Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 434.

Ilionekana hata Rose alikuwa akijua swala la Clellia Allisanto kwani hakuonyesha mshangao wowote na hata Roma alitambua Rose alikuwa akifahamu lakini alishangaa kwanini Dorisi hakuweka wazi swala hilo kwake .

Dorisi ilibidi amuelezee Roma kwa kila kitu kilichotokea , jinsi alivyorudi nyumbani kwake na kumkuta mwanamke ndani ya nyumba yake , mwanamke ambaye alijitambulisha kwa jina la Clellia Allisanto.

Mpaka Dorisi anamaliza kusimulia Roma ilimshangaza sana na kujiuliza huyu Clallia Allisanto alikuwa akimtakia nini mpaka kuanza kuzungumza na Dorisi maswala ya kuzaa nae , swala hili lilimshangaza na kumchanganya kwa wakati mmoja , lakini alishangaa zaidi mara baada ya Clellia Allisanto kuweza kutaja jina la Naira ambaye alikuwa rafiki wa utotoni wa Dorisi.

Roma palepale alijikuta kuna swala likimjjia akilini hapo hapo na ni kama alianza kupata majibu ya kile ambacho alikuwa akijiuliza tokea Edna alivyokutana na huyu Clelia Allisanto.

“Nafikiri stori yako inatengeneza ukweli ambao ulikuwa ukiutafuta”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi kumwangalia mpenzi wake kwa wasiwasi.

“Ukweli wa… Unazungumzia Black Card?”Aliuliza Dorisi akiwa kumbukumbu zake sasa zikikaa sawa na Roma alitingisha kichwa.

Ilibidi Rose aeleweshwe kidogo kuhusu Black Card ili aweze kuelewa kile kinachozungumziwa na alijikuta akishangaa mara baada ya kusikia Dorisi alikuwa na kadi ya benki ambayo ilikuwa na uwezo wa kutoa mabilioni ya hela benki , maelezo hayo ni kama hayakuwa ya kuaminika kabisa kwake lakini kilichomshangaza zaidi ni Roma kusema kadi hio imeunganishwa na akaunti ya benki ya The Doni.

Ilikuwa rahisi sana kugundua Dorisi alikuwa akimiliki Black Card kadi ambayo akaunti yake ya banki inamilikiwa na The Doni ambaye ni Athena lakini Clelia huyo huyo akamtembelea Dorisi na kutaja jina la Naira rafiki wa utotoni wa Dorisi hivyo kwa haraka haraka ni kwamba Clelia ndio Athena.

“Dorisi umesema alikuonyesha picha?”

“Ndio alinionyesha picha akiwa amepiga na Naira kwenye mapozi tofauti tofauti , lakini sehemu moja , walionekana kama wapo kwenye chumba cha hospitali au maabara , lakini sehemu ya kisasa zaidi”Aliongea Dorisi na kumfanya Roma kutabasamu.

“Kuna namna moja ya kumtambua Clalia , ile picha ya Naira si upo nayo?”Aliuliza Roma na Dorisi aliitikia kwa kichwa na Roma akampa ishara ya kumwambia akailete na Dorisi alitii haraka sana na kupandisha ngazi na kushuka na picha ile na Roma alimwangalia Naira aliekuwa kwenye picha hio.

Ukweli Roma hata mara ya kwanza alivyoona hio picha kuna kitu kilimwambia huyo mtoto hakuwa kabisa wa kawaida, hakuelewa kwanini alikuwa akimuona kama sio wa kawaida.

Roma alitoa simu yake na kisha kuipiga picha na kumrudishia Dorisi na baada ya kumaliza alitafuta tena namba ya Makedoni.

“Mfalme Pluto unanipigia tena”Ilisikika sauti ya Makedoni upande wa pili lakini waliongea kwa lugha ya kihebrew.

“Nataka ujaribu kutafuta jina la Naira Ryani , nakutumia picha yake kama jina halitokuwa kwenye mfumo wenu wa taarifa kwa teknolojia ambayo Israeli mnayo , haitashindikana kutoweza kupata taarifa zake”Aliongea Roma kwa kiebrania na kuwafanya Rose na Dorisi kuangaliana na kutabasamu.

“Mfalme Pluto nipe dakika moja , nitumie kabisa hio picha kwa Email nitakurudia mara baada ya kupata majibu”Aliongea na Roma alikata simu na kisha akatuma kwa njia ya email ile picha.

“Hubby hio ni lugha gani uliokuwa ukiongea?”Aliuliza Rose. Na kumfanya Roma kutabasamu.

“Ni Hebrew(Kiebrania)”Alijibu Dorisi na kumfanya Roma kutabasamu lakini Rose kushangaa.

“Dorisi unaonekana kukijua kiebrania?”

“Sijui kuzungumza lakini matamshi ya kiebrania nayajua”

“Hubby ilionekana uliishi sehemu nyingi za dunia , uliwezaje kujua lugha ya kiebrania?”

“Mpenzi wako nina historia ndefu sana”Aliongea Roma.

“Nakumbuka wakati unaanza kuja kwenye usaili tulishangazwa na uwezo wako wa kuzungumza lugha nyingi nadhani ndio kigezo kilichotufanya kukupatia kazi , licha ya kwamba maswali mengi ulijibu”Aliongea Dorisi na kumkumbusha Roma kipindi kile.

“Hahah.. Hubby nasikia mkeo alikuacha njiani ukiwa huna hata mia ndio ukaweza kukutana na Dorisi kwa mara ya kwanza na kumuomba hela ya nauli”Aliongea Rose huku akishindwa kuzuia kicheko.

“Naweza kusema kila mmoja wenu nimeweza kukutana nae kwa mtindo wa aina yake”Aliongea Roma huku akianza kukumbuka namna ambavyo aliweza kukutana na Edna mke wake.

Dorisi na Rose walionekana kucheka sana mara Roma alipowaeleza namna ambavyo alianza mahusiano na Nasra hawakuamini kama Nasra alianza kuvuliwa nguo na kubakia uchi bila kujielewa.

Wakati wakiendeleza stori Roma aliweza kupokea simu kutoka kwa Makedoni na kuweka sikioni .

“Mfalme Pluto nimejaribu kutafuta jina Naira Ryani na nimegundua taarifa ambayo sio ya kawaida”.

“Unamaanisha nini taarifa isiokuwa ya kawaida?”

“Kwanza namna ya kuupata ukweli ilikuwa ngumu kidogo , kwani inaonekana taarifa zinazohusiana na huyu Naira ni Top Confidential ndani ya serikali ya Marekani , nimejaribu kuomba ‘Clearence’ kutumia koneksheni zangu na kuweza ku access faili linalohusiana nae , lakini nilichopata kimeniacha mdomo wazi”

“Unanipa shauku Makedoni hebu nielezee ulichoweza kufahamu”

“Naira ni mtoto wa marehemu Ryan Kennedy , Agent mbobevu aliekuwa chini ya kitengo cha CIA chini ya idara ya SID ,mwaka 1990 taarifa zilionyesha Ryan Kennedy alikuwa akitafutwa na serikali ya Marekani na alikuja kupatikana mwaka 2005 , nikatafuta kwa haraka haraka kwanini Ryan alikuwa akitafutwa na serikali ya Marekani ndipo nilipoweza kupata faili la siri sana ambalo lilinishangaza”Aliongea

“Faili linahusiana na nini?”

“Project Pro Human”Aliongea Makedon na kumfanya Roma kukumbuka kitu lakini hakutaka kwanza kuingilia maongezi ya Makedon.

“Project Pro human kwa taarifa hapa nilizonazo inaonekana ilifanyikia ndani ya taifa la Bolivia kwenye msitu wa Amazoni kilomita kadhaa kutoka La paz , ni project ambayo ilianzishwa kwa siri sana na muuza madawa ya kulevya maarufu kutoka Mexico , mfalme Pluto ngoja nikutumie faili kwa njia salama uweze kujisomea mwenyewe”Aliongea Makedoni na Roma alikubali na ndani ya dakika chache tu faili liliweza kumfikia na alifungua na kuanza kusoma na alijikuta akikunja sura .

Ndio kama unakumbuka vizuri Project Pro human iliofanyika nchini Bolivia basi ndio taarifa ambayo alikuwa akisoma Roma , hakukuwa na utofauti mkubwa , Roma aliweza kukumbuka vitu viwili baada ya kusoma ripoti hio , kwanza kabisa ni stori ya Mellisa Luiz , mwanamama ambaye aliwahi kukutana nae ndani ya hoteli ya Kilimanjaro na kumuelezea kila kilichomtokea mpaka kujikuta kuwa na tatoo kwenye mwili wake ambayo ni kama uraia wa visiwa vya wafu, kitu kingine Roma alichoweza kukumbuka ni Carlos ambaye mpaka muda huo anaofikiria alikuwa ni raia wa visiwa vya wafu , alikumbuka kuna kupindi wakati akiwasiliana na Sauroni alimwambia kwamba walikuwa ndani ya jiji la Palermo Italy kwa ajili ya kumuokoa Carlos ambaye alikuwa akitafutwa na serikali ya Marekani.

Dorisi alimwangalia Roma kwa wasiwasi na kutaka kujua ni kipi ameweza kufahamu.

“Roma umeweza kufahamu nini?”Aliuliza Dorisi na ilibidi Roma ampatie simu yake aweze kusoma mwenyewe , hakuwa na haja ya kumficha.

Dorisi kadri alivyokuwa akisoma alijikuta mikono yake ikianza kutetema huku macho yakiongezeka ukubwa , ni kama alichokuwa akiangalia kwenye karatasi hio lilikuwa jambo la kuogopesha sana.

“Rafiki yako hakuwa wa kawaida Dorisi”Aliongea Roma lakini Dorisi alionekawa kufikiria sana, ilibidi na Rose aweze kusoma faili lakini hata hivyo hakuelewa sana kilichozungumziwa.

“Mama na baba itakuwa walikuwa wanafahamu hili ndio maaa ,,, ndio maana,..”Aliongea Dorisi huku akianza kutokwa na machozi.

“Dorisi unaongea nini, kwanini useme hivyo?”

“Licha ya kwamba nilikuwa mdogo lakini nilikuwa nikielewa maisha ya wazazi wa Naira yalikuwa ni ya kujificha sana . Naira hakuruhusiwa hata kuonekana onekana mtaani na mara nyingi tulicheza ndani ya geti na hata shule hakupelekwa…”

Ni kweli kabisa Naira hakusoma wakati alivyokuwa hapa nchini na wazazi wake hawakuwa na maelezo ya moja kwa moja kwanini Naira hakuwa akieonda shule licha ya kuwa na umri mkubwa.

Naira alimzidi Dorisi kwa takribani miaka minne , hivyo ni rahisi kusema Naira alikuwa dada kwa Dorisi tokea kipindi anazaliwa huko jijini Arusha na kwakuwa familia ya Dorisi na ya Ryani na mke wake Epholia walikuwa na ukaribu , hivyo ni kama waliishi kama ndugu na ndio maana wakati Dorisi ni kichanga alikuwa akilelewa na Naira mpaka Dorisi anakuja kuwa mkubwa wa miaka sita mlezi wake mkubwa alikuwa ni Naira , ni kama walikuwa kitu na mdogo wake na Naira alitokea kumpenda sana Dorisi kama mdogo wake.

Lakini jambo la kushangaza ni kwamba licha ya Dorisi kuanza shule upande wa Naira hakuwa amehudhuria kabisa masomo na jukumu la elimu yake lilibakia kwa wazazi wake , lakini licha ya hivyo Naira alikuwa ni moto wa kuotea mbali kwani alikuwa na kichwa chepesi mno kuliko binadamu wa kawaida , ilifikia kipindi hata hakupenda kabisa kufundishwa na wazazi wake na alichohitaji ni vitabu na sio kufundishwa..

Watu hawakuuliza sana maswali ya kwanini Naira hakuchangamana na watu wengine na yote hio ni kutokana alikuwa mtoto wa kizungu na watu hawakuwa wenye kuhoji sana kwani watoto wa kitanzania walikuwa waoga sana kila walipomuona Naira , lakini pia Naira hakuwapenda kutokana na kwamba akili yake ilikuwa ikipevukwa haraka sana , hivvyo ilikuwa ngumu sana kumwambia acheze na watoto ambao akili zao zilikuwa zikipevuka taratibu sana , hivyo maisha ya Naira yaliishia kuwa ya kipweke na mtu aliechangamana nae alikuwa ni Dorisi na hilo ni kutokana alimchukulia kama mdogo wake.

Kipindi Dorisi ndio anaaanza kujitambua ndipo Naira aliweza kuondoka na wazazi wake lakini ndio ambapo Ryani na Epholia walipoweza kumpoteza Naira wakati Naira akikaribia miaka kumi.

Naira alichukuliwa na Athena na kupelekwa makao makuu ya Zeros organisatioa na ni huko ambako Naira aliweza kupata elimu yake ambayo haikuwa rasmi ya chuo , lakini kutokana na uwezo wake usio wa kawaida aliweza kuwa msaada mkubwa sana hata kufumbua baadhi ya mafumbo ya mpango LADO.

Hivyo ni rahisi kusema Naira alishawahi kushiriki kwenye mpango LADO kama mwanasayansi ijapokuwa mpango huo wakati unaaza hakuwepo.

Huenda pia ikawa kweli kupotea kwa wazazi wa Dorisi ni kutokana na kujua historia iliokuwa nyuma ya Naira.

Roma alifikiria swala hilo kwa mantiki na kuona ni jambo ambalo linawezekana na kilichobakia ni kutafuta uthibitisho tu kama kweli wazazi wa Naira walikufa kwasababu walikuwa wakiujua ukweli kuhusu Naira.

“Dorisi kwasasa hupaswi kua na huzuni nakuahidi nitachimba na kuujua ukweli wote”

“Lakini Hubby kama hayo yote ni ya kweli inamaanisha huyu Naira sio wa kawaida na ni jambo la kuwezekana kwa Naira kuwa na urafiki na The Doni”

“Upo sahihi lakini siamini kama huo ndio ukweli wote , kuna sababu kubwa za The Doni kumfanya Naira rafiki yake , huenda anamtumia kwenye mipango yake”Aliongea.

“Unasema Naira atakuwa hatarini?”

“Kwasasa anaweza kuwa salama lakini baadae anaweza kuwa hatarini”Aliongea Roma na kisha Roma alipiga tena simu kwenda kwa Sauroni.

“Mfalme Pluto nadhani hata wewe umeshangaa”

“Naweza kusema hivyo , lakini dunia ni pana sana na yanayoendelea ni mengi hivyo nishazoea, Nataka unisaidie kuangalia ni eneo gani ambalo Naia yupo kwa sasa”Aliongea Roma.

“Hilo nafanyia kazi , lakini taarifa hapa inaonyesha wazazi wake walimpoteza na hawakuweza kufanikiwa kumpata tena , mfalme Pluto hii ni taarifa kubwa nadhani nitakupatia majibu nikipata chochote”Aliongea na Roma alikubali.

Muda ulikuwa umeenda hivyo Roma aliaga kuondoka huku akihidi akirudi China ataendelea kufatili habari zaidi za Naira pamoja na Clielia Allisanto

Ni asubuhi Roma mara baada tu ya kuamka alitafuta namba ya Profesa Clark ili kujua ana majibu ambayo amepata kwani juzi yake kupitia Sauroni aliweza kumpatia kazi ya kumtafuta Yan Buwen ni wapi alikuwa akifanyia mawasiliano.

“Umepata majibu?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Profesa ambaye alikuwa akiachama kuonekana alikuwa na usingizi.

“Ndio inaonyesha alifanya mawasiliano akiwa Beijing China sijui ni upande upi lakini mwelekeo ni upande wa Kaskazini magharibi sijaweza ku’pin point’ sehemu kwani ‘IP adress’ aliotumia sio ya kawaida lakini nina uhakika anahusika hakuna mtu wa kuweza kufanikisha jambo hili tofauti na Yan Buwen”Aliongea Clark.

“Inaonekana kweli aliweza kuondoka hapa nchini muda mrefu”Aliongea Roma.

“Roma unafikiria kufanya iin juu ya hili, maana kila nikifikiria Yan Buwen kuweza kufanikisha kutengeneza kopi yake inanifanya kuamini ni hatari sana”Aliogea Profesa.

“Ndio maana nataka niende China , naamini kuna maabara huo upande wa Kaskazini magharibi”Aliongea Roma.
[emoji91][emoji91][emoji91]
 
SEHEMU YA 436

Roma hakutaka kumzuia Yan Buwen kabisa kutokuua familia yake , kwanza ni mambo ambayo hayakuwa yakimhusu na pili familia hio ndio iliomwingiza katika mambo ya kutengeneza siraha za maangamizi ili tu kuweza kushindana na Hongmeng.

Lakini hata hivyo swala la kuua familia yake mwenyewe lilimfanya Roma kuuona Yan Buwenn kiumbe cha hatari sana ambacho kwa namna yoyote ile alitakiwa kumwangamiza hapo hapo kwani kitendo alichokifanya hakuweza kufikiria hata siku moja mtu mwenye akili timamu anaweza kufanya..

“Nakubali umekuwa chizi kuliko nilivyofikiria , lakini kabla hatujaanza mapambano yetu niambie kwanini ukaamua kuwa adui yangu , maana hakuna siku yoyote ambayo nilishawahi kukuchokoza”Aliuongea Roma

“Haijalishi chochote kwasasa”Alijibu .

“Kweli! Unaweza usiamini lakini swali langu ndio sababu ambayo imenifanya muda wote nisikuchukulie hatua licha ya kunichokoza mara kibao, nadhani unakitaka kifo sasa”

“Hahaha,.. unafikiri unweza kunishinda mimi?”Aliuliza Yan Biuwen lakini Roma hakumjibu , ukweli alichokitaka ni kujua kwanini ghafla tu Yan Buwen akaanza kumuwinda yeye kwani hakuwa na ugomvi nae.

“Nadhani hata hivyo napaswa kukujibu , mwanzoni sikuwa na haja na wewe kabisa , lakini nilikuja kugundua unamiliki kitu cha thamanni ambacho hakikuwa cha kwako , hata hatua yangu ya kufika Tanzania ilikuwa ni kukipata , unaweza ukashangaa labda kwanini nikakaa Tazania kwa ajili ya tafiti zangu lakini ukweli kabla ya kuja Tanzania nilikuwa na makazi mengine bora zaidi kuliko maabara ile ya kipuuzi kule Tanzania , lakini hata hivyo mimi Yan Buen nimekuwa wa kupata kila ninachokitaka katika dunia hii..”Aliongea

“Ulikuwa ukitaka nini kutoka kwangu?, mpaka sasa kama unahitaji Jiwe la kimungu halipo kwenye umiliki wangu, nini unachokitaka kutoka kwangu”

“Huna haja ya kufahamu , lakini kaa ukikumbuka hivi , kifo chako pekee ndicho kitathibitisha kwamba mimi ndio mmiliki pekee wa dunia , I am strongest man in the world”

“Sijawahi kujitangaza mimi kama ni mmoja wapo ya watu wenye nguvu ndani ya dunia hii”Alijibu Roma.

“Lakini kuna watu wanaamini una nguvu kuzidi mtu yoyote ndani ya dunia hii na ndio maana nitaichukua nafasi yako kwa kukuua”Aliongea Yan Buwen.

“Nani anaamini hivyo?”

“Unaongea sana Hades, haijalishi tena kukuambia kwani mpaka sasa wewe ni mfu”Aliongea na palepale nguvu isioelezeka ilianza kumzingira kiasi cha kutengeneza mwanga flani wa rangi ya Cyan lakini ambao haujakolea sana lakini angavu mno kiasi kwamba ulifanya mazingira kuwa na mwanga , Cyan ni mwanga ambao unazalishwa kati ya rangi ya bluu na kijani katika mwimbi ya wevu 490nm kwenda 520nm , inasemekana kwenye anga la sayari ya Uranus ndio imekithiri.

Sasa mwanga ule ulikuwa ukimzunguka huku ukitengeneza kama wingu flani hivi la rangi hio kuanzia chini kwenye miguu mpaka kichwani huku ukiambatana na upepo mkali, kadri nguvu ilivyokuwa ikizunguka ndio anga lote lilivyoanza kucheza cheza kwa kupinda.

Roma alishangazwa kwani ilikuwa ni nguvu sawa kama ya Clone alilopambana nalo siku chache zilizopita lakini awamu hii nguvu hii ilikuwa kubwa mno.

“I am sue you have come into contact with my creations , So please enjoy it while it last”

“Naamini ushakutana na kiumbe changu , hivyo furahia uwezo wangu kadiri unavyodumu”Aliongea kwa kujigamba huku akicheka kama chizi na kusogelea Roma kwa spidi ya mwanga akilenga eneo la moyo wa Roma.

Roma alishajua alichokifanya Yan Buwen ni kutengeneza mbinu ya kucheza na kanuni za anga kwa kutengeneza uzio nyuzi nyuzi sambamba(disorderly Paraller space fabric) ili kwamba hata kama Roma angekuwa na uwezo wa kutumia kanuni za anga kushambulia basi ashindwe.

Hata hivyo aliamini huenda Yan Buwen alimtegemea angeweza kutumia kanuni za anga kushambulia , lakini yeye alitumia mbinu za kijini.

Roma palepale aliita nguvu ya kijini ya kimaandiko na ilitengeneza ngao flani kama kioo na ni muda huo huo Yan Buwen aliweza kumfikia hivyo mgongano wa ngao na nguvu ya Yan Buwen ulitengeneza mtetembo kama wa bomu huku cheche kama za radi zikisambaa eneo lote kutoka kwenye ile ngao ya Roma aliotengeneza.

Mtikisiko ule ulikuwa mkubwa kiasi kwamba ulisambabisha hata jengo la nyumba hio na ukuta wake kuporomoka chini , lilikuwa ni jambo ambalo lilimshangaza Roma kwani Yan Buwen alikuwa na uwezo mkubwa sana kiasi kwamba ilimshangaza na kujiuliza imekuwaje Yan Buwen kuwa na uwezo mkubwa kiasi hicho kwani mara ya mwisho alionekana kuwa wa kawaida tu.

Yan Buwen mara baada ya kuona pigo lake la kwanza halijafanikiwa alipiga tena kwa mara mbili mfululizo , lakini ngao ya Roma iliuonekana kuwa ngumu , lakini hata hivyo alivyopiga mara ya tatu ilitengeneza uwazi hivyo hakutaka kuchelewasha kwani palepale alilenga ngumi iliojaa mwanga kama wa jiwe la kimungu na kuipitisha kwenye uwazi.

!POW!

Baada ya ngumi ile kumpata vyema Roma kwenye kifua alirushwa kwenda juu kama vile ni mpira huku akizunguka zunguka kwenye hewa na baada ya kufika mwisho alirudi chini kwa spidi lakini palepale alitumia uwezo wake wa kijini kupunguza spidi ya namna anavyoshuka , lakini kabla hajakanyaga Ardhi , Yan Buwen alileta teke lenye nguvu isiokuwa ya kawaida na kwakua alitumia spidi kubwa Roma alizubaa na kushindwa kukwepa.

“Arrgh…”Roma alitoa ukulele mara baada ya kupokea bonge la teke na kwenda kutua kwenye mlima wa mawe yaliorundikwa sehemu moja mara baada ya nyumba ile kubomoka.

Yan Buwen mara baada ya kuona amefanikisha kumpiga mapigo mawiali Roma na kumpeleka chini alipaa juu angani akimwangalia kwa chini.

“Hahaha… naona kupokea kipigo ndio unachoweza pekee , vipi umekuwa mdhaifu kwa kapigo kadogo kutoka kwangu”Aliongea kwa kimandarini akimwangalia Roma aliekuwa akiugulia maumivu chini ya rundo la mawe.

Lakini Roma alivyotaka kusimama vizuri Yan Buwen alimsogelea kutoka juu kama mshale , lakini kabla hajamfikia liliamika jiwe kubwa pembeni na kumlenga Roma.

PUUH!,

Jiwe lilimpiga kisawa sawa Roma na kumfanya kutema damu huku akipiga magoti kwa maumivu.

Alijikuta akipeleka mkono mdomoni na kujifuta huku macho yake yakiwa mekundu kama yanaanza kutoa damu.

Roma alitaitiwa mapema sana tofauti na alivyokuwa akipambana na Poseidon,nguvu aliokuwa nayo Yan Buwen haikuwa ya kitoto.

“Haha.. Etia anaitwa Pluto upuuzi mtupu , wewe ni kichekesho , kwangu nakuona kama kunguni tu ambaye nakuua na vidole , hustahili hata kuwa mshindani wangu pumbavu”Aliongea Yan Buwen na Roma alijitahidi kusimama vizuri baada ya maumivu kupungua.

“Here is my advice for you , I’m reissuing my clone offer , Be my slave and I might let you live”

“Huu ndio ushauri wangu , ninakupatia tena ofa kama nilivyotoa maagizo mwanzo kwa clone langu , kuwa mtumwa wangu na ninaweza kukuacha hai”Aliongea Yan Buwen

“Halafu tena kabla sijasahau , unao warembo wengi , nafikiri pia wanaweza kuwa msaada kwangu nina kwani nina Clones nyingi na zina nyege hatari , itakuwa jambo zuri kama warembo wako watatoa huduma kwao wote , nataka wewe mwenyewe uangalie namna Clones zangu zinavyofanya mapenzi na mademu zako hahahah..”

Kauli yake ni kama ilimfanya Roma aliekuwa amesimama kivulini kurudiwa na nguvu zake zote , kwani hasira zilimpanda kiasi kwmaba zilisambaza nguvu isiokuwa ya kawaida ndani ya eneo lote.

“Unaonekana bado una vinguvu vya kuweza kupambana , ngoja tuone ulichonacho kwa sasa”Aliongea Yan Buwen mara baada ya kuhisi nguvu isiokuwa ya kawaida.

Sasa ukumbuke Roma wakati alivyokuwa akipigana macho yake yalikuwa kawaida kabisa licha ya kwamba yalikuw mekundu , lakini awamu hii Yan Buwen alivyotaja warembo wake na kusikia kuna kopi nyingi zinazofanana nae ,viini vya macho vilibadilika rangi kutoka weusi na kuwa nyekundu na miale kama ya laser.

Yan Buwen mara baada ya kushuhudia Roma kabadilika macho alijikuta ile hali ya kuamini angeweza kushinda pambano ilimpotea mara moja

Roma sasa alikuwa kama nusu shetani kwanza ,alitoa ulimi na kulamba damu zilizokuwa zikimtoka kwenye midomo yake.

“Niliamua kutokuwa siriasi na wewe , kwasababu nilikuwa nikihofia kulikorofisha anga lakini sasa hivi sina haja ya kucheza mchezo wa kitoto na wewe , nitakuonyesha nini maana ya kupigwa na radi harafu na kupona”

“Haha unaongea sana , kuna mtu unajaribu kumsubiria…”Aliongea lakini kabla ya kumaliza sentensi yake palepale aliposimama ni kama alikuwa akivutwa na nguvu isiokuwa ya kawaida kiasi kwamba alikuwa akikosa balansi ya kuendelea kudumu kwenye anga lakini wakati huo huo akihisi mkandamizo ambao sio wa kawaida kabisa , huku Roma akiwa amesimama akimwangalia kwa macho ya hasira.

“Hii ni…”Alijikuta akitoa macho mara baada ya kugundua nguvu ni kama zinapotea mwili wake na kumwangalia Roma kwa mshangao.

Uwezo wa Roma ulikuwa umeongezeka zaidi ya mara ishirini kuliko alivyokuwa akipambana mwanzo , alikuwa ni kama mtu mwingine kabisa.

Wingu lilianza kuzunguka juu kama vile mvua inataka kunyesha na nyota zilizokuwa zikionekana zilibwa na wingu.

BOOM, BOOM, BOOM

Ngurumo kali ilipiga ikiambatana na radi lakini ambayo haikufika chini huku mawingu yakizidi kusuguana na kusababisha umeme.

Roma aliangalia juu angani mara baada ya ngutumo na kuona ahueni na kisha alipiga hatua moja mbele , lakini kilichomkuta Yan Buwen ni kwamba aliporomoka chini huku akianza kukosa hewa, alikuwa ni kama yupo kwenye chumba chenye moshi mwingi.

“Kwanini umekuwa kimya ghafla , nia yako ya kuniua na kuwachukua wanawake wangu ipo wapi , hii ndio nafasi yako ya mwisho ichukue”Aliongea kwa sauti ndogo lakini ni kama ilikuwa ikitoka juu angani kwani ilikuwa kama mwangwi.

Yan Buwen alijitahidi kushindana na nguvu iliokuwa ikizunzuia kutofanya chochote lakini alishindwa.

Upande wa Roma mwenyewe alihisi mabadiliko yasiokuwa ya kawaida ambayo hakuweza kuyatarajia , siku zote alikuwa akiita nguvu za kijini akitaka kupambana lakini sasa hivi sio kama alikuwa akiziita lakini yeye ni kama ndio nguvu zenyewe za kijini na zilikuwa zikiamua kipi cha kufanya.

“Uli ., ulificha uwezo wako kumbe?”Aliongea Yan Buwen kwa shida sana.

“Unatakiwa kujichukulia wa juu kwani siku zote situmiagi uwezo wangu kwa watu wa kawaida ,, ninaweza kukuua bila ya wewe mwenyewe kujua kama umekufa , nina miaka elfu moja sijawahi kuamshwa na kuwa na nguvu kiasi hichi ndani ya uso huu wa dunia”Iliskika sauti ambayo haika sio ya Roma bali ni kama ya kijini inayomtawala ndio inayoongea.

“Acha kujihisi una uwezo mkubwa sijashindwa bado”Aliongea Yan Buwen na palepale alijikakamua kwa uwezo wake wote na kuchomoka kwenye nguvu iliokuwa ikimzuia chini kutopaa na alifika juu hewani na kumfuata Roma kwa namna ya kurusha shambulizi , lakini Roma alitoa tabasamu la kifedhuli nakukunja kiganja na kisha akakifumbua na kurusha kibao juu angani.

BANG!

Yan Buwen alirudishwa kutoka juu kwa spidi isio kuwa ya kawaida na alishindwa kujiongoza na kwenda kuyavamia mawe ya ukuta kiasi kwamba sehemu aliodondoka ilitoa vumbi zito.

“Inaonekana unaweza kufa kwa pigo moja tu”Aliongea Roma lakini nguvu ilianza kujikusanya tena kwenye mwili wa Yan Buwen kwa kupepesa macho tu.

“Inaonekana kwangu nguvu zako ni za aina yake lakini sio kama za kwangu , ninaweza kuzifyonza zote na kuzitoa kwenye mwili wako nakushauri utii amri kama sijakuua kwa zaidi ya mara kumi”Aliongea Roma vile vile huku sauti ikiwa sio kama ya kwake kwani ilikuwa nzito na ya kuogofya mno.

Yan Buwen alijikusanya kwenye vumbi kwani nguvu zake zilikuwa zimemtoka nyingi na huenda angekuwa mfu kwa wakati huo

“Siwezi kukubali kushindwa…”Aliongea kwa hasira na kuamka kama mwanga wa radi.

BOOM!

Ni vipande vipande vya nyama vilivyosambaa angani , ilionekana Roma alimtegemea ndio maana akamtanguliza na shambulio kama la bomu ambalo lilimsabaratisha

Lakini licha ya kusambararika ilionekana nguvu isiokuwa ya kawaida ikikisanya vile vipande vipande vya nyama pamoja na damu yake kwenda sehemu moja pasipo ya kudondoka chini, lakini Roma hakuteka kuruhusu tukio hilo , alirusha tena pigo lingine na kusambaratisha tena, lakini ajabu tena vipande vilikusanyikka kwa spidi kubwa sana ni kitendo cha kupepesa macho tu Yan Buwen alirudi tena kwenye uhai wake na kumfanya Roma kutoa macho.

Lakini kabla hajaamua cha kufanya ni nini , palepale mwili wa Yan Buwen ulibadilika na kufunikwa na suti flani hivi ya aina yake na kumziba mpaka kichwa , ilionekana ilikuwa ni kama ngao

Roma alishangazwa na vazi la Yan Buwen kwani ni kama vile alikuwa akiangalia muvi ya Avenger end game.

“You can’t kill me , I have this..”Aliongea Yan Buwen akiwa amefunikwa kichwa chake kama vile ni Spiderman huku mkononi mwake kukionekana kitu kama kitenesi kikitoa mwanga mkali sana wa mng’ao

“The Godstone,! This whole time it was you?”Aliuliza Roma kwa mshangao usio na kifani huku akimaanisha kwamba kilichomtokea siku ile mpaka kupoteza jiwe hilo la kimungu ,lakini vile vile kule Ufaransa kupoteza teknolojia ya Thanatos , lakini pia kupotea kwa Moses Vampire na Holygrail , mambo yote hayo yalikuwa ni yeye , Roma alijiambia haiwezekani ndio maana alitoa mshangao usio na kifani.

Jambo moja lingine ambalo lilimshangaza Roma ni kwamba lile jiwe lilikuwa limebadilika ukubwa wake na sasa lilikuwa likitoa mwanga mkali sana unaoumiza macho mweupe lakini mfano wa jua , ni haki kusema kwamba Yan Buwen huenda kajua siri ya jiwe hilo.

Yan Buwen hakueleweka alifanya nini na lile jiwe lakini alilirusha juu angani na likanasa na palepale lilitengeneza shimo nyeusi kubwa ambalo anga lake ni kama linachemka kwa spidi kubwa ni kama unaangalia BlackHole , mwili wake ulivutwa kwa kasi sana na lile shimo na akapotea palepale kwa namna ya kuyeyuka.

Roma alijaribu kuzuia shimo liile lakini nguvu yake ilikuwa kubwa mno kiasi kwamba ilimrusha mbali kwa kumkataa.

Roma alijikuta akianza kuhema kwa tabu , mpaka hapo aliamini huenda Yan Buwen alitumia jiwe hilo kuweza kuwa na nguvu kama hizo , ilikuwa mantiki kufikiria hivyo , lakini swali aliwezaje kufahamu kanuni za anga kirahisi hivyo kwanni hakuwa na uungu wowote ndani yake

Pumbavu”Aloijikuta akitoa tusu huku aking’ata meno yake kwa hasira kwa kitendo cha Yan Buwen kumkimbia , alijua aliweza kumtoroka kwa kutumia jiwe la kimungu, ijapokuwa miaka mingi lilikuwa chini ya umiliki wake lakini hakuwahi kufikiria jiwe hilo linauwezo mkubwa mpaka wa kutengeneza shimo jeusi angani na kuwa kama njia ya kutoroka.

“Hades usiwaze hatoweza kukushambulia kwa muda hahah..”Ilikuwa ni sauti ambayo inasikika kwenye kichwa chake na kumfanya kutoa macho , ilikuwa ni hali kama ya mtu mwenye ugonjwa wa kuchanganyikiwa.

“Wewe ni nani?”Aliuliza Roma huku sauti yake ikisikika vyema sasa lakini macho yake hayajatoka kwenye rangi ya uwekundu.

“Hehe .. umenipa jina mwenyewe unaweza kuendelea kuniita kwa jina la nguvu ya kimaandiko naishi ndani ya mwili wako , mimi na wewe ni ndugu wa damu chanda na pete una mwili mzuri sana kwa ajili ya mimi kuishi”Sauti ilisikika kwenye akili yake na kumfanya Roma kushika kichwa kwa namna ya kuchanganyikiwa.

“Achia akili yangu”

“Sawa kwasasa nitakuachia akili yako , lakini kadri unavyozidi kuwa na nguvu ya kijini itafikia siku lazima nitaiongoza akili yako kabisa,mwili wako unanifaa sana ngoja niendelee kulala nikisubiria siku yangu ya kurudi uraiani”Iliongea Sauti na kumfanya Roma ang’ate meno yake kwa hasira na palepale macho yake yalirudi kwenye hali yake ya kawaida na ile sauti ikapotea kwenye akili yake.

Alijikuta jasho likimtoka mno hakuelewa ni nini kinachomtokea hata hivyo ni kweli kabisa wakati anajaribu kupambana na Yan Buwen kwa uwezo wake wote ni kama mwili wake hakua ukiuongoza yeye kwenye mapambano, ni kama akili yake ilikuwa ikifanya kazi nusu na nusu nyingine ilitawaliwa.

Lakini hata hivyo Roma alitabasamu kifedhuli kutokana na kwamba ndani ya mwili wa Yan Buwen wakati alivyokuwa amemshikilia kichawi alimwingizia nguvu ya kijini kwenye mwili wake, kitendo ambacho hata yeye akili yake hakuelewa kwanini alifanya hivyo lakini kwa sauti iliomwongelesha anaelewa kwamba ni mtego.

Aliamini lazima mwili wake Yan Buwen utakuwa kwenye maumiu makali , kwani inaonekana nguvu ya jiwe la kimungu na za kijini haipatani ndio maana wakati anasogelea shimo jeusi tofauti na kumezwa yeye alitupwa mbali kwa ishara kwamba shimo lile linamkataa yeye.

Lakini Roma sauti aliokuwa akiisikia kwenye kichwa chake ilimfanya kuwa na wasiwasi lakini hata hivyo aliamini huenda ni akili yake mwenyewe , hivyo aliamua kupuuzia lakini bado roho yake haikuwa na amani.

“Au kuna athari za kutumia kanuni ya kimaandiko?”Roma alijikuta akianza kuwaza mwenyewe huku akiangalia uharibifu uliofanyika.

“Roma nini kimetokea , wewe ndio umeharibu hizi nyumba zote?”Ilisikika sauti kutoka hewani na kumfanya Roma kuangaliai juu alikuwa ni Omari alieonekana ndio anafika.

“Umewezaje kusafiri umbali mrefu mpaka hapa bila kukasiriha anga?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Kuna namna ya kusafiri pasipo kukasirisha aga , nnimefunzwa huko Hongmeng, pumbavu kabisa nimechelewa daah sijaona pambano”Aliongea huku akiongekana kulalamika.

Njia ambayo anazungumzia Omari ya kusafiri pasipo kukasirisha anga ni kusafiri kwa vituo , yaani unaweza kupaa kwa kilomota kadhaa na kisha ukatulia kwa dakika kumi na tano then unaendelea tena kwa kilomota kadhaa , mpaka ufikie eneo husika , uzuri ni kwamba tu nguvu za kichawi zenyewe zinakupeleka sehemu unayonuia kufika haina haja ya kuwa na ramani kichwani lakini athari kubwa ni kwamba kila kituo lazima kiwe ni maji au bahari, yaani kwa mfano ukatoka Tanzania na madhumuni ya kwenda China basi unatakiwa usafiri na uelekeo wa bahari tu ili kila ukifikisha kilomita kadhaa , unatumbukia majini na kukaa huko kwa dakika kumi na tano na unaibuka tena unasafiri tena kwa kilomita kadhaa halafu unaingia tena majini unajificha ndani ya maji kwa dakika kumi na tano unaibuka tena , ilikuwa ni mbinu ngumu kwani inahitaji ujasiri lakini inakuwezesha kusafiri kwa muda mfupi.

Hivyo kimahesabu ni kwamba Omari alianza safari kabla ya Roma kwani kuna vituo vingi sana ndani ya maji ambavyo lazima Omari alipumzika kabla ya kuendelea na safari.

Hivyo unaweza ukaona jini linaibukia baharini usiku ukashangaa lakini ukweli ni kwamba bahari au ziwa ni njia salama ya majini kusafiri pasipo kukumbana na malipizi ya anga.

“Taarifa za Yan Buwen kuua familia yake zinasambaa sana kuna rafiki yangu hapa China nilianza kufikia kwake na kupata habari hizo , inasemekeana walinzi ndio walitoa habari, Vipi umefanikiwa kumdhibiti”Aliuliza Omari huku akikagua namna eneo lilivyoharibika.

“Amenitoroka bwana”Alijibu Roma kinyonge.

“Hapana , amewezaje kutoroka mbele yako nadhani ni afadhari nimekuja baada ya mapambao kuisha huenda ningekufa hapa hapa, maana huenda ningepatwa na hasira na kushindwa kujizuia mpaka kumpiga ngumi”

“Unashindwa vipi kujizuia au kwasababu mwanamke wako kamtia mimba?”Aliuliza Roma kwa kejeli.Lakini Omari alionekana kutopendezwa na swali lake

“Najua huenda huna hela yoyote na pia mavazi yako yamechafuka , twende kuna sehemu salama ya sisi kwenda kula msoni na kupata hifadhi ya kulala”Aliongea Omari.

“Nani kakuambia sina pakuishi”Aliongea Roma na palepale licheza na anga , kilikuwa ni kitendo kama alichofanya Clelia allisanto wakati akitoa kiboksi cha uwa angani.

“Hades kuna uwezekano na mimi kujifunza namna ya kutunza vitu kwenye anga?”

“Uwezekano huo huna , nina nguvu ya kiuungu ndani yangu ndio maana naweza pia kujifunza kanuni za anga , wewe ni binadamu wa kawaida ambaye umejifunza mbinu za kijini”Aliongea Roma huku akiangalia kipi cha kuchukua kwenye shimo ambalo linatumika kama sehemu ya kuhifadhia vitu kwenye anga , aliachana na pete na kisha akachukua kadi ya benki na passport yake ya kusafiria.

“Hivi ni vibali ambavyo vinaweza kunipatia makazi kwenye hoteli yoyote hapa nchini China pambana kivyako sijakuambia unifuate huku China”Aliongea na kabla hata Omari hajaongea neno , palepale Roma alipotea na kumuacha Omari akiwa kwenye mshangao.

“Pumbavu zako Hades , nimekufuata mpaka China halafu umeniacha nitakupata tu”Aliongea Omari huku akiangalia baiti moja iliofukukiwa na mchanga uliotokana na kuharibika kwa nyumba na alisikitika kidogo na kisha akapotea ndani ya eneo hilo mara baaada ya kusikia magari ya polisi yakisogelea hilo eneo.

Unafikiri sauti iliomuongelesha Roma inatokana na nguvu za kijini anazojifunza , kama kweli ataendelea kupanda levo je nguvu ya kimaandiko itaweza kutawala akili yake , nini kitaendelea tukutane kesho.
Hatariiii
 
Vipo vigongo vingi.uku ukipata arosto.unaamia kwingine .wala akuna haja ya kuuliza kila ck lini mwendelezo.
 
Kesho ndio leo naona unatuletea miyeyusho tu bwana singanojr..
Kwamba anayeyusha sio? Wacha ajibu kwa vitendo kabla siku haijageuka.

SinganoJr. aka Roma Romani, uje mzee weekend haisogei kwa wapenda hadithi yako.
 

SEHEMU YA 444.​

Edna na Roma mara baada ya kuingia eneo la sebuleni waliweza kukutana na sura nne ngeni ,kulikuwa na mwanaume mwenye kitambi na mwili mkubwa alievalia suti , mwanaume mwingine alikuwa ni mzungu. , wengine wawili walikuwa ni mabodigadi.​

Kuhusu mzungu alikuwa mrefu wa kama inchi sita na nusu , ana nywele nyeupe aina ya blonde akiwa amevalia shati rangi ya pink na suruali ya kitambaa, mwonekano wake ilikuwa ngumu sana kuweza kukadiria umri wake , lakini alikuwa ni kijana kabisa huenda hata Roma akawa mkubwa.​

Roma na Edna mara baada ya kufika eneo hilo la sebuleni yule bwana mweusi mwenye kitambi alisimama, Roma hakumfahamu lakini upande wa Edna alimfahamu huyo mwanaume kwani alikuwa ni mwanasiasa maarufu tu.​

“CEO Edna umerudi?, naomba unisemehe kwa kufanyia ziara ya kushitukiza asubuhi asubuhi”​

“Usijali muheshimiwa karibu sana”Aliongea Edna.​

“Mr Roma nadhani hatujawahi kukutana ana kwa ana , kwa jina naitwa Abasi Nguya ni waziri wa Uwekezaji , biashara na Viwanda”Alijitambulisha.​

“Karibu sana bwana Abasi Nguya”Aliongea Roma lakini Edna macho yake yote yalikuwa kwa mzungu ambaye alikuwa akitoa tabasamu , ilionekana ni kama wameshakutana kabla ya ujiio huo.​

“Mr Maksim? Why are you here?”Aliuliza Edna kwa kingereza akimuuliza bwana mzungu kwanini yupo hapo.​

Roma mara baada ya kuona mke wake anamfahamu huyo mzungu alijiuliza ni wapi wamekutana.​

“Edna unamfahamiana nae?” Aliuliza Roma na kabla hajajibu yule mwanaume alimsogelea Roma.​

“Hello I’m Maksim frome the Klyuchevsky familly in Russia , its honor to visit your home, I met CEO Edna at the international bussiness and economics meeting yerstaday”​

“Habari naitwa Maksim kutoka familia ya Klyuchevsky kutoka Urusi , ni heshima kwangu kutembelea hapa nyumbani kwako , nilikutana na CEO Edna kwenye kikao cha uchumi na biashara za kimataifa siku ya jana”Aliongea yule bwana kabla hajampa nafasi Edna kujibu.​

Roma hakuweza kujua kama siku ya jana kulikuwa na kikao cha aina hio hata hivyo asingejua kwani alikuwa kwenye mgogoro na mke wake.​

“Mr Maksim amekuja mpaka hapa kwa nia ya kuongea na nyie wote juu ya ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi , nimepewa kazi hii na mheshimiwa raisi kuwa mtu kati kwenye mazungumzo”Aliongea bwana Abasi Nguya.​

“Mazungumzo ya kidiplomasia ndani ya nyumba yangu , mbona kama ni swala ambalo halijakaa sawa”Aliongea Roma.​

“Hapana Mr Roma , inawezekana sehemu hii sio sahihi , lakini serikali haiwezi kufanya maamuzi ya moja kwa moja bila makubaliano kati yako na mke wako kuhusu maswala ya kibiashara , hivyo kauli yako ni muhimu pia kwenye mzungumzo yetu” Baada ya kuongea hivyo Roma aliamua kwenda kukaa na wote wakakaa chini kwa ajili ya mazungumzo.​

Licha ya bwana Maksim kusema kwamba alikuwa ashasikia habari zake , lakini aliihisi bwana huyo alikuwa akimfahamu kwa jina la zaidi ya Roma ,kama si hivyo asingefika nyumbani na kuhusishwa kwenye maswala ambayo mke wake anaweza kufanya maamuzi kama siku zote.​

“Familia anayotokea bwana Maksim ni moja ya familia kubwa ndani ya taifa la Urusi na hata Raisi wa sasa wa Urusi yupo madarakani kutokana na sapoti kubwa kutoka kwenye familia ya bwana Maksim , ndio wameshikilia uchumi wa Nishati ya nyuklia , Gesi asilia na Petroli Urusi yote, Hata hivyo wanajiendesha kwa siri sana ndio maana hawana umaarufu mkubwa”Aliongea Mheshimiwa Nguya na kumfanya Edna kushangazwa na taarifa hio , siku ya jana mara baada ya kukutana nae alimchukulia poa kumbe alikuwa mtu mzito sana.​

Urusi ni nchi ambayo imejaaliwa rasilimali nyingi za kinishati , msingi wa biashara ya Vexto ni uingizaji wa asilimia hamsini za mafuta kutoka nje ya nchi hivyo mazungumzo hayo ya kibiashaa kama yanegeenda sawa ingekuwa ni faida kubwa sana kwa kampuni yake na huenda hata gharama ya mafuta ya Petroli zilizokuwa juu kwa sababbu ya vita kati ya Ukraine na Urusi ingepungua, lakini sio hivyo tu kama kutakuwa na makubaliano ya kibiashara kampuni nyingi ndani ya Afrika mashariki kwa ujumla zingepatwa na ukichaa, Edna alijikuta mwili wake ukimsimsika.​

“Mr Maksin jana hukuzungumzia swala lolote linalohusiana na ushirikiano wa kibiashatra , kwanini iwe leo?”Aliuliza Edna kwa kingereza huku akionyesha shauku kwenye macho yake , hata hivyo Edna alizaliwa kuwa mfanyabiashara hivyo eneo kama hilo lilikuwa la kwake kabisa kutawala.​

“Miss Edna my proposal ties with my background I do not wish to reveal it to the general public right now”​

“Edna Pendekezo langu linafungamana na ubini ambao sitamani kuweka wazi sasa hivi”Aliongea na kumfanya Edna kushangaa , lakini Maksim alibadilisha mkao na kisha akamwangalia Roma na Edna kwa pamoja.​

“Pendekezo langu nataka kampuni ya Vexto kuvunja mkataba na Princess Clark”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na kauli hio lakini aliendelea kuongea.​

“Nimekuja hapa nchini kwa ajili ya Clark , Clark ni mchumba wangu na hata mipango ya ndoa yetu ni makubaliano kati ya familia yangu na Rothchild, lakini kutokana na kutokuelewana ndio akaingia mkataba na Kampuni ya Vexto pamoja na serikali ya Tanzania ili tu kuweza kuepuka kufunga ndoa , jambo ambalo ni matusi kwa familia yangu na familia ya kifalme kutoka Wales , hivyo ujio wangu hapa Tanzania ni kwa ajili ya kumrudisha Urusi ili taratibu za ndoa ziendelee”​

Roma maneno hayo hakuyapenda kabisa , ijapokuwa Catherine alishamwambia kwamba Clark alipaswa kuolewa lakini hakujisumbua kuuliza ni familia gani anaozeshwa, lakini alishangaa kujua ni moja ya familia ya Ma oligarch kutoka Urusi.​

Mpaka hapo Roma kuna kitu kilimjia akilini , huenda Clark anatolewa kafara kutokana na yale yanayoendelea ndani ya bara la ulaya , Uingeeza ni kati ya nchi ambazo zinategemea sana rasilimali nishati kutoka Urusi , ukijumlisha na Vita vinavyoendelea huenda ndio ilipelekea Rothchild kutaka kufanya makubaliano ya kibiashara yanayofunganishwa na ndoa, hata hivyo alikuwa akijua familia ya Rothchilds siku zote ilichokuwa ikijali ni pesa sio utu.​

Unapaswa pia kujua kwamba Klyuchevisky ndio wapo nyuma ya chama tawala ndani ya Urusi.​

Edna sasa ndio anajua ujio wa Profesa Clark sio wa kibiashara bali alikuwa akikimbia ndoa, akili yake ilianza kuzunguka kwani maongezi hayo hayakuwa ya kibiashara tu bali yalionekana kama tishio kwa biashara zake , ukizingatia pia kampuni yake ilikuwa ikijihusisha na biashara ya mafuta kutoka Urusi , aliona hata kama hatomwachia Clark kuondoka kwa kuvunja mkataba lakini hakuwa na uwezo wa kuziia swala hilo kwani asingeweza kushindana na familia kubwa kama hio.​

Mkataba wake na Clark ulikuwa ni wa faida kubwa huko mbeleni kama angefanikiwa kutengeneza dawa za magonjwa ambayo yamekuwa yakiangamiza jamii ya Afrika kwa makusudi kabisa kwa ajili ya faida ya Wazungu , lakini hata hivyo upande mwingine wa kibiashara aliamini familia hio ingeweza kumlipa fidia ya kuvunja mkataba.​

Hivyo kama Edna angekataa kuvunja mkataba ni dhahiri kwamba alikuwa akishindana na serikali kubwa zote za bara la Ulaya kwani Rothchild ndio watawala wa bara lote kwanzia Ufaransa ambako kuna tawi lake la kibiashara mpaka Uingereza na Ujerumani, lakini pia Urusi moja kwa moja.​

Edna alijikuta akigeuza kichwa na kumwangalia Roma , aliamini yeye pekee ndio ambaye anaweza kufanya maamuzi kwa wakati huo.​

Ikumbukwe kwamba Edna pia kama angevunja mkataba , sifa ya kampuni yake ingeshuka , kwanni siku ya juzi kwenye mahafali pale Chuo kikuu cha Mlimani dhumuni la mkataba wake na Profesa Clark lilikuwa bayana kwamba ni kusaidia nchi za Afika kujitegemea katika maswala ya utafiti wa utengenezaji wa madawa kwa magonjwa sugu,, jambo ambalo lilipokelewa kwa uchanya na mataifa mengi ya Afrika ambayo yalichoshwa na kunyenyekea wazungu, hivyo kama angevunja mkataba kwa ajili ya pesa ingemletea sifa mbaya na kampuni ingeathirika zaidi.​

“Edna nini mawazo yako juu ya hili”Aliongea Roma lakini Edna alisita kutoa jibu moja kwa moja.​

“Mr Maksim nadhani tuone kwanza masharti yako kwanza juu ya kuhitaji kuvunja mkataba na kampuni yangu , Kama nitakubali moja kwa moja lazima utambue kwamba pesa tu haiwezi kutatua tatizo lakini pia taswira ya kampun itaathirika , nadhani umekuja hapa ukiwa umefanya utafiti na umeona siku tatu hizi baada tu ya kutangaza nia yetu ya utafiti wa madawa hisa za kampuni yangu zilipanda kwa zaidi ya asilimia kumi”Aliongea Edna huku akijitahidi kujituliza ili kutumia akili yake ya kibiashara katika kufanya maamuzi.​

Maksim alibadilisha mkao tena huku akionekana kama mtu alietarajia swali hilo kutoka kwa Edna kwani alitabasamu.​

“Kwanza kabisa kampuni yako Tanzu iliopo ndani ya bara la Ulaya itapata kibali cha kufanya biashara upande wa Mashariki yote ya Ulaya ,Nimefahau kwamba mara ya mwisho ulivyokuwa Ufaransa uliweka wazi nia yako ya kutengeneza mirija ya kibiashara upande huo wa mashariki kwa kujipanua zaidi , lakini licha ya juhudi kubwa ulizoweka hilo halijafanikiwa mpaka sasa hivyo tutafanikisha ndoto yako, Pili biashara ya utafiti wa madawa sugu na mafunzo ya wanasayansi wazawa utaendelea kama kawaida lakini kwa kutumia wataalamu wabobevu ambao watatoka moja kwa moja Urusi nakuziba nafasi ya Profesa Clark na ninakuhakikishia kupitia wataalamu wetu ndani ya miaka mwili utakuwa na mafanikio unayoyata. Tatu na mwisho kabisa , tunajua mpaka sasa kuna mkataba wa kudumu uliosainiwa na Raisi wa awamu ya tatu wa biashara ya mafuta kati ya serikali na kampuni ya Vexto, tunapanga kuongeza kiasi cha mafuta yanayoingia Tanzannia kwa gharama ya nafuu chini ya thamani ya soko, lakini pia kampuni yako itapewa kipaumbele ya kupata malighafi zinazotokana na ‘Petreleum extraction”​

Edna alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha fidia zote zilikuwa ni kubwa kiasi kwamba hakuhitaji kufikiria mara mbili mbili na kama angekubali inamaanisha kwamba angezidi kuwa tajiri , ni kichaa tu ambaye angekataa dili kama hilo , ukizingatia pia kama angevunja mkataba na Clark ilikuwa na faida ya ziada kwake pia kwani angezuia uwezekano wa mahusiano ya kimapenzi kati ya Roma na Profesa Clark..​

Maksim baada ya kushusha bomu hilo la ofa kichaa alikaa kwa kuegamia kabisa , alijua kama kweli Edna ni mfanyabiasha asingeweza kukataa ofa yake.​

“Edna ofa ambazo zimetajwa na bwana Maksim ni kubwa mno na faida yake sio kwako tu bali ni kwa watanzania kwa ujumla na Serikali inaangazia swala hili kwako kwa matarajio chanya kutoka kwako kwani lina faida pia ya kidiplomasia baina ya nchi zetu mbili , huna haja ya kuwa na wasiwasi na Profesa Clark kwani familia yake ishafanya mawasiliano na Profesa ili kusitokee lawama yoyote”Alipigilia msumari waziri Nguya.​

“Kama ofa yenu ni ya kweli basi nita…”​

“Hapana” Roma alimkatisha mke wake baada ya kuona anataka kukubali na kauli yake ilifanya chumba kuwa kimya hata Edna mwenyewe alitetema na kuwa mpole​

“Haya mazungumzo yanapaswa kwanza kukubaliwa na Clark , hata kama atakubali kuvunja mkataba na hataki kuolewa basi nasema hivi hakuna wa kumtoa hapa nchini”Aliongea Roma.​

“Mr Roma nakufahamu kwa jina lingine ambalo hata familia ya Rothchild wanaliogopa kila linapotajwa , lakini hata hivyo haimaanishi kwamba unaweza kufanya maamuzi ambayo yanaingilia maswala ya kisiasa na uchumi wa dunia kwa ujumla wake , una nguvu kubwa lakini hata hivyo sio kama hufuatiliwi , makosa kidogo tu yanaweza kusababisha migogoro mkubwa kati ya Tanzania na mataifa makubwa”​

“Kwahio unanitishia si ndio ?”Aliongea Roma kwa Kingereza huku akisugua vidole vyake vya mikono ambavyo vishaanza kumuwasha.​

“Sikutishii ila nina kuhabarisha , kwa ninavyofahamu pia wewe ni mtoto wa raisi wa taifa hili na pia familia yako imefungamana na jeshi kwa muda mrefu , hivyo siamini kwamba hata wanafamilia wanaweza kukaa chini na kuangalia unaharibu maswala ya Diplomasia ambayo ni maslahi mapana kwa Wananchi”​

“Bwana Maksim nadhani kuna kitu kimoja unapaswa kujua , mimi nikiamua jambo langu kichwani basi hakuna mtu wa kunizuia kulitimiza , sintojali taifa na tafia kuingia kwenye vita kama inaleta maana ya kupata ninachotaka,msimamo wangu siku zote mwenye nguvu anaongoza njia na dhaifu anamfuata mwenye nguvu”Aliongea Roma na kumfanya bwana Maksim sura kumshuka.​

“Kama unakataa mapendekezo yangu nitaihusisha wizara ya mambo ya nje kushughulikia hili swala na nakuhakikisha hili swala halitopita kirahisi kama unavyodhani na sio kwa Tanzania tu lakini pia hata kwa Clark ambaye unajaribu kumkingia kifua , heshima yake aliojijengea ndani ya muda mrefu itaharibika itaharibika ndani ya siku moja”​

Waziri Nguya sofa lilianza kuwa la moto , serikali ilimwamini katika mazungumzo hayo ndio maana akatumwa kama mtu kati , lakini kile anachokiona hapo hakuna namna ya kufikia kwenye makubaliano kwa amani.​

“Roma unafanya nini , unaonaje tukitulia na tukizungumza hili swala bila mtafaruku”Aliongea Edna kwa wasiwasi kwani alimuona Roma kama bomu ambalo lingelipuka muda wowote ,lakini Roma ni kama hajamsikia.​

“Oh tena… CEO Edna kwa taarifa nilizokuwa nazo una madaraka kamili juu ya kampuni ya Vexto , kwanini unataka kushikiliwa kimaamuzi na mume wako kwenye maswala ya kibiashara , hili ni swala linalokuhusu wewe sio Roma , na hata hivyo nimeweza kupata taarifa kwamba upo vizuri sana likija swala la biashara”Aliongea huku akisimama na kutaka kupiga hatua kutoka nje , lakini Roma alitoka kwenye sofa na kumkinga kwa mbele akimzuia asipige hatua, alikasirishwa na kauli yake na kuichukulia kama tusi mbele ya mke wake.​

“Unataka kufanya nini .?.” Aliongea Maksim huku akianza kushangazwa na mabadiliko ya ghafla ya Roma, kwani alikuwa ni kama mtu mwingine kabisa kwa jinsi alivyokuwa na hasira.​

Maksim alimkwepa akitaka kumpita kwa pembeni lakini kabla hajatimiza azma yake Roma alimshika Shingo kwa nyuma na kumfanya Maksim kushindwa kupiga hatua​

“Usijione wa thamani sana tena ndani ya nyumba yangu , hupaswi kabisa hata kukaa meza moja na mimi mbwa wewe ..”Aliongea Roma huku sauti yake ikiwa nzito na palepale alimgeuza kama anachezeshwa Tango na ile anageuka alipigwa ngumi yenye ujazo mkubwa wa nguvu za kijini eneo tumboni na mkono wa Roma ulizama ndani na akauchomoa kwa nguvu na kusababisha damu kusambaa pamoja na nyama nyama.​

“Aaarrggh!!”​

Edna alifumba macho akishindwa kuangalia , Waziri pamoja na mabodigadi walishindwa kuzuia mshangao wao huku na kukimbilia nyuma ya Edna na kusimama.​

Maksim alidondoka chini huku akionekana kushindwa kuzuia maumivu anayoyasikia huku damu zikimtoka mfululizo , lakini Roma alimshika kwenye shingo kwa mara nyingine na kumtupia nje kama furushi akijua kabisa bwana huyo ni wa kufa.​

“Unaweza kutoa taarifa kwa kila kichotokea hapa ndani bila ya kubadilisha neno, na kama itatokea tatizo lolote njoo niambie nitakusaidia nitakusaidia kulirekebisha”Aliongea Roma akimwangalia Waziri Nguya pasipo kujali mikono wake uliojaa mabonge ya damu.​

Edna alishindwa kuhema kwa tukio aliloshuhudia , mwanzoni akili yake ilikuwa kwenye ofa , lakini sasa hivi hakuwa akifikiria kingine zaidi ya kuwa na hofu kwa kile kilichomkuta Mzungu.​

Muda ule ule waziri alipotaka kuongea neno , wote walijikuta wakiangalia nje na kushuhudia kitu ambacho hakikuwa cha kawaida , kwanza Maksim alisimama akionekana mzima kabisa , ni kama hakuguswa kabisa kwani sehemu aliopigwa ngumi na kutobolewa tumbo ilirudi kama kawaida , lakini muda huo huo sura yake ya kizungu ilibadilika na kuanza kutengeneza michirizi ya ukijani uliokolea kwenye macho , huku meno yake yakirefuka na kucha vile vile ziliongezeka ukubwa , ilikuwa picha ya kushanganza na kuwafanya wale mabodigadi wote kurudi nyuma na kumuacha Roma akiwa mbele peke yake​

“Your strength is realy unbeleivable Pluto …”Alisimama huku akionekana kama Vampire na hata tabasamu lake lilitisha mno.​

Roma palepale akili yake ilifanya kazi mara baada ya Maksim kupona kwa haraka sana , lakini pia kucha zake kuchomoza na meno kurefuka na kuwa na mwonekano usiokuwa na utofauti na Vampire.​

“Nimekumbuka ….Wolverines!!!, wewe ni mwendelezo wa kizazi cha White wolf kutoka Urusi , katika familia ya kifalme mliojipatia jina la Wolverines…”Aliongea Roma huku awamu hii akionyesha hali ya kuwa na msisimko usio na kifani ni kama ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na watu wa namna hio.​

“Hahaha.. sasa ushanifahamu hivyo huna cha kunifanya , hatupo kwenye kizazi cha karne ya tano sasa hivi , hilo jina lishapotea na kubakia sisi ambao ni binadamu wa kawaida , tumekuwa watawala wa siri karne na karne ndani ya taifa la Urusi , Sisi ni wafalme wa Nchi zote za mashariki ya Ulaya., ulichokifanya leo kimeingiza Tanzania kwenye orodha ya nchi adui zetu”Aliongea na baada ya kumaliza palepale alipotea mbele kwa namna isioelezeka.​

.​

SEHEMU YA 445​

Roma hakutaka kumfukuzia , hata hivyo alishawahi kusikia habari juu ya jamii ya siri sana iliokuwa imejibatiza kwa jina la Wolverines, lakini hakuwahi kuamini kuhusu stori hizo kwani kwake ilikuwa kama hadithi.​

Wolverines ni jamii kama Vampire ambayo simulizi zake zilisikika sana kati ya karne ya tano mpaka mwishoni mwa karne ya kumi na tano , katika zama hizo waliaminika kuwa binadamu ambao ni jamii ya Vampire , lakini utofauti wao ni kwamba Wolverine hawakuwa wakiathiriwa na mwanga wa jua kama ilivyo kwa Vampires na walikuwa na nguvu kubwa sana kwenye mapambano kuliko hata jamii ya Vampire yenyewe na waliweza kuishi hata nyakati za mchana na hawakutegemea damu ya binadamu kuishi bali wanakunywa damu ya mnyama anaefahamika kwa jina la Wolverine au White Wolf(Mbwa mwitu) na ndio chanzo cha jina lao, inasemekena mbinu pekee ya kuweza kuwaua ni kwa kunyofoa moyo wao.​

Waziri Nguya alihisi ni kama yupo kwenye ndoto ya kutisha , hakuamini angeanza siku kwa kushuhudia kitu cha namna hio , lakini upande wa Edna licha ya kuwa kwenye mshangao , lakini alishindwa hata kutetemeka zaidi ya kuangalia mikono ya Roma iliotapakaa damu ni jambo ambalo kwa mwanamke halivumiliki lakini kwa Edna ilikuwa jambo ambalo ni kama amewahi kuliona kabla.​

“Unaweza kwenda kuripoti kama ulivyoona hapa bila kuacha neno”Aliongea Roma akimwambia mheshimiwa waziri na kisha alipita na kuingia ndani na kwenda kuosha mikono jikoni kwenye sink.​

Edna alijikukta akitembea kwa kusita sita na kwenda kujibwaga kwenye sofa akiwa kama mtu ambaye hakuwa akijua kilichokuwa kikiendelea na hata Roma alivyotoka jikoni aliishia kumwangalia kwa maswali mengi.​

“Nadhani umeona mwenyewe kilichotokea , ijapokuwa mpaka sasa sijui ni kwasababbu ipi familia yake kutaka kumuozesha kwa viumbe wa ajabu ,, lakini siwezi kuruhusu swala hilo litokee”​

“Hivi unajiona unachokifanya mbele yangu?”​

“Nakuambia siwezi kumruhusu Clark kuolewa na wanyama”​

“Acha mambo yako ya kumlinda mwanamke mbele yangu Roma, utanikasirisha”​

“Nisamehe kama kauli yangu inaziumiza hisia zangu lakini huo ndio msimamo wangu , sidhani kwa ulichoshuhudia hata wewe mwenyewe ungekubaliana nacho”Aliongea Roma lakini muda huo huo Bi Wema na Blandina walishuka kutoka juu wakiwa na wasiwasi.​

Na walishangazwa zaidi mara baada ya kuona damu zilizokuwa zimetapakaa karibu na mlango na kutaka kujua nini kimetokea.​

Muda huo huo alipokuwa akitaka kuuliza , sauti ya gari kutoka nje ujio wa mtu zilisikika na mlango palepale ulifunguliwa na alionekana Profesa Clark aliekuwa akihema kwa nguvu.​

Alikuja akiwa amevalia koti la maabara na ilionekana kabisa alitoka kazini muda huo kwa mwonekano wake.​

Aliangalia damu zilizotapakaa na hakujali sana zaidi ya kupita na kumsalimia Blandina na Bi Wema na kisha akasalimiana na Edna aliekuwa akifikicha macho.​

“Kwanini umekuja ukiwa hivyo?”Aliuliza Roma na Profesa aliingiza mkono wake kwenye koti na kuibuka na kijichupa kama vile vya kuhifadhia chanjo(Vials) na kumpatia Roma.​

Ni ‘antidote’ , niliogopa ningechelewesha ndio maana nikaja mwenyewe haraka haraka , unatakiwa kumpatia na kumeza kwa kupitia mdomoni tu”Aliongea na kumshangaza Roma.​

“Umeweza kufanikisha ndani ya muda mfupi hivi?”​

“Damu ya mgonjwa wako nilipoifanyia majaribio niliweza kubaini amewekewa kimiminika ambacho ni kama sumu ambayo inashambbulia DNA za mwili, ni kimiminika ambacho kimetenenezwa kwa kuunganisha DNA na RNA za virusi ishirini na nne,, kimiminika hiko kinafahamika kwa jina la ‘Tribute to Maria’ , ni siraha ya kibailojia ambayo imefanyiwa majaribio nchini Urusi kwenye maabara ya siri ifahamikayo kwa jina la Nicene , mwezi uliopita kuna wanafunzi wangu i waliiuliza maswali baadhi yanayohusina na sayansi ya uundaji wa mchanganyiko wa virusi pamoja na namna Chanjo yuake inavyowezekana kutengenezeka na niliwapa majibu na kushauri wasijaribu kuunda siraha hio kwani ni hatari sana kwa maisha ya binadamu lakini inaonekana waliendelea na kazi yao”​

“Kwanini jina la ‘Tribute to Maria’ na vipi kuhusu hii maabara ya Nicene?”​

“Kwanza kabisa hiki kimiminika kiligundulika kwa mara ya kwanza katika karne ya kumi na moja kihistoria , ulikuwa ni mwendelezo wa tamaduni za kimiminika(Siki) alichopewa Yesu wakati wa kusulubishwa , utofauti ni kwamba Kimiminika hiki na Siki ni vitu viwili tofauti kwani katika karne ya kumi na moja kiliongezewa ubora wenye dhamira tofauti kabisa na kuanzia hapo kikaendelea kuboreshwa na katika Karne ya kumi na sita ndipo kilipobatizwa jina la Kinywaji cha Heshima Kwa Maria kupitia vita baina ya dini ya kikristo na waislamu wa Uturuki.​

Kila mturuki ambaye alikamatwa alilazimishwa kunywa kimiminika hiko kama atakataa kukubali kubatizwa na kuwa mkristo , sasa pale mateka anapolazimishwa kunywa hiko kimiminika wanajeshi(crusaders) walipiga kelele ‘Heshima kwa Maria’(Tribute to Maria) aliemzaa Mwana wa Mungu.​

Baada ya vita uwepo wa kinywaji huo ulipotea kabisa kwa kupigwa marufuku na kanisa la Roma , mpaka miaka ya hivi karibuni kulipogundulika tena kimiminika kilichopewa jina hili hili ambacho wanasayansi waliokuwa chini ya kanisa la Orthodoxy huko Urusi walikipatia jina kwa kuamini ni mwendelezo wa kimiminika kile kile kilichotumiwa katika vita vya kusambaza dini ya kikristo, kuhusu Nicene ni jina la maabara iliokuwa nchini Uturuki ambayo ilihusika kutengenezea kimiminika hicho wakati wa vita na baada ya vita kuisha maabara hio ilihamishiwa nchini Urusi mpaka leo hii na ndio ilioendeleza sayansi ya kutengeneza kimiminika kipya ambacho ni kama siraha ya kibailojia”Aliongea Clark kwa muda mrefu na kumshangaza Edna na Roma kwani maelezo hayo ni kama yalikuwa mapya kwao.​

Ndio kama utakuwa mtu wa historia basi utaweza kugundua jina la Nicene limetokena na jina la Nicaea kwa kilatini kilichotoholewa kutoka lugha ya kigiriki , lakini kwa kiswahili inafahamika kwa jina la Nikea , maana ya jina hilo ni mji wa ushindi ambayo kwa sasa unafahamika kwa jina la Iznik huko Uturuki.​

“Kwahio kama ni kweli hii maabara ipo eneo gani nchini Urusi na wanapata hela ya ufadhili kutoka wapi au ni serikali?”Aliuliza Roma.​

“Hio taarifa ni ya siri na mimi mwenyewe sijui , labda umjaribu rafiki yako Makedon kutoka Mossad nadhani atakuwa na majibu , udhalishwaji wa kimiminika hiko ulipigwa marufuku sana na kanisa la Catholic na Orthodoxy kwa kutumia jina la Maria, lakini licha ya hivyo hakuna kilichobadilika naamini kuna ajenda kubwa ya siri ambayo inaendelea , naweza pia kuamini huenda serikali ya Urusi haihusiki kabisa”​

“Okey nitajaribu kuwasiliana na Makedon aweze kunipa mwanga”Aliongea Roma huku akikuna kichwa.​

“Halafu nimesahau swali moja, kama mtu atakuwa amepatiwa hiko kimimnika kuna uwezekano wa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwani kwa melezo yako naweza kusema ni kirusi”​

“Hakika ni kirusi lakini lakini tunaita kimiminika kutokana na kwamba ni muunganiko wa virusi ishirini na nne vilivyodhalisha majimaji , bahati nzuri ni kwamba kinasambaa kama kirusi cha HIV , lakini naamini kuna uwezekano kikawa kimeongezewa ubora wa kusambaa kwa njia ya hewa ili kutumika kama siraha ya kibailojia inayosambulia Genes”​

“Umesema kuna wanafunzi wako wako waliulizia maswali juu ya hiko kimiminika , je unahisi ndio waliotengeneza ?”​

“Inawezekana kwani kati ya wanafunzi wangu mmoja wapo alikuwa ni mrusi”Aliongea.​

“Hawa wanafunzi wako kila wanapoenda ni kusababisha matatizo tu, kwanini unafundisha vichaa”Aliongea Roma​

“Roma nadhani hata wewe unafahamu ule msemo wa kwamba elimu inapaswa kutolewa kwa watu wote bure na kwa usawa , ndio nilichofanya, sina haki ya kumjaji mwanafunzi wangu anakwenda kufanyia nini elimu anayoipata ili mradi napokea heshima yangu kama mwalimu wao , wakishamaliza elimu yao siwajibiki kwa wanachofanyia elimu yao”​

“Lakini huogopi kwmaa inaweza ikatokea mmoja wapo kukugeuka na kukudhuru?”​

“Unajua nini Roma, licha ya kwamba Yan Buwen amekuwa kichaa lakini mafanikio yake yamenishangaza , likija swala la utafiti wa kisayansi ukimtoa Profesa Shelukindo nadhani ni yeye pekee kidogo anaeweza kunikaribia”​

Edna aliekuwa kimya muda wote aliona akili yake inakuwa nzito , kila siku anavyozidi kuishi na Roma aliweza kufahamu mambo mapya zaidi , huku mengi yakiwa ya kutisha zaidi na mazito kweli kweli..​

“Edna naomba unisamehe…”Aliongea Clark na kumfanya Edna kushangaa kwanini anaombwa msamaha.​

“Nilipishana na gari mbili wakati nakuja hapa , mojawapo ni gari ambayo namfahamu mmiliki wake na alikuja jana nyumbani kwangu , kwa uwepo wa hizi damu hapa naamini Roma ameweza kumfanyia jambo”Aliongea na kumfanya Edna kidogo kukosa neno la kuongea.​

Alijisikia vibaya kuona Mwanamke mwenzake analazimishwa kuozeshwa kwenye familia ya Mashetani .​

“Edna najua ukaribu wangu na Roma unaweza kukufanya ujisikie vibaya lakini naomba nikwambia usiwe na wasiwasi kabisa , sina mpango wa kuwa kidudu mtu kwenye mahusiano yenu , Roma aliniokoa mimi na mama yangu miaka mingi iliopita nikiwa mdogo na kama sio yeye nisingeweza kuwepo kwenye dunia hii , kwangu Roma ni mwokozi wangu , kama unahisi uwepo wangu hapa Tanzania unakufanya usijisikie vizuri niambie tu, sitokasirika nitaondoka mara moja, ninaweza kuagiza wanafunzi wangu na kuendeleza project yetu, Natumaini maisha yako na Roma kuwa yenye furaha…”​

“Inatosha Clark ,hakuna tatizo lolote mimi na Edna tupo sawa kabisa , kinachoniumiza ni hawa Klyuchevsky , bora hata wangekuwa ni Vampire lakini Wolverines , pumbavu kabisa siwezi kuruhusu ukaolewa na hawa viumbe na ukaja kuzaa mdudu, Catherine na familia yako watakuwa vichaa”​

“Usimlaumu sana mama , hana nguvu kubwa juu ya Rothchild miaka iliopita familia ya klyuchevisky walisaidia sana kwenye uchumi wa familia hivyo ni kama kulipa fadhila na hata hivyo sikuwa na mchumba na ni haki yangu kuoelewa. Binafsi nimeonea nisichukulie hili swala kuwa kubwa sana kwani hata kama nitaolewa kwao sio kwa ajili ya kuzaa ila ni kama maonyesho tu”​

“Kwahio unapanga kuolewa kwa hayo maonyesho?”​

“Ndio , ndoa yangu itatatua shida kubwa ya kiuchumi inayoendelea baina ya Urusi na Uingereza katika maswala ya nishati.. Roma nafahamu unajua haya sina haya ya kuelezea zaidi ni wajibu ambao unanihusu”​

Roma alitaka kuongea lakini Edna alimzuia kwa kumshika mkono.​

“Edna unataka kuongea nini?”​

“Mimi sioni tatizo la Maksim kabisa kumuoa , anaweza kuwa tofauti na binadamu lakini ni kijana mzuri , kinachoangaliwa ni moyo wake ulivyo ,mabadiliko yake ya muda mfupi yasiwape uhalali wa kujaji mapenzi yake kwa Clark wala kumsema vibaya Maksim, mimi nadhani Clark ukubali kuolewa tu”Aliongea Edna na kauli yake ilishangaza kila mmoja.​

Roma moja kwa moja alijua Edna hakuwa akipenda uwepo wa Clark ndani ya Tanzania hivyo anapanga kuhakikisha anaondoka moja kwa moja kwa kuoelewa.​

“Edna upo sahihi sana , Roma nadhani nishafikisha kilichonileta hivyo kwaherini”Aliongea Clark na kisha alitoka kwa kukimbilia nje akitoa machozi na ndani ya muda mfupi mngurumo wa gari ulisikika ukififia nje ya geti.​

Blandina na Bi Wema walikaa kimya muda wote , hawakutaka kuingilia swala hilo kwa namna yoyote , waliamini ni maswala ya wao kumalizana wenyewe.​

Roma hata yeye hakupenda kauli ya Edna ambayo imemfanya Clark kuondoka namna hio , alijua lazima muda huo angeenda kulia , alisimama na kutoka eneo la sebuleni na kupandisha kwenye chumba chake.​

“Roma unaweza kukasirika utakavyo lakini sijutii kwa kauli yangu, nipo tayari kufanya chochote ambacho kitalinda amani ya familia yangu”Aliongea na kumfanya Roma kusimama na kumwangalia kisha akatingisha kichwa na kuendelea kwenda juu.​

********​

Upande mwingine ndani ya hoteli ya Johari Rotana katika chumba cha Presidential Suite alionekana Maksim aliesimama kwenye dirisha akiangalia upande wa nje wa jiji huku akiwa ameshikilia glasi ya mvinyo mkononi.​

Alionekana kama mtu ambaye hakuwa ametoka kwenye kupatiwa kibano na Roma mpaka kupoteza vipande vya utumbo mpana , muda huo alikuwa amejifunga taulo mwili mzima akiwa msafi na sura yake ya Kihandsome boy , hakuna mtu ambaye anaweza kuamini kwamba anaweza kubadilika sura na kuwa wa kutisha.​

Nyuma yake alionekana mwanamke wa kizungu ambaye amepiga magoti chini akiangalia mgongo wa bwana Maksim.​

“Boss misheni ulionipa ya kumshawishi kiongozi wa Alshababu kutumia wanajeshi wake imefannikiwa na mpaka sasa wapo tayari mpakani na kombora lilojaa kimiminika cha ‘Tribute To Maria’ lipo kwenye mkao wa utayari kuelekea Tanga, nahitaji oda yako tu kuendelea na misheni”Aliongea na kumfanya Maksim kutabasamu.​

“Kama nilivyotarajia mpango utaenda sawa , Mkuu wa Alshabab kasemaje baada ya kusikia kifo cha mtoto wake?”​

“Yupo ni mwenye hasira kubwa sana na hasira yake imefanya kumshawishi kwa urahisi mpaka kukubali mpango wetu”Aliongea huku akitabasamu kifedhuli.​

Kama Roma angekuwepo hapo angeweza kumfahamu mara moja huyo mwanamke na huenda asingefanya kosa ile juzi kumruhusu kumtoroka , alikuwa ni Aishapova.​

Mtoto ambaye alikuwa akizungumziwa juu ya kifo chake ni Shedrack Kengeu ambaye halikuwa jina lake halisi, kwanza ni msomali na ni mara chache sana kukutana Msomali anaitwa Shedrack Kengeu, ukweli Shedrack alikuwa mtoto wa kundi la Alshabab ambaye alitumwa Tanzania kwa mishenni maalumu ya kuhakikisha kuna makubalianao ya kibiashara kati ya Kundi la kihalifu la ZoaZoa pamoja Alishabab kupitisha siraha kupitia mipaka ya Tanzania.​

Miezi kadhaa iliopita Samweli Nguluma ambaye ni baba yake Benadetha alikataa kufanya biashara baina ya Alshababu na ZoaZoa kwa kuogopa serikali ya Tanzania kugundua , baada ya Samweli kutokubali dili hilo Alshababu kwa kumtumia Shedrack walimshawishi mke wa bwana Samweli Nguruma afahamikae kwa jina la Zuwena kumsaliti mume wake kwa kumuua na kisha awe mkuu wa kundi hilo na kisha afanye biashara ya kupitisha siraha za kivita kwenda kwa kundi la Alshabab.​

Lakini kabla ya Zuwena kutimiza azma yake ya kumuua mpango wake ulivuja na Samweli Nguluma ndipo aliposhitukia mchezo mapema na kumuwekea mtego, mpango wa Zuwena ni kumuua Samweli nchini Congo siku tatu zilizopita na Samweli alitumia mtego huo huo kumnasa mke wake na ushahidi na hakumpa tena msahama zaidi ya kumchapa Risasi ya kichwa.​

Taarifa ilipomfikia Mika kuhusu mama yake kupigwa risasi nchini Congo na Mzee wake ndipo alipotorokea Bagamoyo , lakini Alshababu hawakukata tamaa mara baada ya mpango A kufeli , hivyo walianzisha mpango B ambao ulikuwa ni kumtumia Mika,​

Shedrack ambaye alipewa jukumu la mipango yote A na B alikuwa tayari na ukaribu sana na Mika kwa muda mrefu kwa kuhakikisha mipango yote inafanyika kwa wakati mmoja na ukweli pia ni Kwamba Shedrack hakuwa Shoga kama Roma alivyomuona bali alikuwa akiigizia ili serikali ya Tanzania isije kufatilia taarifa zake.​

Sasa haikueleweka ilikuwaje mpaka Maksim kuweza kufanya mawasiliano na Kundi hilo la wapiganaji haramu , lakini mara baada ya Mika kumpiga risasi mtoto wa mkuu wa kosi hilo la Alshababu , Aishapova alitoa taarifa kwenda Alshababu kwamba mhusika wa kifo cha Shedrack Kengeu(Jina feki) ameuliwa na Roma.​

Ilionekana kabla ya ujio wa Aishapova Tanzania walikuwa kwenye majadiliano ya siri , lakini ni hakika kwamba mkuu wa kundi hilo baada ya kupata taarifa ya kifo cha mwanae moja kwa moja itakuwa alijenga kisasi na Romampaka kumpelekea kutoa kikosi ambacho kimejificha mpakani Tanza na Kombora la kimiminika cha kirusi kilichopewa jina la Tribute To Maria.​

“Vipi kuhusu Clark?”Aliuliza Maksim kwa kirusi.​

“Princes amerudi nyumbani kwake, kwa uchunguzi niliofanya tumegundua kuna maabara ndani ya nyumba anayoishi”​

“Endeleeni kumfatilia kwa umakini na jiandaeni muda wowote nitatoa maagizo ya kumteka”Aliongea kwa Kirusi.​

“Bosi mpaka sasa nimeshindwa kukuelewa , kwanini unataka sana kumuoa Princess Clark licha ya kuonyesha utomvu wa nidhamu ninavyoona hapaswi kuwa sehemu ya wanafamilia wa Klyuchevsky”​

“Unajua nini kuhusu mimi wewe .. simuoi kwasababu nampenda ila namuona kwasababu ya akili yake …”​

“Akili?”​

“Tumetumia akili nyingi pamoja na muda kutegeneza kirusi cha Tribute to Maria ,, kama mpango wetu ukiweza kufanikiwa hakuna nchi itakayoweza kutengeneza chanjo ndani ya mwaka mmoja , mtu anaeweza kuvuruga kila kitu ni Clark pekee, unachotakiwa kuelewa kirusi hiki kimetengenezwa na mwanafunzi wake ambaye yupo chini yetu na kama huyu Myahudi hatutomdhibiti atatengeneza chanjo ndani ya masaa machache na mpango kufeli”​

“Kwahio unachofanya ni kuweza kumdhibiti asiweze kutengeneza Chanjo?”​

“Upo sahihi , Familia ya Rothchild imekubali Clark aolewe kwa siri na familia yetu kwasababu wanaamini kwamba ataendelea kuwa na msimamo wake wa kutojihusha na utengenezaji wa siraha za kimaangamizi huku wao kuendelea kupata gesi asilia kupitia Nord stream , naweza kusema kwamba wanajidanganya ,Wolverine tuna mbinu nyingi za kuweza kumwendesha binadamu na kutufanyia mambo bila hata yeye kujielewa na huo ndio mpango , ni sawa na kupiga ndege wawili kwa jiwe moja , tutazuia utengenezwaji wa chanjo ya Tribute to Maria lakini pia tutaweza kutumia akili ya Clark kufanikisha uundaji wa siraha nyingine kubwa , Urusi ipo duniani kwa kuwa mbabe wa dunia na sio Wamarekani”Aliongea​

“Boss unazungumzia Totem of Hypnotism katika kukontrol akili yake?”​

“Nadhani unanipata vyema , angekubali kuoelewa na mimi bila shida yoyote nisingefikia huko”​

“Lakini bosi vipi kuhusu Hades , uwezo wake lazima tuuzingatie?”​

“Usiwe na wasiwasi mpango tuliouandaa ni kwa ajili ya kumdhibiti asifanye jambo la kijinga, amenichokoza kwa kunidhalilisha leo lakini nitamlipa kwa kumuelimisha nini maana ya nguvu ya Kluychevsky hata mtangulizi wake hakuwahi kutuchokoza”.​

“Boss huu mpango kama utafanikiwa , tutakuwa ni wakuogopeka sana , mheshmiwa Raisi amekuwa ni mwenye kupinga mipango yetu , lakini baada ya kuona matunda ya mpango lazima atatoa kibali mwenyewe , naahidi nitakuwa mtu wa kwanza kumuua yule mwanamke Lilith, wapuuzi wale wanatusumbua sana , Wolverine lazima tuisimamishe Urusi itawale Dunia tena”Aliongea Aishapovakwa kujigamba.​

ITAENDELEA.​

 

SEHEMU YA 446.

Aishapova alionekana kuwa na munkari kweli kwa kuona kwamba muda si mrefu watu wa jamii yao wanakwenda kuwa na nguvu juu ya jamii nyingine katika ulimwengu usio onekana.

Wakati akiendelea kumwangalia bosi wake kwa namna ya kumuhusudu mara akili yake palepale ilifanya kazi na kukumbuka tukio moja.

“Boss siku ya juzi baadhi ya wanajeshi wetu walimnywesha Mtoto wa kundi la ZoaZoa kimiminika cha Tribute to Maria, inawezekana Hades akawa amempeleka kwa Profesa Clark kwa ajili ya kutengenezewa chanjo”

“Unaongea nini?”Alibadilika na kugeuka na teke ambalo lilimpata Aishapova kifuani na kwenda kumtupa kwenye mlango.

“Nena kachuchunguze sasa hivi nini kiliendelea , kama usemayo ni kweli mumteke muda huu na kuondoka nae , usimpatie nafasi akatengeneza chanjo”Aliongea kwa hasira na Aishapoiva aliitikia huku akikohoa damu na kuondoka kwenye chumba hicho .

Upande Mwingine Roma baada ya Clark kuondoka nyumbani kwake alijikuta akiingia kwenye mawazo ya hapa na pale , akifikiria namna ya kutatua tatizo lililokuwa likiendelea , Roma hakuwa na hasira kwa kauli ya mke wake ya kuunga mkono Clark kwenda kuolewa na Maksim aliona Edna alikuwa akijitahidi kufanya maamuzi ambayo hayawezi kuathiri familia , lakini pia hakuwa kwenye nafasi ya kukasirika kwani yeye ndio chanzo cha matatizo yote.

Roma alitoa simu na kisha alimpigia mwanajeshi wa The Eagles aliekuwepo karibu na kisha akampatia Chanjo ile iliotengenezwa na Clark na kumpa maelekezo apeleke nyumbani kwa Benadetha na apatiwe Mika.

Roma mara baada ya kurudi chumbani kwake kwa mara nyingine alizitafuta namba za Makedoni na kisha akafanya mawasiliano moja kwa moja na kumpa maelezo ya kuchunguza kuhusu taarifa za Nicene Lab.

Muda huo huo alimtafuta Tanya awape maagizo kundi lake la Yamata Sect kufanya uchunguzi kwanzia kwenye hoteli ya Bagamoyo one na kujua dhamira ya uwepo wa wanajeshi wa Urusi aliowaua siku ya juzi , aliamini kuna jambo kubwa ambalo lilikuwa linaendelea na alitaka kulifahamu.

Baada ya kumaliza kuwasiliana na Tanya alimpigia Diego na kumpa maagizo ya ulizi wa Profesa Clark kuongezewa , aliamini lazima Maksim angefanya jaribio la kumteka Clark hivyo hakutaka kutoa mwanya huo kufanikiwa.

“Mfalme kuna taarifa nyingine imetufikia?”Aliongea Diego

“Taarifa gani?”

“Kuna tishio la kigaidi ambalo limepangwa kufanywa na kundi la Alshababu kati ya mpaka wa Tanga na mkoa wa pwani , taarifa zinaonyesha wanajeshi hao wanataka kuachia bomu lenye siraha ya kibaiolojia”Aliongea Diego na kumshangaza Roma.

“Unamaanisha Tribute to Maria?”

“Ndio Mfalme Pluto , ni taarifa ambayo tumeipata muda huu hivyo hatujaithibitisha na uchunguzi wetu”

“Imetumwa na nani?”

“Kuhusu mtu alietuma kwetu hajaweka wazi jina lake , ni kama hakutaka kujitambulisha lakini inaonekana nia ni sisi kuchukua hatua”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo.

“Fanyeni kwanza uchunguzi kuthibitisha taarifa hio na juu zaidi tufahamu ni kwanini wanajeshi hawa wanataka kutumia Tanzania kama sehemu ya majaribio, unaweza kumtafuma Omari Tozo akawarahisishia katika uchunguzi, ukikamilisha nakupa ruhusa ya kuamua cha kufanya ili kuhakikisha tukio hilo halifanikiwi na kuleta matatizo kwa raia”

“Sawa mfalme Pluto nakuhakikishia kila kitu kitaenda sawa”Alijibu Diego na Roma alikata simu huku akihema kwa nguvu , alijua tukio hilo lilikuwa likimuunganisha na mwanamke aliekuwa akifahamika kwa jina la Aishapova lakini hata hivyo alimini hakuna kitu kinafanyika bila ya sababu.

Nusu saa mbele aliweza kupokea simu kutoka kwa Makedoni na Roma aliipokea haraka haraka.

“Mfalme Pluto watu wetu wamejaribu kutafuta taarifa zinazohusiana na maabara ya Nicene kupitia mfumo wa utunzaji taarifa wa KGB na tumeweza kufahamu Nicene ni maabara iliofufuliwa upya mwaka 1940 na mwanasayansi aliefukuzwa jeshini chini ya serikali ya Kisoviet , alifukuzwa kutokana na Marekani kuishutumu Urusi kumtumia mwanasayansi huyo kufanya utafiti juu ya siraha za kibaiolojia , hivyo kufukuzwa kwake ilikuwa ni kwa ajili ya kuzima kashfa hio , lakini hata hivyo hakuacha kufanya utafiti wake kwani baada ya kutoka jeshi alifufua maabara ya Nicene kwa kushirikiana na familia ya Kyluchevsky”Aliongea Makedon.

“Kwahio unaamaanisha kwamba familia hio ndio ipo nyuma ya tafiti zinazoendelea ndani ya maabara ya Nicene?”

“Ndio Mfalme Pluto , kutokana na ukubwa na nguvu ya familia hii ni watu wachache sana wanaojua kinachoendelea ndani ya maabara hio , wanafunzi wawili ambao walikuwa chini ya Profesa Clark wanafanya kazi ndani ya hio maabara na kama kweli wanaboresha kimiminika cha Tribute to Maria basi tutakuwa hatarini, labda tu”

“Labda Profesa Clark aweze kutengeneza chanjo si ndio?”Alimalizia Roma.

“Ndio Mfalme , Nadhani Klyuchevsky wanamuhitaji Clark kwa ajenda binafsi na sio kwa ajili ya ndoa, inaonekana kama asipokuwepo upande wao anaweza kuharibu mipango yao ndio maana wametoa pendekezo la ndoa”

“Umefanya vizuri kunipatia taarifa ila kwasasa nataka utafute eneo maabara hio ilipo na kisha umpe taarifa zote Sauroni”

“Mfalme Pluto kwanini unataka kumpa kazi kichwa maji kama Sauroni , hii tunapaswa kuifanyia kazi wenyewe Mossad”

“Wanajeshi wenu hawawezi kushindana na Wolverines kutokana na uwezo wao wa kujiponyesha”

“Lakini Mfalme Pluto hata The Eagels hawawezi , tena hapa tunazungumzia Wolverines na sio Vampires”

“Kama wakishindwa nitaingia kazini mwenyewe na wengine wote waliosambaa sehemu tofauti tofauti nitawapa kazi kikosi cha Expendable”

“Aaa Mfalmeee..Expendable!!, unaonekana kuwa na hasira kuliko nilivyodhania niliamini huwezi kwenda mbali mpaka kuwatumia wanajeshi wa kikosi cha Expendable”

“Walitakiwa kujiandaa mara baada ya kumfanya Clark kuwa kete yao kwenye mchezo wa Chess”

“Mfalme Pluto mpango wako wa mwisho ni upi?”

“Huyu Maksim anaonekana kadhamiria kweli kumuoa Clark , lakini atawezeje kutimiza azma yake kama hatokuwa na familia tena”Aliongea Roma na kumfanya Makedoni upande wa pili kunyamaza , aliamini kabisa alichokuwa akimaanisha Pluto ni kwamba angeua wanafamilia wote wa jamii ya Wolverine.

*******

Upande mwingine ndani ya ikulu ya Mheshimiwa Senga kulikuwa na kikao cha dharula.

Kikao kiliitishwa mara baada ya serikali kupata taarifa za tishio la ugaidi kutoka ubalozi wa Marekani , baada ya taarifa hio kufikia usalama wa taifa vikosi vya uchunguzi vilipewa maagizo ya kufanya uchunguzi wa haraka sana kuithibitisha.

Watu wanne walikuwa wameketi kwenye meza , akiwemo Raisi mwenyewe ,Mheshimiwa waziri mkuu , waziri wa ulinzi , Mkurugezi wa kitengo cha usalama wa taifa , Mkuu wamajeshi na mkuu wa jeshi la polisi.

Mheshimiwa Senga alimpa ishara mkuu wa idara ya kitengo cha usalama wa taifa kutoa maelezo kwa ufupi juu ya kile kinachoendelea.

“Tumeweza kupokea taarifa kutoka ubalozi wa Marekani inayoelezea tishio la kigaidi linalotaka kufanywa upande wa mkoa wa Tanga , kwa maelezo ambayo wametupatia ni kwamba siku mbili zilizopita katika mkoa wa Pwani wilaya ya Bagamoyo kulitokea tukio la kiharifu ambalo lilipelekea mmiliki wa hoteli ya Bagamoyo one kupoteza maisha”

“Nimesikia kwa muda mrefu juu ya hii hoteli na skendo zake lakini sikuwahi kujua mmiliki wake”Aliongea Afande Tozo.

“Bwana Shedrack Kengeu ndio mmiliki”Alijibu na Mheshimiwa alimpa ishara ya kuendelea.

“Ni kweli kwamba kwa muda mrefu serikali yetu ilikuwa ikifahamu mmiliki kuwa Shedrack Kengeu ,lakini kupitia ubalozi wa Marekani tumeweza kugundua mmiliki wa hoteli ya Bagamoyo one ni mtu mwingine”

“Unamaaisha nini kusema mmiliki ni mtu mwingine”

“Maelezo yanaonyesha Shedrack anaimiliki hoteli ya Bagamoyo One baada ya kupewa nguvu kisheria(Power of Attorney), lakini wamiliki wa hoteli hio ni kampuni ifahamikayo kwa jina Dalai , iliosajiliwa mwaka 2018 katika visiwa vya Shelisheli , baada ya kufatilia kampuni hii ya Dalai imegundulika ni kampuni hewa(Shell Company) ambayo iliuzwa kwa kampuni ya Talhat kutoka Somalia, mmiliki mkuu wa hisa ndani ya kampuni ya Talhat ni Mahmood Tarf ambaye ni mfungwa nchini Botswana”Aliongea na kufanya wote kuangaliana kwani ni kama hawajaelewa.

“Kwahio kwa maelezo yako unataka kumaanisha nini bwana Kizito”Aliuliza Mheshimiwa Waziri mkuu.

“Mahmood kabla ya kukamatwa nchini Botswana alikuwa akihusishwa kuwa mkuu wa kikosi cha wapiganaji wa Alshababu mpaka alipohamisha madaraka yake kwa mdogo wake afahamikae kwa jina la Faruq Tarf , huyu bwana ni mfanyabiashara pia na ameoa mwanamke wa Kitanzania afahamike kwa jina la Zumaridi kutoka Mwanza”

“Maelezo yamekuwa marefu kidogo , tunataka kujua tishio la kiusalama linaungana vipi na Bagamoyo one”Aliongea IGP.

“Zumarid kabla hajahamia nchini Tanzania akitokea Somalia alipokuwa akiishia na mume wake Faruq alishajifungua mtoto wa kiume na hata hivyo hakupewa nafasi ya kurudi nchini na mtoto wake afahamikae kwa jina la Sharf , lakini miaka minne iliopita Sharf aliweza kurudi kwa mama yake Zumarid na kubatizwa kuwa mkristo na kupewa jina la Shedrack Kengeu”.

Baada ya Sharf kukaa nchini kwa jina la Shedrack Kengeu ,mwaka mmoja mbele ndipo ujenzi wa hoteli ya Bagamoyo One ulipo anza na kukamilika mwaka jana , hivyo ukifuatilia muunganiko wote huo utadugnua Sharf baba yake ni mkuu wa kikosi cha Alshababu na kwa uchunguzi uliofanyika hivi karibuni ilionyesha Shedrack Kengeu kuwa na mahusiano ya karibu na kundi la ZoaZoa kutoka Kahama , mahusiano haya yalionekana kuwa na ajenda ambayo ilionyesha Shedrack alikuwa akimshawishi mkuu wa kundi hilo kusaidia kupitisha siraha za kivita kupitia Tanzania kwenda kwenye kambi ya Alshababu ombi ambalo ilionekana halikukubaliwa”

“Hii ni taarifa pia ambayo tumeletewa na Ubalozi kupitia idara ya CIA ,inaoneysha walikuwa wakifuatiia kwa ukaribu sana familia ya Klyuchesky kutoka Urusi na wameweza kugundua familia hio kufanya mawasiliano na mkuu wa kikosi cha Alshababu kwa kumtumia undercover agent afahamikae kwa jina la Aishapova”Aliongea kwa kuonyesha picha ambayo anaonekana Aishapova akiwa amesimama na mwanaume alievalia kanzu, lakinni hata hivyo sura ya mwanaume huyo haikuonekana kwani alijifunga usoni kwa Skafu na kuacha macho tu kuonekana.

Aliweka kituo na akachukua karatasi na kisha kumpatia mheshimiwa Senga na akamalizia kwa wanakikao wote.

“Picha unazoziona hapo Mheshimiwa zimetumwa kwetu kutoka makao makuu ya CIA na hao ni wanajeshi wa kundi la Alshababu wakiwa mpakani kuingia Tanzania na siraha aina ya bomu la kibailojia”

“Alshababu kwanini wanataka kutuchokoza ,hatujawahi kuwa na ugomvi nao?”Aliuliza Afande Tozo

“Waamarekani wanaamini kwamba kutokana na mazungumzo kati ya familia ya Kyluchevsky na Alahababu yalianza kwa muda mrefu , wanaamini kitendo cha kufa kwa Shedrack Kengeu nchini Tanzania yalimwamsha Faruq na kutaka kulipiza kisasi cha mwanae , lakini hata hivyo wanaamini kuna zaidi ya sababu ambayo hwaifahamu mpaka sasa”

“Ineleta maana , ni mara chache sana kwa wanajeshi wa Alshabau kutaka kujiletea uhasama na jeshi letu , lakini huyu Shedrack kwanini amakufa”

“Kwa taarifa tulizoweza kukusanya ni kwamba Shedrack kauliwa na Roma Ramoni , ambaye ndio aliesababisha tukio la kiharifu ndani ya hoteli ya Bagamoyo one , baada ya kufika kumchukua mtoto wa Samweli Nguluma , lakini hata hivyo tukio hilo lilitokea mara baada ya gari lake kutegeshewa bomu na kulipuka, hivyo inaonekana muhusika alikuwa Shedrack na Roma alimuua kwa kulipiza kisasi”

“Roma Ramoni?”Aliuliza mheshimiwa huku akionyesha hali ya mshangao na hasira kuanza kujitengeneza.

“Ndio mheshimiwa, lakini hata hivyo hatuwezi kuamini moja kwa moja kwamba Alshababu wanataka tu kulipiza kisasi inawezekana kuna sababu nyingine ndio maana Klyuchevsky wamehusika”

“Nashindwa kuelewa moja kwa moja , ukijumlisha swala la Profesa Clark na Kifo cha Samweli Nguluma halikai sawa na taarifa tuliokuwa nayo, kama Wamarekani wapo sawa kuhusu Klyuchevsky kufanya mazungumzo na Alshababu kwa muda mrefu basi tunaweza kuamini kuna zaidi ya sababu”

“Mheshimiwa huyu Profesa Clark anahusikaje na familia hii ya Klyuchevsky?”Aliuliza Waziri Wa ulinzi na Mheshimiwa Senga aligundua kweli hakuwa ametoa mwongozo wa kile kilichokuwa kikiendelea.

Lakini palepale mlango wa ofisi hio ulifunguliwa na mwanamama afahamikae kwa jina la Fatuma ambaye alpandishwa cheo kutoka kuwa msemaji wa ikulu mpaka kuwa katibu mkuu wa Ikulu.

“Mheshimiwa Afande Kweka yupo kwenye line anataka kuongea na wewe”Aliongea mwanamama Fatuma na mheshimiwa alimpa ishara ya kumpatia simu.

“Senga nasikia upo kwenye kikao na wakuu waandamizi wa usalama wa nchi”

“Nadhani taarifa imekufikia , tamaa za mjukuu wako zinaingiza nchi kwenye matatizo”Aliongea Raisi Senga.

“Mjukuu wangu au mtoto wako, hata hivyo nimekupigia kukutaarifu kwmaba haina haja ya kuendelea na kikao”Aliongea Afande Kweka.

“Unamaanisha nini haina haja ya kuendelea na kikao?”

“Tayari Mjukuu wangu kashaingia kazini na muda si mrefu utapata taarifa ya tishio la kigaidi kuzimishwa, lazima tukubali kuna utofauti mkubwa kati yako na Roma , wewe wakati unaendelea kufanya vikao yeye tayari anashughulikia tatizo”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Senga kungata meno kwa hasira kwani aliona kama baba yake anamtusi.

ITAENDELEA JMATANO -WATSAPP ME 0687151346

 
Back
Top Bottom