Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Ila ya kumsapoti singanojr hauna! Au unadhan anatumia makamasi kupost humu? Ona basi aibu! Na post yako hii ya ki selfish
Ww Ni kunguni au chawa?

Unadhan wote wanaoingia humu Wanategemea wifi ya ofis Kama wewe? Ulitaka nisomeje bila kununua bando?

Kama ww unamsapot, ndo unatutangazia hapa kuwa ww unasapoti?

Ww si chawa Wala kunguni, ww Ni pimbi

Kwahiyo, wote wanaosoma hii simulizi wametoa sh ngapi? Unajiona una akili kweli Yan, mtumie basi hata kamilion ili uwe mfadhili wetu
 
Karibun kwenye group..huku wenzenu tuko mbaliiii ni dozi ya per day tunakunjwa ikupungua sana ni kutwa X 2 .. acheni ubahili wenu huo wa kubania vi buku jero.
Shauri yenu 😎
 
Ila ya kumsapoti singanojr hauna! Au unadhan anatumia makamasi kupost humu? Ona basi aibu! Na post yako hii ya ki selfish
Tatizo Singano naye anakosea mfano mimi namtafuta huwa arespond chochote unadhani inanipa picha gani ndiyo maana tunabaki kusubiri huku, maana nilimuuliza katika phone number yake anipe utaratibu lakini kimya.
 
Karibun kwenye group..huku wenzenu tuko mbaliiii ni dozi ya per day tunakunjwa ikupungua sana ni kutwa X 2 .. acheni ubahili wenu huo wa kubania vi buku jero.
Shauri yenu [emoji41]
Sasa huku unafanya Nini matako wewe.....


[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Sasa huku unafanya Nini matako wewe.....


[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
Ahahahahah nimekuja kufanya unoko tuu...si unakumbuka enzi zile za kishule shule mtu anakuona jinsi unavyopotea kujibu swali af anakuchora tuu huku anacheka kimoyo moyo.....

Au anajua kabisa umefeli af anakuja kukuuliza umepata ngapi???😂😂😂
 
Tatizo Singano naye anakosea mfano mimi namtafuta huwa arespond chochote unadhani inanipa picha gani ndiyo maana tunabaki kusubiri huku, maana nilimuuliza katika phone number yake anipe utaratibu lakini kimya.
Oya singanojr unaitwa huku..heb muunge mwana kwenye mavitu ya ukweli kule
 
Tatizo Singano naye anakosea mfano mimi namtafuta huwa arespond chochote unadhani inanipa picha gani ndiyo maana tunabaki kusubiri huku, maana nilimuuliza katika phone number yake anipe utaratibu lakini kimya.
nitafute watsapp 0687151346 nipo online utaoata mwendelezo chapu na kujoin group Hades yupo USA anakiwasha [emoji1787]

Ngoja niweke mwendelezo hapa tulale vyedi
 
nitafute watsapp 0687151346 nipo online utaoata mwendelezo chapu na kujoin group Hades yupo USA anakiwasha [emoji1787]

Ngoja niweke mwendelezo hapa tulale vyedi
Sawa mkuu naona na kule Meta ushatupia ..ahahah...
 
TUNAENDELEA

SEHEMU YA 326

“Miss Edna familia yangu miaka ya hivi karibuni imevutiwa na kufanya uwekezaji ndani ya Taifa la Tanzania hususani upande wa maswala ya kifedha, na kampuni ya ‘JR Group of Companies’ ndio ambayo nimetuvutia kutokana na ‘Model’ ya biashara zake

“Lakini Kampuni ya JR haijihusishi na maswala ya Fedha , huduma wanazotoa ni za udhalishaji wa bidhaa , Mahoteli , pamoja na Usafirishaji”.

“Ni kweli , ninachozungumzia ni wewe kunisaidia kufungua benki ya kibiashara kwa kupitia jina la Kampuni ya JR , familia yangu pekee ndio itakuwa tayari kutoa mtaji”Aliongea Edward na kumfanya sasa Edna kuelewa anachomaanisha.

Alichokuwa akimaanisha Edward ni kwamba alikuwa akitaka kutumia kampuni ya JR kufungua benki ndani ya Tanzania kwa njia isio ya moja kwa moja, yaani Benki itambulike inamilikiwa na kampuni ya JR lakini nyuma ya pazia wamiliki wa benki hio watakuwa ni familiaya Rothchild.

Sasa Edna anapata kuelewa sasa namna ambavyo familia hii inasifiika kuliteka soko la fedha duniani, uwekezaji wao kwenye mataifa mengi siku zote haukuwa ule wa moja kwa moja, na hili limeifanya familia hii kutokuwa maarufu duniani na kuonekana kama familia ambayo haina umiliki mkubwa wa mali miaka ya hivi karibuni , lakini ukweli ni kwamba familia hii uwekezaji wao ni wa siri mno na ni watu wachache sana ambao wanaweza kuelewa ni kiasi gani kwa ujumla ambacho familia hii inamiliki.

“Masharti yako ni yapi?”Aliuliza Edna na Edward alitabasamu.

“Nahitaji asilimia ishirini na tano ya hisa za kampuni ya JR na baada ya hapo tutasaini ‘Stock Nominee Agreement’ hii itakupa fursa ya kuendelea kuwa na nguvu ndani ya kampuni ya JR licha ya kwamba utakuwa na umiliki wa asilimia 25 wa hisa”Aliongea Edward.

Stock Nominee Agreement ni kitendo ambacho mtu anakubali kumiliki hisa kwa niaba ya mtu mwingine na kufanya maamuzi yote yanayohusiana na hisa hizo, sasa mkataba wa aina hio una sababu nyingi na moja wapo huenda mmiliki wa hisa hataki kujulikana hivyo anampa mtu mwingine uhalali wa kusimamia hisa kwa niaba yake , sasa hiko ndio alichokuwa akitaka kufanya Edward , yaani asilimia 25 za hisa Edward azinunue kwa pesa taslimu halafu Edna kuendelea kumiliki hisa hizo kwa niaba ya familia hio ya Rothchild, kwahio Edna atabakia na hisa ishirini na tano na muda huo huo atakuwa pia na maamuzi ya hisa 25 za familia ya Rothchild .

“Nakubali lakini kwa sharti moja”Aliongea Edna na kumfanya Edward kutabasamu , hakuamini mazungumzo yake yamekuwa marahisi hivyo.

“Nipo tayari kukuuzia asilimia 24 pekee sio ishirini na tano”Aliongea Edna na Edward alifikiria kidogo huku akimwangalia Profesa Clark.

“Thank you Miss Edna , Then its Deal”Aliongea Edward na Edna alitingisha kichwa na kisha alisimama na kupeana mkono na Edward na makubaliano yakawa hivyo , Edna kuuza asilimia ishirini na nne ya hiza za kampuni wakati huo huo akiendelea kumiliki hisa hizo kwa niaba ya familia ya Rothchild.

“Ni wakati gani napaswa kuonana na huyo mmiliki wa kampuni ya Aba , maana baada ya hapa nina kikao , kwa maelezo yenu nadhani swala la kwanza ni kuonana nae”Aliongea Edna.

“Actually Miss Edna mmiliki wa kampuni ya Aba yupo hapahapa hotelini ni mmiliki wa hii hoteli ya Yams lakini pia ni mpishi ndani ya hii hoteli pamoja na baadhi ya migahawa na wiki hii yote anahudumu ndani ya hii hoteli”Aliongea Edward na kumfanya Edna kushangaa na kabla mshangao haujamalizika , alionekana mwanaume ambaye amevalia sare za jikoni akiwasogelea huku akiwa ameshikilia mkononi Wine.

“Persephone hii ni zawadi yangu kwako”Aliongea yule mwanaume na kumfanya Edna kumwangalia kwa kumshangaa, na kilichomfanya kumshangaa ni kwamba mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa akimfahamu kama moja ya mpishi namba moja duniani kwa Zaidi ya miaka mitano mfululizo, Mr Alfin Kelphin ndio jina lake huyo mwanaume aliekuwa mbele yake, kitu cha pili ambacho kilimfanya Edna kushangaa ni mpishi huyo kumuita kwa jina la Persephone, jina ambalo watu walikuwa wakimwita licha ya kwamba hakua akijua undani Zaidi wa jina hilo.

Profesa Clark pia alionekana kumkumbuka mwanaume aliekuwa mbele yake , kwani siku kadhaa nyuma aliweza kugongana nae ndani ya mgahawa wa Ling Sichuan, ila kwa ProfesaClark alionekana kuwa wa kawaida tu , licha ya kwamba Mr Kelphin kuwa mtu maarufu.

“Princess Clark we meet again”Aliongea Mr Kelphin huku akimwangalia Profesa Clark usoni kwa tabasamu na Profesa Clark hakuongea Zaidi ya kuinamisha kichwa akikubali kwamba wanakutana kwa mara ya pili, Profesa Clark alionyesha kama mtu ambaye hakupendezwa sana na mwonekano wa Mr Kelphin.

Sasa usisahau kwamba huyu Mr Kelphin ndio Poseidon na ndio maana alikuwa akimfahamu Ednakwa jina la Persephone..

Edna alipokea zawadi ya chupa ya mvinyo mweupe yenye chata la Chetau Lafite ya mwaka 1869, Edna aliangalia jina la Mvinyo hio na kujikuta akishangaa kwani hakuwa mgeni na ‘Brand’ hio ya Wine.

“Chetau Lafite , it’s one of the most expensive wines in our Celler’s , Mr Kelphin I see that you have made an Effort to choose a gift for Miss Edna to match her”

“Chetau Lafite , ni moja ya mvinyo wa bei ghali sana ambao uppo kwenye hifadhi yetu, Mr Kelphin naona umeweka juhudi kubwa kwenye kuchagua zawadi ambayo inaendana na Miss Edna”Aliongea Edward na kumfanya Kelphin kutabasamu na kisha kuvuta kiti na kuketi.

“The best Gift comes from the heart not Store , Miss Persephone , I am honered to meet you for the first time , you may be surprised but Hades is a very good friend of mine”

“Zawadi njema inatoka moyoni sio kutoka kwenye Akiba, Miss Peresphone imekuwa heshima kwangu kukutana na wewe kwa mara ya kwanza , unaweza ukashangaa lakini Hades ni rafiki yangu mwema”Aliongea Mr Kelphin huku akiweka tabasamu la kigentleman mbele ya Edna.

Sasa Edna baada ya kusikia jina la ‘Hades’ alikumbuka Roma ndio aliekuwa akiitwa kwa jina hilo.

“Nafurahi pia kukutana na mtu uliejijengea heshima kwenye kwenye jamii katika maswala ya mapishi, mimi pia ni moja ya wafuasi wako na imekuwa heshima kupokea zawadi hii kutoka kwako”Aliongea Edna na kumfanya Kelphin kutabasamu.

Baada ya maongezi ya dakika chache, hatimae mazungumzo ya kibiashara yalianza haraka kwani Edna alikuwa na kikao na kampuni ya Yamakuza pamoja na Maple.

Sasa katika mazungumzo hayo ilionekana kila kitu kilikwisha kumalizwa na Edward pamoja na Mr Kelphin na kilichokuwa kikiongelewa ni mikakati ya kumaliza mgogoro uliokuwepo.

*******

Nasra ilibidi kudanganya mara baada ya mama yake kuwauliza yeye na Roma juu ya siku gani wanatarajia kufunga ndoa , ukweli Nasra aliamini Roma hawezi kumuoa kwani alishamuoa tayari Edna, hivyo hakuwahi kufikiria swala la ndoa, hivyo ilionekana alikuwa amejiandaa namna ya kujibu swali hilo mara pale mama yake atakapo uliza..

Mama yake Nasra alionekana kumkubali Roma kwa asilimia mia moja , kwanza anamkataaje kwa mfano , kwani licha ya Roma kuonekana kuvalia kawaida , lakini alionekana kuwa ni mwenye pesa nyingi , ukizingatia pia kijijjini wengi wanaamini watu wanaotoka mjini mara zote wanakuwa na pesa , hivyo ilikuwa moja ya sababu ya mama yake Nasra kumkubali.

Usiku Roma alilala peke yake akimpisha Nasra kulala na mama yake ili kupata wasaa wa kuongea ukijumlisha kwamba hawakua wameoanana muda mrefu , lakini pia siku ambayo inafuata iliwapasa kurejea jijini Dar ss Salaam.

Licha ya kwamba mama yake na Nasra alikuwa akiishi kijijini ila alikuwa akielewa namna ambavyo Nasra aliweza kufadhiliwa na familia ya Edna, hivyo mama Nasra alijihisi pia ni mtu mwenye deni na familia ya Edna na alipanga siku moja Kwenda mjini kwa ajili ya kuonana na Edna ili kushukuru kwa kile familia hio ilichofanya kwa mtoto wake mpaka kufikia mafanikio aliokuwa nayo.

“Mama twende ukaishi na mimi mjini?”Aliongea Nasra na kumfanya mama yake kufikiria kidogo.

“Lakini Nasra tushajenga , unafikiri hii nyumba tutamwachia nani?”

“Tunaweza kuipangisha, naamini hatuwezi kukosa mpangaji ukizingatia nyumba hii ipo karibu na Shule, tunaweza kuwapangisha walimu”

“Hilo linawezekana kweli , kwani washawahi pia kuja kuomba kupanga hapa, lakini wazo la Kwenda kuishi Dar sikuwahi kulifikiria, sidhani pia kama litakuwa jambo zuri kwani ndio unakaribia kuolewa hivyo mwanangu”Aliongea Mama yake Nasra na kumfanya Nasra kuvuta pumzi.

“Ni sawa mama , lakini kutokana na majukumu yangu nashindwa kuja huku mara kwa mara , lakini pia sipendezwi kabisa na tabia za baba nataka uachane na Maisha haya yote ya manyanyaso na ukaishi na mimi”

“Nipe muda mwanangu nitafikiria , naweza pia hata kuja kukaa miezi kadhaa ukishaolewa narudi hapa kijijini , nishapazoea kuondoka ni vigumu”Aliongea na kumfanya Nasra kukubaluana nae.

Baada ya siku kupita saa sita kamili ndio Roma na Nasra walianza safari ya kurudi jijini Dar , huku Nasra akiahidiana na mama yake kuja baada ya wiki moja kupita , kumtembelea .

Upande wa Roma licha ya kwamba alionekana wa kawaida , lakini alikuwa akikumbuka maneno ya yule mwanamke ambaye alikutana nae njiani , lakini pia alikuwa akikumbuka jambo ambalo lilikuwa likimsumbua mama yake , hivyo shauku yake ya kutaka kujua kile kinachoendelea kuwa kubwa Zaidi.

“Nimemmisi sana Najma”Aliongea Nasra wakati wakiwa wanapita Msata na Roma alimwangalia na kutabasamu kidogo.

“Najma amejaliwa roho nzuri sana , hakukusaidia wewe tu , mimi pia alinisaidia nilivyofika hapa jijini”

“Ungekuwa unajali juhudi zake angalau usingemuacha akaenda masomoni kinyonge”Aliongea Nasra na kumfanya Roma kumwangalia Nasra kwa mshangao.

“Unamaanisha nini Kwenda masomoni kinyonge?”

“Inamaana haufahamu kama Njma alienda masomoni Marekani kwa ufadhili wa mke wako?”Aliuliza Nasra na kumfanya Roma kupunguza mwendo wa gari , Habari hio ilikuwa mpya kwake kabisa.
 
SEHEMU YA 327

Kwa jinsi Roma alivyoshangaa ilimfanya Nasra kuamini Roma hakuwa na taarifa za Edna kumfadhili Najma Kwenda masomoni nchini Marekani.

Na hio ilikuwa kweli kabisa , baada ya Roma siku ile kufahamu matibabu ya Juma yalifadhiliwa na mke wake hakuendelea kufatilia kabisa maendeleo ya Juma lakini pia kwa Najma vile vile , moja ya sababu ambayo ilimfanya kutotaka kuwa na ukaribu wa mara kwa mara na Najma ni juu ya hisia zake , aliamini kukaa mbali na msichana huyo ndio kumsaidia.

Sasa Roma hakufahamu kama Najma alikuwa amekwisha Kwenda masomini nchini Marekani, jambo hili lilimshangaza sana mara baada ya kufahamu mke wake ndio aliefanikisha hilo.

“Unataka kuniambia Edna mke wangu kafadhili masomo ya Najma bila sababu?”Aliuliza Roma.

“Siwezi kufahamu , ila ninachohisia nadhani kuna makubaliano yaliofanyika kati ya Najma na Edna , maana kutokana na yaliotokea ni ngumu kwa Edna kutoa kiasi cha pesa kwa ajili ya matibabu ya Juma na wakati huo huo kumepekea Nasra masomoni”Aliongea Nasra na Roma aliona ni kweli huenda kuna jambo ambalo mke wake alikubaliana na Najma na alijiambia atakuja kufahamu tu , aliamini sana katika kumtendea mtu wema , lakinisiku zote wema ukizidu huibua mashaka na ndicho ambacho alihisi.

Roma baada ya kumfikisha Nasra nyumbani kwake, moja kwa moja alichukua uelekeo wa Kwenda nyumbani na ndani ya nusu saa tu alikuwa ashafika na kuingiza gari ndani mara baada ya kufunguliwa na Derick.s

Nyumba ilionekana kutulia kuliko isivyokuwa kawaida na muda ambao Roma alikuwa akiingia hapo ndani ilikuwa imetimia saa kumi na moja za jioni.

Roma baada ya kuingia ndani , eneo la Sebuleni aliweza kukutana na Bi Wema , ambaye alionekana alishatambua uijio wake kwani alimlaki kusalimiana nae.

“Bi Wema Lanlan yupo wapi?”.

“Miss Mage , alikuja na kumchukua na kumpeleka kuangalia Wanyama , wametoka tokea asubuhi pamoja na Qiang”

Roma baada ya kusikia jina la Mage , alikumbuka hakuwa ameonana na huyo mrembo Polisi kwa siku kadhaa tokea mara ya mwisho kukutana kutokana na tukio la Salah, licha ya kwamba waliishi wakiwa majirani.

Ukweli Roma muda mwingine alijihisi ni kama mkatili kwani alikuwa na wanawake wengi lakini hakuwahi hata mara moja kuanza kuwatafuta hata kwa kuwatumia jumbe za meseji.

Roma alinyoosha moja kwa moja mpaka ndani kwake na kuweka mwili wake sawa kwa kuoga na kubadili nguo na alivyomaliza alichukua simu yake na kutafuta namba ya Tanya , huku dhumuni lake lilikuwa ni kuafahamu kile kilichokuwa kikiendelea ndani ya Hongkong.

Roma baada ya kuongea na simu kwa madakika kadhaa na kupewa taariufa ambazo zilimridhisha alijitupia kitandani na muda aliokuja kushituka ilikuwa ni usiku wa saa moja , alipiga mswaki na baada tu ya kumaliza alishuka mpaka sebuleni.

“Ankoo.!!”Aliita Lanlan na kumkimbilia, Roma alitabasamu na kumbeba Lanlan juu juu.

“Chubi umeshinda wapi siku nzima?”

“Aunt Mage alinipeleka kuona Wanyama, nimeona Simba , Twiga na na Manyani”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu na kushindwa kuelewa kwanini Lanlan alikuwa akipenda kuona Wanyama kwa kiasi kikubwa , Roma alimwangalia Mage aliekuwa ameketi kwenye sofa akimwangalia kwa macho yenye kuonyesha alikuwa na mambo mengi yanapita kichwani kwake.

“Baba na mwana”Aliongea Mage na Roma alitabasamu huku akimkagua mrembo huyo.

“Tumependezana sio?”

“Hakika, ukiwa na mtoto kama hivyo unaonekana kuwa mtu mzima Zaidi na upo siriasis na Maisha.”Aliongea Mage na Bi Wema alichangia na yeye, lakini Roma kwa namna flani hivi aliona Mage amemtupia na dongo. Hasa hapo kwenye kuwa siriasi na Maisha.

Kwa jinsi ilivyoonekana ni kama Mage alisuburia Edna asafiri, kwani Roma baada ya kuketi kwenye masofa Mage alisema anaenda kusaidiana na Bi Wema kuandaa chakula.

“Bi Wema halafu sijamuona Mama”Aliongea Roma,ukweli aliamini mama yake atakuwa yupo nyumbani kwa baba yake , kwani hapakuwa mbali , lakini aliona aulize.

“Kaenda nyumbani kusalimia ila ameahidi anarudi kabla ya chakula cha usiku”Aliongea Bi Wema na Roma alitingisha kichwa kuelewa.

Mage aliekuwa jikoni alijitahidi sana kujipikisha, alitaka kuchukua pointi mbele ya mwanaume anaempenda, yaani Roma na ndio maana wakati anafika hapo asubuhi yake alikuwa amebeba mahitaji maalumu ya kupikia na hata Bi Wema alipofika jikoni alisaidia vitu vichache tu na kumuacha Mage kuendelea mwenyewe.

Saa moja kama na nusu alianza kurudi Yezi . akafuatia Sophia ambaye alitoka kumsalimia babu yake na kabla hata ya wanafamilia hao hawajakaa mezani aliingia Blandina ambaye alionekana kuchoka mno licha ya kwamba ametoka nyumbani kwao ,Roma kwajinsi alivyomuona mama yake , alimuonea huruma.

Juhudi za Mage zilionekana kuzaa matunda kwani kila mmoja alifurahia chakula mno , akiwemo Lanlan na Roma ambao walikua Zaidi ya robo tatu ya chakula chote.

Baada ya kumaliza kula Roma ndio aliechuua jukumu la kumsindikiza Mage , sasa wakati Mage anatoka hapo ndani, huku nyuma Blandina alikuwa na wasiwasi mno , aliona kila dalili ya Mage kuwa na ukaribu wa Zaidi , kiasi ambacho kwa umri wake huo aliamini wawili hao walikuwa kwenye mapenzi , sasa mama huyu jambo hilo lilimchanganya na kujiuliza Roma alikuwa akielewa anachokifanya au tamaa zimemzidi kupitiliza , maana alishindwa kuelewa mwisho wake utakuaje na kuna muda aliona huenda yote hayo yanatokea kutokana na mazingira ambayo Roma amekulia.

Baada kama nusu saa kupita hatimae Roma aliweza kurudi nyumbani na ile anakaribia kuingia mlango mkubwa , Mama yake Blandina aliekuwa ameketi eneo la bustanini alimwita.

Kwasababu Roma ndio kwanza alikuwa amerudi kutoka safarini , ilibidi kumuelezea mama yake juu ya safari yake ya Kwenda kijijini na Roma alimuelezea namna ambavyo amepokelewa.

“Roma mwanangu unataka kuoa mke wa pili? , maana bado sijaelewa mpaka sasa mipango yako”

“Mke wa pili siwezi kuoa mama , tayari Edna ni mke wangu”

“Sasa kama hutaki kuoa mke wa pili imekuwaje ukaenda kujitambulisha nyumbani kwa Nasra ,kama huna nia ya kumuoa?”

“Nasra atabakia kuwa mwanamke wangu tu mama , ila kuhusu ndoa Hapana na uzuri licha ya kwamba sitaki kumpoteza mwanamke yoyote ambaye nipo nae kwenye mahusiano , lakini kama kuna atakae fanya maamuzi ya kuniacha kwa hiari yake basi siwezi kumng’ang’ania abaki kwangu ilihali siwezi kumtimizia kile anachotaka, ila kama wataendelea na mimi kwa mapenzi yao basi siwezi kuwaacha”Aliongea Roma na kumfanya Blandina kuvuta pumzi kwa nguvu na kuzishusha maana mpaka hapo aliona kuna kazi kubwa sana, kwanza hakukuwa na mapenzi ya karibu kati ya Roma na Edna , lakini baada ya mwanae kutatua tatizo la umbali uliokuwepo na mke wake yeye anaongeza wanawake mpaka Kwenda kujitambulisha , lakini licha ya hivyo alishindwa kabisa kuingizia neno.

“Na huyu Mage pia una mahusiano nae?” Roma alijikuta akikuna kichwa kutokana na swali hilo la mama yake , ukweli alikuwa akijionea aibu muda mwingine.

“Naweza pia kusema hivyo mama”.

“Roma mimi naamini unaelewa unachokifanya na sitaki sana kukuingilia kwenye maswala yako ya kimahusiano , lakini wasiwasi wangu upo kwa Edna”

“Mama kuhusu Edna , hilo lisikuumize kichwa sana , Edna ni mke wangu na siku zote atabakia kuwa mke wangu na naamini kuna sababu kubwa ya Edna kuwa mke wangu , mpaka sasa tumefikia hatua ambayo siamini kama Edna anaweza kunikatia tamaa na kuniacha”Aliongea na kumfanya Blandina kumwangalia Roma na kisha aligeuza uso wake na kuangalia maji.

“Ni Vyema kama anagalau unamjua mkeo, ila unachopaswa pia kuelewa sisi wanawake tunazo tabia ambazo tunafaana kwa asilimia kubwa , unaweza ukamuona Edna katulia lakini itafikia kipindi anaweza kuchoka na kuchukua maamuzi magumu”Aliongea Blandina na Roma aliona mama yake ana pointi ya msingi , lakini hata hivyo hakuwa na chakufanya , kama kweli Edna atachukua hayo maamuzi magumu kwa sababu ya wanawake aliokuwa nao basi aliona atakuwa kwenye hali ambayo hataweza kuwa na chaguzi ya aidha kumuacha Edna au kuwaacha wanawake wengine.

“Mama nadhani ni muda sasa wa kunieleza kile ambacho kinakusumbua , unaonekana kupauka kwa mawazo mama yangu”Aliongea Roma.

“Jumapili iliopita nilivyoenda kituoni niliweza kukutana na Raisi Kamau pamoja na Raisi Jeremy”Aliongea Blandina kwa unyonge na kumfanya Roma kushangaa.

“Wote wawili kwa pamoja , walikuwa wakihitaji nini?”Aliuliza Roma na Blandina alivuta pumzi nyingi akijiandaa kuongea.

********

“Miss Edna nitoe shuktani zangu za dhati kabisa kwa kuweza kufanya swala hili ambalo lilikuwa likituumiza kichwa kumalizika kwa urahisi , kama sio wewe huenda kungekuwa na mvutano mkubwa sana”Aliongea Tikayi mara baada ya kikao cha pamoja kumalizika na kufikia kwenye makubaliano , huku katika maongezi hayo Edna akionekana ndio aliekuwa kinara kusuluhisha swala hili la mgogoro ya kimaslahi na kampuni ya Aba.

Ukweli licha ya kwamba Edna aliweza kumaliza mgogoro huo , lakini aliona ni kama hakuwa amefanya kitu kabisa , kwani kila kitu kimetokea kutokana na yeye kuwa na cheo cha Persephone yaani mke wa Hades

Swala la mgogoro huo kama sio konekesheni , basi lingechukua sura mpya na kupelekea mauzo ya hisa za kampuni yake kushuka kwa kiasi kikubwa jambo ambalo hakuwa tayari kabisa kuona likitokea hata kidogo , kwani alikuwa na mipango mingi sana na kampuni yake, hivyo vikwazo vikubwa kama hivyo hakutaka kabisa vimkwamishe kufikia malengo aliojiwekea.

Kilichofanyika ilikuwa rahisi sana , Edward aliweza kutumia ushawishi wake kumtumia Mr Kelphin kumaliza swala hilo , Kelphin alishindwa kukataa na hio ni kutokana na kwamba , licha ya Ye Chen na Morri kushirikiana kugundua hio teknolojia ya material mapya , lakini kutokana na mkataba ambao walisaini wanasayansi hayo na taasisi ya utafiti ya Yamakuza , ulikuwa ikionyesha asilimia arobaini ya umiliki wa teknolojia huo upo chini ya kampuni huku wagunduzi wakiwa na aslimia therathini kwa kila mmoja, hivyo kitendo cha Ye Chen Kwenda kuuza teknolojia hio kwa kampuni ya Aba , lilikuwa ni swala la ukiukwaji wa vipengele vya kimkataba , licha ya kwamba Ye Chen alishavunja mkataba na tasisi ya Yamakuza kabla ya kuhamia Aba.

Sasa kilchofanyika sio kwamba Yamakuza wangeshindwa kesi kutokana na Ushahidi uliokuwepo , lakini ambacho hawakutaka kama kampuni ni uchelewashwaji wa uzinduzi wa material hayo ,kwani terehe ilikwisha tolewa tayari na mikataba mingi na makampuni ilikwisha kusainiwa , hivyo kama kesi hio ingeendelea kusikilizwa katika mahakama ya kimataifa Usuluhishi , ingechukua Zaidi ya miezi sita mpaka kukamilika, jambo ambalo lingepelekea hasara Zaidi, na ndio maana hatua ya kuyamaliza maswala hayo kibiashara ilikuwa busara kuyamaliza chini kwa chini.

Edna akibakia na asilimia zake zilezile za faida kama awali ,lakini upande wa kampuni ya Yamakuza wakipata hasara ya asilimia kumi kama fidia ya Kwenda kwa Ye chen ambaye alishikiri katika ugunduzi , lakini wakati huo huo na Mori akiingia hasara ya kutoa fidia ya asilimia kumi Kwenda kwa Ye Chen kwa makubaliano yaliofkiwa.

Kilicho msaidia Edna pamoja na kampuni ya Maple kutoingia hasara ni kutokana na kwamba mkataba wao ulikuwa ni wa usambazaji na Marketing pekee , bali sio wa umiliki wa teknolojia, hivyo mgogoro ulikuwa ukiwagusa Yamakuza moja kwa moja , huku yeye na kampuni yake wakiguswa kwa njia isiokuwa ya moja kwa moja.

Ni muda wa usiku sasa ,Edna alikuwa ndani ya chumba chake akiwa amesimama akiangalia upande wa nje wa jiji hili la Hongkong huku mkononi akiwa ameshikilia bangiri ambayo alipatiwa siku mbili zilizopita na babu yake Roma.

Edna alionekana kuwaza mambo mengi kwa wakati mmoja , lakini kubwa Zaidi ni juu ya yeye pamoja na Roma, mawazo yake yalimfanya mpaka kugeuka na kuangalia chupa ya Mvinyo ambayo alikuwa ameiweka Mezani, Chupa ambayo alikuwa amepewa kama zawadi na Mr Kelphin , zawadi ambayo gharama yake kwa haraka haraka ni Zaidi ya milioni mia nne za kitanzania, sasa Edna hakuwa mjinga kwa mtu mzito kama Kelphin mwenye hadhi yake kwenye jamii kumpa zawadi kubwa ya namna hio , aliamini urafiki uliokuwepo baina ya Roma na Mr Kelphin ulikuwa mkubwa mno na hilo ndio lilimfikirisha , lakini pia pamoja na maswala yake ya kibiashara yalivvyokuwa rahisi kwa msaada wa familia ya Rothchild.

Alitoka dirishani na kutembea mpaka kwenye meza ya kioo na kisha kunyanyua ile chupa ya mvinyo na kuiangalia kama mtu ambaye alikuwa akiishangaa, lakini katika hali ya kushangaza , ghafla Edna alijikuta akirudisha ile chupa chini haraka sana kama vile ilikuwa ya moto huku akianza kutetemeka akiwa ameshikilia kichwa , hali ile iliendelea kwa dakika kama nne hivi ..

“Aarrggg….!!!”Edna alijikuta akishika kichwa huku akionekana kupitia maumivu makali sana ya kichwa lakini wakati huo huo matukio ambayo hayakueleweka kwenye kichwa chake kuanza kupita kwa kasi , alikuwa kama mtu ambaye alipoteza kumbukumbu na sasa zinaanza kurejea upya na katika picha hizo mchanganyiko za matukio moja wapo ni mwanaume anaefanana na Mr Kelphin kumpatia chupa ya Mvinyo hio hivo iliokuwepo hapo ndani kwake ,yaani tukio la siku hio ni kama lilishawahi kumtokea katika Maisha yake na siku hio limejirudia upya , sasa kumbukumbu hizo zinamfanya kupitia maumivu makali mno ya kichwa.

“Mamaaa…!!!!”

“Puuus!!!”Edna alijikuta akidondoka chini palepale na kutua kwenye zuria na kupoteza fahamu
 
SEHEMU YA 328

Edna alikuja kushituka ikiwa ni usiku kabisa muda wa saa mbili , akiwa amelala kwenye zuria la manyoya, mrembo huyu alijinyanyua kivivu na kukaa kitandani huku taulo alilovalia kuusaliti mwili wake,.

Hakuelewa ni nini kimemsababishia kuuma kwa kichwa ,katika akili yake hakuweza tena kukumbuka kumbukumbu ambazo zilikuwa zikipita kwenye kichwa chake , alichokumbuka muda huo ni maumivu makali ya kichwa ya ghalfa , maumivu ambayo muda huo hakuwa akiyahisi kabisa , ni kama hakukuwa kumetokea kitu.

Siku iliofuata Edna aliweza kukutana na Edward na wakasainishana mkataba wa maswala ya uwekezaji ndani nya kampuni ya JR Group , Edna alikuwa na haki kisheria ya kufanya maamuzi kwa niaba ya JR kutokana na kwmaba alikuwa ni Mwenyekiti ndani ya bodi ya wakurugezi , hivyo licha ya kwamba maamuzi ya kiutendaji ya kampuni yalikuwa yakifanywa na Matrida , lakini kuhusu maswala ya uwekezaji pamoja na maswala ya hisa , yote yalikuwa yakifanywa na mwenyekiti.

Asilimia ishirini na nne za hisa zilikuwa na thamani ya dola bilioni moja na nusu, ukweli tokea kampuni ya JR Group kuwa kwenye mikono ya Matilda, hisa zake zilipanda kwa kiasi kikubwa mno , hela ambayo Edna alitumia kununulia hisa za kampuni hio ilikuwa ndogo kulingana na thamani ya hisa za kampuni hio kwa soko la siku hio, hivyo unaweza kusema kwamba alikuwa ametengeneza faida mara mbili kwa hela ambayo aliingiza ndani ya kampuni ya JR.

“Miss Edna ni jambo jema sana kwasisi kufanya kazi kwa pamoja katika maswala ya kibiashara , ijapokuwa nina uhusiano wa karibu na Mr Roma , lakini uhusiano wa moja kwa moja kati ya familia yetu na wewe kama mfanyabiashara ni jambo ambalo ni la faida sana kwa kampuni yako na nikukaribishe muda wowote kuwekeza ndani ya Uingereza”Aliongea Edward mara baada ya kukamilisha utiaji Saini wa mkataba huo.

“Nashukuru sana Mr Edward ni heshima kwangu pia kupata nafasi ya kuwa karibu na familia yako”Aliongea Edna na walipeana mikono na kisha wakaagana na kinachobakia sasa ni kwa upande wa Edna kufanya kikao na bodi ya wakurugenzi wa makampuni ya JR ili kuweka mkakati wa uanzishwaji wa benki ya kibiasara ndani ya Tanzania.

*******

Upande wa Tanzania ilikuwa ni usiku , Roma na mama yake walikuwa eneo la bustanini wakiendeleza maongezi yao.

Roma alipata kusikiliza maelezo yote ya kile kilichotokea siku ya Jumapili na mpaka mama yake anatia nukta katika maelezo yake , sasa alipata kuelewa kwanini mama yake alikuwa akionekana kuwa katika hali ya mawazo.

Katika maelezo ya mama yake kuna kitu alihisi hakipo sawa kabisa , alijiuliza kwanini wazee hao ghafla tu wakapatana na wakaamua kusapotiana na kumtaka mama yake kurudi nchini Kenya ,Roma aliamini huenda kuna jambo ambalo linaendelea ambalo hakuwa akilifahamu , lakini kwa wakati huo aliamini jambo moja la kwanza katika hatua yakumsaidia mama yake , ni kuhakikisha vituo vyote alivyojenga mama yake vinaendelea kuendeshwa bila ya kuingiliwa na maswala ya kisiasa, yaani kusiwe na mamlaka yoyote kutoka serikalini ambayo wanaweza kuingilia utendaji kazi wa viuto hivyo.

“Mama hili swala hukupaswa likusumbue kabisa kichwa wakati nipo , nakuahidi hakuna mtu yoyote ambaye ana uwezo wa kukutoa kwenye himaya yangu tena , nitakulinda kwa kadri ya uwezo wangu, hivyo hao wazee wape jibu lao, huondoki hapa Tanzania kwa namna yoyote ile”Aliongea Roma kwa msisitizo.

“Wasiwasi wangu Roma nijuu ya hivi vituo, kwangu vile vituo ni ibada ambayo nilinuia kuendelea nayo mpaka roho itakapoacha mwili wangu katika uso wa hii dunia”Aliongea.

“Mama niamini mimi hakuna mtu wa kukugusa , nikisema wa kukugusa namaanisha kwamba hakuna mtu wa kukugusa kimwili mpaka kiroho, umesema vituo hivyo ni kama ibada kwako basi swala hili liko upande wako wa kiroho , hivyo nitalishughulikia na unapaswa kua na amani mama yangu”Aliongea Roma na kisha alimtoa mama yake kutoka kwenye bustani na wakaelekea ndani , ijapokuwa Blandina aliamua kumwamini Roma , lakini hakuwa akijua ni kwa namna gani ambavyo Roma anakwenda kumsaidia katika swala lake.

Ukweli ni kwamba Blandina alikuwa nyumbani kwao mchana wote akimuomba msaada baba yake kumsaidia katika swala hilo , lakini licha ya kuomba kwa mzee huyo hakukuwa na msaada wowote, Zaidi ya mzee huyo kumwambia kwamba arudi nchini Kenya kama ilivyopendekezwa au akamueleze swala hilo Roma mtoto wake kwani anayo nguvu ya kumsaidia.

Na ikumbukwe kwamba Mzee Atanasi na Afande Kweka siku zote walikuwa wakimtaka Blandina kurudi nchini Kenya , lakini Blandina alikuwa anagoma kufanya hivyo.

Sasa Blandina baada ya kuona hakuwa na msaada na mtu wa kumshirikisha swala lake ndipo alipopanga kumuelezea Roma , ijapokuwa hakutaka kumpa mzigo mtoto wake , lakini aliamini kuwa muwazi ndio jambo la busara zaidi kufanya kwa wakati huo, hakupenda kufanya maamuzi ambayo mwisho wa siku yaka uweka uhusiano wake yeye na mwanae kuporomoka.

Upande wa Roma hakutaka kwanza kukurupuka kutatua swala ambalo mama yake amemuambia , ukweli ni kwamba alikuwa na njia nyingi sana ya kudili na swala hilo kwa mfano alijiambia ana uwezo wa kutumia ubabe wake , lakini kwa wakati huo usiku alitaka kwanza kupima ni njia ipi sahihi ya kulitatua swala hilo , lakini wakati huo huo alipanga kufahamu ni nini ambacho kinaendelea mpaka maraisi hao ambao alitegemea kuendelea kuwa na bifu kuungana na kumtaka mama yake kurudi Kenya.

Roma baada ya kuwaza hatimae aliweza kumkumbuka Christine , aliamini Christine pekee ndio ambaye ana uwezo wa kutatua swala hili kwa kutumia koneksheni zake na hio ni kutokana na kwamba Christine au Aphrodite alikuwa na nguvu sana ndani ya serikali ya Marekani na alikuwa sehemu ya Deep State ndani ya nchi hio , licha ya kwamba Christine alikuwa akifahamika kama mwanamuziki , lakini vitengo vya siri vya taifa la Marekani vilikuwa vikimtambua Christine kama moja ya miungu kumi na mbili hivyo alikuwa na heshima yake.

Roma aliweka swala hilo kiporo kwanza kwa usiku huo , alijiambia kukishakucha ataenda hotelini kwa Christine na kuzungumza nae kwa ajili ya hilo swala , lakini pia kuzungumza nae maswala ya kampuni ya Vexto Media , Roma hakuwa amesahau kwamba alikuwa na jukumu la kumshawishi Christine kukubaliana na yeye kufanya ‘Interview’ kwa kutumia TV yao mpya ambayo wanatarajia kuizindua hivi karibuni kabla ya mashindano ya kuibua vipaji hayajaanza , Roma alipanga kwenye kichwa chake kuhakikisha kampuni ya Vexto media inafanya vizuri ili kumfanya mke wake Edna kufurahi.

Siku ya asubuhi , yaani Alhamisi baada ya kukamilisha taratibu za kifamilia moja kwa moja alifanya safari mpaka Mbezi Beach Maple Hoteli kwa ajili ya kuonana na Christine na hio ni baada ya kuwasiliana na Christine na kumwambia kwamba kama anahitaji kumuona amfuate yeye mwenyewe , na Roma hakutaka kuleta ubishi , kwakua yeye ndio aliekuwa na shida , ilibidi atii wito na kuanza safari ya kuelekea Mbezi Beacha Maple hotel.

Wakati akiwa safarini mawazo yake pia hayakuacha kumkumbuka Neema Luwazo kwani tokea amtibie Mzee Chino alifanya mawasiliano na yeye mara moja tu.

Ndani ta dakika arobaini tayari aliweza kuingiza gari yake ndani ya hoteli ya kisasa ya Maple hoteli , Hoteli hii ni moja ya hoteli nzuri sana ndani ya jiji la Dar es salaam , inaingia kwenye kumi ya hoteli bora Zaidi ndani ya Tanzania , yenyewe ikishika namba ya pili baada ya Serena Hoteli kwa hadhi ya kimataifa na ndio maana Christine alichagua hoteli hio.

Uwepo wa Christine ndani ya hoteli ya Maple ulikuwa ukifahamika kwa wafanyakazi wa hoteli hio pekee na kutokana na sheria zoa hoteli hio hakuna mfanyakazi ambaye alikuwa akiruhusiwa kutoa taarifa ya uwepo wa Star huyo nchini Tanzania.

Hivyo uwepo wa Christine Stewart ndani ya Tanzania hakukuwa ukifahamika licha ya kwamba alikuwa na Zaidi ya siku tano tokea kuwa hapa Tanzania.

“Nahitaji kuonana na mgeni chumba namba 87”Aliongea Roma mara baada ya kufika mapokezi na baada ya kutamka hayo maneno wahudumu wawili wa kike na mmoja wa kiume walianza kumwangalia Roma kwanzia juu mpaka chini , ni kama walikuwa wakimtathimini na kumpima kama alikuwa na hadhi ya kuonana na mgeni aliekuwa ndani ya chumba namba 67 , kwani mgeni wao alikuwa ni wa hadhi ya juu kiasi kwamba hata usalama wa hoteli hio uliimarishwa kwa kiwango kikubwa sana.

Roma baada ya kuona anaangaliwa sana na wahudumu hao kwanza ilibidi ajichunguze yeye mwenyewe kuona kama alikuwa na kasoro , lakini alivyojiangalia alijjiona kabisa yuko fiti na tatizo lilikuwa moja tu , alivalia kikawaida sana , shati la mikono mifupi la maua maua na suruali ya jeans.

“Samahani kaka una miadi nae?”Aliuliza yule mhudumu wa kike mmoja mwenye sura ya kirembo lakini hakujaliwa shepu.

“Nadhani kuna utaratibu wa kuwasiliana na mgeni na kuthibitisha ujio wangu , naitwa Roma Ramoni”Aliongea Roma na yule mfanyakazi alimpa ishara yule wa kiume kupiga simu chumba namba 87 na ndani ya dakika moja tu wale wahudumu waliinamisha vichwa vyao kwa heshima mbele ya Roma na kumruhusu Kwenda na Roma alitabasamu na kutembea kuelekea chumba hicho , huku akiacha wahudumu hao huku nyuma wakiangaliana na kujiuliza Roma ni nani mpaka akawa na miadi na mtu mzito kama Christine.

Christine ni kama alisubiria Roma akaribie ndio aende kuoga , kwani Roma ile anaingia ndani ya chumba hiko cha kifahari alimkuta mwanamke huyo akiwa uchi na alichoziba yalikuwa ni manyonyo tu.

Christine baada ya kumuona Roma ameingia , alijongea mpaka kwenye Dressing table na kukaa kiushawishi huku akichukua mafuta aina ya Lotion na kuendelea kujipaka kimadaha , sasa Roma ilibidi asimame kwanza aangalie vitendo cya huyu mwanamke , ukweli Roma mara baada ya kuambiwa aje ndani ya hoteli hio aliamini hilo ndio jambo ambalo angelikuta na matarajio yake hayakuwa mbali na kile alichofikiria , lakini hata hivyo , licha ya Christine kuwa na uzuri usiovumilika mbele ya mwanaume yoyote rijali alishaweka nadhiri kutotembea na mwanamke huyo kwa namna yoyote ile, na huo haukua mtego wa kwanza kwa Chrisitne kumuwekea Roma , mara nyingi Roma kila alipokuwa akienda Marekani lazima awekewe mitego ya aina mbalimbali na mrembo huyo lakini siku zote atakachokifanya Roma baada ya kupandishwa mzuka na Chrisitne ataenda kutafuta mwanamke mwingine na kufanya nae mapenzi ilimradi kupunguza munkali.

Upande wa Chrisitne ukweli alishindwa kuelewa ni kwanini Hades siku zote alikuwa akimuepuka , mrembo huyo tokea kifo cha mpenzi wake Hades wa Zamani kitokee , hakuwahi kufanya mapenzi na mwanaume yoyote yule , kwani wote walikuwa wa kawaida kwake na hawakua na hadhi ya kutembea nae , hivyo mtu pekee ambaye kwake alikuwa akimfaa , alikuwa ni Hades pakee , lakini licha ya mitego yake yote mbele ya Hades , hakuna siku ambayo mwanaume huyo alitoa mkuyenge wake na kuingiza kwenye sehemu zake za siri , Christine alijaribu kuuliza ni sababu gani ambayo inamfanya kutotaka kufanya nae mapenzi , lakini Hades hakuwa na majibu ya kueleweka ,swala ambalo lilimfanya Chrisinte kuumiaa, lakini licha ya hivyo hakukata tamaa hata siku moja , aliamini siku moja lazima Hades atafanya nae mapenzi.

“Christine nimekuja nina shida nataka unisaidie , unaonaje ukivaa vizuri kuliko kufanya vitendo ambavyo vinatesa hisia zangu”Aliongea Roma na Christine alimgeukia Roma na kumwangalia kwanzia juu na macho yake kuishia upande wa zipu ya suruali na baada ya kuona sehemu ile imetuna , alitabasamu na kisha alitoa kijitaulo ambacho kipo kwenye mwili wake na kisha akamsogelea Roma

Roma alijiambia moyoni haitokuja kutokea mwanaume akaweza kuchomoka kwenye mtego wa mwanamke kama Christine, kwani ana kila mbinu ya kumfanya mwanaume yoyote ndani ya dunia hii kufanya nae mapenzi , ikumbukwe mrembo huyu ameishi miaka mingi sana hapa duniani kwa sura tofauti tofauti , sasa katika sura zote ambazo ashawahi kuzivaa katika Maisha yake ni sura za wanawake maarufu sana ambao wameandikwa sana kwenye historia ya dunia na moja ya sura ambayo ashawahi kuishi nayo ni ya Princes wa Wales aliefahamika kwa jina la Diana
 
SEHEMU YA 329

Christine alifanya utundu wake wote kwa kutumia uzoefu wa Zaidi ya miaka 1000 yote alioweza kuishi hapa Duniani , lakini Roma hakuchukua hatua ya kumshughulikia mrembo huyo , kitendp ambacho kilimfanya Christine kukata tamaa na kuvaa taulo lake na kuketi kwenye Sofa.

“Hades ni lini utaniambia sababu ya wewe kunikataa , licha ya juhudi zangu nilizoweka miaka na miaka kukupata?”Aliuliza Chrisitne huku akiweka sura ambayo haikuonyesha hasira bali ilionyesha hali ya kukata tamaa.

“Hata kama nikikuelezea hutoweza kunielewa Christine , kuna sababu kubwa ya mimi sitaki kujihusisha na wewe na muda ukiwadia nitakueleza”Aliongea Roma huku akiketi kwenye sofa, huku jibu lake likionesha kutomridhisha mrembo huyu maarufu.

“Ni shida gani unataka msaada wangu , Hades nakudai fadhila nyingi sana na hujawahi kuchukua hatua ya kuzilipa hata siku moja”

“Unachozungumza ni sahihi, lakini Chrisitine ukumbuke sisi ni marafiki na hatuwezi kuhesabiana fadhila tunazofanyiana na ndio maana nimekuja hapa bila kufikiria kwasababu nina shida nataka unisaidie , Ofcourse sio kama nimekosa namna ya kutatua tatizo hili, ila kupitia wewe kwako linaweza kuisha haraka”

“Okey nielezee nione nakusaidia ama sikusaidii maana unanikera kwa kitendo chako cha kutotaka kunifanya , sijui unaniona mzee au nini”Aliongea Christine na kumfanya Roma kuelezea shida aliokuwa nayo mama yake na mpaka anamaliza Christine alitoa tabasamu la kejeli.

“Ninachoamini kuna nguvu kubwa myuma ya maraisi hawa wa Afrika Mashariki , ndio maana wanatumia kila mbinu za kumrudisha mama yangu Kwenda nchini Kenya”Alimalizia Roma.

“Kwahio unataka nikusaidie vipi hapo Hades?”

“Nataka unisaidie kutoa onyo kwa wahusika”Aliongea Roma na kumfanya Christine kucheka.

“Onyo Kwenda kwa nani Hades na nafahamu vipi wahusika”

“Christine swala hili naamini watu wa UNICEF wanahusika kwa kivuli cha umoja wa mataifa , hivyo naamini unaweza kunisaidia katika hili”

“Hades naweza kuongea na watu wa umoja wa mataifa lakini unachopaswa kuelewa sasa hivi sekretari anafikia mwisho wake na kuna hati hati mwaka huu kabla ya kuisha rekodi nyingine inaweza kutengenezwa”

“Rekodi gani?”

“Mwanamke wa kwanza kuwa General Secretary wa umoja wa mataifa na ninachodhania naomba kisije kuwa kweli”Aliongea Christine na kisha alinyoosha mkono na kuchukua chupa ya mvinyo na kujimiminia kwenye glass na kisha alikunja nne na kufanya mapaja yake alioyafunika na taulo kuonekana waziwazi, upande wa Roma alishindwa kumuelewa Christine anataka kumaanisha nini.

“Mbona unaongea kimafumbo , unadhania kitu gani?”Aliongea Roma na kumfanya Christine kutabasamu.

“Hades haya yote unashindwa kuyajua kutokana na tabia yako ya kutaka kujihusisha na siasa , lakini ninachokuambia siasa ya sasa ndio inatawala dunia , licha ya wanasiasa kutokuwa na mchango mkubwa kwenye jamii kama ilivyokuwa wanasayansi na wafanyabishara , lakini wanasiasa ndio kila kitu , nakushauri kwanzia sasa uanze kujiweka karibu na siasa”

“Siwezani kabisa na siasa na siwezi kujiingiza huko Christine kwasababbu nitavunja sheria zangu nilizojiwekea”

“Hades unajua tofauti kubwa iliokuwepo kati yako na Hades wa zamani?”

“Sijawahi kufatilia”

“Hata ungefuatilia usingeweza kumfahamu Hades kuliko ninavyomfahamu mimi, isitoshe ulifahamina nae kwa muda mfupi sana”

“Nielezee ni nini tofauti yangu na Hades”

“Hades alikuwa ni nusu mwanasiasa , kwa maneno marahsi alikuwa ni mtu ambaye ni ‘flexible’ kuliko ilivyo wewe na huenda ungekuwa kama Hades ungefanya juu chini Jiwe la Kimungu kutoruhusu litue kenye mikono ya Athena”.

“Jiwe la Kimungu linaingia vipi na mambo ya kisiasa?”

“You are King of underwold you should know this better than me and Hades you don’t know us completely even though you are considered to be among us”

“Wewe ndio mfalme wa ulimwengu wa wahalifu na unatakiwa kuelewa swala hili vizuri na Hades hufahamu kuhusu sisi kabisa ijapokuwa unazingatiwa kama mmoja wetu”

“Unachoongea Christine ni kweli sijui chochote kuhusu nyie na sitaki kufahamu ni siri ngapi mnazo, na hata nitake kujua naweza nisifanikiwe kwani tuna utofauti mkubwa sana , nyie mmeishi ndani ya dunia hii karne kwa karne , lakini jambo moja ninaamini kujifahamu mimi mwenyewe inatosha”Aliongea Roma na maneno yake yalimkumbusha mara ya mwisho alivyokuwa akipambana na Hades wa zamani, neno ambalo Hades wa zamani alimwambia ni kujifahamu yeye mwenyewe ni nani.

“Know yourself and you will save the world”

“Hades nitakusaidia kuhusu swala lako lakini kuna jambo moja tu ambalo nataka leo kukushauri na naomba ulizingatie sana”.

“Nakusikiliza Aphrodite”

“Don’t let Athena take the Godstone again and if it happens never trust us again”

“Usije ukamruhusu Athena kuchukua jiwe la Kimungu tena na kama itatokea usituamini tena”Aliongera Athena na kumfanya Roma kushangaa.

“Lakini nilishakueleza Athena amelichukua tayari inakuwaje kukawa na mara nyingine tena , sikuelewi Christine”

“Even I don’t understand but we believe in prophecy that was given many years ago and Athena is fighting against it to come true”

“Hata mimi sielewi, lakini tunaamini katika unabii uliotolewa miaka mingi iliopita na Athena anapigania unabii huo usitimie”Aliongea Christine.

“Ni Unabii gani uliotolewa?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“It will be either you or us , it will be the beginning to the new End or The End to the new beginning”

“Itakuwa ni wewe au ni sisi , itakuwa mwanzo Kwenda mwisho mpya au mwisho Kwenda mwanzo mpya”Aliongea Christine.

“Huo ndio unabii unaozungumzia?”

“Nimetamka kama ulivyoandikwa na kutabiriwa , maana yake Zaidi ni kwamba wote sisi tulikuwa tukitarajia kuzaliwa kwako kwasababu wewe unaweza ukawa mwisho wetu au mwanzo wetu, Dunia sasa imetulia kwasababu Athena hajaupata moyo wa Gaia na wewe ndio njia ya upatikanaji wa moyo huo”

“Moyo wa Gaia?” Aliuliza Roma , ukweli asubuhi hio mazungumzo hayo yalimfanya kushangaa Zaidi na zaidi.

“Ndio nadhani unafahamu ni nini kilichomtokea Zeus katika historia ya kale ambayo haikuwekwa wazi mpaka leo hii”

“Aliuliwa na majini”Alijibu Roma.

“Ndio Zeus aliuliwa na majini lakini kifo chake kilikuwa tayari kishatabiliwa na Cassandra na ndio huyo huyo ambaye alitabili Zeus atapoteza kitu cha thamani Zaidi kwetu”Aliongea

“Kitu cha Thamani ni kitu gani?”

“Moyo wa Gaia, aliekuwa akiumiliki ni Zeus na ulihifadhiwa kwenye Godstone na wakati Zeus alivyoanza safari ya Kwenda ulimwengu wa majini alificha jiwe hilo sehemu ambayo anaifahamu yeye peke yake , lakini bahati mbaya ndio akaja kuuliwa na hivyo jiwe hilo likapotea , lakini kutokana na unabii tunaamini uwepo wako katika kundi letu ndio njia pekee ya kufikia mahali ambapo Zeus ameficha jiwe hilo na hiko ndio anachokiamini Athena lakini na sisi pia na siku ambayo moyo wa Gaia(Godstone) ukafika kwenye mikono ya Athena itakuwa ni mwisho Kwenda mwanzo mpya , kama utaweza kumzuia Athena itakuwa ni mwanzo Kwenda mwisho mpya”Aliongea Christine na kumfanya Roma kushangaa.

“Kwahio mimi kupata cheo cha uungu ni jambo ambalo lilitabiliwa , kwanini sijawahi kusikia juu ya huu utabiri?”

“Ndio maana nikakuambia kwamba hujui chochote kuhusu sisi na nilichokuambia ni kama zawadi yangu kwako kama rafiki yako , hivyo kua makini Athena yupo nyuma yako akikufuatilia kwa kila unachokifanya kwasababu wewe ndio njia ya kumfanya kupata kile anachokitaka”Aliongea Christine na kumfanya Roma kuanza pia kukumbuka maneno ya yule mwanamke kule Lushoto.
 
SEHEMU YA 330.

Ni muda wa saa kumi za jioni Roma na Lanlan walionekana wakiwa ndani ya jengo laTerminal namba tatu , sehemu ya kusubiria wageni wanaowasili, uchangamfu wa Lanlan wakati akiongea na mjomba wake Roma Ramoni ulifanya baadhi ya watu waliofika kwa ajili ya kupokea wapendwa wao kuwaangalia kwa namna ya wivu , uzuri wa Lanlan ulifanya kuwa kivutio ndani ya eneo hilo.

“Anko Mama mbona hafiki , Lanlan amemmisi sana mama yake”Aliongea Lanlan kama kawaida yake na kumfanya Roma atabasamu , wakati huu Lanlan ameshikilia Ice Cream huku kila akiilamba macho yote yalielekea sehemu ya kutokea wageni.

“Chubi Anko pia amemisi mke wake na mke wangu ni wa kwangu peke yangu”

“Anko mimi sio Chubi na Mama ni wa Lanlan peke yake na mama anampenda Lanlan ndio maana atamletea zawadi”

“Lanlan unaonaje tukapinga, mama yako ananipenda mimi na ataniletea zawadi na wewe hakuletei”

“Mama yake Lanlan ataniletea zawadi na wewe Anko hakuletei”Alijibu Lanlan huku akipitisha kidole kwenye kidole cha Roma wakipinga.

“Mh kuna watu wanabahati jamani ,nitafurahije nikipata katoto kama kale”

“Hehe.. Suzy kwa mwonekano wako na mchumba wako Kibwengo hio ndoto ifute kwenye kichwa chako”

“Halafu Dorca usiniaze nishasema uache kumuita mpenzi wangu kwa jina la Kibwengo, unapenda kunichokoza”

“Heheh ,, kinachokukasirisha nini wakati mchumba wako jina lake ni Kibwengo Khamisi, kuna muda nafikiria wazazi wa mchumba wako walikuwa wakiwaza nini mpaka wakaamua kumwita mtoto wao jina la Kibwengo”

Hao ni wadada wawili waliokuwa wameketi karibu na alipokaa Roma na Lanlan na hayo ndio ilikuwa mitazamo yao juu ya Roma na Lanlan bila kusahau mpenzi wa Dorca afahamikae kwa jina la Kibwengo.

Dakika kama kumi na tano mbele hatimae tangazo la ndege ya Emirate kutua ndani ya uwanja huo ilisikika na Roma alimshika Lanlan mkono, wote kwa pamoja wakiwa na hamu ya kumuona Edna.

Upande wa Roma maneno aliozungumza na Christine ni kama aliyapotezea kama ilivyo kawaida yake , Roma alikuwa na sheria moja tu katika Maisha yake kutojisumbua na mambo ambayo hana uhakika nayo, alipenda kudili na yale tu ambayo anauhakika nayo na ambayo yapo mbele ya macho yake , lakini sio yale ambayo ni ya kufikirika na ndio maana aliamua kupotezea maneno ya Christine na alijiambia katika akili yake kama maneno yake ni sahihi basi yeye anaisubiria hio siku ya utabiri kwa hamu zote.

Upande wa kampuni yake ya Vexto siku hio alikuwa ashatoa taarifa ya uthibitisho juu ya Christine kukubali kufanya interview siku ya uzinduzi wa Tv Channeli yao m jambo ambalo lilipokelewa kwa shangwe na Daudi pamo ja na Wendy na walihakikisha watatumia kila nyenzo kuhakikisha kila mtu anaufahamu na siku hio yenyewe na hio ni kwa ku’promote’ kwenye mitandao pamoja na kwenye chaneli za Tv Tofauti tofauti,

Matangazo mbalimbali pia yanayohusiana na shindano la vipaji vya uimbaji wa muziki pamoja na uigizaji yalikuwa yamesambaa kwenye barabara nyingi katikati ya jiji la Dar , lakini pia kwenye baadhi ya mitandao , huku mirejesho ya watu wanaojiandaa na kujiingiza kwenye mashindano hayo ukiwa ni mkubwa mno na hilo lilidhihirisha kazi nzuri ambayo wafanyakazi wa Vexto Media upande wa Marketing walikuwa wakifanya.

Ni ndani ya dakika ishirini mara baada ya ndege kutua , Lanlan ndio aliekuwa wa kwanza kumuona mama yake akitokezea sehemu ya kusubiria wageni.

“Anko mama wa Lanlan yule”Aliongea Lanlan huku akijaribu kutoa mkono wake wake kwenye kiganja cha Roma , lakini Roma alikuwa ameshikilia vizuri , alikuwa akitegemea Lanlan akishamwona mama yake atamkibilia hivyo kuweza kugonga watu na ndio maana hakutaka kumuachia.

Upande wa Edna mara baada tu ya kufika ndani ya eneo hilo alijikuta akisimama mara baada ya kumuona Roma aliesimama na Lanlan , alionekana mrembo huyu ni kama hakutegemea kuwaona watu hao wawili wakiwa pamoja , moyo wake ulipata joto ambalo sio la kawaida , kwake picha hio ilimfurahisha sana.

Edna alikuwa amependeza mno na hakuwa amevalia mavazi ya suti kama alivyoondoka bali alivalia kama mdada wa kileo, suruali na Jeans pamoja na tisheti ndio mavazi Edna aliovalia na kumfanya kuonekana mrembo kuliko wanawake wote waliokuwa ndani ya hilo eneo.

Edna hakuwa peke yake bali alikuwa ametangulizana na Alhaji CEO kampuni ya Maple na bwana huyu baada ya Edna kusimama alijikuta akiangalia mbele na hapo ndipo alipomuona Roma akiwa amesimama na mtoto ambaye alimshangaza kutokana na uzuri wake , lakini pia namna ambavyo anafanana na Edna , sasa jambo hilo lilimshangaza kwani hakuwa na taarifa , wala hakuwahi kusikia popote Edna ashawahi kuwa na mtoto.

“Madam Boss kumbe una mtoto mzuri vile?”Aliongea Alhaji na kumfanya Edna kutabasamu na kuanza kutembea huku akiwa ameshikilia mkoba wake akiwasogelea Roma na Lanlan huku uso wake ukiwa umepambwa na tabasamu.

Watu wote waligeuza macho kuangalia ni nini kimemfanya mrembo huyo kuwa na tabasamu mwanana namna hio na kuzidi kupendeza.

Upande wa Roma alijiambia lilikuwa wazo zuri sana lililopendekezwa na Sophia kuja na Lanlan kumpokea Edna , kwani matokeo yake alikuwa akiyaona laivu.

“Mom,,,!!!:Lanlan baada tu ya kuachiwa mkono wake alimkimbilia Edna na kumkumbatia na Roma ilibidi na yeye asogee mpaka waliposimama.

“Mr Roma tunaonana tena “Aliongea Alhaji kwa tabasamu na kisha alimpatia Roma begi dogo la kuburuza akimpa ishara ni la Edn.

“Hongera sana Mr Roma kwa kuwa na familia nzuri”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu na kisha walipeana mkono na Alhaji akatangulia.

Edna alimwangalia Roma na alijikuta akiachia tabasamu bila kupenda alionekana kufurahishwa na kitendo cha Roma kuja na Lanlan , licha ya kutokuwategemea.

“My Babe Wife umeenda siku hizi mbili lakini umerudi urembo wako ukiwa umeongezeka kwa kiwango kikubwa, usiniambie umerekebisha kidogo sura ili mume nizidi kukupenda”Aliongea Roma huku akiweka tabasamu na Edna alitabasamu kidogo .

“Una makengeza labda”Alijibu Edna huku akimshika mkono Lanlan na kuanza kutembea huku wakiongea na dakika chache tu mbele waliweza kufika kwenye gari aliokuja nayo Roma.

“Lanlan nimekuletea zawadi za kutosha tukifika nyumbani nakuonyesha”Aliongea Edna na kumfanya Lanlan kushangilia na kumwangalia Roma kwa macho ya ushindi.

“Wife inamaana unayemkumbuka ni Lanlan tu na mimi mumeo niliepiga magoti usiku mzima kupiga maombi urudi salama haujanikumbuka”Aliongea Roma huku akijifanyisha kaonewa na Edna alimwangalia.

“Ukweni hawajambo?”Aliuliza Edna na Roma badala ya kujibu aliwasha gari na kukaza macho barabarani na kuanza kusogeza gari , ni kama alikuwa akielewa Edna anakoelekea kwenye mazungumzo aliotaka kuanzisha na mpaka hapo aliamini Lanlan ndio kamzidi.

“Vipi safari imekuwa ya mafanikio?”Aliuliza Roma.

“Shukrani kwako Hades safari imekuwa ya mafanikio”Aliongea Edna kwa namna ya utani akitumia jina la Hades na kumfanya Roma kutabasamu na mpaka hapo aliamini kuna jambo ambalo limetokea.

“Nielezee kilichotokea basi wife sio kuishia kuniita Hades”Aliongea Roma.

“Nikajua unataarifa na kila kilichojili nadhani sio kama nilivofikiria Hades”Aliongea Edna na kuanza kumuelezea safari ilivyokuwa namna alivyokutana na Tanya na kujua kile kilichotokea Japani namna alivyoweza kumiliki kundi la Yamata Sect, lakini pia hakuacha kuelezea namna ambavyo alikutana na Clark ,Edward na Mr Alfin Kelphin pamoja na zawadi aliopatiwa , ambacho hakuelezea Edna ni kilichomtokea hotelini , kitendo cha kudondoka na kupoteza fahamu.

“Alfin Kelphin ndio mmiliki wa kampuni ya Aba?”

“Nikajua unamjua vizuri , inaonekana maneno yake juu ya wewe kuwa rafiki yake ni ya uongo”

“Sijasema ni ya uongo ila juu ya umiliki wake wa makampuni ya Aba sijawahi kufahamu hilo , hata hivyo mke wangu nimefurahi umetatua shida zako kwa haraka na kurejea nchini maana kwa jinsi nilivyokumisi huenda ningefanya safari ya dharula kuja Hongkong”

“Mbona unaruka baadhi ya mambo?”

“Nimeruka nini sasa mke wangu”

“Hujaongea chochote kuhusu Tanya mwanamke ambaye aliniteka Tanzania lakini Ghafla tu akawa kijakazi wako”Aliongea Edna na kumfanya Roma akune kichwa ukweli aliona hakuna maelezo ya kuongea hapo.

“Kule Ufaransa ukajinasibu kwamba utanieleza kila kitu unachofanya , lakini matokeo yake ukavunja ahadi yako , ilianza kwa Apollo na Artemis na baada ya pale ukawa umesahau, kumbe ulienda Japani ukakamatika na Seventeen feki, lakini sio hivyo tu kumbe mwenzetu unakitu cha thamani ‘Godstone’ unakaa nacho hatuambiani”

“Kwahio sababu ya kuninunia siku ile Ufaransa ilikuwa ni kwasababu sikukueleza kuhusu Alice na kaka yake, lakini ulijuaje kama wanaitwa Apollo na Artemis nakumbuka ulikuwa umepoteza fahamu”Aliongea Roma.

Ukweli hakuelewa ilikuwaje Edna akamfahamu Alice kuwa Artemis na Stern kuwa Apolo kwani alichokuwa akikumbuka ni kwamba Edna alikuwa hana fahamu zozote.

“Waulize Apollo na Artemiss watakua na majibu ya swali lako”Aliongea Edna na kumfanya Roma sasa kuelewa huenda Siku ile Alice na Stern hawakumfanya Edna kupoteza fahamu , lakini kama ni kweli Roma aliona basi Edna ni mtu hatari sana kwenye kuweka mambo moyoni , kwani mambo yaliotendeka siku ile hayakuwa ya kawaida , kwa mfano kitendo cha Roma kuongea na Roho ya Depney lilikuwa ni jambo ambalo sio la kawaida kwa binadamu wa kawaida kulishuhudia na kutulia tuli.

Roma alikuwa na shauku kujua ni kwa kiasi gani ambacho Edna alieweza kuelewa siku ile.

“Wife kuhusu Japa..”

“Huna haja ya kujitetea Roma yalishapita”Aliongea Edna akimkatisha Roma kuongea na Edna alimgeukia Lanlan aliekuwa bize kuchezea simu.

Dakika chache mbele waliweza kufika nyumbani na kupokelewa na Roma alibeba begi la Edna na Kwenda nalo chumbani , huku Lanlan akifuata nyuma nyuma kuagalia ni Zawadi gani alizoletewa na mama yake , alionekana kuwa na shauku kubwa na hata Roma alilitambua hilo.

Baada ya Roma kutua begi kitandani alimwangalia Lanlan na kisha akapiga hatua kutoka Kwenda kwenye chumba chake.

“Nimekuletea Zawadi pia Rma usiondoke”Aliongea Edna kwa sauti kavu huku akimpita Roma na Kwenda kuketi kitandani kichomvu na kumfanya Roma amwangalie kwa mshangao , hakuamini kama kweli Edna mke wake kabisa na ukauzu wake amemkumbuka mpaka kumletea zawadi, tabasamu lilikuwa nje nje.

Unafikiri kwanini Edna akapatwa na kichwa cha ghalfa , Jiwe lingine analozungumzia Aphrodite liko wapi?


ITAENDELEA ALHAMISI NINAWEKA RATIBA ILI USITESEKE NA AROSTO KWANI SIO MAKUSUDI YA KULETA SIMULIZI HII HAPA JUKWAANI .
UKITAKA KUNIUNGA MKONO UNAKARIBISHWA , NICHEKI WATSAPP 0687151346 NITAKUJIBU NA KUKUPA UTARATIBU WA MWENDELEZO KWA ANAETAKA
 
Back
Top Bottom