Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Wakuu hii kitu ni kali na haijaisha yaani ukitaka kuifaidi kama una nguvu ya kiuchumi ifate what's up.

Mkuu Singano jr big up
 
SEHEMU YA 88

Mrembo Edna hakuonekana kuwa na Amani kabisa siku nzima ya Jumamosi , licha ya kwamba siku hii alienda kazini , lakini ukweli ni kwamba hakuna jambo lolote la maana ambalo alifanya akiwa kazini , kichwa chake kilionesha hali ambayo haikuwa kwenye utulivu kabisa.

Na ilipotimu saa saba mchana alirudi moja kwa moja nyumbani huku akiendelea kuwaza ni kipi kimempata Roma mpaka wakati huo hajarudi nyumbani,licha ya kwamba Magdalena alikuwa amemtoa hofu ya kwamba Roma atarudi akiwa salama lakini bado hisia zake juu ya jambo baya kumtokea Roma zilikuwa juu.

“Miss Roma atarudi , hupaswi kuwa na wasiwasi sana”Aliongea Bi Wema ambaye alimuona Edna kwa jinsi alivyokuwa amenyongea mno, na aliona njia pekee ya kumuweka sawa ni kumfariji , licha ya kwamba hata yeye mwenyewe hakuwa na uhakika na kile ambacho kimemkuta Roma mpaka kutoonekana nyumbani kwa takribani masaa ishirini na nne.

Saa Tano kamili za usiku mrembo Edna alionekana bado hakuwa ni mwenye kupata usingizi kabisa , licha ya kwamba alikuwa akijilazimisha , aliishia kuangalia mdoli wake uliokuwa kwenye kitanda, mdoli ambao alikuwa amepewa na Roma kama zawaidi.

Ilikuwa ni asubuhi ya saa kumi na mbili Edna alionekana akiwa kwenye usingizi huku akiwa amekumbaitia mdoli wake , haikueleweka mrembo huyu alikuwa amelala saa ngapi , lakini kwa namna ambavyo amelala ilionesha kabisa, alipitiwa akiwa katikati ya kusubiria mume wake arudi.

Bi Wema alikuwa ashaamka kama kawaida mapema tu kwa ajili ya kufanya usafi na kuandaa kifungua kinywa , alikuwa akijua siku hii ya leo , kwa Edna alikuwa akitakiwa kwenda Kiwangwa kwa ajili ya kuwatembelea watoto yatima kama ilivyokuwa desturi yake.

Saa moja kama na nusu ndio muda ambao Edna alishuka kutoka kwenye chumba chake kwa ajili ya kunywa chai, alionekana tayari ashajiandaa kwani alikuwa ameshikilia mkoba wake kabisa akiwa amevaa na kupendeza.

“Morning Bi Wema”Alisalimia Edna huku akiketi kwenye kiti.

“Morning Miss ! ,Unaonekana kuchoka Edna, umepata usingizi kweli jana?”Aliuliza Bi wema huku akimwangalia Edna ambaye ni kweli alionekana kuwa mchovu tofauti na siku zingine.

“Bi Wema na mimi umenihesabu”Ilikuwa ni sauti iliowafanya Bi Wema na Edna kugeuza macho kumwangalia mtu aliekuwa akishuka kutoka juu , alikuwa ni Roma alievalia Track Suit.

“Mr Roma!! Umerudi saa ngapi?”Ilikuwa ni swali la Bi Wema huku Edna yeye akimwangalia Roma huku akiwa ni kama hakuwa akiamini kama mtu aliekuwa mbele yake ni Roma,lile fukuto la wasiwasi lilimshuka na sasa alijisikia ahueni.

“Niimerudi jana usiku Bi Wema,sikuona haja ya kuwaamsha,ilikuwa usiku sana”Aliongea Roma huku akisogea kwenye meza na kuketi , huku akimwangalia Edna ambaye muda wote alikuwa akimwangalia mwanaume aliekuwa mbele yake ni kama alikuwa akitafuta jambo ambalo halipo sawa kwenye mwili wa Roma.

“My Wife mumeo nimerudi , lakini huoneshi furaha”Aliongea Roma aliekuwa akimwangalia Edna.

“Ulienda wapi Roma bila hata ya kutupa taarifa unajua ni kiasi gani tulivyokuwa na wasiwasi”Aliongea Edna aliekuwa siriasi , maana kwa jinsi Roma alivyokuwa akionekana, hakuonesha dalili yoyote huko alipokuwepo kulikuwa na tatizo na ndio maana Edna mawazo mabaya yakaingia kwenye kichwa chake na kudhania huenda alikuwa kwa mwanamke.

“Ndio Mr Roma , Miss Edna alikuwa ni mwenye mawazo mengi sana juu yako , alikuwa akidhani kuna jambo baya limekutokea ndio maana hujaonekana tokea juzi usiku wa lile tukio”Aliongezea Bi Wema.

Ukweli ni kwamba Licha ya Roma kuulizwa hayo maswali , hakuwa tayari kumwambia mke wake au Bi Wema kama alikuwa akipigana na Ares na baada ya hapo akaenda kwenye sherehe na Rose na akaua Zaidi ya watu ishirini peke yake.

“Bi Wema nilikuwa na jambo ambalo limenifanya kushindwa kurudi mapema”Aliongea Roma huku akivuta kikombe na kujiwekea maziwa na Edna kwa jibu hilo aliona kabisa Roma alikuwa akimficha kumwambia ukweli wa sehemu aliotoka na hivyo hakuona haja ya kuendelea kuuliza sana, alichoshukuru kwake tu ni kama amerudi akiwa salama.

“Wife unaonaje tukienda wote kutembelea watoto leo?”.

“Itakuwa vyema Miss kama utaenda na Roma”Alikazia Bi Wema alijua wawili hao wakienda pamoja watapata wasaa wa kuwa karibu na huenda Roma akamweleza mke wake ni wapi alipokuwa na kuyajenga.

Edna Baada ya kuona Bi Wema na yeye kaunga mkono hoja hakuona sababu ya kupinga swala hilo.

Ndani ya dakika kadhaa tu Roma na Edna walikuwa wakitoka kwenye gari ya pamoja wakielekea Bagamoyo Kiwangwa kwa ajili ya kutembelea watoto yatima.

Edna ni kama hakuwa na dini , kwani hakueleweka kuwa mwislamu na pia hakueleweka kama ni mkristo, yeye alichoamini kwenye akili yake kusaidia wenye uhitaji ni njia sahihi ya yeye kumtumikia Mungu na ndio maana kila ifikapo jumapili siku yake ya mapumziko lazima aende akawatembelee watoto Yatima hawa waliokuwa ndani ya kituo cha Son and Daughter Orphanage.

Kwenye gari hakukua na stori kabisa , Edna alionekana kuchoka mno siku hii ya leo na Roma jambo hili lilimshangaza kwani mke wake alilala mapema tu , mahitaji ya kwenda nayo Edna aliagiza tokea jana hivyo m safari yao ilikuwa ni ya moja kwa moja.

Ndani ya masaa kadhaa tu walikuwa wakiingia ndani ya geti la kituo hiki , Roma alisalimiana na Mama Issa kwa ukarimu huku Edna kama kawaida alikuwa akisalimiana na watoto kwa furaha.

Roma alisaidiana na wafanyakazi kushusha mizigo na baadhi ya watoto pia ambao walikuwa wakubwa na ndani ya dakika chache zoezi hilo lilikuwa limemalizika.

Edna leo hii alichukua jukumu la kuwasimulia watoto hadithi , jambo ambalo lilimshangaza Roma , kwa jinsi alivyomuona Edna alijua hakuwa na uwezo wowote wa kujua baadhi ya hadthi za kitoto ,lakini Edna alionekana kuwa na hadithi nyingi ambazo ziliwavutia watoto kweli na walionekana kumsikiliza kwa umakini.

“Romaa..!!!”Ilikuwa ni sauti ambayo ilimshitua Roma ambae alikuwa amefumba macho kwa kuegamia kiti akianza kuutafuta usingizi kusogeza muda.

“Najma ..!!!!,Unafanya nini hapa?”Lilikuwa ni swali la Roma kwenda kwa mrembo Najma alievalia dela na ushungi wa kitambaa cha pinki , Roma alishangazwa na uwepo wa Najma ndani ya hiki kituo , hakuwa na taarifa kama Najma alikuwa akifanya kazi ya kufundisha hapa.

“Nafanya kazi hapa nina kama wiki mbili sasa”Aliongea Najma huku akionesha hali ya kuwa kawaida tu , hakuonesha hali ya utofauti labda kwa kushangaa kwanini Roma yupo hapa.

“Kumbe…!!”Aliongea Roma kwa mshangao huku akiwamnngalia mrembo huyu mwenye kuheshimu dini yake kwa jinsi alivyokuwa mpole , Roma hakuwa amekutana na Najma kwa kipindi cha muda mrefu kidogo , tokea siku aliompelekea Juma Hospitalini.

“Na wewe je? , sikuwa nikifahamu unakujaga huku”Aliongea Najma huku akiangalia upande wa Edna aliekuwa bize kuhadhithia watoto.

“Ndio sina tabia ya kutembelea sehemu kama hizi , nipo hapa na mke wangu”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna , ambaye sasa alionesha kumaliza kusimulia hadithi na watoto walikuwa wakitawanyika ,jambo ambalo lilimshanganza ni hadhithi gani hio ambayo Edna kawahadithia watoto kwa muda mfupi hivyo.

“Najma ..Umefika?”Aliongea Edna akiwa ni mwenye tabasamu akiwasogelea.

“Ndio shosti”Alijibu huku wakisogeleana na kukumbatiana na kumfanya Roma azidi kushangazwa na ukaribu wa Edna na Najma.

“Najma nilikuambia nitakutambulisha kwa mume wangu nadhani leo imetimia , huyu ni Roma ndio mume wangu ,Roma huyu ni rafiki yangu Bi Wema aliekuwa akikuambia na ambaye ananifundisha kupika , anaitwa Najma ni mwalimu hapa”Aliongea Edna pasipokujua kuwa Najma na Roma wanafahamiana.

“Nashukuru kukufahamu Mr Roma,hakika umepata mke mzuri sana”Aliongea Najma huku akiweka uso wa kuigiza mbele ya Roma na Edna.

“Nafurahi pia kukufahamu Najma rafiki wa mke wangu”Aliongea Roma na kisha akarudi kwenye kiti chake , huku Edna akiingizia Stori na Najma na kumfanya Roma apate ahueni , kwani mpaka hapo ni kama hali ya hewa kwake ilikuwa imebadilika na hakutaka tena kubaki hapo ndani.

“Roma leo nimechoka sitoweza kukaa muda mrefu inabidi tuondoke nikapumzike”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashukuru ndani kwa ndani maana hata yeye hakutaka kukaa hapo ndani , kwani kila alipokuwa akikutanisha macho na Najma alijiona kama mwanaume mwenye hatia mbele ya mrembo huyu.

Ndani ya kama nusu saa Roma na Edna walimaliza kuagana na Bi Issa kwa ajili ya kurejea nyumbani .

“Najma nitakupigia simu , nataka uje upaone ninapoishi sawa?”Aliongea wakati akiagana na Najma , wakati huu Roma alikuwa tayari kwenye gari na ashaliwasha.

“Sawa Edna nitakuja usijali”Aliongea Najma na baada ya hapo wakaachiana na Edna alipanda kwenye gari na Roma akalitoa taratibu.

Najma alishindwa kuelewa machozi yalitoka wapi , kwani yalianza kutiririka mfululizo pasipo ya yeye mwenywe kujielewa.

“Unaonekana kumpenda Roma”Ilikuwa ni sauti iliomgutusha Najma na kufuta machozi harakaharaka na kugeuka kwani sauti ilikuwa nyuma yake na ile anageuka alikutana na sura ya mwanaume ambaye hakuwa akimfahamu.

“Naitwa Elvice Temba”Aliongea mwanaume yule huku akiwamgalia Najma kwa tabasamu , haikueleweka Elvice kafika saa ngapi hapo ndani pasipo kuonana na Roma na Edna.

“Unaonekana kuwa huru mbele ya rafiki yako kuliko hata kwa Dorisi”Aliongea Roma wakati wakipita Kerege.

“Ndio nampenda sana Najma ni rafiki mzuri kwangu ,nipo huru kwake kutokana na kwamba ananichukulia kama rafiki ya levo sawa na yake , tofauti na Dorisi ambaye licha ya urafiki wetu ananichukulia pia kama bosi wake”.

“Hongera mke wangu kwa kupata rafiki mrembo”Aliongea Roma huku akiwa ni mwenye kutabasamu na Edna alimkodolea macho Roma , alijua ni nini huyu mwanaume anafikiria.

“Roma ole wako umguse Najma nakuambia utakuwa mwisho wetu ,nimeacha yapite kwa Dorisi na Nasra ila kwa Najma ni tofauti”

“Hey!!!,Wife mbona umefikiria mbali hivyo , yaani unaniona kila mwanamke mzuri nitalala nae”

“Sio kama nafikiria mbali na kutahadharisha tu , mimi sijali hao wanawake wako hata ulale na kila mwanamke hainihusu , ila sio kwa Najma”Aliongea Edna na kisha akaegamia kiti kuonesha hakutaka kuongea tena na ilibidi Roma akaze macho barabarani





*****

Rose licha ya kwamba Roma alimpigia simu kumtoa hofu ya kuwa sawa , lakini mwanadada huyu akili yake bado haikuwa sawa hata kidogo , kila alipokuwa akikumbuka tukio la jana moyo wake ulikuwa ukimuuma sana, kwanza kabisa mwanadada huyu alikuwa sio mwenye kujali na mabadiliko ya jana ya Roma , alikuwa ashajua tokea mwanzo Roma hakuwa ni mtu wa kawaida kabisa na alikuwa ashajiandaa kisaikolojia , lakini licha ya kwamba mwanadada huyu alikuwa akitegenea Roma kutokuwa wa kawaida ila mbadiliko ya jana yalikuwa ni ya kushangaza sana kwake , yaani ni mbadiliko ambayo hakuwa akiyategemea.

Rose aliona licha ya Roma kubadilika na kumuokoa katika hali kama ile ya kuzingirwa na kundi la Fupa Faru pamoja na Black Mamba , aliona kuna kitu ambacho hakikuwa sawa kwa upande wa Roma , alikuwa akikumbuka namna ambavyo Roma alikuwa akishindana na mwili wake , ni hisia ambazo ni kama alikuwa akipitia yeye , yaani kile ambacho kilikuwa kikiendelea kwa Roma ni kama kilikuwa kikiendelea kwenye mwili wake , aliona kabisa Roma alikuwa akishindana na maumivu , hakuelewa kwa uhakika hali ambayo alikuwa nayo Roma ,ila jambo moja ambalo mrembo huyu alikuwa na uhakika nalo ni kwamba Roma alikuwa akipitia maumivu makali lakini pia kushindana na mabadiliko yake yakimwili kiasi kilichomfanya Roma kupotea ndani ya eneo la tukio.

Unajua jana baada ya Roma kujitahidi kujirudisha katika hali ya kawaida na kushindwa , alichukua maamuzi ya kutoweka ndani ya tukio ili ugonjwa wake usije ukarudi na akapoteza uwezo wa kuiongoza akili yake na kuleta madhara , na kwa wakati ule jambo la pekee ambalo Roma aliona linaweza kumsaidia ni dawa ambazo alipewa na Profesa Clark wakati alipokuwa Japani , na ndio maana ile anapotea kwenye macho ya Rose alikuja kuibukia chumbani kwake kama jini na kumeza kidongea kimoja kati ya alivyokuwa amepewa na hapo ndipo aliporudi kwenye hali yake ya ubinadamu , licha ya kwamba alikuwa akipitia maumivu makali.

Rose alifanikiwa kumkamata baba yake na sasa alikuwa amemfungia kama Mateka , vijana wake waliendelea kusafisha vijana wa kundi la Situ waliokuw awameshikilia jimbo lake la kibiashara la Kibiti.

Upande wa Black Mamba hali haikuwa nzuri kwani vijana wote walionda kumsaidia Situ walikufa wote pamoja na kiongozi wao Hassani , Rose alikuwa amekasirishwa na kitendo cha Black Mamba kuingilia kwenye mgororo wake, yeye na baba yake na hili aliona hawezi kuliacha lipite kirahisi , alipanga kutumia uchokozi huo kwa faida yake ,na pia uzuri ni kwamba kundi la Black Mamba vijana wake wengi ambao waliokuwa ni tegemeo ndio hao ambao walikuwa wamekufa wakiwa pamoja na kiongozi wao na hii inamfanya Rose kuwa na kundi lenye nguvu Zaidi ndani ya jii la Dar es salaam katika biashara ya madawa ya kulevya.

Na alikuwa tayari ashafanya mawasiliano na Meya wa jiji la Dodoma kwa ajili ya wao kukutana kwani Rose alikuwa akimfahamu Meya huyu kama mtu aliekuwa akiongoza kwa siri kundi hili la Black Mamba, licha ya kwamba Meya alipokea kwa mshituko juu ya taarifa ya vijana wake wote kufariki , lakini kutokana na ukubwa wa tatizo alikubali kuonana na Rose na kuongea ili kuweka misingi yao ya kibiashara vizuri pasipo kuwa na ugomvi , lakini licha ya hivyo Rose hakutaka kulipitsha hivyohivyo , alipanga kuhakikisha Black Mamba wanalipa kwa uchokozi wao wa kuingilia mambo ambayo hayakuwa yakiwahusu.

******

Ilikuwa ni siku ya pili yake yaani jumanne Roma akiwa kazini , akiwa bize kucheza gemu , simu yake iliokuwa mfukoni ilianza kuita mfululizo kiasi cha kumfanya Asubirishe gemu lake alilokuwa akicheza na kuangalia ni kiumbe gani aliekuwa akimpigia muda huo , kwani hakuwa na watu wengi sana mbao humpigia mara kwa mara .

Baada ya kuangalia jina alikuta ni namba ngeni lakini ya kitanzania , alipokea pasipo kujiuliza mara mbili mbili.

“Hellolw!”Ilikuwa ni sauti ya kike.

“Nazungumza na nani?”Aliuliza Roma.

“Roma unashindwa vipi kuijua sauti yangu”

“Ndio useme sasa wewe ni nani kama umeona nimeshindwa kuitambua”Aliongea Roma huku upande wa pili ukiwa kimya kwa dakika kadhaa.

“Ni mimi Neema”Roma alivuta pumzi mara baada ya kusikia mtu huyo ni mrembo Waziri.

“Kumbe ni wewe waziri”

“Sio waziri Neema”

“Okey Neema mrembo , kwanini umenipigia?”

“Uko wapi sasa hivi?”Roma alishangazwa na swwali hilo.

“Nipo Job”

“Okey !nimekupigia simu nataka kujua kama usiku wa leo tunaweza kuonana”
 
SEHEMU YA 89

Roma alishindwa kumkatalia Neema , kwanza kitendo tu cha mwanamama huyu kutaka kuonana nae usiku kilimpa mushikeli, yeye alijua kabisa huenda mwanamama huyu alikuwa akimwitia kwa ajili ya mapenzi , lakini hakutaka kulipa swala hilo kipaumbele , alitaka kufika ili kujua ni kipi ambacho Neema anataka mpaka kuonana nae, hakufikiria tena onyo alililopewa na mke wake kuhusu kutomsogelea Neema.

Baada ya kukata simu aliendelea kucheza gemu kama kawaida kwa dakika kadhaa tu na simu yake ilianza kuita tena kiasi cha kuona leo kuna nini mbona anapigiwa sana, ilikuwa ni namba mpya pia na hili lilimpa hamasa ya kujua ni nani aliekuwa akimpigia muda hup baada yaNeema.

“Hellow!”Ilikuwa ni sauti ya mwanamke pia ambayo Roma hakuitambua maramoja

“Naongea na nani?”

“Ni mimi Chaneli ”Ilisikika sauti upande wa pili na kumfanya Roma macho yake yaongezeke ukubwa, alijikuta akikumbuka tukio zima la Chaneli.

“Ndio mrembo Chaneli niambie”Aliongea Roma huku akiachia tabasamu , huku akikumbuka mtu anaeongea alikuwa na jinsia mbili.

“Nimekupigia naomba tuonane kama utakuwa na muda”Aliongea

“Saa ngapi na wapi?”

“Hata sasa hivi itakuwa sawa”Aliongea Chaneli na kumfanya Roma afikirie kwa madakika kadhaa.

“Okey tuonane baada ya nusu saa, niambie uko wapi?”

“Nipo Landmark Hotel”

“Okey nitafika hapo baada ya nusu saa”Aliongea Roma huku akigeuza macho akiwaangalia wafanyakazi wenzake waliokuwa bize na majukumu yao na alinyanyuka pasipo kuaga na kutoka.

Roma hakutumia usafiri wa gari lake , aliona atumie Mwendokasi kwenda kukutana na Chaneli , alitaka ajue ni kipi Chaneli anataka kuongea nae , lakini pia katika akili yake alijiambia kabisa kwa asilimia kubwa huenda anaitiwa kwasababu ya Mapenzi.

Siku hii ya leo abiria wlaiokuwa wakitumia Mwendokasi walikuwa ni wengi sana kiasi cha kumfanya Roma kujutia kutokutumia gari , ila kwasababu alikuwa ashatembea mpaka hapo kituoni , aliingia kwenye gari na safari ikaanza.

Ndani ya dakika kadhaa tu alifika na kuelekea upande wa jengo hili Refu la hoteli , alimpigia simu Chaneli na kumwambia waonenane kwenye eno la Mgahawa.

Kwa jinsi Chaneli alivyokuwa akionekana ilikuwa ni Dhahiri kabisa alikuwa ameamua kuwa mwanamke kabisa na sio mwanaume tena.

“Umpendeza”aliongea Roma kwa kujiamini na kukaa kwenye kiti huku Chaneli akijisikia vizuri.

“Nimetoroka kazini Chaneli ni vyema kama utaenda moja kwa moja”Aliongea Roma mara baada ya muhudumu kumletea chakula , alipanga kula kabisa na hii ni baada ya Chaneli kumwambia aagize chochoe atalipia na Roma aliona hio ni ofa nzuri na hakutaka kuikataa.

“Nakupenda Roma”Aliongea Chaneli na kumfanya Roma atulie kidogo pasipo kula kwa sekunde na kisha akaendelea kula kwa dakika kadhaa huku Chaneli akiwa anamwangalia Roma kwa tabasamu , na kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana utadhania kabisa huyu ni mwanamke , hakuwa na Dosari yoyote ya kuonekana mwanamke.

“Kwanza kabla hatujaendelea nataka kujua vipi na wapi umenifahamu , maana sidhani kama tulishawahi kuonana”Aliongea Roma huku akimwangalia.

“Nishawahi kuokuona kwa mara kadhaa , kama maratatu hivi , mara ya kwanza ilikuwa ni ndani ya hoteli ya JR, mara ya pili ni ndani ya hoteli ya New Afrika na Mara ya nne ni Kwenye kusanyiko”aliongea Chaneli na kumfanya Roma ashangae, kwani licha ya yeye kusema hivyo hakuna siku ambayo alishawahi kumuona.

“Mbona mimi sijawahi kukuona kwenye hayo maeneo yote?”

“Usingeniona kwani nilikuwa nikiigiza kuwa mwanaume”Roma alishangaa.

“Uliwezaje kuigiza kama mwanaume kwa kipindi chote pasipo ya watu kugundua kama una jinsia mbili?”

“Nilizaliwa nikiwa na sauti nzito kama ya mwanaume , licha ya kwamba nguvu ya kuwa mwanamke ilikuwani kubwa sana kwangu kuliko ya kuwa mwanaume”

“Kwahio Sauti yako ya kiume imeenda wapi?”

“Mwezi uliopita nilifanya ‘Voice Feminization Surgery’ na kubadilisha sauti yangu na kuwa ya kike”Roma alishangazwa na hilo.

“Na uliwezaje kuishi bila ya watu kugundua baada ya kufanya upasuaji?’Chaneli alitabasamu.

“Kuna teknolojia inaitwa ‘Laser Vocal Tuning’ ndio ilionipa uwezo wa muda kuigiza kama mwanaume”Roma alitingisha kichwa kuonyesha kwamba ameelewa , hakutaka kuuliza Zaidi kuhusu hayo mambo kwani aliona yatamchukua muda mrefu mpaka kuyaelewa.

Voice Feminization Surgery(Feminization Laryngoplasty) ni upasuaji ambao unafanyika kwa kupunguza ukubwa wa kiboksi cha sauti(Voice Box) na kufupishwa kwa ‘Vocal Cords’ na hii inatokana na kwamba Vocal Cord na Voice Box za mwanaume na mwanamke zinatofautiana katika urefu na ukubwa.,zipo ‘Procedures’Nyingi ambazo hufanyika kwa mtu kubadilisha sauti.

“Kwahio Chaneli umenipendea nini?”

“Nakupendea kwa namna unavyojamini Roma na jinsi usivyokuwa wa kawaida , tokea siku ya kwanza nakuona Mbagala uliiteka akili yangu kwa jinsi ulivyombeba Mrembo Edna”Aiongea na Hapa Roma alishangaa kidogo,na kujiuliza inakuwaje kumbe siku ile kuna watu walikuwa wakimfahamu Edna lakini waliacha yeye kumbeba na kwenda nae geto

“Kwanini hakuniuzuia licha ya kwamba ulikuwa ukijua mwanamke niliembeba hakuwa Kahaba kama nilivyodhania?”Aliuliza Roma na kumfanya Chaneli acheke.

“Sikutaka kuingilia , nilikuwa najua mpango mzima wa Edna kuwa katika hali ile na ndio maana nikakaa kimya , lakini nikashukuru kwa wakati mmoja ulivyotokea na kumbeba, mwanzoni nilijua wewe ni mlinzi wa Edna na umekuja kumuokoa , lakini nilivyokuja kufatilia na kupata ukweli , ‘I was Shocked na nilijikuka nikikupenda Zaidi”

“Niambie mpango mzima ulikuwaje?”Aliuliza Roma pasipo kumzingatia Chaneli ambaye alikuwa akionesha mushikeli wa kuelezea tukio zima lilivyokuwa , huku akjishika kifua chake ambacho kilimshangaza Roma kwani Chaneli alionekana kuwa na manyonyo.

“Mpango ulikuwa ni rahisi tu Roma , mkeo aliwekewa madawa kwenye kinywaji ili Abubakari akafanye nae mapenzi huku wakirekodi tukio kwa ajili ya kumtengenezea Edna udhaifu ambao ungemfanya akubali kila jambo analoambiwa na Abubakari”Aliongea Chaneli na kumfanya Roma apandwe na hasira , kwanza ukweli ni kwamba licha ya tukio lile la kulala na Edna liishe hakuwahi kuwaza kabisa juu ya kile kilichokuwa kimetokea mpaka Edna akawa vile , ili hali alikuwa ni Bikra , lakini siku hii ya leo ndio anapata kujua ukweli kutoka kwa Chaneli, alijiambia Abu siku akiingia kwenye kumi na nane zake hawezi kumuacha hai, lakini pia Roma alijiuliza kwanini Edna hakufanya chochote juu ya hili , inamaana hakuwa na taarifa kama siku ile yote yaliomtokea yalikuwani ya kupangwa.

“Chaneli nadhani mpaka sasa ushajua nimeoa na niseme tu naziheshimu hisia zako kwangu , lakini siwezi kukubali”aliongea Roma na Chaneli hakukasirika , Alitabasamu .

“Usijali Roma nilichokuwa nataka ni kukueleza kama nakupenda kwa dhati kabisa na kupitia wewe angalu nitaweza kuishi kwa furaha na Amani , lakini pia nimefarijika sana wewe kuja kuniona kabla sijaondoka, licha ya kwamba nilikupigia sikuwa na uhakika kama utaweza kuja nilibahatisha tu”Aliongea chaneli huku akiweka uso wa huzuni.

“Unaelekea wapi Chaneli?”

“Kwasasa nitaenda kuishi Korea Kusini kwa muda ,pia nikifanya ‘Plastick surgery’ kubadilisha muonekano wangu kabisa , sina cha kufanya hapa Tanzania kwa sasa?”

“Vipi kuhusu baba yako?”

“Baba kapatwa na kiharusi na sasa yupo hospitalini , mke wake anamwangalia”

“Unasemaje mke wake , wewe sio mama yako?”

“Mama yangu ashafariki muda tu nikiwa na miaka kumi na moja”

Roma alielewa na wakaagana Na chaneli , Roma alishukuru kwa Chaneli kumuelewa juu ya kutozikubali hisia zake , aliogopa Chaneli kuwa king`anganizi.

Roma alipanga kurudi kazini kupoteza muda na kisha kwenda nyumbam.

“Wewe vipi unanichafua na mafuta yako mimi , hebu toa ndoo yako karibu yangu”Ilikuwa ni sauti ya mwanamke kukereka ,Roma aliangalia ni nini kimemsibu huyu mwanamke ambaye kwa kumwangalia tu alionekana wale wanawake ambao wamejichubua ngozi kwa kutumia kemikali .

Roma alimuona mwanadada mdogo hivi wa rangi mchanganyiko ,ambao Roma hakuelewa ni mchanganyiko wa mzungu au mwarabu , kwani licha ya msichana huyu kuwa mrembo , lakini alionesha kuwa wa tofauti kidogo na raia wengi ambao amezoa kuwaona , wenye mchanganyiko wa Rangi.

Roma sasa aligundua kwanini yule mwanamke alikuwa akilalama na hii ni kutokana na kwmba Mwendokasi ulikuwa umejaa , halafu huyu msichana alikuwa amebeba ndoo ambayo kwa harakaharaka aligundua ilikuwa na mafuta na kutokana na watu kubanana yule mwanamke nguo yake ikachafuka

“Nisamehe Mama”Aliongea kwa upole yule msichana.

“Nikusamehe nini ushanichafua , hebu toa ndoo yako bwana”Aliongea mwanamke alionekana kuwa na kisirani kisichokuwa cha kawaida,Roma alimuonea huruma mdada na kumwambia asogee karibu yake aweke ndoo.

“Unaweza kuchafuka na wewe”

“Siwezi kuchafuka wewe weka tu”Aliongea Roma kwa kutabasamu , huku msichana huyu wa lika la miaka kumi na nane akika nyuma yake, nusu saa mbele yule msichana alisogeza ndoo yake , alionekana alitaka kushuka.

“Unataka kushuka?”Aliuliza Roma.

“Ndio nashukia Azikiwe”Roma Alitabasamu na kutingisha kichwa na gari ilisimama kwenye kituo cha Azikiwe na Roma pia na yeye alishuka.

“Anko kumbe na wewe ulikuwa ukishukia hapa?”Aliuliza yule mwanadada shombe na kumfanya Roma atabasamu.

“Ndio , au unadhani nakufuata?”

“Hapana nimeuliza tu”

“Okey !unaonaje sasa ukinipatia waleti yangu niondoke”Aliongea Roma na kumfanya huyu mwanadada kutoa macho , hakujua mtu aliekuwa mbele yake alijuaje kama amemwimbia.

“Anko kumbe muda wote ulikuwa ukijua nimekuibia na umekausha , basi shika wallet yako na naona unisamehe”Aliongea yule msichana kwa aibu na kumfanya Roma atabasamu.

Ukweli ni kwamba Roma wakati akiwa amesimama kwenye Mwendokasi , alipata hisia za waleti yake kuchomolewa , aliokuwa ameiweka mfuko wa nyuma na alihakikisha mtu ambaye kaichomoa na kisha kutulia , hakutaka kuleta mtafaruku palepale kwani aliona huenda Msichana angaletewwa shida na ndio maana alitulia kuona ni wapi anashukia ili achukue waleti yake kistaarabu.

Roma baada ya kukabidhiwa waleti yake hakutaka kuongea Zaidi , alianza kupiga hatua kuondoka eneo hili , huku akimuacha yule mwanadada akimwangalia kwa nyuma.

“Wife natoka kidogo , sitokula leo”Aliongea Roma aliekuwa amevaa Jeans na tisheti , na hii ilikuwa ni muda wa saa moja kama na nusu hivi za usiku na Edna alikuwa akiangalia runinga sebuleni , alionekana kuwa na mudi nzuri leo kwani ni mara chache sana Edna kukaa sebuleni.

“Unaenda kuonana na Neema?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma ashangae ,inakuwaje Edna akajua mtu anaenda kuonana nae alikuwa ni Neema Luwazo.

“Ndio kaniomba tuonane , ila umejuaje bebi , usiniambie siku hizi umeniwekea watu wanaonifatilia”

“Sina muda wa kukufuatilia mimi na maisha yako , ni kwamba alioniomba namba yako asubuhi alivyokuja ofisini kwangu”Aliongea Edna na kumfanya hapa Roma aelewe kumbe Neema alikuja ofisini kwa Edna.

“Okey Wife nimekuelewa usiku mwema”Aliongea Roma huku akianza kupiga hatua kuelelekea mlango wa kutokea.

“Kwahio Roma maneno yangu niliokuambia ukae mbali na yule mwanamke haiutaji kuyazingatia?”Aliuliza Edna ambaye alionekana kuketrka muda huu.

“Wife kaniomba tukutane na sio kama kuna kitu kinaendelea kati yetu , hivyo napaswa kutii wito”

“Unaweza kwenda”Aliongea Edna huku akirudisha macho yake kwenye runinga na Roma hakujali sana.
 
SEHEMU YA 90

Roma alikuwa tayari ashawasiliana na Neema luwazo sehemu ya makutano yao, licha ya kwamba Roma alishangazwa na umbali wa eneo ambalo Neema alikuwa amechagua , eneo la Mbezi Beach ila aliona haina tabu

Roma hakujali sana, alichukulia kama fursa ya kuendesha gari umbali mrefu, kwanza sio kama alikuwa na shida ya mafuta , hakuwa nayo ,kwani pesa ya mafuta ilikuwa ni ya mke wake Edna.

Dakika kama arobaini hivi alikuja kukutana na Neema Luwazo karibu na kanisa la KKKT Mbezi beach ,Neema usiku huu alikuwa pia yupo kwenye gari yake kubwa aina ya Range Rover Spot , alishusha kioo.

“Nifuatishe nyuma kuna sehemu nataka twende”Alionea Neema na Roma alitingisha kichwa huku Neema akipandisha kioo cha gari yake na kuanza kulitoa taratibu kulekea upande wa Tegeta ,dakika chache mbele baada ya kutoka barabara kuu hatimae waliweza kuingia sehemu ambayo Roma hakuwa akiifahamu , yeye alichofanya nikufatisha tu gari ya Neema , walikuja kuegesha gari zao na kisha wakatoka.

Neema usiku huu alikuwa amependeza kweli , alikuwa amevalia gauni na kijikoti cha suti rangi ya Bluu na raba nyeupe.

“Umependeza”Aliongea Roma huku akimwangalia Neema , mbaye kwa usiku huu hakuonekana yule mwanamke ambaye alikuwa akiwahenyesha wenzake bungeni kwa maswali yake wakati wa kuachangia hoja.

Neema alitabasamu huku akimwangalia Roma , alionekana alikuwa akimwangalia kwa maswali mengi .

“Unapajua hapa au ushawahi kufika?”Aliuliza Neema

“Sijawahi kufika hapa , kwanza ningeweeza vipi kufika wakati nilianza kutembea na matajiri juzi tu baada ya kumuoa Edna mwanamke tajiri”aliongea Roma, huku wakisogea sehemu ambayo kulikuwa na viti , hii sehemu ilikuwa nzuri sana , ilikuwa ni Fukwe yenye upepo wa hali ya juu , lakini pia iliojengwa vizuri sana kwa watu kupumzika na hata pia kulala , palikuwa na hoteli kubwa tu sehemu hii.

“Hapa ni Upepo Beach Garden , nimewekeza hapa, hio hoteli ni ya kwangu”aliongea Neema na kumfanya Roma aangalie lijihoteli la nyota tano lililokuwa mbele yake.

“Kuna muda najiulizaga kwanini kila mwanamke ambaye nimetokea kujuana nae ana hela kuliko mimi”Aliongea Roma.

“Na hilo pia unajali Roma?”

“Wewe unaonaje?”Aliuliza Roma mara baada ya wao kuketi ndani ya eneo hili ambalo usiku huu palionekana kutokuwa na watu wengi , licha ya kwamba baadhi ya watu wapo, tena wakiwa na wapenzi.

“Unaonekana kama usiekuwa ni mwenye kujali watu wenyepesa na hili naweza kusema limenifanya nikuone wa tofauti na vijana wengi”aliongea Neema huku akitabasamu na muda huohuo alisogea mzee mmoja.

“Neema naona leo umekuja hapa na mgeni kwa mara ya kwanza?”Alikuwa ni mzee hivi mwenye Mvi japo sio nyingi , alikuwa amevalia mavazi ya uhudumu ndani ya hili eneo na kumfanya Roma ashangae inakuwaje mzee kama huyu akafanya kazi kama hio.

“Ndio Mzee Chino , huyu ni Roma ni rafiki yangu”Aliongea Neema akimtambulisha Roma na mzee akatabasamu.

“Roma huyu ni Mzee Chino ni mmiliki wa hili eneo lakini pia anaweza kua kama baba yangu baada ya mama na baba kufariki”Aliongea Neema na kumfanya Roma ashangazwe na mambo mawili, kwanza juu ya Mzee huyu kumiliki eneo hili la fukwe na wakati huhuo akifanya kazi za uhudumu hakuonesha kabisa kama mmiliki , lakini pia Juu ya Wazazi wa Neema kufariki.

“Kijana unabahati sana , unaonekana kuwa ‘Special’ kwa Neema hajawahi kuja na mwanaume hapa ni mara ya kwanza, Zaidi ya kuja na mtoto wake pekee”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Neema aone aibu kidogo na Roma alitabasamu.

“Sasa Mzee unaonekana unapesa lakini imenishangaza unaonekana kuwa muhudumu au ndio swaga za kuwavutia warembo”alitania Roma na kumfanya Neema kucheka.

“Kijana una maneno sana , ninachokifanya ni kitu ninachokipenda , licha ya Eneo hili Neema kujenga hoteli yake , lakini huu mgahawa ni wa kwangu na ninapenda kufanyakazi ya kuhudumia watu kwani inanikutanisha na watu tofauti tofauti , lakini pia ndio kazi ninayopenda , nimeanza kufanya kazi hii wakati nikiwa namfukuzia mama yake Neema”Aliongea Mzee Chino Bila aibu na kumfanya Roma ashangae.

“Kwahio ilikuwaje sasa Mzee Chino , ulimpata Mama yake Neema?”

“Nimpate wapi alinipa sharti la kuacha kazi yangu ya uhudumu niwe nae , nikakataa , akaniacha akaenda kwa mwanaume mwingine mwenye pesa Zaidi yangu”aliongea Mzee chino

“Mzee Chino tuletee supu yako ile unayotengezaga na chapatti pembeni”Aliongea Neema kukatisha maongezi na Mzee chino alitii na kwenda kuleta , ila kwa Roma alishangazwa inakuwaje Waziri akaagiza Chapati na supu usiku wote huu.

“Unashangaa ! kila ninapokuja hapa mara nyingi napenda kunywa supu ya Samaki”Aliongea Neema na Roma alimwelewa ,ukweli ni kwamba hata yeye alikuwa amemisi sana aina hio ya chakula.

‘Seafood’ ni vyakula ambavyo Roma alikuwa na muda mrefu tokea afike Tanzania hajavigusa kabisa , na aliona sio mbaya kwa usiku huo kupata aina hio ya chakula , Roma aliona kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana walikuwa kwenye ‘Date’.

“Nilijua Mkeo atakukataza kuja kuonana na mimi?”.

“Na amenikataza , ila sikutaka kumtii kwasababu nilishaweka ahadi ya kuonana na wewe”.

“Nijikuwa sina jinsi Zaidi ya kumuomba namba yako Roma , sikutaka kujificha mbele yake , kama angenikatalia namba yako nisingelazimisha hata tuonane , lakini alivyonipatia nikaona hakuwa na shida ya mimi na wewe kuonana”Aliongea Neema kwa sauti ya kawaida na wakati huohuo Chino alileta kile Neema alichoagiza mabakuli mawili , Roma baada ya kuona mifupa ya samaki na nyama nyama alipandwa na hamu ya kushughulikia msosi huo.

“Neema inabidi unitambulishe vizuri , siamini kama kuna urafiki unaoendelea hapa”Aliongea Mzee Chino huku akindoka akiwa na tabasamu na Neema aliishia kutabasamu.

“Unajua kwanini nimechagua hii sehemu?”Aliuliza Neema.

“Mimi najuaje wewe ndio umenileta hapa”

“Nilivyokuwa mdogo Mama alikuwa akipendelea kunileta sana hapa, ni kama kumbukumbu pekee ambayo ameniachia , kila ninapokuwa sina Amani nakuja hapa, nakaa natulia then kesho nitaondoka nikiwa mpya, na nilijiambia siku nikipata mwanaume ambaye nitatokea kumpenda kwa dhati nitamleta hii sehemu”Aliongea Neema kwa hisia na wakaangaliana na Roma.

“Lakini mwanaume ambaye nilikuwa nikimuota amechelewa sana kuja kwenye maisha yangu mpaka nikiwa na umri huu”

“Neema mbona unaonekana kama ndio unanifungukia sasa”Aliongea Roma na Neema akatabasamu baada ya kuona namna Roma anavyonyoosha maneno.

“Unajua Roma unaonekana muhuni sana wakucheza na wanawake na bado nikashangaa kwanini mwanamke kama Dorisi akakupenda na pia Edna kuwa mke wako na mimi mwenyewe pia kukupenda kiasi hiki”

“Sasa kwanini unaonekana ni mwenye kunipenda , mimi mwenywe najua sijatulia na udhaifu wangu mkubwa ni wanawake , kwanini licha ya kulijua hilo unaonekana kunipenda?”

“Kwasababu sisi wanawake ni tofauti na nyie wanaume , nyie ili mumpende mwanamke mnaangalia vitu vingi ,kama vile uzuri . upole na vigezo kibao , ila kwetu sisi hatuna sababu ya kumpenda mwanaume, ukimkuta mwanamke kapenda kweli na ukamuuliza kwanini kapenda atashindwa kukupa jibu , ila kwa mwanaume ni rahisi kukupa jibu kwanini kampenda mwanamke wake”Aliongea na Roma licha ya kwamba alikuwa akisikiliza lakini alikuwa bize na chakula chake , alikunwa akitafuna yaani, hakuwa ni mwenye kuchanganywa na mwanamke kama waziri kumfungukia yeye kwake aliona ni kawaida,ingekuwa ni vijana wengine wakakutana na hali kama hio huenda wangekuwa wapo tofauti sana na Roma.

“Kwahio huna sababu nyingine ambayo inakufanya kunipenda , yaani huwezi eleza kwanini unanipenda?”

“Licha ya kwamba unaonekana mwanaume ambaye huwezi kutulizwa na mwanamke mmoja ,ila ninashauku ya kukujua Roma , najua kabisa haupo wa kawaida , kila siku ambayo tumekutana mimi na wewe lazima unishangaze ,ni mwanaume ambaye hautabiriki na hii imenipa shauku Zaidi ya kuwa na ukaribu na wewe ili kukujua”

Aliongea Neema na Roma akamwangalia mrembo huyu ambaye kwake ki umri walikuwa wamepishana sana , licha ya kwamba Neema kuonekana mdogo lakini umri ulikuwa umeenda na hakuna mtu wa kukataa hilo ni vile tu kwamba alikuwa ni mwanamke wa kujitunza na pesa pia ilikuwa imemfanya kuonekana mdogo.

Roma alimalizia supiu yake lakini kwa Neema alionekana hata hamu ya kuendelea kula hakuwa nayo.

“Lakini Neema unajua kabisa mimi nina mke ,na nisiwe muongo hapa hata kama nikikubalia ujue sitoweza kucheza kwenye matarajio yako kama mwanamke ambaye ana mwanaume anaempenda”Aliongea Roma na Neema alitabasamu na kisha akanyanyuka.

“Unaonaje tukitembea tembeatembea mpaka kule”Aliongea na Roma hakubisha, alinawa mikono na kisha akanyanyuka .

“Nishazeeka tayari kwasasa Roma ,ki ufupi mimi sipo kama wasichana wa miiaka ishirini ambao watatamani vitu vikubwa kwa mwanaume , kwasasa nina kila kitu pesa na pia nina mtoto ,ninajua una mke na hilo nitaenda kuliheshimu na pia na mheshimu Edna , lakini ukweli ni kwamba licha ya kwamba unaonekana kuwa kijana mdogo , lakini nimetokea kukupenda sitaki unifanyie kikubwa , ila nitapenda kama utakuwa na mimi wakati nitakapokuhitaji”Aliongea Neema kwa hisia huku akisimama mbele ya Roma akiangalia upande wa baharini.

Na Roma hakujua cha kujibu kwa wakati huu , siku zote alikuwa ni mwenye kuanza wanawake lakini leo hii , yeye ndio kaanzwa na pia mwanamke aliembele yake alikuwa tayari ashaonja utamu wake.

Roma alimsogelea Neema kwa nyuma na kumkumbatia na kumfanya mwanamama huyu atabasamu na ajisikie vizuri sana , upande wa Roma hakutaka kuuliza sana juu ya Edna kumtahadharisha kuachana na Neema ,kwanza hakuwa akiogopa kiumbe chochote kwenye hii dunia kwanini aogope kuwa na mwanamke aliekuwa mbele yake ambaye anataka kuweka kumbukumbu kabla ya kuingia kwenye uzee wake.

Kadri sekunde na dakika zilizvyokuuwa zikisogea miili yao ilipata Joto la mapenzi na Neema ndio wa kwanza kugeuka na kugusisha midomo na Roma na kuanza kunyonyana kimahaba , huku Roma na yeye ekipitisha mikono kwenye mwinuko wa Mrembo Neema Luwazo.

“Cling .. Cling …Cling”

Ni simu ya Neema ndio iliowakatishia utamu na Neema hakutaka kupuuzia simu iliokuwa inaita alijitoa kwa Roma na kisha akaangalia ninani anapiga na jina lilisomeka ‘My daughter’.

Roma hakujua Neema alikuwa akiongea nini na simu kwani Neema alisogea mbali kidogo ,baada ya dakika kama moja za Neema kuongea na Simu , alimsogelea Roma.

“Naona jambo letu leo litaishia hapa nina dharula tutapanga siku nyingine ya kuonana”Aliongea Neema na kumfanya Roma atoe macho , yaani hakuamini hii pisi leo inamuacha hivihivi pasipo kumpa kidogo ukizingatia joto lake limepanda kwa kiwango kikubwa.

“Unaniachaje hivi sasa Neema?”Aliuliza Roma .

“Ni jambo muhimu sana , ni juu ya mtoto wangu naomba niondoke nitakutafuta siku nyingine”Aliongea Neema na alionekana hakuwa tayari kusubiri jibu kutoka kwa Roma alianza kupiga hatua kuondoka.

Wakati Roma akijiuliza cha kufanya kwa wakati huo , kwani hali yake haikuwa sawa kabisa na alihitaji kampani ya mwanamke kwa usiku huo , mara simu yake ilianza kuita , aliitoa na kuangalia jina na aliona aliekuwa akipiga ni Nasra , Roma alijikuta akimkumbuka huyu mrembo maana tokea arudi Japani hawajaonana.

“Bebi Nasra naona umenikumbuka leo,halafu unaonekana kuwa sehemu yenye makelele upo nyumbani kweli?”

“Sipo nyumbani nifuate , nipo Kidimbwi”aliongea Nasra upande wa pili na kumfanya Roma ashangae , kwanza hakuwa akipajua Kidimbwi ni wapi.

“Kidimbwi ndio wapi Nasra?”

“Ni ufukweni Kidimbwini nifuate”Aliongea Nasra na kukata simu , alionekana alikuwa amelewa , Roma hakutaka kubaki hapo , alitembea kuitafuta gari yake.

Baada ya dakika chache tu alikuwa ashaifikia na kutafuta Kidimbwi ilipo maana Gari lake lilikuwa na uwezo wa kuonyesha ramani , na alitabasamu baada ya kuona hakuwa mbali na sehemu yenyewe ni kilomita kama moja tu hivi kutoka alipo.

Nasra alionekana kujiinamia chini kwenye Meza , haikueleweka alikuwa na nani hapo ndani kwani muda huu ,alikuwa peke yake na jambo hili lilimshangaza Roma.

“Mbona upo peke yako na unafamya nini hapa ?”Aliongea Roma.

“Nilikuja na marafiki zangu niliomaliza nao chuo ndio wameondoka na kuniacha na siwezi kuendesha gari nikiwa mlevi hivi”aliongea Nasra huku akijinyanyua kilevi na Roma alimshikilia.

Roma hakuona haja ya kumrudisha Nasra Mikocheni , kwani asingeweza kuacha gari yake hapo , alichoona ni kuchukua chumba ili waweze kuondoka asubuhi.

*****

Ilikuwa ni muda wa asubuhi , Roma aliamshwa na simu akiwa ndani ya hoteli na Nasra ambaye alikuwa amejilaza vibaya kweli , na hii ni baada ya wao wawili kumaliza kufanya mapenzi usiku kucha na staili yao ambayo Roma alimwambia Nasra inaitwa ‘Facing The Ocean’.

“Diego kuna nini ?”Aliuliza Roma baada ya kuona jina la mpigaji ni Diego na alijua lazima kutakuwa na tatizo.

“Your Majesty ! nadhani usiku wa leo haujalala nyumbani”

“Ndio”

“Chiara na John walifika nyumbani kwako kwa ajili ya jukumu lao la kazi , lakini hali walioikuta haikuwa shwari , geti walikuta lipo wazi na pia vijana wanaotoa ulinzi hawana fahamu ”Aliongea Diego na hapa Roma aliona kweli kuna tatizo.

Alikurupuka harakaharaka na kisha akavaa nguo zake .

“Diego hebu jaribuni kufatilia nin kimetokea ninafika nyumbani mara moja kuona tatizo ni nini”Aliongea Roma haraka haraka na kisha akakata simu , na akamuamsha na Nasra na kumwambia kuna dharula na ataondoka wa kwanza na hata hakusubiria jibu , alifungua mlango na kutoweka ndani ya eneo hilo.

Ndani ya kama nusu saa tu hivi ,Roma alikuwa akiingia Kigamboni nyumbani kwake , na ni kweli ile anafika geti lilikuwa wazi na hata mlango wa mbele wa nyumba yao ulikuwa wazi pia , alikimbilia ndani mpaka sebuleni huku akiita jina la Edna na hakukuwa na majibu , lakini ile amesimama ,alivyoangalia kwenye meza ya kioo aliona kikaratasi cha rangi ya njano kilichokuwa kimebandikwa kwenye Meza ba gundi.

“Your Majest Pluto ,Jumba unalokaa ni kubwa sana na tumeshangazwa , Tupo na mkeo pamoja na Mama wa nyumbani , ukiwataka wakiwa hai tuletee jiwe la Kimungu(Godstone),Sehemu ni Mabwepande , uje peke yako…Cc Froma Yamata Sect”Kilikuwa ni kikratasi ambacho kimeandikwa kwa lugha ya kijapani.

END OF SEASON 3 HAVE NICE WEEKEND
ITAENDELEA SIKU YOYOTE

ACHA KUTESEKA NA AROSTO CHANGIA 2000 KUENDELEA HALAFU NICHEKI WATSAPP 0687151346 UUNGANISHWE NA GURPU , AU KAMA HUPENDI GRUPU NITAKUTUMIA INBOX, KILA SIKU VIPANDE VITAT , KWA SASA TUPO SEASON 5 KIPANDE CHA 130



NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
 
SEHEMU YA 90

Roma alikuwa tayari ashawasiliana na Neema luwazo sehemu ya makutano yao, licha ya kwamba Roma alishangazwa na umbali wa eneo ambalo Neema alikuwa amechagua , eneo la Mbezi Beach ila aliona haina tabu

Roma hakujali sana, alichukulia kama fursa ya kuendesha gari umbali mrefu, kwanza sio kama alikuwa na shida ya mafuta , hakuwa nayo ,kwani pesa ya mafuta ilikuwa ni ya mke wake Edna.

Dakika kama arobaini hivi alikuja kukutana na Neema Luwazo karibu na kanisa la KKKT Mbezi beach ,Neema usiku huu alikuwa pia yupo kwenye gari yake kubwa aina ya Range Rover Spot , alishusha kioo.

“Nifuatishe nyuma kuna sehemu nataka twende”Alionea Neema na Roma alitingisha kichwa huku Neema akipandisha kioo cha gari yake na kuanza kulitoa taratibu kulekea upande wa Tegeta ,dakika chache mbele baada ya kutoka barabara kuu hatimae waliweza kuingia sehemu ambayo Roma hakuwa akiifahamu , yeye alichofanya nikufatisha tu gari ya Neema , walikuja kuegesha gari zao na kisha wakatoka.

Neema usiku huu alikuwa amependeza kweli , alikuwa amevalia gauni na kijikoti cha suti rangi ya Bluu na raba nyeupe.

“Umependeza”Aliongea Roma huku akimwangalia Neema , mbaye kwa usiku huu hakuonekana yule mwanamke ambaye alikuwa akiwahenyesha wenzake bungeni kwa maswali yake wakati wa kuachangia hoja.

Neema alitabasamu huku akimwangalia Roma , alionekana alikuwa akimwangalia kwa maswali mengi .

“Unapajua hapa au ushawahi kufika?”Aliuliza Neema

“Sijawahi kufika hapa , kwanza ningeweeza vipi kufika wakati nilianza kutembea na matajiri juzi tu baada ya kumuoa Edna mwanamke tajiri”aliongea Roma, huku wakisogea sehemu ambayo kulikuwa na viti , hii sehemu ilikuwa nzuri sana , ilikuwa ni Fukwe yenye upepo wa hali ya juu , lakini pia iliojengwa vizuri sana kwa watu kupumzika na hata pia kulala , palikuwa na hoteli kubwa tu sehemu hii.

“Hapa ni Upepo Beach Garden , nimewekeza hapa, hio hoteli ni ya kwangu”aliongea Neema na kumfanya Roma aangalie lijihoteli la nyota tano lililokuwa mbele yake.

“Kuna muda najiulizaga kwanini kila mwanamke ambaye nimetokea kujuana nae ana hela kuliko mimi”Aliongea Roma.

“Na hilo pia unajali Roma?”

“Wewe unaonaje?”Aliuliza Roma mara baada ya wao kuketi ndani ya eneo hili ambalo usiku huu palionekana kutokuwa na watu wengi , licha ya kwamba baadhi ya watu wapo, tena wakiwa na wapenzi.

“Unaonekana kama usiekuwa ni mwenye kujali watu wenyepesa na hili naweza kusema limenifanya nikuone wa tofauti na vijana wengi”aliongea Neema huku akitabasamu na muda huohuo alisogea mzee mmoja.

“Neema naona leo umekuja hapa na mgeni kwa mara ya kwanza?”Alikuwa ni mzee hivi mwenye Mvi japo sio nyingi , alikuwa amevalia mavazi ya uhudumu ndani ya hili eneo na kumfanya Roma ashangae inakuwaje mzee kama huyu akafanya kazi kama hio.

“Ndio Mzee Chino , huyu ni Roma ni rafiki yangu”Aliongea Neema akimtambulisha Roma na mzee akatabasamu.

“Roma huyu ni Mzee Chino ni mmiliki wa hili eneo lakini pia anaweza kua kama baba yangu baada ya mama na baba kufariki”Aliongea Neema na kumfanya Roma ashangazwe na mambo mawili, kwanza juu ya Mzee huyu kumiliki eneo hili la fukwe na wakati huhuo akifanya kazi za uhudumu hakuonesha kabisa kama mmiliki , lakini pia Juu ya Wazazi wa Neema kufariki.

“Kijana unabahati sana , unaonekana kuwa ‘Special’ kwa Neema hajawahi kuja na mwanaume hapa ni mara ya kwanza, Zaidi ya kuja na mtoto wake pekee”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Neema aone aibu kidogo na Roma alitabasamu.

“Sasa Mzee unaonekana unapesa lakini imenishangaza unaonekana kuwa muhudumu au ndio swaga za kuwavutia warembo”alitania Roma na kumfanya Neema kucheka.

“Kijana una maneno sana , ninachokifanya ni kitu ninachokipenda , licha ya Eneo hili Neema kujenga hoteli yake , lakini huu mgahawa ni wa kwangu na ninapenda kufanyakazi ya kuhudumia watu kwani inanikutanisha na watu tofauti tofauti , lakini pia ndio kazi ninayopenda , nimeanza kufanya kazi hii wakati nikiwa namfukuzia mama yake Neema”Aliongea Mzee Chino Bila aibu na kumfanya Roma ashangae.

“Kwahio ilikuwaje sasa Mzee Chino , ulimpata Mama yake Neema?”

“Nimpate wapi alinipa sharti la kuacha kazi yangu ya uhudumu niwe nae , nikakataa , akaniacha akaenda kwa mwanaume mwingine mwenye pesa Zaidi yangu”aliongea Mzee chino

“Mzee Chino tuletee supu yako ile unayotengezaga na chapatti pembeni”Aliongea Neema kukatisha maongezi na Mzee chino alitii na kwenda kuleta , ila kwa Roma alishangazwa inakuwaje Waziri akaagiza Chapati na supu usiku wote huu.

“Unashangaa ! kila ninapokuja hapa mara nyingi napenda kunywa supu ya Samaki”Aliongea Neema na Roma alimwelewa ,ukweli ni kwamba hata yeye alikuwa amemisi sana aina hio ya chakula.

‘Seafood’ ni vyakula ambavyo Roma alikuwa na muda mrefu tokea afike Tanzania hajavigusa kabisa , na aliona sio mbaya kwa usiku huo kupata aina hio ya chakula , Roma aliona kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana walikuwa kwenye ‘Date’.

“Nilijua Mkeo atakukataza kuja kuonana na mimi?”.

“Na amenikataza , ila sikutaka kumtii kwasababu nilishaweka ahadi ya kuonana na wewe”.

“Nijikuwa sina jinsi Zaidi ya kumuomba namba yako Roma , sikutaka kujificha mbele yake , kama angenikatalia namba yako nisingelazimisha hata tuonane , lakini alivyonipatia nikaona hakuwa na shida ya mimi na wewe kuonana”Aliongea Neema kwa sauti ya kawaida na wakati huohuo Chino alileta kile Neema alichoagiza mabakuli mawili , Roma baada ya kuona mifupa ya samaki na nyama nyama alipandwa na hamu ya kushughulikia msosi huo.

“Neema inabidi unitambulishe vizuri , siamini kama kuna urafiki unaoendelea hapa”Aliongea Mzee Chino huku akindoka akiwa na tabasamu na Neema aliishia kutabasamu.

“Unajua kwanini nimechagua hii sehemu?”Aliuliza Neema.

“Mimi najuaje wewe ndio umenileta hapa”

“Nilivyokuwa mdogo Mama alikuwa akipendelea kunileta sana hapa, ni kama kumbukumbu pekee ambayo ameniachia , kila ninapokuwa sina Amani nakuja hapa, nakaa natulia then kesho nitaondoka nikiwa mpya, na nilijiambia siku nikipata mwanaume ambaye nitatokea kumpenda kwa dhati nitamleta hii sehemu”Aliongea Neema kwa hisia na wakaangaliana na Roma.

“Lakini mwanaume ambaye nilikuwa nikimuota amechelewa sana kuja kwenye maisha yangu mpaka nikiwa na umri huu”

“Neema mbona unaonekana kama ndio unanifungukia sasa”Aliongea Roma na Neema akatabasamu baada ya kuona namna Roma anavyonyoosha maneno.

“Unajua Roma unaonekana muhuni sana wakucheza na wanawake na bado nikashangaa kwanini mwanamke kama Dorisi akakupenda na pia Edna kuwa mke wako na mimi mwenyewe pia kukupenda kiasi hiki”

“Sasa kwanini unaonekana ni mwenye kunipenda , mimi mwenywe najua sijatulia na udhaifu wangu mkubwa ni wanawake , kwanini licha ya kulijua hilo unaonekana kunipenda?”

“Kwasababu sisi wanawake ni tofauti na nyie wanaume , nyie ili mumpende mwanamke mnaangalia vitu vingi ,kama vile uzuri . upole na vigezo kibao , ila kwetu sisi hatuna sababu ya kumpenda mwanaume, ukimkuta mwanamke kapenda kweli na ukamuuliza kwanini kapenda atashindwa kukupa jibu , ila kwa mwanaume ni rahisi kukupa jibu kwanini kampenda mwanamke wake”Aliongea na Roma licha ya kwamba alikuwa akisikiliza lakini alikuwa bize na chakula chake , alikunwa akitafuna yaani, hakuwa ni mwenye kuchanganywa na mwanamke kama waziri kumfungukia yeye kwake aliona ni kawaida,ingekuwa ni vijana wengine wakakutana na hali kama hio huenda wangekuwa wapo tofauti sana na Roma.

“Kwahio huna sababu nyingine ambayo inakufanya kunipenda , yaani huwezi eleza kwanini unanipenda?”

“Licha ya kwamba unaonekana mwanaume ambaye huwezi kutulizwa na mwanamke mmoja ,ila ninashauku ya kukujua Roma , najua kabisa haupo wa kawaida , kila siku ambayo tumekutana mimi na wewe lazima unishangaze ,ni mwanaume ambaye hautabiriki na hii imenipa shauku Zaidi ya kuwa na ukaribu na wewe ili kukujua”

Aliongea Neema na Roma akamwangalia mrembo huyu ambaye kwake ki umri walikuwa wamepishana sana , licha ya kwamba Neema kuonekana mdogo lakini umri ulikuwa umeenda na hakuna mtu wa kukataa hilo ni vile tu kwamba alikuwa ni mwanamke wa kujitunza na pesa pia ilikuwa imemfanya kuonekana mdogo.

Roma alimalizia supiu yake lakini kwa Neema alionekana hata hamu ya kuendelea kula hakuwa nayo.

“Lakini Neema unajua kabisa mimi nina mke ,na nisiwe muongo hapa hata kama nikikubalia ujue sitoweza kucheza kwenye matarajio yako kama mwanamke ambaye ana mwanaume anaempenda”Aliongea Roma na Neema alitabasamu na kisha akanyanyuka.

“Unaonaje tukitembea tembeatembea mpaka kule”Aliongea na Roma hakubisha, alinawa mikono na kisha akanyanyuka .

“Nishazeeka tayari kwasasa Roma ,ki ufupi mimi sipo kama wasichana wa miiaka ishirini ambao watatamani vitu vikubwa kwa mwanaume , kwasasa nina kila kitu pesa na pia nina mtoto ,ninajua una mke na hilo nitaenda kuliheshimu na pia na mheshimu Edna , lakini ukweli ni kwamba licha ya kwamba unaonekana kuwa kijana mdogo , lakini nimetokea kukupenda sitaki unifanyie kikubwa , ila nitapenda kama utakuwa na mimi wakati nitakapokuhitaji”Aliongea Neema kwa hisia huku akisimama mbele ya Roma akiangalia upande wa baharini.

Na Roma hakujua cha kujibu kwa wakati huu , siku zote alikuwa ni mwenye kuanza wanawake lakini leo hii , yeye ndio kaanzwa na pia mwanamke aliembele yake alikuwa tayari ashaonja utamu wake.

Roma alimsogelea Neema kwa nyuma na kumkumbatia na kumfanya mwanamama huyu atabasamu na ajisikie vizuri sana , upande wa Roma hakutaka kuuliza sana juu ya Edna kumtahadharisha kuachana na Neema ,kwanza hakuwa akiogopa kiumbe chochote kwenye hii dunia kwanini aogope kuwa na mwanamke aliekuwa mbele yake ambaye anataka kuweka kumbukumbu kabla ya kuingia kwenye uzee wake.

Kadri sekunde na dakika zilizvyokuuwa zikisogea miili yao ilipata Joto la mapenzi na Neema ndio wa kwanza kugeuka na kugusisha midomo na Roma na kuanza kunyonyana kimahaba , huku Roma na yeye ekipitisha mikono kwenye mwinuko wa Mrembo Neema Luwazo.

“Cling .. Cling …Cling”

Ni simu ya Neema ndio iliowakatishia utamu na Neema hakutaka kupuuzia simu iliokuwa inaita alijitoa kwa Roma na kisha akaangalia ninani anapiga na jina lilisomeka ‘My daughter’.

Roma hakujua Neema alikuwa akiongea nini na simu kwani Neema alisogea mbali kidogo ,baada ya dakika kama moja za Neema kuongea na Simu , alimsogelea Roma.

“Naona jambo letu leo litaishia hapa nina dharula tutapanga siku nyingine ya kuonana”Aliongea Neema na kumfanya Roma atoe macho , yaani hakuamini hii pisi leo inamuacha hivihivi pasipo kumpa kidogo ukizingatia joto lake limepanda kwa kiwango kikubwa.

“Unaniachaje hivi sasa Neema?”Aliuliza Roma .

“Ni jambo muhimu sana , ni juu ya mtoto wangu naomba niondoke nitakutafuta siku nyingine”Aliongea Neema na alionekana hakuwa tayari kusubiri jibu kutoka kwa Roma alianza kupiga hatua kuondoka.

Wakati Roma akijiuliza cha kufanya kwa wakati huo , kwani hali yake haikuwa sawa kabisa na alihitaji kampani ya mwanamke kwa usiku huo , mara simu yake ilianza kuita , aliitoa na kuangalia jina na aliona aliekuwa akipiga ni Nasra , Roma alijikuta akimkumbuka huyu mrembo maana tokea arudi Japani hawajaonana.

“Bebi Nasra naona umenikumbuka leo,halafu unaonekana kuwa sehemu yenye makelele upo nyumbani kweli?”

“Sipo nyumbani nifuate , nipo Kidimbwi”aliongea Nasra upande wa pili na kumfanya Roma ashangae , kwanza hakuwa akipajua Kidimbwi ni wapi.

“Kidimbwi ndio wapi Nasra?”

“Ni ufukweni Kidimbwini nifuate”Aliongea Nasra na kukata simu , alionekana alikuwa amelewa , Roma hakutaka kubaki hapo , alitembea kuitafuta gari yake.

Baada ya dakika chache tu alikuwa ashaifikia na kutafuta Kidimbwi ilipo maana Gari lake lilikuwa na uwezo wa kuonyesha ramani , na alitabasamu baada ya kuona hakuwa mbali na sehemu yenyewe ni kilomita kama moja tu hivi kutoka alipo.

Nasra alionekana kujiinamia chini kwenye Meza , haikueleweka alikuwa na nani hapo ndani kwani muda huu ,alikuwa peke yake na jambo hili lilimshangaza Roma.

“Mbona upo peke yako na unafamya nini hapa ?”Aliongea Roma.

“Nilikuja na marafiki zangu niliomaliza nao chuo ndio wameondoka na kuniacha na siwezi kuendesha gari nikiwa mlevi hivi”aliongea Nasra huku akijinyanyua kilevi na Roma alimshikilia.

Roma hakuona haja ya kumrudisha Nasra Mikocheni , kwani asingeweza kuacha gari yake hapo , alichoona ni kuchukua chumba ili waweze kuondoka asubuhi.

*****

Ilikuwa ni muda wa asubuhi , Roma aliamshwa na simu akiwa ndani ya hoteli na Nasra ambaye alikuwa amejilaza vibaya kweli , na hii ni baada ya wao wawili kumaliza kufanya mapenzi usiku kucha na staili yao ambayo Roma alimwambia Nasra inaitwa ‘Facing The Ocean’.

“Diego kuna nini ?”Aliuliza Roma baada ya kuona jina la mpigaji ni Diego na alijua lazima kutakuwa na tatizo.

“Your Majesty ! nadhani usiku wa leo haujalala nyumbani”

“Ndio”

“Chiara na John walifika nyumbani kwako kwa ajili ya jukumu lao la kazi , lakini hali walioikuta haikuwa shwari , geti walikuta lipo wazi na pia vijana wanaotoa ulinzi hawana fahamu ”Aliongea Diego na hapa Roma aliona kweli kuna tatizo.

Alikurupuka harakaharaka na kisha akavaa nguo zake .

“Diego hebu jaribuni kufatilia nin kimetokea ninafika nyumbani mara moja kuona tatizo ni nini”Aliongea Roma haraka haraka na kisha akakata simu , na akamuamsha na Nasra na kumwambia kuna dharula na ataondoka wa kwanza na hata hakusubiria jibu , alifungua mlango na kutoweka ndani ya eneo hilo.

Ndani ya kama nusu saa tu hivi ,Roma alikuwa akiingia Kigamboni nyumbani kwake , na ni kweli ile anafika geti lilikuwa wazi na hata mlango wa mbele wa nyumba yao ulikuwa wazi pia , alikimbilia ndani mpaka sebuleni huku akiita jina la Edna na hakukuwa na majibu , lakini ile amesimama ,alivyoangalia kwenye meza ya kioo aliona kikaratasi cha rangi ya njano kilichokuwa kimebandikwa kwenye Meza ba gundi.

“Your Majest Pluto ,Jumba unalokaa ni kubwa sana na tumeshangazwa , Tupo na mkeo pamoja na Mama wa nyumbani , ukiwataka wakiwa hai tuletee jiwe la Kimungu(Godstone),Sehemu ni Mabwepande , uje peke yako…Cc Froma Yamata Sect”Kilikuwa ni kikratasi ambacho kimeandikwa kwa lugha ya kijapani.

END OF SEASON 3 HAVE NICE WEEKEND
ITAENDELEA SIKU YOYOTE

ACHA KUTESEKA NA AROSTO CHANGIA 2000 KUENDELEA HALAFU NICHEKI WATSAPP 0687151346 UUNGANISHWE NA GURPU , AU KAMA HUPENDI GRUPU NITAKUTUMIA INBOX, KILA SIKU VIPANDE VITAT , KWA SASA TUPO SEASON 5 KIPANDE CHA 130



NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
Safi
 
SEHEMU YA 90

Roma alikuwa tayari ashawasiliana na Neema luwazo sehemu ya makutano yao, licha ya kwamba Roma alishangazwa na umbali wa eneo ambalo Neema alikuwa amechagua , eneo la Mbezi Beach ila aliona haina tabu

Roma hakujali sana, alichukulia kama fursa ya kuendesha gari umbali mrefu, kwanza sio kama alikuwa na shida ya mafuta , hakuwa nayo ,kwani pesa ya mafuta ilikuwa ni ya mke wake Edna.

Dakika kama arobaini hivi alikuja kukutana na Neema Luwazo karibu na kanisa la KKKT Mbezi beach ,Neema usiku huu alikuwa pia yupo kwenye gari yake kubwa aina ya Range Rover Spot , alishusha kioo.

“Nifuatishe nyuma kuna sehemu nataka twende”Alionea Neema na Roma alitingisha kichwa huku Neema akipandisha kioo cha gari yake na kuanza kulitoa taratibu kulekea upande wa Tegeta ,dakika chache mbele baada ya kutoka barabara kuu hatimae waliweza kuingia sehemu ambayo Roma hakuwa akiifahamu , yeye alichofanya nikufatisha tu gari ya Neema , walikuja kuegesha gari zao na kisha wakatoka.

Neema usiku huu alikuwa amependeza kweli , alikuwa amevalia gauni na kijikoti cha suti rangi ya Bluu na raba nyeupe.

“Umependeza”Aliongea Roma huku akimwangalia Neema , mbaye kwa usiku huu hakuonekana yule mwanamke ambaye alikuwa akiwahenyesha wenzake bungeni kwa maswali yake wakati wa kuachangia hoja.

Neema alitabasamu huku akimwangalia Roma , alionekana alikuwa akimwangalia kwa maswali mengi .

“Unapajua hapa au ushawahi kufika?”Aliuliza Neema

“Sijawahi kufika hapa , kwanza ningeweeza vipi kufika wakati nilianza kutembea na matajiri juzi tu baada ya kumuoa Edna mwanamke tajiri”aliongea Roma, huku wakisogea sehemu ambayo kulikuwa na viti , hii sehemu ilikuwa nzuri sana , ilikuwa ni Fukwe yenye upepo wa hali ya juu , lakini pia iliojengwa vizuri sana kwa watu kupumzika na hata pia kulala , palikuwa na hoteli kubwa tu sehemu hii.

“Hapa ni Upepo Beach Garden , nimewekeza hapa, hio hoteli ni ya kwangu”aliongea Neema na kumfanya Roma aangalie lijihoteli la nyota tano lililokuwa mbele yake.

“Kuna muda najiulizaga kwanini kila mwanamke ambaye nimetokea kujuana nae ana hela kuliko mimi”Aliongea Roma.

“Na hilo pia unajali Roma?”

“Wewe unaonaje?”Aliuliza Roma mara baada ya wao kuketi ndani ya eneo hili ambalo usiku huu palionekana kutokuwa na watu wengi , licha ya kwamba baadhi ya watu wapo, tena wakiwa na wapenzi.

“Unaonekana kama usiekuwa ni mwenye kujali watu wenyepesa na hili naweza kusema limenifanya nikuone wa tofauti na vijana wengi”aliongea Neema huku akitabasamu na muda huohuo alisogea mzee mmoja.

“Neema naona leo umekuja hapa na mgeni kwa mara ya kwanza?”Alikuwa ni mzee hivi mwenye Mvi japo sio nyingi , alikuwa amevalia mavazi ya uhudumu ndani ya hili eneo na kumfanya Roma ashangae inakuwaje mzee kama huyu akafanya kazi kama hio.

“Ndio Mzee Chino , huyu ni Roma ni rafiki yangu”Aliongea Neema akimtambulisha Roma na mzee akatabasamu.

“Roma huyu ni Mzee Chino ni mmiliki wa hili eneo lakini pia anaweza kua kama baba yangu baada ya mama na baba kufariki”Aliongea Neema na kumfanya Roma ashangazwe na mambo mawili, kwanza juu ya Mzee huyu kumiliki eneo hili la fukwe na wakati huhuo akifanya kazi za uhudumu hakuonesha kabisa kama mmiliki , lakini pia Juu ya Wazazi wa Neema kufariki.

“Kijana unabahati sana , unaonekana kuwa ‘Special’ kwa Neema hajawahi kuja na mwanaume hapa ni mara ya kwanza, Zaidi ya kuja na mtoto wake pekee”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Neema aone aibu kidogo na Roma alitabasamu.

“Sasa Mzee unaonekana unapesa lakini imenishangaza unaonekana kuwa muhudumu au ndio swaga za kuwavutia warembo”alitania Roma na kumfanya Neema kucheka.

“Kijana una maneno sana , ninachokifanya ni kitu ninachokipenda , licha ya Eneo hili Neema kujenga hoteli yake , lakini huu mgahawa ni wa kwangu na ninapenda kufanyakazi ya kuhudumia watu kwani inanikutanisha na watu tofauti tofauti , lakini pia ndio kazi ninayopenda , nimeanza kufanya kazi hii wakati nikiwa namfukuzia mama yake Neema”Aliongea Mzee Chino Bila aibu na kumfanya Roma ashangae.

“Kwahio ilikuwaje sasa Mzee Chino , ulimpata Mama yake Neema?”

“Nimpate wapi alinipa sharti la kuacha kazi yangu ya uhudumu niwe nae , nikakataa , akaniacha akaenda kwa mwanaume mwingine mwenye pesa Zaidi yangu”aliongea Mzee chino

“Mzee Chino tuletee supu yako ile unayotengezaga na chapatti pembeni”Aliongea Neema kukatisha maongezi na Mzee chino alitii na kwenda kuleta , ila kwa Roma alishangazwa inakuwaje Waziri akaagiza Chapati na supu usiku wote huu.

“Unashangaa ! kila ninapokuja hapa mara nyingi napenda kunywa supu ya Samaki”Aliongea Neema na Roma alimwelewa ,ukweli ni kwamba hata yeye alikuwa amemisi sana aina hio ya chakula.

‘Seafood’ ni vyakula ambavyo Roma alikuwa na muda mrefu tokea afike Tanzania hajavigusa kabisa , na aliona sio mbaya kwa usiku huo kupata aina hio ya chakula , Roma aliona kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana walikuwa kwenye ‘Date’.

“Nilijua Mkeo atakukataza kuja kuonana na mimi?”.

“Na amenikataza , ila sikutaka kumtii kwasababu nilishaweka ahadi ya kuonana na wewe”.

“Nijikuwa sina jinsi Zaidi ya kumuomba namba yako Roma , sikutaka kujificha mbele yake , kama angenikatalia namba yako nisingelazimisha hata tuonane , lakini alivyonipatia nikaona hakuwa na shida ya mimi na wewe kuonana”Aliongea Neema kwa sauti ya kawaida na wakati huohuo Chino alileta kile Neema alichoagiza mabakuli mawili , Roma baada ya kuona mifupa ya samaki na nyama nyama alipandwa na hamu ya kushughulikia msosi huo.

“Neema inabidi unitambulishe vizuri , siamini kama kuna urafiki unaoendelea hapa”Aliongea Mzee Chino huku akindoka akiwa na tabasamu na Neema aliishia kutabasamu.

“Unajua kwanini nimechagua hii sehemu?”Aliuliza Neema.

“Mimi najuaje wewe ndio umenileta hapa”

“Nilivyokuwa mdogo Mama alikuwa akipendelea kunileta sana hapa, ni kama kumbukumbu pekee ambayo ameniachia , kila ninapokuwa sina Amani nakuja hapa, nakaa natulia then kesho nitaondoka nikiwa mpya, na nilijiambia siku nikipata mwanaume ambaye nitatokea kumpenda kwa dhati nitamleta hii sehemu”Aliongea Neema kwa hisia na wakaangaliana na Roma.

“Lakini mwanaume ambaye nilikuwa nikimuota amechelewa sana kuja kwenye maisha yangu mpaka nikiwa na umri huu”

“Neema mbona unaonekana kama ndio unanifungukia sasa”Aliongea Roma na Neema akatabasamu baada ya kuona namna Roma anavyonyoosha maneno.

“Unajua Roma unaonekana muhuni sana wakucheza na wanawake na bado nikashangaa kwanini mwanamke kama Dorisi akakupenda na pia Edna kuwa mke wako na mimi mwenyewe pia kukupenda kiasi hiki”

“Sasa kwanini unaonekana ni mwenye kunipenda , mimi mwenywe najua sijatulia na udhaifu wangu mkubwa ni wanawake , kwanini licha ya kulijua hilo unaonekana kunipenda?”

“Kwasababu sisi wanawake ni tofauti na nyie wanaume , nyie ili mumpende mwanamke mnaangalia vitu vingi ,kama vile uzuri . upole na vigezo kibao , ila kwetu sisi hatuna sababu ya kumpenda mwanaume, ukimkuta mwanamke kapenda kweli na ukamuuliza kwanini kapenda atashindwa kukupa jibu , ila kwa mwanaume ni rahisi kukupa jibu kwanini kampenda mwanamke wake”Aliongea na Roma licha ya kwamba alikuwa akisikiliza lakini alikuwa bize na chakula chake , alikunwa akitafuna yaani, hakuwa ni mwenye kuchanganywa na mwanamke kama waziri kumfungukia yeye kwake aliona ni kawaida,ingekuwa ni vijana wengine wakakutana na hali kama hio huenda wangekuwa wapo tofauti sana na Roma.

“Kwahio huna sababu nyingine ambayo inakufanya kunipenda , yaani huwezi eleza kwanini unanipenda?”

“Licha ya kwamba unaonekana mwanaume ambaye huwezi kutulizwa na mwanamke mmoja ,ila ninashauku ya kukujua Roma , najua kabisa haupo wa kawaida , kila siku ambayo tumekutana mimi na wewe lazima unishangaze ,ni mwanaume ambaye hautabiriki na hii imenipa shauku Zaidi ya kuwa na ukaribu na wewe ili kukujua”

Aliongea Neema na Roma akamwangalia mrembo huyu ambaye kwake ki umri walikuwa wamepishana sana , licha ya kwamba Neema kuonekana mdogo lakini umri ulikuwa umeenda na hakuna mtu wa kukataa hilo ni vile tu kwamba alikuwa ni mwanamke wa kujitunza na pesa pia ilikuwa imemfanya kuonekana mdogo.

Roma alimalizia supiu yake lakini kwa Neema alionekana hata hamu ya kuendelea kula hakuwa nayo.

“Lakini Neema unajua kabisa mimi nina mke ,na nisiwe muongo hapa hata kama nikikubalia ujue sitoweza kucheza kwenye matarajio yako kama mwanamke ambaye ana mwanaume anaempenda”Aliongea Roma na Neema alitabasamu na kisha akanyanyuka.

“Unaonaje tukitembea tembeatembea mpaka kule”Aliongea na Roma hakubisha, alinawa mikono na kisha akanyanyuka .

“Nishazeeka tayari kwasasa Roma ,ki ufupi mimi sipo kama wasichana wa miiaka ishirini ambao watatamani vitu vikubwa kwa mwanaume , kwasasa nina kila kitu pesa na pia nina mtoto ,ninajua una mke na hilo nitaenda kuliheshimu na pia na mheshimu Edna , lakini ukweli ni kwamba licha ya kwamba unaonekana kuwa kijana mdogo , lakini nimetokea kukupenda sitaki unifanyie kikubwa , ila nitapenda kama utakuwa na mimi wakati nitakapokuhitaji”Aliongea Neema kwa hisia huku akisimama mbele ya Roma akiangalia upande wa baharini.

Na Roma hakujua cha kujibu kwa wakati huu , siku zote alikuwa ni mwenye kuanza wanawake lakini leo hii , yeye ndio kaanzwa na pia mwanamke aliembele yake alikuwa tayari ashaonja utamu wake.

Roma alimsogelea Neema kwa nyuma na kumkumbatia na kumfanya mwanamama huyu atabasamu na ajisikie vizuri sana , upande wa Roma hakutaka kuuliza sana juu ya Edna kumtahadharisha kuachana na Neema ,kwanza hakuwa akiogopa kiumbe chochote kwenye hii dunia kwanini aogope kuwa na mwanamke aliekuwa mbele yake ambaye anataka kuweka kumbukumbu kabla ya kuingia kwenye uzee wake.

Kadri sekunde na dakika zilizvyokuuwa zikisogea miili yao ilipata Joto la mapenzi na Neema ndio wa kwanza kugeuka na kugusisha midomo na Roma na kuanza kunyonyana kimahaba , huku Roma na yeye ekipitisha mikono kwenye mwinuko wa Mrembo Neema Luwazo.

“Cling .. Cling …Cling”

Ni simu ya Neema ndio iliowakatishia utamu na Neema hakutaka kupuuzia simu iliokuwa inaita alijitoa kwa Roma na kisha akaangalia ninani anapiga na jina lilisomeka ‘My daughter’.

Roma hakujua Neema alikuwa akiongea nini na simu kwani Neema alisogea mbali kidogo ,baada ya dakika kama moja za Neema kuongea na Simu , alimsogelea Roma.

“Naona jambo letu leo litaishia hapa nina dharula tutapanga siku nyingine ya kuonana”Aliongea Neema na kumfanya Roma atoe macho , yaani hakuamini hii pisi leo inamuacha hivihivi pasipo kumpa kidogo ukizingatia joto lake limepanda kwa kiwango kikubwa.

“Unaniachaje hivi sasa Neema?”Aliuliza Roma .

“Ni jambo muhimu sana , ni juu ya mtoto wangu naomba niondoke nitakutafuta siku nyingine”Aliongea Neema na alionekana hakuwa tayari kusubiri jibu kutoka kwa Roma alianza kupiga hatua kuondoka.

Wakati Roma akijiuliza cha kufanya kwa wakati huo , kwani hali yake haikuwa sawa kabisa na alihitaji kampani ya mwanamke kwa usiku huo , mara simu yake ilianza kuita , aliitoa na kuangalia jina na aliona aliekuwa akipiga ni Nasra , Roma alijikuta akimkumbuka huyu mrembo maana tokea arudi Japani hawajaonana.

“Bebi Nasra naona umenikumbuka leo,halafu unaonekana kuwa sehemu yenye makelele upo nyumbani kweli?”

“Sipo nyumbani nifuate , nipo Kidimbwi”aliongea Nasra upande wa pili na kumfanya Roma ashangae , kwanza hakuwa akipajua Kidimbwi ni wapi.

“Kidimbwi ndio wapi Nasra?”

“Ni ufukweni Kidimbwini nifuate”Aliongea Nasra na kukata simu , alionekana alikuwa amelewa , Roma hakutaka kubaki hapo , alitembea kuitafuta gari yake.

Baada ya dakika chache tu alikuwa ashaifikia na kutafuta Kidimbwi ilipo maana Gari lake lilikuwa na uwezo wa kuonyesha ramani , na alitabasamu baada ya kuona hakuwa mbali na sehemu yenyewe ni kilomita kama moja tu hivi kutoka alipo.

Nasra alionekana kujiinamia chini kwenye Meza , haikueleweka alikuwa na nani hapo ndani kwani muda huu ,alikuwa peke yake na jambo hili lilimshangaza Roma.

“Mbona upo peke yako na unafamya nini hapa ?”Aliongea Roma.

“Nilikuja na marafiki zangu niliomaliza nao chuo ndio wameondoka na kuniacha na siwezi kuendesha gari nikiwa mlevi hivi”aliongea Nasra huku akijinyanyua kilevi na Roma alimshikilia.

Roma hakuona haja ya kumrudisha Nasra Mikocheni , kwani asingeweza kuacha gari yake hapo , alichoona ni kuchukua chumba ili waweze kuondoka asubuhi.

*****

Ilikuwa ni muda wa asubuhi , Roma aliamshwa na simu akiwa ndani ya hoteli na Nasra ambaye alikuwa amejilaza vibaya kweli , na hii ni baada ya wao wawili kumaliza kufanya mapenzi usiku kucha na staili yao ambayo Roma alimwambia Nasra inaitwa ‘Facing The Ocean’.

“Diego kuna nini ?”Aliuliza Roma baada ya kuona jina la mpigaji ni Diego na alijua lazima kutakuwa na tatizo.

“Your Majesty ! nadhani usiku wa leo haujalala nyumbani”

“Ndio”

“Chiara na John walifika nyumbani kwako kwa ajili ya jukumu lao la kazi , lakini hali walioikuta haikuwa shwari , geti walikuta lipo wazi na pia vijana wanaotoa ulinzi hawana fahamu ”Aliongea Diego na hapa Roma aliona kweli kuna tatizo.

Alikurupuka harakaharaka na kisha akavaa nguo zake .

“Diego hebu jaribuni kufatilia nin kimetokea ninafika nyumbani mara moja kuona tatizo ni nini”Aliongea Roma haraka haraka na kisha akakata simu , na akamuamsha na Nasra na kumwambia kuna dharula na ataondoka wa kwanza na hata hakusubiria jibu , alifungua mlango na kutoweka ndani ya eneo hilo.

Ndani ya kama nusu saa tu hivi ,Roma alikuwa akiingia Kigamboni nyumbani kwake , na ni kweli ile anafika geti lilikuwa wazi na hata mlango wa mbele wa nyumba yao ulikuwa wazi pia , alikimbilia ndani mpaka sebuleni huku akiita jina la Edna na hakukuwa na majibu , lakini ile amesimama ,alivyoangalia kwenye meza ya kioo aliona kikaratasi cha rangi ya njano kilichokuwa kimebandikwa kwenye Meza ba gundi.

“Your Majest Pluto ,Jumba unalokaa ni kubwa sana na tumeshangazwa , Tupo na mkeo pamoja na Mama wa nyumbani , ukiwataka wakiwa hai tuletee jiwe la Kimungu(Godstone),Sehemu ni Mabwepande , uje peke yako…Cc Froma Yamata Sect”Kilikuwa ni kikratasi ambacho kimeandikwa kwa lugha ya kijapani.

END OF SEASON 3 HAVE NICE WEEKEND
ITAENDELEA SIKU YOYOTE

ACHA KUTESEKA NA AROSTO CHANGIA 2000 KUENDELEA HALAFU NICHEKI WATSAPP 0687151346 UUNGANISHWE NA GURPU , AU KAMA HUPENDI GRUPU NITAKUTUMIA INBOX, KILA SIKU VIPANDE VITAT , KWA SASA TUPO SEASON 5 KIPANDE CHA 130



NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
Sasa hawa walinzi wa kizungu wana kazi gani hadi Edna na bi wema wametekwa?
 
Back
Top Bottom