Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Kwani jamaa hauna mengine ya kufanya. Jenga nchi!!! Utashinda ukidraw attention yake lakini niko sure ataona maandishi yako ya vilio atakapomaliza ya kwake. Wacha kulilia pipi mwenzangu.
Nafikiri upo kwenye joto! Unatafuta upigwe mimba! You can go any where until you got what you need! So acha kiherehere! Moja hyo! Mbili mi sijengi nchi asee nnajenga yangu, tatu sijakuandikia wew nyege zako ndo zinakufanya ubabaike na maandish ya wa2! Mwisho acha ushoga! Ni dhambi kubwa na ni kinyume na mila na desturi zetu! Pimbi ww
 
Nafikiri upo kwenye joto! Unatafuta upigwe mimba! You can go any where until you got what you need! So acha kiherehere! Moja hyo! Mbili mi sijengi nchi asee nnajenga yangu, tatu sijakuandikia wew nyege zako ndo zinakufanya ubabaike na maandish ya wa2! Mwisho acha ushoga! Ni dhambi kubwa na ni kinyume na mila na desturi zetu! Pimbi ww
🤣🤣
Ninapenda mwelekeo wa haya maongezi. Mara eti pimbi, sijui shoga,eti nyege! Tuliza joto kijana mdogo. Wacha KULIA!! BWANA NYEGE Tulia!!!🤣🤣🤣
 
SEHEMU YA 385.

Licha ya kusikia swali la Kizwe , lakini Lekcha hakujibu na kuendelea na shughuli yake ya kujiandaa kwa ajili kwenda kufanya kazi yake ya kuokota chupa.

“Mbona hunijibu , unanionea huruma?”Aliuliza Kizwe awamu hii akiwa siriasi.

“Nimekusaidia kwasababu nimetaka kufanya hivyo , mimi na wewe nadhani anaetakiwa kumuonea mwenzake huruma , una miguu yote miwili mimi nina mmoja wa kawaida na mmoja wa bandia , unafikiri mtu kama mimi mwenye Maisha duni ninaweza kukuonea huruma?, Sikujui wewe ni nani ila naamini sio mwanamke unaetokea katika familia ya kawaida”

“Unahitaji kufahamu stori yangu?”

“Huo muda wa kuanza kukusikiliza kwasasa hakuna , nahitaji Kwenda kuendelea na kazi yangu wewe mwanamke, vaa nguo zako ule hiko chakula tuondoke”Aliongea na kumfanya Kizwe kuvaa dela jipya na kisha akaanza kula, kwa muda huo hakuona haja ya kuchagua chakula alijali kujaza tumbo.

Lekcha na yeye alikula kidogo na kisha kumuachia sehemu kubwa Kizwe amalizie.

“Una watu wa kuwasiliana nao , kama unataka kuondoka siwezi kukuzuia , ila sina nauli ya kukupatia , lakini kama utavumilia hadi jioni siwezi kukosa kitu”.

“Unapata kiasi gani kwa kuuza chupa?”

“Napata hela ambayo inanitosha kula na kulipia hapa?”.

“Kama ni hivyo huwezi kunipa hela ya kunitosha kama nauli ya kupanda ndege”.

“Sijasema nataka kukupatia nauli ya kupanda ndege”

“Kwahio ulikuwa unazungumzia nauli gani?”

“Ya kupanda daladala na Kwenda kwa ndugu zako ukatafute nauli , ulifikiri sijui unatokea Rwanda?”.

“Ulijua mimi ni mtu wa Rwanda?”

“Ni rahisi sana kumfahamu mtusi , nishawahi kuishi ndani ya jamii yao”Aliongea na kumfanya Kizwe kushangaa.

“Wewe ni nani haswa?”Aliuliza Kizwe kwa wasiwasi.

“Nishakuambia sitaki kufahamu upande wako na vilevile sipendi ufahamu upande wangu”Aliongea Lekcha huku akianza kujikusanya kwa kuanza safari ya kuondoka.

“Nina hela nyingi sana , nahitaji kupiga simu tu kuweza kuzipata”Aliongea na kumfanya Lekcha kusimama na kumwangalia.

“Umenisaidia na sasa nipo hai , nitakusaidia pia kutoka katika biashara unayofanya , umri wako unakuruhusu kufanya makubwa”

“Sitaki hela zako”Aliongea na kumfanya Kizwe kushangaa , inakuwaje mtu akakataa hela wakati anauza chupa kuzipata.

“Una uhakika hutaki hela?”

“Ndio sitaki hela , ningekuwa nikizitaka ningekuwa nazo nyingi”Aliongea.

“Kama hutaki hela unataka kitu gani?”Aliuliza Kizwe na Lekcha alishindwa kuongea chochote na kisha akatoka nje na dakika kama tano tu hivi alirudi akiwa ameshika simu ndogo na kumpatia.

“Mwenyewe kasema ina dakika zisizozidi mbili , nadhani zinakutosha kuwasiliana”Aliongea na kumfanya Kizwe kutabasamu na kisha kupokea simu na kuandika namba ambazo alionekana kuzikariri na aliweza kuongea kwa Kinyarwanda kwa nusu dakika tu na kisha akamrudishia.

“Nahitaji tuondoke wote, msaidizi wangu atanifuata muda si mrefu”Aliongea na kumfanya Lekcha kufikiria kidogo.

“Kwanini unahisi ninaweza kukubaliana na ombi lako? , ijapokuwa unaweza kuwa na pesa kama uavyojigamba haimaanishi kwmaba ninaweza kukubali kuondoka na wewe”Aliongea na kumfanya Kizwe kuvuta pumzi, hajawahi kukutana na mtu mgumu kama Lekcha.

“Umesema hutaki hela lakini sijui unachotaka , ninachokuwambia sio kukupa pesa ila ni kukupatia unachotaka , kama unaamini naweza kufanikisha uamuazi ni wa kwako kukubali kuondoka na mimi au kubaki”Aliongea Kizwe na kisha akakaa kwenye godoro.

Ni ndani ya dakika chache tu simu ile ndogo iliita tena na Kizwe alimwambia Lekcha aipokee na atoe maelekezo ya mtu kufika hapa walipo na Lekcha aliipokea na kufanya kama alivyoambiwa kwa kutumia lugha ya Kingereza na baada ya kumaliza alianza kumwangalia Kizwe kuanzia chini mpaka juu na upande wa Kizwe alifanya hivyo hivyo alimwangalia Lekcha kwa namna ya kumchunguza na kisha alisimama , alivaa vijisendo na kufungua mlango na kutoka akimuacha Lekcha ndani.

Ni ndani ya dakika kama tano tu hivi ilionekana gari ndogo nyeupe aina ya Toyota Crown athlete ikisimama mita kadhaa kutoka kwenye geti la nyumba ya Juma , baada ya gari ile kusimama alishuka mwanadada aliekuwa amevaa suruali ya kitambaa pamoja na blazia ya rangi ya samawati na kusogea upande ambao amesimama Kizwe.

“Miranda Thank you”Aliongea Kizwe na kumfanya yule mwanadada kumwangalia bosi wake kwa wasiwasi.

“Bosi nini kimekupata tulikuwa ni wenye wasiwasi , mheshimiwa pia ni mwenye wasiwasi kila saa anapiga simu”Aliongea Miranda.

“Sina muda wa kuelezea kilichonitokea Miranda ,ila kwasasa nahitaji sehemu tulivu kutulia, sitaki mtu yoyote kujua nilipo, ndio maana nikakupa maelekezo ya kuja peke yako”Aliongea na Miranda alitingisha kichwa kwa heshima na kisha alimpa ishara ya bosi wake kuelekea kwenye gari , lakini Kizwe alionekana kusita sita kwani mpaka muda huo bado Lekcha hakuwa ametoka, alisimama kwa dakika moja na kisha akaenda kuingia garini naMiranda akaliwasha kwa ajili y a kulitoa.

“Subiri”Aliongea Kizwe huku akiangalia upande wa getini alimuona Lekcha akija kwa namna ya kuchechemea kusogelea gari yao na hata msaidizi wake alishangazwa na mwanaume huyo.

“Ndio alienisaidia mpaka unaniona muda huu , tutaondoka nae”

“Okey Madam”Alijibu na kisha akatoka na kumfungulia Lekcha mlango na kuingia ndani na Kizwe alijikuta akimwangalia Lekcha na kisha akatabasamu.

“Sijui kwanini nakufuata , ila nipo tayari kuongozana na wewe”

“Kama ilivyokuwa kwangu kukufuata bila ya sababu”

“Yes”

“Hahaha…wise choice”Aliongea na kisha palepale gari ikaondoshwa huku Mwajabu aliesimama kwenye geti akiwa anashangaa tukio zima , alikuwa ameambiwa muda huo na Lekcha kwamba anaweza asirudi kabisa hivyo alimkabidhi kabisa ufunguo na kumwambia amsaidie kufikisha taarifa zake kwa Juma.

Sasa wakati gari ikikatiza kwenye kiwanda cha biscuit , ilianza kufuatiliwa kwa nyuma na gari nyingine aina ya Aud nyeusi , hata walipochukua barabara ya kwenda Chamazi gari hio ilikuwa nyuma yao.

Dakika chache mbele gari ilikuja kusimama Maji matitu na kukunja kulia kuingia ndani ya hoteli ya nyota tano ya JR iliokuwa maeneo hayo , hii ni hoteli ambayo Roma alimpata Edna hapo kwa kumdhan ia ni kahaba.

Sasa jambo moja tu ambalo Kizwe alishindwa kujua ni kwamba alikuwa akifuatiliwa na watu waliokuwa wakimfatilia ni wa serikali ya Rwanda , sasa haikueleweka walikuwa na maagizo gani.

********

Matilda alijikuta akifuta jasho mara baada ya kusikia stori nzima ya mdogo wake juu ya mwanaume wake wa kichina kumkataa akiwa mjamzito, Matilda alimuone sana huruma , ukweli alikuwa akijua hilo litatokea kwani alikuwa akiwaelewa wachina sana likija swala la mahusiano na watu weusi , hivyo aliamini hata mdogo wake anakwenda kukutana na kadhia ambayo wengine wote wamekumbana nayo , lakini hakuamini kama ni mapema hibvyo , lakini kubwa zaidi ni mdogo wake kubeba mimba.

Wakati Matilda anaingia kwenye chumba cha Queen kilichomshangaza ni namna vitu vilivyotapakaa chini huku na huko na ilionekana kazi yote hio ni ya Queen , huku mdogo wake akiwa amelala sakafuni akiwa kama mtu aliekuwa kwenye maombolezo.

Sasa kilichomfanya Queen kuwa kwenye hali kama hio ni kutokana na kwamba Yan Buwen alikuwa ashaondoka ndani ya hoteli ya Serena na hakuwa na mawasiliano nae , ikimaanisha kwamba hakuwa na namna ya kuwasiliana nae kabisa , kwani hata namba ambayo alikuwa akitumia Yan Buwen imeshafutiwa usajili hivyo kutokuwa hewani.

“Pole sana mdogo wangu , hauna haja ya kuwa hivi , kilichotokea kishatokea na tayari ni mjamzito unatakiwa kufikiria hali ya mtoto na yako kwa sasa”

“Nina tamani kufanya hivyo dada yangu , lakini nampenda sana Yan Buwen na sijui kama nitaweza kumuacha”

“Mtu ashakuacha na hujui namna ya kuwasiliana nae halafu unasema huwezi kumuacha?”Aliongea Matilda kwa namna ya mshangao.

“Dada naamini Yan Buwena ananipenda na atanirudia tu , nitamzalia huyu mtoto kumuonyesha mapenzi yangu kwake”Aliongea huku akilia na kumfanya Matilda kumuonea sana huruma , alijua mdogo wake akili yake haikuwa sawa kwa wakati huo na hata kama akijaribu kumshauri haitosaidia kwani ni mapema mno kukubali ukweli kama ameachwa.

Muda huo huo wakati Queen akiomboleza na kubembelezwa na dada yake , iliingia gari nyingine aina ya kirikuu na kisha akatoka Omari aliebeba ua akiwa amevalia suti na kutembea kuelekea ndani na kisha aliulizia kuhusu Queen na akaambiwa yupo chumbani kwake , mfanyakazi alipotaka Kwenda kumuita Queen, Omari alimpa ishara kwamba ataenda mwenyewe.

Omari hapa hakuwa na jicho moja , kwani macho yote yapo kawaida kabisa na ni ngumu sana kujua kama jicho lake lingine lilikuwa la kijini.

Omari baada ya kufika mbele ya mlango wa chumba cha Queen aligonga kwa dakika na mlango ulifunguliwa na kukutanisha macho na Matilda.

“Omari.. unafanya nini hapa, karibu”Aliongea Matilda pasipo ya kufungua mlango , aliangalia nyuma na kumwambia mdogo wake Omari amefika.

“Sitaki kuonana nae , mwambie aondoke”Aliongea na kauli yake ilisikika mpaka kwa Omari.

“Naomba umpatie hii zawadi yangu ni kwa ajili yake , ili kumuweka sawa”

“Queen baba yako kaniambia kinachokusumbua , lakini jua nipo tayari kulea mtot aliekuwa tumboni kwako kama mwanangu na nitahakikisha unamsahau huyo mpuuzi aliekusababishia maumivu”Aliongea na kumfanya Matilda kushangaa.

“Unamaanisha nini Omari”

“Nahitaji kumuoa Queen”Aliongea bila ya aibu.

“Mwanaume alienipa mimba sio mpuuzi Omari , naomba uondoke sitaki kukuona na siwezi kuolewa na wewe na haitokuja tokea” Ilisikika sauti kutoka ndani

********

Siku iliofuata ilikuwa ni siku ya Ijumaa, Roma aliweza kufika kazini kama kawaida huku akiwa na tabasamu pana lillopamba uso wake, mahusiano yake na Edna yalionekana kuimarika kwa siku hizo mbili kwa kiwango kikubwa na hilo ndio lilimfurahisha.

Baada ya kusalimiana na wafanyakazi wake akiwemo Daudi na Wendy alienda moja kwa moja mpaka ofisini , siku hio Amina alitoa taarifa kwamba hatofika kazini , hivyo kazi zote ni kama zilimuangukia Roma kufanya , mezani kulikuwa na mafaili mengi yalipangwa yakisubiri ayafanyie kazi.

Kabla hajayagusa aliingia Daudi na kutoa taarifa fupi ya siku tatu zote ambazo hakuwepo kazini na Daudi aliweza kumpa taarifa kwamba Sophia angerudi wiki inayofuata siku ya Jumanne na kampuni ilikuwa katika utaratibu wa kuwaandalia wasanii wote menejimenti binafsi itakayo wasimamia.

“Kuhusu Menejimenti ya Sophia nitamsaidia mwenyewe , wengine mnaweza kuendelea nao kama kampuni”Aliongea Roma na Daudi aliitikia , hakutaka kubisha kwani alijua Sophia ni ndugu na Roma hivyo maswala ya upendeleo yalikuwa ni lazima kutokea.

Baada ya Daudi kutoka alipitia mafaili yote kwa kutumia uchawi ili kurahisisha kazi na ndani ya dakika kadhaa aliona hakuna cha maana cha kudili nacho na aligeukia tarakishi yake kwa ajili ya kucheza gemu , lakini simu yake iliita kabla hata ya kufungua na alipoangalia mpigaji alikuwa Rose, alitabasamu na kisha akapokea.

“Hubby nimekumiss”Ilisikika sauti upande wa pili”

“Nimekumiss pia mrembo wangu , uko poa?”

“Niko poa mpenzi , nilihitaji kukuona siku ya leo , kuna ushauri nataka kukuomba”Aliongea Rose na Roma alimkubalia palepale na kumuahidi atakuja muda wa jioni.

Roma baada ya kukata simu alimkumbua mke wake Edna na alitafuta namba yake na kumpigia na simu ilipokelewa upande wa pili.

“Wife nimekumiss sana , unaonaje tukipata chakula cha mchana pamoja”.

“Mhmh! Okey”

“Nitakuja kukuchukua muda ukifikika”

“Sawa!, utanisindikiza pia kwenda benki ya Swiss”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.

“Benki ya Swiss, kufanya nini?”

“Kuna kitu nahisi mama kaniachia ila sijui ni nini , inaonekana ni kitu muhimu sana kwa namna alivoweza kuniambia kwa namna ya fumbo”Aliongea Edna upande wa pili na kumfanya Roma , kuona hatimae Edna kaweza kufumbua fumbo la uwepo wa Deposit Box ndani ya Swiss.

“Okey wife nitakuja kukuchukua na tutaenda wote , lakini tutaanza kwanza kupata chakula cha mchana”

“Okey”Alijibu Edna na kisha Roma akakata na kuegamia kiti.

Licha ya kwamba alikuwa akihofia kilichoachwa ndani ya boksi hilo kinaweza kumsababishia Edna mawazo baada ya kuufahamu ukweli juu ya kifo cha mama yake , lakini asingeweza kumzuia.
 
SEHEMU YA 386.

Roma ilivyotimia saa saba kamili alitoka kwenye jengo hilo la kampni yake na moja kwa moja kuanza safari ya kuelekea Posta ilipo kampuni ya Vexto na ndani ya madakika kadhaa tu aliweza kufika na kuegesha gari upande wa chini karibu na la mke wake na akamtumia Edna ujumbe wa maandishi na ndani ya dakika chache tu Edna aliekuwa amevalia suti alitokea , alikuwa na mudi nzuri kweli kwa muonekano wake na kumfanya kuwa membo Zaidi.

Roma alitoka kwenye gari na kisha akamfungulia mke wake kama boss na kumfanya Edna kuingia ndani ya gari na yeye akazunguka upande wa pili na kuingia ndani.

“Nimemiss Sophia , anarudi lini?”aliuliza Edna

“Jumanne ndio wanarudi”Aliongea Roma na kuondoa gari taratibu.

“Umejuaje kama umeachiwa kitu ndani ya benki ya Swiss?”Aliuliza Roma.

“Unakumbuka siku tulivyoenda Ikulu?”

“Ndio nakumbuka”

“Nilipatiwa Flash na mheshimiwa Senga siku ile na kwa maelezo yake alisema iliachwa na mama yangu na nilipaswa kuwa nayo, nilipokuja kuangalia ndani yake niligundua, kuna jambo ambalo lilikuwa likiendelea kwenye Maisha ya Mama pasipo ya mimi kufahamu” Edna alianza kumuelezea Roma namna ambavyo aliweza kugundua kuwa mama yake alikuwa na kisasasi ambacho hakuwa amekiweka wazi huku akimtaka yeye awe ni mwenye kukamilisha kisasi hicho , lakini pia Edna alimuelzea Roma kuhusu orodha ya kampuni ambazo zimeachwa na mama yake.

Roma alijikuta akishangaa kuhusu maelezo ya Edna , hakuamini kama mke wake alimficha jambo hilo kwa muda mrefu , lakini hakuwa kwenye nafasi ya kumlaumu Edna kwa wakati huo kutokana na kwamba kipindi kile hakuwa akimwamini vizuri na ndio kwanza walikuwa wameoana kimkataba.

“Kwahio kitendo cha kuichukua kampuni ya JR sababu ilikuwa ni hio orodha?”

“Ndio !Nilijua mama alikuwa akiniambia kampuni zote zilizopo kwenye orodha anataka kuwa chini ya Vexto ndio maana nikaanza na JR”.Aliongea Edna na muda huo walikuwa wanaingia sasa kwenye mgahawa na waliona wasimamaishe mazungumzo yao na wakaendelee kuongea wakiwa wanapta chakula cha mchana.

Wote baada ya kuingia kwenye mgawaha wa Rosella mtaa wa Azikiwe , waliagiza chakula na Roma alimwambia Edna aendelee kumuelezea.

Edna aliendelea kumwambia Roma namna alivyoshindwa kung’amua kuhusu Swiss In.

“Hili jina la Swiss In lilikuwa likinipa mashaka , kwani niliamini mama asingeweza kuorodhesha kitu ambacho kipo nje ya uwezo wangu na tulikuwa tukijaribu kufuatilia kwa muda mrefu na kugundua hakuna kampuni ya Swiss In”

“Na ulifahamu vipi?”

“Suzzane ndio alienisaidia kufumbua fumbo hili”Aliongea Roma na sasa kuelewa nini kimetokea na kujiambia inamaana Suzzane kashindwa kumvumilia mpaka akaamua kumuelezea , lakini kwa wakati huo hakutaka kumwambia mke wake alishawahi kuongea na Suzzane.

Edna wakati alivokuwa akielezea tukio hilo alionekana kutokuwa sawa kimawazo alikuwa na hofu na kile atakachokutana ndani ya benki ya Swiss ya kuhifadhi vitu ndio maana alitaka Kwenda na Roma mume wake.

Baada ya kula chakula huku Roma akijitahidi kumfurahisha , hatimae safari ya Kwenda benki ya Swisss ilianza na hapakuwa mbali , ni umbali wa nusu kilomita tu kutoka walipokuwepo.

Edna na Roma baada ya kuingia ndani na kuelezea shida yao na kufuata taatibu za mwanzo mhudumu alitabasamu kwa namna ya kuwachangamkia na kisha aliwaambia wamfuate.

Waliongozwa mpaka upande wa chini kabisa ya jengo kwa kutumia Lift na kuja kutokezea kwenye korido pana ndefu ambayo ilikuwa na boksi za chuma nyingi zenye namba kila upande kulia na kushoto na mbele , ilikuwa ni sehemu ambayo ina hewa ambayo inaendeshwa kwa mitambo, Roma alihisi vitu vinayvohifadhiwa humu vingi ni vya thamani kutokana na hewa inavyodhibitiwa.

“Boksi ni hili hapa wateja wetu, unaweza kutumia Fingerprint kufungua au Nywira , ukikosea mara tatu, kisanduku kitazuiwa kufungiwa kwa siku kumi na nne huku uthibitisho wa umiliki ukiendelea”Aliongea kwa Kingereza safi na Edna alitingisha kichwa na aliwaacha.

“Unaifahamu nywira?”

“Nafikiri hivyo, mama alikuwa anatumia nywira ya aina moja katika vitu vingi ambavyo ni binafsi kwake”

“Na unaifahamu?”

“Ndio ni herufi kumi na moja”Aliongea Edna na palepale alianza kubonyeza sehemu ya kuingiza namba”

“I9989819206”Aliandika Edna na Roma aliweza kuikariri haraka sana na alichogunuda ni kwamba nywira hio ilikuwa ni mwaka wa kuzaliwa wa Edna ambao uliandikwa kwenda mbele na kinyunyume lakini herufi 206 alishindwa kuijua inamaanisha nini.

Sanduku lile lilifunguka kama mlango wa CD na Edna na Roma wote kwa pamoja waliweza kuona bahasha ya Khaki ndani yake na Edna aliitoa kwa kuichunguza na kisha akampatia Roma , aliangalia ndani kama kulikuwa na kitu kingine lakini ilionekana kitu pekee kilichohifadhiwa humo ndani ni hio bahasha.

“Tutakwenda kuigunfulia baada ya kufika kwenye gari”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na kisha wakafunga kiboksi kile na kisha walitumia utaratibu ule ule na kisha wakatoka baada ya kusaini.

Baada ya wote kuingia kwenye gari , Edna alionekana kuwa na shauku kweli ya kujua kilicho ndani yake , lakini Roma alimkataza kufungua na kumwambia atulie kwanza.

“Mbona unaelekea upande huo?”

“Tunaelekea nyumbani”Aliongea Roma.

“Nahitaji kurudi Kazini nina majukumu mengi Roma”Alilalamika Edna.

“Edna nisikilize kuna hisia mbaya zinaniambia kilichopo kwenye hii bahasha kinaweza kukutoa machozi, nataka uangalie ukiwa nyumbani na watu wote wanaokupenda wakiwa pembeni yako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia Roma kwa wasiwasi.

“Kuna kitu unajua huniambii?”Aliuliza Edna.

Ukweli Roma hata sababu ya kumpeleka kwanza mgahawahi kula na kushiba ulikuwa ni mpango wake , aliamini huenda ndani ya bahasha hio kuna taarifaa ambayo itakuwa kubwa sana kwa Edna , hivyo kumletea mawazo na kishindwa kula.

Roma hakutaka kujibu swali la Edna kabla ya kujua ni kitu gani kipo ndani ya bahasha hio , alijiamia atampa Edna maelezo kutokana na kile ambacho kitakuwa kwenye bahasha hio..

Dakika chache tu waliweza kufika nyumbani na Bi Wema na Blandina walishangazwa na kurudi kwao nyumbani mapema siku hio tena wakiwa pamoja.

“Mama Lanlan yuko wapi?”Aliuliza Edna mara baada ya kutokumuaona Lanlan eneo hilo na Blandina na Bi Wema waliangaliana.

“Babu yake kaja kumchukua na ameondoka na Qianq Xi”Alijibu Bi Wema na kumfanya Edna kumwangalia Roma.

“Yule mzee anapenda kufanya mambo bila kuaga ,alishindwa vipi kutupigia simu kama anamchukua mtoto wetu”Aliongea Roma huku akikunja sura.

“Sio mzee , yule ni babu yako Roma”Aliongea Blandina.

“Hakuna shida ameenda kwa babu yake Roma”Aliongea Edna huku akimshika mkono Roma na wakaanza kupanda juu.

“Miss kama hamjakula chakula niwaandalie”Aliongea Bi Wema.

“Bi Wema msiwe na wasiwasi tulipitia mgahawani kabla ya kuja nyumbani”Aliongea Edna na Blandina alitabasamu.

“Okey mmefanya vizuri mnaweza Kwenda kupumzika sasa”Aliongea Blandina kwa bashasha pasipo kujua kama wenzie wamerudi kwa jambo maalumu.

Wote waliingia chumbani na Edna mara baada ya kufika tu alitaka kuangalia ni kipi kipo kwenye bahasha hio , ambayo ameachiwa na mama yake kwa namna ya kificho.

Roma hakutaka kumzuia alimwacha afungue mwenyewe huku yeye akiketi pembeni yake, Edna mara baada ya kufungua ndani yake aliweza kutoa karatasi zilizopigwa pini , ni nyaraka mbili tofauti.

Edna aliweka moja kwenye mapaja na kuanza kupitia iliokuwa ni ya kwanza ambayo juu kabisa ilikuwa na nembo ya hospitali ya Muhimbili, Edna alijikuta akipatwa na mshangao usiokuwa wa kawaida huku akisoma haraka haraka ile karatasi.

Karatasi alioshikilia Edna ilikuwa ni maelezo ya matibabu ya Kliniki ambayo alikuwa akifanya mama yake, Edna hakuwa mjinga kufahamu maelezo ya kidaktari , kila kitu kilikuwa wazi, picha ya kadi la Kliniki lilikuwepo na kila kitu kilionyesha kwamba mama yake alikuwa ni mjamzito wa mapacha, Roma aliona mabadiliko ya Edna ila alishindwa kuongea chochote .

Sasa kitu kilichokosekana kwenye karatasi ile ni cheti cha kuzaliwa , kulikuwa na taarifa ya mahudhurio ya Kliniki pekee ikionyesha Raheli alipokuwa mjamzito alikuwa na ‘Multiple Pregnancy” lakini hakuna taarifa inayoonyesha wakati wa kuijifungua nini kilitokea.

Edna baada ya kuona taarifa ya kwenye karatasi ya kwanza haijampa jibu , kwa papara alichukua karatasi nyingine na kuanza kuisoma na hii ilimtoa machozi na kumfanya kutetemeka.

Karatasi ya pili ilikuwa ni cheti cha matibabu cha mama yake kutoka hospitali ya Mayo Clinic Marekani , Edna alijitahidi kuelewa cheti hicho lakini ni kama hakuwa akielewa kile anachosoma na kumpatia Roma.

Roma alichuku karatasi zote na kuzisoma moja moja kwa umakini na kuishia kukunja sura , ijapokuwa mategemeo yake yalikuwa Zaidi ya karatasi hizo , lakini hio taarifa ilikuwa sio ya kawaida.

**********

Upande wa hoteli ya JR , Kizwe aliweza kurudi kwenye mwonekano wake ule ule aliokuwa nao kabla ya kubakwa , kwa upande wa Lekcha alikuwa amebadilika sana kimwonekano kwani aliweza kuwa msafi mno na kuwa na mavazi mapya ambayo yalimfanya kuwa Handsome.

Hata Kizwe mwenyewe alishangazwa na muonekano mzuri wa Lekcha, licha ya kuwa na mguu wa bandia lakini mavazi ya suti yalikuwa yamemkaa vyema sana, kiasi kwmaba huwezi kumfahamu kama siku ya jana tu alikuwa akiokota makopo.

Siku hio ya asubuhi baada ya jana yake kuhamia ndani ya hoteli hio ya JR ,Kizwe aliweza kumpeleka Lekcha saluni kwa ajili ya kuwekwa sawa mwonekano wake , Kizwe alifanya mambo kwa tahadhari sana na hata yule msaidizi wake almpa maagizo ya kuondoka na kujifanyisha hajui mahali alipo, sasa haikueleweka Kizwe alikuwa na mpango gani kichwani, lakini baada ya kuamka alivaa hijab na miwani na kisha wakatoka na Lekcha Kwenda saluni.

Baada ya wawili hao kurudi hotelini mara baada ya Lekcha kuwekwa mwonekano wake sawa , Kizwe alijikuta akimwangalia Lekcha kama vile amekuwa mtu mpya kwake , alimwangalia kwa madakika kadhaa na alijikuta akishindwa kuvumilia na kumvaa Lekcha mdomoni na kuanza kupeana mabusu nyevu ambayo yaliamsha hisia za Lekcha zilikolala na dakika kumi zilikuwa nyingi sana kwani Kizwe alianza kulalamika kwa raha alizokuwa akipata kutoka kwa Lekcha, haikueleweka alikuwa ameshapona maumivu ya kubakwa jana yake , lakini wakati huo alionekana kuwa kwenye ulimwengu mwingine na alichokuwa akihisi kwenye mwili wake sio maumivu bali ni raha isioelezeka.

Dakika ishirini mbele alishika shuka lililotandikwa kitandani na kulivuta kwa nguvu kwa mikono yote miwili huku akishindwa kuhimili hisia zake na kujikuta akitoa ukulele kwa sekunde na kisha kifua chake kikapanda na kushuka na kuanza kuhema kama mbwa aliekimbia maili nyingi na haikuwa kwake tu hata kwa Lekcha hivyohivyo alijikuta akihema sana na kisha alijibwaga pembeni na kulala chali , huku wote wakiwa uchi na safari yao ikawa imefika mwisho.
 
SEHEMU YA 387.

Edna hakuamini kama mama yake kifo chake kilikuwa ni cha kusababishwa na mtu , ijapokuwa alikuwa akipata hisia mbaya kila akikumbuka namna mama yake alivyougua ghafla na kufariki, lakini siku zote alikuwa ni mwenye kuomba jambo ambalo alikuwa akilihisi lisiwe kweli , lakini sasa ndio anapata kuujua ukweli kwamba kile alichokuwa akihisi kilikuwa ni cha kweli, moyo wake uliuma.

Hata Habari ya mama yake kuwa mjamzito wa mapacha ilifunikwa na Habari ya sumu.

Ripoti ambayo Edna alipata kuisoma ilikuwa ni ripoti ile ile ambayo Roma aliweza kuitambua kutoka kwa Dokta Robert , ripot ya Raheli kuwekewa sumu ambayo ilikosa matibabu ambayo ndio ilipelekea kifo cha Raheli.

Kwahio katika ripoti inayotoka kwenye karatasi hio ilimfanya Edna sasa kuelewa kwamba kifo cha mama yake kilisababishwa na mtu , lakini bado hakujua mtu huyo ni nani kwa maana kwamba mama yake hakuelezea Zaidi.

Edna baada ya kuomboleza kwa lisaa aliinua macho yake na kumwangalia Roma.

“Kwanini nahisi ulikuwa ukijua haya yote Roma?”Aliongea Edna na kumfanya Roma kufikiria kidogo na kisha akamwangalia kwa kumuhurumia

“Edna swala la mama yako nalifahamu , lakini sina muda mrefu tokea nilijue”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia kwa namna ya mshangao ni kama vile hakuwa akimfahamu Roma kuwa mume wake.

“Naomba usikasirike , kwasababu ushajua basi nadhani ni muda wa kukuelezea nilivyofahamu”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutingisha kichwa kumuashiria kwamba anamruhusu.

“Unakumbuka tukio la Salah kuja nyumbani kuwashambulia wakati nilipokuwa Japan?”Aliuliza Roma na kumfanya Edna kutingisha kichwa lakini kujiuliza kwa wakati mmoja tukio hilo linahusiana nini na mama yake.

“Unakumbuka pia ulishuhudia mwenyewe nikimuua Salah kwa mikono yangu?”

“Ndio nakumbuka na ndio tukio ambalo linanifikirisha mpaka leo hii na sikuwahi kujibu maswali yangu”Aliongea Edna na kisha Roma akaanza kumuelzea Edna kilichotokea , namna ambayo Christen alivyofika Tanzania mpaka kuja kuwaokoa , alimuelezea juu ya teknolojia ya ‘Ressurection Fluid’(Kimiminika) inavyofanya kazi kwenye mwili wa binadamu aliekufa , Roma aliendelea kumuelezea jinsi alivyochukua jukumu la kuanzisha uchunguzi wa kutafuta kujua ni kwaninin Raheli alihusishwa katika mpango wa majaribio na kampuni ya MAYA pamoja na INNOVA, Roma aliendelea pia kuelezea namna ambavyo uchunguzi ulivyofanyika mpaka kumfikia Suzzane.

Maelezo yote Roma aliomwambia Edna yalikuwa ya kushangaza sana lakini katika maelezo yote, kilichomuumiza sana ni kitendo cha mama yake kuwa katika mpango wa majaribio na kuwekewa hiko kimiminika ambacho kiligeuka sumu na kumuua

Roma alitumia Zaidi ya nusu saa nzima kumuelekeza Edna kila kitu na mpaka anamaliza Edna alitoa machozi vya kutosha , hakujua kwamba kipindi alichokuwa masomoni mama yake alikuwa akipitia mateso ya aina hio , jambo hilo kwake lilimuuma sana na alikuwa ni kama anamuona mama yake alivyokuwa akiteseka peke yake pasipo ya kuwa na mtu wa kumshirikisha.

Edna alijikuta akikumbuka siku ambayo mama yake alifika chuoni kwake kumtembelea mwezi mmoja kabla ya kufariki akitokeaMarekani na alijikuta hisia za maumivu zikimzidia na Roma aliweza kuona Edna anaweza kupatwa na shida na palepale alimfanyia uchawi wake na Edna akapotelea usingizini.

Roma alijikuta akipumua kwa nguvu , alijiua hayo yote yangetokea ndio maana hakutaka Edna kufahamu mpaka atakapo muona kuwa tayari kuukabili ukweli , lakini suzzane alionekana kuharakisha mambo na kuanza kumfungulia kodi Edna mpaka akafahamu uwepo wa ‘Deposti box’.

Roma baada kumpunguza nguo Edna alimlaza kitandani na kisha akamfunika vizuri na baada ya kumaliza alisogelea ile bahasha na kuangalia kama ndani kuna kitu cha ziada na ile anakung’uta kulidondoka kitu chini na alivyoangalia aligundua ni memori kadi.

Roma alishangaa kuona kikadi kile cha kuhifadhia taarifa na aliamini huenda kuna Zaidi ya taarifa ambazo ziliachwa.

Roma alichukua bahasha ile pamoja na memori ile na kisha akatoka kwenye chumba cha Edna na Kwenda kwenye chumba chake na baada tu ya kufika alitafuta kifaa cha kumsaidia kuingiza memori sehemu husika ili isome kwenye tarakishi iliopo ndani ya chumba chake.

Aliweza kufanya hivyo ndani ya dakika nne tu alifanikiwa na baada ya kuifungua tu ilionekana ilikuwa imefungwa kwa nywira , Roma alitabasamu na kisha akaandika passwoed ile ile aliomuona Edna akiingiza kule benki na memori ile ilifunguka na kumfanya kutabasamu.

Memori ilionekana kuwa na mafaili mawili , moja ilikuwa ni ‘Vidio file’ na faili lingine lilikuwa ni ‘Audio’ , Roma alianza na faili la Audio na kuanza kusikiliza mwanzo mwisho bila hata ya kutumia visikilizishi kwani aliweka kwa sauti.

Roma alichoweza kusikia ni kile kile ambacho Dr Elvice Danniel aliweza kusikia , ilikuwa ni sauti ya Raisi Barack Mabo pamoja na Raisi Kigombola pamja na sauti ya mtu alieitwa Chriss.

Agent 13, Agent 17 , Mpango LADO”Ndio vitu ambavyo vilimfanya Roma mwili wake kumsisimka ajabu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kama kitenesi huku hasira zikianza kumzidia kiasi kwamba mwili wake ulianza kutoa mvuke na palepale macho yake yalibadilika rangi na kuwa ya njano kwa sekunde kadhaa na kisha akarudi kwenye hali yake ya kawaida.

Roma alionekana kuweza kufanikiwa kuutawala mwili wake ndani ya sekunde tu mara baada ya kuhisi mabadiliko na moyo wake ulianza kudunda kawaida na alijituliza , alijikuta akishukuru sana kuweza kufikia levo ya Mzunguko Kamili kwani kama sio hivyo asingeweza kujiongoza na kuruhusu hisia kumtawala na kubadilika mwili wake na kufanya mambo ya ajabu , hata yeye hakujua kwanini moyo wake uliweza kupitia mabadiliko ya ghafla mara baada ya kusikiliza sauti hizo.

Ukweli ni kwamba Roma hakuwa na uelewa wowote wa mpango LADO kabisa kama una muhusu yeye na ndio kwanza anasikia hayo maneno tena kutoka kwa raisi Barack Mabo , lakini jambo moja ambalo lilimhakikishia kitu ,ni kwamba kutajwa kwake kama Ajenti namba 13 na Ajenti 17 ni jambo ambalo linamfanya kujua kwamba huenda kilichokuwa kikiendelea kule kisiwani ndio kinachohusiana na neno hilo la mpango LADO.

Roma alijikuta akikaa chini na kuanza kufikiria na hata kusahau kama kuna faili lingine ambalo hakuliangalia , alianza kukumbuka Maisha yake ya nyuma na Seventeen , ijapokuwa hawakuwa na kumbukumbu zote za kilichotokea kwenye kile kisiwa lakini alikuwa na baadhi ya kumbukumbu , alikumbuka Maisha ya kwenye kisiwa vyema kabisa mpaka siku ambayo aliweza kutoroka pamoja na Seventeen.

Roma kumbukumbu za utoto wake alizokuwa nazo ni za kisiwani yeye alikuwa na miaka kama kumi nan ne na Seventeen akiwa tayari ni mkubwa kabisa wa miaka kama kumi hivi na alikuwa akijitambua kabisa , sasa unachotakiwa kuelewa mpango LADO wakati unaanzishwa Seventeen alikuwa na siku zisizozidi tatu tokea kuzaliwa kwake , kwa maana hio ni kwamba Roma hakuwa na kumbukumbu za miaka Zaidi ya kumi nyuma.

Na Roma anafahamu amekutana na Seventeen wakiwa tayari ni wakubwa , lakini kuna Zaidi ya kumbukumbu ambazo zimefutwa za wakati wote wa mwanzo wa mpango LADO.

*********

ATLANTIC OCEAN-ISLAND X

PROJECT LADO MONITORING

CENRE(PLMC)

Ni ndani ya chumba cha ufuatiliaji wa projekti LADO ndani ya kambi ya siri duniani iliopo chini ya Zeros organisation , watu walikuwa wakiendelea na majukumu yao kama kawaida , huku wengi wao wakiwa bize , lakini pia kuna wale ambao hawakuwa bize.

Sifa moja ya hii kambi ni kwamba kila kinachoendelea katika mipango inayoendeshwa huwa inafatiliwa kwa masaa yote , hivyo watu walikuwa wakifanya kazi kwa ‘Shift’.

Katika idara ya PLMC kulikuwa na zamu ya watu watano watano wanaofanya kazi kwa kupokezana , idara hii ilikuwa ikisimamiwa na watu wawili Carlos Franklin pamoja na Dyana Tighert.

Diana Tighert ndio kiongozi mkuu akitoka Carlos na ndio mfanyakazi pekee ambaye ana umri mkubwa na alikuwa na miaka Zaidi ya ishirini na tano tokea aanze kufanya kazi chini ya Zeros Organisation.

Inasemekana mwanamama huyu alikuwa ni jasusi wa idara ya MI6 kabla ya kujiunga na Zeros organisation na alikuwa chini ya idara hio kama mwanasayansi upande wa tafiti na uwezo wake ndio ulioweza kumuweka juu ya wenzake katika idara hii ya PLMC.

Upande wa Carlos yeye alikuwa ni muamerika mweusi na Carlos tofauti na wenzake wote alikuwa ni mwanasayansi ambaye alitoka FBI katika idara ya Forensic investigation, uwezo wa Carlos ulikuwa mkubwa sana na ndio maana aliingizwa katika mpango LADO.

Viongozi hawa wa juu ni watu ambao wanajivunia sana na kazi yao na wanachokifanya kinawapelekea kuhisi kama wao ndio wanaoendesha dunia ,Zeros organisation ndio taasisi ya siri ambayo ilikuwa ikifahamu kuhusu uwepo wa miungu watu ndani ya dunia , viumbe ambavyo vimetoka katika sayari nyingine.

Hio ni siri kubwa ambao imetunzwa miaka na miaka hivyo jambo hilo lenyewe linawafanya kuwa sehemu ya watu wanaofahamu siri hio na kuna idara Zaidi ya kumi na mbili ndani ya Zeros organisation ambazo zinafatilia kwa ukaribu miungu yote , hivyo hio Zeros haikuwa kwa Hades pekee au Agent 13 na 17 kama wanavyotambulika bali kuna idara zingine.

Sasa muda wa saa kumi na mbili kamili kabla ya zamu ya waliongia usiku kuisha vijana watano waliokuwa ndani ya idara ya PLMC waliokuwa wakikodolea macho skrini zao, walijikuta wote kwa pamoja wakishituka kwa pamoja baada mistari flani iliokuwa ikicheza cheza kwenye skrini zao kuonyesha kupitia babadiliko yasiokuwa ya kawaida kwa sekunde kadhaa na kisha kurudi katika hali ya kawaida.

Vijana hawa watatu wakiwa ni wanaume na wanawake wakiwa ni wawili walijikuta wakiangaliana na palepale mmoja alisimama.

“Nitamtaarifu Director”Aliongea na kumfanya wale wengine wote kukubaliana nae na palepale alichukua simu yake na kuingiza namba na kuweka mkonga sikioni.

“Agent 13 activated his energy Sir … Okey”Aliongea na kisha kurudisha mkonga chini na wenzake wote wakamwangalia.

“Amesemaje?”

“Wanakuja?”

“Anakuja au wanakuja?”

“Amesema anamtaarifu na Madam Dyana”aliongea na wote kwa pamoja wakacheka.

Ndani ya madakika kadhaa tu alifika mwanamama Dyana pamoja na Carlos huku wote wakiwa kwenye mavazi ya kuchukulia mazoezi na jasho lilionekana kuwatoka.

“Nini kinaendelea?”

“Ajent 13 inaonekana kutumia uwezo wake”Aliongea na kisha alirudisha kile kilichotokea ambacho kimerekodiwa kwenye skrini na wote kwa pamoja waliangalia.

“Amefikisha levo ipi?”

“Yellow Sir”Alijibu mwingine na Carlos na Diana waliangaliana.

“Ametumia kwa sekunde 5 tu na kurudi kwenye hali yake ya kawaida , unafikiri inamaanisha nini?”

“He is angry”Alijibu Carlos akimaanisha kwamba yupo kwenye hasira.

“Wasiliana na Jasoni kujua ni kipi kinaendelea”Aliongea na mmoja wa wale vijana alibonyeza tarakishi yake kwa haraka sana na ndani ya dakika moja tu mawasiliano yaliunganishwa Kwenda kwa Jason.

“Jason nini kinaendelea , Ajent 13 ametumia uwezo wake leo hii”

“Madam tunazo picha za matukio ya leo , lakini hakuna cha ziada ambacho kimeonekana kutokea”Aliongea Jasoni kwa njia ya video na alionekana upande mwingine aliokuwepo ni kama yupo kwenye ndege chumba cha Rubani kutokana na vifaa vilivyomzunguka.

Muda ule ule picha mbalimbali zilianza kuonekana kwenye skrini zao , moja ilimuonyesha Roma akitoka nyumbani muda wa asubuhi Kwenda kazini , nyingine zilionyesha Roma akiingia ndani ya kampuni , nyingine baada ya kutoka , nyingine akiwa aningia ndani ya jengo la benki ya Swiss akiwa ameambatana na Edna mke wake, hata baada ya kutoka na Kwenda nyumbani.

“Ajent 13 amebadilika sana na hajaua mtu kwa muda mrefu , wote tulitarajia atamuua yule mwanamke lakini alimuacha hai , lakini leo hii hali yake imebadilika , nini kinaendelea?”

“Madam ukilinganisha data zetu zilizopita na za leo , Ajenti 13 ametumia sekunde tano tu kuweza kutumia uwezo wake na kuwa wa kawaida , inaonyesha kabisa anakuwa binadamu wa kawaida , tumejaribu kufanya utafiti wa mapigo yake ya moyo kwa muda wa wiki moja na juzi tumeweza kuona mapigo yake yameshuka chini sana na kufikia sawa na ya binadamu wa kawaida”Aliongea mwanadada alievalia mwiani na tisheti lake la rangi ya bluu lenye nembo ya Sifuri.

“Kuna kitu kinaendelea …”

“What is it Diana?”

“Siwezi kujua Carlos , ila kama hali kama hii itaendelea siku za mbeleni tutashindwa kabisa kumfuatilia na hilo litakuwa jambo la hatazi Zaidi, ila tunatakiwa kuwa makini endapo atarejewa na kumbukumbu ambazo hatutaki kuzikumbuka”Aliongea Diana.

“Kwahio tunafanya nini?”

“Ngoja ni wasiliane na Mheshimiwa anipe maelekezo, Dhoruba nyekundu watakuwa na chakufanya”Aliongea Diana.

“Kazi yetu imekuwa ya upande wa kisayansi Zaidi , lakini likia swala la Field wanahusika Redstorm, nafikiri kwasasa tuendelee na kazi yetu ya ufatiliaji kama kuna mabadiliko tutaweza kuarifiwa”Aliongea Carlos na kish ana yeye akatka akifuatishana na Diana.

“Mnadhani ni kweli Ajent 13 anaweza kuwa binadamu wa kawaida?”

“Haiwezekani kuwa wa kawaida lakini itafikia hatua mwili wake kuwa kama wa binadamu wa kawaida”Aliongea mwanadada mmoja.

“Makumbuka maneno ya Dr Naira”Aliuliza mwingine.

“Wote tunakumbuka alisema itafikia hatua ya kufikia hii kambi kuisambaratisha na huo wakati hakuna ambaye ataweza kujua amefikaje”

“Mnafikiri kadri anavyoonekana kuwa binadamu wa kawaida ndio anavyokuwa hatari Zaidi?”.

“Ndio maana umeona Madam Diana alivyo na wasiwasi wote tuliweza kumfahamu kutokana na data zinazoingia , lakini sasa hivi data zinaingia na hatuwezi kuzitafsiri , hili ndio jambo la hatari ambalo naamini hata wakubwa wanalifohofia”

“Natamani hio siku kufika , niweze kutoka kwenye hili gereza”Aliongea mwenzake na wakaangaliana, lakini walikuja kukatishwa maongezi yao mara baada ya wenzao wengine kufika awamu hii wasichana walikuwa ni watatu na wanaume walikuwa wawili.
 
SEHEMU YA 388.

Roma sasa anajua mpango uliomfanya kuwa tofauti na binadamu wa kawaida ndio huo unajulikana kwa jina la mpango LADO , lakini hata hivyo anashindwa kujua mwanzo wa mpango huo ilikuwaje , kwani kwenyye sauti alioweza kusikia ni jina lake tu pekee likitajwa pamoja la Seventen kufanana na Edna , kwa ufupi Roma hakuwa na uelewa kama mpango LADO ulianzia kwa kupotea kwa ndege ya shirika la M Airline.

Roma hakuwa na uelewa kwamba watu waliohusika na mpango huo na babu yake Afande Kweka alikuwa akihusika kwa asilimia mia moja na ndio aliekuwa mratibu mkuu wa kumwingiza huko yeye na Seventeen .

Roma hakuwa akijua kama Hades za Zamani alikuwa akimwandaa kuwa mrithi wake tokea zamani na mpango wake kufanikiwa , Hakuwa akitambua pia kuwa adui yake mkuu ambaye mawazo yake yote yanatakiwa kumfikiria ni Athena kutokana na mipango yake ya kutaka kuibadilisha dunia.

Mambo mengi yalilikuwa yakitokea pasipo yeye kujua na yote hayo yaliwezekana kutokana na kwamba watu waliomtengeneza walikuwa makini na kazi yao na walikuwa wakitumia akili nyingi sana kuendeleza kile walichokianzisha na kufanya kiendelee kubakia siri na huenda hata Maisha yake ndani ya Tanzania ni kwasababu wameruhusu au hawakuwa na namna ya kumzuia kutoishi Tanzania kutokana na kwamba wangeweza kumpa akili ya kutaka kujua kilichotokea miaka mingi nyuma.

Zeros Organisation na Dhoruba Nyekundu ni taasisi shirikishi ambazo zinafanya kazi kwa usiri mkubwa sana na kuhakikisha kila mpango wao unafanikiwa na hili linawezekana kutokana na kwamba hawakuwa wenyewe bali walikuwa wakipata sapoti kutoka kwenye mataifa mengi ndani ya dunia , mataifa ambayo yana nguvu katika Nyanja zote.

Roma aliketi kwenye sofa ndani ya chumba chake huku akirudia rudia kusikiliza faili lile la Audio , aliweza kufanya hivyo kwa mara tatu zote na kuweza kupata baadhi ya taarifa kupitia hio Audio , jambo la kwanza aliloweza kugundua, ni juu ya Mpango LADO , alitaka kujua angalau ilikuwaje huu mpango akawa ni mhusika yeye na Seventeen na sio watu wengine , lakini pia alitaka kujua Serikali ya Marekani wanahusikaje na mpango LADO , lakini pia alitaka kufahamu ni kwa vipi hio Audio File ikamfikia Raheli, Roma hakuwa mjinga , alikuwa akielewa ulinzi na teknolojia ya hali ya juu ya serikali ya Kimarekani, hivyo hata kama walitumia ikulu ya Tanzania , ni ngumu sana mazungumzo ya raisi wa taifa hilo kuvuja labda tu iwe kuna mbinu Zaidi ya zile ambazo serikali ya Marekani inazifahamu na ndio maana jambo hilo likaweza kufanikiwa.

Kuna hisia mbaya ambazo alikuwa nazo kwenye moyo wake , lakini hakutaka kuzitilia maanani kwa wakati huo , alikuwa na watu ambao wanaweza kuchambua kwa undani file hilo la sauti za watu na kufanya uchunguzi wa kina na kutoa majibu na watu hao ni The Eagles pekee.

Ukweli ni kwamba Roma licha ya kwamba alikuwa akijiuliza ilikuwaje akawa na maisha aliokuwa nayo , Maisha ya kuingizwa maabara , Maisha ya kuishi kisiwani peke yake yeye na Seventeen , Maisha ya kuwa na mwili usiokuwa wa kawaida kutokana na damu yake kuwa na kirusi.

Lakini sasa mara baada ya kukutana na Hades wa Zamani na kupewa uongozi wa juu na umiliki wa visiwa vya wafu , hakupenda sana kufatilia nini kilitokea mpaka akawa na maisha aliokuwa nayo, hakutaka kufuatilia kwanini hakuwa na kumbukumbu za utoto wake , kiasi kwamba hata wazazi wake hakuwa akiwakumbuka, ijapokuwa aliweza kurudi nchini Tanzania kwa ajili ya kufuatilia asili yake , lakini hakuwa na mpango wa kuchimba yaliopita kutokana na kutafuta familia yake.

Lakini sasa wakati ule na huu ni tofauti , sasa hivi alikuwa na familia tayari , alikuwa na mke na alikuwa na mtoto Lanlan , lakini alikuwa na watu wengi anaowapenda ambao usalama wao ulikuwa ni wajibu wake , aliwaza kama akiendelea kuwa katika kiza kinene basi itafikia wakati atashindwa kuwalinda wale anaowapenda na kama kutatokea jambo ambalo litahatarisha Maisha ya wapendwa wake , basi atakuwa ni mtu wa majuto makuu kuliko alivyoshindwa kumlinda Seventeen.

Jambo lingine ambalo aliweza kulifikiria ni kikadi ambacho Suzzane alimpatia , kikadi ambacho kilikuwa na nembo ya visiwa vya wafu pamoja na jina lake , Roma alikuwa akikumbuka kabisa kutoka kwenye maneno ya Suzzane kwamba nyaraka zile zilipaswa kupewa yeye kwa maana kwamba ni kama alikuwa akisubiriwa , hivyo maswali mengi yalizidi kukijaza kichwa chake , alijiuliza kama kikadi kile ni kweli kilikusudiwa kupewa yeye basi hata faili aliloacha Raheli lilikusudiwa kwake , lakini kama ni Raheli ndio aliekusudia kumpatia faili hilo kamfahamu vipi , Roma aliona hakuna namna ya Raheli kumfahamu na jibu ambalo aliona linaweza kuleta mantiki ni Hades wa Zamani kuhusika, kama alivyohusika kwa Mellisa , Tajiri Khalifa na wengineo.

“Kuna jambo sijawahi kufuatilia kuhusu Hades wa Zamani , nahisi jambo hili Christen analifahamu”Aliwaza Roma huku akiamini huenda Christen alikuwa akifahamu chochote kuhusu mipango ya Hades wa Zamani ambayo yeye hakuwa amemwambia.

Roma alijiambia ni lazima amtafute Christen ili amuulize baadhi ya vitu ambavyo hakuwa akivifahamu kutoka kwa Hades wa Zamani , kwani walikuwa na ukaribu mkubwa tena ukaribu wa mapenzi.

Roma hakutaka kwanza kuchosha Zaidi kichwa chake , alitaka kuweka kwanza swala alililogundua kiporo kwani kuna maswala mengi ambayo hakuwa akiyajua.

Baadaa kutulia aligeukia faiili lingine sasa , faili hili lilikuwa ni lile ambalo kuna Vido ndani yake ,Roma aliichezesha Vidio ile na palepale ilionekana sura ya mwanamke mrembo , ijapokuwa mwanamke aliekuwa akionekana kwenye skrini umri ulikuwa umeenda kidogo , lakini urembo wake haukuwa umepotea sana.

Alikuwa ni mama yake Edna , Raheli Adebayo ndio aliekuwa kwenye Skrini iliokuwa mbele yake na mpaka hapo alijua faili hili lilikusudiwa moja kwa moja Kwenda kwa Edna.

Roma aliangalia Vidio yote yenye dakika tano na kujikuta hata mwonekano wake kuwa sio wa kawaida kabisa , maneno aliokuwa akiongea Raheli kwenye hio vido yalimfanya kuhisi uchungu uliojaa huruma nyingi , yalikuwa ni maneno ya huzuni sana ambayo Raheli alikuwa akiongea akimwambia mtoto wake Edna , Roma alijiambia Edna akija kusikiliza kila kitu alichoongea mama yake basi hali yake itakuwa mbaya Zaidi.

Huu sio wakati mzuri kwa Edna kujua kila kitu , nitamuelezea wakati akiwa tayari kuukabili ukweli, kilichopo humu ndani nitakifanyia kazi kimya kimya na kujua ukweli wote ndio nitakapo muambia , kwa jinsi Edna alivyo akifahamu hili , ataishi Maisha kama ya mama yake, maisha ya kulipiza kisasi jambo ambalo halitakuwa na faida kwake”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake huku akitoa ile memori kadi mkononi na kisha akaihifadhi.

Roma baada ya kutuliza kichwa chake, aliingia bafuni na kuoga na kisha akajitupa kitandani na kupotelea usingizini , hakuwa akitaka kukumbuka kabisa alichosikia na kuona , kwa wakati huo alitaka kwanza kupotezea , kuhusu Edna alijua atalala masaa mengi kidogo , hivyo hakuwa na wasiwasi lakini aliamini Edna akiamka itakuwa habari nyingine.

Muda wa jioni Roma aliamka kutoka usingizini na kisha alijisafisha na kujiandaa kwa ajili ya Kwenda kumuona Rose , alikuwa akikumbuka ahadi yake na Rose hivyo hakutaka kutoitimiza.

Roma muda mwingine alishukuru sana kuwa na wanawake waliokomaa akili kwani kama si hivyo asingeweza kugawa muda wake na kuwa nao kwa wakati na ndio maana kama mmoja wao ataamua kumpigia na kumuhitaji basi ni lazima angalau atimize ahadi.

Roma alitoa maagizo ya Edna kutoamshwa mpaka atakaporudi na ndipo alipoanza safari ya kuelekea Mbagala Rangi tatu.

Dakika chache tu mbele aliweza kufika Club B , Roma alikuwa na muda mrefu kidogo hajafika hapo na hio ni kutokana na kwamba mara nyingi alikuwa akikutana na Rose nje ya eneo hilo la biashara.

Ilikuwa ni muda wa saa moja, hivyo watu walishaanza kujaa na kuchangamsha eneo lote , Roma alishangazwa na mabadiliko ya eneo hili kwani sehemu ilikuwa ikipendeza Zaidi ikiashiria Rose alifanya baadhi ya maboresho.

Roma alinyoosha moja kwa moja mpaka vyumba vya VIP kwa ajili ya kumtafuta Rose na hio ni mara baada ya Zonga kumpatia taarifa kwamba Rose yupo upande wa pili.

“Hubby!”Aliita Rose na kumfanya Roma kushangaa kwani hakuwa Rose peke yake ndani ya eneo hilo bali alikuwepo na Dorisi pia.

“Dorisi unafanya nini hapa?”Aliuliza Roma akimwangalia Dorisi aliekuwa ameketi kwenye sofa akiwa ameshikilia glasi ya mvinyo mwekundu.

“Mimi na Rose ni marafiki nimekuja kumtembelea”Aliongea Dorisi na kumfanya Roma kushangazwa na jambo hilo na kujiuliza wawili hao urafiki wao ulianza lini kwani hakuwa na taarifa kama washawahi kukutana tofauti na kwenye mashindano ya Kizazi nyota yaliofanyika wiki kadhaa zilizopita.

Roma ilibidi asogee na kisha akaketi kwenye sofa huku akiwaangalia wanawake wake wote wawili walivyokuwa warembo na kupendeza kuwa pamoja.

“Hubby! Usiniambie hupendi sisi tukiwa marafiki?”

“Sio kama sipendi ila nimeshangazwa kwa nyie kuwa marafiki”

“Ni kwasababu muda wote uko bize na mkeo na kututelekeza , ndio maana hujui hata ni kipi kinaendelea kwenye Maisha yetu”Aliongea Rose na kumfanya Roma kujihisi ni mwenye hatia.

“Babe unajua tofauti na wenzangu , mimi ndio ambaye ninakuona mara chache sana , Dorisi unafanya nae kazi kwenye kampuni moja hivyo ni rahisi kuonana, Nasra na Amina pia lakini mimi pekee ndio ambaye naishi huku pembeni ya jiji , huwa nakumisi sana lakini nashindwa kuchukua…”Rose aliishia katikati baada ya Roma kumsogelea na kumpiga busu na kuishia kutoa macho.

“Babe Rose haina haja ya kuendelea kulalamika , najua sikutendei vizuri kama mpenzi wako na nimekuwa mbinafsi siku zote kwa kujali nafsi yangu, hili mimi mwenyewe linanifanya kua mwenye hatia juu yako na kwa wengine wote”

“Ndio maana tumeamua kukuita kukushirikisha mbinu ambayo inaweza kutatua changamoto yetu”.

“Mbinu gani hio?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Rose anahamia nyumbani kwangu Kimara na tutaanza kuishi pamoja nimechoka kuishi peke yangu ndani ya lile jumba”Aliongea Dorisi na kumshangaza Roma na wote kwa pamoja wakamuangalia.

“Mnamaanisha au mnanitania?”

“Mimi na Dorisi ni marafiki na tunashare mwanaume mmoja, hakutakuwa na ubaya kama tukiishi sehemu moja itakupunguzia safari za kuja huku”Aliongea Rose na kujikuta akitabasamu kifedhuli , hakuelewa vichwa vya hao wanawake vinafikiria nini , lakini mpaka hapo aliona ni jambo la kheri kwake na hakuna ubaya.

Picha ya kulala na wanawake wawili kwa wakati mmoja ilimjia akilini na kujikuta mwili ukisisimka , ijapokuwa sio mara yake ya kwanza kufanya hivyo lakini alikuwa na muda mrefu hajafanya hivyo.

“Rose vipi kuhusu hapa, ulijenga karibu ili kusimamia club yako?”

“Hapa napanga kumuachia Zonga , nataka niachane kabisa na maswala ya Club pamoja na kuongoza kundi langu na kazi zote afanye Zonga kwa kushirikiana na wenzake”

“Rose anapanga kufungua duka la nguo na urembo Ubungo , hivyo kukaa kwangu ni karibu Zaidi na sehemu yake ya kazi”Aliongea na kumfanya Roma kuelewa.

“Mimi sina tatizo kama Rose ndio unachopenda kufanya hakuna shida , isitoshe nitainjoi kuwa na warembo wangu wote kwenye kitanda kimoja”Aliongea Roma huku akiweka tabasamu lililojaa ufedhuli ndani yake , mawazo yake yote aliokuwa nayo yalimpotea kabisa baada ya kukutana na warembo hao lakini kubwa Zaidi kilichomfurahisha ni Rose na Dorisi kuwa na mpango wa faida kwake.

“Wewe mwanaume huna aibu umeshindikana , unaongeaje hivyo bila hata ya kupepesa macho”Aliongea Dorisi na kisha akamwangalia Rose na kujikuta wote wakacheka.

Ilionekana Roma alichoitwa hapo ni huo mpango wa Dorisi kuishi na Rose na hakukuwa na lingine, Roma hakuwa tayari kupoteza sana muda hapo , alikuwa akipanga kuondoka mapema ili kumrudia Edna , alijua akiamka atakuwa na maumivu hivyo angalau anatakiwa kuwa pembeni yake.

“Malkia wa biashara hajambo?”

“Edna mke wangu yupo kwenye wakati mgumu napanga kurudi mapema leo”Aliongea Roma na kuwafanya kushangaa.

“Ana shida gani?”

“Jambo lile unalofahamu Rose kuhusu mama yake”.

“Maskini.. !Ndio amefahamu leo?”Aliuliza na kumfanya Dorisi kuchanganyikiwa kwani hakuwa akijua lolote.

“Dorisi nadhani haufahamu kilichotokea , Rose atakuelezea sina mpango wa kukaa sana hapa , Rose kama kuna shida yoyote kwenye biashara yako utanieleza”

“Usijali kuhusu biashara yangu kwa muda huu, ningejua Edna yupo kwenye tatizo nisingekuita”

“Uliniambia kabla hajafahamu ndio maana nimeona kutimiza ahadi”Aliongea Roma na kisha alimkiss Dorisi kwa kumshitukiza na kuaga.

Sasa wakati Roma anatoka hapo ndani akiingia upande wa korido ya vyumba vya VIP alijikuta akikutana na mtu ambaye hakutarajia kumuona hapo ndani kwenye hio Bar, ni kama alikuwa akimfananisha lakini alipomkaribia alikuwa ni yeye kabisa, akiwa ameongozana na mwanaume ambaye hamfahamu.

“Naona umeamua kuishi na aibu nilitegemea mpaka sasa ungekuwa mfu”Aliongea Roma mara baada ya kuwafikia.

Haikueleweka Kizwe alikuwa akifanya nini ndani ya Club B usiku huo , lakini alikuwa hapo akiwa ameongozana na Lekcha , Kizwe alikuwa amevalia suti pamoja na hijab kichwani na miwani nyeusi , huku Lekcha yeye akiwa amevalia shati la mikono mifupi la mfano wa jeans pamoja na miwani , alikuwa amependeza haswa.

Kizwe ndio aliekuwa wa kwanza kumuona Roma na alisimama kwani hakumtegemea kumuona ndani ya eneo hilo na hata mabadiliko yake ya ghafla yalimshangaza Lekcha.

Unachotakiwa kuelewa Club B haikujengwa kwa ajili ya watu kunywa bia tu kwani ilikuwa na eneo la watu wengi ambalo limekaa kama Bar za kawaida lakini pia ilikuwa na Vyumba ambavyo watu ambao walitaka kupata vinywaji kwa hali ya utulivu walikuwa wakilipia na hii ndio sifa kubwa ambayo ilivumisha sana Club hio , ijapokuwa haikuwa kama Casino , lakini ilikuwa ni ya hadhi kubwa, sasa kuna mageti mawili ya kuingilia ndani ya Club hio , kuna geti la mbele na geti la mwanzoni kabisa mwa barabara , geti la mwanzoni ndio linakuunganisha moja kwa moja ndani ya Bar lakini la mbele linakuunganisha moja kwa moja na vyumba VIP , lakini unaweza kupitia geti la mwanzoni kuingia vyumba vya VIP na Roma ndio njia yake siku zote kila akifika anapita geti la mwanzoni na kisha kuingia vyumba vya VIP.

Moja ya faida kubwa ambayo Rose anaipata ndani ya Club B ni kwenye vyumba hivyo vya VIP , kwani watu hawatumii tu kulewa bali pia mazungumzo ya biashara haramu yalikuwa yakifanyikia humo.

Sasa ukisikia koneksheni za ‘Black Market’ ni rahisi kuipata ndani ya Club hii na Rose alikuwa na Koneksheni zote na hiki ndio ambacho kilikuwa kikimpatia sana hela ukiachana na biashara ya madawa ya kulevya.

Makundi mengine ndani ya Dar kwa mfano Black Mamba yenyewe yalikuwa na koneksheni ya ‘Black Market’ , lakini kutokana na Roma kuwapunguza nguvu hivyo ndani ya Club B ndio sehemu iliokuwa ikiaminika Zaidi, Rose alikuwa na takribani vyumba Zaidi ya therathini ndani ya eneo hilo , vingine alivifanya kama vya kulala na vingine kama ofisi ndogo za mazungumzo.

Lekcha baada ya kumsikia sasa Roma akiongea ndio aliweza kugundua ni kwanini Kizwe alibadilika na kuonekana kama mtu aliepandwa na jaziba ghafla.

“Bahati mbaya sikuweza kufa kama ulivyotegemea”Aliongea Kizwe , ijapokuwa alikuwa na hasira na Roma lakini alikuwa akimuogopa pia , alikumbuka kila kitu kilichotokea kule Bagamoyo mpaka kujikojolea na kunya kabisa.

“Kwa jinsi mnavyoonekana nahisi kabisa huyu mwanaume ndio kakusaidia?”Aliongea Roma huku akimwangalia Lekcha.

“Why Do you care”Aliongea Lekcha kwa jeuli.

“Lazima niwe najali , mimi nilichokuwa nataka ni huyu mwanamke kujiua yeye mwenyewe kwa aibu”

“Hajakufa sasa na mimi ndio nilimuokoa una kingine cha kuongea?”Aliongea Lekcha kwa majigambo, lakini upande wa Kizwe alitamani kuwa na nguvu za ziada au hata siraha ammalize pale pale Roma , lakini hakuwa na ujasiri hata wa kutamka neno.

Roma alijikuta akitabasamu na kushangazwa na namna ambavyo Lekcha anajiamini , Roma mara nyingi ashawahi kukutana na watu wanaojiamini lakini Lekcha alikuwa ni mwenye kujiamini mno kuliko wote na alimwangalia machoni kabisa.

Kizwe alikuwa na wasiwasi , alijua huenda Roma akaendeleza unyama wake na hakutegemea pia kama anaweza kukutana nae maeneo hayo akiwa kwenye harakati zake za kulipiza kisasi..

“Kwanini ulimsaidia pasipo ya kumjua?”Aliuliza Roma.

“Kwasababu nilikuwa na uwezo wa kumsaidia hakuna sababu nyingine”Aliongea kwa Kingereza.

“Unampenda?”Aliuliza Roma na Kizwe macho yote kwa Lekcha ambaye alionekana kunywea ghafla.

“Unajali nini kama nampenda au simpendi, umesema ulitaka ajiue na nimemuokoa nadhani haina haja ya kuendelea kumkandamiza, ulichofanya kwake kinatosha”

“Okey! Umeongea sahihi , sina haja ya kumkandamiza mwanamke hivyo nitawaacha na mambo yenu , lakini nakushauri uwe makini?”Aliongea Roma na kisha kuwapita.

“Kwanini niwe makini , kama mimi ndio niliemsaidia unafikiri anaweza kunifanya chochote kibaya?”

“Nadhani hujanielewa sijakuambia uwe makini na yeye bali uwe makini na mimi” Aliongea Roma na kisha aliachana nao na kuendelea na safari , hakutaka tena kumjali Kizwe kwani alijua asingemfanya lolote kwa kwakati huo kutokana na kuwa na udhaifu wake , lakini alishangaa Kizwe kuweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida na kuonekana kama hakuna kilichotokea , aliamini huenda Lekcha akawa na ushawishi usiokuwa wa kawaida mpaka kumuweka sawa.

Kizwe alijikuta akiguswa na namna ambavyo Lekcha alisimama kwa ajili yake , ukweli ni kwamba Kizwe licha ya kuwa mume wa Jeremy lakini hakuwa akihisi ni mwenye kupendwa tokea siku alipogundua Jeremy mume wake anatoka kimapenzi na Raheli rafiki yake , kuanzia siku hio matazamo wake ni kama ulibadilika na ndio maana hakujiheshimu kama mke na kuamua kutoka kimapenzi na Raisi Kigombola na Allesandro Bianchi mkurugenzi wa Innova kwa ajili ya kutimiza tu azma yake.

Lakini Kizwe kwa muda wa siku hizo mbili alizokuwa na Lekcha alijihisi kupenda na vilevile kupendwa, alijihisi kama amerudi miaka Zaidi ya ishirini nyuma wakati akianza kuyajua mapenzi.
 
SEHEMU YA 389.

Ni ndani ya dakika kadhaa tu tokea Kizwe kuingia ndani ya eneo hilo la VIP Club B , ziliingia gari tatu nyeusi aina ya Range Rover geti la mbele kiasi kwamba zilimfanya hata Zonga aliekuwa akisimamia wafanyakazi wengine kuwa na wasiwasi ,haikuwa kawaida kuona gari tatu kwa pamoja kuingia pamoja eneo kama hilo la starehe.

Wakati gari hizi zikiingia hapo ndani, muda huo huo Kizwe na Lekcha walikuwa wakitoka kupitia geti la mbele na ni upande huo huo ambao gari zilikuwa zimesimama na baada ya wawili hao kutoka kabisa kulisogelea gari lililowaleta , milango ya zile gari tatu ilifunguliwa na wanaume ambao wote walivaa suti kuwasogelea.

Kizwe alijikuta akihamaki , lakini kabla hajakaa sawa aliweza kumuona Miranda msaidizi wake akitoka kwenye gari iliokuwa nyuma kabisa na mpaka hapo aliweza kufahamu ni nini kinaendelea.

Na alimwangalia Miranda jinsi anavyotembea kumsogelea na alijikuta hasira zikimjaa , kuna hali iliokuwa ikimwambia watu hawa kumzunguka eneo hilo ni kitendo cha usaliti alichofanya Miranda.

“Madam samahani , lakini mheshimiwa ametoa oda ya kurudishwa Rwanda”Aliongea Miranda.

“Miranda umenisaliti..nilikuamini sana”

“Madam I am sorry natiii maagizo ya mkuu wa nchi”Aliongea Miranda na kisha aliwapa ishara wale wanaume Weusi walioavalia suti , walikuwa ni wanausalama kwa jinsi walivyokuwa wakionekana , sasa haikueleweka walikuwa ni wa kitanzania au wa Rwanda , bali Miranda ndio alietambulika kama Mrwanda.

Lakini pia haikueleweka ni sababu ipi iliowaleta Kizwe na Lekcha ndani ya Club B.

Baada ya Lekcha na Kizwe kuingizwa ndani gari hizo, ziliondoshwa haraka sana na kufanya eneo kutulia.

****

Raisi Jeremy mara baada ya kuangalia Vidio ambayo ilimshitusha na kumuumiza sana alijikuta akipandwa na ghadhabu kubwa kiasi kwamba kama sio Linda aliengia ndani ya ofisi hio kwa haraka kumtuliza, huenda angepatwa na tatizo la kiafya.

Linda mara baada ya kupata taarifa kwamba kuna barua pepe iliokuwa ikihusiana na Mke wa Raisin a kutumwa moja kwa moja kwa Jeremy alijua kuna tatizo na haraka alifika ndani ya ofisi ya Jeremy kuangalia ni nini kimetumwa na hapo ndipo alipomkuta Jeremy akiwa kwenye hali isiokuwa nzuri na kumtuliza kwa kutumia mbinu zake alizojifunzia kwenye kundi la Yamaguchi.

Baada ya kuona Jeremy katulia ndipo alipoangalia kilichotumwa na alijikuta akipagawa mara baada ya kuangalia Vidio ya mke wa raisi.

“Jeremy!!!”Aliita Linda kwa kumwangalia Raisi Jeremy ambaye alikuwa akihema kwenye kiti chake cha mzunguko.

“Usiniulize chochote maana sina majibu”Aliongea Jeremy kwa lugha ya Kinyarwanda.

“Sikuulizi mheshimiwa kuhusu hili nataka kujua maagizo yako?”Aliongea Linda kwa namna ya huruma mno, alikuwa akimpenda sana raisi Jeremy.

Linda tokea siku ambayo aliweka wazi mpango wa Lorraine kuhusishwa katika ndege ya M Airline yeye na Jeremy hawakuwa na ukaribu kama waliokuwa mwanzo na mara nyingi wakikutana ni maswala ya kazi basi jambo ambalo lilikuwa likimuumiza mno.Jeremy alijituliza kwa madakika kadhaa na kisha akamwangalia Linda

“Unashauri nifanye nini juu ya hili , Mke wangu aliaga anakwenda Tanzania kumsaidia mwanangu Edna, lakini leo hii zinakuja picha chafu za namna hii , kipi napaswa kuamua kwa sasa?”Aliongea Jeremy kwa hasira.

“Mheshimiwa huna namna ya kufanya maamuzi kwa sasa nadhani ni vizuri kama tukifahamu kilichotokea kabla ya kufanya maamuzi mengine , lakini wakati huo huo tukiendelea kumfatilia Madam kwa ukaribu”Aliongea Linda.

“Linda hili swala kama litasambaa mtandaoni itakuwa ni kashfa kubwa kwangu na kwa watu wote waliohusika nataka lifanyike kimya kimya na kwa umakini mkubwa . siku moja tu inawatosha kufahamu nini kilitokea nchini Tanzania na baada ya hapo nataka kumuona mke wangu hapa nchini”

“Sawa mheshimiwa”Alijibu Linda na kisha akaondoka.

Taarifa za kufuatiliwa kwa kile kilichotokea mpaka Kizwe kukutwa na mkasa wakurekodiwa akifanya mapenzi na watu walionekana kama vichaa zilibakia kwa Linda tu , lakini kutokana na kwamba Linda alitaka kujua kile kilichotokea Tanzania ili arudishe majibu kwa Raisi Jeremy haikuwa na jinsi kutumia majasusi waliokuwa Tanzania kufanya uchunguzi ni nini kimetokea mpaka mke wa raisi kukumbwa na kadhia ya namna hio..

Licha ya kwamba walikuwa na faili la Video chafu hio lakini hawakujua Kizwe alikuwa upande gani ndani ya jiji la Dar na ndio maana majasusi waliopewa kazi ya kumtafuta walimtumia Miranda ambaye ni msaidizi wa karibu sana wa Kizwe kwa kuamini kwamba kama Kizwe kuna mtu atawasiliana nae basi lazima atakuwa ni Miranda.

Sasa kitendo cha Kizwe kupiga simu kwa Miranda kumfuata Mbagala alikuwa akijiingiza mwenyewe kwenye mtego kwani Miranda na vijana wa usalama wa taifa la Rwanda na mpaka Miranda anamtoa bosi wake na kumpeleka JR hoteli vijana walikuwa nyuma yake.

Mara baada ya Miranda kuwafikisha Kizwe hotelini wakati wa kutoka alidakwa na wanausalama na kupelekwa moja kwa moja mpaka Msasani ubalozini kwa ajili ya mahojiano.

Miranda alibanwa kisawa sawa kwa zaidi ya masaa tisa , mwanzoni hakuwa tayari kuongea chochote kinachohusiana na bosi wake , lakini mara baada ya kuongea na raisi Jeremy mwenyewe kwa njia ya simu ndipo aliposema kila kitu.

Mahojiano ya Kizwe yalikuwa yakifanyika laivu kabisa na Raisi Jeremy alikuwa akisikia kila kitu alichoweza kuongea Miranda, sasa siku hio ilikuwa ni ya pili yake muda wa saa kumi kamili.

Raisi Jeremy alishangazwa sana na kile alichoongea Miranda , hakuamini kama mke wake siku zote alikuwa akiishi kwa maigizo.

Jeremy kupitia maelezo ya Miranda anapata kujua Mke wake alikuwa akijua siku zote juu ya Edna kuwa mtoto wake, katika maelezo ya Miranda hakugusia kama Kizwe alikuwa amehusika katika kifo cha Raheli kwani hakuwa akijua chochote kutokana na kwamaba Kizwe hakumshirikisha kwenye baadhi ya mambo , hivyo alichopata kujua Raisi Jeremy kupitia Miranda ni kwamba Kizwe ndio aliehusika na tukio la juzi la kampuni ya Edna kuvuja kwa taarifa zake kwa kushirikiana na Ernest Komwe ambaye Miranda aliweka wazi kwamba ni ndugu yake na Edna upande wa Mama.

“Nahitaji kujua taarifa zote za huyu Ernest Komwe hususani ndugu zake na kila kitu na namna alivyokutana na mke wangu”Aliongea Kizwe mara baada ya mahojiano na Linda alichukua agizo hilo la kulipasia kwa vijana wake kuanza kazi.

“Vipi kuhusu mke wangu Linda , haujanipatia taarifa yoyote mpya zaidi ya kuniambia yupo ndani ya hoteli?”

“Mheshimiwa..”Linda alionekana kusita sita kumuelezea Mheshimiwa Jeremy.

“Linda weka kila kitu wazi , ni nini mnanificha , nimekupa kazi ya kumfuatilia hivyo nahitaji taarifa yote ya kila kitu anachofanya na alichofanya”aliongea kwa namna ya kufoka.

“Mheshimiwa katika video ilitumiwa kuna mwanaume alie onekana kuwa wa mwisho”Aliongea Linda na kumfanya Raisi.

“Ana nini huyo wa mwisho, Linda sitaki uniambie nirudie kuiangalia ile video chafu kwani inanitia kichefu chefu”

“Sitaki urudie kuiangalia mheshimiwa , ninachomaanisha mwanaume huyo wa mwisho ndio alieonekana kumsaidia Madam”

“Kumsaidia kivipi wakati alihusika kumbaka?”

“Ni kweli mheshimiwa alionekana kumbaka , lakini baada ya hapo wameonekana kuwa pamoja na tumeweza pia kutega Kamera ndani ya chumba cha hoteli ya JR na tumeweza kurekodi baadhi ya matukio”Aliongea Linda na kisha alitoa simu yake kwenye mfuko wa suruali ya kitambaa na kisha kumpatia Mheshimiwa Jeremy,

Sasa ilionekana wakati Kizwe anampeleka Lekcha saluni kuweka nywele zake sawa, ndio muda ambao wanausalama walitega Kamera ndani ya chumba cha hoteli alichokuwa analala Kizwe , sasa ijapokuwa jambo hilo lilikuwa kinyume na maadili kwa mke wa raisi , lakini walitaka kujua nini kinaendelea kati ya Lekcha na Kizwe , kutokana na kwamba walipatwa na wasiwasi , kwani Lekcha ndio alieonekana kuwa wa mwisho kumnyandua Kizwe lakini baada ya hapo Kizwe alionekana kutokumkasirikia huyo mwanaume na kufanya mpaka maamuzi ya kumchukulia chumba ndani ya hoteli.

Unajua Kizwe alichukua vyumba viwili wakati anafika na Lekcha , lakini mara baada ya Lekcha kutoka saluni na kupendeza na kuwa mtu katika watu ilimfanya Kizwe kuvutiwa nae na kufanya nae mapenzi, basi ndio ikawa kama chumba cha Lekcha kimetelekezwa , sasa wasichokuwa wakielewa ni kwamba kila walichokuwa wakikifanya kilikuwa kikionekan na kurekodiwa.

Raisi Jeremy aliangalia kila kitu kilichotokea siku nzima , kwanzia Kize mke wake alivyoenda na Lekcha saluni , walivyorudi na kufanya mapenzi, kila kitu aliona na alijikuta akiumia sana.

Ukweli kwa Raisi Jeremy sio kwamba ilikuwa mara ya kwanza kwa Kizwe kuchepuka , Jeremy alikuwa akijua mahusiano yaliokuwepo kati ya mke wake na Raisi Kigombola na ndio maana Raisi Jeremy na Kigombola hawakuwa wakipatana kabisa, lakini kilichomfanya Jeremy kutomuuliza Kizwe ni kutokana na kwmaba hakuwahi kupata Ushahidi wa moja kwa moja , kama mke wake alikuwa na mahusiano nje ya ndoa, hivyo kukosa ujasiri wa kumuuliza.

Kuna wakati Jeremy hakuwa akijihusisha mapenzi kabisa na Kizwe kutokana na migogoro waliokuwa nayo ,lakini licha ya kwamba waliishi kwa kutokuwa na mapenzi , hawakuwa na uwezo wa kuachana kutokana na nafasi yake kama raisi wa nchi , lakini pia ilifikia siku kumsamehe kutokana na kwamba hata yeye pia alikuwa na hatia ya usaliti.

“Linda nadhani unanidharau sana kwa kuwa na mke kama huyu?”

“Sikudharau mheshimiwa bali nakuonea huruma kwa kuwa na mke kama Kizwe”Aliongea na kumfanya Jeremy kufumba macho na kuegamia kwenye kiti chake , alikuwa akijitahidi sana kujituliza , hakutaka kuathirika kiafya kwnai alikuwa na safari ndefu bado kama kiongozi wa nchi hio ya Rwanda.

“Mheshimiwa unapanga kufanya nini , Mke wako leo hii usiku atafikishwa hapa nchini kama ulivyoagiza?”

“I will kill her Linda”Aliongea Jeremy na kumfanya Linda kutoa macho.

“Uko siriasi?”

“Yes, hii itakuwa ni siri yako na yangu Linda , wewe ndio utasimamia kifo chake , sitaki ndugu zake wafahamu kuhusu hili, nataka kifo chake kionekane cha asili Zaidi na sio cha kutengenezwa”

“Mheshimiwa naomba ufikirie mara mbili swala hili?”Alionea Linda kwa wasiwasi.

“Huo ndio uamuzi wangu Linda , nahitaji Kizwe kufa na wewe ndio utasimamia na hilo litafanyika baada ya mimi kuongea nae”

“Mheshimiwa Hapana siwezi”Aliongea Linda kwa wasiwasi.

“Linda kama unataka nikuamini tena unatakiwa kuandaa mazingira ya Kizwe kufa , sijui ni kwa namna gani utafanikisha lakini nataka wananchi wa Rwanda kuamini amekufa kwa kifo cha asili, lakini pia familia yangu kutofuahamu lolote kuhusu kilichotokea Tanzania”Aliongea na kumfanya Linda kutingisha kichwa kuashiria kukubali

“Kuhusu huyu mwanaume , nahitaji kumjua ni nani kwa kila kinachomuhusu kabla sijakutana nae , wakifika nchini wapelekwe State Area D na hawaruhusiwi kuonana na mtu yoyote”Aliongea Mheshimiwa Jeremy akiwa siriasi.

Alionekana kudhamiria kabisa kumuua mke wake kwa kile kitendo alichokifanya.

“Hades hii yote ni kazi yako nadhani unatarajia kuona nitafanya maamuzi ya namna gani ndio maana ukaamua kumdhalilisha mkewangu , nitakupatia ulichoomba”Aliwaza Jeremy.

Ndio muhisika aliweza kumjua ni Roma , kwani kila kitu kilikuwa wazi na aliamini Edna mtoto wake hawezi kuwa katili namna ya kuagiza mke wake kudhalilishwa.

Lakini Raisi Jeremy hakuamini kama Roma alifanya maamuzi ya kumpa adhabu ya aina hio mke wake kwa ajili tu ya kushirikiana na Ernest Komwe kuvujisha nyaraka za kampuni , Raisi Jeremy alikuwa na wasiwasi huenda kuna Zaidi ya sababu ya Roma kufanya alichokifanya na ndio maana alitaka kumhoji mke wake yeye mwenyewe siku inayofuata ilikujua ni mangapi maovu ameyatenda pasip yeye kujua na baada ya hapo ndipo amuue Lekcha pamoja na mke wak.

Kwake yalikuwa ni maamuzi magumu , lakini aliamini ili kuishi kwa amani na kuondokana na udhaifu ambao utamfanya kuishi kwa woga siku zote basi ni kuhakikisha Kizwe anakufa kwa namna ambayo wengine wataamini amekufa kifo cha asili.

********

Roma hakuwa na wasiwasi kabisa , hakuwa akimhofia kabisa Kizwe kuwa hai na kuonekana kujiamini , moja ya sababu ya kutomhofia Kizwe ni kwamba Jeremy bado hajafanya maamuzi na hiko ndio ambacho kilikuwa kikimpa shauku ya kutaka kujua ni maamuzi gani atayachukua mara baada ya kupata filamu ya kisanaa iliotengenezwa na Adeline.

Roma alijiambia huenda Edna mke wake akijua aina ya adhabu ambayo amempatia mke wa baba yake , angemuona shetani lakini yeye mwenyewe alijiambia likija swala la usalama wa watu wake anaowapenda basi atafanya yale mambo yote ambayo kwa macho ya kibinadamu yanaweza kuonekana ya kishetani.

Akiwa njiani aliweza kupigiwa na Afande Kweka , ambaye alikuwa akimpatia taarifa kwama Lanlan atalala huko na siku inayofuata atasafiri nae Kwenda Iringa kwenye mashamba yake ya mifugo.

“Roma nimewasiliana na mke wako , nitaondoka na mjukuu wangu Lanlan kuona urithi wa familia yetu”Aliongea Afande Kweka kwa sauti yake ya kibabe ya moja kwa moja.

“Mzee umesema umewasiliana na mke wangu?”

“Siku hizi umekuwa hausikii vizuri kuna mwingine nani wa kumuaga”Aliongea Afande Kweka. Na kumfanya Roma ambaye anaendesha gari kushangaa kwani nguvu za kichawi alizomuwekea Edna ni za usingizi wa masaa Zaidi ya kumi na sita.

“Itakuwa mama au Bi Wema wamemuamsha , nilifanya makosa kutowaambia kinachoendelea”Aliwaza Roma.

“Mzee kwahio unanipa taarifa au unaniomba ruhusa?”

“Nakupa taarifa , kama unataka kuongozana na mimi litakuwa jambo zuri itatuweka karibu Zaidi kama wanafamilia , lakini pia utaweza kuona urithi wako”

“Siwezi Kwenda ni ghafla, lakini pia sina mpango wa kurithi chochote, unaweza kumrithisha Lanlan”

“Huwezi kukimbia urithi wa familia”Aliongea.

“Kwahio unapanga kunilazimisha?”

“Unaweza ukahisi urithi hauna maana kwako kutokana na vihela ulivyokuw anavyo, lakini hilo ni tofauti kwa vitukuu , asili ndio inamtambulisha mtu, unaweza kuwa na majina mengi lakini utabakia kuwa na damu ya familia”Aliongea lakini Roma hakuwa akimsikiliza kwa umakini , jambo kubwa ambalo muda huo lilikuwa kichwani kwake ni Edna mke wake.

Baada ya madakika kadhaa tu Roma aliweza kuingiza gari ndani ya nyumba na kulipaki kwenye gereji kisha akatembea mpaka ndani na alijikuta akiwa kwenye mshangao mara baada ya kumkuta Edna anaangalia taarifa ya Habari ya saa mbili.

“Roma umerudi , ndio ntunamalizia kuandaa chakula”Aliongea Blandina huku akiwa ameshikilia bakuli akielekea jikoni.

“Mama ulimuamsha?”

“Wala hatukumuamsha sisi ulivoondoka ndio aliamka na akataka kuingia jikoni ndio tukamzuia kwani anaonekana amechoka”Aliongea Blandina na kumfanya roma kuingiwa na wasiwasi na kumsogelea Edna.

“Edna..!!”Aliita Roma na Edna aligeuka na kumwangalia lakini Roma mwili wake ulijaa baridi , alijiuliza nini kinaendelea , kwanini Edna anaonekana kuwa sawa kama hakuna kitu kilichotokea.
 
SEHEMU YA 390.

Kilichotokea kwa Edna kuamka mapema nje ya muda Roma alioukadilia ni kama kile kile kilichotokea Ufaransa, wakati Roma akipambana na Depney , sasa haikueleweka kwanini Edna kuathiriwa kidogo sana na nguvu zao miungu , kwani ufaransa aliemlaza kwenye usingizi alikuwa ni Apollo..

Edna aliamka ndani ya lisaa limoja tu , yaani wakati Roma alivyokuwa usingizini ndio muda ambao Edna aliamka na kuanza kuomboleza.

Edna tokea siku ambayo aliweza kujua siri ya mama yake , siri aliopata kupitia flash Disk aliopewa na raisi Kigombola , alikuwa akitegemea siku moja atakuja kugundua kitu ambacho kitakuja kumuumiza sana kihisia.

Ikumbukwe katika flash ambayo Raisi Senga alimpatia Edna , hakukuwa na maelezo mengi , alichokigundua Edna ni kwamba mama yake alikuwa na kisasi alichokuwa akikiendeleza, lakini pia akampa kazi hio ya kisasi yeye kuikamilisha , huku akiacha orodha ya kampuni ambazo hakukuwa na maelezo yoyote kwamba alichokuwa akitakiwa kufanya ni nini mpaka alipokuja kugundua uwepo wa ‘Deposit Box’ ndani ya Swiss In, ambapo ndani yake ilikuwa imebeba bahasha iliokuwa na taarifa ambayo ndio inamfanya kuwa kwenye hali ya huzuni na majonzi.

Raheli Adebayo katika stori yake ya kimaisha mara baada ya kujua ukweli kwamba mtoto wake Lorraine, pacha wake na Edna anaishi kwa jina la Agent 17, ndio kisasi chake kilianza rasmi , lakini kutokana na kwamba watu ambao walikuwa na mtoto wake kuwa wakubwa serikalini, aliamini pesa pekee ndio zitakazo muwezesha kutimiza azma yake, Azma ya kumrudisha mtoto wake huyo ili kutoendelea kujutia kosa alilolifanya miaka mingi nyuma , kosa la kukubali kumuachia Lorraine Kwenda kulelewa na Raisi Jeremy jambo ambalo lilipelekea kadhia ambayo mtoto wake amekutana nayo mpaka kubadilishwa jina , lakini bahati mbaya mpaka anakufa hakuwa ametimiza Azma yake.

Kwahio ni rahisi kusema kwamba Edna sasa anajua kifo cha mama yake ni cha kutengenezwa , lakini hafahamu kama kuna Zaidi ya kile anachokifahamu ambacho kilikuwa kikiendelea kwenye Maisha ya mama yake, anajua tu kwamba mama yake alikuwa mjamzito wa Watoto mapacha lakini hakuwa akielewa pacha mwenzake yupo wapi.

Edna alikaa kitandani akiwa peke yake huku machozi yakiwa yanamtiririka , kila akijaribu kuyafikiria maisha magumu ambayo mama yake alikuwa akiishi moyo wake ulimuuma na alijidharau mno kwa kutogundua kama mama yake alikuwa akipitia kipindi kigumu , yeye kama mtoto alijihisi alikuwa na haki ya kuwa karibu na mama yake lakini kutokana na ubize wa masomo akashindwa kujua kile kinachoendelea.

Baada ya kuwaza na kuwazua alijikuta akifuta machozi yake na kisha akachukua picha ya mama yake iliokuwa pembeni kwenye kijimeza na kisha akaishika kwa kuikodolea macho , lakini kadri alivyokuwa akiangalia alijikuta machozi yakizidi kumtoka kwa mara nyingine , mrembo Edna alionekana kuwa katika hali ya huzuni mno.

“Mom naomba unisamehe , sikuwepo karibu yako wakati ulipokuwa unapitia kipindi kigumu , I am so so….”Alijikuta akishindwa kuendelea na kuanza kulia kwa kwikwi awamu hii kwa takribani nusu saa nzima alizitumia kuomboleza , mpaka aliponyamaza mwenyewe.

“Nitautafuta ukweli wote na nitahakikisha nalipa kisasi kwa ajili yako mama yangu , ndio njia pekee ambayo naamini utanisamehe kwa kutokufahamu kama ulikuwa ukipitia magumu mengi”Aliwaza Edna huku hali yake ikirejea upya , ijapkuwa hakuonyesha furaha , lakini alionekana kuacha kulia na kuwa na sura iliojaa usiriasi.

Saa moja za jioni ndio alishuka kutoka chini huku akiwa ashaongea na halmashauri ya kichwa chake , alishajiambia kwenye akili yake kwamba vita ndio inaanza , vita ya kulipa wale waliohusika kumfanyia mama yake majaribio ya kisayansi mpaka kupelekea kifo chake , alikuwa ashafanya maamuzi tayari , maamuzi ambayo ili kuyakamilisha alitakiwa kuwa na nguvu na sio kukaa kitandani kuomboleza , alitakiwa kuwa jasiri ambaye muda wowote yupo tayari kukabiliana na maumivu ili kutimiza malengo yake.

Muda ambao alikuwa akishuka kutoka juu ndio muda ambao Afande Kweka alipiga simu kumwambia kwamba ataondoka na Lanlan Kwenda nae Iringa kwenye mashamba yake na Edna jibu alilotoa ni kwamba mpaka amshirikishe mume wake Roma kwanza ,lakini Afande Kweka alimwambia atampigia mwenyewe simu kumjulisha.

Roma alienda kukaa karibu na mke wake na kisha kumshika mkono , Blandina aliekuwa amesimama alijiua kuna kinachoendelea , lakini hakutaka kuingilia na alitembea mpaka jikoni kwa ajili ya kuandaa chakula.

Edna alimwangalia Roma alieshika mkono wake , huku akiwa na sura isio jaa furaha wala huzuni , ilikuwa ni sura yake ile ile ya kikauzi ambayo imezoeleka.

“Edna mke wangu , najua unapitia kipindi kigumu kwa sasa na sijui namna ya kurudisha furaha yako, jana nilikuambia nitakuwa bega kwa bega na wewe kwa nyakati zote za furaha na huzuni hilo ndio nilaloweza kukuahidi”Aliongea Roma na Edna alimwangalia Roma kwa dakika kama moja huku vitu vingi vikipita kwenye kichwa chake , haikueleweka alikuwa akifikiria nini lakini alionekana kuwa na hisia mchanganyiko , hisia za kumlaumu Roma kwanini alimficha juu ya Suzzane , kwanini alimficha mara baada ya kujua ukweli juu ya mama yake lakini wakati huo huo aliamini Roma alikuwa na sababu ya kumficha na huenda hata yeye angekuwa kwenye nafasi yake angeweza kufanya hivyo lakini wakati huo huo akiwa na hisia kwamba mambo yote yameanza kuwa hadharani kwasababu ya uwepo wa Roma kwenye Maisha yake.

Edna alijikuta akitoa machozi na kisha alimsogelea Roma na kumkumbatia na kuanza kulia kwa kwikwi , kitendo ambacho kiliwafanya Bi Wena na Blandina waliokuwa wakiandaa chakula kutoka kuangalia kuna nini kinaendelea.

“Roma kwanini Edna yuko hivi umemfanya nini?”Aliongea Blandina kwa wasiwasi huku akimsogelea Edna na kumshika mikono kwa namna ya upendo na Bi Wema na yeye alimsogelea na kukaa mbele yake , huku upande wa Yezi aliekuwa juu chumbani kwake pia akishuka chini aliona jambo hilo na kumsogelea dada yake wa hiari pia.

Wanafamilia wote walionekana kuwa na wasiwasi na Edna na walitaka majibu, kitendo cha Edna kuona kila mwanafamilia alikuwa na wasiwasi juu yake alijikuta akiinua macho yake na kumwangalia Roma kwa huzuni.

“Edna nisikilize kuna hisia mbaya zinaniambia kilichopo kwenye hii bahasha kinaweza kukutoa machozi, nataka uangalie ukiwa nyumbani na watu wote wanaokupenda wakiwa pembeni yako”Edna alijikuta akikumbuka maneno ya Roma na sasa anaelewa alikuwa akimaanisha nini.

Maisha yake yalikuwa yamebadilika sana , alikuwa na watu wengi waliokuwa wakimpenda tofauti na kipindi cha Maisha yake ya nyuma , sasa alikuwa na familia kubwa ambayo yote inamjali sana.

Edna ilibidi awaelezee kile alichogundua , stori yake iliwafanya kila mmoja kushangazwa na jambo hilo na kuhuzunika kwa wakati mmoja na wote walijikuta wakimfariji.

Roma alipendezwa sana na jambo hilo , swala la kuwa na familia iliokuwa inakujali kwa kila kitu , yalikuwa ni Maisha ya kipekee na alijua nini maana yakuwa na familia Maisha yake ya nyuma alikosa kujua radha halisi ya kuwa na familia na hapo yeye mwenyewe ni kama alikuwa katika hatua za kujifunza nini maana ya familia.

Wakati akiendelea kuwaangalia wanafamilia wake , simu yake iliokuwa kwenye mfuko ilianza kuita mfululizo aliitoa na kuangalia jina la mpigaji na alijikuta akishanga, kwani alikuwa ni rafiki yake Makedoni kutoka Mossad.

Roma alinyanyuka na kisha alipandisha juu kwa ajili ya kuongea na Makedoni , kwani aliamini ikitokea Makedoni akianza kumtafuta yeye basi kuna jambo kubwa ambalo limetokea.

“Your Majesty Pluto were you too bored after not killing anyone for two years , why did you destroy the American Fleet entirely” Ilisikika sauti ya kitetemeshi kutoka kwa Makedoni akimuuliza Roma kwamba amechoshwa na kutoua mtu kwa miaka miwili ndio maana akaharibu meli ya kivita ya Kimarekani.

Roma macho yalimtoka , hakuelewa Makedoni alikuwa akimaanisha nini , Meli ya Kimarekani , mtu yupo Tanzania kwanini aharibu Meli ya kivita ya kimarekani ,

“Makedon , What is this nonsense ? what did I do which even I am not privy to?”Aliuliza Roma kwamba ni ujinga gani Makedoni anaongea juu ya kufanya jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakuwa na uelewa nalo.

*******

Ni siku nyingine kabisa alionekana Raisi Jeremy akiwa ndani ya ofisi yake , huku mkononi akiwa ameshikilia picha ndogo , picha ambayo ambayo alikuwa akionekana yeye na mke wake Kizwe wakiwa kwenye pozi la tabasamu huku Kizwe akiwa amevalia gauni la harusi.

Raisi Jeremy picha hio alikuwa akiangalia tokea jana yake usiku alipompa maagizo Linda kwa ajili ya kuandaa mpango wa kumuua Kizwe , mheshimiwa huyu licha ya kufanya maamuzi ya kumuua Kizwe lakini haikumaanisha kwamba hakuwa akiumia ndani kwa ndani, ukweli alikuwa kwenye majonzi makubwa , Kizwe ni mwanamke ambaye alitoka nae mbali sana tokea kabla hata hajawa raisi wa nchi hio ya Rwanda , walipitia nyakati tofauti tofauti , za furaha na zile za huzuni..

Lakini licha ya histora yao, aliamini Kizwe hakuwa na mapenzi kwake tena na kumuweka hai karibu yake ni hatari zaidi, kitendo cha kuweza kuishi kwa kumuigizia kilimfanya hata yeye mwenyewe kumuogapa na kujiuliza ni mangapi Kizwe amemficha , ni mangapi ambayo amefanya pasipo yeye kujua, ndio alikuwa ni mke wake lakini alimuona kama vile amemfahamu juzi na sio miaka mingi iliopita..

Mheshimiwa Jeremy na mke wake Kizwe walibahatika kupata Watoto wawili pekee ,mmoja akiwa ni Desmond ambaye ndio aliekuwa wa kwanza na wa pili alikuwa ni msichana anaefahamika kwa jina la Kyler.

Kyler alikuwa ni marehemu baada ya kupata ajali kwenye mashindano ya magari nchini Marekani wakati alipokuwa masomoni , hivyo unaweza kusema ni Desmond pekee ambaye alibakia kwenye uzao wake ambaye anaweza kumfanya kama mrithi.

“Forgive me Kizwe Mke wangu?”Aliongea Raisi Jeremy kwa huzuni na kisha ile picha ambayo ilikuwa kwenye mikono yake aliichana vipande vinne na kisha akatupia kwenye dastibin.

Muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Linda ambaye amevalia suti ya rangi nyeusi iliomkaa vyema mwilini pamoja na shati rangi ya ugoro ndani yake.

“Mheshimiwa hili ni faili la taarifa za mwanaume aliekuwa na Madam”Aliongea Linda na kisha akampatia raisi Jeremy lile faili na kuanza kulisoma na kadri alivyokuwa akiendelea kusoma alijikuta akishangaa.

“Hii taarifa ni sahihi?”

“Ni sahihi mheshimiwa hata ndugu zake wapo hapa nchini , jimbo la Mashariki”Aliongea na kumfanya Jeremy kufikiria kidogo na kisha akaliweka chini.

“Vipi kuhusu maagizo mengine niliokupatia”

“Kila kitu kipo tayari mheshimiwa, tutampa dawa ambayo itamfanya moyo wake kufeli , ni njia nzuri zaidi ambayo itafanya watu wasitilie mashaka kifo chake”Aliongea Linda kwa huzuni kidogo.

“Okey , nitaelekea State Area D , nikishamaliza mazungumzo ,mpango huo utafuatia”

“Mheshimiwa una uhakika na hili?”

“Linda nishafanya maamuzi tayari na hakuna wa kunizuia tena”Aliongea Raisi Jeremy na kisha alisimama kwa ajili ya kuondoka.

State Area D ni moja ya maeneo maarufu ndani ya Rwanda, eneo hili umaarufu wake ulitokana na kwamba yalikuwa makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Sasa muda huo wa asubuhi ulinzi ndani ya hili eneo ulikuwa umeimarishwa mno tokea jana usiku , sabababu kubwa ya kuimarishwa kwa ulinzi ndani ya eneo hilo na makachero wa serikali ni kutokana na maagizo ya raisi mwenyewe mara baada ya Kizwe na Lelcha kufikishwa kwa siri sana nchini kwa ndege binafsi ya kijeshi.

Kwenye watu ambao walikuwa kwenye maswali mengi ni Lekcha tokea siku ya jana anapandishwa ndege mpaka kufikishwa nchini Rwanda kwake kila kitu ilikuwa ni mshangao , hakuwa akijua ni kipi kinaendelea na alishindwa kuuliza pia , kwani alitenganishwa na Kizwe.

Sasa baada ya kutolewa kwenye ndege na kuingizwa kwenye gari ya pamoja na walinzi ndio alipata nafasi ya kuongea na Kizwe.

“Hey nini kinaendelea , hawa watu walitotuleta hapa ni wakina nani?”Aliuliza Lekcha.

“Vipi una wasiwasi?”

“Wasiwasi , mimi niwe na wasiwasi nishakuwa kwenye hali hatarishi kuliko hata hii , kwanini niwe na wasiwasi, unafikiri kwanini nina mguu bandia , yote haya ni Maisha magumu niliopitia kama nilikuwa tayari kushindana na wanyama wakali kwanini niogope binadamu wachache wanaotaka kunidhuru?”

“Wanyama ni rahisi kuwafukuza kwa hila , lakini kuhusu binadamu ni Habari nyingine , binadamu ni kiumbe kisichotabilika na hatari Zaidi”Aliongea Kizwe na tabasamu la uchungu mno.

“Hey hupaswi kuwa na huzuni kiasi hiki kama vile familia yako yote imekufa , wewe ndio ulitendwa kwanini unaonekana kama mwenye kuogopa kama vile kuna mtu kakuwekea siraha kwenye kichwa chako?”Aliuliza Lekcha lakini kabla hajajibiwa gari ilisimama ndani ya eneo hilo la Area D na geti lilifunguliwa na kuingizwa ndani.

……..

Saa tano kamili za asubuhi ndio muda ambao raisi Jeremy aliweza kufika ndani ya eneo hili la Area D, safari yake ambayo ilikuwa ya kimya kimya akiwa ametangulizana na Linda pamoja na walinzi wachache.

Baada ya kufika tu aliongozwa na wanajeshi wawili waliokuwa wana siraha za moto kuzunguka upande wa nyuma na kuingia kwenye moja ya jengo kati ya matatu yaliokuwa ndani ya eneo hilo la makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Baada ya kuingia ndani ya chumba aliweza kukutana na sura mbili , ya kwanza ikiwa ni ya mke wake Kizwe na ya pili ilikuwa ni ya Lekcha , wote wakiwa wameketi kwenye masofa wakiwa chini ya ulinzi mkali.

“Nafikiri unanichukia kwa staili niliokurudisha nchini Rwanda?”Aliuliza Raisi Jeremy bila salamu mara baada ya kumwangalia Kizwe kwa dakika kadhaa.

“Kitendo cha kuja mpaka hapa kwa ajili ya kukutana na mimi licha ya yote , nadhani napaswa kushukuru”Aliongea Kizwe. Na kumfanya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Kwanini uliamua kumchokoza Roma?”Aliuliza kwa kifaransa awamu hii.

“Hindsitght is real bitch , you know that ? You might as well say that I shouldn’t have taken action against that little bitch”

“Nyuma ya pazia ndio kuna mbwa halisi na ndio alietoa maagizo na unafahamu hilo? , unaweza pia kusema sikupaswa kuchukua hatua kwa mbwa huyo mdogo”Aliongea kwa namna ya kimafumbo hapo alikuwa akimlenga Edna na alijibu kwa Kingereza.

“Kaa kimya , kwanini unamwita kwa jina la kukera namna hio , unapaswa kufahamu sasa ni mtoto wangu na pia ni mdogo wake Desmond”Aliongea kwa hasira.

“Mtoto wako.. hahaha… hio mimi inanihusu nini? , Edna ni matokeo ya usaliti wako ulionifanyia , kama sio Afande Athumani babu yake kumlinda ningekuwa nishamuua mpaka wakati huu”Aliongea kwa hasira.

“Sijakuleta hata kwa ajili ya ngonjera zako?”Aliongea Raisi Jeremy

“Uko sahihi kabisa , kama nisiposema ninachotaka nani anajua kama naweza kutopata nafasi tena?”

“Ni bora kama ungeendelea kuniigizia kwa Maisha yako yote na kufanya mambo yako kwa umakini, sisi ni wanandoa lakini kudanganyana ingekuwa bora Zaidi kuliko kilichokutokea kama mke wa raisi, Kizwe nilitamani sana siku utakayogundua juu ya Edna ndio mwanzo wetu mpya na kuzika yaliopita , lakini kwa hili linaloendelea najikuta sina chaguo lingine”Aliongea huku uso wake ukibadilika.

“Unaogopa Jeremy ninaweza kukufanyia jambo baya Zaidi kwa kuweza kukuigizia miaka mingi , unaogopa naweza pia kukutoa kwenye nafasi yak kutokana na nguvu yangu ndani ya taifa hili , hivyo unahisi mimi kuwa hai ni hatari Zaidi kwako”

“Unaweza kuwa sahihi , umepotea siku chache tu lakini mabaraza yote yanataka kujua taarifa zako na serikali kwasasa haiko na utulivu , hata kama nikikuua sasa hivi maswali mengi yataibuka”Aliongea Jeremy.

“Kwahio unataka kunifanya nini?”

“Nina mtu tayari ashaandaa sindano ya kimiminika , ambayo itakuwa na uwezo wa kukufanya kama mgonjwa ambaye moyo wake umefeli , nitaelezea uma baada ya kifo chako kama mke wa raisi lakini mwanaharakati wa taifa hili kwamba baada ya kuwa nje ya nchi ulipatwa na tatizo ambalo lilipelekea tatizo la moyo na kutokuonekana kwako hadharani kwa siku hizi chache ni kutokana na kwamba ulikuwa chini ya uangalizi wa madaktari wakijaribu kuokoa afya yako , lakini mwisho wa siku hakuna kilichowezekana kwani hali yako ilikuwa kwenye hatua ya mwisho kabisa”Aliongea Jeremy bila ya kuwa na huzuni kabisa , alionekana ashavunja ndoa yake na kizwe moyoni mwake pekee na hakuna chochote ambacho anajutia.

Kizwe alijikuta akishangazwa kabisa na maneno ya mume wake yakimtoka bila wasiwasi kabisa.

“Sikuweza hata siku moja kufikiria kama itakuja siku mume wangu ndio anaagiza kifo changu , maneno yanakutoka kana kwamba hatukuwahi kupendana hapo kabla , hakika wewe ni raisi wa taifa hili ambaye unapambana kwa maendeleo makubwa Zaidi , Hahahaha… haha,, mbinu yako Jeremy ni nzuri sana na haiwezi kabisa kuacha maswali kama kweli nitakufa kwa shida ya moyo ni mbinu nzuri sana umefikiria”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kufumba macho kwa hisia na kisha akayafumbua.

“Dawa utakayopewa itakuletea maumivu katika mchakato mzima wa kuathiri moyo wako , nilitamani kufanya kifo chako kisiwe cha maumivu lakini hakuna mbinu mbadala Zaidi ya hii , Kizwe nakuhakikishia baada ya kifo chako mwanao Desmond atarithi kila kitu changu nakuahidi”Aliongea

“Hakika utamrithisha kila kitu , sio kwasababu unampenda bali ni kwasababu hauna mbadala hahahaha.., kuna muda nishawahi kufikiria kama Edna angekuwa mwanaume agekuwa na nafasi sawa na Desmond? , kinachoniumiza siku zote kila nilivyojitahidi kujitoa kwa ajili ya Desmond lakini hukukubali msaada wangu na kunipenda kama mkeo bali mawazo yako yalikuwa kwa mpuuzi Raheli na mtoto wake muda wote”Alifoka lakini Jeremy alishindwa kumjibu alimwacha aongee kwani ndio siku yake ya mwisho ya uhai hata hivyo.

“Kwasababu nitakufa muda wowote naomba nikuambie siri ambayo niliificha kwa miaka mingi , ili kukuonysha ni kwa kiasi gani wewe ni mbumbumbu “

“Siri gani?”

“Miaka iliopita sio kweli kwamba Raheli alikufa kwa kansa ya damu iliompelekea moyo wake kufeli”

“Unataka kumaanisha nini?”Aliongea Jeremy kwa wasiwasi.

“Namaanisha kama unavyofikiria , najua hakuwahi kufikiria lakini daktari Hubery aliekuwa akimhudumia Raheli alikuwa chini yangu na vipimo vyake vya kimatibabu vilivyotolewa hospitalini vyote vilikuwa ni feki, hakuna ugonjwa uliomuua bali nilimuua mimi kwa mikono yangu”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kuanza kutetemeka kwa hasira.

“Wewe mwanamke ni shetani wa aina gani , hivi unajua ni kwa kiasi ganri Raheli alikuwa akikujali , ni kweli nilikuwa na uhusiano nae lakini hakutaka uhusiano wake na mimi kukuathiri hata kidogo , ndio maana akaamua kuolewa na mwanaume asiekuwa na mapenzi nae , aliishi bila ya kunitafuta na siku zote mimi ndio niliekuwa nikimsumbua ,kwanini hukujali yote hayo na alikuwa rafiki yako?”Aliongea kwa hasira mno , huku macho yake yakiwa mekundu.

“Niite shetani na majina mengine ,lakini siku zote nilikuwa mwenye kupta ninachokitaka”Aliongea bila ya hatia.

“Sawa ulichokifanya kishakwisha kufanyika , ni wakati wa kulipwa kwa makosa yako , jitafakari kwa matendo yako yote kabla ya sumu ya kifo haijaletwa kwako na kuchomwa”Aliongea na kisha alimwangalia Lekcha.

“Kwasababu huyu bwana wako ndio aliekuokoa lakini pia ameweza kusikiliza kila kitu, tulichoongea hapa angalau safari yako haitakuwa ya kinyonge mnaweza kuendelza mapenzi yenu mbele ya safari huko kuzimu”Aliongea na kisha akaondoka kwenye chumba hicho na kuwaacha marehemu watarajiwa.

MWISHO WA SEASON 13

Unafikiri ni nani alieharibu meli ya kivita ya Marekani , je ni Hades kama alivyosema Makedoni.

Yan Buwen na teknolojia yake ya Growth acceleration kama ni kutengeneza Clone ya Roma basi atahitaji angalau miezi minne , swali je amefanikiwa nje ya miezi minne.

Je kifo cha Kizwe ndio mwanzo wa Jeremy kumtangaza Edna kama mtoto wake , unafikiria Desmond atakuwa na hali gani akijua baba yake ndio aliemuua mama yake.

Yajayo yanafurahisha sanaaaaaa…..

OYA ACHA UBAHILI BWANA NI BUKU TATU TU KUJIUNGA GRUPU TUPO SEHEMU YA 460 , NICHEKI NAMBA 0687151346 ONLY WATSAPP

SEE YOU SOON
 
SEHEMU YA 386.

Roma ilivyotimia saa saba kamili alitoka kwenye jengo hilo la kampni yake na moja kwa moja kuanza safari ya kuelekea Posta ilipo kampuni ya Vexto na ndani ya madakika kadhaa tu aliweza kufika na kuegesha gari upande wa chini karibu na la mke wake na akamtumia Edna ujumbe wa maandishi na ndani ya dakika chache tu Edna aliekuwa amevalia suti alitokea , alikuwa na mudi nzuri kweli kwa muonekano wake na kumfanya kuwa membo Zaidi.

Roma alitoka kwenye gari na kisha akamfungulia mke wake kama boss na kumfanya Edna kuingia ndani ya gari na yeye akazunguka upande wa pili na kuingia ndani.

“Nimemiss Sophia , anarudi lini?”aliuliza Edna

“Jumanne ndio wanarudi”Aliongea Roma na kuondoa gari taratibu.

“Umejuaje kama umeachiwa kitu ndani ya benki ya Swiss?”Aliuliza Roma.

“Unakumbuka siku tulivyoenda Ikulu?”

“Ndio nakumbuka”

“Nilipatiwa Flash na mheshimiwa Senga siku ile na kwa maelezo yake alisema iliachwa na mama yangu na nilipaswa kuwa nayo, nilipokuja kuangalia ndani yake niligundua, kuna jambo ambalo lilikuwa likiendelea kwenye Maisha ya Mama pasipo ya mimi kufahamu” Edna alianza kumuelezea Roma namna ambavyo aliweza kugundua kuwa mama yake alikuwa na kisasasi ambacho hakuwa amekiweka wazi huku akimtaka yeye awe ni mwenye kukamilisha kisasi hicho , lakini pia Edna alimuelzea Roma kuhusu orodha ya kampuni ambazo zimeachwa na mama yake.

Roma alijikuta akishangaa kuhusu maelezo ya Edna , hakuamini kama mke wake alimficha jambo hilo kwa muda mrefu , lakini hakuwa kwenye nafasi ya kumlaumu Edna kwa wakati huo kutokana na kwamba kipindi kile hakuwa akimwamini vizuri na ndio kwanza walikuwa wameoana kimkataba.

“Kwahio kitendo cha kuichukua kampuni ya JR sababu ilikuwa ni hio orodha?”

“Ndio !Nilijua mama alikuwa akiniambia kampuni zote zilizopo kwenye orodha anataka kuwa chini ya Vexto ndio maana nikaanza na JR”.Aliongea Edna na muda huo walikuwa wanaingia sasa kwenye mgahawa na waliona wasimamaishe mazungumzo yao na wakaendelee kuongea wakiwa wanapta chakula cha mchana.

Wote baada ya kuingia kwenye mgawaha wa Rosella mtaa wa Azikiwe , waliagiza chakula na Roma alimwambia Edna aendelee kumuelezea.

Edna aliendelea kumwambia Roma namna alivyoshindwa kung’amua kuhusu Swiss In.

“Hili jina la Swiss In lilikuwa likinipa mashaka , kwani niliamini mama asingeweza kuorodhesha kitu ambacho kipo nje ya uwezo wangu na tulikuwa tukijaribu kufuatilia kwa muda mrefu na kugundua hakuna kampuni ya Swiss In”

“Na ulifahamu vipi?”

“Suzzane ndio alienisaidia kufumbua fumbo hili”Aliongea Roma na sasa kuelewa nini kimetokea na kujiambia inamaana Suzzane kashindwa kumvumilia mpaka akaamua kumuelezea , lakini kwa wakati huo hakutaka kumwambia mke wake alishawahi kuongea na Suzzane.

Edna wakati alivokuwa akielezea tukio hilo alionekana kutokuwa sawa kimawazo alikuwa na hofu na kile atakachokutana ndani ya benki ya Swiss ya kuhifadhi vitu ndio maana alitaka Kwenda na Roma mume wake.

Baada ya kula chakula huku Roma akijitahidi kumfurahisha , hatimae safari ya Kwenda benki ya Swisss ilianza na hapakuwa mbali , ni umbali wa nusu kilomita tu kutoka walipokuwepo.

Edna na Roma baada ya kuingia ndani na kuelezea shida yao na kufuata taatibu za mwanzo mhudumu alitabasamu kwa namna ya kuwachangamkia na kisha aliwaambia wamfuate.

Waliongozwa mpaka upande wa chini kabisa ya jengo kwa kutumia Lift na kuja kutokezea kwenye korido pana ndefu ambayo ilikuwa na boksi za chuma nyingi zenye namba kila upande kulia na kushoto na mbele , ilikuwa ni sehemu ambayo ina hewa ambayo inaendeshwa kwa mitambo, Roma alihisi vitu vinayvohifadhiwa humu vingi ni vya thamani kutokana na hewa inavyodhibitiwa.

“Boksi ni hili hapa wateja wetu, unaweza kutumia Fingerprint kufungua au Nywira , ukikosea mara tatu, kisanduku kitazuiwa kufungiwa kwa siku kumi na nne huku uthibitisho wa umiliki ukiendelea”Aliongea kwa Kingereza safi na Edna alitingisha kichwa na aliwaacha.

“Unaifahamu nywira?”

“Nafikiri hivyo, mama alikuwa anatumia nywira ya aina moja katika vitu vingi ambavyo ni binafsi kwake”

“Na unaifahamu?”

“Ndio ni herufi kumi na moja”Aliongea Edna na palepale alianza kubonyeza sehemu ya kuingiza namba”

“I9989819206”Aliandika Edna na Roma aliweza kuikariri haraka sana na alichogunuda ni kwamba nywira hio ilikuwa ni mwaka wa kuzaliwa wa Edna ambao uliandikwa kwenda mbele na kinyunyume lakini herufi 206 alishindwa kuijua inamaanisha nini.

Sanduku lile lilifunguka kama mlango wa CD na Edna na Roma wote kwa pamoja waliweza kuona bahasha ya Khaki ndani yake na Edna aliitoa kwa kuichunguza na kisha akampatia Roma , aliangalia ndani kama kulikuwa na kitu kingine lakini ilionekana kitu pekee kilichohifadhiwa humo ndani ni hio bahasha.

“Tutakwenda kuigunfulia baada ya kufika kwenye gari”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na kisha wakafunga kiboksi kile na kisha walitumia utaratibu ule ule na kisha wakatoka baada ya kusaini.

Baada ya wote kuingia kwenye gari , Edna alionekana kuwa na shauku kweli ya kujua kilicho ndani yake , lakini Roma alimkataza kufungua na kumwambia atulie kwanza.

“Mbona unaelekea upande huo?”

“Tunaelekea nyumbani”Aliongea Roma.

“Nahitaji kurudi Kazini nina majukumu mengi Roma”Alilalamika Edna.

“Edna nisikilize kuna hisia mbaya zinaniambia kilichopo kwenye hii bahasha kinaweza kukutoa machozi, nataka uangalie ukiwa nyumbani na watu wote wanaokupenda wakiwa pembeni yako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia Roma kwa wasiwasi.

“Kuna kitu unajua huniambii?”Aliuliza Edna.

Ukweli Roma hata sababu ya kumpeleka kwanza mgahawahi kula na kushiba ulikuwa ni mpango wake , aliamini huenda ndani ya bahasha hio kuna taarifaa ambayo itakuwa kubwa sana kwa Edna , hivyo kumletea mawazo na kishindwa kula.

Roma hakutaka kujibu swali la Edna kabla ya kujua ni kitu gani kipo ndani ya bahasha hio , alijiamia atampa Edna maelezo kutokana na kile ambacho kitakuwa kwenye bahasha hio..

Dakika chache tu waliweza kufika nyumbani na Bi Wema na Blandina walishangazwa na kurudi kwao nyumbani mapema siku hio tena wakiwa pamoja.

“Mama Lanlan yuko wapi?”Aliuliza Edna mara baada ya kutokumuaona Lanlan eneo hilo na Blandina na Bi Wema waliangaliana.

“Babu yake kaja kumchukua na ameondoka na Qianq Xi”Alijibu Bi Wema na kumfanya Edna kumwangalia Roma.

“Yule mzee anapenda kufanya mambo bila kuaga ,alishindwa vipi kutupigia simu kama anamchukua mtoto wetu”Aliongea Roma huku akikunja sura.

“Sio mzee , yule ni babu yako Roma”Aliongea Blandina.

“Hakuna shida ameenda kwa babu yake Roma”Aliongea Edna huku akimshika mkono Roma na wakaanza kupanda juu.

“Miss kama hamjakula chakula niwaandalie”Aliongea Bi Wema.

“Bi Wema msiwe na wasiwasi tulipitia mgahawani kabla ya kuja nyumbani”Aliongea Edna na Blandina alitabasamu.

“Okey mmefanya vizuri mnaweza Kwenda kupumzika sasa”Aliongea Blandina kwa bashasha pasipo kujua kama wenzie wamerudi kwa jambo maalumu.

Wote waliingia chumbani na Edna mara baada ya kufika tu alitaka kuangalia ni kipi kipo kwenye bahasha hio , ambayo ameachiwa na mama yake kwa namna ya kificho.

Roma hakutaka kumzuia alimwacha afungue mwenyewe huku yeye akiketi pembeni yake, Edna mara baada ya kufungua ndani yake aliweza kutoa karatasi zilizopigwa pini , ni nyaraka mbili tofauti.

Edna aliweka moja kwenye mapaja na kuanza kupitia iliokuwa ni ya kwanza ambayo juu kabisa ilikuwa na nembo ya hospitali ya Muhimbili, Edna alijikuta akipatwa na mshangao usiokuwa wa kawaida huku akisoma haraka haraka ile karatasi.

Karatasi alioshikilia Edna ilikuwa ni maelezo ya matibabu ya Kliniki ambayo alikuwa akifanya mama yake, Edna hakuwa mjinga kufahamu maelezo ya kidaktari , kila kitu kilikuwa wazi, picha ya kadi la Kliniki lilikuwepo na kila kitu kilionyesha kwamba mama yake alikuwa ni mjamzito wa mapacha, Roma aliona mabadiliko ya Edna ila alishindwa kuongea chochote .

Sasa kitu kilichokosekana kwenye karatasi ile ni cheti cha kuzaliwa , kulikuwa na taarifa ya mahudhurio ya Kliniki pekee ikionyesha Raheli alipokuwa mjamzito alikuwa na ‘Multiple Pregnancy” lakini hakuna taarifa inayoonyesha wakati wa kuijifungua nini kilitokea.

Edna baada ya kuona taarifa ya kwenye karatasi ya kwanza haijampa jibu , kwa papara alichukua karatasi nyingine na kuanza kuisoma na hii ilimtoa machozi na kumfanya kutetemeka.

Karatasi ya pili ilikuwa ni cheti cha matibabu cha mama yake kutoka hospitali ya Mayo Clinic Marekani , Edna alijitahidi kuelewa cheti hicho lakini ni kama hakuwa akielewa kile anachosoma na kumpatia Roma.

Roma alichuku karatasi zote na kuzisoma moja moja kwa umakini na kuishia kukunja sura , ijapokuwa mategemeo yake yalikuwa Zaidi ya karatasi hizo , lakini hio taarifa ilikuwa sio ya kawaida.

**********

Upande wa hoteli ya JR , Kizwe aliweza kurudi kwenye mwonekano wake ule ule aliokuwa nao kabla ya kubakwa , kwa upande wa Lekcha alikuwa amebadilika sana kimwonekano kwani aliweza kuwa msafi mno na kuwa na mavazi mapya ambayo yalimfanya kuwa Handsome.

Hata Kizwe mwenyewe alishangazwa na muonekano mzuri wa Lekcha, licha ya kuwa na mguu wa bandia lakini mavazi ya suti yalikuwa yamemkaa vyema sana, kiasi kwmaba huwezi kumfahamu kama siku ya jana tu alikuwa akiokota makopo.

Siku hio ya asubuhi baada ya jana yake kuhamia ndani ya hoteli hio ya JR ,Kizwe aliweza kumpeleka Lekcha saluni kwa ajili ya kuwekwa sawa mwonekano wake , Kizwe alifanya mambo kwa tahadhari sana na hata yule msaidizi wake almpa maagizo ya kuondoka na kujifanyisha hajui mahali alipo, sasa haikueleweka Kizwe alikuwa na mpango gani kichwani, lakini baada ya kuamka alivaa hijab na miwani na kisha wakatoka na Lekcha Kwenda saluni.

Baada ya wawili hao kurudi hotelini mara baada ya Lekcha kuwekwa mwonekano wake sawa , Kizwe alijikuta akimwangalia Lekcha kama vile amekuwa mtu mpya kwake , alimwangalia kwa madakika kadhaa na alijikuta akishindwa kuvumilia na kumvaa Lekcha mdomoni na kuanza kupeana mabusu nyevu ambayo yaliamsha hisia za Lekcha zilikolala na dakika kumi zilikuwa nyingi sana kwani Kizwe alianza kulalamika kwa raha alizokuwa akipata kutoka kwa Lekcha, haikueleweka alikuwa ameshapona maumivu ya kubakwa jana yake , lakini wakati huo alionekana kuwa kwenye ulimwengu mwingine na alichokuwa akihisi kwenye mwili wake sio maumivu bali ni raha isioelezeka.

Dakika ishirini mbele alishika shuka lililotandikwa kitandani na kulivuta kwa nguvu kwa mikono yote miwili huku akishindwa kuhimili hisia zake na kujikuta akitoa ukulele kwa sekunde na kisha kifua chake kikapanda na kushuka na kuanza kuhema kama mbwa aliekimbia maili nyingi na haikuwa kwake tu hata kwa Lekcha hivyohivyo alijikuta akihema sana na kisha alijibwaga pembeni na kulala chali , huku wote wakiwa uchi na safari yao ikawa imefika mwisho.
Ohooo
 
Nipo ndugu yangu, baada ya kuona uzi umeingiliwa huku wakitusagia kunguni basi nimebaki nasoma kimyakimya.
Hahahaaaa Kuna wadau wanatusagia kunguni vibaya mno sie tunao subiri huruma ya mwandishi uku jukwaani.
 
SEHEMU YA 390.

Kilichotokea kwa Edna kuamka mapema nje ya muda Roma alioukadilia ni kama kile kile kilichotokea Ufaransa, wakati Roma akipambana na Depney , sasa haikueleweka kwanini Edna kuathiriwa kidogo sana na nguvu zao miungu , kwani ufaransa aliemlaza kwenye usingizi alikuwa ni Apollo..

Edna aliamka ndani ya lisaa limoja tu , yaani wakati Roma alivyokuwa usingizini ndio muda ambao Edna aliamka na kuanza kuomboleza.

Edna tokea siku ambayo aliweza kujua siri ya mama yake , siri aliopata kupitia flash Disk aliopewa na raisi Kigombola , alikuwa akitegemea siku moja atakuja kugundua kitu ambacho kitakuja kumuumiza sana kihisia.

Ikumbukwe katika flash ambayo Raisi Senga alimpatia Edna , hakukuwa na maelezo mengi , alichokigundua Edna ni kwamba mama yake alikuwa na kisasi alichokuwa akikiendeleza, lakini pia akampa kazi hio ya kisasi yeye kuikamilisha , huku akiacha orodha ya kampuni ambazo hakukuwa na maelezo yoyote kwamba alichokuwa akitakiwa kufanya ni nini mpaka alipokuja kugundua uwepo wa ‘Deposit Box’ ndani ya Swiss In, ambapo ndani yake ilikuwa imebeba bahasha iliokuwa na taarifa ambayo ndio inamfanya kuwa kwenye hali ya huzuni na majonzi.

Raheli Adebayo katika stori yake ya kimaisha mara baada ya kujua ukweli kwamba mtoto wake Lorraine, pacha wake na Edna anaishi kwa jina la Agent 17, ndio kisasi chake kilianza rasmi , lakini kutokana na kwamba watu ambao walikuwa na mtoto wake kuwa wakubwa serikalini, aliamini pesa pekee ndio zitakazo muwezesha kutimiza azma yake, Azma ya kumrudisha mtoto wake huyo ili kutoendelea kujutia kosa alilolifanya miaka mingi nyuma , kosa la kukubali kumuachia Lorraine Kwenda kulelewa na Raisi Jeremy jambo ambalo lilipelekea kadhia ambayo mtoto wake amekutana nayo mpaka kubadilishwa jina , lakini bahati mbaya mpaka anakufa hakuwa ametimiza Azma yake.

Kwahio ni rahisi kusema kwamba Edna sasa anajua kifo cha mama yake ni cha kutengenezwa , lakini hafahamu kama kuna Zaidi ya kile anachokifahamu ambacho kilikuwa kikiendelea kwenye Maisha ya mama yake, anajua tu kwamba mama yake alikuwa mjamzito wa Watoto mapacha lakini hakuwa akielewa pacha mwenzake yupo wapi.

Edna alikaa kitandani akiwa peke yake huku machozi yakiwa yanamtiririka , kila akijaribu kuyafikiria maisha magumu ambayo mama yake alikuwa akiishi moyo wake ulimuuma na alijidharau mno kwa kutogundua kama mama yake alikuwa akipitia kipindi kigumu , yeye kama mtoto alijihisi alikuwa na haki ya kuwa karibu na mama yake lakini kutokana na ubize wa masomo akashindwa kujua kile kinachoendelea.

Baada ya kuwaza na kuwazua alijikuta akifuta machozi yake na kisha akachukua picha ya mama yake iliokuwa pembeni kwenye kijimeza na kisha akaishika kwa kuikodolea macho , lakini kadri alivyokuwa akiangalia alijikuta machozi yakizidi kumtoka kwa mara nyingine , mrembo Edna alionekana kuwa katika hali ya huzuni mno.

“Mom naomba unisamehe , sikuwepo karibu yako wakati ulipokuwa unapitia kipindi kigumu , I am so so….”Alijikuta akishindwa kuendelea na kuanza kulia kwa kwikwi awamu hii kwa takribani nusu saa nzima alizitumia kuomboleza , mpaka aliponyamaza mwenyewe.

“Nitautafuta ukweli wote na nitahakikisha nalipa kisasi kwa ajili yako mama yangu , ndio njia pekee ambayo naamini utanisamehe kwa kutokufahamu kama ulikuwa ukipitia magumu mengi”Aliwaza Edna huku hali yake ikirejea upya , ijapkuwa hakuonyesha furaha , lakini alionekana kuacha kulia na kuwa na sura iliojaa usiriasi.

Saa moja za jioni ndio alishuka kutoka chini huku akiwa ashaongea na halmashauri ya kichwa chake , alishajiambia kwenye akili yake kwamba vita ndio inaanza , vita ya kulipa wale waliohusika kumfanyia mama yake majaribio ya kisayansi mpaka kupelekea kifo chake , alikuwa ashafanya maamuzi tayari , maamuzi ambayo ili kuyakamilisha alitakiwa kuwa na nguvu na sio kukaa kitandani kuomboleza , alitakiwa kuwa jasiri ambaye muda wowote yupo tayari kukabiliana na maumivu ili kutimiza malengo yake.

Muda ambao alikuwa akishuka kutoka juu ndio muda ambao Afande Kweka alipiga simu kumwambia kwamba ataondoka na Lanlan Kwenda nae Iringa kwenye mashamba yake na Edna jibu alilotoa ni kwamba mpaka amshirikishe mume wake Roma kwanza ,lakini Afande Kweka alimwambia atampigia mwenyewe simu kumjulisha.

Roma alienda kukaa karibu na mke wake na kisha kumshika mkono , Blandina aliekuwa amesimama alijiua kuna kinachoendelea , lakini hakutaka kuingilia na alitembea mpaka jikoni kwa ajili ya kuandaa chakula.

Edna alimwangalia Roma alieshika mkono wake , huku akiwa na sura isio jaa furaha wala huzuni , ilikuwa ni sura yake ile ile ya kikauzi ambayo imezoeleka.

“Edna mke wangu , najua unapitia kipindi kigumu kwa sasa na sijui namna ya kurudisha furaha yako, jana nilikuambia nitakuwa bega kwa bega na wewe kwa nyakati zote za furaha na huzuni hilo ndio nilaloweza kukuahidi”Aliongea Roma na Edna alimwangalia Roma kwa dakika kama moja huku vitu vingi vikipita kwenye kichwa chake , haikueleweka alikuwa akifikiria nini lakini alionekana kuwa na hisia mchanganyiko , hisia za kumlaumu Roma kwanini alimficha juu ya Suzzane , kwanini alimficha mara baada ya kujua ukweli juu ya mama yake lakini wakati huo huo aliamini Roma alikuwa na sababu ya kumficha na huenda hata yeye angekuwa kwenye nafasi yake angeweza kufanya hivyo lakini wakati huo huo akiwa na hisia kwamba mambo yote yameanza kuwa hadharani kwasababu ya uwepo wa Roma kwenye Maisha yake.

Edna alijikuta akitoa machozi na kisha alimsogelea Roma na kumkumbatia na kuanza kulia kwa kwikwi , kitendo ambacho kiliwafanya Bi Wena na Blandina waliokuwa wakiandaa chakula kutoka kuangalia kuna nini kinaendelea.

“Roma kwanini Edna yuko hivi umemfanya nini?”Aliongea Blandina kwa wasiwasi huku akimsogelea Edna na kumshika mikono kwa namna ya upendo na Bi Wema na yeye alimsogelea na kukaa mbele yake , huku upande wa Yezi aliekuwa juu chumbani kwake pia akishuka chini aliona jambo hilo na kumsogelea dada yake wa hiari pia.

Wanafamilia wote walionekana kuwa na wasiwasi na Edna na walitaka majibu, kitendo cha Edna kuona kila mwanafamilia alikuwa na wasiwasi juu yake alijikuta akiinua macho yake na kumwangalia Roma kwa huzuni.

“Edna nisikilize kuna hisia mbaya zinaniambia kilichopo kwenye hii bahasha kinaweza kukutoa machozi, nataka uangalie ukiwa nyumbani na watu wote wanaokupenda wakiwa pembeni yako”Edna alijikuta akikumbuka maneno ya Roma na sasa anaelewa alikuwa akimaanisha nini.

Maisha yake yalikuwa yamebadilika sana , alikuwa na watu wengi waliokuwa wakimpenda tofauti na kipindi cha Maisha yake ya nyuma , sasa alikuwa na familia kubwa ambayo yote inamjali sana.

Edna ilibidi awaelezee kile alichogundua , stori yake iliwafanya kila mmoja kushangazwa na jambo hilo na kuhuzunika kwa wakati mmoja na wote walijikuta wakimfariji.

Roma alipendezwa sana na jambo hilo , swala la kuwa na familia iliokuwa inakujali kwa kila kitu , yalikuwa ni Maisha ya kipekee na alijua nini maana yakuwa na familia Maisha yake ya nyuma alikosa kujua radha halisi ya kuwa na familia na hapo yeye mwenyewe ni kama alikuwa katika hatua za kujifunza nini maana ya familia.

Wakati akiendelea kuwaangalia wanafamilia wake , simu yake iliokuwa kwenye mfuko ilianza kuita mfululizo aliitoa na kuangalia jina la mpigaji na alijikuta akishanga, kwani alikuwa ni rafiki yake Makedoni kutoka Mossad.

Roma alinyanyuka na kisha alipandisha juu kwa ajili ya kuongea na Makedoni , kwani aliamini ikitokea Makedoni akianza kumtafuta yeye basi kuna jambo kubwa ambalo limetokea.

“Your Majesty Pluto were you too bored after not killing anyone for two years , why did you destroy the American Fleet entirely” Ilisikika sauti ya kitetemeshi kutoka kwa Makedoni akimuuliza Roma kwamba amechoshwa na kutoua mtu kwa miaka miwili ndio maana akaharibu meli ya kivita ya Kimarekani.

Roma macho yalimtoka , hakuelewa Makedoni alikuwa akimaanisha nini , Meli ya Kimarekani , mtu yupo Tanzania kwanini aharibu Meli ya kivita ya kimarekani ,

“Makedon , What is this nonsense ? what did I do which even I am not privy to?”Aliuliza Roma kwamba ni ujinga gani Makedoni anaongea juu ya kufanya jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakuwa na uelewa nalo.

*******

Ni siku nyingine kabisa alionekana Raisi Jeremy akiwa ndani ya ofisi yake , huku mkononi akiwa ameshikilia picha ndogo , picha ambayo ambayo alikuwa akionekana yeye na mke wake Kizwe wakiwa kwenye pozi la tabasamu huku Kizwe akiwa amevalia gauni la harusi.

Raisi Jeremy picha hio alikuwa akiangalia tokea jana yake usiku alipompa maagizo Linda kwa ajili ya kuandaa mpango wa kumuua Kizwe , mheshimiwa huyu licha ya kufanya maamuzi ya kumuua Kizwe lakini haikumaanisha kwamba hakuwa akiumia ndani kwa ndani, ukweli alikuwa kwenye majonzi makubwa , Kizwe ni mwanamke ambaye alitoka nae mbali sana tokea kabla hata hajawa raisi wa nchi hio ya Rwanda , walipitia nyakati tofauti tofauti , za furaha na zile za huzuni..

Lakini licha ya histora yao, aliamini Kizwe hakuwa na mapenzi kwake tena na kumuweka hai karibu yake ni hatari zaidi, kitendo cha kuweza kuishi kwa kumuigizia kilimfanya hata yeye mwenyewe kumuogapa na kujiuliza ni mangapi Kizwe amemficha , ni mangapi ambayo amefanya pasipo yeye kujua, ndio alikuwa ni mke wake lakini alimuona kama vile amemfahamu juzi na sio miaka mingi iliopita..

Mheshimiwa Jeremy na mke wake Kizwe walibahatika kupata Watoto wawili pekee ,mmoja akiwa ni Desmond ambaye ndio aliekuwa wa kwanza na wa pili alikuwa ni msichana anaefahamika kwa jina la Kyler.

Kyler alikuwa ni marehemu baada ya kupata ajali kwenye mashindano ya magari nchini Marekani wakati alipokuwa masomoni , hivyo unaweza kusema ni Desmond pekee ambaye alibakia kwenye uzao wake ambaye anaweza kumfanya kama mrithi.

“Forgive me Kizwe Mke wangu?”Aliongea Raisi Jeremy kwa huzuni na kisha ile picha ambayo ilikuwa kwenye mikono yake aliichana vipande vinne na kisha akatupia kwenye dastibin.

Muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Linda ambaye amevalia suti ya rangi nyeusi iliomkaa vyema mwilini pamoja na shati rangi ya ugoro ndani yake.

“Mheshimiwa hili ni faili la taarifa za mwanaume aliekuwa na Madam”Aliongea Linda na kisha akampatia raisi Jeremy lile faili na kuanza kulisoma na kadri alivyokuwa akiendelea kusoma alijikuta akishangaa.

“Hii taarifa ni sahihi?”

“Ni sahihi mheshimiwa hata ndugu zake wapo hapa nchini , jimbo la Mashariki”Aliongea na kumfanya Jeremy kufikiria kidogo na kisha akaliweka chini.

“Vipi kuhusu maagizo mengine niliokupatia”

“Kila kitu kipo tayari mheshimiwa, tutampa dawa ambayo itamfanya moyo wake kufeli , ni njia nzuri zaidi ambayo itafanya watu wasitilie mashaka kifo chake”Aliongea Linda kwa huzuni kidogo.

“Okey , nitaelekea State Area D , nikishamaliza mazungumzo ,mpango huo utafuatia”

“Mheshimiwa una uhakika na hili?”

“Linda nishafanya maamuzi tayari na hakuna wa kunizuia tena”Aliongea Raisi Jeremy na kisha alisimama kwa ajili ya kuondoka.

State Area D ni moja ya maeneo maarufu ndani ya Rwanda, eneo hili umaarufu wake ulitokana na kwamba yalikuwa makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Sasa muda huo wa asubuhi ulinzi ndani ya hili eneo ulikuwa umeimarishwa mno tokea jana usiku , sabababu kubwa ya kuimarishwa kwa ulinzi ndani ya eneo hilo na makachero wa serikali ni kutokana na maagizo ya raisi mwenyewe mara baada ya Kizwe na Lelcha kufikishwa kwa siri sana nchini kwa ndege binafsi ya kijeshi.

Kwenye watu ambao walikuwa kwenye maswali mengi ni Lekcha tokea siku ya jana anapandishwa ndege mpaka kufikishwa nchini Rwanda kwake kila kitu ilikuwa ni mshangao , hakuwa akijua ni kipi kinaendelea na alishindwa kuuliza pia , kwani alitenganishwa na Kizwe.

Sasa baada ya kutolewa kwenye ndege na kuingizwa kwenye gari ya pamoja na walinzi ndio alipata nafasi ya kuongea na Kizwe.

“Hey nini kinaendelea , hawa watu walitotuleta hapa ni wakina nani?”Aliuliza Lekcha.

“Vipi una wasiwasi?”

“Wasiwasi , mimi niwe na wasiwasi nishakuwa kwenye hali hatarishi kuliko hata hii , kwanini niwe na wasiwasi, unafikiri kwanini nina mguu bandia , yote haya ni Maisha magumu niliopitia kama nilikuwa tayari kushindana na wanyama wakali kwanini niogope binadamu wachache wanaotaka kunidhuru?”

“Wanyama ni rahisi kuwafukuza kwa hila , lakini kuhusu binadamu ni Habari nyingine , binadamu ni kiumbe kisichotabilika na hatari Zaidi”Aliongea Kizwe na tabasamu la uchungu mno.

“Hey hupaswi kuwa na huzuni kiasi hiki kama vile familia yako yote imekufa , wewe ndio ulitendwa kwanini unaonekana kama mwenye kuogopa kama vile kuna mtu kakuwekea siraha kwenye kichwa chako?”Aliuliza Lekcha lakini kabla hajajibiwa gari ilisimama ndani ya eneo hilo la Area D na geti lilifunguliwa na kuingizwa ndani.

……..

Saa tano kamili za asubuhi ndio muda ambao raisi Jeremy aliweza kufika ndani ya eneo hili la Area D, safari yake ambayo ilikuwa ya kimya kimya akiwa ametangulizana na Linda pamoja na walinzi wachache.

Baada ya kufika tu aliongozwa na wanajeshi wawili waliokuwa wana siraha za moto kuzunguka upande wa nyuma na kuingia kwenye moja ya jengo kati ya matatu yaliokuwa ndani ya eneo hilo la makazi maalumu ya raisi Jeremy.

Baada ya kuingia ndani ya chumba aliweza kukutana na sura mbili , ya kwanza ikiwa ni ya mke wake Kizwe na ya pili ilikuwa ni ya Lekcha , wote wakiwa wameketi kwenye masofa wakiwa chini ya ulinzi mkali.

“Nafikiri unanichukia kwa staili niliokurudisha nchini Rwanda?”Aliuliza Raisi Jeremy bila salamu mara baada ya kumwangalia Kizwe kwa dakika kadhaa.

“Kitendo cha kuja mpaka hapa kwa ajili ya kukutana na mimi licha ya yote , nadhani napaswa kushukuru”Aliongea Kizwe. Na kumfanya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Kwanini uliamua kumchokoza Roma?”Aliuliza kwa kifaransa awamu hii.

“Hindsitght is real bitch , you know that ? You might as well say that I shouldn’t have taken action against that little bitch”

“Nyuma ya pazia ndio kuna mbwa halisi na ndio alietoa maagizo na unafahamu hilo? , unaweza pia kusema sikupaswa kuchukua hatua kwa mbwa huyo mdogo”Aliongea kwa namna ya kimafumbo hapo alikuwa akimlenga Edna na alijibu kwa Kingereza.

“Kaa kimya , kwanini unamwita kwa jina la kukera namna hio , unapaswa kufahamu sasa ni mtoto wangu na pia ni mdogo wake Desmond”Aliongea kwa hasira.

“Mtoto wako.. hahaha… hio mimi inanihusu nini? , Edna ni matokeo ya usaliti wako ulionifanyia , kama sio Afande Athumani babu yake kumlinda ningekuwa nishamuua mpaka wakati huu”Aliongea kwa hasira.

“Sijakuleta hata kwa ajili ya ngonjera zako?”Aliongea Raisi Jeremy

“Uko sahihi kabisa , kama nisiposema ninachotaka nani anajua kama naweza kutopata nafasi tena?”

“Ni bora kama ungeendelea kuniigizia kwa Maisha yako yote na kufanya mambo yako kwa umakini, sisi ni wanandoa lakini kudanganyana ingekuwa bora Zaidi kuliko kilichokutokea kama mke wa raisi, Kizwe nilitamani sana siku utakayogundua juu ya Edna ndio mwanzo wetu mpya na kuzika yaliopita , lakini kwa hili linaloendelea najikuta sina chaguo lingine”Aliongea huku uso wake ukibadilika.

“Unaogopa Jeremy ninaweza kukufanyia jambo baya Zaidi kwa kuweza kukuigizia miaka mingi , unaogopa naweza pia kukutoa kwenye nafasi yak kutokana na nguvu yangu ndani ya taifa hili , hivyo unahisi mimi kuwa hai ni hatari Zaidi kwako”

“Unaweza kuwa sahihi , umepotea siku chache tu lakini mabaraza yote yanataka kujua taarifa zako na serikali kwasasa haiko na utulivu , hata kama nikikuua sasa hivi maswali mengi yataibuka”Aliongea Jeremy.

“Kwahio unataka kunifanya nini?”

“Nina mtu tayari ashaandaa sindano ya kimiminika , ambayo itakuwa na uwezo wa kukufanya kama mgonjwa ambaye moyo wake umefeli , nitaelezea uma baada ya kifo chako kama mke wa raisi lakini mwanaharakati wa taifa hili kwamba baada ya kuwa nje ya nchi ulipatwa na tatizo ambalo lilipelekea tatizo la moyo na kutokuonekana kwako hadharani kwa siku hizi chache ni kutokana na kwamba ulikuwa chini ya uangalizi wa madaktari wakijaribu kuokoa afya yako , lakini mwisho wa siku hakuna kilichowezekana kwani hali yako ilikuwa kwenye hatua ya mwisho kabisa”Aliongea Jeremy bila ya kuwa na huzuni kabisa , alionekana ashavunja ndoa yake na kizwe moyoni mwake pekee na hakuna chochote ambacho anajutia.

Kizwe alijikuta akishangazwa kabisa na maneno ya mume wake yakimtoka bila wasiwasi kabisa.

“Sikuweza hata siku moja kufikiria kama itakuja siku mume wangu ndio anaagiza kifo changu , maneno yanakutoka kana kwamba hatukuwahi kupendana hapo kabla , hakika wewe ni raisi wa taifa hili ambaye unapambana kwa maendeleo makubwa Zaidi , Hahahaha… haha,, mbinu yako Jeremy ni nzuri sana na haiwezi kabisa kuacha maswali kama kweli nitakufa kwa shida ya moyo ni mbinu nzuri sana umefikiria”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kufumba macho kwa hisia na kisha akayafumbua.

“Dawa utakayopewa itakuletea maumivu katika mchakato mzima wa kuathiri moyo wako , nilitamani kufanya kifo chako kisiwe cha maumivu lakini hakuna mbinu mbadala Zaidi ya hii , Kizwe nakuhakikishia baada ya kifo chako mwanao Desmond atarithi kila kitu changu nakuahidi”Aliongea

“Hakika utamrithisha kila kitu , sio kwasababu unampenda bali ni kwasababu hauna mbadala hahahaha.., kuna muda nishawahi kufikiria kama Edna angekuwa mwanaume agekuwa na nafasi sawa na Desmond? , kinachoniumiza siku zote kila nilivyojitahidi kujitoa kwa ajili ya Desmond lakini hukukubali msaada wangu na kunipenda kama mkeo bali mawazo yako yalikuwa kwa mpuuzi Raheli na mtoto wake muda wote”Alifoka lakini Jeremy alishindwa kumjibu alimwacha aongee kwani ndio siku yake ya mwisho ya uhai hata hivyo.

“Kwasababu nitakufa muda wowote naomba nikuambie siri ambayo niliificha kwa miaka mingi , ili kukuonysha ni kwa kiasi gani wewe ni mbumbumbu “

“Siri gani?”

“Miaka iliopita sio kweli kwamba Raheli alikufa kwa kansa ya damu iliompelekea moyo wake kufeli”

“Unataka kumaanisha nini?”Aliongea Jeremy kwa wasiwasi.

“Namaanisha kama unavyofikiria , najua hakuwahi kufikiria lakini daktari Hubery aliekuwa akimhudumia Raheli alikuwa chini yangu na vipimo vyake vya kimatibabu vilivyotolewa hospitalini vyote vilikuwa ni feki, hakuna ugonjwa uliomuua bali nilimuua mimi kwa mikono yangu”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kuanza kutetemeka kwa hasira.

“Wewe mwanamke ni shetani wa aina gani , hivi unajua ni kwa kiasi ganri Raheli alikuwa akikujali , ni kweli nilikuwa na uhusiano nae lakini hakutaka uhusiano wake na mimi kukuathiri hata kidogo , ndio maana akaamua kuolewa na mwanaume asiekuwa na mapenzi nae , aliishi bila ya kunitafuta na siku zote mimi ndio niliekuwa nikimsumbua ,kwanini hukujali yote hayo na alikuwa rafiki yako?”Aliongea kwa hasira mno , huku macho yake yakiwa mekundu.

“Niite shetani na majina mengine ,lakini siku zote nilikuwa mwenye kupta ninachokitaka”Aliongea bila ya hatia.

“Sawa ulichokifanya kishakwisha kufanyika , ni wakati wa kulipwa kwa makosa yako , jitafakari kwa matendo yako yote kabla ya sumu ya kifo haijaletwa kwako na kuchomwa”Aliongea na kisha alimwangalia Lekcha.

“Kwasababu huyu bwana wako ndio aliekuokoa lakini pia ameweza kusikiliza kila kitu, tulichoongea hapa angalau safari yako haitakuwa ya kinyonge mnaweza kuendelza mapenzi yenu mbele ya safari huko kuzimu”Aliongea na kisha akaondoka kwenye chumba hicho na kuwaacha marehemu watarajiwa.

MWISHO WA SEASON 13

Unafikiri ni nani alieharibu meli ya kivita ya Marekani , je ni Hades kama alivyosema Makedoni.

Yan Buwen na teknolojia yake ya Growth acceleration kama ni kutengeneza Clone ya Roma basi atahitaji angalau miezi minne , swali je amefanikiwa nje ya miezi minne.

Je kifo cha Kizwe ndio mwanzo wa Jeremy kumtangaza Edna kama mtoto wake , unafikiria Desmond atakuwa na hali gani akijua baba yake ndio aliemuua mama yake.

Yajayo yanafurahisha sanaaaaaa…..

OYA ACHA UBAHILI BWANA NI BUKU TATU TU KUJIUNGA GRUPU TUPO SEHEMU YA 460 , NICHEKI NAMBA 0687151346 ONLY WATSAPP

SEE YOU SOON
BWANA Singanojr sio ubahili wa kutoa buku tatu ila jistori limeanza kupoteza ladha
 
Singanojr ukumbuke pia uku una wahitaji ndugu yangu usiwe kimya sana..
Kama itakupendeza leo tukumbuke na sisi..
 
Back
Top Bottom