Mkushi w jani
JF-Expert Member
- Oct 2, 2021
- 1,798
- 1,570
Kweli kbsa maana weekend imepoa sana hii hamna mechMkuu singanojr salute [emoji111] weekend hii tushushie vitu Mkuu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kweli kbsa maana weekend imepoa sana hii hamna mechMkuu singanojr salute [emoji111] weekend hii tushushie vitu Mkuu
asante kwa simulizi nzuri mkuu, Roma atarudi kweli, atafanikiwa kumkula Edna?SEHEMU YA 82
BUDDAPEST- HUNGARY 1990
Ni asubuhi na mapema ndani ya mji mkuu wa Hungaria unaofahamika kwa jina la Budapest, mji ambao una wakazi Zaidi ya milioni moja, pembezoni mwa mto Danubi inaonekana familia nzima ya Mzee Kovac Smith ikiwa mezani kwa ajjili ya chai ya asubuhhi , wazungu wanaita Breakfast.
Jumla ya wanafamilia hawa ni Wanne , yaani Mzee Kovac mwenyewe ambaye ni tajiri maarufu ndani ya jiji hili la Buddapest , lakini pia alikuwepo Anna ambaye ni mke wa Kovac pamoja na watoto wao wawili , yaani Levente pamoja na dada yake Zoe.
Zoe na Levente walionekana kwenye mavazi yao ya shule huku mzee Kovac akiwa kwenye mavazi yake ya suti , akiwa ashajiandaa kwenda kwenye biashara zake , kwani mzee huyu alikuwa akimiliki kampuni yake ndani ya jiji hili la Buddapest.
“Levente mwalimu wako jana kanipigia simu , mara nyingi unaondoka kabla ya vipindi kuisha , nataka uniambie unaendaga wapi?”Aliongea Bi Anna kwa lugha ya kihungari, huku akiwamngalia Levente ambaye alikuwa na nywele zake za kujikunjakunja , ni kama alikuwa amevalishwa wigi na macho yake flani hivi ya rangi ya blue .
Levente alimwangalia mama yake na kisha akamgeukia baba yake ambaye alimpa ishara ya kumjibu mama yake kwa swali aliloulizwa , lakini licha ya kijana huyu kuulizwa swali hilo alionekana kukosa majibu.
“Dadi Levente kila siku anasoma hadithi za miungu ya Ugiriki”aliongea Zoe na kuwafanya wazazi hawa wamawangalie Levente.
Walikuwa wakijua moja ya hobi ya kijana Levente ni kusoma hadithi , tena hadithi ambazo zilikuwa zikihusiana na miungu ya kale , lakini licha ya wazazi hawa kujua hilo walichukulia tu jambo hilo kama hobi kwa mtoto wao.
“Levente what do you want to Acoomplish in the future”
“I want to revive the Greek God`s”Aliongea Levente akimaanisha kwamba anataka kufufua miungu ya kale ya Ugiriki baada ya kuulizwa na baba yake ni jambo gani anataka kukamilisha kwenye maisha yake ya baadae.
Jibu hilo lilimuacha mdomo wazi Mr Kovac , kwanza alishangazwa na jibu hilo kwani Levente ndio kwanza alikuwa na miaka saba, lakini wazazi hawa walichukulia swala hilo kawaida tu kwa mtoto kuota mambo ambayo hayawezekani kutokana na umri wake.
“Kama kweli unahitaji kufufua miungu ya Ugiriki unatakiwa kusoma kwa bidii”Aliongea Kovac ili tu kumfanya mtoto wake asome kwa bidii , kwani aliona ndoto yake haikuwa na uhalisia wowote, lakini mzee huyu pia alikuwa akiamini Levente atakuja kukamilisha jambo kubwa sana kwenye maisha yake kutokana na uwezo wake mkubwa wa akili, kiufupi Levente alikuwa ni Genius.
Utaratibu wa familia hii ni kabla ya Mzee Kovac kwenda kwenye majukumu yake lazima awapeleke watoto wake wote kwenye shule ambayo kila mmoja wao alikuwa akisomea na baada ya hapo ndio ataelekea kazini kwake , sio kama alishindwa kuwapa wafanyakazi ,bwana huyu kufanya hivyo , ila ni ile hali ya kupenda kufanya hivyo tu ndio iliomfanya Mzee huyu kuwapelekea watoto wake mwenyewe.
Zoe kalikuwa ni kasichana karembo kweli ukikaangalia m, unaweza kumfananisha na Rihana kwa muonekano wake , na macho yake yenye kiini cha rangi ya bluu , alikuwa ni kivutio sana kwa watoto wenzake , lakini pia kwa watu wazima na jambo hili lilimfanya Mzee Kovac kumpenda sana mke wake kwa kumletea duniani mtoto wa kike mzuri kiasi hiko, alijivunia kama baba kila alipokuwa akiongozana na watoto wake kwenda shuleni.
Mzee kovac aliwaacha watoto wake kama kawaida baada ya kuwafikisha sehemu husika , huku akimpa msisitizo Levente kutokipindia vipindi.
Baada ya kuhakikisha watoto wake washaingia darasani alipanda gari yake na kutokomea kazini katikati ya jiji.
Lakini baada ya dakika kama kumi na tano ya Mzee Kovac kupotelea na gari yake Levente alisogea upande wa Barabarani , kwani shule yao ilikuwa pembezoni mwa barabara iliokuwa ikiunganisha Budapest na baadhi ya sehemu zingine kama vile Bratislava na Slovakia.
Sasa Levente ile ya kufika tu barabarani ilisimama gari aina ya Trabant(Gari maarufu sana za miaka ya tisini ndani ya Budapest) na Levente aliingia ndani ya gari hio na ikaondolewa kwa spidi.
Ndani ya madakika chache tu , walikuwa wakiingia ndani msitu wa Gemence,msitu ambao ni sehemu ya mbuga ya wanyama inayofahamika kwa jina la Duna.
Gari aliopanda Levente ilikuja kusimama baada ya kutoka barabara kuu na kuingia upande wa kushoto kilometa moja, sehemu iliokuwa na nyumba ndogo tu ambayo kwa harakaharaka ungeiona ni nyumba ya chumba kimoja tu na jiko.
Levente mara baada ya kutoka akiwa na uniform zake alitingishiana kichwa na bwana mmoja mwenye ndevu nyingi mtu mzima ambaye ndie aliekuwa dereva na kisha bwana huyo akageuza gari na kuondoka , yaani kwa hali ni kama jamaa huyo alimleta tu Levente ndani ya eneo hilo .
Baada ya levente kuingia ndani ya kile kijumba alimsogelea mzee mmoja hivi mzee sana ambaye alikuwa na mindevu mingi ambayo ina mvi , kwa kumwangalia tu huyu mzee ungejua hana siku nyingi za kuishi duniani, nywele zake zote zilikuwa nyeupe na alikuwa akiota moto.
“Professor Banos , I am Here”Aliongea Levente na Babu ambaye alikuwa akiitwa Profesa Banos alitingisha kichwa kivivu sana.
Levente alitoa mikate iliokuwa kwenye begi lake , na haikujulikana aliiweka saa ngapi na kisha alimsogezea profesa Banosi na kumpatia , haikueleweka kwanini mtu anefahamika kwa jina la Profesa akaishi msituni na , msitu huu ulikuwa ukitisha kwelikweli ndani ya miaka hio , hakukua na sauti Zaidi ya ndege na baadhi ya wanyama waliokuwa wakiongea kwa lugha zao.
“Nenda kamalizie Projekti , hakikisha unafuata taratibu na hatua nilizokueleza”Aliongea mzee huyu kivivu kwa lugha ya kihungaria na Levente alitingisha kichwa na akageuka na kusogelea Zulia la mkeka lililotandikwa chini na kisha akafungua mlango wa mbao na kutumbukia ndani kwa kutumia ngazi.
Eneo la sehemu ambayo Levente ameingia halikuwa na mwanga mwingi , ila kulikuwa na taa zilizofungwa za umeme , haikujulikana chanzo cha umeme huo ni nini.
Lakini ndani ya eneno hili kulikuwa ni kama maabara ambazo muonekano wake ni ule wa kizamani kabisa na haikua ya kisasa sana, chini hakukuwa na sakafu ya kujengwa Zaidi ya mchanga , lakini mpangilio ulikuwa ni mzuri kwani kulia na kushoto kulikuwa na vifaa vingi vya Mbao halafu katikati kulikuwa na meza ndefu ambayo ilikuwa na madumu ya maj, hili eneo lilikuwa ni kubwa na kwa harakaharaka utatambua hili eneo ni Handaki.
Levente baada ya kusogea mita kadhaa mbele aliingia kwenye chumba kidogo upande wa kulia na ile anatoka alikuwa amebadilika , alivaa mavazi mengine mfano wa yale ya kidaktari (PPE) lakini muundo wa kizamani.
Kwa urefu na umri vilimfanya Levente kushangaza sana , kwani usingeamini mtoto kama huyo ambaye ndio kwanza ameingia darasa la kwanza , ndio mwenye kufanya mambo kama hayo , ilikuwa ikishangaza , lakini pia kuthibitisha uwezo wa akili wa Levente kwa wakati mmoja.
Eneo hili la handaki lilikuwa na kona nne ukitembea mpaka katikati unakutana na muunganiko wa sehemu nne zilizojengwa kwa muudno wa msalaba , na kwa jinsi palivyokuwa ni Dhahiri eneo hili lilijengwa miaka mingi sana kwani kwa juu kulikuwa na uozo na majani majani aina ya’Fern’.
Basi Levente mara baada ya kufika katikati alichukuwa kona inayoelekea magharibi na hapa ndipo alipoingia kwenye uwazi ambao ulikuwa na meza katikati ambazo zote zilikuwa na maboksi ambayo yalikuwa yamejengwa kwa mfumo wa kama vibanda vya kufugia kuku kwani pande zote nne zilikuwa zimezibwa na mbao lakini upande mmoja ulikuwa na uwazi uliokuwa na wavu na karatasi ngumu inayopitisha mwanga(Transparent)
Pembeni kutoka kwenye meza hii kubwa ambayo ilikuwa imejengezwa maboksi kwa juu kulikuwa na makabati yaliotengenezwa kwa muundo mzuri tu na kila kabati likiwa na mlango pamoja na kitasa pamoja na jina.
12 GOD`S( Zeus,Athena , Hermes , Hades ,Aphrodite, Demeter,Hera ,Dionysus,Appolo,Ares,Poseidon,Artemis)Hayo ndio majina yaliokuwa yameandikwa kwa kila mlango wa kabati hizo kwa jumla yake kumi na mbili huku chini yake ya hizo kabati kukiwa na neno ‘SPECIMENS’
Kwenye meza pia kulikuwa na jumla ya makabati kumi na mbili yaliokuwa na majina sawa kama ilivyokuwa kwenye makabati ya ukurani.
Sasa baada ya Levente kuingia hapa ndani kwanza alitabasamu na mwili wake ukamsisimka.
Ndani ya aya makabati ambayo yalikuwa kwenye meza kulikuwa na mapanya makubwa tu, kwa ukubwa wa panya buku.
Levente alipita kwa kila boksi huku akiangalia mapanya hayo kwa tabasamu kubwa , yaani kijana huyu alionekana kufurahishwa na uwepo wa mapanya ndani ya hilo eneo , alitembea taratibu mpaka alivyofika kwenye boksi la Ares.
“Ares leo nitaanza na wewe”Aliongea mtoto huyu anaekwenda kwa jina la Levente na kisha alisogelea kabati lililokuwa lipo hapo ndani kenye jina la Ares na kisha akalifungua na kutoa aina flani hivi ya unga mfano wa poda uliokuwa kwenye chupa na kisha akauweka kwenye kiganja cha mkono wake na akafungua kwa upande wa juu wa kibanda cha panya na kisha alimwaga ule unga na Panya lile lilianza kula kwa fujo ule unga wa poda na kumfanya Mtoto Levente kutabasamu , na ndani ya dakika chache tu Panya lile lilidondoka chini na kulala.
Baada ya levente kuona panya lenye jina la Ares limedondoka chini na kulala , aligeukia kabati kwa mara nyingine na akatoa vichupa viwili, kimoja kikiwa na jina la Al-Virus huku kikiwa na chata ya fuvu , na kijichupa kingine kikiwa na picha ya moto , huku chini kikiwa na jina la ‘Stabilizer’ majina yote yalikuwa yameandikwa kwa lugha ya kingereza.
Alivuta bomba kubwa kama zile za hospitalini na kisha baada ya hivyo alichukua kile kichupa kilichokuwa na majimaji na kisha akaweka sindano na kutoboa kwa upande wa juu na kunyonya yale maji kwenye kijichupa kile kiasi , kisha akaweka sindano ile na Bomba mezani.
Alitumia hatua za wali kutoa tena maji ya kwenye kijichupa(vials) kingine na kuweka mezani , na baada ya hapo akafungua kwa mkono kabati la panya alielala na kisha akamtoa na kumuweka mezani.
Licha ya kuwa mtoto lakini alikuwa hana hofu kabisa, na alionekana kujiamini kwa asilimia mia moja huyu mtoto wa kizungu, baada ya taratibu hizo , alichukua bomba la kwanza na kisha akamchoma panya yule na sindano ya Kirusi Al na baada ya hapo akachoma tena sindano ya ‘Stabilizer’ na baada ya kuridhika alimrudisha panya yule kwenye boksi na akafunga na kisha aliangalia saa ya mshale ya kizamani iliokuwa kwenye meza na ni kama alikuwa akihesabu dakika , ilichukua dakika kumi tu kupita , lile panya lilishituka , lakini awamu hii ililikuwa likiongezeka ukubwa kama vile tofu la unga wa ngano ambalo limetiwa hamira , yaani panya alikuwa ni panya buku lakini kadiri muda ulivyokuwa unaongezeka , alikuwa akizidi kuwa mkubwa kiasi kwamba Levente alikuwa na hofu, kwani aliona kama panya huyo anakwenda kupasuka.
“Come on Ares , Don’t bust … Come on Ares”Aliongea kijana huyu kwa sauti yake ya kitoto iliosikika ndani ya chumba hiki kwa dakika kadhaa , huku panya lile likizidi kuwa kubwa na sasa lilikuwa likilingana na sungura ambaye ana mimba ya watoto wengi , na tumbo la panya lile lilikuwa likicheza cheza kama spika inayopiga mdundo mzito huku likiwa limesimama sehemu moja bila kusogea.
Levente alionekana kuwa na wasiwasi kweli , alikuwa akiliangalia panya hilo kwa umakini sana , huku akihesabu kila dakika, kijana huyu mdogo aliendelea kuangalia saa kwa wasiwasi , huku panya lile lenye ukubwa wa sungura sasa lilikuwa limeacha kuongezeka lakini tumbo lake liliendelea kucheza cheza kama vile dundo la Singeli.
“Yeeee..ssss!, Yes, yes …..”Kijana huyu furaha ilimtawala huku akishangilia mpaka akakaa chini na kuinuka kwa wakati mmoja , wakati huu panya buku mwenye ukubwa wa Sungura tumbo lake lilikuwa limeacha kucheza sana na sasa lilienda kawaida.
‘Boom’
Ulikuwa ni mpasuko wa kikabati kilichokuwa na Panya lile ndani na kutoboa kwa nguvu na kwenda kugonga kwenye makabati ya upande wa pili kiasi kwamba mshindo wa nguvu ulisambaa kwenye chumba chote.
Kijana mdogo Levente alianza kuogopa kwani alikoswa koswa na Panya hili, ambalo sasa lilikuwa lipo bila ya kizuizi chochote,Levente baada ya kuona hali imebadilika kalianza kukimbia na kusimama upande wa kabati kwa nyuma karibu na mlango akiendelea kuangalia lile panya ambalo sasa lilikuwa likijipigiza kwa nguvu ukutani kama vile limepandwa na kichaa.
Lakini wakati huu sasa Levente wakati akiwa anafurahia na mafanikio hayo ,kwani ilionekana ndio kitu alichokuwa akitaka kitokee , mara alisikia shindo za viatu zilizokuwa zikija nyuma yake.
“Profesa Ban…..”Aliita lakini kabla hajamaliza.
“Paaa… Paaaa”
Ni risasi mbili zilizopigwa kwa wakati mmoja na kwenda kutua kwa kijana Levente na palepale vazi lake la kidaktari likachafuka kwa damu na huo ndio ukawa mwisho wa Mtoto Genius Levente.
Hakuwa mtu mmoja tu alieingia hapa ndani , walikuwa kama watano hivi huku wote wakiwa wamevalia mavazi meusi , huku wakiwa wameziba pua zao na mavifaa flani hivi kama yale ya wapiga mbizi ambayo yalionesha yalikuwa yakiwapa hewa safi.
“Chukua kila kitu kwenye makabati,Mnadakika moja tu”
Aliongea Bwana ambaye aliumtandika Levente kwa risasi na akasogelea lile panya na kulitandika na Risasi mfufulizo na palepale likalala chini likiwa linaonesha hali ya kufa na yule bwana aliekuwa na mabuti marefu meusi , ambayo yalieonesha kama ni ya kijeshi , alianza kuweka vitu kama sumaku kwenye meza ile ya mbao kwa kila boksi lenye panya na ile kumaliza tu na vijana wake watatu walikuwa washaweka kila kitu kwenye masanduku yao ya chuma waliokuwa wamebeba na kisha wakapeana ishara na kuondoka ndani ya eneo hili.
Nje kabisa Profesa Banosi alionekana kufa muda mrefu kwa kupigwa Risasi pia.
Wale watu ambao walikuwa na sare ambazo hazikueleweka ni watu waliotoka wapi, walionekana kuja na chopa yenye rangi za kijeshi ambayo bado ilionekana ikizungusha panga lake huku rubani akionekana akiwaangalia mabwana hawa waliokuwa wakiisogelea chopa kwa mwendo wa kujiamini kabisa.
Baada ya wote kuingia kwenye Chopa ilinyanyuliwa na kuacha upepo uliokuwa ukipeperusha miti na ile wanafika usawa wa juu tu.
‘Boom,Boom,Booom’
Ikawa ndio mwisho wa Profesa Banosi pamoja na kijana mdogo Levente na projekti yao , kijana akawa amekufa na ndoto yake ya kufufua miungo ya kigiriki , kwani walikuwa wamelipuliwa na mabomu ambayo yalifanya eneo hilo kutitia na kufunikwa na mchanga , ni kama walizikwa kabisa.
Hii ni historia iliotokea miaka hio ya Tisini ndani ya jiji la Budappest msitu wa Gemence , nini kilitokea baada ya hapo kwa Tajiri Kovac , Zoe na Bi Anna.
ITAENDELEA. JUMATANO
UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 100 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA
NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
Duuuh mambo yanazidi kuwa ya motoSEHEMU YA 82
BUDDAPEST- HUNGARY 1990
Ni asubuhi na mapema ndani ya mji mkuu wa Hungaria unaofahamika kwa jina la Budapest, mji ambao una wakazi Zaidi ya milioni moja, pembezoni mwa mto Danubi inaonekana familia nzima ya Mzee Kovac Smith ikiwa mezani kwa ajjili ya chai ya asubuhhi , wazungu wanaita Breakfast.
Jumla ya wanafamilia hawa ni Wanne , yaani Mzee Kovac mwenyewe ambaye ni tajiri maarufu ndani ya jiji hili la Buddapest , lakini pia alikuwepo Anna ambaye ni mke wa Kovac pamoja na watoto wao wawili , yaani Levente pamoja na dada yake Zoe.
Zoe na Levente walionekana kwenye mavazi yao ya shule huku mzee Kovac akiwa kwenye mavazi yake ya suti , akiwa ashajiandaa kwenda kwenye biashara zake , kwani mzee huyu alikuwa akimiliki kampuni yake ndani ya jiji hili la Buddapest.
“Levente mwalimu wako jana kanipigia simu , mara nyingi unaondoka kabla ya vipindi kuisha , nataka uniambie unaendaga wapi?”Aliongea Bi Anna kwa lugha ya kihungari, huku akiwamngalia Levente ambaye alikuwa na nywele zake za kujikunjakunja , ni kama alikuwa amevalishwa wigi na macho yake flani hivi ya rangi ya blue .
Levente alimwangalia mama yake na kisha akamgeukia baba yake ambaye alimpa ishara ya kumjibu mama yake kwa swali aliloulizwa , lakini licha ya kijana huyu kuulizwa swali hilo alionekana kukosa majibu.
“Dadi Levente kila siku anasoma hadithi za miungu ya Ugiriki”aliongea Zoe na kuwafanya wazazi hawa wamawangalie Levente.
Walikuwa wakijua moja ya hobi ya kijana Levente ni kusoma hadithi , tena hadithi ambazo zilikuwa zikihusiana na miungu ya kale , lakini licha ya wazazi hawa kujua hilo walichukulia tu jambo hilo kama hobi kwa mtoto wao.
“Levente what do you want to Acoomplish in the future”
“I want to revive the Greek God`s”Aliongea Levente akimaanisha kwamba anataka kufufua miungu ya kale ya Ugiriki baada ya kuulizwa na baba yake ni jambo gani anataka kukamilisha kwenye maisha yake ya baadae.
Jibu hilo lilimuacha mdomo wazi Mr Kovac , kwanza alishangazwa na jibu hilo kwani Levente ndio kwanza alikuwa na miaka saba, lakini wazazi hawa walichukulia swala hilo kawaida tu kwa mtoto kuota mambo ambayo hayawezekani kutokana na umri wake.
“Kama kweli unahitaji kufufua miungu ya Ugiriki unatakiwa kusoma kwa bidii”Aliongea Kovac ili tu kumfanya mtoto wake asome kwa bidii , kwani aliona ndoto yake haikuwa na uhalisia wowote, lakini mzee huyu pia alikuwa akiamini Levente atakuja kukamilisha jambo kubwa sana kwenye maisha yake kutokana na uwezo wake mkubwa wa akili, kiufupi Levente alikuwa ni Genius.
Utaratibu wa familia hii ni kabla ya Mzee Kovac kwenda kwenye majukumu yake lazima awapeleke watoto wake wote kwenye shule ambayo kila mmoja wao alikuwa akisomea na baada ya hapo ndio ataelekea kazini kwake , sio kama alishindwa kuwapa wafanyakazi ,bwana huyu kufanya hivyo , ila ni ile hali ya kupenda kufanya hivyo tu ndio iliomfanya Mzee huyu kuwapelekea watoto wake mwenyewe.
Zoe kalikuwa ni kasichana karembo kweli ukikaangalia m, unaweza kumfananisha na Rihana kwa muonekano wake , na macho yake yenye kiini cha rangi ya bluu , alikuwa ni kivutio sana kwa watoto wenzake , lakini pia kwa watu wazima na jambo hili lilimfanya Mzee Kovac kumpenda sana mke wake kwa kumletea duniani mtoto wa kike mzuri kiasi hiko, alijivunia kama baba kila alipokuwa akiongozana na watoto wake kwenda shuleni.
Mzee kovac aliwaacha watoto wake kama kawaida baada ya kuwafikisha sehemu husika , huku akimpa msisitizo Levente kutokipindia vipindi.
Baada ya kuhakikisha watoto wake washaingia darasani alipanda gari yake na kutokomea kazini katikati ya jiji.
Lakini baada ya dakika kama kumi na tano ya Mzee Kovac kupotelea na gari yake Levente alisogea upande wa Barabarani , kwani shule yao ilikuwa pembezoni mwa barabara iliokuwa ikiunganisha Budapest na baadhi ya sehemu zingine kama vile Bratislava na Slovakia.
Sasa Levente ile ya kufika tu barabarani ilisimama gari aina ya Trabant(Gari maarufu sana za miaka ya tisini ndani ya Budapest) na Levente aliingia ndani ya gari hio na ikaondolewa kwa spidi.
Ndani ya madakika chache tu , walikuwa wakiingia ndani msitu wa Gemence,msitu ambao ni sehemu ya mbuga ya wanyama inayofahamika kwa jina la Duna.
Gari aliopanda Levente ilikuja kusimama baada ya kutoka barabara kuu na kuingia upande wa kushoto kilometa moja, sehemu iliokuwa na nyumba ndogo tu ambayo kwa harakaharaka ungeiona ni nyumba ya chumba kimoja tu na jiko.
Levente mara baada ya kutoka akiwa na uniform zake alitingishiana kichwa na bwana mmoja mwenye ndevu nyingi mtu mzima ambaye ndie aliekuwa dereva na kisha bwana huyo akageuza gari na kuondoka , yaani kwa hali ni kama jamaa huyo alimleta tu Levente ndani ya eneo hilo .
Baada ya levente kuingia ndani ya kile kijumba alimsogelea mzee mmoja hivi mzee sana ambaye alikuwa na mindevu mingi ambayo ina mvi , kwa kumwangalia tu huyu mzee ungejua hana siku nyingi za kuishi duniani, nywele zake zote zilikuwa nyeupe na alikuwa akiota moto.
“Professor Banos , I am Here”Aliongea Levente na Babu ambaye alikuwa akiitwa Profesa Banos alitingisha kichwa kivivu sana.
Levente alitoa mikate iliokuwa kwenye begi lake , na haikujulikana aliiweka saa ngapi na kisha alimsogezea profesa Banosi na kumpatia , haikueleweka kwanini mtu anefahamika kwa jina la Profesa akaishi msituni na , msitu huu ulikuwa ukitisha kwelikweli ndani ya miaka hio , hakukua na sauti Zaidi ya ndege na baadhi ya wanyama waliokuwa wakiongea kwa lugha zao.
“Nenda kamalizie Projekti , hakikisha unafuata taratibu na hatua nilizokueleza”Aliongea mzee huyu kivivu kwa lugha ya kihungaria na Levente alitingisha kichwa na akageuka na kusogelea Zulia la mkeka lililotandikwa chini na kisha akafungua mlango wa mbao na kutumbukia ndani kwa kutumia ngazi.
Eneo la sehemu ambayo Levente ameingia halikuwa na mwanga mwingi , ila kulikuwa na taa zilizofungwa za umeme , haikujulikana chanzo cha umeme huo ni nini.
Lakini ndani ya eneno hili kulikuwa ni kama maabara ambazo muonekano wake ni ule wa kizamani kabisa na haikua ya kisasa sana, chini hakukuwa na sakafu ya kujengwa Zaidi ya mchanga , lakini mpangilio ulikuwa ni mzuri kwani kulia na kushoto kulikuwa na vifaa vingi vya Mbao halafu katikati kulikuwa na meza ndefu ambayo ilikuwa na madumu ya maj, hili eneo lilikuwa ni kubwa na kwa harakaharaka utatambua hili eneo ni Handaki.
Levente baada ya kusogea mita kadhaa mbele aliingia kwenye chumba kidogo upande wa kulia na ile anatoka alikuwa amebadilika , alivaa mavazi mengine mfano wa yale ya kidaktari (PPE) lakini muundo wa kizamani.
Kwa urefu na umri vilimfanya Levente kushangaza sana , kwani usingeamini mtoto kama huyo ambaye ndio kwanza ameingia darasa la kwanza , ndio mwenye kufanya mambo kama hayo , ilikuwa ikishangaza , lakini pia kuthibitisha uwezo wa akili wa Levente kwa wakati mmoja.
Eneo hili la handaki lilikuwa na kona nne ukitembea mpaka katikati unakutana na muunganiko wa sehemu nne zilizojengwa kwa muudno wa msalaba , na kwa jinsi palivyokuwa ni Dhahiri eneo hili lilijengwa miaka mingi sana kwani kwa juu kulikuwa na uozo na majani majani aina ya’Fern’.
Basi Levente mara baada ya kufika katikati alichukuwa kona inayoelekea magharibi na hapa ndipo alipoingia kwenye uwazi ambao ulikuwa na meza katikati ambazo zote zilikuwa na maboksi ambayo yalikuwa yamejengwa kwa mfumo wa kama vibanda vya kufugia kuku kwani pande zote nne zilikuwa zimezibwa na mbao lakini upande mmoja ulikuwa na uwazi uliokuwa na wavu na karatasi ngumu inayopitisha mwanga(Transparent)
Pembeni kutoka kwenye meza hii kubwa ambayo ilikuwa imejengezwa maboksi kwa juu kulikuwa na makabati yaliotengenezwa kwa muundo mzuri tu na kila kabati likiwa na mlango pamoja na kitasa pamoja na jina.
12 GOD`S( Zeus,Athena , Hermes , Hades ,Aphrodite, Demeter,Hera ,Dionysus,Appolo,Ares,Poseidon,Artemis)Hayo ndio majina yaliokuwa yameandikwa kwa kila mlango wa kabati hizo kwa jumla yake kumi na mbili huku chini yake ya hizo kabati kukiwa na neno ‘SPECIMENS’
Kwenye meza pia kulikuwa na jumla ya makabati kumi na mbili yaliokuwa na majina sawa kama ilivyokuwa kwenye makabati ya ukurani.
Sasa baada ya Levente kuingia hapa ndani kwanza alitabasamu na mwili wake ukamsisimka.
Ndani ya aya makabati ambayo yalikuwa kwenye meza kulikuwa na mapanya makubwa tu, kwa ukubwa wa panya buku.
Levente alipita kwa kila boksi huku akiangalia mapanya hayo kwa tabasamu kubwa , yaani kijana huyu alionekana kufurahishwa na uwepo wa mapanya ndani ya hilo eneo , alitembea taratibu mpaka alivyofika kwenye boksi la Ares.
“Ares leo nitaanza na wewe”Aliongea mtoto huyu anaekwenda kwa jina la Levente na kisha alisogelea kabati lililokuwa lipo hapo ndani kenye jina la Ares na kisha akalifungua na kutoa aina flani hivi ya unga mfano wa poda uliokuwa kwenye chupa na kisha akauweka kwenye kiganja cha mkono wake na akafungua kwa upande wa juu wa kibanda cha panya na kisha alimwaga ule unga na Panya lile lilianza kula kwa fujo ule unga wa poda na kumfanya Mtoto Levente kutabasamu , na ndani ya dakika chache tu Panya lile lilidondoka chini na kulala.
Baada ya levente kuona panya lenye jina la Ares limedondoka chini na kulala , aligeukia kabati kwa mara nyingine na akatoa vichupa viwili, kimoja kikiwa na jina la Al-Virus huku kikiwa na chata ya fuvu , na kijichupa kingine kikiwa na picha ya moto , huku chini kikiwa na jina la ‘Stabilizer’ majina yote yalikuwa yameandikwa kwa lugha ya kingereza.
Alivuta bomba kubwa kama zile za hospitalini na kisha baada ya hivyo alichukua kile kichupa kilichokuwa na majimaji na kisha akaweka sindano na kutoboa kwa upande wa juu na kunyonya yale maji kwenye kijichupa kile kiasi , kisha akaweka sindano ile na Bomba mezani.
Alitumia hatua za wali kutoa tena maji ya kwenye kijichupa(vials) kingine na kuweka mezani , na baada ya hapo akafungua kwa mkono kabati la panya alielala na kisha akamtoa na kumuweka mezani.
Licha ya kuwa mtoto lakini alikuwa hana hofu kabisa, na alionekana kujiamini kwa asilimia mia moja huyu mtoto wa kizungu, baada ya taratibu hizo , alichukua bomba la kwanza na kisha akamchoma panya yule na sindano ya Kirusi Al na baada ya hapo akachoma tena sindano ya ‘Stabilizer’ na baada ya kuridhika alimrudisha panya yule kwenye boksi na akafunga na kisha aliangalia saa ya mshale ya kizamani iliokuwa kwenye meza na ni kama alikuwa akihesabu dakika , ilichukua dakika kumi tu kupita , lile panya lilishituka , lakini awamu hii ililikuwa likiongezeka ukubwa kama vile tofu la unga wa ngano ambalo limetiwa hamira , yaani panya alikuwa ni panya buku lakini kadiri muda ulivyokuwa unaongezeka , alikuwa akizidi kuwa mkubwa kiasi kwamba Levente alikuwa na hofu, kwani aliona kama panya huyo anakwenda kupasuka.
“Come on Ares , Don’t bust … Come on Ares”Aliongea kijana huyu kwa sauti yake ya kitoto iliosikika ndani ya chumba hiki kwa dakika kadhaa , huku panya lile likizidi kuwa kubwa na sasa lilikuwa likilingana na sungura ambaye ana mimba ya watoto wengi , na tumbo la panya lile lilikuwa likicheza cheza kama spika inayopiga mdundo mzito huku likiwa limesimama sehemu moja bila kusogea.
Levente alionekana kuwa na wasiwasi kweli , alikuwa akiliangalia panya hilo kwa umakini sana , huku akihesabu kila dakika, kijana huyu mdogo aliendelea kuangalia saa kwa wasiwasi , huku panya lile lenye ukubwa wa sungura sasa lilikuwa limeacha kuongezeka lakini tumbo lake liliendelea kucheza cheza kama vile dundo la Singeli.
“Yeeee..ssss!, Yes, yes …..”Kijana huyu furaha ilimtawala huku akishangilia mpaka akakaa chini na kuinuka kwa wakati mmoja , wakati huu panya buku mwenye ukubwa wa Sungura tumbo lake lilikuwa limeacha kucheza sana na sasa lilienda kawaida.
‘Boom’
Ulikuwa ni mpasuko wa kikabati kilichokuwa na Panya lile ndani na kutoboa kwa nguvu na kwenda kugonga kwenye makabati ya upande wa pili kiasi kwamba mshindo wa nguvu ulisambaa kwenye chumba chote.
Kijana mdogo Levente alianza kuogopa kwani alikoswa koswa na Panya hili, ambalo sasa lilikuwa lipo bila ya kizuizi chochote,Levente baada ya kuona hali imebadilika kalianza kukimbia na kusimama upande wa kabati kwa nyuma karibu na mlango akiendelea kuangalia lile panya ambalo sasa lilikuwa likijipigiza kwa nguvu ukutani kama vile limepandwa na kichaa.
Lakini wakati huu sasa Levente wakati akiwa anafurahia na mafanikio hayo ,kwani ilionekana ndio kitu alichokuwa akitaka kitokee , mara alisikia shindo za viatu zilizokuwa zikija nyuma yake.
“Profesa Ban…..”Aliita lakini kabla hajamaliza.
“Paaa… Paaaa”
Ni risasi mbili zilizopigwa kwa wakati mmoja na kwenda kutua kwa kijana Levente na palepale vazi lake la kidaktari likachafuka kwa damu na huo ndio ukawa mwisho wa Mtoto Genius Levente.
Hakuwa mtu mmoja tu alieingia hapa ndani , walikuwa kama watano hivi huku wote wakiwa wamevalia mavazi meusi , huku wakiwa wameziba pua zao na mavifaa flani hivi kama yale ya wapiga mbizi ambayo yalionesha yalikuwa yakiwapa hewa safi.
“Chukua kila kitu kwenye makabati,Mnadakika moja tu”
Aliongea Bwana ambaye aliumtandika Levente kwa risasi na akasogelea lile panya na kulitandika na Risasi mfufulizo na palepale likalala chini likiwa linaonesha hali ya kufa na yule bwana aliekuwa na mabuti marefu meusi , ambayo yalieonesha kama ni ya kijeshi , alianza kuweka vitu kama sumaku kwenye meza ile ya mbao kwa kila boksi lenye panya na ile kumaliza tu na vijana wake watatu walikuwa washaweka kila kitu kwenye masanduku yao ya chuma waliokuwa wamebeba na kisha wakapeana ishara na kuondoka ndani ya eneo hili.
Nje kabisa Profesa Banosi alionekana kufa muda mrefu kwa kupigwa Risasi pia.
Wale watu ambao walikuwa na sare ambazo hazikueleweka ni watu waliotoka wapi, walionekana kuja na chopa yenye rangi za kijeshi ambayo bado ilionekana ikizungusha panga lake huku rubani akionekana akiwaangalia mabwana hawa waliokuwa wakiisogelea chopa kwa mwendo wa kujiamini kabisa.
Baada ya wote kuingia kwenye Chopa ilinyanyuliwa na kuacha upepo uliokuwa ukipeperusha miti na ile wanafika usawa wa juu tu.
‘Boom,Boom,Booom’
Ikawa ndio mwisho wa Profesa Banosi pamoja na kijana mdogo Levente na projekti yao , kijana akawa amekufa na ndoto yake ya kufufua miungo ya kigiriki , kwani walikuwa wamelipuliwa na mabomu ambayo yalifanya eneo hilo kutitia na kufunikwa na mchanga , ni kama walizikwa kabisa.
Hii ni historia iliotokea miaka hio ya Tisini ndani ya jiji la Budappest msitu wa Gemence , nini kilitokea baada ya hapo kwa Tajiri Kovac , Zoe na Bi Anna.
ITAENDELEA. JUMATANO
UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 100 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA
NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
Akirudi aanzeNa Roma Wako Chumbani na Edna banaJumatano mbona palefu
parefu sana atupe ata kimoja leo tutambeJumatano mbona palefu
Mbona alishaliwa kabla ya mkataba wa ndoaWatu wanataka kuona Edna analiwa tunda kimasihara [emoji2]
Very soon [emoji817]Akirudi aanzeNa Roma Wako Chumbani na Edna bana
Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
Watu wanataka atoe ushirikiano😀😀Mbona alishaliwa kabla ya mkataba wa ndoa
Ewaaaaaaa...ule ulikuwa ni ubakaji maana alikuwa tilalila ...tunataka atoe mzigo mwenyewe bila gogoro[emoji23][emoji23][emoji23]Watu wanataka atoe ushirikiano[emoji3][emoji3]
Kumbe leo Jumaatanoo wadau mnafuatilia kinyama aseeMkuu leo vipande viongezeke basi
Si ndio leo anko au ndio mpaka usku??Very soon [emoji817]