Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Nipo na nimefungua hii code makusudi ili Hawa wanaolalamika lalamika waende kule! Mkuuu hii ni kazi inapaswa kuheshimiwa na upate unachostahili
😄😄usitufanyie hivo we jamaa Singano anatuelewa sisi walala hoi anatufanyia hisani sasa unataka kutukaanga dah!
 
Hizi hadithi Zingine kuchelewa kwisha ni kwamba watunzi hawazingatii ratiba. Kama Sio hivyo zingeisha mapema. Ni kama vile wanatengeneza arosto kiaina singanojr
 
Hizi hadithi Zingine kuchelewa kwisha ni kwamba watunzi hawazingatii ratiba. Kama Sio hivyo zingeisha mapema. Ni kama vile wanatengeneza arosto kiaina singanojr
kweli mkuu ndo kama ile haditi yake ya HADES eti tulisoma miaka miwili humu na hii nayo ya HAMZA ndo kama hivi tutaisoma mpaka 2026 yaani ujinga tu wanaboa ni kipi cha kusoma miaka miwili utadhani tunachukua degree.!
 
kweli mkuu ndo kama ile haditi yake ya HADES eti tulisoma miaka miwili humu na hii nayo ya HAMZA ndo kama hivi tutaisoma mpaka 2026 yaani ujinga tu wanaboa ni kipi cha kusoma miaka miwili utadhani tunachukua degree.!
😃😃😃
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR.


Regina alikuwa katika mshangao maana ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Shangazi akiwa na uwezo wa kuzimisha watu wenye mafunzo ya kininja. Asichokijua Regina ni kwamba Shangazi alikuwa ni mwanajeshi na yupo kwenye maisha yake si kama shangazi yake tu, bali kama mlinzi wake kwa ajili ya kulinda nafsi nyingine iliyolala ndani yake.

“Shangazi, umefikaje hapa?” aliuliza Regina akiwa na mshangao.

“Hata kama wakubwa wa familia wamekwisha kuondoka, jina la familia linatakiwa kudumu. Nimeshindwa kuvumilia kusubiria nyumbani, ndiyo maana nimekuja kwa ajili ya kukupa ulinzi. Hamza pia yupo mwenyewe tu, hivyo si rahisi kukulinda na kudili na adui kwa wakati mmoja,” aliongea Shangazi.

Upande wa Hamza, hakushangazwa na uwezo wa Shangazi hata kidogo. Ukweli ni kwamba alishamuona si mtu wa kawaida tokea siku ambayo anatia mguu katika nyumba ya Regina, ni hivyo tu hakutaka kumchimba kiundani.

“Shangazi, naomba umlinde Regina kwa sasa. Ngoja niende nikawatafute,” alisema Hamza.

“Vipi kuhusu Mzee Wilson?” aliuliza Shangazi.

“Ametutoka tayari.”

“Nini!?” Shangazi alijikuta akitoa macho na mwili wake ulianza kumtetemeka.

“Kuhusu kilichotokea, ngoja Regina atakuambia. Mimi napaswa kuwahi, la sivyo nitachelewa,” aliongea Hamza.

Shangazi aliishia kumwangalia Regina na palepale alimkumbatia kwa nguvu huku machozi yakimtiririka. Alimuonea huruma; anakwenda kumzika bibi yake na baba yake kwa wakati mmoja.

Hamza, licha ya kwamba moyo wake haukutaka kuwaacha wenyewe, kwa wakati huo muda ulikuwa ni mali hivyo alipaswa kuwahi.

Mara baada ya kushuka kwenye lifti, alimpigia Afande Himidu na kumwambia nia yake ya kuwafukuza wahalifu. Afande huyo alimwambia Hamza awahi Gati ya Kigamboni Naval Base atakutana na wanajeshi wa kitengo cha Malibu.

Hamza, mara baada ya kupata taarifa hiyo, hakutaka kuchelewa hata kwa sekunde. Uzuri ni kwamba hoteli ya Dar Lux ilikuwa eneo la Kigamboni, hivyo haikumchukua muda mrefu kufika.

Kitendo cha kukaribia tu eneo hilo, gari SUV ya kijeshi ilisimama karibu yake na mlango ulifunguliwa haraka haraka na mwanaume na mwanamke. Mwanaume alikuwa amevalia kombati za kijeshi rangi nyeusi na koti la kuzuia risasi kifuani, na mwanamke alikuwa amevalia kombati za kijeshi za kikosi maalum cha Malibu. Hawakuwa peke yao; kulikuwa pia na Afande Norbert Geza na baadhi ya wanajeshi wa kikosi chake.

Hamza aliwatupia macho wale waliokuwa wa kwanza kushuka kwenye gari na aliishia kutingisha kichwa baada ya kuona walikuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi, na wote walikuwa wakifuatilia levo ya mzunguko kamili.

“Mr. Hamza...” aliekuwa wa kwanza kuita ni Norbert. Licha ya kwamba siku kadhaa zilizopita alipokea kichapo kutoka kwa Hamza, lakini muda huo ni kama ameweka kinyongo pembeni na sasa alikuwa na macho ya heshima na woga kiasi.

“Ilikuwaje mkachezewa akili? Yaani bado mmegundulika lakini mkaendelea kufuatilia magari yao?” aliongea Hamza.

Kauli yake ile iliwafanya wanajeshi hao kushikwa na soni juu ya kile kilichotokea; dakika ambayo waligundua gari waliokuwa wakiifukuza haikuwa na mateka, walikuwa wamekwisha kuchelewa muda mrefu.
"Wewe ni nani, unadhani una vigezo vya kutoa maoni yako juu ya utendaji wetu kama jeshi?" Aliongea mwanaume ambaye alianza kutoka kwenye gari akitangulizana na mwanamke.

"Mimi kuwa nani sio muhimu kwako. Mmeshajiandaa na boti tayari? Kuna uwezekano wametuacha umbali wa nusu saa na itakuwa ngumu kuwafikia," aliongea Hamza.

"Wewe inakuhusu nini kama tumeita boti ama hatujaita? Na unajuaje wamekimbilia baharini? Kuna uwezekano wamejificha eneo lingine la nchi kavu na wamekudanganya uamini wapo baharini."

"Hivi unadhani hili kundi la roho zinazotangatanga ni wajinga au nyie ndio wajinga? Kama wakiendelea kubakia hapa jijini ni swala la muda tu kukamatika maana hakuna njia watakayopita bila kuonekana. Unadhani kundi la kihalifu la daraja B linaweza kuwa na akili za kijinga namna hiyo?"

"Wewe ni nani kuwa na ujasiri wa kutukana kikosi chetu?" Aliongea yule bwana kwa hasira.

"Afande, huyu ndiye aliyetuma ripoti kwenda kwa Mshauri Mkuu. Ila haijalishi hata kama unafahamiana na Mshauri Mkuu, haimaanishi una mamlaka ya kutunyooshea vidole," aliongeza kwa dharau.

Kapteni Norbert, mara baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, aliingilia kati mara moja. Alijua wanajeshi wenzake hawakuwa wakimfahamu Hamza.

"Hamza, hawa ni makomandoo wa kitengo cha Malibu. Wanafahamika kwa majina yao ya msimbo, Kanali Mwiba na Kanali Barafu. Ndio wanaongoza hii misheni," aliongea Kapteni Norbert kwa upole, akijaribu kutuliza hali.
“Sijali kama nyie ni makanali au majenerali, fanyeni haraka tupate helikopta na boti, la sivyo wakishaingia maji ya kimataifa itakuwa ngumu kuwakamata tena,” alisema Hamza kwa msisitizo.

“Kama wakifikia maji ya kimataifa, maana yake ni mwisho wetu na jeshi haliwezi kuendelea kuwafuatilia,” aliongea Afande Mwiba.

“Watu wamelipua bomu ndani ya ardhi ya Tanzania, wameteka na kuua halafu unasema hujali kama wakikimbilia nje ya mpaka wa Tanzania, au ni kwa sababu mnawaogopa?” Hamza aliuliza kwa hasira.

“Angalia maneno yako, dogo. Usijione kwa sababu unafahamiana na Mshauri Mkuu unaweza kudharau jeshi,” alisema Afande Mwiba huku uso wake ukiwa na hasira mbele ya Hamza.

Wakati huo, geti la kuingia ndani ya gati ya kijeshi lilifunguliwa, na taarifa ya boti kuwa tayari ilitolewa. Hamza hakutaka kupoteza muda; aliongoza njia ili awahi, lakini Afande Mwiba na Afande Barafu walimzuia mbele yake.

“Wewe ni raia tu, huruhusiwi kutufuata kwenye hii misheni. Hatuendi kucheza,” alisema Afande Mwiba akiwa siriasi.

Hamza alijiambia kama sio heshima kwa Afande Himidu, muda huu huyu bwana angekuwa anaugulia maumivu.

“Relax, bro, sihitaji ulinzi wako. Mwili wa baba mkwe wangu upo kwenye mikono ya watekaji, na kwa namna yoyote natakiwa kuurudisha kwa ajili ya kuzikwa,” alisema Hamza, akijiambia angalau Regina apate nafasi ya kumzika baba yake.

“Tuwie radhi, Mr. Hamza. Hili lishakuwa chini ya jeshi tayari, na sio swala binafsi. Hatuwezi kukuruhusu kuongozana na sisi na chochote kikikutokea tukose namna ya kujibu mbele ya Mshauri Mkuu,” alisema Afande Barafu kwa upole.

Ukweli ni kwamba Afande Himidu licha ya kutoa maagizo ya kesi zote zinazomhusu Hamza kufungwa, hakuelezea sababu ni nini zaidi ya agizo la moja kwa moja. Hivyo, Kanali Mwiba na Afande Barafu hawakumchukulia siriasi, walimuona ni mtu wa kawaida tu ambaye hana mafunzo ya kijeshi.

Hamza aliishia kushusha pumzi na hakutaka kuendelea kuelezea zaidi, bali alipiga hatua kuelekea upande wa boti iliko.

“Simama wewe, hujasikia nilichokuwa nikisema?” Aliongea Afande Mwiba kwa hasira mara baada ya kuona Hamza hakuwa na nia ya kumsikiliza onyo lake.

Baada ya kuona Hamza hataki kusimama, alimsogelea kwa kasi na kutaka kumshika kola ya shati. Lakini mkono wa kushoto wa Hamza ulikuwa na kasi mno kwani alimshika Afande Mwiba kiganja chake na kumwangalia kwa macho ya kutisha.

“Ukiendelea kunichelewesha, sitojali kukutupa baharini,” alisema Hamza kwa ukali.

Afande Mwiba hakujua amekamatwa vipi na Hamza. Kitendo kile kama mwanajeshi kilimfanya kuona ni dharau kiasi cha kuanza kupandwa na hasira.
“Kwa mafunzo yako kidogo, ndiyo maana unaleta kiburi mbele yangu, lakini nikuambie, sheria ni sheria. Hata kama unafahamiana na Mshauri Mkuu, haina maana mbele ya sheria. Kikosi changu kipo kwenye misheni, na mimi kama kamanda wa misheni hii nikitoa maagizo, unapaswa kutii,” alisema Afande Mwiba kwa ukali, na ghafla tu msisimko wa nguvu za nishati ya mbingu na ardhi ulianza kujikusanya kwenye mwili wake, misuli yake ikawa migumu kama jiwe.

“Usipoachia kiganja changu, nitauvunja mkono wako kwa shambulizi linalokuja,” aliongea Afande Mwiba kwa sauti kali.

“Kwa uwezo wako mdogo huu, unadhani utaweza hata kunigusa?” Hamza alijibu, huku akiwa hajabadilika muonekano wake hata kidogo.

“Nadhani hujui hata unaongea na nani sasa hivi. Acha kunilazimisha kuwa siriasi, utaumia,” alisema Afande Mwiba, lakini Hamza aliishia kumwangalia kwa kejeli, akijiambia kuwa Mwiba ndiye hajui nani anashindana naye.

“Kanali, achana naye. Kwa ajili ya Mshauri Mkuu, ngoja afanye anavyotaka. Isitoshe, kwa wingi wetu, kundi la nafsi zinazotangatanga hawawezi kuwa tishio,” alisema Afande Barafu, au Kanali Caroline kwa jina lake la kawaida.

Kanali Mwiba alisita kidogo, lakini baada ya kumfikiria Afande Himidu, alijizuia na kuachana na Hamza.

“Ukija kutumbukia baharini, usije kunililia kuomba msaada maana sitokusaidia,” alisema kwa kejeli, na baada ya kauli hiyo alikimbilia kuelekea boti.

“Twendeni. Norbert, wasiliana na Afande Kwavava aendelee kufuatilia baharini kama kuna boti yoyote ya kutilia mashaka,” alisema Afande Caro huku akipiga hatua kusogelea Speedboat.

“Sawa, Afande!” alijibu Afande Norbert kwa saluti na wakati huo akitembea, alikuwa akifanya mawasiliano kwa simu ya upepo.

Hamza, mara baada ya kuingia ndani ya boti, aliishia kuangalia wanajeshi hao walivyokuwa na majigambo, na mdomo wake ulicheza kwa kejeli.

Ilikuwa ni sawa kwao kujisikia wapo juu, kwani wanajeshi wote ambao walikuwa chini ya Kitengo cha Malibu ndio waliaminika kuwa na uwezo wa juu sana kati ya wanajeshi wote. Hii ni kutokana na kwamba mafunzo yao hayakuwa ya kawaida tu; yalichanganya na mafunzo ya nguvu za ziada kama vile kuvuna nishati za mbingu na ardhi.

Hamza, hata hivyo, mpango wake haukuwa kujipatia umaarufu kutoka kwao. Alichokuwa akihitaji kufanikisha kwa muda huo ni kupata mwili wa baba yake Regina na kisha awaue wahusika wote waliotekeleza kifo chake.

Mara baada ya wote kupanda ndani ya boti hiyo ya mwendokasi, iliwashwa na kuanza kushika kasi kuelekea katikati ya bahari ikifukuzia watekaji.

Ilikuwa ni boti ya kijeshi, hivyo ilikuwa na mafuta ya kutosha, lakini vilevile ilikuwa na ya ziada, na sio hivyo tu, kulikuwa na vifaa vya kujiokolea ikitokea dharura.

Hazikupita hata dakika kumi baada ya kutoka katika gati hiyo ya kambi ya jeshi, waliweza kupokea taarifa kutoka kwa Afande Kwavava na kuambiwa kuna boti ya uvuvi inayokimbia kwa kasi kuelekea maji ya kimataifa.

Baada ya taarifa hiyo, dereva wa boti hiyo aliongeza spidi mara mbili kwa ajili ya kuikamatia.

&&&&

Ndani ya boti ya uvuvi iliyokuwa ikitembea kwa spidi kubwa kuelekea katikati ya maji ya kimataifa, Mzee Benjamini, James, na Lamla walikuwa hawatulii kama vile wamekalia kaa la moto.

“Mzee Tui, watu wa Kitengo cha Malibu ni wa aina gani? Ni wanajeshi au polisi?” aliuliza James.

“Kama ni jeshi la kawaida ama polisi, nisingekuwa na wasiwasi namna yote hii. Ukisikia Malibu ni kitengo cha jeshi ambacho wanajeshi wake wana mafunzo si tu ya kupambana kwa silaha lakini pia ya kupambana na nguvu za giza. Mwanzo walikuwa wakikiita Kitengo cha Wachawi ila walikipa jina la Malibu kama heshima kwa Afande Malibu, mmoja wa wanajeshi walioweka historia katika kitengo hicho,” aliongea Mzee Tui, ambaye alikuwa na taarifa zote maana hata yeye alikuwa mmoja wa wanajeshi wa kikosi hicho.

“Kumbe ni hatari hivyo? Isije wakaja na meli za kivita tu?” James aliuliza kwa wasiwasi.

“Hilo haliwezekani, isitoshe tupo kwenye boti ya uvuvi tu,” alijibu Mzee Tui.

“Tui, kama tukishafika katika maji ya kimataifa kwa spidi hii, si inamaanisha mipango yetu yote imefeli, maana itakuwa ngumu kwa sisi kurudi Dar tena?” James aliuliza kwa hofu.

“Kufeli!? Mmepoteza nyie. Hamkujua mipaka yenu. Zidi ya mateka ndiyo maana akajiua. Isije mkawa na mawazo ya kwamba mimi ndiye nimesababisha hii misheni kufeli?” Mzee Tui alijibu kwa hasira.

“Wewe! Kwa hiyo unasema sisi ndiyo tumeifelisha? Yaani tumekubali kukulipa zaidi ya bilioni ishirini za Kitanzania, halafu kazi unataka kufanya nusu nusu?” Lamla aliongea kwa hasira.

“Kazi yenu imekamilika nusu na malipo mlionipatia ni nusu yake. Sidhani mpaka hapa tunadaiana,” aliongea Mzee Tui, na kauli yake iliwafanya Benjamini na wenzake kukamaa miili.

“Mpaka sasa nimepoteza vijana wangu wengi katika hii misheni, na inanifanya nione hata kiasi mlichonipatia ni kidogo kwa ajili ya kulipa fidia kwa familia zao. Hivyo kama msipomalizia kiasi kilichobakia, msije ongea chochote kuhusu kuendelea kuwafanyia kazi na pia kuhusu usalama wenu mtajua wenyewe,” alisema kwa msisitizo.

“Mzee Tui, unamaanisha nini? Kwa hiyo unapanga kutuacha katikati ya bahari wenyewe? Hivi ndiyo mnavyotimiza masharti ya mkataba?” aliuliza Mzee Benjamini kwa hasira.

“Kaa kimya. Kwanza kabisa, tushatimiza kazi yetu yote kulingana na makubaliano. Lakini kutokana na ujinga wenu mmefanya hii misheni kuvurugika. Pili, mpaka sasa hamna uwezo wa kutulipa kiasi kilichobakia na bado mnataka vijana wangu waendelee kuwafanyia kazi. Hamuoni mnakuwa wajinga?” Mzee Tui alijibu kwa ukali.

Benjamini na James walijikuta wakikosa maneno. Walikuwa na wasiwasi na woga mno na hawakuweza kujizuia kumtolea macho Lamla. Walikuwa wakimlaumu kwa kumpandisha munkari Mzee Wilsoni mpaka akachukua maamuzi ya kujimaliza.

“Mnaniangalia nini sasa wakati mlikuwa mkifurahia kumuona Wilsoni anateseka?” alisema Lamla.

“Yaani bado tu unapata ujasiri wa kuongea hivyo. Kama sio uwezo wako mdogo wa kushindwa kumdanganya Bi Mirum, unadhani tungefikia katika hii hali?” aliuliza Mzee Benjamini kwa hasira, lakini hata hivyo walikatishwa malumbano yao na watu waliosogea upande huo.
"Bosi, tumeweza kufanikiwa kufanya mazungumzo na The Shark na tutaweza kukutana nao upande mwingine," alisema mmoja wa vijana wa Mzee Tui.

"Vizuri sana. Endeleeni kuendesha kwa spidi yote. Tukifanikiwa kukutana na The Shark mbeleni, wanajeshi wa Malibu hawawezi kutukamata tena," aliongea Mzee Tui.

"Mzee Tui, The Shark ndio watu gani?" aliuliza James.

"Ni maharamia wa baharini. Kapteni Kenny ni rafiki yangu kwa miaka mingi. The Shark wanafanya shughuli zao katika ukanda wa Bahari ya Afrika Mashariki na Kati na ndio maharamia pekee wanaopatikana kwenye ukanda huu. Kwa msaada wao, Malibu hawawezi kutushambulia tukiwa kwenye maji ya kimataifa maana kuwashambulia The Shark ni kuchokozana na Al-Shabab."

"Hivi kumbe kuna maharamia wa baharini siku hizi?"

"Ndio maana meli nyingi za mizigo zinasafiri na wanajeshi, lakini hata hivyo maharamia hawa wa siku hizi ni tofauti. Mara nyingi hawaibi meli ila wanajihusisha na Black Market, ndio maana nchi hazitilii sana mkazo kuwaondoa," aliongea.

Black Market ni soko la ulimwengu wa giza au underworld market, soko ambalo kila kitu ambacho kinaonekana kuwa haramu au kuvunja sheria kinauzwa. The Shark licha ya kuitwa maharamia, hawakuwa majambazi kamili. Walikuwa ni wafanyabiashara wa bidhaa za kimagendo na haramu ikiwemo madawa ya kulevya na bidhaa zingine. Moja ya sababu kubwa ya The Shark kuogopeka ni kutokana na ushirika wake mkubwa wa kibiashara na makundi ya kigaidi ikiwemo Al-Shabab.

Wakati wakiendelea na maongezi, hatimaye waliweza kuona meli kubwa ya mizigo iliyoizungukwa na boti ndogo ndogo za kivita zilizokuwa na mikonga mikubwa ya mtutu wa kurusha mabomu.

"Ile ndio meli ya maharamia, mbona ni kama meli ya jeshi la nchi?" aliuliza Mzee Benjamini akionyesha mshangao.

Hakutaka kuamini kwamba meli kubwa ile na pia boti za kivita zinazoizunguka ni za maharamia. Mzee huyo kila alipokuwa akisikia neno haramia, alijua ni watu walioamua kuwa majambazi, ambao wanaiba kwa ajili ya kupeleka mkono kinywani.

"Vitu kama hivyo wanatoa kwa Shardbearer’s ambao wanakuwa kama madalali wa vifaa vya kivita vilivyoisha muda wake na taasisi za giza. Unadhani ni kwanini majeshi mengi yanawaogopa?" aliongea Tui.

Dakika chache mara baada ya boti yao kuvuka mpaka wa Tanzania na maji ya kimataifa, hatimaye waliweza kushuhudia bendera juu ya meli ile iliyokuwa na chata kubwa la samaki aina ya papa.

Eneo la deki ya meli hiyo, walionekana watu mbalimbali, weusi na weupe, waliokuwa wamesimama. Walikuwa na mwonekano wa kichafu na kwa jinsi walivyoacha ndevu ni kama hawakutaka sura zao kuonekana.
 
SEHEMU YA 88.

“Hey Rafiki yangu Tui, kwannini unaonekana kama kituko?”Aliongea mwanaume wa kirusi aliekuwa na mindevu mingi huku akiwa ameshikilia kiko, kichwani akiwa amevaa kofia ya kijeshi iliochakaa na kuchanika.

“Kenny naomba nikusumbue awamu hii , kwasababu ya hawa wapuuzi watatu misheni niliokuwa nikifanyia kazi Tanzania imevurugika”Aliongea Tui kwa kingereza safi.

“Hahaha..come up!, it wasn’t first time anyway”Aliongea kwa kinegereza akimwambia apande juu maana hata hivyo sio mara yake ya kwanza kuomba msaada.

“Ila usisahau ukiingia Mombasa kututafutia wanawake warembo”Aliendelea kuongea na muda ule aliwapa ishara vijana wake kuweka ngazi ili Tui na watu wake wapande juu ya meli.

“Tui hawa watu ulioambatana nao ni sehemu ya watu wako?”Aliuliza.

“Hapana , hawa ndio walikuwa mabosi wangu kwenye misheni niliokuwa nikifanya lakini wamefanya makosa na kuharibu kila kitu , bado hawajanilipa hela iliobakia”

“Kumbe, kama ni hivyo sidhani kama kuna haja ya kujipa mzigo wa kuwachukua”Aliongea Kenny.

“Kapteni Kenny tafadhari naomba usituache hapa , familia yetu bado ina hela na tukishafika eneo salama tutakulipa”Aliongea Mzee Benjamini.

“Kama mna hela zpo wapi , sisi ni maharamia na hakuna mmoja wetu mwenye akaunti benki , malipo sisi tunapokea cash mkononi , kama sio hela tunapokea madini au vito ..”Aliongea Kenny huku akikunja sura na kuvuta moshi wa sigara kwenye kiko chake.

“Nina hii saa ya Patek Phillippe , thamani yake ni Dollar milioni mbili”Aliongea Mzee Benjamini na haraka haraka alivua ile saa na Kenny aliinyakua kutoka kwenye mikonoo yake haraka na kuwarushia watu wake.

“Hio saa haina thamanni kubwa hata kama nikiiuza , labda kama unataka kubakia wewe peke yako kwenye hii meli” Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Mzee Benjamini kumwangalia Mzee Tui kwa macho ya kuomba.

“Mzee Tui naomba utusaidie , kama tukirudi na hii boti ya uvuvi ni dhahiri kabisa tutakamatwa na jeshi la Tanzania”Aliongea Mzee Benjamini kwa sauti ya kubembeleza.

Walikuwa wakijua kama Hamza alikuwa na uwezo wa kuwasiliana na jeshi basi kama wakikamatwa Hamza hatowaacha salama.

Isitoshe walishakwisha kumuua Mzee Wilsoni hivyo kinachokwenda kutokea ni kulipiziwa kisasi.

“Mnisamehe lakini sitaki kufanya mambo kuwa magumu kwa Kapteni Kenny , vinginevyo ni kutoa tu bilioni kumi zilizobakia”Aliongea Tui akiwakataa wenzake.

Muda huo Kenny macho yake yalitua kwenye mwili wa Lamla na tabasamu la uovu lilipamba sura yake.

Lmla alikuwa amevalia suruali hivyo ya jeansi na kufanya umbo lake kujichora vizuri.

Ijapokuwa alikuwa ashaanza kuzeeka lakini alikuwa mwanamke anaeishi katika mazingira ya kitajiri hivyo muonekano wake ulikuwa ukivutia.

“Huyo mwanamke naona sio mbaya sana , kwanza vijana wangu wamechoka kutumia wanawake ambao tupo nao ndani ya meli kwa mwezi mzima na tulikuwa na mpango wa kwenda kununua wengine Somalia …”Aliongea huku akichezea uchebe.

Lamla mara baada ya kusikia kauli hio vigoti vya miguu vlianza kumlgea na kujikuta akitetemeka.

“Hapana… mimi sio aina ya wanawake wanaojiuza..”Aliongea akijitetea,alikuwa katika kiwango cha juu mno cha woga na alijificha nyuma ya Mzee Benjamini.

“Benja naogopa , usiwahurusu kunifanyia kitu kibaya”Aliongea lakini muda uleule James na baba yake waliangaliana kwa ishara.

“Hebu sogea mbele huko”Aliongea Mzee Benjamini huku akimsukumia Lamla mbele yake na kumfanya adondoke chini.

“Kapteni Kenny tutakuuzia huyu mwanamke , tafadhari naomba mimi na mtoto wangu utufikishe afukweni salama”Aliongea Mzee Benjamini.

Mzee Bejamini na mwanae walikuwa na kiasi cha pesa nje ya nchi lakini vilevile walikuwa na ushirikiano na Mstaafu Mgweno hivyo waliamini kama watafika nchi kavu watakuwa na kiasi cha kutosha cha kuanzia upya, hivyo kumuuza Lamla haikuwa hasara..

Kitendo cha Kumsikia mpenzi wake Benja akimuuza kwa hao maharamia uso wake ulipauka dakika ilele.

“Benja wewe ni mnyama , yaani nimeshirikiana na wewe kwa zaidi ya miaka kumi tena nikakuzalia mtoto wa kiume halafu unanifanyia hivi?”

Ulimwengu wake wote ulikumbwa na giza ghafla tu na alijihisi alikuwa akitumbukia shimoni.

Mzee Benjamini aliishia kuweka mikono yake kwenye bega la james huku akimwangalia Lamla kwa kejeli.

“Mtoto wangu wa kiume ninaemtambua ni James pekee , Frank uliemzaa ni mjinga zaidi ya ujinga na pengine ashaingia kwenye maswala ya upinde”Aliongea.

“Mshenzi mkubwa wewe , hivi nyie wanaume kwanini mnakuwa kama mbwa?”Aliongea kwa kulaani huku akianza kulia lakini Mzee Benjamini hakujali kilio chake.

“Kapteni Kenny tafadhari tunaomba utufikishe nchi kavu”Aliongea.

“Hahaha...napenda watu wa aina yako ambao hamjali ni mbinu gani mnatumia kujilinda , haha wewe ni mkatili sana , safii”Alongea Kenny na kisha aliwageukia vijana wake.

“Mnasubiri nini, mpelekeni ndani akaonje joto la Papa”

Mara baada ya kuongea kauli hio maharamia wale kwa furaha kubwa walimkamata kwa nguvu Lamla na kisha kuingia nae kwenye Cabin.

Lamla alijifanyisha kutaka kuleta ushindani lakini alipokea vibao vya nguvu vilivyomfanya kushikwa na ukichaa huku macho yake yakiwa meupe kama mtu aliekosa tumaini tena.

Mzee Benjamini na James walijikuta wakifuta jasho la paji la uso mara baada ya kuponea chupu chupu , lakini sasa dakika hio hio boti ya jeshi la Tanzania iliweza kuonekana katika macho yao.

“Kenny wanajeshi wa Tanzania wale wanakuja?”Aliongea Mzee Tui na mara baada ya kuangalia alijikuta akitoa kicheko cha kejeli.

“Kwa walivyo wachache vile watatufanya nini , wakithubutu kutufukuzia kwenye maji ya kimataifa tutawalipua na kuwa chakula cha samaki”Aliongea kwa kujiamini huku akiwapa ishara vijana wake kuondoka eneo hilo.

Upande wa kikosi cha Malibu walijikuta wakikunja sura mara baada ya kuona meli za maharamia.

“ Ni The Shark wale ,Simamisha boti , haina haja ya kuendelea kuwafukuzia”Aliongea Afande Caro lakini kauli yake ilimfanya Hamza kushangaa , mpango wake haukuwa ni kuishia hapo.

“Yaani wahalifu wapo mbele yetu , mnataka tusimamishe na kurudi , mnaogopa nini?”Alongea

“Kama umekuja kwa ajili ya kuchukua maiti ya baba mkwe wako itakuwa kwenye ile boti ya uvuvi , haina haja ya kuwafukuzia wakiwa kwenye maji ya kimataifa”Aliongea Afande Caro

“Ni kakundi kadogo tu ka maharamia , mnachotakiwa ni kushirikiana na mimi na hakuna kitakachotokea”Aliongea Hamza.

“Wewe mjinga hebu kaa kimya , unafikiri Kapteni Kenny wwa The Shark ni mwanajeshi wa kawaida , ana mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na anakaribia levo ya Nafsi na pia ana watu zaidi ya mia wanaomzunguka, unadhani tutashindana nae vipi?”

Hamza mara baada ya kuona meli le inaanza kuondoka , hakutaka kupoteza muda tena na Afande Mwiba.

“Kama hamtaki kushirikiana na mimi bas bakieni kwenye boti na nitadili na hili swala mwenyewe”Aliongea Hamza.

“Unajifanya wewe ndio Mshauri mkuu , utaweza kufanya nini bila msaada wetu?”

“Msiwe na waswasi na mimi , punguzeni mwendo maana mkisogea karibu watawashambulia”Aliongea Hamza na baada ya hapo alirudi nyuma kwenye ukingo wa boti na kuvuta pumzi nyingi na muda uleule nywele zake zilisimama, akiwa amevuta nguvu zake zote alifyatuka mbio kama mwanariadha na mguu wake wa mshio kukanyaga boti aliisababishia kuyumba kiasi cha kutaka kuzama lakini kilichotokea baada ya hapo wanajeshi wote walitoa macho kama wamebanwa na mlango.

Hamza alikuwa ni kama kombolra lilivyofyatuliwa na sasa linaelekea kushambulia shabaha. Spidi yake iliwafanya wanajeshi wa kitengo cha Malibu kuishia kuona kivuli tu kikipotea kwenye macho yao.

Hamza alienda kutua kwenye boti ile ya uvuvi na nguvu aliotua nayo ilifanya na yenyewe izame eneo la mbele.

Hakuna alieweza kuamini , umbali kutoka walipokuwa na boti ile ni kama mita miasaba hivi au zaidi lakini Hamza alifanikiwa kuruka na kuifikia.

“Haiwezekani ni mbingu gani katumia kuruka umbali ule?”

Kapteni Norbert na wenzake macho yaliwatoka wakati wakiangalia tukio hilo likitokea .

“Hii haiwezi kuwa mbinu ya kuvuna nishati , hakuna msisimko wa kinishati unaomtoka?”

“Haiwezekani isiwe mbinu ya kuvuna nishati , unataka kusema ametegemea nguvu ya miguu yake pekee kuruka mita zote hizo?”Walijikuta wakibishana wao kwa wao.

Afande Mwiba na Kanali Caro wenyewe hawakuamini , sio kwamba hawakuwa na uwezo wa kuruka , kwa kutegemea nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kwa levo waliofikia uwezo huo wanao lakini kuruka kwao hakuwezi kuwa umbali mrefu kwasababu bado hawajabobea kwenye mbinu ya Floating water

Kuruka ukiwa kwenye ardhi ni tofauti na kuruka ukiwa kwenye bahari , mbinu ya nishati mara nyingi inategemea ardhi na mbingu na sio mbingu na maji na ili uweze kuruka umbali mrefu kwenye maji unatakiwa ujifunze pia mbinu nyingine ya kuvuna nishati kati ya mbingu(anga) na Maji(bahari). Ukifanikiwa katika hio mbinu utakuwa na uwezo wa kutembea juu ya maji bila kutumbukia na mbinu hio ndio huitwa Floating water movement.

Sasa kwa watu kama Afande Mwiba hawakuwahi kuona mtu akiruka kama kichaa na kuweza kufanikiwa kufikia umbali uliokusudiwa kama huo.

“Huyu Hamza inamaana miguu yake imefungwa injini za roketi , amewezaje kuruka umbali wote ule?”Walishangaa maana kila kitu kilikuwa kikienda kinyume na kile ambacho wamejifunza.

“Hata hivyo kama kitu kibaya kikimkuta ni dhahiri lawama zote tutabebeshwa , tunapaswa kusogea mbele angalau kumlinda”Aliongea Afande Caro au Kanali Barafu.

“Acha ujinga , unataka kututafutia matatizo, ndio maana nilikuwa nikipinga kuja na sisi”Aliongea Afande Mwiba kwa hasira.

Kilichowapa wasiwasi ni kwamba hata kama Hamza ameonyesha uwezo wa kuruka ubali wote huo , bado hakuwa ametumia mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , hivyo kwa macho yao bado ni wa kawaida.

Licha ya Afande Mwiba kupinga lakini wanajeshi walikuwa wakipokea zaidi maagzo kutoka kwa Afande Caro ambae ni senior , hivyo boti yao ilianza kuongeza mwendo.

Upande mwingine Kenny na Mzee Tui na wengine walijikuta wakishangaa , mwanzoni walidhania wanajeshi wa Malibu wataacha kuwafukuzia kwasababu walikuwa na uwezo wa kuwazamisha katka maji ya kimataifa bila kubeba lawama.

Dakika hio hio wakati macho yao yakiwa makini na boti ya wanajeshi ghafla tu kitu kilishuka kutoka juu angani na kutua kama bomu juu ya meli yao.

Alikuwa ni Hamza ambae alitua kama vile ni Batman na baada ya kusimama vizuri alianza kuwaangalia mmoja baada ya mwingine

Macho yake na nywele zake zilizokuwa zikichemka iliwafanya watu wote kuanza kuingiwa na hofu maana ni kama walikuwa wakiangaliana na jini Medusa.

“Mlidhani mnaweza kunikimbia mara baada ya kusababisha matatizo , kama ningejua ningewamaliza muda mrefu tu”Aliongea Hamza huku akimwangalia Benjamini na James.

Mzee Benjamini na mwanae walikuwa wameshikwa na woga kiasi cha kutaka kujikojolea na haraka walienda kujificha nyuma ya Mzee Tui na Kapteni Kenny.

“Wewe sio mtu ni jini?”Aliongea James huku akijiambia alikuwa akiwaza nini kupambana na mtu wa aina hio.

“Mzee Kenny tumelipia kwa ajili ya kuwa ndani ya hi meli , usije ukaacha tuchukuliwe” Aliongea Mzee Benjamini

“Jukumu langu lilikuwa ni kuwapeleka nchi kavu lakini sikuahidi kama nitawalinda , huyu mwanajeshi wa Malibu anaonekana kuwa na uwezo mkubwa mno na hatutaki uadui nae bila sababu”Aliongea Kenny.

“Huyu sio mwanajeshi wa Malibu ni msaidizi wa mkurugenzi ndani ya kampuni ya Dosam”Aliongea James.

“Kumbe!, lakini bado swala hili halituhusu”Alongea huku akitingisha mabega,

Benjamini na mwanae walijikuta wakipauka mno , mwisho wa siku kundi hilo lilitaka kuwatelekeza tena.

Mzee Tui alihisia kabisa uwezo wa Hamza ni ngumu kuutabiria na alijikuta akiwa makini kutojiingiza kwenye matatizo zaidi.

“Hamza hakika wewe sio mpiganaji wa kawaida , kwa namna ulivyoruka umetufumbua macho ya tusivyokuwa tukijua , kama unataka kumchukua Benjamini na mwanae sisi hatutokuzuia maana ushirikiano wetu umekwisha kumalizika”Aliongea.

Hamza alimwangalia Mzee Tui na kisha kundi lake lote la nafsi zinazotangatanga.

“Umenielewa vibaya kuja kwangu hapa sio kwa ajili ya kukamata mtu”

“Sio kukamata?!!”Walijikuta wakishangaa wote wasijue Hamza anadhamiria kufanya nini.

“Sio familia ya Benjamini pekee iliosababisha kifo cha baba mkwe wangu, bali ni kundi lote la Wandering souls , lakini mpo wengi sana kitu ambacho kitakuwa kigumu kuwakamata wote na kuwarudisha Tanzania, hivyo ni bora niwapunguze kwa kuwaua hapa hapa”Aliongea Hamza na kufanya kila mtu juu ya boti hio kuwa kimya na mwonekano wa Mzee Tui ulibadlika.

“Hamza unaweza ukawa hujui , Kapteni Kenny ni rafiki yangu , hata kama una uwezo mkubwa sidhani kama utafanikwa kutushinda wote tukiunganisha nguvu”Aliongea na Hamza aligeuza macho yake kwa Kenny.

“Vipi mkuu unataka kuwasaidia?”Aliuliza Hamza na swali lake lilimfanya Kenny kucheka.

“Kama unataka kumuua rafiki yangu katika meli yangu , nini kitatokea juu ya taswira yetu tulioijenga kwa miaka mingi?, ngoja nikushauri kwa umri wako huo nakusifia kwa levo uliofikia lakini kama unataka kufikia juu zaidi ni bora ukaacha hili lipite , nipo tayari hata kukuruhusu kutumia meli yetu”Aliongea

“Nimeuliza swali moja unatoa majibu mengi , ushauri wako unanihusu nini?”Aliongea Hamza.

“Kijana unakwenda kulipa kwa maneno yako ya kiburi”Aliongea Kenny huku macho yake yakichanua.

Wakati huo wanajeshi waliokuwa kwenye Boti ya Mwendokasi walikuwa washaifikia meli hio na wamesimama pembeni yake.

Muda uleule Kanali Mwiba na Kanali Barafu walitumia mbnu za nishati na kuruka kwenda kutua juu ya deki ya meli hio.

“Hamza unataka kufanya nini?”Aliongea Afande Mwiba huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi na shauku.

“Hili eneo ni maji ya kimataifa na mnenifuata na kuvamia meli yangu , hii ni dharau kwangu mimi kama Kenny”Aliongea

“Kapteni Kenny hatuna nia ya kupigana na kundi lako la The Sharks , tupo hapa kwa ajili ya kumkamata Benjamini na mtoto wake , wamekiuka sheria na wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria za Tanzania”

“Kama ni hivyo hakuna shida , hatuna ugomvi na Malibu kwa muda mrefu , hivyo wachukueni na mumchukue na huyu kijana wenu”Aliongea.

“Hamza, Shuka juu ya meli , kwani hujaridhika na kukamatwa kwa Benjaini na mtoto wake na kuuchukua mwili wa baba mkwe wako?”Aliongea Afande Caro.

“Nitaridhika kama nikiona kundi lote la Nafsi zinazotangatanga wamekufa”Aliongea

“Hamza una kiburi kilichopitiliza , hata kama wanajeshi wa Malibu wakiungana na wewe , huwezi kutushinda mimi na Bro Kenny”Aliongea Mzee Tui.

Hamza hakujibu badala yake aliinua kidole chake na kunyooshea bendera yao iliokuwa ikipepea.

“Juu kabisa ya bendera yenu katika kichwa cha Shark mmeweka nembo ya Giant rifle , maana yake mpo chini ya OCN-DMONS , si ndio?”Aliuliza Hamza.

Baada ya swali hilo muonekano wa Kapteni Kenny ulibadilika palepale na kuonyesha mshangao kidogo.

“Kijana unaonekana kuwa na macho ya ki uchunguzi , hata wanajeshi wa Malibu wameshindwa kugundua ulichoona wewe”Aliongea na kauli yake ilimfanya Afande Mwiba na Afande Barafu kushangaa baada ya kusikia kauli hio.

Hawakuweka umakini kwenye bendera mwanzoni na mara baada ya kuangalia waliweza kuona kitu.

“Nyie mna ushirikiano na Sea Demons?”Aliuliza Kamanda Mwiba kwa mshangao.

“Upo sahihi , sasa hivi tupo chini ya Mkuu Vithn wa kundi la Sea Demons , mko slow mno kwa kitengo kikubwa cha Malibu kutogundua hili kwa muda mrefu”Aliongea Kapteni Kenny.

“Kamanda Mwiba na Caro nyuso zao zilijikunja na watu waliokuwa nyuma yao walionekana kutoelewa kinachoendelea.

“Kapteni wanamaanisha nini kuhusu Seas Demons?”Aliuliza Afande Gamale swali akilielekezea kwa Kapteni Norbert.

“Ktu chepesi hicho hujui , iko hivi duniani kuna umoja wa makundi mawali makubwa ya kiharamia ambayo ni Ice Sea whale hunters na kundi lingine la kitajiri maarufu kama Sea Demons , makundi haya yote ni daraja A katika ulimwengu wa giza , Haramia mkuu wa kundi la Sea Demons anatambulika kama Leviathan au maarufu kama Sea Monster , sasa haya makundi yote mawili yana ushirikiano na kampuni kubwa tatu za kimataifa za kuuza siraha kimagendo na kati ya moja ya kampuni hizo inaongozwa na jamaa maarufu wa ulimwengu wa giza anaefahamika kwa jina la Greed Mamen au Big mmiliki mkubwa wa meli kumi za kusafirisha siraha pamoja na manowari , vinginevyo unadhani kwanini makundi makubwa kama hayo yanaitwa daraja la kwanza maana yake ni kwamba wameunda makundi madogo madogo ya kiharamia ikiwemo The Sharks kwa ajili ya kurahisisha biashara zao , kwa kipindi kirefu hawa The Sharks ndio waingizaji wakubwa wa siraha kwa kundi la kigaidi la Al-shabab na baadhi ya makundi ya wapiganaji upande wa Congo, sasa ili kutambua haya makundi nani yupo chini yao unaangalia nembo kwenye bendera yao ukiona ni Giant Rifle maana yake wapo chini ya Sea Demons

Afande Mwiba na Afande Barafu walikuwa wakijua kuhusu maharamia wa bahari wa daraja la kwanza na kutokana na hali ilivyo waliona hawapasi kuwachokoza The Sharks.

Ukweli ni kwamba dunia ya kawaida inaweza iyachukulie makundi haya kama ya kihalifu lakini uwepo wake umeidhinishwa na serikali kubwa duniani na yote hayo ni kwa ajili ya kurahisisha biashara za siraha katika maeneo yote ya dunia bila kujali wanaemuuzia ni Gaidi ama ni nchi.

“Hili lishakuwa tatizo tayari”Aliongea Hamza huku akikuna kichwa chake.

“Ni vizuri ushajua , hivyo acha kujitafutia matatizo na mchukue Benjamini na mtoto wake na sisi tutaondoka”

“Mtaondoka , kuondoka kwenda wapi?”Aliuliza Hamza

“Hamza acha ujinga , unataka kujiingiza kwenye matatizo kwa jambo dogo kama hili , hivi unajua uwezo wa Leviathan , hata kama Mshauri mkuu angekuwa hapa asingekubali kuendelea”Alongea Afande Caro lakini Hamza alimpotezea.

“Mkuu , hivi umesema unaitwa Kenny?”Aliongea Hamza akiwa na usra ya upole

“Ndio , ushawahi kunisikia popote?”

“Sijawahi kukusikia kabisa”

“Kama ni hivyo unataka nini?”

“Nataka kuua watu wa kundi la Nafsi zinazotanga tanga hivyo usiingilie”

“Haha… kijana nadhani kuna tatizo kwenye akili yako , hivi unajua unaongea na nani?”Aliongea Kenny na mara baada ya kupunga mkono wake wanajeshi wake wote walikoki bunduki zao kumnyooshea Hamza.

Ndani ya sekunde tu hali ya meli hio ilibadilika na kuwa yenye ukinzani mkubwa.

“Hamza , hebu acha basi , hakuna wa kukusaidia wakikushambulia”Aliongea Kanali Caro kwa hasira.

“Hamza nakushauri ufuate ushauri wa wanajeshi wa Malibu na kuondoka kimya kimya , hapa sio Tanzania ni maji ya kimataifa na hata tukikuua hatuwezi kulaumiwa kisheria “Aliongea Tui.

“Mkuu Kenny naona ni kama umedhamiria kulinda hili kundi ?”

“Kwahio vipi kama nimeamua , sogea uone usipogeuka kiota cha nyuki, kama sio kuiheshimu Tanzania ningeshakumaliza sasa hivi”Aliongea kwa hasira.

Kamanda Mwiba mara baada ya kuona hali inaelekea kubaya alisogea bele ya Hamza na kumshika tai.

“Hamza acha uwendawazimu, hebu tuondoke hapa”Aliongea lakini Hamza alirudia kumshika Kamanda Mwiba mkono wake kwa nguvu.

“Kama unataka kuondoka wewe ondoka mwenyewe acha kunizuia ninachotaka kufanya”

“Acha ujinga , hata Mshauri mkuu hawezi kukusaidia katika hili , ngoja nikushikishe adabu pengine akili itakukaa sawa”Aliongea na palepae alianza kukusanya nguvu ya ndani ya mwili wake na kuufanya mwili kutuna , vidole vitatu vya mkono wake wa kulia vilichomoza kucha na kutaka kumtoboa Hamza kwenye mkono.

Lakini sasa licha ya kutumia nguvu kubwa kutaka kumuathiri Hamza hakuna matokeo yoyote yaliotokea , kiufupi Hamza hakuathirika hata kidogo , ilikuwa ni kama mtoto anaejaribu kupambana na baba yake.

“Mnunurisho wa nguvu zako upo hatua ya kwanza kuingia levo ya anga katika mizunguko theratini na sita , kwa uwezo huu mdogo unapata wapi ujasiri wa kujileta mbele yangu kama kichaa?”Aliongea Hamza na palepale nguvu ya mwili wake ilibadilika na kuleta msisimko ambao ni kama eneo lote limefunkwa na nguvu za giza.

Kitendo kile kilimfanya Afande Mwiba kuwa kama amegandishwa , kama mwanajeshi mwenye nishati za mbingu na ardhi alijihis muda wowote atageuka kuwa barafu .

“Wewe… wewe.,.”Alijikuta akikosa neno la kuongea maana katika maisha yake hakuwahi kuhisi nguvu kubwa kiasi hicho.

Alichokifanya Hamza ni kumsukuma kwa nguvu Kamanda Mwiba na matokeo yake alikuwa ni kama kiroba cha Cement kilichochorushwa kutoka kwenye gari ya mizigo kwenda chini

“Chubwiiii…!!!”

Kamanda Mwiba alitumbukia baharini .

Wanajeshi wa kitengo cha Malibu walishishitushwa sana na jambo hilo , walitarajia Kamanda Mwiba kumdhibiti Hamza lakini matokeo yake alidhibitiwa yeye.

“Mwibaa.!!!”

Kamanda Caro alijikuta akipiga ukulele wa king’ora , hakupata hata muda wa kumsaidia kwani kila kitu kilitokea kwa ghafla sana .

“Mnaangalia nini rukeni mkamsaidie”Aliongea Afande Caro akiwapa maagizo Afande Norbert na wenzake.

Waliokuwa kwenye mshangao zaidi ni Kapteni Kenny na Mzee Tui na kundi lake

Hawakuelewa kwasababu wanajeshi wa kitengo cha Malibu walikuwa wakijaribu kumlinda Hamza lakini matokeo yake Hamza ndio anaewaadhibu.

Kubwa zaidi ni kwamba msisimko ambao Hamza alitoa ulifanya kila mmoja kujihisi mapigo yake ya moyo yakisimama.

What will happen?”

ITAAENDELEA.

WATSAPP ME 0687151346
 
SEHEMU YA 88.

“Hey Rafiki yangu Tui, kwannini unaonekana kama kituko?”Aliongea mwanaume wa kirusi aliekuwa na mindevu mingi huku akiwa ameshikilia kiko, kichwani akiwa amevaa kofia ya kijeshi iliochakaa na kuchanika.

“Kenny naomba nikusumbue awamu hii , kwasababu ya hawa wapuuzi watatu misheni niliokuwa nikifanyia kazi Tanzania imevurugika”Aliongea Tui kwa kingereza safi.

“Hahaha..come up!, it wasn’t first time anyway”Aliongea kwa kinegereza akimwambia apande juu maana hata hivyo sio mara yake ya kwanza kuomba msaada.

“Ila usisahau ukiingia Mombasa kututafutia wanawake warembo”Aliendelea kuongea na muda ule aliwapa ishara vijana wake kuweka ngazi ili Tui na watu wake wapande juu ya meli.

“Tui hawa watu ulioambatana nao ni sehemu ya watu wako?”Aliuliza.

“Hapana , hawa ndio walikuwa mabosi wangu kwenye misheni niliokuwa nikifanya lakini wamefanya makosa na kuharibu kila kitu , bado hawajanilipa hela iliobakia”

“Kumbe, kama ni hivyo sidhani kama kuna haja ya kujipa mzigo wa kuwachukua”Aliongea Kenny.

“Kapteni Kenny tafadhari naomba usituache hapa , familia yetu bado ina hela na tukishafika eneo salama tutakulipa”Aliongea Mzee Benjamini.

“Kama mna hela zpo wapi , sisi ni maharamia na hakuna mmoja wetu mwenye akaunti benki , malipo sisi tunapokea cash mkononi , kama sio hela tunapokea madini au vito ..”Aliongea Kenny huku akikunja sura na kuvuta moshi wa sigara kwenye kiko chake.

“Nina hii saa ya Patek Phillippe , thamani yake ni Dollar milioni mbili”Aliongea Mzee Benjamini na haraka haraka alivua ile saa na Kenny aliinyakua kutoka kwenye mikonoo yake haraka na kuwarushia watu wake.

“Hio saa haina thamanni kubwa hata kama nikiiuza , labda kama unataka kubakia wewe peke yako kwenye hii meli” Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Mzee Benjamini kumwangalia Mzee Tui kwa macho ya kuomba.

“Mzee Tui naomba utusaidie , kama tukirudi na hii boti ya uvuvi ni dhahiri kabisa tutakamatwa na jeshi la Tanzania”Aliongea Mzee Benjamini kwa sauti ya kubembeleza.

Walikuwa wakijua kama Hamza alikuwa na uwezo wa kuwasiliana na jeshi basi kama wakikamatwa Hamza hatowaacha salama.

Isitoshe walishakwisha kumuua Mzee Wilsoni hivyo kinachokwenda kutokea ni kulipiziwa kisasi.

“Mnisamehe lakini sitaki kufanya mambo kuwa magumu kwa Kapteni Kenny , vinginevyo ni kutoa tu bilioni kumi zilizobakia”Aliongea Tui akiwakataa wenzake.

Muda huo Kenny macho yake yalitua kwenye mwili wa Lamla na tabasamu la uovu lilipamba sura yake.

Lmla alikuwa amevalia suruali hivyo ya jeansi na kufanya umbo lake kujichora vizuri.

Ijapokuwa alikuwa ashaanza kuzeeka lakini alikuwa mwanamke anaeishi katika mazingira ya kitajiri hivyo muonekano wake ulikuwa ukivutia.

“Huyo mwanamke naona sio mbaya sana , kwanza vijana wangu wamechoka kutumia wanawake ambao tupo nao ndani ya meli kwa mwezi mzima na tulikuwa na mpango wa kwenda kununua wengine Somalia …”Aliongea huku akichezea uchebe.

Lamla mara baada ya kusikia kauli hio vigoti vya miguu vlianza kumlgea na kujikuta akitetemeka.

“Hapana… mimi sio aina ya wanawake wanaojiuza..”Aliongea akijitetea,alikuwa katika kiwango cha juu mno cha woga na alijificha nyuma ya Mzee Benjamini.

“Benja naogopa , usiwahurusu kunifanyia kitu kibaya”Aliongea lakini muda uleule James na baba yake waliangaliana kwa ishara.

“Hebu sogea mbele huko”Aliongea Mzee Benjamini huku akimsukumia Lamla mbele yake na kumfanya adondoke chini.

“Kapteni Kenny tutakuuzia huyu mwanamke , tafadhari naomba mimi na mtoto wangu utufikishe afukweni salama”Aliongea Mzee Benjamini.

Mzee Bejamini na mwanae walikuwa na kiasi cha pesa nje ya nchi lakini vilevile walikuwa na ushirikiano na Mstaafu Mgweno hivyo waliamini kama watafika nchi kavu watakuwa na kiasi cha kutosha cha kuanzia upya, hivyo kumuuza Lamla haikuwa hasara..

Kitendo cha Kumsikia mpenzi wake Benja akimuuza kwa hao maharamia uso wake ulipauka dakika ilele.

“Benja wewe ni mnyama , yaani nimeshirikiana na wewe kwa zaidi ya miaka kumi tena nikakuzalia mtoto wa kiume halafu unanifanyia hivi?”

Ulimwengu wake wote ulikumbwa na giza ghafla tu na alijihisi alikuwa akitumbukia shimoni.

Mzee Benjamini aliishia kuweka mikono yake kwenye bega la james huku akimwangalia Lamla kwa kejeli.

“Mtoto wangu wa kiume ninaemtambua ni James pekee , Frank uliemzaa ni mjinga zaidi ya ujinga na pengine ashaingia kwenye maswala ya upinde”Aliongea.

“Mshenzi mkubwa wewe , hivi nyie wanaume kwanini mnakuwa kama mbwa?”Aliongea kwa kulaani huku akianza kulia lakini Mzee Benjamini hakujali kilio chake.

“Kapteni Kenny tafadhari tunaomba utufikishe nchi kavu”Aliongea.

“Hahaha...napenda watu wa aina yako ambao hamjali ni mbinu gani mnatumia kujilinda , haha wewe ni mkatili sana , safii”Alongea Kenny na kisha aliwageukia vijana wake.

“Mnasubiri nini, mpelekeni ndani akaonje joto la Papa”

Mara baada ya kuongea kauli hio maharamia wale kwa furaha kubwa walimkamata kwa nguvu Lamla na kisha kuingia nae kwenye Cabin.

Lamla alijifanyisha kutaka kuleta ushindani lakini alipokea vibao vya nguvu vilivyomfanya kushikwa na ukichaa huku macho yake yakiwa meupe kama mtu aliekosa tumaini tena.

Mzee Benjamini na James walijikuta wakifuta jasho la paji la uso mara baada ya kuponea chupu chupu , lakini sasa dakika hio hio boti ya jeshi la Tanzania iliweza kuonekana katika macho yao.

“Kenny wanajeshi wa Tanzania wale wanakuja?”Aliongea Mzee Tui na mara baada ya kuangalia alijikuta akitoa kicheko cha kejeli.

“Kwa walivyo wachache vile watatufanya nini , wakithubutu kutufukuzia kwenye maji ya kimataifa tutawalipua na kuwa chakula cha samaki”Aliongea kwa kujiamini huku akiwapa ishara vijana wake kuondoka eneo hilo.

Upande wa kikosi cha Malibu walijikuta wakikunja sura mara baada ya kuona meli za maharamia.

“ Ni The Shark wale ,Simamisha boti , haina haja ya kuendelea kuwafukuzia”Aliongea Afande Caro lakini kauli yake ilimfanya Hamza kushangaa , mpango wake haukuwa ni kuishia hapo.

“Yaani wahalifu wapo mbele yetu , mnataka tusimamishe na kurudi , mnaogopa nini?”Alongea

“Kama umekuja kwa ajili ya kuchukua maiti ya baba mkwe wako itakuwa kwenye ile boti ya uvuvi , haina haja ya kuwafukuzia wakiwa kwenye maji ya kimataifa”Aliongea Afande Caro

“Ni kakundi kadogo tu ka maharamia , mnachotakiwa ni kushirikiana na mimi na hakuna kitakachotokea”Aliongea Hamza.

“Wewe mjinga hebu kaa kimya , unafikiri Kapteni Kenny wwa The Shark ni mwanajeshi wa kawaida , ana mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na anakaribia levo ya Nafsi na pia ana watu zaidi ya mia wanaomzunguka, unadhani tutashindana nae vipi?”

Hamza mara baada ya kuona meli le inaanza kuondoka , hakutaka kupoteza muda tena na Afande Mwiba.

“Kama hamtaki kushirikiana na mimi bas bakieni kwenye boti na nitadili na hili swala mwenyewe”Aliongea Hamza.

“Unajifanya wewe ndio Mshauri mkuu , utaweza kufanya nini bila msaada wetu?”

“Msiwe na waswasi na mimi , punguzeni mwendo maana mkisogea karibu watawashambulia”Aliongea Hamza na baada ya hapo alirudi nyuma kwenye ukingo wa boti na kuvuta pumzi nyingi na muda uleule nywele zake zilisimama, akiwa amevuta nguvu zake zote alifyatuka mbio kama mwanariadha na mguu wake wa mshio kukanyaga boti aliisababishia kuyumba kiasi cha kutaka kuzama lakini kilichotokea baada ya hapo wanajeshi wote walitoa macho kama wamebanwa na mlango.

Hamza alikuwa ni kama kombolra lilivyofyatuliwa na sasa linaelekea kushambulia shabaha. Spidi yake iliwafanya wanajeshi wa kitengo cha Malibu kuishia kuona kivuli tu kikipotea kwenye macho yao.

Hamza alienda kutua kwenye boti ile ya uvuvi na nguvu aliotua nayo ilifanya na yenyewe izame eneo la mbele.

Hakuna alieweza kuamini , umbali kutoka walipokuwa na boti ile ni kama mita miasaba hivi au zaidi lakini Hamza alifanikiwa kuruka na kuifikia.

“Haiwezekani ni mbingu gani katumia kuruka umbali ule?”

Kapteni Norbert na wenzake macho yaliwatoka wakati wakiangalia tukio hilo likitokea .

“Hii haiwezi kuwa mbinu ya kuvuna nishati , hakuna msisimko wa kinishati unaomtoka?”

“Haiwezekani isiwe mbinu ya kuvuna nishati , unataka kusema ametegemea nguvu ya miguu yake pekee kuruka mita zote hizo?”Walijikuta wakibishana wao kwa wao.

Afande Mwiba na Kanali Caro wenyewe hawakuamini , sio kwamba hawakuwa na uwezo wa kuruka , kwa kutegemea nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kwa levo waliofikia uwezo huo wanao lakini kuruka kwao hakuwezi kuwa umbali mrefu kwasababu bado hawajabobea kwenye mbinu ya Floating water

Kuruka ukiwa kwenye ardhi ni tofauti na kuruka ukiwa kwenye bahari , mbinu ya nishati mara nyingi inategemea ardhi na mbingu na sio mbingu na maji na ili uweze kuruka umbali mrefu kwenye maji unatakiwa ujifunze pia mbinu nyingine ya kuvuna nishati kati ya mbingu(anga) na Maji(bahari). Ukifanikiwa katika hio mbinu utakuwa na uwezo wa kutembea juu ya maji bila kutumbukia na mbinu hio ndio huitwa Floating water movement.

Sasa kwa watu kama Afande Mwiba hawakuwahi kuona mtu akiruka kama kichaa na kuweza kufanikiwa kufikia umbali uliokusudiwa kama huo.

“Huyu Hamza inamaana miguu yake imefungwa injini za roketi , amewezaje kuruka umbali wote ule?”Walishangaa maana kila kitu kilikuwa kikienda kinyume na kile ambacho wamejifunza.

“Hata hivyo kama kitu kibaya kikimkuta ni dhahiri lawama zote tutabebeshwa , tunapaswa kusogea mbele angalau kumlinda”Aliongea Afande Caro au Kanali Barafu.

“Acha ujinga , unataka kututafutia matatizo, ndio maana nilikuwa nikipinga kuja na sisi”Aliongea Afande Mwiba kwa hasira.

Kilichowapa wasiwasi ni kwamba hata kama Hamza ameonyesha uwezo wa kuruka ubali wote huo , bado hakuwa ametumia mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , hivyo kwa macho yao bado ni wa kawaida.

Licha ya Afande Mwiba kupinga lakini wanajeshi walikuwa wakipokea zaidi maagzo kutoka kwa Afande Caro ambae ni senior , hivyo boti yao ilianza kuongeza mwendo.

Upande mwingine Kenny na Mzee Tui na wengine walijikuta wakishangaa , mwanzoni walidhania wanajeshi wa Malibu wataacha kuwafukuzia kwasababu walikuwa na uwezo wa kuwazamisha katka maji ya kimataifa bila kubeba lawama.

Dakika hio hio wakati macho yao yakiwa makini na boti ya wanajeshi ghafla tu kitu kilishuka kutoka juu angani na kutua kama bomu juu ya meli yao.

Alikuwa ni Hamza ambae alitua kama vile ni Batman na baada ya kusimama vizuri alianza kuwaangalia mmoja baada ya mwingine

Macho yake na nywele zake zilizokuwa zikichemka iliwafanya watu wote kuanza kuingiwa na hofu maana ni kama walikuwa wakiangaliana na jini Medusa.

“Mlidhani mnaweza kunikimbia mara baada ya kusababisha matatizo , kama ningejua ningewamaliza muda mrefu tu”Aliongea Hamza huku akimwangalia Benjamini na James.

Mzee Benjamini na mwanae walikuwa wameshikwa na woga kiasi cha kutaka kujikojolea na haraka walienda kujificha nyuma ya Mzee Tui na Kapteni Kenny.

“Wewe sio mtu ni jini?”Aliongea James huku akijiambia alikuwa akiwaza nini kupambana na mtu wa aina hio.

“Mzee Kenny tumelipia kwa ajili ya kuwa ndani ya hi meli , usije ukaacha tuchukuliwe” Aliongea Mzee Benjamini

“Jukumu langu lilikuwa ni kuwapeleka nchi kavu lakini sikuahidi kama nitawalinda , huyu mwanajeshi wa Malibu anaonekana kuwa na uwezo mkubwa mno na hatutaki uadui nae bila sababu”Aliongea Kenny.

“Huyu sio mwanajeshi wa Malibu ni msaidizi wa mkurugenzi ndani ya kampuni ya Dosam”Aliongea James.

“Kumbe!, lakini bado swala hili halituhusu”Alongea huku akitingisha mabega,

Benjamini na mwanae walijikuta wakipauka mno , mwisho wa siku kundi hilo lilitaka kuwatelekeza tena.

Mzee Tui alihisia kabisa uwezo wa Hamza ni ngumu kuutabiria na alijikuta akiwa makini kutojiingiza kwenye matatizo zaidi.

“Hamza hakika wewe sio mpiganaji wa kawaida , kwa namna ulivyoruka umetufumbua macho ya tusivyokuwa tukijua , kama unataka kumchukua Benjamini na mwanae sisi hatutokuzuia maana ushirikiano wetu umekwisha kumalizika”Aliongea.

Hamza alimwangalia Mzee Tui na kisha kundi lake lote la nafsi zinazotangatanga.

“Umenielewa vibaya kuja kwangu hapa sio kwa ajili ya kukamata mtu”

“Sio kukamata?!!”Walijikuta wakishangaa wote wasijue Hamza anadhamiria kufanya nini.

“Sio familia ya Benjamini pekee iliosababisha kifo cha baba mkwe wangu, bali ni kundi lote la Wandering souls , lakini mpo wengi sana kitu ambacho kitakuwa kigumu kuwakamata wote na kuwarudisha Tanzania, hivyo ni bora niwapunguze kwa kuwaua hapa hapa”Aliongea Hamza na kufanya kila mtu juu ya boti hio kuwa kimya na mwonekano wa Mzee Tui ulibadlika.

“Hamza unaweza ukawa hujui , Kapteni Kenny ni rafiki yangu , hata kama una uwezo mkubwa sidhani kama utafanikwa kutushinda wote tukiunganisha nguvu”Aliongea na Hamza aligeuza macho yake kwa Kenny.

“Vipi mkuu unataka kuwasaidia?”Aliuliza Hamza na swali lake lilimfanya Kenny kucheka.

“Kama unataka kumuua rafiki yangu katika meli yangu , nini kitatokea juu ya taswira yetu tulioijenga kwa miaka mingi?, ngoja nikushauri kwa umri wako huo nakusifia kwa levo uliofikia lakini kama unataka kufikia juu zaidi ni bora ukaacha hili lipite , nipo tayari hata kukuruhusu kutumia meli yetu”Aliongea

“Nimeuliza swali moja unatoa majibu mengi , ushauri wako unanihusu nini?”Aliongea Hamza.

“Kijana unakwenda kulipa kwa maneno yako ya kiburi”Aliongea Kenny huku macho yake yakichanua.

Wakati huo wanajeshi waliokuwa kwenye Boti ya Mwendokasi walikuwa washaifikia meli hio na wamesimama pembeni yake.

Muda uleule Kanali Mwiba na Kanali Barafu walitumia mbnu za nishati na kuruka kwenda kutua juu ya deki ya meli hio.

“Hamza unataka kufanya nini?”Aliongea Afande Mwiba huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi na shauku.

“Hili eneo ni maji ya kimataifa na mnenifuata na kuvamia meli yangu , hii ni dharau kwangu mimi kama Kenny”Aliongea

“Kapteni Kenny hatuna nia ya kupigana na kundi lako la The Sharks , tupo hapa kwa ajili ya kumkamata Benjamini na mtoto wake , wamekiuka sheria na wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria za Tanzania”

“Kama ni hivyo hakuna shida , hatuna ugomvi na Malibu kwa muda mrefu , hivyo wachukueni na mumchukue na huyu kijana wenu”Aliongea.

“Hamza, Shuka juu ya meli , kwani hujaridhika na kukamatwa kwa Benjaini na mtoto wake na kuuchukua mwili wa baba mkwe wako?”Aliongea Afande Caro.

“Nitaridhika kama nikiona kundi lote la Nafsi zinazotangatanga wamekufa”Aliongea

“Hamza una kiburi kilichopitiliza , hata kama wanajeshi wa Malibu wakiungana na wewe , huwezi kutushinda mimi na Bro Kenny”Aliongea Mzee Tui.

Hamza hakujibu badala yake aliinua kidole chake na kunyooshea bendera yao iliokuwa ikipepea.

“Juu kabisa ya bendera yenu katika kichwa cha Shark mmeweka nembo ya Giant rifle , maana yake mpo chini ya OCN-DMONS , si ndio?”Aliuliza Hamza.

Baada ya swali hilo muonekano wa Kapteni Kenny ulibadilika palepale na kuonyesha mshangao kidogo.

“Kijana unaonekana kuwa na macho ya ki uchunguzi , hata wanajeshi wa Malibu wameshindwa kugundua ulichoona wewe”Aliongea na kauli yake ilimfanya Afande Mwiba na Afande Barafu kushangaa baada ya kusikia kauli hio.

Hawakuweka umakini kwenye bendera mwanzoni na mara baada ya kuangalia waliweza kuona kitu.

“Nyie mna ushirikiano na Sea Demons?”Aliuliza Kamanda Mwiba kwa mshangao.

“Upo sahihi , sasa hivi tupo chini ya Mkuu Vithn wa kundi la Sea Demons , mko slow mno kwa kitengo kikubwa cha Malibu kutogundua hili kwa muda mrefu”Aliongea Kapteni Kenny.

“Kamanda Mwiba na Caro nyuso zao zilijikunja na watu waliokuwa nyuma yao walionekana kutoelewa kinachoendelea.

“Kapteni wanamaanisha nini kuhusu Seas Demons?”Aliuliza Afande Gamale swali akilielekezea kwa Kapteni Norbert.

“Ktu chepesi hicho hujui , iko hivi duniani kuna umoja wa makundi mawali makubwa ya kiharamia ambayo ni Ice Sea whale hunters na kundi lingine la kitajiri maarufu kama Sea Demons , makundi haya yote ni daraja A katika ulimwengu wa giza , Haramia mkuu wa kundi la Sea Demons anatambulika kama Leviathan au maarufu kama Sea Monster , sasa haya makundi yote mawili yana ushirikiano na kampuni kubwa tatu za kimataifa za kuuza siraha kimagendo na kati ya moja ya kampuni hizo inaongozwa na jamaa maarufu wa ulimwengu wa giza anaefahamika kwa jina la Greed Mamen au Big mmiliki mkubwa wa meli kumi za kusafirisha siraha pamoja na manowari , vinginevyo unadhani kwanini makundi makubwa kama hayo yanaitwa daraja la kwanza maana yake ni kwamba wameunda makundi madogo madogo ya kiharamia ikiwemo The Sharks kwa ajili ya kurahisisha biashara zao , kwa kipindi kirefu hawa The Sharks ndio waingizaji wakubwa wa siraha kwa kundi la kigaidi la Al-shabab na baadhi ya makundi ya wapiganaji upande wa Congo, sasa ili kutambua haya makundi nani yupo chini yao unaangalia nembo kwenye bendera yao ukiona ni Giant Rifle maana yake wapo chini ya Sea Demons

Afande Mwiba na Afande Barafu walikuwa wakijua kuhusu maharamia wa bahari wa daraja la kwanza na kutokana na hali ilivyo waliona hawapasi kuwachokoza The Sharks.

Ukweli ni kwamba dunia ya kawaida inaweza iyachukulie makundi haya kama ya kihalifu lakini uwepo wake umeidhinishwa na serikali kubwa duniani na yote hayo ni kwa ajili ya kurahisisha biashara za siraha katika maeneo yote ya dunia bila kujali wanaemuuzia ni Gaidi ama ni nchi.

“Hili lishakuwa tatizo tayari”Aliongea Hamza huku akikuna kichwa chake.

“Ni vizuri ushajua , hivyo acha kujitafutia matatizo na mchukue Benjamini na mtoto wake na sisi tutaondoka”

“Mtaondoka , kuondoka kwenda wapi?”Aliuliza Hamza

“Hamza acha ujinga , unataka kujiingiza kwenye matatizo kwa jambo dogo kama hili , hivi unajua uwezo wa Leviathan , hata kama Mshauri mkuu angekuwa hapa asingekubali kuendelea”Alongea Afande Caro lakini Hamza alimpotezea.

“Mkuu , hivi umesema unaitwa Kenny?”Aliongea Hamza akiwa na usra ya upole

“Ndio , ushawahi kunisikia popote?”

“Sijawahi kukusikia kabisa”

“Kama ni hivyo unataka nini?”

“Nataka kuua watu wa kundi la Nafsi zinazotanga tanga hivyo usiingilie”

“Haha… kijana nadhani kuna tatizo kwenye akili yako , hivi unajua unaongea na nani?”Aliongea Kenny na mara baada ya kupunga mkono wake wanajeshi wake wote walikoki bunduki zao kumnyooshea Hamza.

Ndani ya sekunde tu hali ya meli hio ilibadilika na kuwa yenye ukinzani mkubwa.

“Hamza , hebu acha basi , hakuna wa kukusaidia wakikushambulia”Aliongea Kanali Caro kwa hasira.

“Hamza nakushauri ufuate ushauri wa wanajeshi wa Malibu na kuondoka kimya kimya , hapa sio Tanzania ni maji ya kimataifa na hata tukikuua hatuwezi kulaumiwa kisheria “Aliongea Tui.

“Mkuu Kenny naona ni kama umedhamiria kulinda hili kundi ?”

“Kwahio vipi kama nimeamua , sogea uone usipogeuka kiota cha nyuki, kama sio kuiheshimu Tanzania ningeshakumaliza sasa hivi”Aliongea kwa hasira.

Kamanda Mwiba mara baada ya kuona hali inaelekea kubaya alisogea bele ya Hamza na kumshika tai.

“Hamza acha uwendawazimu, hebu tuondoke hapa”Aliongea lakini Hamza alirudia kumshika Kamanda Mwiba mkono wake kwa nguvu.

“Kama unataka kuondoka wewe ondoka mwenyewe acha kunizuia ninachotaka kufanya”

“Acha ujinga , hata Mshauri mkuu hawezi kukusaidia katika hili , ngoja nikushikishe adabu pengine akili itakukaa sawa”Aliongea na palepae alianza kukusanya nguvu ya ndani ya mwili wake na kuufanya mwili kutuna , vidole vitatu vya mkono wake wa kulia vilichomoza kucha na kutaka kumtoboa Hamza kwenye mkono.

Lakini sasa licha ya kutumia nguvu kubwa kutaka kumuathiri Hamza hakuna matokeo yoyote yaliotokea , kiufupi Hamza hakuathirika hata kidogo , ilikuwa ni kama mtoto anaejaribu kupambana na baba yake.

“Mnunurisho wa nguvu zako upo hatua ya kwanza kuingia levo ya anga katika mizunguko theratini na sita , kwa uwezo huu mdogo unapata wapi ujasiri wa kujileta mbele yangu kama kichaa?”Aliongea Hamza na palepale nguvu ya mwili wake ilibadilika na kuleta msisimko ambao ni kama eneo lote limefunkwa na nguvu za giza.

Kitendo kile kilimfanya Afande Mwiba kuwa kama amegandishwa , kama mwanajeshi mwenye nishati za mbingu na ardhi alijihis muda wowote atageuka kuwa barafu .

“Wewe… wewe.,.”Alijikuta akikosa neno la kuongea maana katika maisha yake hakuwahi kuhisi nguvu kubwa kiasi hicho.

Alichokifanya Hamza ni kumsukuma kwa nguvu Kamanda Mwiba na matokeo yake alikuwa ni kama kiroba cha Cement kilichochorushwa kutoka kwenye gari ya mizigo kwenda chini

“Chubwiiii…!!!”

Kamanda Mwiba alitumbukia baharini .

Wanajeshi wa kitengo cha Malibu walishishitushwa sana na jambo hilo , walitarajia Kamanda Mwiba kumdhibiti Hamza lakini matokeo yake alidhibitiwa yeye.

“Mwibaa.!!!”

Kamanda Caro alijikuta akipiga ukulele wa king’ora , hakupata hata muda wa kumsaidia kwani kila kitu kilitokea kwa ghafla sana .

“Mnaangalia nini rukeni mkamsaidie”Aliongea Afande Caro akiwapa maagizo Afande Norbert na wenzake.

Waliokuwa kwenye mshangao zaidi ni Kapteni Kenny na Mzee Tui na kundi lake

Hawakuelewa kwasababu wanajeshi wa kitengo cha Malibu walikuwa wakijaribu kumlinda Hamza lakini matokeo yake Hamza ndio anaewaadhibu.

Kubwa zaidi ni kwamba msisimko ambao Hamza alitoa ulifanya kila mmoja kujihisi mapigo yake ya moyo yakisimama.

What will happen?”

ITAAENDELEA.

WATSAPP ME 0687151346
Dah sio tabia nzuri Mr Hades, haya bwana thanks
 
SEHEMU YA 88.

“Hey Rafiki yangu Tui, kwannini unaonekana kama kituko?”Aliongea mwanaume wa kirusi aliekuwa na mindevu mingi huku akiwa ameshikilia kiko, kichwani akiwa amevaa kofia ya kijeshi iliochakaa na kuchanika.

“Kenny naomba nikusumbue awamu hii , kwasababu ya hawa wapuuzi watatu misheni niliokuwa nikifanyia kazi Tanzania imevurugika”Aliongea Tui kwa kingereza safi.

“Hahaha..come up!, it wasn’t first time anyway”Aliongea kwa kinegereza akimwambia apande juu maana hata hivyo sio mara yake ya kwanza kuomba msaada.

“Ila usisahau ukiingia Mombasa kututafutia wanawake warembo”Aliendelea kuongea na muda ule aliwapa ishara vijana wake kuweka ngazi ili Tui na watu wake wapande juu ya meli.

“Tui hawa watu ulioambatana nao ni sehemu ya watu wako?”Aliuliza.

“Hapana , hawa ndio walikuwa mabosi wangu kwenye misheni niliokuwa nikifanya lakini wamefanya makosa na kuharibu kila kitu , bado hawajanilipa hela iliobakia”

“Kumbe, kama ni hivyo sidhani kama kuna haja ya kujipa mzigo wa kuwachukua”Aliongea Kenny.

“Kapteni Kenny tafadhari naomba usituache hapa , familia yetu bado ina hela na tukishafika eneo salama tutakulipa”Aliongea Mzee Benjamini.

“Kama mna hela zpo wapi , sisi ni maharamia na hakuna mmoja wetu mwenye akaunti benki , malipo sisi tunapokea cash mkononi , kama sio hela tunapokea madini au vito ..”Aliongea Kenny huku akikunja sura na kuvuta moshi wa sigara kwenye kiko chake.

“Nina hii saa ya Patek Phillippe , thamani yake ni Dollar milioni mbili”Aliongea Mzee Benjamini na haraka haraka alivua ile saa na Kenny aliinyakua kutoka kwenye mikonoo yake haraka na kuwarushia watu wake.

“Hio saa haina thamanni kubwa hata kama nikiiuza , labda kama unataka kubakia wewe peke yako kwenye hii meli” Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Mzee Benjamini kumwangalia Mzee Tui kwa macho ya kuomba.

“Mzee Tui naomba utusaidie , kama tukirudi na hii boti ya uvuvi ni dhahiri kabisa tutakamatwa na jeshi la Tanzania”Aliongea Mzee Benjamini kwa sauti ya kubembeleza.

Walikuwa wakijua kama Hamza alikuwa na uwezo wa kuwasiliana na jeshi basi kama wakikamatwa Hamza hatowaacha salama.

Isitoshe walishakwisha kumuua Mzee Wilsoni hivyo kinachokwenda kutokea ni kulipiziwa kisasi.

“Mnisamehe lakini sitaki kufanya mambo kuwa magumu kwa Kapteni Kenny , vinginevyo ni kutoa tu bilioni kumi zilizobakia”Aliongea Tui akiwakataa wenzake.

Muda huo Kenny macho yake yalitua kwenye mwili wa Lamla na tabasamu la uovu lilipamba sura yake.

Lmla alikuwa amevalia suruali hivyo ya jeansi na kufanya umbo lake kujichora vizuri.

Ijapokuwa alikuwa ashaanza kuzeeka lakini alikuwa mwanamke anaeishi katika mazingira ya kitajiri hivyo muonekano wake ulikuwa ukivutia.

“Huyo mwanamke naona sio mbaya sana , kwanza vijana wangu wamechoka kutumia wanawake ambao tupo nao ndani ya meli kwa mwezi mzima na tulikuwa na mpango wa kwenda kununua wengine Somalia …”Aliongea huku akichezea uchebe.

Lamla mara baada ya kusikia kauli hio vigoti vya miguu vlianza kumlgea na kujikuta akitetemeka.

“Hapana… mimi sio aina ya wanawake wanaojiuza..”Aliongea akijitetea,alikuwa katika kiwango cha juu mno cha woga na alijificha nyuma ya Mzee Benjamini.

“Benja naogopa , usiwahurusu kunifanyia kitu kibaya”Aliongea lakini muda uleule James na baba yake waliangaliana kwa ishara.

“Hebu sogea mbele huko”Aliongea Mzee Benjamini huku akimsukumia Lamla mbele yake na kumfanya adondoke chini.

“Kapteni Kenny tutakuuzia huyu mwanamke , tafadhari naomba mimi na mtoto wangu utufikishe afukweni salama”Aliongea Mzee Benjamini.

Mzee Bejamini na mwanae walikuwa na kiasi cha pesa nje ya nchi lakini vilevile walikuwa na ushirikiano na Mstaafu Mgweno hivyo waliamini kama watafika nchi kavu watakuwa na kiasi cha kutosha cha kuanzia upya, hivyo kumuuza Lamla haikuwa hasara..

Kitendo cha Kumsikia mpenzi wake Benja akimuuza kwa hao maharamia uso wake ulipauka dakika ilele.

“Benja wewe ni mnyama , yaani nimeshirikiana na wewe kwa zaidi ya miaka kumi tena nikakuzalia mtoto wa kiume halafu unanifanyia hivi?”

Ulimwengu wake wote ulikumbwa na giza ghafla tu na alijihisi alikuwa akitumbukia shimoni.

Mzee Benjamini aliishia kuweka mikono yake kwenye bega la james huku akimwangalia Lamla kwa kejeli.

“Mtoto wangu wa kiume ninaemtambua ni James pekee , Frank uliemzaa ni mjinga zaidi ya ujinga na pengine ashaingia kwenye maswala ya upinde”Aliongea.

“Mshenzi mkubwa wewe , hivi nyie wanaume kwanini mnakuwa kama mbwa?”Aliongea kwa kulaani huku akianza kulia lakini Mzee Benjamini hakujali kilio chake.

“Kapteni Kenny tafadhari tunaomba utufikishe nchi kavu”Aliongea.

“Hahaha...napenda watu wa aina yako ambao hamjali ni mbinu gani mnatumia kujilinda , haha wewe ni mkatili sana , safii”Alongea Kenny na kisha aliwageukia vijana wake.

“Mnasubiri nini, mpelekeni ndani akaonje joto la Papa”

Mara baada ya kuongea kauli hio maharamia wale kwa furaha kubwa walimkamata kwa nguvu Lamla na kisha kuingia nae kwenye Cabin.

Lamla alijifanyisha kutaka kuleta ushindani lakini alipokea vibao vya nguvu vilivyomfanya kushikwa na ukichaa huku macho yake yakiwa meupe kama mtu aliekosa tumaini tena.

Mzee Benjamini na James walijikuta wakifuta jasho la paji la uso mara baada ya kuponea chupu chupu , lakini sasa dakika hio hio boti ya jeshi la Tanzania iliweza kuonekana katika macho yao.

“Kenny wanajeshi wa Tanzania wale wanakuja?”Aliongea Mzee Tui na mara baada ya kuangalia alijikuta akitoa kicheko cha kejeli.

“Kwa walivyo wachache vile watatufanya nini , wakithubutu kutufukuzia kwenye maji ya kimataifa tutawalipua na kuwa chakula cha samaki”Aliongea kwa kujiamini huku akiwapa ishara vijana wake kuondoka eneo hilo.

Upande wa kikosi cha Malibu walijikuta wakikunja sura mara baada ya kuona meli za maharamia.

“ Ni The Shark wale ,Simamisha boti , haina haja ya kuendelea kuwafukuzia”Aliongea Afande Caro lakini kauli yake ilimfanya Hamza kushangaa , mpango wake haukuwa ni kuishia hapo.

“Yaani wahalifu wapo mbele yetu , mnataka tusimamishe na kurudi , mnaogopa nini?”Alongea

“Kama umekuja kwa ajili ya kuchukua maiti ya baba mkwe wako itakuwa kwenye ile boti ya uvuvi , haina haja ya kuwafukuzia wakiwa kwenye maji ya kimataifa”Aliongea Afande Caro

“Ni kakundi kadogo tu ka maharamia , mnachotakiwa ni kushirikiana na mimi na hakuna kitakachotokea”Aliongea Hamza.

“Wewe mjinga hebu kaa kimya , unafikiri Kapteni Kenny wwa The Shark ni mwanajeshi wa kawaida , ana mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na anakaribia levo ya Nafsi na pia ana watu zaidi ya mia wanaomzunguka, unadhani tutashindana nae vipi?”

Hamza mara baada ya kuona meli le inaanza kuondoka , hakutaka kupoteza muda tena na Afande Mwiba.

“Kama hamtaki kushirikiana na mimi bas bakieni kwenye boti na nitadili na hili swala mwenyewe”Aliongea Hamza.

“Unajifanya wewe ndio Mshauri mkuu , utaweza kufanya nini bila msaada wetu?”

“Msiwe na waswasi na mimi , punguzeni mwendo maana mkisogea karibu watawashambulia”Aliongea Hamza na baada ya hapo alirudi nyuma kwenye ukingo wa boti na kuvuta pumzi nyingi na muda uleule nywele zake zilisimama, akiwa amevuta nguvu zake zote alifyatuka mbio kama mwanariadha na mguu wake wa mshio kukanyaga boti aliisababishia kuyumba kiasi cha kutaka kuzama lakini kilichotokea baada ya hapo wanajeshi wote walitoa macho kama wamebanwa na mlango.

Hamza alikuwa ni kama kombolra lilivyofyatuliwa na sasa linaelekea kushambulia shabaha. Spidi yake iliwafanya wanajeshi wa kitengo cha Malibu kuishia kuona kivuli tu kikipotea kwenye macho yao.

Hamza alienda kutua kwenye boti ile ya uvuvi na nguvu aliotua nayo ilifanya na yenyewe izame eneo la mbele.

Hakuna alieweza kuamini , umbali kutoka walipokuwa na boti ile ni kama mita miasaba hivi au zaidi lakini Hamza alifanikiwa kuruka na kuifikia.

“Haiwezekani ni mbingu gani katumia kuruka umbali ule?”

Kapteni Norbert na wenzake macho yaliwatoka wakati wakiangalia tukio hilo likitokea .

“Hii haiwezi kuwa mbinu ya kuvuna nishati , hakuna msisimko wa kinishati unaomtoka?”

“Haiwezekani isiwe mbinu ya kuvuna nishati , unataka kusema ametegemea nguvu ya miguu yake pekee kuruka mita zote hizo?”Walijikuta wakibishana wao kwa wao.

Afande Mwiba na Kanali Caro wenyewe hawakuamini , sio kwamba hawakuwa na uwezo wa kuruka , kwa kutegemea nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kwa levo waliofikia uwezo huo wanao lakini kuruka kwao hakuwezi kuwa umbali mrefu kwasababu bado hawajabobea kwenye mbinu ya Floating water

Kuruka ukiwa kwenye ardhi ni tofauti na kuruka ukiwa kwenye bahari , mbinu ya nishati mara nyingi inategemea ardhi na mbingu na sio mbingu na maji na ili uweze kuruka umbali mrefu kwenye maji unatakiwa ujifunze pia mbinu nyingine ya kuvuna nishati kati ya mbingu(anga) na Maji(bahari). Ukifanikiwa katika hio mbinu utakuwa na uwezo wa kutembea juu ya maji bila kutumbukia na mbinu hio ndio huitwa Floating water movement.

Sasa kwa watu kama Afande Mwiba hawakuwahi kuona mtu akiruka kama kichaa na kuweza kufanikiwa kufikia umbali uliokusudiwa kama huo.

“Huyu Hamza inamaana miguu yake imefungwa injini za roketi , amewezaje kuruka umbali wote ule?”Walishangaa maana kila kitu kilikuwa kikienda kinyume na kile ambacho wamejifunza.

“Hata hivyo kama kitu kibaya kikimkuta ni dhahiri lawama zote tutabebeshwa , tunapaswa kusogea mbele angalau kumlinda”Aliongea Afande Caro au Kanali Barafu.

“Acha ujinga , unataka kututafutia matatizo, ndio maana nilikuwa nikipinga kuja na sisi”Aliongea Afande Mwiba kwa hasira.

Kilichowapa wasiwasi ni kwamba hata kama Hamza ameonyesha uwezo wa kuruka ubali wote huo , bado hakuwa ametumia mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , hivyo kwa macho yao bado ni wa kawaida.

Licha ya Afande Mwiba kupinga lakini wanajeshi walikuwa wakipokea zaidi maagzo kutoka kwa Afande Caro ambae ni senior , hivyo boti yao ilianza kuongeza mwendo.

Upande mwingine Kenny na Mzee Tui na wengine walijikuta wakishangaa , mwanzoni walidhania wanajeshi wa Malibu wataacha kuwafukuzia kwasababu walikuwa na uwezo wa kuwazamisha katka maji ya kimataifa bila kubeba lawama.

Dakika hio hio wakati macho yao yakiwa makini na boti ya wanajeshi ghafla tu kitu kilishuka kutoka juu angani na kutua kama bomu juu ya meli yao.

Alikuwa ni Hamza ambae alitua kama vile ni Batman na baada ya kusimama vizuri alianza kuwaangalia mmoja baada ya mwingine

Macho yake na nywele zake zilizokuwa zikichemka iliwafanya watu wote kuanza kuingiwa na hofu maana ni kama walikuwa wakiangaliana na jini Medusa.

“Mlidhani mnaweza kunikimbia mara baada ya kusababisha matatizo , kama ningejua ningewamaliza muda mrefu tu”Aliongea Hamza huku akimwangalia Benjamini na James.

Mzee Benjamini na mwanae walikuwa wameshikwa na woga kiasi cha kutaka kujikojolea na haraka walienda kujificha nyuma ya Mzee Tui na Kapteni Kenny.

“Wewe sio mtu ni jini?”Aliongea James huku akijiambia alikuwa akiwaza nini kupambana na mtu wa aina hio.

“Mzee Kenny tumelipia kwa ajili ya kuwa ndani ya hi meli , usije ukaacha tuchukuliwe” Aliongea Mzee Benjamini

“Jukumu langu lilikuwa ni kuwapeleka nchi kavu lakini sikuahidi kama nitawalinda , huyu mwanajeshi wa Malibu anaonekana kuwa na uwezo mkubwa mno na hatutaki uadui nae bila sababu”Aliongea Kenny.

“Huyu sio mwanajeshi wa Malibu ni msaidizi wa mkurugenzi ndani ya kampuni ya Dosam”Aliongea James.

“Kumbe!, lakini bado swala hili halituhusu”Alongea huku akitingisha mabega,

Benjamini na mwanae walijikuta wakipauka mno , mwisho wa siku kundi hilo lilitaka kuwatelekeza tena.

Mzee Tui alihisia kabisa uwezo wa Hamza ni ngumu kuutabiria na alijikuta akiwa makini kutojiingiza kwenye matatizo zaidi.

“Hamza hakika wewe sio mpiganaji wa kawaida , kwa namna ulivyoruka umetufumbua macho ya tusivyokuwa tukijua , kama unataka kumchukua Benjamini na mwanae sisi hatutokuzuia maana ushirikiano wetu umekwisha kumalizika”Aliongea.

Hamza alimwangalia Mzee Tui na kisha kundi lake lote la nafsi zinazotangatanga.

“Umenielewa vibaya kuja kwangu hapa sio kwa ajili ya kukamata mtu”

“Sio kukamata?!!”Walijikuta wakishangaa wote wasijue Hamza anadhamiria kufanya nini.

“Sio familia ya Benjamini pekee iliosababisha kifo cha baba mkwe wangu, bali ni kundi lote la Wandering souls , lakini mpo wengi sana kitu ambacho kitakuwa kigumu kuwakamata wote na kuwarudisha Tanzania, hivyo ni bora niwapunguze kwa kuwaua hapa hapa”Aliongea Hamza na kufanya kila mtu juu ya boti hio kuwa kimya na mwonekano wa Mzee Tui ulibadlika.

“Hamza unaweza ukawa hujui , Kapteni Kenny ni rafiki yangu , hata kama una uwezo mkubwa sidhani kama utafanikwa kutushinda wote tukiunganisha nguvu”Aliongea na Hamza aligeuza macho yake kwa Kenny.

“Vipi mkuu unataka kuwasaidia?”Aliuliza Hamza na swali lake lilimfanya Kenny kucheka.

“Kama unataka kumuua rafiki yangu katika meli yangu , nini kitatokea juu ya taswira yetu tulioijenga kwa miaka mingi?, ngoja nikushauri kwa umri wako huo nakusifia kwa levo uliofikia lakini kama unataka kufikia juu zaidi ni bora ukaacha hili lipite , nipo tayari hata kukuruhusu kutumia meli yetu”Aliongea

“Nimeuliza swali moja unatoa majibu mengi , ushauri wako unanihusu nini?”Aliongea Hamza.

“Kijana unakwenda kulipa kwa maneno yako ya kiburi”Aliongea Kenny huku macho yake yakichanua.

Wakati huo wanajeshi waliokuwa kwenye Boti ya Mwendokasi walikuwa washaifikia meli hio na wamesimama pembeni yake.

Muda uleule Kanali Mwiba na Kanali Barafu walitumia mbnu za nishati na kuruka kwenda kutua juu ya deki ya meli hio.

“Hamza unataka kufanya nini?”Aliongea Afande Mwiba huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi na shauku.

“Hili eneo ni maji ya kimataifa na mnenifuata na kuvamia meli yangu , hii ni dharau kwangu mimi kama Kenny”Aliongea

“Kapteni Kenny hatuna nia ya kupigana na kundi lako la The Sharks , tupo hapa kwa ajili ya kumkamata Benjamini na mtoto wake , wamekiuka sheria na wanapaswa kufikishwa mbele ya sheria za Tanzania”

“Kama ni hivyo hakuna shida , hatuna ugomvi na Malibu kwa muda mrefu , hivyo wachukueni na mumchukue na huyu kijana wenu”Aliongea.

“Hamza, Shuka juu ya meli , kwani hujaridhika na kukamatwa kwa Benjaini na mtoto wake na kuuchukua mwili wa baba mkwe wako?”Aliongea Afande Caro.

“Nitaridhika kama nikiona kundi lote la Nafsi zinazotangatanga wamekufa”Aliongea

“Hamza una kiburi kilichopitiliza , hata kama wanajeshi wa Malibu wakiungana na wewe , huwezi kutushinda mimi na Bro Kenny”Aliongea Mzee Tui.

Hamza hakujibu badala yake aliinua kidole chake na kunyooshea bendera yao iliokuwa ikipepea.

“Juu kabisa ya bendera yenu katika kichwa cha Shark mmeweka nembo ya Giant rifle , maana yake mpo chini ya OCN-DMONS , si ndio?”Aliuliza Hamza.

Baada ya swali hilo muonekano wa Kapteni Kenny ulibadilika palepale na kuonyesha mshangao kidogo.

“Kijana unaonekana kuwa na macho ya ki uchunguzi , hata wanajeshi wa Malibu wameshindwa kugundua ulichoona wewe”Aliongea na kauli yake ilimfanya Afande Mwiba na Afande Barafu kushangaa baada ya kusikia kauli hio.

Hawakuweka umakini kwenye bendera mwanzoni na mara baada ya kuangalia waliweza kuona kitu.

“Nyie mna ushirikiano na Sea Demons?”Aliuliza Kamanda Mwiba kwa mshangao.

“Upo sahihi , sasa hivi tupo chini ya Mkuu Vithn wa kundi la Sea Demons , mko slow mno kwa kitengo kikubwa cha Malibu kutogundua hili kwa muda mrefu”Aliongea Kapteni Kenny.

“Kamanda Mwiba na Caro nyuso zao zilijikunja na watu waliokuwa nyuma yao walionekana kutoelewa kinachoendelea.

“Kapteni wanamaanisha nini kuhusu Seas Demons?”Aliuliza Afande Gamale swali akilielekezea kwa Kapteni Norbert.

“Ktu chepesi hicho hujui , iko hivi duniani kuna umoja wa makundi mawali makubwa ya kiharamia ambayo ni Ice Sea whale hunters na kundi lingine la kitajiri maarufu kama Sea Demons , makundi haya yote ni daraja A katika ulimwengu wa giza , Haramia mkuu wa kundi la Sea Demons anatambulika kama Leviathan au maarufu kama Sea Monster , sasa haya makundi yote mawili yana ushirikiano na kampuni kubwa tatu za kimataifa za kuuza siraha kimagendo na kati ya moja ya kampuni hizo inaongozwa na jamaa maarufu wa ulimwengu wa giza anaefahamika kwa jina la Greed Mamen au Big mmiliki mkubwa wa meli kumi za kusafirisha siraha pamoja na manowari , vinginevyo unadhani kwanini makundi makubwa kama hayo yanaitwa daraja la kwanza maana yake ni kwamba wameunda makundi madogo madogo ya kiharamia ikiwemo The Sharks kwa ajili ya kurahisisha biashara zao , kwa kipindi kirefu hawa The Sharks ndio waingizaji wakubwa wa siraha kwa kundi la kigaidi la Al-shabab na baadhi ya makundi ya wapiganaji upande wa Congo, sasa ili kutambua haya makundi nani yupo chini yao unaangalia nembo kwenye bendera yao ukiona ni Giant Rifle maana yake wapo chini ya Sea Demons

Afande Mwiba na Afande Barafu walikuwa wakijua kuhusu maharamia wa bahari wa daraja la kwanza na kutokana na hali ilivyo waliona hawapasi kuwachokoza The Sharks.

Ukweli ni kwamba dunia ya kawaida inaweza iyachukulie makundi haya kama ya kihalifu lakini uwepo wake umeidhinishwa na serikali kubwa duniani na yote hayo ni kwa ajili ya kurahisisha biashara za siraha katika maeneo yote ya dunia bila kujali wanaemuuzia ni Gaidi ama ni nchi.

“Hili lishakuwa tatizo tayari”Aliongea Hamza huku akikuna kichwa chake.

“Ni vizuri ushajua , hivyo acha kujitafutia matatizo na mchukue Benjamini na mtoto wake na sisi tutaondoka”

“Mtaondoka , kuondoka kwenda wapi?”Aliuliza Hamza

“Hamza acha ujinga , unataka kujiingiza kwenye matatizo kwa jambo dogo kama hili , hivi unajua uwezo wa Leviathan , hata kama Mshauri mkuu angekuwa hapa asingekubali kuendelea”Alongea Afande Caro lakini Hamza alimpotezea.

“Mkuu , hivi umesema unaitwa Kenny?”Aliongea Hamza akiwa na usra ya upole

“Ndio , ushawahi kunisikia popote?”

“Sijawahi kukusikia kabisa”

“Kama ni hivyo unataka nini?”

“Nataka kuua watu wa kundi la Nafsi zinazotanga tanga hivyo usiingilie”

“Haha… kijana nadhani kuna tatizo kwenye akili yako , hivi unajua unaongea na nani?”Aliongea Kenny na mara baada ya kupunga mkono wake wanajeshi wake wote walikoki bunduki zao kumnyooshea Hamza.

Ndani ya sekunde tu hali ya meli hio ilibadilika na kuwa yenye ukinzani mkubwa.

“Hamza , hebu acha basi , hakuna wa kukusaidia wakikushambulia”Aliongea Kanali Caro kwa hasira.

“Hamza nakushauri ufuate ushauri wa wanajeshi wa Malibu na kuondoka kimya kimya , hapa sio Tanzania ni maji ya kimataifa na hata tukikuua hatuwezi kulaumiwa kisheria “Aliongea Tui.

“Mkuu Kenny naona ni kama umedhamiria kulinda hili kundi ?”

“Kwahio vipi kama nimeamua , sogea uone usipogeuka kiota cha nyuki, kama sio kuiheshimu Tanzania ningeshakumaliza sasa hivi”Aliongea kwa hasira.

Kamanda Mwiba mara baada ya kuona hali inaelekea kubaya alisogea bele ya Hamza na kumshika tai.

“Hamza acha uwendawazimu, hebu tuondoke hapa”Aliongea lakini Hamza alirudia kumshika Kamanda Mwiba mkono wake kwa nguvu.

“Kama unataka kuondoka wewe ondoka mwenyewe acha kunizuia ninachotaka kufanya”

“Acha ujinga , hata Mshauri mkuu hawezi kukusaidia katika hili , ngoja nikushikishe adabu pengine akili itakukaa sawa”Aliongea na palepae alianza kukusanya nguvu ya ndani ya mwili wake na kuufanya mwili kutuna , vidole vitatu vya mkono wake wa kulia vilichomoza kucha na kutaka kumtoboa Hamza kwenye mkono.

Lakini sasa licha ya kutumia nguvu kubwa kutaka kumuathiri Hamza hakuna matokeo yoyote yaliotokea , kiufupi Hamza hakuathirika hata kidogo , ilikuwa ni kama mtoto anaejaribu kupambana na baba yake.

“Mnunurisho wa nguvu zako upo hatua ya kwanza kuingia levo ya anga katika mizunguko theratini na sita , kwa uwezo huu mdogo unapata wapi ujasiri wa kujileta mbele yangu kama kichaa?”Aliongea Hamza na palepale nguvu ya mwili wake ilibadilika na kuleta msisimko ambao ni kama eneo lote limefunkwa na nguvu za giza.

Kitendo kile kilimfanya Afande Mwiba kuwa kama amegandishwa , kama mwanajeshi mwenye nishati za mbingu na ardhi alijihis muda wowote atageuka kuwa barafu .

“Wewe… wewe.,.”Alijikuta akikosa neno la kuongea maana katika maisha yake hakuwahi kuhisi nguvu kubwa kiasi hicho.

Alichokifanya Hamza ni kumsukuma kwa nguvu Kamanda Mwiba na matokeo yake alikuwa ni kama kiroba cha Cement kilichochorushwa kutoka kwenye gari ya mizigo kwenda chini

“Chubwiiii…!!!”

Kamanda Mwiba alitumbukia baharini .

Wanajeshi wa kitengo cha Malibu walishishitushwa sana na jambo hilo , walitarajia Kamanda Mwiba kumdhibiti Hamza lakini matokeo yake alidhibitiwa yeye.

“Mwibaa.!!!”

Kamanda Caro alijikuta akipiga ukulele wa king’ora , hakupata hata muda wa kumsaidia kwani kila kitu kilitokea kwa ghafla sana .

“Mnaangalia nini rukeni mkamsaidie”Aliongea Afande Caro akiwapa maagizo Afande Norbert na wenzake.

Waliokuwa kwenye mshangao zaidi ni Kapteni Kenny na Mzee Tui na kundi lake

Hawakuelewa kwasababu wanajeshi wa kitengo cha Malibu walikuwa wakijaribu kumlinda Hamza lakini matokeo yake Hamza ndio anaewaadhibu.

Kubwa zaidi ni kwamba msisimko ambao Hamza alitoa ulifanya kila mmoja kujihisi mapigo yake ya moyo yakisimama.

What will happen?”

ITAAENDELEA.

WATSAPP ME 0687151346
Asante mkuu
 
Back
Top Bottom