SEHEMU YA 428.
Mwanaume Chriss ambaye anaekutana na Suzzane alikuwa ndio moja ya vijana ambao walikuwa wakiaminiwa na Mheshimiwa Barack Mabo mpaka pale Chriss alipofanikisha kurekodi mazungumzo ya raisi na yeye mwenyewe lakini pia mazungumzo ya Raisi Kigombola na Raisi Barack Mabo.
Na baada ya Chriss kurekodi sauti hizo ndipo alipompatia mfanyakazi wa ikulu wa kitengo cha mawasiliano afahamikae kwa jina la Suphian Kangasi na ndio huyo Suphiani Kangasi alievujisha sauti hizo kwenda kwa Raisi Jeremy Paul lakini wakati huo huo akikabidhi sauti hizo kwa jasusi Dr Elvice Daniel kwa kumpa maagizo wa sauti hizo kupatiwa na Chriss.
Chriss anabanwa na serikali ya Marekani ili kusema nani alikuwa anashirikiana nae mpaka kufanikisha kurekodi sauti hizo pamoja na teknolojia aliotumia lakini Chriss anaonyesha hali ya kuchanganyikiwa kwani anashindwa kujibu maswali anayoulizwa na mwisho wa siku wanasaikolojia wanahitimisha Chriss kuugua ugonjwa wa Munchauson Syndrome.
Serikali ya Marekani ikiwa imemfungia gerezani wanajikuta kwenye sintofahamu mara baada ya Chriss kupotea kwa namna isioelezeka na utorokaji wake gerezani unakuwa kitendawili, FBI kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama wanamtafuta Chriss kwa kujaribu kufumbua fumbo la namna alivyotoroka lakini wanashindwa kuelewa.
Swala la kutoroka kwa Chriss akiwa kizuizini linamfikia mheshimiwa Barack Mabo na raisi huyo mara baada ya kufikiria sana anahitimisha huenda Chriss alitoroshwa na sehemu ya miungu , kwani kwa mazingira ya Chriss aliotorokea anaamini hakuna binadamu wa kawaida anaeweza kufanya hivyo na kufanikisha , lakini swali linabakia kama Chriss katoroshwa na miungu je ni kwasababu ipi na kwanini miungu hio ifanye hivyo anaendelea kufikiria na kufikia kwenye hitimisho kwamba huenda hata kitendo cha kufanikisha kurekodiwa kwa sauti yake ndani ya ikulu ya Tanzania kumefanikishwa na sehemu ya miungu.
Katika taifa ambalo linaongoza kwa kupitia mambo ya ajabu ni taifa la Marekani , huenda kila raisi aliehudumu ndani ya ikulu ya White hose amepitia mambo ambayo hayafikiriki kwa akili za kawaida na moja ya maajabu makubwa ni namna ambavyo watuhumiwa kupotea kwa namna isivyokuwa ya kawaida.
Huenda kwenye faili la watuhumiwa ambao wametoroka kwenye mazingira ya kutatanisha na kutafutwa mpaka leo ni wengi na katika majina hayo huwezi kukosa jina la Chriss Alton , Carlos , Phill Knight, Shekhe Assad , Afshar Bahman na wengine wengi.
Mambo haya yameishia kubakia kitendawili na sababu ni kwamba hata kama ndani ya ikulu kuwahisi miungu kwa kazi hizo waliishia kupotezea kuokana na sera ya utunzaji wa siri ya miungu hio chini ya kitengo cha Zeros.
Lakini sasa jambo ambalo limebakia kuwa kiza kwao ni kwamba kati ya watu wote waliopotea ndio asilimia kubwa huunda jamii ya siri ambayo inajiita Ant – Illuminat , jamii ambayo inatumia nembo ya visiwa vya wafu katika kujitambulisha , jamii ambayo mwanzilishi wake ni Hades.
Chriss sasa anarudi Tanzania kwa misheni maalumu baada ya kutokukamilisha kile alichokianzisha, haijulikani mara baada ya kutoka Marekani aliishi wapi na alifanya nini lakini kwa mara ya kwanza anaonekana ndani ya Taifa la Tanzania na mtu wa kwanza katika misheni yake anaonana na Suzzane.
“Kwanza nikupe pole kwa kumpoteza mpenzi wako , nilipata kusikia mlikuwa kwenye hatua za mwisho za kufunga ndoa mpaka umauti ulipomkuta”Aliongea Chriss na kumfanya Suzzane kuwa na huzuni kidogo.
“Nishapoa kwa sasa lakini Elvice ameshindwa kufutika kwenye akili yangu na ndio maana mtu yoyote anapotaja jina lake kwa namna ya kumfahamu naguswa sana”
“Miss Suzzane najua una kisasi ndani ya moyo wako kwa wale waliohusika na kifo cha mpenzi wako lakini nikueleze kwamba Chriss na Raheli walikuwa kwenye vita , hivyo naweza kusema wamekufa wakiwa mashujaa, hivyo pale mwanajeshi anapokufa kwenye vita sio kwamba vita inakwisha bali wanaobaki ndio wanaendeleza na ndio tunachokwenda kukifanya , siku ya leo nataka kukupa mwanga kwanini Elvice mpenzi wako alikufa na ni vita ya namna gani ambayo alikuwa akipigana ili tuone kama upo tayari kuendeleza pale alipoishia”Aliongea na kupozi.
“Vita aliokuwa akipigania Elvice na Boss wako Raheli ilikuwa ni ya kuiponya dunia na ugonjwa unaoanza kuonyesha dalili”
“Unamaanisha nini kusema ugonjwa unaoanza kuonyesha Dalili?”Aliuliza Suzzane huku akionyesha hali ya kuchanganyikiwa lakini bwana Chriss anaonekana kuwa kwenye utulivu wa hali ya juu.
“Miss Suzzane wewe ni dini gani?”Aliuliza.
“Mimi ni mkristo tu kwa jina kutokana na wazazi wangu kuwa wakatoliki”Aliongea.
“Unamaanisha wewe ni mkristo ambaye huzingatii sana maswala ya dini?”Aliuliza na Suzzane alitingisha kichwa.
“Kupitia dini yako unatafsiri vipi mwendendo wa dunia ya sasa kwa mtazamo wa kimaadili katika Dini?”Suzzane alishangazwa na swali hilo lakini aliishia kujibu kwa kifupu na kusema dunia kwa kupindi cha sasa kuna mmomonyoko wa maadili mkubwa tofauti na zamani , akagusia kidogo maswala ya ndoa za jinsia moja ambazo baadhi ya makanisa wanaanza kutambua na mambo mengine husianishi.
“Well! Ulichozungumza ni sahihi kabisa na sipaswi kuongezea zaidi ila ninachotaka kukufahamisha alichokuwa akipigania mpenzi wako ni kile kinachoendelea kwasasa, kitu ambacho napenda kuita dalili za ugonjwa ambapo umebainisha wewe mwenywe’Aliongea na kumfanya Suzzane kuonekana kuchanganyikiwa.
“Kama nilivyokwisha kujitambulisha mimi ni mwanachama wa jamii ya siri ya Ant -Illuminat basi jamii yetu inaenda kinyume na jamii ya siri ya Illuminat , labda kwa kukurahisishia mambo unayoyaona kwa sasa ambayo ni dalili ya ugonjwa ni kwamba yanasababishwa na jamii nyingi za siri ambazo zipo chini ya Illuminat”Aliongea , ijapokuwa Suzzane hakuwa mpenzi sana wa habari za kutunga kama vile uwepo wa Freemason na jamii nyingi za siri lakini alikuwa akisikia kuhusu hizo jamii na kwenye maisha yake hakuwahi kuamini kama zipo na kufanya kazi.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba Elvice alikuwa ndani ya jamii hii ya Ant illuminat?”
“Elvice alikuwa ni mwanachama anaeandaliwa lakini bahati mbaya umauti ulimkuta akiwa katika kutimiza wajibu na watu waliohusika na kifo chake ni hawa Illuminat , Miss Suzzane dhumuni la mazungumzo haya sio kukuchanganya ila kwanza ni kukubadilisha mtazamo wako pamoja na sumu iliopo ndani ya moyo wako , ninachojaribu kukuambia Elvice alikuwa kwenye mapambano kama mwanajeshi na amefia vitani na mapambano hayana budi kuendelea m hivyo kwa leo sitokuelezea zaidi kuhusu jamii yetu bali kile ninachotaka kutoka kwako”Aliongea
“Unataka nini kutoka kwangu?”
“Kabla sijakuelezea ninachotaka kutoka kwako haswa na kile ambacho unapaswa kufanya, nataka kuzungumza na Miss Edna na nitaweka wazi kile ambacho kimesababisha kifo cha Elvice haswa ni nini akiwa vitani”Aliongea na kumfanya Suzzane kushangaa.
“Kama ni swala la bosi wangu nadhani unao uwezo wa kuongea nae moja kwa moja sio kupitia mimi”
“Kuhusu kuongea na bosi wako moja kwa moja uwezekano huo upo lakini swala hili linakuhusu pia kama linavyomhusu Edna ,nataka upange namna ya mimi kukutana na Edna pasipo ya mume wake kufahamu na mengine muhimu zaidi utayajua hapo hapo”Aliongea na kumfanya Suzzane kufikiria.
“Nitajaribu lakini eneo nitachagua , pili lazima uniahidi utanielezea kila kitu kilichotokea na kumfanya Elvice kuingia kwenye vita na watu wasiofahamika”
“Naahidi kukuelezea kila kitu kama utakamilisha ombi langu , lakini swala la mwisho ninalotaka kujua kutoka kwako ni kwa kiasi gani Edna anajua kuhusu pacha wake?”Aliongea na kumfanya Suzzane kutoa mshangao.
“Unazungumzia nni?”
“Oh kwa mshangao wako nadhani hautokuwa na ufahamu juu ya boss wako kuzaliwa na pacha wake, naamini huenda hata yeye mwenyewe hajui , kama ni hivyo naamini ushahidi wa sauti haujamfikia”Aliongea .
“Unamaanisha nini kuhusu ushahidi wa sauti?”Aliuliza Suzzane huku akianza kuchangamka na Chriss aliokota kile kikadi kwenye meza na kisha akamuonyesha ile nembo ya visiwa vya wafu iliokuwa kwenye kikadi hicho.
“Niambie umefahamu vipi kuhusu hii nembo?”
“Nilikuwa na kikadi mfano wa hiki ambacho kilikuwa na jina la Hades kama sikosei na nimempatia mume wake Edna”Aliongea Suzzane.
“Alright miss Suzzane fanya kama nilivyo kuelezea , hakikisha naonana na Miss Edna pasipo ya mume wake kufahamu na nitakuelezea kuhusu ushahidi wa sauti , ndio jibu la kwanini Elvice alikufa”Aliongea na kumfanya Suzzane kutingisha kichwa kukubali lakini bado akiwa kwenye hali ya kuchanganyikiwa , hususani sehemu ya pacha wa Edna pamoja na ushahidi wa sauti.
Suzzane mara baada ya kuingia kwenye gari yake alijikuta akivuta pumzi na kuanza kukumbuka moja ya kazi ambayo alipewa na Edna.
Edna mara baada ya kujua kwamba Suzzane alimficha kwa muda mrefu juu ya yale aliokuwa akiyajua juu ya kifo cha mama yake kusababishwa na watu kwa kufanyia mwili wake majaribio alijikuta akiwaza sana kwanini Suzzane alikuwa alimficha juu ya jambo hilo na aliweza kukutana na Suzzane na kumuhoji na ndipo Suzzane alipomwambia Edna kwamba maagizo aliopewa na mama yake ni kwamba nyaraka aliokuwa ameachiwa alipaswa kumpatia mume wake na sio yeye na ndio maana alikaa kimya.
Edna alishangazwa sana na jibu hilo , lakini kilichomchanganya zaidi ni kwanini mama yake kutoa maagizo hayo na zaidi ni pale Suzzane alipomtaja kabisa Hades kwa jina lake.
Yaani Suzzane alimwambia kwamba nyaraka alipaswa kupatiwa Hades na sio yeye , sasa kitendawili hiko kilimchanganya sana Edna kwani kauli ya mama yake ni kama aliona atakuja kuolewa na Roma ndio maana akatamka maneno hayo.
Swali alilokuwa nalo Edna tokea anaongea na Suzzane na kutaka kujua sababu ya kumficha ndio swali ambalo alikuwa nalo Roma , yaani wote walikuwa wakijiuliza kwanini Mama yake Edna akafahamu Roma na Edna kukutana na mwishoe kuwa mume na mke , kilikuwa ni kitendawili ambacho hata Suzzane pia hakuwa akijua jawabu lake , lakini kwa upande wa Roma kuna kitu ambacho alikuwa akihisi lakini hakuwa na uhakika sana lakini aliamini jibu hilo linahusiana na mtangulizi wake yaani Hades wa Zamani.
Sasa Suzzane aliekaa kwenye gari lake ndani ya eneo la maegesho alikuwa akijiuliza swali la namna moja , lakini kubwa zaidi alikumbuka wiki kadhaa nyumba bosi wake Edna alimpa kazi ya kutafuta taarifa za miaka mingi iliopita zinazohusiana na mama yake wakati alipokuwa mjamzito, taarifa ambazo ameshindwa kabisa kuzipata licha ya kufatilia sana ndani ya hospitali ya Muhimbili , lakin mara baada ya muda huo kumaliza maongezi yake na Chriss ni kama sasa anajua nini Edna anajaribu kutafuta , aliamini huenda bosi wake alikuwa alishafamu kuzaliwa na pacha wake.
“Nitampelekea ripoti kesho na nitajua zaidi , huenda kuna kitu ambacho aliweza kupata ndani ya benki ya Swiss na hataki kuniambia , nadhani ndio ushahidi wa sauti anaozungumzia Chriss , nitaongea nae na kumshawishi kuonana na Chriss pia”Aliwaza Suzzane na kisha aliwasha gari lake na kuondoka eneo hilo
Upande wa Chriss mara baada ya Suzzane kuondoka alionekana kuongea na simu.
“Ndio nimemaliza kufanya nae mazungumzo na nimempa kazi ya kunikutanisha na Edna”.
“Kazi nzuri , unapanga kufanya nini baada ya kuonana nae?”
“Nadhani Hades kamficha mambo mengi kuhusu pacha wake , napanga kumwambia kila kitu kuhusu mpango LADO”
“Shekhe anasemaje?”
“Niumewapa maelezo kama ulivyonielezea na wametokea kuamini na wameniruhusu kuendelea na misheni yangu ila sijawaelezea inahusiana na nini moja kwa moja , niendelee kama ilivyopangwa?”
“No there are some changes of plan”
“Hapana , kuna mabadiliko ya mpango”Ilisikika sauti upande wa pili na kumfanya Chriss kushangaa.
“What..”
“Ambacho kilishindikikana kufanyika miaka nane iliopita awamu hii nataka ukitekeleze , ndio namna pekee ya kufanya mpango wetu kufanikiwa”
“Boss unamaanisha…?”
“Yes na ukifanikisha potea mara moja , nadhani umefunzwa kwa kazi hio , na unajua Alama ambayo inatakiwa kubakia eneo la tukio?”
“Ndio boss”.
“Then Good , I will call you myself as soon as I receive good news of success”
“Basi vizuri , nitakupigia mwenyewe mara tu baada ya kusikia taarifa nzuri ya mafanikio”Aliongea na kisha simu ikakatwa.
“F**ck kama sitokamilisha kwa ustadi wa hali ya juu naweza kupoteza maisha , natakiwa kuhakikisha swala hili linaenda vizuri”Aliwaza Chriss.
*********
Roma na Afande Maeda waliweza kukutana ndani ya hoteli hio katika eneo la mgahawa na kuanza mazungumzo yao mara moja.
“Okey Afande nadhani uanze kuzungumza , maana umenificha mambo mengi ambayo naamini unayajua na yananihusu mimi”Aliongea Roma mara baada ya kupatiwa vinywaji walivyoagiza.
“Nadhani unajua mengi zaidi kuliko mimi Mr Roma , lakini sio mbaya nitaeleza yale machache ambayo nayajua lakini pia kuweka lengo langu wazi la kutaka kufanya mazungumzo haya na wewe muda huu”Aliongea Afande na Roma alitingisha kichwa.
“Nadhani kama mwanajeshi unaelewa kwamba kuna mstari wa utenganisho kati ya jeshi na siasa licha ya kwamba wakuu wetu wa mwisho kimadaraka ni mwanasiasa”
“Ndio maana sipendi mwanasiasa ambae sio mwanajeshi na sipendezwi sana na demokrasia kwani ni chanzo cha matatizo mengi”Aliongea Rom na kumfanya Afande Maeda kucheka kidogo.
“Huo ndio mtazamo wako?”
“Nina mitazamo mingi”
“Ni wajibu wa jeshi kufatilia mambo yote ambayo yanagusa usalama wa nchi moja kwa moja ndio maana miezi michache iliopita jeshi lilianza kufatilia baadhi ya vikao vya siri ambavyo vilikuwa vikifanyika kwa siri kati ya Raisi mstaafu Kigombola na Jenerali wa jeshi la China bwana Yang Gongming , lakini licha ya hivyo pia serikali ina makubaliano na jeshi la china katika maswala ya utengenezwaji wa siraha za kivita”
“Ni jambo la kawaida kwa jeshi kama la Tanzania kuwa na makubaliano kwa nchi zilizoendelea katika maswala ya siraha , lakini siku zote makubaliano yanakuwa ‘Mutual’ , kwa maana kwamba pande zote lazima zinafaidika hivi ndio ambacho kinalifanya taifa letu kuendelea kuwa na ushirikano wa karibu na China kwa miaka mingi , lakini licha ya hivyo miaka ya hivi karibuni ushirikiano kati ya viongozi wa jeshi na Mheshimiwa mstaafu umeongozeka kwa kiasi kikubwa jambo ambalo sisi kama jeshi linatufanya kuona kama hatari na ndio llilipelekea kuanza kuweka watu wetu ndani ya ‘Circle’ ya mheshimiwa mstaafu ili kujua baadhi ya mambo muhimu ya kiusalama yanayoendelea , na katika kufatilia ndipo tulipokuja kugundua makubaliano ya mheshimiwa Kigombola na Afande Yang”Aliongea
“Makubaliano gani?”
“Makubaliano yaliopo ni kuhusu Yan Buwen kupewa ‘clearence’ ya kutumia maabara ya siri ya Even Lab, haya ni makubaliano ambayo kama jeshi yalitufikirisha , kwani ndani ya China kuna maabara bora zaidi kuliko Even Lab na hata kabla ya Yan Buwen kuhamia hapa nchini alikuwa akifanya kazi chini ya maabara ya kijeshi katika kitengo cha ugunduzi wa teknolojia za siraha”
“Unataka kusema kwamba kifo cha Profesa Shelukjindo kilisababishwa na Serikali ya China na ya Tanzania , kama ni kweli kwanini?”Aliuliza Roma ijapokuwa alikuwa na uhakika kiasi huenda Yan Buwen alikuwa akitengeneza siraha kwa kutumia kanuni na gunduzi zilizoachwa na Profesa Shelukindo.
“Kuhusu sababau halisi sijaipata moja kwa moja lakini kutoka na msururu wa matukio tunaamini kuna kitu kikubwa sana ambacho Yan Buwen anatengeneza ndani ya maabara na kinachofanya kupata hisia hizi ni mara baada ya ukamilishwaji wa mpango wa kupatikana kwa damu yako ,. Mwanzoni nilichulia swala hili kawaida sana , lakini mara baada ya wiki kadhaa kupokea taarifa ya wewe kushambulia meli ya kivita ya kimarekani moja kwa moja niliamini huenda kuna uhusiano mkubwa sana na kile kinachoendelea ndani ya maabara hio”
“Kuhusu damu yangu kuchukuliwa ni swala ambalo niliweza kufahamu lakini sikutaka sana kulipa kipaumbele sana , lakini nilishangazwa baada ya shushu wako kunielezea juu ya mpango wa upatikanaji wa damu yangu nilihisi kuna mchezo unajaribu kufanya”
“Hakuna mchezo ambao unafanyika kwa upande wa jeshi , lakini hata hivyo swala la damu nilikuwa bado tukilifanyia ufumbuzi na sasa kwa mbali nadhani tunapata majibu ambayo tunayategemea”
“Kwanini mnamruhusu mstaafu kuweza kuhatarisha usalama wa nchi kwa kufadhili mamluki?”
“Hatuwezi kumchukulia hatua Mheshimiwa mstaafu kwasababu jeshi letu sio kama la nchi nyingine , ndani ya jeshi kuna siasa nyingi hivyo unaweza kusema kupata wanajeshi wasioegemea upande mmoja ni bahati sana , tunafanya mambo kwa akili ili kuepusha migogoro, kuna wanajeshi wapo ‘ neurtral’ lakini kuna wale ambao wanam mtii mheshimiwa mstaafu, ni rahisi kusema kila raisi anaetoka madarakani ana wanajeshi wake wanaomtii na kusikiliza maagizo yake waachotofautiana ni ule ukubwa wake”Aliongea Afande Maeda na kumshangaza kidogo Roma , lakini hata hivyo maswala ya jeshi la Tanzania hayakuwa yakimhusu kabisa.
“Kama kazi mmeishidnwa nitawasaidia , nitaanza na huyu Mzee Longoli kumuua kwa kunichokoza na kisha atafuatia mheshimiwa mstaafu, huyu mpuuzi Yan Buwen chochote anachotengeneza huko ndani ya maabara hakiwezi kunipatia shida na siku akiingia kwenye kumi na nane zangu nitamuuua”Aliongea Roma.
“Mr Roma nikusihi usije ukamuua Mzee Longoli kwani ni moja ya watu wenye mizizi kwenye taifa hili”Aliongea na kumfanya Roma kukunja sura.
“Huyu Longoli anahuika hahusiki kuiba damu yangu?”
“Anahusika lakini ninachotaka kuongea ni kwamba mambo bado tunalifanyia kazi , nimetaka kukutana na wewe mapema ili kukusihi jambo hili utuachie sisi”
“Kazi hio unaifanyia kisiasa zaidi na mwanajeshi na siasa ni vitu viwili tofauti , nitamuua kwanza huyu Longoli na nitakusaidia kupata majibu ambayo wewe mwenyewe bado huyajui, ili kulinda usalama wa nchi hupaswi kuzunguka zunguka kuondoa tishio , unahitaji majibu ya haraka pasipo kujali jina la mtu ndani ya serikali”Aliongea Roma na kisha alisimama.
“Afande haya mazungumzo yashaisha , umeongea sana ila nilichotaka kutoka kwako ni kuthibitisha mambo mawili tu , kama kweli huyu anaejiita Longoli anahusika au Lah na jibu langu umenipatia anahusika , unaonekana kuwa na maswali mengi sana nitakusaidia kwenye maswala ya uchunguzi”Aliongea Roma na kisha hakutaka kusubiri jibu aliondoka akimuacha Afande Maeda akiwa mdomo wazi.
Roma baada ya kutoka tu ndani ya eneo hilo alitoa simu yake na kumpigia Diego na alionekana kuna maagizo ambayo alikuwa akimpatia na kisha akatabasamu na kuziendea lift, ndani ya dakika chache tu alikuwa kwenye chumba 104 na baada ya kugonga mlango ulifunguliwa na Rose aliekuwa amejifunga taulo Rangi nyeupe kuanzia kwenye kifua na likaishia kwenye magoti.
Rose alimwangalia Roma kwa tabasamu flani hivi la kihuni na kisha alimshika ukosi wa shati na kumvutia ndani ya chumba na Roma na yeye alijilegeza na kuingia kizembe.
“Leo ni kutekwa staili” Ilisikika sauti ya Roma.
Upande wa Afande Maeda mara baada ya Roma kumuacha alipangusa simu ya kwa sekunde kadhaa na kisha akaweka sikioni.
“Mmefikia wapi?”Aliuliza.
“Yupo tayari kwenye Safe House Afande”
“Okey kazi nzuri”Aliongea na kisha aling’ata meno kwa hasira na kutoka eneo hilo .
*****
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa Edna alienda kazini kama kawaida huku kazi ya kufuatilia makazi mapya aliachiwa Roma.
Upande wa Edna asubuhi hio aliweza kupokea simu kutoka kwa Suzzane akimwambia kwamba anakuja kuonana nae ofisini kwani kuna ripoti anataka kumpatia na Edna alikubali huku akiwa na shauku ni kipi ambacho Suzzane anataka kumwambia kwani alimpa kazi muhimu sana.
Edna mara baada ya kufika kazini aliweza kupita kwenye idara baadhi na kuweza kutoa maagizo na mpaka anakuja kumaliza idara zote ilikuwa saa tano kamili na aliweza kuingia ofisini kwake na kisha akatulia kwenye kiti chake na haikupita muda mrefu Recho aliingia na kumpa taarifa ya kufika kwa Suzzane na Edna alimpa ruhusa ya kuingia.
“Enhe umefikia wapi?”Aliuliza Edna mara tu ya kusalimiana na Suzzane.
“Taarifa zimekuwa ngumu sana kupatikana , tumejaribu kutumia mpaka pesa lakini inaonekana hospitali haina taarifa”Aliongea Suzzane na kumfanya Edna kunyong’onyea.
“Vipi kuhusu manesi au madaktari wa kipindi hicho?”
“Tumejaribu kufuatilia na tumeweza kupata wawili ambao walikuwa wakihudumu kwa kipindi hicho lakini taarifa zao ni za kusikitisha , wote walishapoteza maisha”
“Nadhani kulikuwa na changamoto kweli kwa Taifa kama Tanzania kwenye utunzaji wa kumbukumbu hata hivyo ni miaka mingi iliopita na teknolojia haikuwa kubwa sana”Aliongea Edna kwa namna ya kukata tamaaa na Suzzane alimwangalia Edna na kisha akauvaa ujasiri.
“Edna unachotaka kujua ni kuhusu mama yako kujifungua mapacha si ndio?”Aliuliza Suzzane na kumfanya Edna amwangalie Suzzane kwa mshangao.
“Suzzane nadhani nilikuambia tu utafute taarifa na sijakuelezea kama zinahusiana na mimi kuzaliwa na pacha wangu?”Aliuliza Edna.
“Ni kweli kabisa hata mimi swala hili sikulifahamu mpaka siku ya jana”Aliongea na kumfanya Edna kumwangalia kwa kiulizo.
“Unamaanisha nini?”Aliuliza Edna na Suzzane ilibidi amuelezee kwa ufupi namna ambavo aliweza kupokea simu kwa mtu aliejitambulisha kwake kwa jina la Chriss na kumuelezea namna ambavyo anajua nini kilimuua Dr Elvice Daniel na kuomba kukutana nae ili aweze kuongea nae.
Aliendelea kumwambia namna ambavyo alaiweza kuonana na Chriss ndani ya hoteli ya Eunice na namna mazungumzo yao yalivyokuwa.
Mpaka Suzzane anamaliza kuongea Edna alishangazwa mno na taarifa hio na kujawa na shauku pia ya kumjua Chriss.
“Kwahio umesema amezungumzia mimi kuzaliwa na pacha wangu!!?”
“Ndio anasema ataongea zaidi mara baada ya kukutana”
“Lini anataka tukutane?”
“Kaniambia kwanza swala lenyewe linatakiwa kuwa siri , na kuhusu mahali na muda ni mimi ninapanga na kumtaarifu”
“Okey hili ni swala muhimu sana kwangu , tutakutana nae kesho unaweza kupanga eneo lolote ambalo unaona litafaa na utanitaarifu”
“Boss napanga iwe kule mji wa kisasa kwenye nyumba yangu , ni sehemu salama zaidi”Aliongea Suzzane na kumfanya Edna kufikiria kidogo.
“Okey sio mbaya hata pale ni mahali sahihi zaidi”Aliongea Edna na Suzzane alitingisha kichwa na kisha kuaga. Wakiwa kwenye makubaliano ya siku inayofuata waweze kukutana na Chriss mahali anapoishi Suzzane.
*******
Taratibu zote za kuhamia kwenye nyumba mpya zilikamilika kwa asilimia mia moja na kila kitu kilihamishwa kwa msaada wa kampuni.
Hivyo Dorisi , Rose , na Nasra wakawa majirani , mama yake Nasra alionekana kushangazwa sana na ukubwa jumba hilo kiasi kwamba alimshukuru mara kibao Edna kwa kuwezesha swala hilo , ijapokuwa hata kule kwenye Apartment walipokuwa wakiishi palikuwa pazuri lakini eneo la jumba hilo palikuwa pazuri zaidi ukilinganisha na ukubwa wake.
Saa moja za jioni ndio muda ambao waliweza kumaliza kupangilia kila kitu na hata Sophia aliweza kurudi kuona mahali familia yake ilipohamia na alipapenda mwenyewe kutokana na uzuri wa nyumba lakini pia kufurahishwa na eneo kuwa kubwa mno ndani ya uzio tofauti na Oysterbay.
Kwasababu kila mtu alichoka na kazi nzima ya kupanga ilibidi waende kula mgahawani chakula cha usiku wazo ambalo Roma alipendekeza na kuonekana bora.
Na familia nzima walitoka na kwenda katika moja ya mgahawa uliokuwa ndani ya eneo hilo ambalo ulikuwa wa hadhi ya juu, ulikuwa ni mgahawa wenye floor mbili yaani juu na chini na Edna ndio alipendekeza wakakae upande wa juu na hilo ni kutokana na uwepo wa Sophia ambaye ni maarufu , hawakutaka usumbufu.
Baada ya familia nzima kuingia ndani ya eneo hilo , huku wakipotezea baadhi ya macho yanayowaangalia walikaa kwenye meza mbili tofauti lakini zilizokuwa karibu karibu huku wakiongea na kucheka.
Edna yeye alikaa meza moja na Lanlan, Sophia pamoja na Roma huku Qiang Xi , Mama yake Roma na Bi Wema wakikaa meza moja.
Wakati Edna akiwa bize kuangalia Menu ya chakula kwa ajili ya kuagiza kuna jambo lilimvutia macho Roma na kumfanya agune kiasi cha kumfanya Edna kumwangalia kwa mshangao.
Alikuwa ni mhudumu wa kiume aliechanganya rangi , alionekana kushikilia sinia ya plastic kubwa yenye sahani nne juu yake za vyakula huku akieleka kwenye meza moja ambayo imekaliwa na familia ya watu wanne mmoja ni msichana mdogo miaka kama kumi na tano hivi na mwingine alikuwa ni mvulana mkubwa kuliko msichana huku wakiwa na wazazi wao , mmoja alikuwa ni mzee wa makamo miaka kama hamsini hivi na mwingine mwanamama mweupe ambaye pia alionekana kuwa na miaka kama arobaini.
Roma alimwangalia yule muhudumu anavyoendelea kuweka sinia kubwa liliojaa sahani nne jumla yake , ambapo ilikuwa ni oda kwa wanafamilia ,moja kwa moja alijua huenda ndio kwanza wanafika hapo ndani kama wao .
Baada ya mhudumu yule kuweka oda ile kwa kila mmoja pamoja na vijiko na Umma alianza kupiga hatua na kuondoka lakini Roma palepale alinuia maneno flani hivi na Sahani zote nne ni kama zilipeperushwa na upepo chakula chote kumwagika.
Lakini ajabu ni kwamba licha ya tukio lile yule mwanaume shombe shombe mhudumu hakugeuka zaidi ya kuondoka na kushuka ngazi kuelekea chini huku wale wateja wakilalamika kwa kumuita na kufanya baadhi ya watu waliokuwa hapo ndani kushangazwa na kitendo hicho.
“Nakuja naenda kujisaidia”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia kwa wasiwasi na kumtingishia kichwa aondoke , ni kama Edna alielewa kauli ya Roma ndio maana akawahi kuruhusu.
Roma alitembea taratibu mpaka chini na kisha akafuata mlango na kutoka nje na baada ya kutoka kwenye eneo la bustani karibu na maegesho aliangalia kulia na kushoto lakini hakuka sawa masikio yake yenye uwezo wa kusikia hata nzi alieoko mita kadhaa yalihisi mvumo wa kitu.
Swiiiii…!!” ulisikika mlio na palepale Roma alinyanyua mkono wake na kudaka kisu mfano wa Dagger kilichorushwa kumdhuru na alikiangalia mkononi nakukijuta akitoa macho ya mshangao.
“Zero assassin!!!” Kisu kile kilikuwa na nembo ya Zero Assasin na kujiuliza Zero wanafanya nini Tanzania
Roma aliangalia yule mwanaume na kuona akitokomea upande wa pili wa ukuta na Roma palepale alipotea na ile anaibuka alikuwa mbele ya yule mwanaume na kumshangaza.
“Who are you?”Aliuliza yule mwanaume kwa namna ya kushangaa
“Nikuulize wewe ni nani unaewekea watu sumu kwenye chakula huku ukitumia nembo ya kundi la New Zero Assassin”Aliongea Roma kwa kingereza na kumfanya bwana yule kushangaa kwa wasiwasi kutokana na kugundulika.
“Wewe ni nani?”Aliuliza kwa mara nyingine na Roma alimrushia kisu chake kwa namna ya kumrudishia na yule bwana shombe shombe alikidaka huku akishangaa shangaa akimwangalia Roma usoni..
Shughulli ya Yan Buwen inakuja
Mwendelezo ni jumapili au j4
Mkuje Watsapp kumenoga unalipia aftatu tu tupo sehemu ya 500 namba ya watsapp ni 0687151346