Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 318

Roma aliweza kufika nyumbani kwa Afande Kweka na ilionekana walikuwa wakisubiriwa kwa hamu , kwani hapo ndani ilikuwa ni kama sherehe ambayo ilikuwa ikiendelea kwa jinsi mpangilio ulivyo.

Mzee Kweka mwenywe ndio aliweza kutoka mpaka nje kwa ajili ya kumpokea mjuukuu wake Denisi ambaye alimtoa kafara kwa ajili ya ugonjwa wake miaka mingi iliopita , sasa anarejea nyumbani kama mwana mpotevu.

Afande Kweka alikuwa akisubiria kwa hamu sana siku ambayo Roma atakanyaga mguu ndani ya familia yake.

Edna kwa mapokezi aliopokewa nayo , lakini pia namna ulinzi ulivyoimarishwa ndani ya hili eneo ndio aliweza kujua nguvu aliokuwa nayo Mzee Kweka.

Unachopaswa kujua familia ya Mzee Kweka ndio ambayo ina nguvu namba mja ndani ya taifa la Tanzania , na hio sio kwasababu Raisi Senga alikuwa raisi, Hapana, bali ni ushawishi mkubwa aliokuwa nao Afande kweka kwenye majeshi ya Tanzania.

Ma afande wengi waliokuwa ndani ya jeshi walikuwa wakimuheshimu sana Afande Kweka na mara nyingi kwenye mambo mengi walikuwa wakihitaji busara zake .

Hivyo hata kwa wanasiasa wanaotaka kuwa maraisi ,walikuwa wakihitaji sana sapoti kutoka kwa Afande Kweka , lakini hata hivyo sio familia ya Mzee Kweka pekee ambayo ilikuwa na nguvu Zaidi , familia ya Mheshimiwa Kigombola pia ni moja ya familia zenye nguvu kisiasa ndani ya taifa la Tanzania , Raisi Kigombola alikuwa na vijana wengi ambao amewaingiza ndani ya serikali wakiwa kama viongozi wakubwa kipindi alivyokuwa raisi na mpaka alipostaafu.

Unaweza kusema kwamba moja ya viongozi ambao walijijengea mazingira ya kuwa na nguvu ndani ya Tanzania basi ni Familia ya Kigombola ikiongozwa na mheshimiwa Kigombola mwenyewe, hio ndio famulia yenye nguvu kisiasa nchini , lakini familia pia nyingine ambayo ilikuwa na nguvu sana ndani ya Tanzania ni familia ya Mzee Atanasi anakozaliwa Blandina , Familia ya Mzee Atanasi ukubwa wake ni kwenye uchumi, familia hii ilikuwa imeteka kwa kiasi kikubwa uchumi wa Tanzania , kwani imewekeza kwa kila Nyanja ,huku ikiongozwa na Tajiri Mohamedi Azizi, hivyo unaweza kusema uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa ulikuwa umeshikiliwa na familia hii ya Mzee Atanasi , Familia nyingine ya nne ambayo ilikuwa na ushawishi pande zote ni familia ya Nyerere , familia hii licha ya kwamba hawakuwa wakionekana sana hadharani , lakini ndio familia ambayo ilikuwa na ushawishi pande zote yaani kuanzia kwenye uchumi , siasa na jeshi na hii familia inafanana kwa kiasi kikubwa na familia ya Karume kutoka Visiwani , licha ya familia ya karume kuwa na nguvu sana Visiwani lakini pia ilikuwa na ushawishi mkubwa upande wa bara na inasemekana kati ya familia ya Nyerere na Karume ndio wanaoshikilia siri kubwa iliopo chini ya muungano, ssajambo moja ambalo unatakiwa kuelewa ni kwamba familia ya hii kutoka visiwani ndio inashikilia asilimia Zaidi ya therathini ya makampuni yote ya Maya hapa Tanzania.

“Edna karibuni sana nyumbani , Roma karibu sana nyumbani”Ilikuwa ni sauti ya ukarimu ya mwanamama Damasi mke wa Raisi Senga , ilishangaza sana kuwepo ndani ya familia hio kwa siku hio kuwapokea Roma na Edna .

Roma alikuwa akimfahamu mke wa raisi Senga , kwani walishakutana Zaidi ya mara mbili , mara ya kwanza alivyoenda ikulu na mara ya pili mwanamama huyo alivyompigia magoti kwa ajili ya kumsaidia Denisi.

“Asante sana mama, Lanlan msalimie Bibi”Aliongea Edna kwa Kingereza akimtaka Lanlan kumsalimia bibi yake.

“Goodmorning Grandma”Aliongea Lanlan.

“Wow! , jamani katoto kazuri kweli, hajui kuongea Kiswahili?””

“Ndio, Anajua kingereza pekee”

“Mr Roma karibu sana nyumbani baada ya miaka mingi”Aliongea Mzee Kweka baada ya kuwasogea na kukatisha maongezi kati ya Damasi na Edna.

“Mzee Kwani nilishawahi kufika hapa?”

“Unaweza ukawa hujawahi kufika hapa, lakini hapa ndio makao makuu ya ukoo wa Kweka na wewe ni mwanaukoo kabla ya kupotea , hivyo wewe sio mgeni bali ni mwenyeji unaerudi , karibu sana nyumbani”Aliongea Mzee Kweka. Kwa bashasha kubwa.

“Edna karibu sana nyumbani kwako , huyu bwana kakuoa lakini hajawahi kukuleta nyumbani , karibu sana kwa mara ya kwanza kwenye familia yetu”Aliongea na kumfanya Edna amwangalie Roma kwanza na Roma alimkonyeza.

“:Asante sana babu , nimekaribia”Aliongea Edna na mzee Kweka alitingisha kichwa huku macho yake akiyageuzia kwa Lanlan na kuanza kumtathimini kwa dakika kadhaa.

“Lanlan msalimie babu”Aliongea Edna na Lanlan alimsogelea Mzee Kweka na kushika mkono wake na kuuweka kichwani.

“Goodmorning Grandpa”Aliongea Lanlan na kumfanya Mzee KWeka kuachia tabasamu la kizee huku akimshika mkono Lanlan.

Muda huo wote walisogea mpaka eneo maalimu ambalo limeandaliwa nje ya jumba hili la Mzee Kweka kwa ajili ya kukaa.

Macho ya Roma hayakuwa yameridhika kabisa , kwani alikuwa akimtafuta Zenzhei na hiko ndio ambacho kilimleta hapo nyumbani , kama sio Zenzhei asingekanyaga mguu wake hapo ,kwanza hakuwa akipenda sana mambo ya ukoo kwani aliyatafsini kama mambo yaliopitwa na wakati na yeye hakuwa akihitaji ukoo kuwa na nguvu.

Mzee Kweka alionekana kuzoeana haraka na Lanlan na kumfanya hata Edna kushangazwa na Lanlan kuweza kuzoea watu wapya haraka, tofauti na Watoto wengine.

“Hahahaha….Kwahio Lanlan anapenda kula , kuangalia Wanyama na kufanya nini?”

“Na kuendesha Farasi na Tembo”Aliongea Lanlan na kumfanya Mzee Kweka kucheka Zaidi na kushangazwa na Lanlan.

“Lanlan ushawahi kuendesha tembo?”Aliuliza Roma.

“Mama yake Lanlan amenifundisha kuendesha Tembo na farasi , Lanlan anapenda Wanyama, Grandpa nataka kuona Wanyama”

“Grandpa atampeleka Lanlan kuona Wanyama”

“Grandpa promise me!”

“Grandpa anaahidi atampeleka Lanlan kuona Wanyama”Aliongea Mzee Kwek ana kumfanya Lanla kuripukwa na furaha , huku watu wote wakishindwa kuongea wakiwaangalia Lanlan na mzee Kweka, ndio waliteka mazungumzo na hata ule ukaribisho ulizidiwa na maongezi ya Lanlan, uzuri pia ni kwambwa wanafamilia karibia wote walikuwa wakielewa lugha ya kingereza.

Zilipita dakika kadhaa tu , alionekana na Denisi akiingia ndani ya jumba hili la Mzee Kweka akiwa anatumia gari yake aina ya Audi, alipokelewa vyema na wafanyakazi na kuelekezwa upande wa nyuma sehemu ambayo watu wote wameketi.

“Grandpa nimeitikia wito”Aliongea Denisi mara baada ya kukaribia eneo hilo ambalo limetegenezwa kwa hema.

Roma alimwangalia Dnisi na kujikuta akikunja sura na Denisi alimwangalia Roma na kisha kukunja sura kidogo kabla yakuachia tabasamu.

“Karibu sana Denisi nyumbani”

“Asante sana babu , jambo uliloniitia ni muhimu , nimeona nitakuwa sio muungwana kama nitakosa siku hii ya kumkaribisha kaka yangu na mke wake nyumbani, Roma karibu sana kwenye ukoo wetu”Aliongea Denisi na alisogea upande wa Roma na kumnyooshea mkono kama ishara ya salamu.

“Sipendi kukaribishwa kinafiki , unaweza tafuta sehemu ukakaa ila iwe mbali na mimi”Aliongea Roma pasipo ya kupokea mkono wa Denisi na jambo lile kidogo lilifanya hali ya hewa kuwa ngumu kidogo.

“Shemeji Edna karibu sana kwenye familia yetu ya Kweka , chaguo lako la kuolewa na Bro wangu hapa halikuwa baya, inaonesha unaona sana mbali”Aliongea Denisi na maneno yake licha ya kwamba yalinyooka , lakini yalikuwa na chembe za unafiki ndani yake.

“Denisi tafuta sehemu ya kukaa ukae, tuna mambo mengi ya kuongea leo kama wanafamilia ndio maana nimewaita wote muwe hapa”

“Lakini babu vipi kuhusu baba , yeye hayupo , familia bado haijakamilika”

“Denisi acha kuongea upuuzi , unafikiri ukoo wa Kweka umejengwa na mimi tu Pamoja na baba yako ,wapo wanaukoo wengine ambao hawajafika na siku ikiwadia wote nitawaita kwa ajili ya kumtambulisha Roma ”Aliongea Afande Kweka.

“Naamini hio siku ndio ya kumtambulisha Roma kama kiongozi wa ukoo akirithi nafasi yako?”Aliongea Denisi na kufanya watu wote hapo kushangaa.

“Denisi nifuate”Aliongea Damasi akimwashiria mwanae amfaute ndani na Denisi hakutaka kubisha alifuata nyuma akimuacha Mzee Kweka akiwa kwenye ‘jazba licha ya maneno alioongea Denisi kuwa ya kweli.

“Denisi ndio alivyo , amejaa tabia za kisiasa siasa na na maneno mengi ya mzunguko , msijali sana .. Ooh yeah nilisikia ulimwadabisha inaonekana hajatia adabu”Aliongea Afande Kweka kupoza hali.

“Afande mimi nimekuja kwa ajili ya Zenzhei lakini simuoni hapa”Aliongea Roma akiulizia uwepo wa Zenzhei.

“Zenzhei kaenda kukutana na kaka yake na kaahidii atawahi kurudi na mtaonana”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kushangaa Zenzhei kuwa na kaka.

“Usishangae kuna mambo mengi ambayo unapaswa kuyasikia kutoka kwa Zenzhei”

Upande mwingine asubuhi hio , upande wa Bagamyo baharini , wanaonekana watu wawili ambao kwa kuwaangalia hawakuwa wazawa kutokana na Ngozi zao , watu hawa hawakuwa wengine bali ,mmoja alikuwa ni Zenzhei na mwingine alikuwani Gumila.

Walikuwa wameketi kwenye mchanga huku macho yao yote wakiyaelekezea upande wa baharani , sehemu ambayo mitumbwi mingi ya kufanyia uvuvi ikiwa inaelea , Pamoja na wavuvi waliokuwa wakilanda landa kupokea wenzao ambao ndio kwanza wanrudi kutoka kwenye shughuli za uvuvi asubuhi hio.

“Zenzhei , ulifikaje Tanzania?”Aliuliza Gumila na kumfanya Zenzhei aliekuwa akiangalia baharini kuvuta pumzi.

“Ujio wangu hapa Tanzania zilikua ni harakati za kukutafuta”Aliongea na kumfanya Gumila kushangaa kidogo.

“Ulifahamu vipi nitakuwa ukanda wa Afrika mashariki, usiniambie ulinipeleleza ndani ya kundi la Yamaguchi?”Aliongea Gumila japani huyu , huku leo hii akiwa tofauti na mara ya mwisho tulivyomuona.

“Ni Stori ndefu sana ambayo napaswa kukueleza tokea mara ya mwisho wewe kuondoka lakini pia hata familia yangu kuwa ‘Demoted’”

“Unamaanisha nini kuwa Demoted?”
 
SEHEMU YA 320

“Unapaswa kutoa sadaka ya kitu unachopenda sana kwenye Maisha yako?”Aliongea Balozi na kumfanya Raisi Kamau kushangaa.

“Kitu ninachokipenda?”

“Ndio mheshimiwa Kamau Kamau”Alijibu balozi aliemtembelea raisi Kamau na kumfanya ndugu balozi kutabasamu huku Mheshimiwa kamau akijiuliza ni kitu gani anakipenda sana kwenye Maisha yake , lakini wakati huo huo upande wa Tanzania na Raisi Senga kufikiria ni kitu gani anakipenda Zaidi.

“Tunamuhitaji mkeo kama sehemu ya sadaka”Aliongea ndugu balozi upande wa Kenya.

“Tunamuhitaji mkeo Blandina kama sehemu ya sadaka”Aliongea ndugu balozi upande wa Tanzania, Raisi Senga na Raisi Kamau wote kwa wakati mmoja wakapigwa na butwaa.

“Hapana Blandina sio mke wangu”Alijibu Raisi Senga akimaanisha kwamba Blandina alietajwa sio mke wake, na ndugu balozi akatabasamu.

“Hapana Blandina sio mke wangu tena na ashakufa”Alijibu Raisi Kamau na kumfanya ndugu Balozi kutabasamu.

“Kwa macho ya kawaida ni kweli kabisa Blandina sio mke wako , lakini katika ulimwengu wa Roho ndoa yenu wewe na Blandina ilishakwisha kfungwa na ni yenye kukubalika”Aliongea ndugu balozi akimueleza Raisi Senga.

“Blandina ndio mkeo na mimi na wewe tunajua hajakufa kama wengi wa taifa hili wanavyojua”Aliongea ndugu balozi upande wa Kenya.

“Vipi kuhusu mke wangu Damasi , ndio mke wangu wa halali”

“Mheshimiwa nasikikita kukuambia kwamba Damasi ni mwanamke unaeishi nae na sio mke wako , angalau kwa macho ya kibinadamu ni mke wako , lakini katika ulimwengu wa roho mkeo bado ni Blandina na ndoa yako na yeye haikuwahi kubatilishwa , jambo la kufurahisha Zaidi mheshimiwa unampenda sana Blandina , ni ukweli ambao hutaki tu kuukubali”Aliongea Balozi upande wa Tanzania na kumfanya Raisi Senga kushindwa kuongea neno tena.

“Mheshimiwa haya ndio maandalizi unayotakiwa kufanya kwa ajili ya sadaka kabla ya siku ya ibada, nikutakie utekelezajia mwema”Aliongea ndugu balozi na kisha akanyanyuka , huku akiacha karatasi mezani kwa mheshimiwa Senga.

Sasa upande wa Kenya ilikuwa hivyo hivyo, kila mmoja alipokea nyaraka iliokuwa ikielezea maandalizi ya Sadaka takatifu au kafara.

Sasa katika maelezo ambayo aliachiwa raisi Kamau ni kwamba sheria namba moja alitakiwa kumrudisha Blandina nchini Kenya na kuwa mke wake tena kihalali kabisa , lakini wakati huo huo akimaliza tofauti zake na Raisi Senga kutokaTanzania , huku karatasi ikielezea namna sahihi ya kumrudisha Blandina ,yaani kwa maneno marahisi ni kwamba kila kitu kilikuwa kimeandaliwa na ilikuwa ni kwa Kamau tu kutekeleza , upande pia wa Tanzania Raisi Senga alipata kusoma karatasi iliochwa na yenyewe ilikuwa na maelezo ambayo yanamtaka kwanza kabisa kuhakikisha kunakuwa na amaini kati yake na Kamau , lakini pia wakati huo huo akimsaidia Raisi mwenzake kuhakikisha Blandina anarudi Kenya , huku maelezo namna ya kufanya zoezi hilo yakiwa yanaendelea.

Sasa kwa jinsi kila kitu kilivvyoandikwa ndani ya karatasi hio , ilionyesha kabisa jamii hio ya siri ilikuwa ikimfahamu vyema Blandina kwa kila alichokuwa akikifanya na walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu sana.

Sasa maelezo hayo yote yanaonyesha kwamba Blandina ameweza kufunga ndoa na wanaume wawili kwa wakati mmoja ndani ya ulimwengu wa Kiroho na ndoa yake na wanaume hao kuwa katika kumbukumbu na kukubaliwa moja kwa moja ,sasa swala hili halikueleweka linawezekana vipi, lakini utaelewa hivi punde.

Ni kweli kabisa baada ya Raisi Senga kujiuliza kwenye moyo wake aligundua kabisa alikuwa akimpenda sana Blandina bado na jambo hili liliibuka upya mara baada ya kuambiwa amtoe kafara , moyo wake ni kama umetibuliwa upya.

Upande wa Raisi kamau alikuwa hivyo hivyo , alikuwa akiumia sana mara baada ya kupewa sharti la kumtoa Blandina mwanamke wake kipenzi sadaka.

Sasa jambo ambalo unatakiwa ulifahamu ni kwamba raisi Kamau licha ya kwamba alikuwa amemuoa Blandina kimagumashi , lakini kuna historia kubwa ilikuwa chini yao , upande huo huo Blandina akiwa na historia kubwa sana ilionyuma yake na Senga, halafu jambo la kufutahisha Zaidi kuna historia kubwa iliokuwepo kati ya Raisi Kamau na Raisi Senga.

Sasa hawa mabwana wote wawili ni marafiki na wakatokea kumpenda sana mwanamke mmoja kiasi kwamba kila mtu kwa wakti wake akafunga na mwanamke huyo ndoa ,na ndoa hio ikakubalika katika ulimwengu wa kiroho , yaani kwa maneno marahisi katika mafaili ya ndoa huko kwenye ulimwengu wa kiroho Blandina anatambulika kama mke halali wa Raisi Senga , lakini wakati huo akitambulika kama mke halali wa Raisi Kamau. Huku Damasi na Raisi Senga wakionekana mwanaume na mwanamke wanaoishi pamoj , yaani walionekana walikuwa wakizini tu sio kufanya tendo la ndoa.

Sasa mabwana hawa kutokana na mapenzi yao kwa mwanamke mmoja na mwanamke huyo kuwa sehemu ya kitu wanachopenda sana ndani ya dunia hii wanajikuta wakiwa kwenye mtego wa kutakiwa kumtoa mwanamke huyo kafara.

Sasa unachotakiwa kuelewa hapa ni kwamba Imani za hawa watu wote wawili zilikuwa zipo kwenye majaribio na muda ambao watakubali ni ishara kwamba wapo tayari kuwa wanachama wa Freemason watiifu.

Sasa kwa kile ambacho kimetokea ndani ya kituo cha Son and daughter Ophanage, itoshe kusema kwamba wote kwa Pamoja wameamua kukubaliana na matakwa ya kumtoa Blandina kafara, na hatua ya kwanza ilikuwa ni hatua ya kumrudisha Blandina nchini Kenya, yaani blandina anatakiwa atolewa kafara akiwa tena mke wa raisi Kamau Kamau , huku raisi Senga akitoa baraka zake zote za kumwachia Raisi Kamau Blandina wake.

********

“Blandina utafanya nini juu ya hili, upo kwenye wakati mgumu kweli rafiki yangu , kwanini haya yote yanakupata wewe tu?”Aliongea Mama Issa kwa huzuni na muda huu ni mara baada ya raisi Senga na Kamau kuondoka na kuwaacha Blandina na Mama Issa.

Sasa Blandina aliweza kumueleza Mama Issa kile ambacho kinatokea, kwa maelezo ya Blandina ni kwamba karatasi ambayo amepewa na maraisi hao ilikuwa ikionyesha kwamba vituo vyake vyoote alivyovijenga kwa jasho na damu kwa ajili ya Watoto yatima vitabomolewa , sasa ile karatasi ilikuwa na sahihi za maraisi katika kila nchi ambazo vituo hivi vipo , yaani kulikuwepo na sahihi ya raisi wa Congo tayari, kulikuwa na sahihi ya Raisi wa Sudani tayari.

Lakini haikuwa hivyo tu , kulikuwa na sahihi kutoka umoja wa mataifa inayosimamaia maswala ya Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu , yote hii ilikuwa ni kumfanya Blandina kukubali kurudi Kenya ili kuwa mke wa Raisi kamau na kama atakataa basi vituo hivyo vitabomolewa.

Kwa maneno marahisi ni kwamba nguvu ambayo inamtaka Blandina kurudi Kenya kuwa mke wa Raisi Kamau kwa mara nyingine ilikuwa ni kubwa mno kiasi kwamba hana nguvu ya kulinda vituo hivyo hata kama ataenda kushitaki , kwanza atashitaki wapi kwani watu wanaolinda hizo sheria ndio waliaoamua kuzivunja.

Blandina anazo siku tano tu kuamua cha kufanya , aidha akubaliane na masharti na arudi Kenya au akubali kuishi Tanzania na vituo vyote mpaka cha Son and daughter orphanage kubobolewa.

Blandina aliangalia Watoto waliokuwa wakicheza na Yezi na alijikuta akizidi kuwa kwenye wakati mgumu Zaidi , Watoto waliokuwa mbele yake walionekana kuwa na furaha na walichukulia eneo hilo kama nyumbani kwao , sasa ataanzaje kubomoa kwa ajili ya kitu kidogo kama ndoa.

Asichokijua Blandina ni kwamba alikuwa akiandaliwa kama sadaka kwa ajili ya Imani ya wanaume ambao walitokea kumpenda sana kwenye Maisha yake , Raisi Senga na Kamau.

“Sijui cha kufanya Mama Issa , nitatumia siku mbili hizi kufikiria na niamini mimi nitafanya maamuzi sahihi, Tabea kwa vyovyote vile siwezi kuruhusu Watoto hawa kuteseka tena kwa sababu yangu , Imani yangu ipo kwa hawa Watoto kuliko kitu kingine chochote ndani ya dunia hii na ndio sadaka pekee ambayo naweza kutoa kwa Mungu”Aliongea Blandina na kumfanya Mama Issa Chozi la kiutu uzima kumtoka.

********

Ikawa jioni ikawa asubuhi, hatimae ikawa jioni tena siku ya Jumatatu.

“Mama unaonekana kutokuwa sawa kwa siku hizi mbili”Aliongea Roma marabaada ya kumkuta mama yake akiwa ameketi eneo la nje akiwa amekodolea macho maji ya bwawa la kuogelea.

Ukweli ni kwamba Edna ndio aliekuwa wa kwanza kuona mama mke wake alikuwa kwenye mawazo na ugunduzi huo ndio ulimpelekea Edna kumfauta Roma chumbani kwake kwa ajili ya Kwenda kuongea na mama yake.

“Kumbe hata wewe mke wangu umelishudia hilo , wife unaonekana kumjali sana mama mkwe wako”Aliongea Roma akimwangalia Edna aliesimama mbele yake Roma muda huo mwenyewe alikuwa amevalia bukta tu na kumfanya nyoka yake kuonekana Zaidi kwenye macho ya Edna.

“Acha utani ,vaa ukaongee nae, yupo kule nje bustanini kakaaa ,wewe ni mtu gani hata haujali hali aliokuwa nayo mama yako”Aliongea Edna na Roma alisimama na kumsogelea Edna , sasa kitendo cha kusimama ndio kilizidisha dudu ya Roma kujionyesha wazi , ukijumlisha pia na ukubwa wake ilifanya kudhihirika.

Sasa macho ya Edna yalipotua kwenye Jongoo la Roma , mwili wake ulishikwa na ubaridi mkali mno na kabla hata ya Roma hajamfikia alitoka nduki na kumuacha Roma kutabasamu kifedhuli , alijua ni sababu gani ilimfanya Edna kumkimbia.

Kwa hio Roma aliweza kumsogelea mama yake kumuuliza nini kinamsibu kwani alikuwa kwenye mawazo.

Blandina baada ya kumuona Roma kaketi upande wa kulia kwake , alijikuta akitabasamu na kumwangalia Roma usoni na palepale machozi yalionekana yakitawala mboni za macho yake.

“Roma mwanangu asante sana”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kushangaa , kwanini mama yake analia halafu wakati huo huo anamwambia asante , jambo hili la kuona machozi ya mama yake hakuwa ni mwenye kulipenda.

ITAENDELEA

NJOO WATSAPP UTUMIWE VIPANDE VYA MBELE NA KUUNGANISHWA NA GRUPU 0687151346
 
Unaweza pata PDF ya hii simulizi kutoka episode ya 1 mpaka 300 kwa wale mnao anza kusoma na mnaona ugumu kupitia kila post nitafute watsap 0687151346
 
[emoji119]
 
jioni ya leo
Naaam hili dude imebidi jana nilipige saa 6 usk mpaka saa 8. Yaani ukiliweka tu tunalo...hadithi nzuri sana na ni unpredictable. kama inaisha vile kumbe ndio inaanza...SinganoJr wewe ni Mwamba kabisa. Big up mzee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…