Kama wewe unajihisi hupendi kuua kama zamani haimaanishi mimi sipendi, Seventeen najisikia vizuri sana pale matone ya damu ya moto yanaponirukia usoni mwangu, hizi hisia hazielezeki kabisa, kuchukua Maisha ya binadamu kwa mkono wangu huu ni kitu pekee ambacho hapa duniani kinanifanya nijihisi nimetimiza kusudi maalumu”
“You are the woman I trust the most also the woman I like the most , I’ll get really angry if you oppose me from killing , so I don’t allow you to try to stop me again”
“Wewe ndio mwanamke ninae kuamini sana na ndio mwanamke ambaye nakupenda kuliko , nitapatwa na ghadhabu kuu sana kama tu utanizuia mimi kuua , hivyo naomba usije ukajaribu tena kunizuia kufanya kitu ninachokipenda”Aliongea Thirteen na pasipo hata ya kusubiria jibu alitembea na kumpita Seventeen ambaye alikuwa akibubujikwa na machozi na kuingia ndani ya meli hio ya kivita. Alionekana sio mwenye kujali kabisa hisia za mwanamke huyo mjamzito na alikasirishwa na namna ambavyo anamzuia kuua.
………..
Ni siku nyingine juu ya meli hio hio ya kivita ndani ya chumba chenye kitanda kikubwa anaonekana Thirteen akijiinua kivivu na kilichomfanya kuamka ni njaa aliokuwa nayo , lakini pia alikuwa na ‘Hangover’ ya hatari kwani jana yake mara baada ya kumuacha Seventeen nje hakuongea nae tena na alishindia kunywa bia nyingi alizokutana ndani ya meli hio ya kivita ambayo hata haikuwa ya kwake.
Sasa baada ya kujiinua kivivu huku macho yake yakiwa bado na hali ya ukungu unaotokana na usingizi alijikuta akihisi kitu kigumu pembeni yake , aligeuza mkono wake na kushika kile kitu kigumu na kugundua ni karatasi mfano wa kama gazeti gumu kama yale ya kutegenezea kalenda , alilichukua kipande kile cha karatasi na kisha akakiweka mbele yake ili kuona kwanini kipo juu ya kitanda , baada ya kuangalia mbele yake alijikuta macho yake yakianza kuongezeka ukubwa , kwani karatasi hio ilionekana kuwa na maandishi ambayo yalimshitua mno.
“Thirteen mimi naondoka ,siwezi kuendea kuishi na wewe na kumfanya mwanangu alietumboni kuzaliwa juu ya damu zinazomwagwa kwa mikono yako , umesema huna mpango wa kuacha roho yako ya kikatili , roho ya kimauaji na mimi pia siwezi kuishi na muuaji , nitaenda kusihi mbali na wewe mpaka siku ambayo mtoto wangu atakapo zaliwa na kufahamu baba yake amebadilika. Kwa heri Thirteen”Hayo ndio maandishi yaliokuwepo kwenye barua hio na kumfanya Thirteen kukunja kunja karatasi hio kwa hasira kali mno , hakuamini karatasi hio likuwa na ujumbe wa Seventeen ambao ulikuwa ukimpa maneno ya mwisho ya kwaheri.
******
Masaa kadhaa mbele baada ya Thirteen kusoma barua ilioachwa na Seventeen na kumfanya kuomboleza kwa kuondoka kwake , kwenye kilele kimoja juu ya mwamba pembezoni mwa bahari ya Pasific wanaonekana watu baadhi wakionekana kuvuja damu nyingi mno huku wakiangalia maji yaliokuwa chini yao juu ya mwamba mkubwa waliokalia , sehemu ambayo kama ukidodonka tu basi moja kwa moja unakwenda kuzama kwenye kina kirefu cha bahari.
Watu hao ambao walikuwa wakihisi maumivu ya kuchanwa na kisu mwilini mwao walikuwa wakilazimishwa kujirusha juu ya mwamba huo kwenda chini baharini, na kwakua mtu aliekuwa akiwalazimisha alikuwa akigopesha hakuna mtu ambaye alikuwa na ujasiri wa kujiuliza mara mbilimbili , kila mmoja alijirusha chini ya mwamba huo uliokuwa juu mlimani kila ilipofikia zamu yake.
Thirteen aliekuwa na macho yaliokuwa yamebadilika rangi na kuwa ya kijani, hakuonyesha hali ya kuridhishwa na vifo vya watu ambao wamejirusha na sasa walikuwa wamebakia watu wawili ambao walionekana kuwa ndio viongozi katika kundi hilo la watu ambao amejeruhi kwa mapanga.
“Sijali sana nyie watu mnatokea kwenye kundi lipi la kigaidi , wala nguvu za giza mnazotumia , lakini mmefanya kosa kubwa sana kumteka mwanamke wangu”
“Thirteen even you kill all of us your woman and the child in her belly will be buried with us ,So what if we can’t defeat you even when we cooperate?,once we die while you are still alive you will suffer more than dying”
Ukweli ni kwamba kilichomfanya Thirteen kukamata watu hao ni kutokana na uepepelezi wake ambao ulimpa majibu kwamba baada ya Seventeen kumkimbia kwenye meli hio ya kivita , alitekwa akiwa kwenye meli ndogo na majambazi hao wa baharini (pirates) , sasa alichokuwa akitaka kwa hao watu ni kumueleza ni upande gani Seventeen walikuwa wamemficha , lakini hawakuwa tayari kuongea, ndio maana alianza kuua mmoja mmoja baada ya mbinu zake zote za mateso kukwama.
Wakati akiendelea kuongea na watu wawili wa mwisho ambao walimpandisha hasira za kutamani kuwaua muda huo huo mara mita kadhaa kutoka alipo aliweza kumuona mwanamke akiongea na simu ya upepo na ilionekana mwanamke yule alikuwa akifanya makusudi ili Thirteen aweze kuona na kusikia kwa wakati mmoja.
“Mission failed , initiate Explosion”Aliongea yule mwanamke ndani ya fukwe hii na palepale upande wa pili juu ya mwamba alionekana Seventeen akijirusha majini na wakati huo huo ulionekana mlipuko mkubwa eneo lilelile ambalo amejirusha na kufanya mawimbi ya maji kuongezeka kwa kiasi kikubwa , Thirteen alijikuta akitoa macho mara baada ya kushuhudia Seventeen akijirusha majini na sehemu ile kulipuka.
“Thirteen although our alliance failed to kill you this time, letting you go through the pain of losing the woman and child you love can be considered our victory”
“Thirteen ijapokuwa tumeshindwa kukufanya mtu wetu lakini kukuacha kuendelea kuishi ukiwa na maumivu kwetu ni ushindi pia”Aliongea mwanaume mmoja na pasipo kuruhusu Thirteeen kuwaua , walijirusha kwenye mwamba na kuambaa ambaa kwenda chini ya maji , huku Thirteen akiwa haamini macho yake kama Seventeen aliekuwa mjamzito ndio basi tena.
“Seventeen…. noooo…..!!!”Alijikuta akitoa kilio cha maumivu makali mno , hakuamini mwanamke ambaye alikuwa akimpenda kwa moyo wake wote ndio huyo ambaye amelipuliwa na bomu na kutumbukia kwenye maji
****
Roma alirudi kutoka kwenye kumbukumbu zake ambazo zilimkumbusha mbali sana na kujikuta moyo ukimuuma na kumwangalia mwanamke ambaye yuko mbele yake.
“Yalikuwa makosa yangu kukuacha kupitia maumivu makali kipindi kile , kutotaka kwako kuniona tena ijapokuwa ulikuwa unaishi na pia kupelekea mtoto wetu kufa , hayakuwa makosa yako , lakini hata hivyo nashukuru sana nimekuona ukiwa hai kwa mara nyingine”Aliongea Roma huku akinyanyuka kivivu.
“Thirteen naomba uondoke nyumbani kwangu , siku ya leo itakuwa mara ya mwisho ya mimi kuonana na wewe tena”Aliongea yule mwanamke hulu hasira zikionekana katika macho yake.
“Seventeen ijapokuwa najua nimesababisha yote yale , lakini baada ya tukio lile la ule mlipuko na namna ulivyomezwa na baada ya kudondokea baharini, nilijikuta nikifahamu mambo mengi sana , mambo ambayo yalinifanya nikabadilika kimtazamo kwa asilimia mia moja , niliomboleza kifo chako kwa muda mrefu na niliishi kwa majuto , na baada ya kuona siwezi kupona maumivu ambayo yalisababishwa na kifo chako nilifanya maamuzi ya kurudi nchini Tanzania ambako nilihisi ndio nilipozaliwa na nilivyoweza kukutana na mwanamke ambaye anafanana kama wewe kwa kila kitu , nilihisi ni Mungu pekee ndio aliemleta kwangu kama mbadilishano , lakini mwisho wa siku nilikuja kugundua mwanamke yule licha ya kwamaba mnafanana lakini nafasi zenu kwenye Maisha yangu ni tofauti kabisa , wewe ni kama wewe na yeye ni kama yeye , Seventeen niamini mimi nafasi yako kwenye Maisha yangu haiwezi kufutika
Roma baada ya kuongea risala zake alianza kugeuka na kupiga hatua kuondoka ndani ya nyumba hio , hakutaka kuongea na Seventeen tena.
“Thirteen”Aliita Seventeen na kumfanya Roma kugeuka na kumwangalia na pale ndipo aliposhuhudia machozi kutoka kwa mwanamke aliekuwa mbele yake na mwanamke yule pasipo ya kujiuliza alimkimbilia na kisha akamkumbatia.
“Naomba usiniache tena tafadhari”Aliongea yule mwanamke huku akimkiumbaita Roma na kumfanya kuhisi joto la mwanamke huyo lakini pia pumzi ilitoka katika pua za mrembo huyo mwenye kufanana kwa asilimia mia moja na Seventeen.,
Lakini sasa wakati Roma akijisikia faraja kukumbatiwa na mwanamke anaempenda , mwanamke anaenda kwa jina la Seventen , mara alijikuta akigundua kitu ambacho sio cha kawaida na hio ni mara baada tu ya mwanamke yule kutoka kwenye mwili wake.
Roma aliekuwa amesimama alishitukia kuna Kisu aina ya Dagger kikiwa kimetumbukizwa kwenye moyo wake , huku mwanamke ambaye alikuwa akiuonekana kwa asilimia mia moja kufanana na Seventeen akimwangalia kwa macho ya dharau ni kama vile alikuwa akimdhihaki.
Ni kwamba Roma alishindwa kuelewa ni muda gani ambao amechomwa na kisu hiko kwani mwanzoni hakuhisi aina yoyote yale ya maumivu , lakini baada ya mwanamke yule kuacha kumkumbatia ndio alihisi maumivu makali kutoka kwenye moyo wake na alianza kukosa nguvu na macho kuanza kujaa ukungu na sekunde sitini zilikuwa nyingi sana kwa Roma kwani damu zililoanisha shati lake na palepale akadondoka chini na kufumba macho na haikueleweka kama amekufa ama amefumba macho , ila kwa jinsi kisu kile kilivyozama eneo la moyoni ni dhahiri kabisa kuna uwezekano mdogo wa kuwa hai.
“Hahahahah….. hahahaha….”Alianza kucheka yule mwanamke kwa namna ya dharau kubwa na palepale sura yake ilibadilika na akaonekana kuwa mwanamke wa kijapani , mwanamke ambaye sasa alionekana kuwa ni mmoja ya wanawake kutoka kwenye kundi la Yamata Sect kutokana na aina ya mavazi yake.
“Hii mbinu aliopendekeza Chief sikuamini inaweza kuwa nzuri namna hii , Hades ulieaminika huwezi kufa hatimae leo nimeweza kutekeleza kifo chako , hahahaha….”Aliongea kwa furaha sana huku akijiona kama moja ya watu ambao wametekeleza jambo kubwa kwenye Maisha yake.
ITAENDELEA
ITAENDELEA SIKU YOYOTE , NICHEKI WATSAPP KAMA UMECHOKA KUSUBIRIA 0687151346