singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #1,561
SEHEMU YA 299.
Baada ya Fayezi kutoka ndani ya chumba cha Mke wake Mtarajiwa Amina , alitoka kabisa ndani ya hoteli hio akiwa ametangulizana na wanajeshi wawili kutoka kikosi maalumu ambao wote wamekodiwa na familia yake kwa ajili ya kumpa ulinzi, wote wakiwa wamevalia suti.
Dakika chache mbele walikuja kusimamisha magari yao mawili upande wa pili ndani ya jiji hili la Otaru ,sehemu maarufu sana iliokuwa ikisifika kwa kuwa na huduma ya masaji iliokuwa ya kiwango cha juu sana.
Fayezi alitaka kuweka mwili wake sawa kabla ya siku yake kubwa ya kesho na ndio maana alikuwa ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kufanyiwa masaji, Alikutana na mwanaume mwingine wa kijapani ambaye alikuwa ni wa umri wa kati alievalia suti na alimuongoza kwa heshima kubwa na kwa Pamoja waliingia kwenye jengo ambalo lilikuwa na bango linalowaka taa na maandishi makubwa rangi nyekundu yaliosomoeka kwa juu ‘Clubhouse’.
Wote wawili Pamoja na bwana ambaye alimpokea walionekana wakiwa ndani ya chumba cha masaji huku wakiwa wamezungukwa na wanawake warembo sana waliovalia nusu uchi wakishikwa kwa mikono laini sana wakifanyiwa masaji , kitendo amacho kiliwafanya kujihisi kama vile wapo dunia nyingine kabisa.
Dakika takribani ishirini walikuwa wakiminywa minywa kwanzia makalioni mpaka kwenye shingo , Fayezi licha ya kutozoea huduma hio , lakini alionekana kuifurahia mno.
Wakati wakiendelea kufanyiwa masaji simu ndani ya chumba hiko ilianza kuita mfululizo ikiashria kuna dharula na mhuduu aliekuwa karibu aliichukua na kisha kuipokea baada ya kuona inatokea mapokezi.
“Sir kuna kundi la watu limeingia ndani pasipo ruhusa kutoka mapokezi na wanasema wanawatafuta”Aliongea yule mwanamke na kumfanya bwana yule wa kijapani kumwangalia kwani mhudmu aliongea kwa kijapani .
“Amesema wametokea wapi?”
“Wamesema ni kutoka kundi la Yamata Sect”Aliongea yule muhudumu na kumfanya Fayezi aliekuwa akiendelea kuburudika kuinua kichwa.
“Kama ni Yamata haija haja ya kuwahofia , nina ushirkiano nao katika maswala ya kibiashara hivyo hawana madhara kwetu kwani kila kitu kinaenda sawa”Aliongea Feyezi kwa kingeteza , lakini mara baada ya kumaliza Sentensi yake , kundi la wajapani waliovalia suti wakiwa mchanganyiko wa wanawake na wanaume waliingia ndani ya chumba hiko cha masaji huku nyuso zao zikiwa katika hali ya usiriasi mno.
Fayezi aliwaangalia watu hao na kuona hakuwa akiwatambua hata mmoja , lakini hakujali , alichokuwa akiamini ni kwamba watu hao walikuwa ni moja ya vijana wa Noriko Okawa.
“Wewe ndio unafahamika kwa jina la Fayezi kutoka kampuni ya Emaar Dubai?”Aliuliza kwa Kingereza mwanaume mmoja wa kijapani ambaye sura yote imajaa ndevu huku akiwa na sura ya kutisha.
“Ndio ni mimi , mnashida gani na mimi , kwani kila kitu nilishamalizana na boss wenu?”
“Tumepata taarifa kwamba unafanya biashara ya madawa ya kulevya ndani ya eneo letu jambo ambalo ni kinyume na makubaliano yetu ya kibiashara”
“Madawa ya kulevya!! , hapani sio kweli , boss wenu atakuwa amekosea”
“Hajakosea na ndio alietupatia maelekezo ya kuja hapa, utatoa ushirikiano wako na tutakusachi kama hauna madawa ya kulevya tutakuacha na kuendelea na mambo yako”Aliongea yule bwana ambaye alionekana kuwa ndio kiongozi wa kundi la Yamata Sect.
Lakini hata hivyo Fayezi aligoma kusachiwa na sharti lake lilikuwa ni kuongea kwanza naNoriko Okawa ambaye alikuwa akimjua kama mkuu wa kundi la Yamata na vijana wale hawakuwa na shida , simu ilipigwa kwa boss mwenyewe
“Mr Fayezi wape vijana wangu ushirikiano , tumepewa taarifa unafanya biashara ya heroin ndani ya mji wetu wa kibiashara”Ilisikika suati ya mwanamke upande wa pili na kumfanya Fayezi kutabasamu kifedhuli.
“Nataka kuongea na boss wako”
“Kwanzia leo mimi ndio boss wa Yamata Sect, kama unamuulizia Noriko Okawa basi fahamu kwamba hayupo tena hai”ilisikika sauti na kumfanya Fayezi kushangaa mno ni kama hakuwa akiamini.
“Noriko Okawa hawezi kufa haraka hivyo ,mchana wa leo niliwasiliana nae na hata hivyo mimi sifanyi biashara yoyote ya madawa ya kulevya mmekosea mtu mnaemtafuta”Aliongea Fayezi kwa namna ya kujitetea , lakini watu kumi kutoka kundi la Yamata Sect walionekana kuwa siriasi mno na walikuwa wakitaka tu kusikia amri ya boss wao wachukue hatua.
“Kama unajiamini hauna madawa ya kulevya , basi haina haja ya kuewaletea matatizo vijana wangu unachotakiwa kufanya ni kuwaruhusu kufanya kazi yao , kama alietoa taarifa kakosea basi adhabu itakuwa juu yake”Aliongea Mwanamke aliekuwa kwenye simu na mjapani aliekuwa ni msaidizi wa karibu wa Fayezi alimpa ishara ya kukubaliana na watu hao kumsachi.
“Okey mnaweza kusachi , sina haja ya kuogopa kusachiwa kwasababu najiamini sina madawa ya kulevya ya aina yoyote ile”Aliongea Fayezi na wale vijana wakiongozwa na kiongozi wao aliekuwa akifahami kwa jina la iboru , walianza kufanya ukaguzi wao ndani ya chumba hiko kwa haraka sana , hawakutaka kuchelewa kwani mteja wao alikuwa akionyesha kujiamini sana kutokuwa na madawa ndani ya chumba hiko , hivyo wlaiamini kufanya haraka ni kuokoa muda.
Walinzi wa Fayezi walitaka kuzuia jaribiio hilo , lakini vijana wa Yamata walionekana kuwa tayari kupambana, Fayezi ilibidi kuwapa ishara watulie na kuruhusu zoezi hilo kufanyika kwa dakika chache kwani alikuwa akiamni hakuwa na madawa ya kulecya na hakuwa hata na mpango wa kufanya biashara hizo haramn ndani ya Japani, yeye alikuwepo hapo ndani ya Japani kwa ajili ya kufunga ndoa na mpezni wake Amina , hivyo swala la madawa lilikuwa limemkalia kushoto.
Maninja wale wa kundi la Yamata Sect walitumia dakika kama tatu tu kusachi kwenye suti za Fayezi na yule mchina na hatimae waliweza kuibuka na vijimfuko vya nailoni vitatu vilivyokuwa na unga mweupe ndani yake , na kwa mtaalamu wa haraka haraka angegundua kuwa hayo ni madawa ya kulevya aina ya Heroin kutokana na rangi yake kuwa kama ya unga wa ngano.
“Hapana hayo madawa sihusiki nayo kabisa , sijawahi kupanga kuuza madawa ndani ya Japani na sio hivyo tu Emaar haijawahi kujihusisha na biashara haramu”Aliongea Fayezi kwa kujitetea huku akiwa kwenye mshangao kuona mfuko wake wa suti ndio uliotolewa paketi tatu za madawa hayo.
“Usitufanye sisi ni wajinga , tunaamini vipi hauhusiki, ushawahi kusikia wapi mtu anaeuza madawa ya kulevya akajitangaza, kila mtu anafanya siri na wewe pia ni mmoja ya watu wanaotunza siri katika biashara hii”
“Sio kweli labda hawa wanaofanya masaji ndio wamehusika kunibambikizia madawa hayo , ila sihusiki nayo kabisa na Mungu wangu ni shahidi”Aliongea Fayezi lakini vijana wale walionekana kutokujali kabisa , walichokifanya ni kupiga simu kwa boss wao.
“Boss tumepata kugundua Fayezi ndio muusika anaeuza madawa ndani ya jiji hili , tunapaswa kuchukua hatua gani baada ya hapa”
“Mkamateni na mleteni kambini tumuhoji vizuri”Sauti ya mwanadada Tanya ilisikika na vijana wale mara baada ya kusikika maelekezo hayo walitoa ishara kwa vijana wao kwa ajili ya kumzingira Fayezi , ili kumkamata na kumpeleka kambini kama walivyopewa maagizo na boss wao.
Fayezi alikuwa ni mwenye hasira mno , mpaka hapo aliamini huo ni mtego umeandaliwa kwa ajili ya kumkamatisha hivyo hakuwa tayari kukamatwa kizembe wakat iyeye ni mtoto wa Tajiri kutoka dubai na alikuwa na koneksheni nyingi.
“Naombeni nifanye mawasiliano”Aliongea Fayezi huku akisogelea suruali yake , lakini maninja wa Yamata Sect waliichukua nguo zake na kutoa simu na kisha wakamrushia nguo zake avae haraka na kwakua Fayezi na mwenzake alikuwa uchi , hawakuleta ubishi walivaa.
“Hatuwezi kukupa simu tena kwani mara ya kwanza ulituambia huna madawa na tukakukutan nayo , unatufanya sisi wajinga na hatuwezi kuruhusu”Aliongea yule jamma mwenye kutisha huku akimwangalia Fayezi aliekuwa akivaa mavazi yake kwa haraka.
Walinzi wa Fayezi walidhibitiwa ndani ya dakika chache tu na wale wahudumu pia na wenyewe walidhbitiwa na kwa Fayezi na msaidizi wake pia walidhibitiwa na wote kwa Pamoja walipoteza fahamu palepale na dakika kadhaa mbele walikuwa wakitolewa nje kabisa ya Clubhouse na kuingizwa kwenye gari aina ya Noah Toyota na palepale gari ile iliondolewa na Kwenda kusimama mita kadhaa mbele sehemu yenye miti ya bustani na mlango wa Gari lile ulifunguliwa kwa mara nyingine na Fayezi Pamoja na msaidizi wake walionekana wakitoka ndani ya gari lile na kuanza kupiga hatua kurudi kule walikotoka wakiwa vile vile na mavazi yao yaleyale.
Baada ya Fayezi kutoka ndani ya chumba cha Mke wake Mtarajiwa Amina , alitoka kabisa ndani ya hoteli hio akiwa ametangulizana na wanajeshi wawili kutoka kikosi maalumu ambao wote wamekodiwa na familia yake kwa ajili ya kumpa ulinzi, wote wakiwa wamevalia suti.
Dakika chache mbele walikuja kusimamisha magari yao mawili upande wa pili ndani ya jiji hili la Otaru ,sehemu maarufu sana iliokuwa ikisifika kwa kuwa na huduma ya masaji iliokuwa ya kiwango cha juu sana.
Fayezi alitaka kuweka mwili wake sawa kabla ya siku yake kubwa ya kesho na ndio maana alikuwa ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kufanyiwa masaji, Alikutana na mwanaume mwingine wa kijapani ambaye alikuwa ni wa umri wa kati alievalia suti na alimuongoza kwa heshima kubwa na kwa Pamoja waliingia kwenye jengo ambalo lilikuwa na bango linalowaka taa na maandishi makubwa rangi nyekundu yaliosomoeka kwa juu ‘Clubhouse’.
Wote wawili Pamoja na bwana ambaye alimpokea walionekana wakiwa ndani ya chumba cha masaji huku wakiwa wamezungukwa na wanawake warembo sana waliovalia nusu uchi wakishikwa kwa mikono laini sana wakifanyiwa masaji , kitendo amacho kiliwafanya kujihisi kama vile wapo dunia nyingine kabisa.
Dakika takribani ishirini walikuwa wakiminywa minywa kwanzia makalioni mpaka kwenye shingo , Fayezi licha ya kutozoea huduma hio , lakini alionekana kuifurahia mno.
Wakati wakiendelea kufanyiwa masaji simu ndani ya chumba hiko ilianza kuita mfululizo ikiashria kuna dharula na mhuduu aliekuwa karibu aliichukua na kisha kuipokea baada ya kuona inatokea mapokezi.
“Sir kuna kundi la watu limeingia ndani pasipo ruhusa kutoka mapokezi na wanasema wanawatafuta”Aliongea yule mwanamke na kumfanya bwana yule wa kijapani kumwangalia kwani mhudmu aliongea kwa kijapani .
“Amesema wametokea wapi?”
“Wamesema ni kutoka kundi la Yamata Sect”Aliongea yule muhudumu na kumfanya Fayezi aliekuwa akiendelea kuburudika kuinua kichwa.
“Kama ni Yamata haija haja ya kuwahofia , nina ushirkiano nao katika maswala ya kibiashara hivyo hawana madhara kwetu kwani kila kitu kinaenda sawa”Aliongea Feyezi kwa kingeteza , lakini mara baada ya kumaliza Sentensi yake , kundi la wajapani waliovalia suti wakiwa mchanganyiko wa wanawake na wanaume waliingia ndani ya chumba hiko cha masaji huku nyuso zao zikiwa katika hali ya usiriasi mno.
Fayezi aliwaangalia watu hao na kuona hakuwa akiwatambua hata mmoja , lakini hakujali , alichokuwa akiamini ni kwamba watu hao walikuwa ni moja ya vijana wa Noriko Okawa.
“Wewe ndio unafahamika kwa jina la Fayezi kutoka kampuni ya Emaar Dubai?”Aliuliza kwa Kingereza mwanaume mmoja wa kijapani ambaye sura yote imajaa ndevu huku akiwa na sura ya kutisha.
“Ndio ni mimi , mnashida gani na mimi , kwani kila kitu nilishamalizana na boss wenu?”
“Tumepata taarifa kwamba unafanya biashara ya madawa ya kulevya ndani ya eneo letu jambo ambalo ni kinyume na makubaliano yetu ya kibiashara”
“Madawa ya kulevya!! , hapani sio kweli , boss wenu atakuwa amekosea”
“Hajakosea na ndio alietupatia maelekezo ya kuja hapa, utatoa ushirikiano wako na tutakusachi kama hauna madawa ya kulevya tutakuacha na kuendelea na mambo yako”Aliongea yule bwana ambaye alionekana kuwa ndio kiongozi wa kundi la Yamata Sect.
Lakini hata hivyo Fayezi aligoma kusachiwa na sharti lake lilikuwa ni kuongea kwanza naNoriko Okawa ambaye alikuwa akimjua kama mkuu wa kundi la Yamata na vijana wale hawakuwa na shida , simu ilipigwa kwa boss mwenyewe
“Mr Fayezi wape vijana wangu ushirikiano , tumepewa taarifa unafanya biashara ya heroin ndani ya mji wetu wa kibiashara”Ilisikika suati ya mwanamke upande wa pili na kumfanya Fayezi kutabasamu kifedhuli.
“Nataka kuongea na boss wako”
“Kwanzia leo mimi ndio boss wa Yamata Sect, kama unamuulizia Noriko Okawa basi fahamu kwamba hayupo tena hai”ilisikika sauti na kumfanya Fayezi kushangaa mno ni kama hakuwa akiamini.
“Noriko Okawa hawezi kufa haraka hivyo ,mchana wa leo niliwasiliana nae na hata hivyo mimi sifanyi biashara yoyote ya madawa ya kulevya mmekosea mtu mnaemtafuta”Aliongea Fayezi kwa namna ya kujitetea , lakini watu kumi kutoka kundi la Yamata Sect walionekana kuwa siriasi mno na walikuwa wakitaka tu kusikia amri ya boss wao wachukue hatua.
“Kama unajiamini hauna madawa ya kulevya , basi haina haja ya kuewaletea matatizo vijana wangu unachotakiwa kufanya ni kuwaruhusu kufanya kazi yao , kama alietoa taarifa kakosea basi adhabu itakuwa juu yake”Aliongea Mwanamke aliekuwa kwenye simu na mjapani aliekuwa ni msaidizi wa karibu wa Fayezi alimpa ishara ya kukubaliana na watu hao kumsachi.
“Okey mnaweza kusachi , sina haja ya kuogopa kusachiwa kwasababu najiamini sina madawa ya kulevya ya aina yoyote ile”Aliongea Fayezi na wale vijana wakiongozwa na kiongozi wao aliekuwa akifahami kwa jina la iboru , walianza kufanya ukaguzi wao ndani ya chumba hiko kwa haraka sana , hawakutaka kuchelewa kwani mteja wao alikuwa akionyesha kujiamini sana kutokuwa na madawa ndani ya chumba hiko , hivyo wlaiamini kufanya haraka ni kuokoa muda.
Walinzi wa Fayezi walitaka kuzuia jaribiio hilo , lakini vijana wa Yamata walionekana kuwa tayari kupambana, Fayezi ilibidi kuwapa ishara watulie na kuruhusu zoezi hilo kufanyika kwa dakika chache kwani alikuwa akiamni hakuwa na madawa ya kulecya na hakuwa hata na mpango wa kufanya biashara hizo haramn ndani ya Japani, yeye alikuwepo hapo ndani ya Japani kwa ajili ya kufunga ndoa na mpezni wake Amina , hivyo swala la madawa lilikuwa limemkalia kushoto.
Maninja wale wa kundi la Yamata Sect walitumia dakika kama tatu tu kusachi kwenye suti za Fayezi na yule mchina na hatimae waliweza kuibuka na vijimfuko vya nailoni vitatu vilivyokuwa na unga mweupe ndani yake , na kwa mtaalamu wa haraka haraka angegundua kuwa hayo ni madawa ya kulevya aina ya Heroin kutokana na rangi yake kuwa kama ya unga wa ngano.
“Hapana hayo madawa sihusiki nayo kabisa , sijawahi kupanga kuuza madawa ndani ya Japani na sio hivyo tu Emaar haijawahi kujihusisha na biashara haramu”Aliongea Fayezi kwa kujitetea huku akiwa kwenye mshangao kuona mfuko wake wa suti ndio uliotolewa paketi tatu za madawa hayo.
“Usitufanye sisi ni wajinga , tunaamini vipi hauhusiki, ushawahi kusikia wapi mtu anaeuza madawa ya kulevya akajitangaza, kila mtu anafanya siri na wewe pia ni mmoja ya watu wanaotunza siri katika biashara hii”
“Sio kweli labda hawa wanaofanya masaji ndio wamehusika kunibambikizia madawa hayo , ila sihusiki nayo kabisa na Mungu wangu ni shahidi”Aliongea Fayezi lakini vijana wale walionekana kutokujali kabisa , walichokifanya ni kupiga simu kwa boss wao.
“Boss tumepata kugundua Fayezi ndio muusika anaeuza madawa ndani ya jiji hili , tunapaswa kuchukua hatua gani baada ya hapa”
“Mkamateni na mleteni kambini tumuhoji vizuri”Sauti ya mwanadada Tanya ilisikika na vijana wale mara baada ya kusikika maelekezo hayo walitoa ishara kwa vijana wao kwa ajili ya kumzingira Fayezi , ili kumkamata na kumpeleka kambini kama walivyopewa maagizo na boss wao.
Fayezi alikuwa ni mwenye hasira mno , mpaka hapo aliamini huo ni mtego umeandaliwa kwa ajili ya kumkamatisha hivyo hakuwa tayari kukamatwa kizembe wakat iyeye ni mtoto wa Tajiri kutoka dubai na alikuwa na koneksheni nyingi.
“Naombeni nifanye mawasiliano”Aliongea Fayezi huku akisogelea suruali yake , lakini maninja wa Yamata Sect waliichukua nguo zake na kutoa simu na kisha wakamrushia nguo zake avae haraka na kwakua Fayezi na mwenzake alikuwa uchi , hawakuleta ubishi walivaa.
“Hatuwezi kukupa simu tena kwani mara ya kwanza ulituambia huna madawa na tukakukutan nayo , unatufanya sisi wajinga na hatuwezi kuruhusu”Aliongea yule jamma mwenye kutisha huku akimwangalia Fayezi aliekuwa akivaa mavazi yake kwa haraka.
Walinzi wa Fayezi walidhibitiwa ndani ya dakika chache tu na wale wahudumu pia na wenyewe walidhbitiwa na kwa Fayezi na msaidizi wake pia walidhibitiwa na wote kwa Pamoja walipoteza fahamu palepale na dakika kadhaa mbele walikuwa wakitolewa nje kabisa ya Clubhouse na kuingizwa kwenye gari aina ya Noah Toyota na palepale gari ile iliondolewa na Kwenda kusimama mita kadhaa mbele sehemu yenye miti ya bustani na mlango wa Gari lile ulifunguliwa kwa mara nyingine na Fayezi Pamoja na msaidizi wake walionekana wakitoka ndani ya gari lile na kuanza kupiga hatua kurudi kule walikotoka wakiwa vile vile na mavazi yao yaleyale.