Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SHETANI RUDISHA NAFSI ZETU​

MTUNZI:SINGANOJR​





SEHEMU YA 165.

Fire and Ashes rebirth.

(Nyakasura).

Hamza alijikuta akijifuta damu zilizokuwa zikitoka katika mgongo wake na kisha alimwangalia Roja na wenzake.

“Ninachotaka ni kumuua Master wenu tu , kama na nyie mnataka kufa sogeeni”Aliongea Hamza.

“Acha majigambo , humuwezi Master wetu”

“Kweli , kutuweza sisi usidhani utamuweza na Master”

Wafuasi wale wa Mzee Farook walianza kumtetea Master wao lakini maneno yao yalikuwa yamejaa hatia , hakuna aliekuwa na ujasiri kumsogelea Hamza tena , uwezo wake ulikuwa haupimiki.



“Kama mmeamua kuwa mashabiki endeleeni”Aliongea Hamza mara baada ya kuona wale wafuasi wa Master Farook wakianza kumpa sifa ambazo aliamini hakuwa nazo.

Mara baada ya kuongea maneno hayo , aliruka mara moja chini kuazima nguvu za miguu na ile anaruka mara ya pili aligeuka kuwa kama mshale akiruka uelekeo wa alipo Master Farook.

Mzee Farook mwanzoni alidhania kama Hamza angetaka kumfikia mahali alipo angekimbia kwa kuzunguka mlima huo baada ya kuona hakuwa na ishara yoyote ya kuwa na nishati za mbingu na ardhi lakini hakutegemea Hamza angeruka kama kombora kwa kutegemea nguvu ya miguu yake pekee.

Hamza alikanyaga kwenye jabari moja tu kuongeza nguvu na kisha alifyatuka kwa mara nyingine na kufikia katika jiwe kubwa ambalo alikuwa amekanyaga Master Farook.

Mzee Farook alikuwa katika mshituko mkubwa kwa ndani lakini bado alikuwa kiongozi wa kambi yake hivyo haraka sana alikusanya nguvu zake zote za mbingu na ardhi huku mkono wake ukifikia siraha iliokuwa katika kiuno chake.

“Nadhani hujawahi kutoa machozi mbele ya jeneza. Unadhani kambi yetu ni kama kambi zingine tu kuvamia unavyotaka?”Aliongea Mzee Farook kwa sauti ya chini.

“Ongea yako haiendani na wasiwasi uliokuwa nao . Kama nimeweza kuvunja mbinu yenu ya mizinguko theratini na sita kwanini nikuogope”Aliongea Hamza

“Acha majigambo , umepata bahati kufanikiwa kuepuka safu yetu ya ulinzi . Wewe sio mtu wa kwanza kufanikiwa kutoka katika mtego wa safu yetu, acha kujiona mwamba”

“Kumbe! Sijawahi kuwaza kuna mwingine zaidi yangu. Wewe na mtoto wako ndio watu pekee mnaodhani mna nguvu ya kutosha kwenda mjini na kutibua kampuni ya mke wangu mnavyojisikia kwasababu ya koneksheni zenu. Mambo ya wanaume yalipaswa kumalizwa kiume , haikuwa na haja ya kuingiza watu wa nje”Aliongea Hamza.

“Hahaha! Wewe mtoto haijalishi utasema nini , kwangu mimi nakuona kama kichaa aliejaaliwa mwili wenye utimamu. Hivi unadhani nimesimama kihasra katika huu mlima?”Aliuliza na kauli ile ilimshangaza Hamza na kujiuliza kwanini aanaongea hivyo au ameweka mtego.

Lakini sasa dakika hio hio Mzee Farook mara baada ya kuona Hamza akishangaa alichukulia hio kama nafasi na alifyatuka kumsogelea Hamza huku akinyoosha siraha yake ya upanga mbele.

“Nishati safi , Hasira ya upanga butu!”

Mara baada ya kuongea hivyo upanga wake usio na makali ambao ulitoka katika Alla iliokuwa na umbo la nyoka ulikuwa ukimeremeta mno kiasi cha kuumiza macho baada ya kutawaliwa na nishati ya mbingu na ardhi.

Hamza kuangalia upanga ule alihisi ni kama tayari ushamfikia machoni na kumfanya aongeze umakini na ile anaukwepa kilichosikika ni ‘ siii’ upanga ule ulimpitia kwenye shavu lake na kumfanya kutokwa na damu kiasi.

Hamza alijikuta akigusa shavu lake na kugundua alishatengenezewa kidonda usoni. Alijikuta akishindwa kujizuia na kushikwa na ubaridi mgongoni kwa shambulizi lile.

Nishati safi hasira ya upanga butu ilikuwa ni mbinu nyingine kambi hio ilikuwa ikitumia , mara nyingi upanga unakuwa butu kabisa kiasi kwamba hata kukata mgomba inaweza kuwa ngumu lakini wakati wa kushambulia makali yake hutengenezwa na nishati za mbingu na ardhi. Moja ya sababu ya upanga huo kuachwa butu ni kutokana na aina ya matumizi yake kwenye kushambulia ikiwa mikononi mwa mvuna nishati.

Hamza mara baada ya kukatwa alishangaa, hakutegemea upanga kama huo unaweza kumkata na kumtengenezea kidonda tena ndani ya shambulizi moja.

Hamza sio kwamba hakuwa akiijua mbinu hio ya nishati safi hasira ya upanga butu , ukweli alikuwa akiijua sana lakini ni watu wachache sana waliokuwa wakijifunza kutokana na ugumu wake. Si rahisi kuufanya upanga ambao ni butu kuwa na makali zaidi ya makali ya kiwembe.

Hamza aliona sio haba , Master huyo alistahili jina lake , alitumia mbinu ya kumchanganya kidogo na kisha kumshambulia na aliona kama isingekuwa uzoefu wake wa mapigano angeweza kudhibitiwa na shambulizi moja tu.

Master Farook mara baada ya kuona shambulizi lake la mwanzo limefeli , palepale alibadilisha mbinu yake kwa kuchezesha upanga hewani kwa namna ya kufyeka huku kila akifanya mkato Hamza ni kama alikuwa akihisi vitu kama vinyota vikimchoma mwilini bila kuguswa na upanga ule.

Hamza hakutaka aendelee kumshambulia kwa kutumia upanga huo kumsambabishia maumivu bila ya kumgusa , hivyo aliangalia staili ile ya upanga inavyofyeka hewani na kisha na yeye angeruka kukwepa shambulizi. Isitoshe alijua mbinu ya kutumia upanga butu sio rahisi pia kwa Master Farook maana alihitajika kuunganisha nishati za mbingu na ardhi na upanga huo kabla ya kushambulia kuutengezea Aura ya makali.

“Nadhani ndio maana wanakuita Master na Fabiani kuwa mtoto wako , mbinu ya matumizi ya Upanga butu imekwisha kupitwa na wakati lakini umeweza kuifufua. Hakika kuwa Mkuu wa kambi sio swala jepesi”Aliongea Hamza.

“Acha kuongea ujinga , kama uwezo unao shindana na upanga wangu acha kukwepa”

“Hakuna shida , twende kazi”Aliongea Hamza na palepale alisogea mbele na ile Mzee Farook anataka kutumia upanga wake Hamza alishaushika tayari na mikono yote miwili.

“Arghhhhhhhhhhhhh!

Hamza alinguruma kwa sauti kubwa sana huku akiwa ameushikilia ule upanga na sekunde chache mbele kilichoweza kusikika ni ‘Clang’ na ule upanga kuvunjika vipande viwili.

Kitendo kile cha Hamza kuukata upanga wake ilimfanya Master Farook kurudi hatua nyuma akimwangalia Hamza kwa hofu.

Sifa nyingine ya kufanya upanga huo kuitwa butu ilikuwa ni ule ugumu wake , lakini Hamza kwa kutumia tu nguvu za mikono yake amefanikiwa kuuvunja , ilikuwa ni kutu cha kutisha mno kutoka kwa binadamu.

Hamza aliishia kutupa vipande vya ule upanga na kujiangalia mikononi na aliweza kuona kuvilia kwa damu kwenye mikono yake lakini hakujali.

“Mbinu ya Upanga butu kwangu ni kama kichekesho , kama una siraha nyingine, toa tuone”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu la uovu.

Chini ya kijimlima hicho kulikuwa na wafuasi wa kambi hio na walishangaa baada ya kuona Master wao ameweza kupokonywa mpaka siraha yake na ikavunjwa.

Mzee Farook mara baada ya kuona ameweza kupokonywa upanga wake alijikuta akikasirika sana na aliamua kutumia nishati zake za mbingu na ardhi kumshambulia Hamza.

Muda ule alibadilika na kuanza kutumia mbinu ya mneso wa nyoka na kadri alivyokuwa akitumia mbinu ile miondoko yake iliongezeka spidi kiasi cha mwili wake kuonekana kama kivuli akimshambulia Hamza.

“Kani mtungo!”

Mzee Farook mara baada ya kugundua Hamza mwili wake ulikuwa mgumu sana kushambulia aliona atumie mbinu ya Kani Mtungo kwa ajili ya kushambulia katika maeneo dhaifu ya mwili wake kwa kutumia vidole kwa namna ya kudunga.

Lakini Hamza macho yake yalikuwa ni kama ya mashine kwani sekunde ambayo Master Farook anataka kumshambulia na mkono wake aliruka na teke na kuupiga ule mkono.

“Arghhh!” Mzee Farook alitoa ukulele mkali wa maumivu kutokana na mkono wake kuvunjika.

“Master!!”

Wanafunzi wake walipiga makelele , hawakuweza kuona hata Hamza amempigaje.

Mzee Farook aliishia kujishikiza kwenye mti wa mkaratusi asidondoke chini na bila ya kuongea neno paleplae alitafuta upenyo wa kukimbia kwenda chini baada ya kuhisi hatomuweza Hamza.

Hamza mara baada ya kuona anataka kukimbia hakutaka kumruhusu kirahisi hivyo alimsogelea kwa spidi.

Mzee Farook alikuwa ametumia takribani uwezo wake wote na wakati wa kukimbia hakujali kama wanafunzi wake walikuwa wakimuona , aliishia kupiga kelele akiita jina la Mjomba.

“Mjombaa! Mjombaa kambi ipo matatizoni”Aliongea hivyo huku akiendelea kuomba mjomba huyo kuijitokeza ili kumdhibiti Hamza.

Muda ule Hamza sasa alielewa nini kinachoendelea , aliona Farook ameona uwezo wa kushindana nae hana, na kukimbia huko ni kwa ajili ya kuita msaada zaidi , ilionekana kuna watu wengine ambao walikuwa ndani ya eneo hilo ambao hakuwa amewaona.Alihisi hivyo ila hakuwa na uhakika na alisubiria kumuona huyo mjomba.

Ukweli ni kwamba katika kila kambi ilikuwa na wazee , licha ya Farook kuwa kiongozi haikumaanisha alikuwa peke yake wa kuongoza kambi , kulikuwa na wazee wengine waliokuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na hawakujihusisha moja kwa moja katika shughuli za kambi wao walikuwa tu kama waangalizi.

Licha ya Mzee Farook kuita sana lakini hakuna Mjomba aliejitokeza na kumfanya kuzidi kushikwa na wasiwasi na pia Hamza alikuwa nyuma yake akimkaribia.

Hamza mara baada ya kuona amemkaribia Mzee huyo palepale alijiandaa kufanya shambulizi la kumuua moja kwa moja lakini kabla hajafanya hivyo alihisi joto la ajabu kutoka nyuma yake , joto lililofanya mwili wake kusisimka kwa kuhisi hatari na hakutaka kuchelewa palepale aliruka kwa sarakasi kusogea upande wa kushoto kwa kutumia utashi wake wa akili.

Ile anasogea tu kitu kilichoonekana kama moto kilipita na kwenda kutua chini kusababisha kishindo kama vile lilikuwa ni bomu.

Moto ule ulikuwa na joto kali mno kiasi cha kuyeyusha mawe jambo lililomshangaza mno Hamza na kujikuta akihisi ubaridi wa hofu.

“Wewe ni nani!?”Aliongea Hamza kwa nguvu huku akijihisi moyo wake ulikuwa ukitetemeka.

Mara baada ya kugeuza macho yake kuangalia upande wa juu aliweza kuona kivuli cha mtu juu ya paa la jengo la kambi pembeni ya Sanamu la Nyoka ishara ya kambi hio.

Kila mfuasi wa kambi hio ukimjumlisha na Mzee Farook aliekuwa akikimbia walijikuta wakisimama na kuangalia kwa shauku kubwa uelekeo wa shambulizi lile lilikotokea.

Mara baada ya kuangalai kwa umakini palepale aligundua ni mwanamke mrembo sana alievalia mavazi mekundu ya mtindo wa kileo kama vile anaenda matembezini huku nywele zake zikipeperushwa na upepo.

“Ni wewe!”

Hamza aliweza kumfahamu msichana yule haikuwa mara yake ya kwanza kumuona , alikumbuka mara ya mwisho alimuona club.Hakika ni yule mwanamke mrembo aliekuwa akimwangalia sana lakini muda huo alitoa msisimko na kumfanya asionekane kuwa binadamu licha ya kuwa katika mwonekano wa kibinadamu.

Yule mrembo aliona namna Hamza anavyomshangaa na alimtingishia mabega kwa kumuonyesha ishara ya madoido kama vile anamwambia Hamza amemfananisha.

Muda ule Hamza alivyotaka kuongea kumuuliza kwanini amemshambulia aliweza kusikia sauti ya Mzee Farook kutoka nyuma yake.

“Ewe Nyakasura je ni Afande Simba aliekutuma kuja kuisaidia kambi yetu kudili na huyu kichaa?”Aliuliza kwa nguvu.

Hamza mara baada ya kusikia jina hilo palepale alielewa nini kinaendelea, alijiambia kumbe huyo ndio Nyakasura mwanamke ambae aliaminika kuwa mwanajeshi hatari ndani ya kitengo cha Malibu , ambae pia alitunukiwa cheo cha Askari wa taifa!. Ndio mara yake ya kwanza kumuona Nyakasura katika uhalisia wake, hakuonekana kuwa binadamu kama alivyowaza bali alitoa msisimko wa kiumbe ambacho hakuwahi kukutana nacho, pengine wafuasi hao walimwona kama binadamu lakini kwa Hamza ilikuwa tofauti.

Wafuasi wote wa kambi hio walijikuta wakiwa katika hali ya furaha baada ya kuona mwokozi wao amefika . licha ya kwamba karibia wote hawakuwa wakimfahamu kwa sura lakini wamezisikia sifa zake.

Nyakasura hakujibu swali la mzee Farook , alionekana kumdharau kuongea nae hivyo palepale alitoka juu ya paa na kushuka chini taratibu mithili ya malaika au jini na kwenda kukanyaga ardhi usawa na Hamza alipo.

“Ingawa huyo binadamu hana uwezo mkubwa na amekosa busara lakini bado ni kiongozi wa kambi ya Nyoka na ulinzi wake upo chini ya jeshi.Nimechelewa kidogo tu kufika lakini naona umefanya uharibifu mkubwa, nakushauri ni kheri uache mara moja..”Aliongea Nyakasura.

Hamza macho yake yaliishia kusinyaa , katika kukutana na mshindani wa daraja kubwa namna hio asiemjua asili yake hakutaka kufanya mambo kwa kukurupuka.

Alitaka kujua kwanza mpango wa Nyakasura kuja eneo hilo ni kumzuia tu au kushindana nae ndio achukue hatua.

“Nishawahi kusikia kuhusu jina la Nyakasura na kuambiwa ni msichana mdogo sana lakini sikutegemea ni kiumbe mrembo mno”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu akijaribu kutuliza hali.

“Hilo la mimi kuwa kiumbe mrembo halina ubishi , lakini hata hivyo siwezi kukurhusu kuendelea kufanya uharibifu hapa kwa gia yako ya kunisifia”Aliongea na jibu lake lilimfanya Hamza kucheka kisha akamjibu:

“Lakini pia unapaswa kujua kama nikiamua kumuua Farook hamtoweza kunifanya chochote”.

“Pengine inawezekana lakini ni mpaka utakapojaribu kufanya hivyo, wewe unajuaje kama siwezi kufanya chochote?”Aliuliza Nyakasura.

Hamza alianza kuhisi kadiri alivyokuwa akiongea na huyo mwanamke kivuli chake kilikuwa kikibadilika na kusababisha msisimko wa ajabu. Ilikuwa ni dhahiri alikuwa akiashiria hajafika hapo kwa ajili ya amani.

“Imani yangu inaniambia mimi na wewe hatujawahi kuwa maadui?”Aliuliza Hamza.

“Imani yako inakuambia kweli” Alijibu Nyakasura.

“Kama ni hivyo kwanini ulikuja Dar na kunifuata mpaka kwenye ile club na kuanza kunikodolea macho? Halafu sasa hivi upo mbele yangu ukiwa na nia ya uadui na mimi, Kwanini?” Aliuliza Hamza . Ukweli hakujua ni kitu gani ambacho mkuu wa majeshi Afande Simba alikuwa akimjulisha kumtuma kiumbe kama huyo kuja kuingilia mipango yake.

“Nakuuliza kwasababu kwa uwezo wako sidhani kama Simba anao uthubutu wa kukuagiza..”

Licha ya kuongea, mrembo Nyakasura alishia kupepesa macho yake tu , ijapokuwa yalikuwa yakivutia sana lakini hayakuwa yakiashiria chochote, ki-ufupi alikuwa katika mwonekano wa hali ya kawaida wa ubinadamu.

“Ninachotaka kufanya sihitaji ruhusa kutoka kwa Simba, nimekuja kujionea je ni kama watu wanavyokusifia”Aliongea

“Kwahio Himidu amekuambia kuhusu mimi?”Aliuliza Hamza.

“Ndio, ameongea sana kuhusu wewe ila sijawahi kumuamini”

“Kwanini?”Aliuliza Hamza.

“Kwasababu katika ulimwengu huu na umri niliokuwa nao hakuna binadamu wa kunizidi ki uwezo”Aliongea Nyakasura kwa kujisifia.

Hamza aliona licha ya mwanamke huyo kuwa mrembo ila vilevile alionekana kuwa kama chizi.

Ni kweli alijua msichana huyo hakuwa na asili ya kibinadamu bali asili yake ni ya damu ya ndege phoenix sifa inayompa kila kigezo cha kujiongelea hivyo lakini bado aliona anajipimia kwa vipimo vya juu sana, kitendo cha kutowahi kukutana maana yake bado hakuwa amekutana na wataalamu wengi zaidi duniani.

“Mimi na wewe hakuna uadui kati yetu , lakini kwanini unaniangalia hivyo, naona ni kama kwa muda mrefu sana ulipanga kupigana na mimi”Aliongea Hamza na kumfanya Nyakasura kupindisha mdomo kama wanawake wa kiswahili.

“Nakuangalia vibaya kwasababu nimeboreka”

“Umeboreka!?”

“Ndio! Mpaka sasa sijapata mshindani sahihi wa kupigana nae , hisia za namna hii zinachosha mno. Kwasababu Himidu amekusifia kwa kusema una uwezo mkubwa sana nimejikuta nikipata hamu ya kukutana na wewe ili tupimane”

“Kwahio kunifuata kote kwanzia kule club mpaka huku ilikuwa ni kwa ajili ya kukidhi haja zako za kupigana na mimi , tena nadhani si sawa kusema kupigana , ulikuwa ukitafuta kucheza na mimi?”Aliongea Hamza.

“Vipi haiwezekani sisi kucheza pamoja kwani?”

“Labda baadae tunaweza kucheza , kuna michezo mingi tunaweza kucheza pamoja ninayopenda, kama vile magemu na nk”

“Hio michezo mingi siitaki , ninachotaka ni mchezo wa mapigano basi”Aliongea na kumfanya Hamza kukosa neno la kuongea.

Upande wa wale wafuasi wa kambi hio walijikuta wakiwa katika bumubwazi , ukweli ni kwamba walijua Nyakasura amekuja hapo kwa ajili ya kumuua Hamza lakini ilikuwa tofauti , mwanamke huyo kaja kutafuta wa kupigana nae sio kutoa msaada.

“Nyakasura sina pingamizi kwa wewe kutaka kupigana na mimi , lakini kwasasa nina kazi , ngoja nimalize kumuua kwamza mzee Farook ndio tuanze huo mchezo”Aliongea Hamza na palepale aligeukia upande wa Mzee Farook alipo.

Nyakasura mara baada ya kuona vile palepale mkono wake ni kama ulianza kuwaka moto na ghafla tu donge la moto lilionekana katika viganja vyake na akalirusha kumlenga Hamza.

Hamza mara baada ya kuona shambulizi lile la moto palepale alifyatuka kulia na kukwepa, moto ule uliopotua chini ulitokea mlipuko uliosababisha mawe kuruka juu na miti kuanza kuungua.

“Nimekuambia nataka kumuua huyo mzee kwanza ndio tupigane , lakini mbona unaingilia? Si umesema umakuja kwa ajili ya mapigano”Aliongea Hamza.

“Mzee Farook tutamfanya kuwa tuzo kwa ajili ya pambano letu , nikikupiga na kukushinda atabakia kuwa hai ila ukinishinda unaweza kumua”Aliongea Nyakasura.

Kauli ile iliwafanya wafuasi wa kambi hio kuwa katika mshangao ,hawakuamini Nyakasura angemgeuza master wao kuwa kombe.

Mzee Farook mara bada ya kusikia hivyo alijikuta akisimama tu,hakutubutu kukimbia maana alijua anaweza kumkasirisha Nyakasura na kuishia kutupiwa moto.

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akighairi kwanza kuhusu Mzee Farook na usiriasi wake katika macho uliongezeka zaidi. Mwanzoni alikuwa na mpango wa kupigana na Nyakasura japo mara moja lakini hakudhania pambano lao litawahi namna hio.

“Nimekubali! Na mimi pia nina shauku ya kuona nguvu ya damu ya kiumbe Phoenix”

“Kama kweli unataka kuona nguvu ya damu ya kiphoenix itategemea kama unavyo vigezo vya kunifanya nitumie uwezo wangu wote”Aliongea Nyakasura.

Hamza palepale mwonekano wake uligeuka na kuwa wenye usiriasi baada ya kuona mwanamke huyo anamdhihaki kwa kumwambia hawezi kuonyesha uwezo wake wote . Lakini hata hivyo aliona ana haki maana moto aliokuwa akitengeneza ulikuwa mkali kiasi kwamba ulikuwa ukiyeyusha chuma.

Hamza na Nyakasura hatimae walikuwa sasa peke yao katika uwanja wa vita , kila mmoja akiangalia mbinu za mpinzani wake kitalaamu zaidi.

Mabadiliko ya miili yao hayakujificha kwa wale waliokuwa karibu lakini ukimya wao wa kutokushambuliana uliwafanya wafuasi wa kambi hio kushikwa na wasiwasi kubwa wasijue nini kinakwenda kutokea.

Mkandamizo wa hewa uliokuwa ukitokea katika mazingira hayo uliwafanya kujihisi ni kama vile vifua vyao vimebeba mzigo mzito ambao wanashindwa kuuhimili.

Hatimae hatua ya kwanza ya kusomana msisimko iliisha baina yao na wote kwa pamoja walijiandaa kwa kuanza kushambuliana.

Hamza alipiga hatua ya kwanza ya kuonekana na hatua ya pili spidi yake ilikuwa kubvwa mno kiasi kwamba hakuweza kuonekana vizuri huku akipanga kumshambulia Nyakasura na teke zito.

Nyakasura alisimama katika eneo moja wakati huo akiinua mkono wake wa kushoto uliokuwa ukitoa mwanga wa ajabu wa rangi ya dhahabu na kumfanya aonekane ni kama ameshikilia ngao ya mwanga.

Muda huo Hamza alihisi joto kali sana likisogelea mguu wake , lakini licha ya hivyo hakutaka kuacha kushambulia, tena aliongeza spidi maradufu na kwenda kuvaana na ile ngao ya moto ya Nyakasura.

Hamza aliamini ilimradi shambnulizi lake lina nguvu ya kutosha anaweza kusambaratisha kinga yake ile ya moto.

Nyakasura pia ni kama alikuwa ashajua kwamba ngao yake hio nyepesi isingetosha kumzuia Hamza kumpiga teke , hivyo alihepa kulia akinuia kukwepa shambulizi lile na wakati huo huo akitumia mkono wake wa kulia kumshambulia Hamza na donge la moto.

“Ungua…!!” Nyakasura aliongea kwa sauti ya chini na hapo hapo donge la moto lilimlipuka kutoka mkono wake wa kulia kama uwa la alizeti

Joto alilokuwa akizalisha mwanamke huyo ilifanya hata wale waliokuwa umbali mrefu wahisi ni kama wanaunguzwa na jua la utosi.

“Bam!

Hamza aliuvaa mkono wa Nyakasura na teke na kufanya kiatu chake na suruali kuungua.

Nyakasura baada ya kupigwa teke na kusukumbwa mbali na nguvu ile, alijihisi hali ya ganzi na nyusi zake zilitingishika ikionyesha dhahiri hakuwa akijisikia vizuri. Hamza mara baada ya kukanyaga chini baada ya kufanya shambulio hilo alijikuta akivuta pumzi nyingi sana huku akiangalia mguu wake ambao ulikuwa umeiva na kuwa mwekundu mno kama nyama ya punda kwa kuungua kwa ndani.

Ilikuwa bahati ana spidi kubwa la sivyo mguu wake ungegeuka rosti ya nyama.

“Umewezaje!” Nyakasura aliongea huku akiangalia mguu wa Hamza kutokea mbali na alishindwa kujizuia na kuonyesha hali ya mshangao.

“Unao uwezo wa kuhimili ‘phoenix flames?”Aliongea kwa mshangao.

“Kumbe ndio unaitwa Phonenix flames.. Hehe nilichokifanya ni kushambulia kwa spidi kabla sijaungua”Aliongea Hamza huku aking’ata meno akivumilia maumivu

Hamza aliona akiendelea kupigana kwa staili hio itakuwa ngumu sana kushinda hivyo anapaswa kuongeza spidi na kushambulia kwa kushitukiza.

Lakini tatizo moja ni kwamba Nyakasura alikuwa na uwezo wa kuhimili mateke yake ya tani ikimaanisha kwamba sio tu kwamba alikuwa na uwezo huo wa kimoto lakini vilevile mwili wake ulikuwa timamu.

Hivyo Hamza hakujua mapigo ya kushitukiza yanaweza kuwa na faida.

“Ukiachana na watu wa jamii yetu , wewe ni binadamu wa kwanza ambae umegusana na moto wangu bila ya kuungua . Hakika mwili wako sio wa kawaida kama binadamu wengine”Aliongea Nyakasura huku akionyesha mzuka sana wa kuendelea na pambano hilo.

Hamza mara baada ya kusikia maneno hayo alijihisi ubaridi na kujiambia kwanini mwanamke huyo ni kama anataka kumgeuza mdoli wa kuchezea.

“Ni zamu yangu kushambulia; Mijeledi miwili ya ngoma ya kifoeniksi!”

Sekunde ambayo Nyakasura alitamka hayo maneno alikuwa asharuka hewani huku mkononi akiwa ameshikilia mijeledi ya moto iliokuwa ikinesa nesa.

Kwa chini ilionekana ni kama Kamba ndefu zikidondoka kutoka juu angani.

Hamza alikuwa na kiatu mguu mmoja tu na mara baada ya kuona mijeledi ile ya moto inamsogelea alianza kuikwepa kwa spidi kubwa.

Lakini sasa ardhi ilikuwa ikiunguza mno kiasi kwamba baadhi ya mawe yalianza kuyeyuka na kufanya katika eneo hilo iwe ngumu kukanyaga.

Watu waliokuwa wakiangalia pambano hilo waliona ni kama vile pambano kati ya malaika na binadamu na kufanya wawe katika hali ya shauku mno kuona nani angeshinda pambano hilo.

Muda huo Nyakasura alikuwa akichezesha mijeledi ile ya moto huku akihama hama kwa kuruka na kumfanya aonekane kama kivuli chenye mikia.

Baada ya kuona Hamza anakwepa mashambulizi yake na hakuna namna ya kumfikia , alitua ardhini na kisha alichanua mikono yake kutoka chini kwenda juu huku akitoa sauti kubwa yenye mwangwi.

“Ngoma ya Wafoeniksi na Mvua ya moto!”

Mara baada ya kuongea hivyo palepale anga lilibadilika na kushusha mvua ya moto kama dhoruba ikimsogelea Hamza.

Hamza mara baada ya kuona vile aligundua hapo hana ujanja wa kukwepa shambulizi la aina hio na palepale alikimbia uelekeo wa majengo ya kambi hio na kuingia ndani ya jengo moja karibu yake. Nyakasura hakujali alimfukuzia huko huko huku akishusha mvua katika jengo aliloingia.

Hamza akiwa ndani alisikia harufu nzito sana ya bati kuungua na ndani ya sekunde chache tu alihisi uji uji ukimwangukia huku jengo lote likishika moto.

Mzee Farook mara baada ya kuona tukio hilo , alijikut akishikwa na furaha , palepale aliamini Hamza hachomoki , hakujali kuhusu jengo hilo kuungua ili mradi atakuwa hai maboresho ya kambi hio yataboreshwa. Isitoshe majengo hayo yalikuwa ya serikali.

Lakini upande wa Nyakasura bado aliamini Hamza yupo hai na palepale hakujali moto uliokuwa ukiunguza nyumba hio kwani alikimbia na kuingia ndani.

Moto ule haukuwa na madhara kabisa kwake , ni kama ulikuwa ukimuogopa na kumpisha apite.

“Hebu acha kujificha na toka nje!”Aliongea Nyakasura kwa nguvu na wafuasi wa kambi ile mara baada ya kusikia maneno hayo walishangaa na kujiuliza inamaana Hamza licha ya moto wote huo bado yupo hai.

Baada ya kuongea hivyo Hamza alifyatuka kwenye ziwa la moto ule kwa spidi kubwa akimlenga Nyakasura, miale hio ya moto ilionekana kutokuwa na athari yoyote katika mwili wake . licha ya kuonyesha ishara za kuungua lakini alionekana kutokuhisi maumivu.

Hamza hakutoka kizembe , alichomoka na shambulizi zito la ngumi ambalo alimpiga kiumbe huyo katika eneo la mbavu na kumrusha nje.

Nyakasura baada ya pigo lile la kushitukiza alipepesuka na kwenda kukanyaga kwa nguvu ardhini huku akimfyatulia Hamza moto kwa miguu yake lakini mwamba Hamza alikwepa kwa sarakasi, hata hivyo alishangazwa na wepesi wa Nyakasura kutoa moto kwa wepesi kupitia miguu.

“Unawezaje kutoa kwa urahisi namna hio?”Aliuliza.



SEHEMU YA 165

Hii mbinu tunaita nguzo ya moto, ndio msingi wa jamii yetu , ila naona sio haba kwako pia , unao uwezo wa kutembea juu ya moto”Aliongea.

Hamza huku akikunja sura , ijapokuwa aneo lote lilikuwa limezingirwa na moto lakini moto huo haukuwa wa kawaida lakini licha ya hivyo moto huo haukuwa tishio kwake.

“Nyakasura nadhani tuishie hapa . maana naona nashindwa kukusogelea kukushambulia, na mbinu zako pia haziniletei madhara , kama tukiendelea kwa staili hii ni ngumu kumpata mshindi”Aliongea Hamza.

“Sijatumia hata nusu ya uwezo wangu, nani kasema mshindi hawezi patikana?”

“Kwasababu hata mimi sijatumia nusu ya uwezo wangu”aliongea Hamza.

“Pumbavu!” Aliongea Nyakasura kwa kejeli.

“Kama huamini unaonaje ukitumia uwezo wako wote , kwanini unapoteza muda”

“Kwasababu naweza kukuua”

“Watu wengi washanitamkia hilo neno la kuniua lakini mpaka leo bado nipo hai”

“Kama ni hivyo basi nionyeshe sababu nijue kama kweli unastahili mimi kutumia uwezo wangu wote”

Mara baada ya kuongea hivyo , palepale Nyakasura alifyatuka kumsogelea Hamza kwa spidi huku akiwa amefunikwa na miale ya moto ,wakati huo huo akiwa ameshikilia mijeledi ya moto akipanga kumtandika nayo Hamza.

Hamza alikwepa mijeledi ile ya moto na haraka sana na kisha aliokota jiwe na akamrushia Nyakasura kumponda nalo.

Jiwe lile halikuwa dogo hata kidogo , lakini licha ya kumlenga nalo Nyakasura halikumfikia badala yake lilifunikwa na moto na kuanza kumeguka , ingawa halikumeguka lote kutokana na kuwa kubwa.

Mjeledi ule wa moto aliokuwa ameshikilia Nyakasura uligeuka na kuwa kama mkuki na kuligonga lile jiwe na kudondoka chini na kugeuka vipande vipande.

Hamza palepale alitumia nafasi hio kwa mara nyingine na kuchukua jabali lingine na kumrushia Nyakasura.

“Ngoma ya Wafoeniksi Pigo la radi!!

Nyakasura mara baada ya kuongea vile palepale mijeledi ile ya moto iliokuwa katika mikono yake iliungana kwa kusuguana na kuanza kutengeneza cheche za nishati ya ajabu kama ya umeme . kila kitu kilitokea ndani ya sekunde tu.

Mara baada ya kugeuza moto wake na kuwa kama radi alilenga lile jiwe na mara baada ya kugusana ulitokea mlipuko mkubwa wa bomu.

Boom!!

Jabari lile lilisambaratishwa na kuwa vipande vipande . Shambulizi la Hamza likawa limefeli na aliishia kuruka kujitenga mbali na mlipuko ule. Nyakasura pia jasho lilianza kumtoka na macho yake yalipepesa kwa haraka wakati akimwangalia Hamza.

Kawaida hakupaswa kutumia mbinu hio ya pigo la radi kwa mtu kama Hamza kutokana na nguvu yake ya uharibifu,ukweli ni kwamba hakuwahi kutumia pigo hilo kwa binadamu lakini kutokana na Hamza kuwa na mwili usioumia alijikuta akilazimika kufanya hivyo.

“Nyakasura naona kukusogelea imekuwa ngumu kabisa”Aliongea Hamza huku akitingisha kichwa.

Hatimae alikuwa ameielewa nguvu ya Wafoeniksi, Kiumbe huyo katika ubinadamu, ukiachana na kuwa na mwili ulioimara na kuwa na spidi kubwa ya kujibu mashambulizi, kubwa zaidi ni kwamba hakuonyesha udhaifu kabisa katika mbinu yake ya kucheza na moto.

Uwezo wake wa kucheza na moto , ulikuwa ni muunganiko wa mbinu ya kushambulia na kujilinda kwa wakati mmoja . Kuhusu mbinu yake ya Phoenix Dance, kulikuwa na mengi yenye kubadilika , ilikuwa ni mbinu hatari sana ambayo inamfanya kuwa na uwezo wa kushambulia kwa mbali.

Hamza yeye uwezo wake wa kushambulia ulikuwa ni wa kibinadamu zaidi , alitegemea nguvu zake za mwili katika kushambulia hivyo ili afanikishe alihitaji kumsogelea karibu Nyakasura jambo ambalo lilionekana kuwa gumu.

Kibaya zaidi ni kwamba, Nyakasura mbinu zote alizoonyesha zilikuwa ni za kawaida sana . Bado hajatumia uwezo wake halisi katika mashambulizi .

“Ni ngumu sana pia kukushambulia , ingawa umekosa mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi lakini umebarikiwa miguu yenye nguvu kubwa sana kiasi kwamba spidi yako ya kukimbia nashindwa kuhimana nayo. Unakimbia kama Jini Pepo”Aliongea Nyakasura.

“Unamaanisha nini kusema nakimbia kama Jini pepo, kwani hakuna namna nzuri ya kufananisha kukimbia kwangu . Kusema nakimbia kama pepo kwanini nahisi kama unanitukana”Hamza alilalamika.

“Una spidi kama Jini pepo”Aliongea Nyakasura akimpotezea .

“Sasa kama unajua huniwezi kunikamata likija swala la spidi , kwanini bado unataka tuendelee kupigana ilihali hakutokuwa na matokeo. Kwanini tusiishie hapa?”Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu.

“Ijapokuwa siwezi kukukamata kwa spidi yako , huwezi kuondoka hapa kama bado unapanga kumuua Mzee Farook. Hivyo huna namna zaidi ya kuendelea kupigana na mimi mpaka nishinde”.

“Tufanye makubaliano mengine , nipo tayari kukubali siku nyingine turudie kupigana na tutaweka tuzo nyingine”Aliongea Hamza.

“Hapana ! Sitaki”Aliongea huku uso wake ukigeuka na kuwa wa kikauzu zaidi.

“Bila kukuunguza mimi na wewe kupigana hakujaisha”Aliongea

“Kuniunguza , ukiniunguza si utaniua?”

“Hata ukifa sijali. Leo ni mpaka mshindi apatikane”

“Wewe kwaninii unang’ang’ania iwe leo , tunaweza kupanga siku nyingine, nyie wanawake mna nini kwani?”Aliongea Hamza maana alikuwa amechoka kweli kushindana na Nyakasura , haikueleweka alikuwa akimugogopa au vipi.

“Sisi wanawake ndio tulivyo, lazima leo ajulikane mshindi hata kama tutakesha hapa”Aliongea na palepale kwa mara nyingine alimsogelea Hamza kwa ajili ya kuanza mashambulizi.

Nyakasura alifyatuka kwa sakari mzunguko kama mara tatu hivi na kisha alitengeneza mpira wa moto, kama vile ni mchezaji alipiga teke mpira ule wa moto kumwendea Hamza.

Wakati huo huo akiongea maneno ambayo hayakueleweka na ghafla tu ule mpira wa moto ulibadilika na kuwa kimbunga cha moto ambacho kilizidi kukua kadri kilivyokuwa kikikusanya upepo.

Hamza mara baada ya kuona jambo hilo aliishia kung’ata meno huku akijiambia haamini kama maajabu hayo ya moto kutoka kwa huyo mwanamke yana mwisho wake.

Hamza mara baada ya kuona vile hakutaka kusubiri moto ule wa ajabu kumvaa na palepale alitimua nduki kuelekea ndani ya majengo ya kambi hio.

“Acha kukimbia wewe mshenzi muoga sana”Aliongea Nyakasura kwa hasira huku na yeye akianza kumfukuza.

Mwili wake wote ulikuwa umefunikwa na moto na kuwa kama jua na kumfanya kadri alivyokuwa akimfukuza Hamza ndio alivyozidi kutengerneza machafuko ya moto ndani ya kambi hio.

Kitendo cha kufukuzana katika mejengo ya kambi alipelekea kuharibu mazingira yake kwa kuyaunguza , kama sio majengo mengi kujengwa kwa mawe yangeshabomoka kabisa.

Mzee Farook na wenzake kuona namna kambi yao inavyoteketea kwa moto walijikuta wakitamani kutoa kilio . Uvumilivu uliwashinda na kujikuta wakipiga magoti na kuanza kumuomba Kiumbe Nyakasura aache anachokifanya kwani anazidi kuharibu eneo hilo.

“Ee Nyakasura tunaomba usitishe…!!” Waliongea lakini sasa Nyakasura hakuwasikiliza.

Baada ya kukimbizana kwa nusu saa hatimae kambi karibia yote ilikuwa ikiteteketea kwa moto na kufanya ionekane ni kama mlima wote ulikuwa ukiungua .

Mpaka kufikia hapo wafuasi wa kambi hio wasingeweza kuendelea kukaa hapo tena , hivyo walikimbilia chini ya mlima.

Nyakasura baada ya kuona anashindwa kumkamata Hamza zaidi ya kusababisha moto aliishia kusimama katika sehemu moja huku akihema kwa nguvu na kung’ata meno kwa hasira huku akimwangalia Hamza kwa chuki.

“Kiumbe Mrembo nadhani hii inatosha sasa , kwa uwezo wangu wa kukimbia hata kama wewe sio binadamu utaishia kuchoka tu. Unaonaje ukirudi nyumbani uoge utakate kisha ulale kidogo na usipoteze muda juu ya jambo hili dogo”Aliongea Hamza kwa kubembeleza.

Mara baada ya wafuasi wa kambi hio kusikia Hamza akiongea hivyo walimuunga mkono palepale.

“Ni kweli Ee Nyakasura , tupo tayari kumtoa Mzee Farook kuchukuliwa na Hamza . hatuwezi kuendelea kuona unauguza kambi yote”Sauti ilisikika.

“Mjomba!!”Aliita Mzee Farook akionekana mwanaume mtu mzima mwenye mvi kichwani akiwa amesimama. Mzee huyo alikuwepo hapo muda mrefu ila kutokana na watu kuwa bize kuangalia pambano hawakuwa wamemuona. Ndio mzee ambae Master Farook alimwita kwa ajili ya kuomba msaada.

Mjomba huyo alishukuru hajapigana na Hamza maana kwa show aliokuwa akiangalia licha ya kuwa na uwezo kumzidi Farook lakini bado aliona Hamza sio saizi yake.

Sasa muda huo huyo mzee baada ya kuona namna kambi hio ilivyokuwa ikiteketea kwa moto aliona msababishaji mkubwa ni Farook kwa kuwa na maamuzi ya kukurupuka, ndio maana alisema kama Nyakasura angekubali kuacha Hamza angepatiwa Farook amuue tu.

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio licha ya kutokumjua huyo mzee , alijikuta akisikia furaha, hakuona haja ya kuendeleza mapigano hayo kama kambi hio ipo tayari kumpatia Mzee Farook na mwanae Fabiani.

“Nani kawaambia nimechoka?”Aliuliza Nyakasura huku sauti yake ikitoa mlio flani wa kuumiza masikio kama vile ni maiki mbovu.

“Subirini muone”Aliongea na palepale alifyatuka na kwenda kutumbukia kwenye lindi la moto katika nyumba zile za kambi.

Mara baada ya kuingia katika ule moto cha kushangaza nguo zake nyekundu hazikuungua kabisa , kinyume chake ile miale ya moto iligeuka na kuwa kama vile ni roho na kuanza kumwingia Nyakasura kupitia macho, pua na mdomo. Kadri alivyokuwa akihema moto ule ulizidi kuingia na kumfanya aonekane kiumbe wa ajabu mno, alidhihirisha kabisa hakuwa binadamu.

Baada ya kutoka katika moto ule , ile hali ya uchomvu aliokuwa nayo ilimpotea kabisa na kuonekana kama kazaliwa upya . Tukio lile liliwashitua wafuasi wote akiwemo Hamza.

“Huo nii… ni kama inavyohadithiwa..!”Aliongea Hamza kwa mshangao.

“Usishangae,hii ndio asili ya damu yetu , tumeumbwa kwa moto na majivu na tunazaliwa upya kupitia moto na majivu, ‘Fire and Ashes Rebirth’” Aliongea Nyakasura.

“Sikutegemea ni kweli .. hakika ina tisha”Aliongea Hamza huku akikumbuka stori kadhaa kuhusu kiumbe Foeniksi(Phoenix), inasemekana kwamba kiumbe huyo hata kama awe amekufa akiweka karibu na moto au majivu anapona mara moja na kuwa mpya ili mradi nafsi yake iwe haijapotea.Ukweli ni kwamba hakuna anaejua kama njia hio ni kufufuka ama ndio kuzaliwa upya lakini katika simulizi zao kiumbe Phoenix hakuwahi kufa.

Ili mradi kuwe na moto au majivu ya kutosha anao uwezo wa kurudisha uwezo wake wote au uhai,chakula cha viumbe hao si hiki cha kibinadamu bali ni moto na majivu.

Nyakasura sasa baada ya kutoka katika huo moto alikuwa mpya kabisa na msisimko katika mwili wake uliongezeka maradufu huku akizidi kuonekana kujiamini.

“Enhe umesema bado unajihisi kuwa na nguvu za kutosha ? Ni muda wa kuona nani ataanza kuchoka”Aliongea Nyakasura na kumfanya Hamza kutoa tabasamu lililojaa uchungu.

“Kushindana kwa namna hio sio haki , kwahio kila ukichoka utaingia kwenye moto na kurudiwa na nguvu zako? Kufanya hivyo haitoletea maana tena”Aliongea Hamza akilalama kama vile anaonewa.

“Usiwe na wasiwasi , nitakuambia namna ya kunishinda , kwanza hakikisha unanizuia nisiingie katika moto na sitoweza kupona , pili niue kwa pigo moja tu na hakikisha nafsi yangu haigusani na moto wala majivu na kupelekea kuzaliwa upya. Nadhani utaweza kufanya hivyo?”Aliongea

Hamza alijikuta akishika kiuno. Ukweli ni kwamba hakuwa kabisa na uhakika wa kumshinda Nyakasura, vipi kuhusu kuua mwili wake na nafsi kwa wakati mmoja na kumzuia asigusane na jivu wala moto, inawezekana vipi?.

Kuhusu pia kumzuia asigusane na moto ni swala ambalo haliwezekani maana muda huo ni kama amejitengenezea bahari ya moto kwani kila mahali kuzunguka, moto ulikuwa ukiwaka na kama wataendelea kupigana katika mazingira hayo wanaweza kupigana mwezi mzima.

Ijapokuwa Hamza mwili wake ulikuwa umepita asili ya ubinadamu lakini asingeweza kupigana na kiumbe huyo kwa zaidi ya mwezi , hivyo ni hakika angekufa wa kwanza.

“Hakuna namna nyingine tukazungumza?’Aliuliza Hamza kinyonge huku akijishika paji la uso.

Kwasababu alisafiri mpaka kuja ndani ya hio kambi hakutaka kuondoka bila kumshughulikia Mzee Farook na mtoto wake. Aliogopa kama angewaacha hai kuna uwezekano wakalipiza kisasi kupitia watu wake wa karibu.

“Hakuna namna , umenikasirisha sana hivyo ninachotaka ni kukuunguza tu basi”Aliongea.

“Nikiamua kukimbia huwezi kunikamata , kwanini unahisi naweza kuendelea kupigana na wewe?”

“Nitahakikisha hupati hio nafasi ya kukimbia”Aliongea na palepale mwonekano wake ule wa kibinadamu ulimpotea na sasa kudhihirisha ukuu wake na macho yake yalibadilika kutoka kuwa ya kawaida na kuwa ni yenye kuwaka moto.

Muda uleule alionekana kuwa na kitu kama kisu kidogo mkononi cha madini ya jedi na alishika kidole gumba na kisha alikata eneo la juu la kidole na kufanya tone la damu ambayo sio nyekundu lilitoka , ilikuwa ni damu ya rangi ya njano.

“Damu ya Kifoeniksi!” Hamza alipaniki huku akihisi utosi wa kichwa chake kuwasha, “Usiniambie unapanga kutumia uwezo wako wote kushindana na mimi?”Aliuliza Hamza na Nyakasura hakujibu badala yake alidondoshea tone la damu ile katika kiganja cha mkono wake na alianza kuongea lugha isioeleweka na maneno ya mwisho pekee ndio yaliwezekana kutafisirika.

“Hati takatifu ya mbingu tisa, Damu inayoungua!” Aliongea hivyo akionekana kama vile anasali lakini haikuwa hivyo.

Ngoma takatifu ya Wafoeniksi ya mbingu tisa ndio daraja la juu sana la mapigano ambalo Nyakasura alipata kujifunza chini ya umiliki wa damu yake hio ya kifoeniksi. Ukilinganisha mbinu hio na Hati ya mbingu tisa, maajabu yanazidi kiasi kwamba ni ngumu kuukadiria uwezo wake wote kupitia hati hio ya mbingu tisa kwani kila ujazo wa mbingu moja una uwezo wake tofauti.

Sasa mara baada ya Nyakasura kuongea maneno yale mwonekano wake ulibadilika na kuwa wa tofauti kabisa kuliko mwanzo . Joto la miale ya moto wake liliongezeka mara tatu zaidi na mara baada ya lile tone la damu kuungua lilibadilika na kuwa moto uliosambaa mwili mzima kama vile alikuwa akijiogesha.

Nywele zake na weusi wake wa kibindamu ulipotea na alionekana mweupe wa kumeta meta , ikiwa ngumu kuelezea ndio uhalisia wake au ni kwasababu ya ule moto. Hata sauti yake ilibadilika kabisa na kila neno lake lilitingisha moyo.

“Unapaswa kujivunia kwa hadhi yangu kuamua kupigana na wewe kwa uwezo wangu wote”Aliongea huku sauti yake ikijirudia tudia masikioni.

Palepale moto ulifuka katika mkono wake na kisha aliurushia kuelekea katika nyumba ambazo hazikuwa zimeungua bado. Baada ya wale wafuasi wa kambi hio kuona jambo hilo palepale walishikwa na kiwewe.

Hawakuamini Nyakasura anaweza kuwa na huruma juu yao tena , kwani alibadilika kabisa. Haikuwa hofu tu hata kupumua kwao ilikuwa shida . Hata yule Mjomba ambae alikuwa na uwezo kumzidi Farook alianza kukohoa kwa kushindwa kupumua.

Mtu pekee ambae hakuteswa na mazingira yale ni Hamza pekee ambae alikuwa akimwangalia Nyakasura sio kwa hofu bali kwa shauku kubwa , alishindwa kujizuia kuukubali uwezo wa kiumbe huyo mwenye mwonekano wa ubinadamu na kujiuliza imekuwaje akawa katika mazingira ya Tanzania tena sehemu ya jeshi.

“Enyi Wafuasi wa ufunuo wa Nyoka nisikilizeni , kimbieni kutoka katika hili eneo! Haya mapigano sio ya levo za ubinadamu na tunaweza kufia hapa hapa”Aliongea Mjomba kwa sauti na kauli yake ilitikiwa na wafuasi wote walioanza kutimua nduki kushuka mlima huo.

Mzee Farook mara baada ya kuona hivyo , aliishia kumwangalia Hamza kwa macho makali. Alifikiria nafsini mwake kwamba Hamza anapaswa kuunguzwa na moto wa kiumbe huyo na ndio itakuwa halali yake na mara baada ya kuwaza vile aligeuka kwa ajili ya kukimbia na yeye.

Lakini angejuaje kama Hamza bado hakuwa amemsahau . Baada ya kumuona anataka kukimbia aligeuka haraka.

“Mzee Farook unakimbia kwenda wapi?” Aliuliza.

Nyakasura ni kiumbe wa aina gani kama sio binadamu vipi kuhusu Prisila?

Hamza hana nishati za mbingu na ardhi kama ilivyokuwa Roma , anategemea ubinadamu kushindana. Unadhani atapona?Naziona nyama kwa mbali.

ITAENDELEA Alhamisi
U*na maoni yoyote , unahitaji kuendelea , nitafute watsapp 0687151346.
𝕄𝕜𝕦𝕦 𝕞𝕓𝕠𝕟𝕒 𝕙𝕒𝕦𝕡𝕒𝕥𝕚𝕜𝕒𝕟𝕚 𝕦𝕫𝕚𝕞𝕒 𝕦𝕡𝕠𝕠
 
SHETANI RUDISHA NAFSI ZETU.

MTUNZI:SINGANOJR.

SEHEMU YA 166.
Kimulimuli Gizani.
Hamza alianza kumfukuzia Mzee Farook , huku akimpotezea Nyakasura na moto wake . Alijiambia hata kama akifa lazima amuue kwanza Master Farook.
Lakini hata hivyo kabla hata hajamfikia , Mzee Farook alitupiwa moto na Nyakasura kwa spidi ya juu kiasi kwamba ulitoboa tumbo lake na kilichoweza kusikika ni ‘puch’.
Mzee Farook aliishia kugeuza uso wake kumwangalia Nyakasura na alijikuta akitoa ukulele wa kutotaka kufa na palepale alidondoka chini na kuanza kuungua.
Mwili wake wote uliunguzwa na moto wa Nyakasura kiasi kwamba ni kama amemwagiwa petroli na ndani ya sekunde kadhaa aligeuka majivu.
“Nilikuambia usiondoke , ina maana hukuyachukulia maneno yangu kwa uzito . sasa ni zamu yako kuungua na wewe”Aliongea Nyakasura.
Hamza aliishia kuachama kiasi . Ingawa aliweza kuhisi kitu kikija kutoka nyuma yake , lakini hakuhisi hatari ikimaanisha yeye ndio hakulengwa, lakini alishangaa kuona Nyakasura ndio amemuua Mzee Farook.
Ilishangaza kwasababu Nyakasura ndie aliekuwa akimzuia kutokumuuwa mzee huyo lakini muda huo ni kama amebadilika na hakujali tena kuhusu sheria . Alichokuwa akitaka muda huo ni kupigana basi.
Kuwa na nguvu kubwa hutengeneza ukiburi na hilo ndio alionyesha Nyakasura kiumbe Foeniksi.
“Nyakasura kuna ulazima wa sisi kuendelea? Farook amekufa hivyo mimi naondoka”Aliongea Hamza huku akijiambia kuhusu Fabi hana haja ya kuwa na wasiwasi , kwasababu bila ya baba yake maana yake hakuwa na nguvu yoyote.
“Usijifanye sijui hujapigana na mimi ukiwa siriasi wakati mimi nikikuonyesha nia yangu ya dhati. Ukikimbia wewe sio mwanaume”Aliongea Nyakasura kwa kejeli huku akiinua kichwa chake , moto uliokuwa umezingira mwili wake ulikuwa ukitisha na haikueleweka alikuwa akiwezaje kuudhibiti.
Sehemu tu aliokuwa amekaa kila kitu kumzunguka kilikuwa kikiungua m alikuwa ni kama jua linalotembea , kama mfalme wa ndege wote.
Hamza alishindwa kujizuia na kuishia kutetemeka mwili mzima , hisia za kuwa na mwili kama wake mbele ya kiumbe huyo ilimfanya damu kuchemka na vinyweleo kusimama.
Mpaka hapo busara aliona ni kukimbia na ndio anaweza kupona katika hali hio. Aliona hakuwa na haja ya kuhatarisha uhai wake kudili na kiumbe ambae hakuwa binadamu , maana aliona ili mradi akiwa karibu na moto hawezi kufa.
Lakini licha ya hofu hio aliokuwa nayo , lakini ndani kabisa katika moyo wake asingeweza kukimbia , hadhi yake na utu wake kama mtaalamu wa mapigano ilikuwa imeguswa haswa . ile hali ya kutaka kuendelea kulinda hadhi yake hakutaka kuipoteza kwasababu tu ya miaka mitatu ya kuwa nje ya ulingo.
“Kwasababu umesema mwenyewe basi sina budi zaidi ya kupambana na wewe”Aliongea Hamza na palepale aliinama na kuangalia mwili wake. Nguo zake zote zilikuwa zimeungua na kubakia uchi lakini kwa Nyakasura hakuona tashwishwi ya aina yoyote . Alionekana alikuwa mzoefu wa kuona watu wakiwa uchi.
Ilikuwa ni bahati tu kwamba wao pekee ndio walikuwa juu ya mlima la sivyo ingekuwa kadhia ya mwanaume ambae yupo uchi anapambana na kiumbe mrembo.
Hamza aliishia kutingisha kichwa chake akipotezea mawazo hayo na kisha palepale alivuta pumzi nyingi na kuzishusha mara kadhaa na kadri alivyokuwa akifanya hivyo mpangilio wa pumzi yake ulianza kubadilika , mwanzoni alianza kupumua kwa haraka kama binadamu lakini muda huo alikuwa akitumia muda mrefu kupumua na kushusha pumzi.
Muda ule mwili wa Hamza misuli yake ilianza kutanuka kwa kasi na viungio vya mifupa katika mwili wake vilipiga kelele. Dakika ambayo Hamza aliyafumbua macho , yalikuwa yameingia ndani kwa kuwa siriasi na alipiga hatua moja na kukanyaga chini kwa nguvu.
Boom!
Kitendo cha kukanyaga chini kulitokea kishindo kizito na ardhi ilibonyea kwenda ndani na kutengeneza shimo.
Misuli yake ya kiuno ilionekana kuunganika moja kwa moja na mapaja yake , miguu na hata vidole na kumtengenezea muunganiko mkubwa wenye nguvu.Kila wakia(ounce) ya nguvu ya msuli wake ilikuwa imeungana pamoja na kutengeneza mkusanyiko wa nguvu ya juu.
Kuona vile Nyakasura macho yake yalisinyaa na alijikuta akitingisha kichwa huku akimwemwesa maneno.
“This is very interesting…”Aliongea.
Hamza hakuongea neno , kwa hatua moja alimsogelea Nyakasura bila ya kujali moto wake.
Kwa mbali ilikuwa ni kama vile jua halitaki kupatwa. Miale ya moto ya Nyakasura ilimfunika Hamza na kuunguza kila kitu . Lakini spidi ya Hamza ilikuwa sio kidogo , alikuwa kama mwanga na kumfanya Nyakasura kushindwa kuendana nae kutokana na miale yake ya moto ilitembea katika spidi ya mkondo wa hewa.
Hamza alikuwa akitumia uwezo wake wa kujongea kwa spidi kukwepa miale ya Nyakasura.
Nyakasura upande wake alionekana ni kama ashajua tatizo hilo na hakumfukuzia Hamza na badala yake alisimama katika eneo moja huku akisambaza miale pande zote.
“Ah!
Hamza alinguruma akiamua kuikaribisha baadhi ya miale ambayo aliona hawezi kuikwepa na muda huo huo alisogea kwa spidi kubwa kumshambulia Nyakasura na teke , akilenga maeneo dhaifu ya mwili wake.
Nyakasura mara baada ya kuona Hamza amefanikiwa kupita katika moto wake na sasa anamsogelea , alijikuta akishituka lakini hakutaka kusubiria kizembe.
“Mbawa mbayumbayu!”
Mara baada ya kuongea hivyo ghafla tu moto wake wote ulimfunika na kugeuka mbawa ambazo zilimpaisha kukwepeshwa na shambulizi la Hamza.
Hamza kuona hivyo alijikuta akishikwa na mshituko . Alijikuta akimwangalia Nyakasura akipaa kwenda angani na mbawa zake kwa spidi kubwa kiasi kwamba ndani ya sekunde tu alikuwa mita kadhaa mbali, na kumfanya aonekane kama malaika wa moto.
“Damn.. unaweza hata kupaa!!”
Hamza alijikuta akiamini uwezo wa damu ya kifoeniksi haukuwa wa kawaida kabisa . Ilikuwa kheri kama damu hio ingekuwa na nguvu pekee lakini ilikuwa na nguvu za kimitego nyingi za siri. Hamza yeye hakuwa na uwezo wa kupaa bali alikuwa na uwezo wa kuruka na kama Nyakasura anao uwezo wa kupaa watawezaje kuendelea kupigana.
Nyakasura akiwa hewani alikusanya donge kubwa la moto na mara baada ya kulichezesha kwa sekunde tu liligeuka na kuwa mkuki na kurushia sehemu alipo Hamza , mkuki huo kwa namna ulivyokuwa ukikata hewa ulikuwa ukitoa mlio kama wa ndege Mwewe , lakini sauti yenye kuumiza masikio.
Hamza mara baada ya kuona siraha hio hakuthubutu kabisa kuisogelea karibu na haraka sana alikimbia mbali.
Sekunde mluki ule wa moto ulivyochoma ardhi ulitengeneza wimbi kubwa la moto na kuyeyusha kila jiwe lililokuwa pembeni na kutengeneza shimo.
Nguvu hio ya uharibifu binadamu angeweza kuishuhudia angezimia hapo hapo. Lakini kwa Hamza hakuwa na muda wa kujali sana kuhusu maajabu hayo kwasababu Nyakasura alikuwa akimsogelea kwa kasi na mbawa zake za mbayumbayu.
Hamza aliamini kama akikutana moja kwa moja na nguvu hio ya mbawa inayomsogelea anaweza akawa katika hali mbaya. Kwa macho yake makali aliona kisima cha kuhifadhia maji nyuma ya nyumba za kambi hio zilizoharibika na bila ya kujiuliza mara mbilimbili alitimua mbio kukisogelea.
Nyakasura mara baada ya kuona Hamza anakimbia , alimfukuzia kwa nyuma kwa spidi kubwa huku akirefusha moto wake na kugeuza kuwa mkuki wa mita kadhaa.
Ile Nyakasura anataka kumkaribia Hamza kumchoma na ule mkuki mgongoni, Hamza aliwahi na kama mshale alitumbukia ndani ya kile kisima ‘chubwii’ na kula mbizi na kukoswa koswa na shambulizi.
“Unadhani utakuwa salama ukiingia kwenye maji?”Aliongea Nyakasura na palepale alinyoosha mkono wake na kushika ukuta wa kisima kile huku akisambaza moto mkali na ndani ya sekunde tu kisima kile mawe yake yalianza kuyeyuka huku maji yakianza kushika mvuke.
Muda huo huo Hamza alifyatuka kutoka kwenye kisima hicho kama Samaki na ile anafika nje alimtemea Nyakasura maji mengi kama Kiboko.
Hamza baada ya kufanya vile hakujua acheke ama alie, alidhania akimtemea maji Nyakasura angeuzima moto wake na kumfanya kuwa dhaifu lakini alijisumbua tu . Kwa alivyoona hata kama ingekuwa ni bahari pengine asingezimika.
Hamza palepale aliachana na mbinu ya kufikiria namna ya kuzima moto wake na badala yake aliona namna ya kushinda ni kupigana nae moja kwa moja na hapo ndipo vita ya mvutano ilipoanza.
Hamza alitumia uwezo wake wa kukimbia kumuacha mbali adui yake na wakati huo Nyakasura aliendelea kumfukuzia Hamza huku akimtupia moto na kukwepa mashambulizi yake ya kushitukiza.
Yalikuwa ni mapigano ya kwenda mbele na kurudi nyuma na hakuna alionekana kushinda ama kupoteza pambano.
Baada ya dakika kumi za mvutano , Hamza alikuwa na majeraha mengi ya moto katika mwili wake , huku upande wa Nyakasura akiwa amepigwa mara kadhaa na ilikuwa bahati hakupokea shambulizi la moja kwa moja.
Hamza ili kumshambulia Nyakasura ilibidi ajitoe muhanga wa kuunguzwa na moto lakini wakati huo huo akihakikisha shambulizi lake linamfikia kisawa sawa.
Hamza mara baada ya kutua chini baada ya kufanya shambulizi aliishia kuangalia mikono yake iliogeuka na kuwa mieusi kwa kuungua na alijikuta akipata msongo wa mawazo.
Nyakasura nguvu zilikuwa zimempugnua pia na alikuwa akihema kwa kuitafuta hewa , mbawa za moto alizokuwa nazo zilikuwa zimepotea pia.
“Nyakasura ni muda wa kuacha sasa , tukiendelea hivi tutakufa”Aliongea Hamza.
“Bado mshindi hajapatikana” Aliongea Nyakasura na palepale alivamia jengo la nyumba iliokuwa ikiwaka moto na kwenda kuoga moto.
Hamza mara baada ya kuona hivyo machozi yalitaka kumtoka . Alijiuliza huyu mwanamke anajaribu kufanya nini , wamepigana muda mchache tu lakini bado anataka kujirudisha katika hali yake ya kawaida.
“Hey! Kwa staili hio unadhani utachukua muda gani kumaliza kupigana?”Aliuliza Hamza na Nyakasura hakujali zaidi ya kuvuta pumzi ya moto na ndani ya dakika alitoka akiwa na ari mpya kwa ajili ya kuendelea kupigana.
“Usiwe na wasiwasi maana haitochukua muda mrefu nitakuwa nishakupiga”Aliongea Nyakasura akiwa katika hali ya kujiamini.
“Sidhani kama itawezekana ..”Aliongea Hamza.
“Nini! Usiniambie una mbinu ambayo hujaitumia bado?”Aliuliza Nyuakasura huku akionyesha ishara ya kutokuamini lakini bado aliamini kwa wakati mmoja.
Kwa mtazamo wake , mpaka Hamza kumlazimisha kuoga mara mbili katika moto haikuwa kawaida, ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na binadamu wa daraja la uwezo huo.
Hamza alifanya maamuzi katika moyo wake , uwezo wa kukimbia alikuwa nao , lakini hakutaka kufanya hivyo na njia pekee ya kushinda pambano hilo ni kutumia uwezo wake wa juu sana kumshikisha adabu vinginevyo licha ya kwamba alikuwa na mwili wa kuvumilia maumivu ya kuungua lakini isingekuwa vizuri kuendelea kuunguzwa.
“Ni mara yangu ya kwanza nakwenda kutumia hii mbinu ambayo nimeielewa kwa ufupi sana zidi yako kiumbe Phoenix ,. Sipo tayari kudhalilika nadhani pia hutojilaumu mwishoni”Aliongea Hamza.
Muda uleule mwili wake ulifunikwa na kivuli cha ajabn huku hewa kuzunguka ilianza kutingishika kama vile ni gesi inasambaa angani.
Hamza mwili wake ulianza kudunda kama vile misuli imegeuka na kuwa moyo, ilionekana ni dhahiri ni kama kuna kitu ambacho kipo ndani yake na kinataka kutoka.
Nyakasura alijikuta akikunja ndita . Alijikuta akihisi kuna kitu hakipo sawa kuhusu Hamza licha ya kuwa mbali,mapigo yake ya moyo yalibadilika.
Aliona Hamza ni kama alikuwa amefanana na anga linalomzunguka . Na sehemu aliosimama ni kama vile anga lake linadondoka chini.
“Decompose!”
Aliongea Hamza isieleweke anamaanisha nini na palepale alianza kutingishika kama vile anacheza kibwebwe huku akitamka maneno. Maneno ambayo alikuwa akitamka ni yale ambayo Yonesi alimpatia akimwambia kwamba aliokota maandishi yale jangwani katika misheni ya kijeshi.
Hamza hakuwahi kutumia maandiko yale tokea mara ya mwisho alivyojaribu kujifunza na kumuona mwanamke katika ndoto , sababu ya kuhisi muda huo ni wakati wa kutumia sio kwamba alikuwa na uhakika ila alipanga kujaribu akiwa katika hali ya juu sana ya uwezo wa mwili wake , kwani siku ile hisia alizopata ni kama akili yake ilitawaliwa na mdudu. Moja ya kanuni ya mafunzo ambayo yanajumlisha na nguvu ya kiroho , ili kupata majibu unayoyataka ni lazima kwanza consciosness yako iwe katika hali ya uamko(Active) ili kunyonya nguvu yoyote bila kuathiri nafsi yako. Mbinu hio wataalamu wa mafnnzo hayo wanaita Mgawanyiko wa nafsi na Roho (Soul and Spirit Disintergration).
Mbinu hio hata hivyo ilikuwa na hasara zake , kwasababu inatengeneza mlipuko wa nguvu ya ndani kutokana na kwamba nafsi na roho kiungo chake kikuu ni damu.
Hamza hakujali chochote, muda huo alitaka kuamsha uwezo wake wote wa damu kwa kuichanisha nafsi yake na damu ili kutengeneza mwili ulio huru. Mtego wa nguvu ya miili yetu upo katika nafsi zetu na roho , kuishinda nafsi maana yake ni kujiweka huru.
“Ah!”
Hamza alijikuta akipiga makelele huku akiangalia hewani , macho yake ni kama hayakuwa yake bali yameshikiliwa na kiumbe kingine na lile eneo alilokuwa amesimama lilianza kutitia na kufanya mawe kuporomoka.
Jambo lile lilimshangaza Nyakasura na alisogea mbali huku akijiuliza Hamza anafanya kitu gani. Licha ya kujiuiliza hivyo , ilikuwa ni wazi kabisa mbinu hio Hamza aliotumia imemuongezea nguvu zake maradufu.
Hamza mara baada ya kusimama juu wima , umbo lake ni kama vile lilikuwa limeongezeka maradufu , lakini haikuwa hivyo alikuwa kawaida lakini kivuli chake ndio kilimfanya kuonekana kama vile ameongezeka urefu na upana wa mwili. Ajabu ni kwamba yale majeraha yake yote yalipona mara moja.
Muda huo Hamza alikuwa kama sanamu la Shujaa wa Ugiriki ya kale na alihisi kabisa misuli yake ilikuwa na nguvu isiokuwa ya kawaida . Mwenyewe hakudhania mbinu hio ingemletea hali hio na kumtengenezea pia hali ya kupona.
Mara baada ya kuhisia joto la Nyakasura aliona halikuwa likiunguza kama ilivyokuwa mwanzo , cha kushangaza ni kwamba alijihisi kuwa mwepesi kama unyoya.
Palepale akili yake yote ilikuwa katika mwili wake na ile alivyokanyaga chini ni kama aliinuliwa na upepo na kusogea kwa spidi uelekeo wa Nyakasura alipo huku akiwa ametanguliza ngumi mbele na hakuhofia miale ya moto wake.
Nyakasura upande wake alikuwa amejiandaa pia kwa shambulizi hilo na palepale aliugeuza moto wake kuwa siraha na kushambulia ngumi ile ya Hamza , lakni ilivyogusana na ngumi ile ilisambaratisha na kumfanya ashikwe na mshituko mkubwa na kujiuliza amekuwa shetani wa aina gani. Mara baada ya kuona mkuki wake haukuwa na madhara kwa Hamza aliona akimbie kwa kurudi nyuma lakini muda ule bado ngumi nyingine ya Hamza ilikuwa ikimsogelea.
“Ngao!!”Aliita
Palepale mkono wake wa kushoto uliibuka na ngao ya moto wa Zambarau na kusambaa hewani kama sahani kubwa ya kumfunika mtu asionekane upande wa pili.
Boom!!
Ngumi ya Hamza ilienda kugongana na ile ngao na kutengeneza sauti kubwa yenye kishindo.
Lakini haikuwa mwisho . Hamza mabega yake . misuli ya mikono yake na vidole vilikuwa vikisambaza wimbi la nguvu kiasi kwamba ile ngumi ilimfanya Nyakasura kushindwa kuidhibiti na kufanya ngao itawanyike huku yeye mwenyewe mwili wake ukipepesuka na kumfanya aende kudondokea mwamba chini ya mlima.
Shambulizi la ngumi ambalo Nyakasura alipokea lilimretea majeraha makubwa sana. Pigo lile lilimfanya moto uliokuwa umemzingira mwili wake kupotea mara moja na nywele zake kurudi katika hali ya kawaida.
Nyakasura alijishika kifua huku viashiria vya kutoka damu vilionekana katika mdomo wake . Aliinua kichwa chake na kumwangalia Hamza katika hali ya mkanganyiko huku akijishangaa alikuwa amepata majeraha ya ndani na kujiuliza inawezekana vipi ilihali yeye sio binadamu.
“Wewe kiumbe .. nadhani mpaka sasa hakuna haja ya kuendelea kupigana”Sauti ya besi ilisikika kutoka juu
Nyakasura aliishia kung’ata meno yake kwa hasira na alipiga kibao ardhini kwa hasira na kusimama.
“Bado hujanishinda , pigo moja huwezi kusema shindano limeisha”Aliongea na palepale aliita moto na mbawa kwa mara nyingine na kupanda juu hewani.
Licha ya kwamba alikuwa ameumia , lakini haikutosha kumfanya aache kupambana . Alikuwa akipanga kupanda juu ya mlima ili kwenda kuoga katika moto kujiponyesha.
Hamza hakuwa mzembe , alikuwa akijua huyo msichana anataka kwenda kujirudisha upya katika moto na majivu. Kwasababu alishachoka kupambana nae kusikoisha , hakutaka kumpa nafasi hio. Hivyo alianza kumfukuzia huku akiwa ameshatengeneza ngumi yenye ujazo.
Aliamini ngumi hio ikipata , hata kama hatomuuwa lakini atahakikisha amemjeruhi kiasi cha kutoweza kupaa angani.
Hamza alikuwa ni kama Kombola namna alivyokuwa akimsogelea Nyakasura na ile anafikia miale ya moto hakujali na alipita kwa kasi kiasi cha kusababisha mlipuko mkubwa.
Nyakasura mara baada ya kuhisi mlipuko ule , palepale aligeuka na alijikuta akiwa katika hali ya mshituko kumuona Hamza akimkaribia.
Hamza hakutaka kupoteza muda , baada ya kumsogelea karibu aliiongezea ujazo wa kutosha ngumi yake akinuia kumaliza pambano hilo kwa ngumi moja tu kabla mwanamke huyo hajaingia katika lindi la moto na kujiponyesha.
Lakini sasa dakika hio anataka kushambulia sauti kama ya ngurumo ilisikika kutoka chini ya mlima . Ilionyesha ni dhahiri kuna mtu ambae ametumia nishati ya mbingu na ardhi kusafirisha sauti hio
“Hamza utamuuwa. Acha!!”
Hamza mara baada ya kusikia sauti hio imetoka kwa nani , palepale aliacha kumshambulia. Nyakasura alikuwa amefumba macho mara baada ya kuona hakuna namna ya kuwekepa shambulizi la Hamza na jasho lilimtoka lakini alishangaa baada ya kusikia sauti ya Hamza kuzuiwa kutokuendelea.
Dakika hio hio vivuli vya watu wawili vilitua katika mlima huo . Alikuwa ni Afande Simba na Afande Himidu.
Afande Simba mara baada ya kuona uharibifu uliotokea katika kambi hio na kuzunguka kilele hicho cha mlima aliishia kutingisha kichwa kwa masikitiko na mshangao kwa wakati mmoja.
“Nyakasura nimekutuma kwa ajili ya kuisadia kambi ya nyoka , lakini kwanini umeinguza ?”Aliuliza Afande Simba kwa sauti.
“Mimi nilisema nakuja tu kuangalia ila sikuahidi kama sitoiunguza na moto”Aliongea.
“Wewe…” Fande Simba alijikuta aking’ata meno kwa hasira , “Inaonekana nimekuharibu kwa hiki ulichokifanya , hivi unadhani wafuasi wake watakuchukuliaje? Na hii hasara uliosababisha unadhani nani atailipia? Ni hela za kodi za wananchi na unajua hilo”Aliongea.
“Ubaya ubwela, kama ni hela zipotee tu. Na usinizuie maana bado sijamaliza kupigana”Aliongea kwa kiburi.
“Kupigana! Kama nisingemzuia Hamza ungeweza kukwepa shambulizi lake?” Afande Simba alifoka na kumfanya Nyakasura kung’ata meno kwa hasira.
“Ningekubali anishambulie na kisha kujiponyesha na moto . Wewe jali mambo yako mimi nataka kuendelea kupigana”Aliongea kwa kiburi na kumfanya Afande Simba kushindwa kuongea na kutingisha tu kichwa na palepale aligeuza sura yake na kumwangalia Hamza aliekuwa na mwili uliotuna na misuli kuonekana nje na kumfanya kuoekana mgumu kama mti.Nguvu ya Hamza alioshuhudia ilimtisha mno.
Afande Himidu aliekuwa hapo alimwangalia bosi wake na kumwonyeshea kidole gumba cha kumkubali. Aliona fika bosi wake ambae ameachana na maswala ya kuvuna nishati bado hakuwa mdhaifu.
Mwanzoni alidhani kutokana na Hamza kupoteza uwezo wake wote basi atakuwa hayupo katika levo ileile kama Nyakasura lakini muda huo aliona alikuwa amekosea kuidharau mbinu binafsi ambayo Hamza alikuwa akijifunza.
Hamza aliona hana haja ya kuendelea kupigana tena , hivyo palepale aliachilia nguvu ile nafsi mgawanyo na kurudi katika mwonekano wa kawaida.
“Himidu hebu acha kuniangalia nikiwa uchi na fanya mpango nipate nguo za kuvaa”Aliongea Hamza .
“Hahaha.. sawa bosi , ngoja nimpigie mtu alete nguo haraka sana”Aliongea Himidu huku akiwa na furaha.
“Nani kakuambia tunaacha? Bado sijamalizana na wewe”Aliongea Nyakasura kwa hasira
Hamza aliishia kuona mwanamke huyo ni king’ang’anizi mno , kama wakiendelea kupigana itakuwa ni aidha amuue au auliwe,. Kitu ambacho hakuona kama kitakuwa na maana kutokana na kutokuwa na uadui kati yao.
“Nyaka ukiendelea hivi . nitawasiliana na baba yako kumwambia”Aliongea Afande Simba akionya.
“Wewe ni Simba mshenzi , Simba unaenuka , unaona ni vizuri hivi unavyonifanyia?”Aliongea huku akikanyaga miguu yake chini kwa hasira.
Hamza mara baada ya kuona hivyo alijikuta akifurahi , alijiambia kumbe Nyakasura anae baba ambae anaweza kumkontrol? Tukio hilo alifananisha na namna mwalimu anavyomtishia mwanafunzi kuita wazazi wake.
“Nipo tayari kutokuiambia familia yako juu ya kuunguza kambi ya Nyoka! Kama unataka wafahamu kila kitu ni kheri ukaishia hapa la sivyo utakosa uhuru wako”Aliongea na kumfanya Nyakasura kusaga meno yake kwa hasira huku akimwangalia Hamza.
“Mimi na wewe hatujamalizana , nitakuacha kwasababu ya Simba , ila usiombe tukutane tena!”Aliongea kwa kulalamika.
Hamza hakuwa na muda wa kuendelea kubishana na mwanamke huyo na aliishia kutingisha mabega yake kumpa ishara ya kumkaribisha muda wowote.
Haikuchukua muda mrefu Hamza aliletewa mavazi ya kuvaa na baada ya kuyachukua hatimae Himidu alimsogelea bosi wake.
“Bosi wewe ni hatari . Hii ni mara yangu ya kwanza kumuona Nyakasura kuwa katika hali ya kutaka kulia..”Aliongea Himidu kwa sauti ya chini lakini alisikiwa vizuri tu na Nyakasura na kumfanya azidi kupandwa na hasira.
“Himidu endelea kuropoka tu ukidhani siwezi kukuunguza na mtoto nikuue”Aliongea na Himidu alinywea huku akicheka chinichini.
“Hey! hebu acha kumtishia rafiki yangu na moto wako , kwanza nina njaa maana umenisumbua sana”Aliongea Hamza huku akishika tumbo lake.
“Bosi hio mbinu uliokuwa ukitumia mwisho mwisho , inaitwaje?”
“Unadhani naweza kukuambia kirahisi namna hio , Hio mbinu inaitwa Siri”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Himidu kukosa neno la kuongea. Hata hivyo alijua Hamza hawezi kumwambia.
Muda huo huo kundi la wazee wa kambi ya nyoka walipandisha mlima na kusogea wakiongozwa na Mjomba ambae jina lake ni Mzee Sembe.
Walisikitika sana kuona msingi wote wa kambi yao ulikuwa umeungua kwa moto na macho yao yote yalimwangalia mkuu wa majeshi wakimtaka achukue hatua.
“Mzee Farook yupo wapi ?”Aliuliza Afande Simba huku akimwangalia Hamza na Hamza baada ya kuulizwa hivyo alimnyooshea kidole Nyakasura.
“Ameshakufa.. kauliwa na huyo mrembo”
“Nini!?” Mkuu huyo ndita ilijikunja huku akimwangalia Nyakasura kwa mshangao ,”Kwanini umemuua mzee Farook ikiwa nimekutuma kuja kumsaidia?”





















SEHEMU YA 167.
Wafuasi wa Nyoka mara baada ya kusikia kufa kwa Mzee Farook kumesababishwa na Nyakasura walijikuta wakiwa katika hali ya kumshangaa. Walikuwa wakiokoa maisha yao muda ule na hawakuweza kuona tukio hilo.
“Alikataa kusikiliza nilichomwambia na kukimbia akijifanya anataka kuokoa maisha yake ilihali yalikuwa mkononi mwangu. Mtu kalegea legea mnafanya kiongozi, nimemuuwa mimi”Aliongea Nyakasura kwa kejeli akionyesha hajutii kabisa alichokifanya.
Afande Simba aliishia kuvuta pumzi na kuzishusha huku akimwangalia Mzee Sembe kwa masikitiko.
“Jeshi litasimamia ujenzi upya wa kambi ya nyoka , ni bahati tu mnahifadhi nyaraka zenu muhimu ndani ya pango , hivyo tofauti na hasara ya majengo hakuna hasara kubwa. Kuhusu suala la Farook kutuma wanafunzi wake kwenda kufanya vurugu na kuhatarisha usalama wa raia wa kawaida lilikuwa kosa kisheria hivyo tutaishia hapa”Aliongea
“Asante sana Simba! Ingawa kambi yetu ya nyoka sio tajiri kuzidi taifa lakini tuna kiasi cha kutosha kuijenga upya . Hela na utajiri ni kitu cha kupita ila tunajali sana hadhi na taswira ya kambi yetu. Hatuwezi kumuwajibisha Nyakasura lakini kuhusu huyu Hamza, je hana kosa?”Aliuliza Sembe, alikuwa tayari kumsamehe Nyakasura kutokana na kutokuwa kiumbe wa kawaida lakini kuhusu Hamza hakutaka lipite kirahisi kwa kuwadhalilisha.
Afande Simba alikuwa katika hali ya mkanganyiko , aliishia kumwangalia Hamza na kisha wazee hao wa kambi pamoja na wanafunzi wao wakiwa na hamu kusikiliza maamuzi yake. Baada ya kufikiria kidogo aligeuzia kichwa chake kwa Afande Himidu.
“Mshauri mkuu , unamjua Hamza vizuri . Unadhani tunapaswa kudili nae vipi?”Aliuliza na kumfanya Himidu kuanza kumtukana mkuu huyo ndani kwa ndani baada ya kuona anamtupia mpira . Ila hata hivyo hakuongea na badala yake alikunja mikono yake nyuma na kutembea mpaka mbele ya wazee wa kambi.
“Wazee kuna mambo ni vigumu kuyaongea mbele ya watu wengi. Kwanini tusiende sehemu tulivu na kuongea kidogo ?”Aliongea na Mzee Sembe na wenzake walitingisha kichwa na kukubali na walishuka kuelekea chini ya mlima.
Nyakasura aliishia kumwangalia Hamza kwa macho ya chuki na kisha alimpa ishara ya heshima Afande Simba.
“Mimi natangulia kuondoka . Wewe,nitakutafuta turudie upya”Aliongea akimwashiria Hamza na kisha palepale aliyeyuka na Hamza alipumua kwa ahueni na kisha alimsogelea Afande Simba.
“Simba katika vitu vitatu ambavyo ulihitaji kutoka kwangu vimebakia vitu viwili tu”Aliongea.
“Unasemaje?”, Afande Simba alishikwa na mshangao, “Kwanini?”
“Usiniambie unataka kuwa kinyume na maneno yako , Si ndio wewe ulieniambia nimuache na nikaacha. Unadhani Nyakasura amepona ponaje?”Aliongea Hamza huku akicheka kiuovu.
“Na hio inahesabika? Hivi unajua ungejiingiza katika matatizo ya namna gani kama nisingekuzuia na ukamjeruhi Nyakasura?”
“Mimi sijali kuhusu hilo , vyovvyote vile wewe ndio ulieniambia nimuache , Hivyo ni sawa na mimi kukubaliana na hitajio moja katika yale matatu . Wewe ni mkuu wa jeshi hivyo sidhani utaenda kinyume na maneno yako”Aliongea lakini mkuu huyo uso wake ulionyesha kutokuwa tayari kukubaliana nae. Lakini hata hivyo alikosa njia ya kukataa. Alijiambia akienda kuelezea mbele ya mkuu wake atasema Hamza alimfanyia hila..
“Sijawahi kudhania mtawala wa ulimwengu wa giza mwenye uwezo wa kutingisha ulimwengu anapenda michezo ya hila”Aliongea
“Hakuna cha hila hapo , najaribu kupata haki yangu , kuna tatizo kwani mtu kudai haki yake?”Aliuliza Hamza.
“Basi sawa , tuseme umeshinda katika hili, lakini kwasababu yako kambi ya nyoka imeingia hasara kubwa . Ni ngumu sana kwenda kuelezea kilichotokea hapa kwa viongozi wa kiserikali. Kama hutaki kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria ni vizuri ukionyesha uaminifu wako”
“Uaminifu? Ni uaminifu wa namna gani unahitaji kutoka kwangu ? Ni wafuasi wa Nyoka ndio walifika katika kampuni ya mke wangu na kufanya fujo na nimefika hapa kwa ajili ya kulipa kisasi kulingana na sheria ya ulimwengu wa mapigano . Kuna kosa gani hapo?”
“Ndani ya nchi yetu ya Tanzania kuna sheria moja na hakuna sheria za kimapigano zinazoongoza nchi. Kama unataka kuendelea kuishi kwa amani ndani ya nchi yetu unapaswa kutii sheria bila shuruti”Aliongea na Hamza hakutaka kumjibu na kutaka kujua ni ombi gani anahitaji kutoka kwake.
“Niambie unataka nini kutoka kwangu ili niishi kwa amni?” Aliuliza na kumfanya Afande Simba kutoa tabasamu.
“Mwezi ujao Ulaya kutakuwa na kusanyiko la SETH Great . Nadhani hujasau?”
“Unazungumzia Sytor rating Assembly?”Aliongea Hamza huku akihesabu siku kupitia vidole vyake , “Ni kweli aisee , kama usingenikumbusha ningeshasahau mimi , miaka mitano imepita tayari”.
Seth Association ni jumuiya ambayo inashirikiana na mataifa makubwa ulimwenguni katika kutoa maksi na kupembua mashirika na jamii za siri ulimwengoni kote . Kila baada ya miaka mitano huitishwa kusanyiko la siri ambalo huitwa SETH Great Assembly au maarufu kama Set Rating Assembly.
Sababu ya kusanyiko hilo ni kwa ajili ya kugawa maksi kimadaraja kwa makundi ambayo yamepanda na kushuka katika ulimwengu wa siri.
Ilikuwa ni kama sherehe za ugawaji tuzo kwa wahalifu, tofauti tu ni kwamba sherehe hizo hufanyika kwa siri sana japo zinahudhuriwa na viongozi wakubwa duniani na wanachama wa mashirika ya siri na yale ya giza kama Freemason , Illuminat na mengineyo , haikuwa hivyo tu hata baadhi ya vitengo vya siri vya kiserikali kutoka mataifa mbalimbali hushindanishwa na kukwapua tuzo mfano Malibu pia wanayo haki ya kushiriki wakitaka.
Dunia ina jamii nyingi za siri za milengo ya kulia na kushoto ambazo zinachipua na kupotea na ndio maana wakaweka kipimo cha kutambua jamii ambazo zimeimarika zaidi katika muda huo ili kutambuliwa dunani kote.
Haikujalisha kundi ama kitengo kilikuwa cha ulimwengu wa giza ama ulimwengu wa haki , walipaswa kuweka unafiki pembeni na kisha kufanyiwa evaluation na jumuiya hio ya watoa maksi. Kwa ufupi ni kwamba hata wale wahalifu wa daraja la kwanza Duniani hupewa tuzo na wakati wa kusanyiko hilo wanakuwa nje ya sheria ya taifa husika na badala yake wanakuwa chini ya Sheria ya Seth Association. Kwa mfano wewe ni Jambazi wa kimataifa na Ulaya inakutafuta na ukataka kuhudhuria kusanyiko utaruhusiwa kuhudhuria chini ya ulinzi wa sheria za Seth na baada ya kusanyiko kuisha unapewa muda wa kwenda mafichoni kama kawaida na sheria za ulimwengu wa haki zitaanza kukutafuta upya . Ndio kipindi ambacho majambazi na magaidi hupata fursa ya likizo bila ya hofu ya kukamatwa mpaka kusanyiko liishe.
“Kama unataka serikali isiendelee kufuatilia hili swala basi unapaswa kushiriki chini ya kitengo chetu cha Malibu”
“Afande Simba unatania au? Wewe unajua nishaachana na hayo mambo ya ulimwengu wa giza muda mrefu halafu bado unataka nikashiriki kama mwakilishi wa kitengo chenu cha Malibu?”
“Kwa nafasi yako katika ulimwengu wa siri hata jumuia ya watoa maksi wakisikia sidhani kama watakuwa na furaha . ila sisi kuhusu hilo hatujali maana lipo juu yako”Aliongea
“Kama nikishiriki nitakutana na watu ambao nimepotezana nao kitambo na maadui zangu pia na nikishiriki chini ya kitengo chako ni sawa na kuwatangazia naishi Tanzania , wewe unadhani nitapata amani?”
“Usipokubali pia huwezi kuwa na amani hapa nchini , Unadhani Amiri jeshi mkuu atakubali hivi hivi umemuua ndugu yake . Amini usiamini ndani ya saa moja tu amri ikitoka watu wote ambao una uhusiano nao ikiwemo mkeo watakuwa chini ya ulinzi”Aliongea.
“Afande Simba unanitishia?”
“Sikutishii nakuonyesha njia ya kupita . Haupo peke yako , hata kama isiwe ni kwa ajili yako , kumbuka kuhusu familia yako. Au nakosea?”Aliongea na kisha alitembea na kumshika Hamza bega.
“Kijana wewe ni hatari sana , una nguvu kiasi kwamba nakuonea wivu. Sidhani tokea kale mpaka sasa kuna binadamu ashafikia uwezo wako bila ya kuwa na nishati za mbingu na ardhi. Lakini kumbuka haijalishi mwanaume ana nguvu kiasi gani lazima awe na udhaifu wake . Wapendwa wako na ndugu zako ndio udhaifu ambao unauwa watu wengi wenye nguvu , Hivyo hata kama una nguvu unapaswa kuwa na watu katika mfumo kukulinda. Vinginevyo unadhani hawa wazee ni kipi wanajali , unadhani wanaogopa kwasababu hawawezi kupigana na wewe ana kwa ana . Kama madaraka huna basi kuwa na koneksheni na wenye madaraka . Vinginevyo maadui zako hawatakuangalia uimara wako ulipo bali wataangalia ni wapi udhaifu wako ulipo”Aliongea mkuu wa majeshi.
Hamza licha ya kwamba hakufurahiswa na maneno hayo , lakini vilevile ilikuwa ni kweli. Ijapokuwa alikuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi lakini wengi ni wengi ,wakiamua lao asingeweza kufanya chochote.
“Endelea..”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Simba kucheka.
“Nikiongelea koneksheni , unapaswa kujua kabisa inaweza kukusaidia kutatua matatizo yako mengi , lakini je unajua ni koneksheni gani ngumu mtu kuwa nayo?”Aliuliza.
“Usiniambie ni Kitengo cha Malibu?”
“Hapana! Ni kuwa na koneksheni na raia elfu arobaini wenye nguvu ambao wapo chini ya kamandi. Ili mradi upo ndani ya mipaka ya Tanzania , haijalishi upo angani , ardhini au baharini hakuna mahali ambapo jeshi letu halifiki”Aliongea na kumfanya Hamza aliekuwa katika hali ya umakini akili yake sasa kufanya kazi. Alimwangalia Afande Simba akiwa katika hali ya tabasamu ambalo sio tabasamu.
Aliona ndio maana maneno ya bwana huyo yalikuwa yakishangaza siku hio , kumbe zunguka yote anataka kumungiza jeshini?.
“Niseme ukweli , Simba uwezo wako wa kulobby ni mkubwa mno”Alitania Hamza na kumfanya Afande Simba kucheka.
“Viongozi wanakukubali sana , sizungumzii viongozi wa kisiasa namaanisha viongozi wa jeshi wa juu kabisa wanapagawa sana na mafanikio yako. Ili mradi ukisema ndio jeshi lipo tayari kukupatia cheo cha kuanzia cha Meja Jenerali na kama ukifanya vizuri haitokuwa ngumu kufikia cheo cha Luteni Jenerali ndani ya umri wa miaka therathini tu na kuvunja historia ya kuwa mkuu wa majeshi mwenye umri mdogo zaidi . Kubwa zaidi utakuwa mwenzetu sasa, ndani ya mipaka ya Tanzania hakuna ambae atathubutu kukugusa wewe wala watu wako wa karibu . Vinginevyo utakuwa ni mwenye kuhangaika tu na kulipa visasi” Mara baada ya kuongea hivyo Afande Simba alimwangalia Hamza kwa shauku.
“Vipi unaonaje kuhusu pendekezo langu?”
“Niseme ukweli maneno yako yamefanya damu yangu ichemke , kunipa cheo cha Meja Jenerali kama zawadi itamfanya mtu yoyote moyo kusukuma damu kwa shida .. lakini kwa heshima na taadhima nakataa”Aliongea Hamza.
“Kwanini?” Afande Simba alikunja ndita , “Au umeridhika na kuwa msaidizi ndani ya kampuni ya mke wako?"Aliuliza na Hamza alitingisha kichwa kukataa.
“Ulichopendekeza kinavutia , unanifanya niwe Jenerali na kisha jeshi linakuwa ndio koneksheni yangu . lakini kwa lugha nyepesi nikishakubali maana yake lazima pia nikitumikie cheo changu na kuhusu mimi nimechoka kupigana , ninachotaka ni maisha marahisi. Sitaki usumbufu labda tu nichokozwe. Hao mabosi nawashukuru kwa kunikubali . Lakini nimeishi maisha ya mbwa mwitu na kama nikiingia katika mfumo kuna kitu lazima kitatokea , tena kikubwa tu”Aliongea.
“Una uhakika huhitaji muda wa kufikiria kuhusu hili?”
“Tubadilishe tu masharti , sijioni nikikaa chini na kufikiria kuhusu hili”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Simba kuona utayari wa Hamza katika macho yake na aliishia kukubali kinyonge.
“Basi sawa , ila hata kama haupo tayari kujiunga na jeshi letu bado utapaswa kusafiri na timu yetu ya vikosi vya Malibu kwenda Ulaya . Bila hivyo awamu hii swala la kuharibu kambi ya Nyoka kuwajibika kutakuwa juu yako”
“Kwani kuna haja ya kushiriki katika hilo kusanyiko , kama mnahisi hamna nguvu ya kutosha sioni haja ya kushiriki”
“Upo sahihi hakuna faida ya sisi kushiriki ama kutokushiriki , lakini mwaka huu kwasababu ya kugundulika kwa Earth Axis kuwa chini ya jeshi letu . Ikitokea tumewekewa vikwazo na mataifa ya nje moja kwa moja lawama za wananchi zitaenda kwa serikali na kwa jeshi. Mpaka sasa Serikali ya Marekani kupitia viongozi wao wameshaanza kuiongelea vibaya nchi yetu na ni swala la muda tu kuchukua hatua kwa siri ama kwa njia ya wazi”
“Nyakasura pia atashiriki . Ijapokuwa anahesabika kuwa mtaalamu wa juu katika ulimwengu wa mapigano kama ilivyo lakini asili yake inaweza kuleta sintofahamu nje ya nchi na vilevile hata kama akishiriki uzoefu hana na isitoshe kuna wataalamu wengi ambao bado hajakutana nao . Kwenda kwetu kushiriki ni kwa ajili ya kukuza hadhi ya jeshi vinginevyo kusingekuwa na haja ya kushiriki na kuwapa kazi wanasiasa kutuliza hali , lakini kama mabeberu wataamua kutushambulia iwe moja kwa moja ama kwa njia isio ya moja kwa moja tutakuwa kichekesho kwa dunia kwa nchi ndogo kama yetu kujaribu kutunishiana misuli na taifa kubwa. Ndio maana tunachotaka ni kujijengea hadhi kwanza katika ulimwengu usionekana , ili kam wakitaka kuchukua hatua wajifikirie mara mbilimbili.”Aliongea kwa kirefu.
“Kule Dodoma nilikuambia utupatie teknolojia ya Barham na Baffold ila haukuwa tayari , basi kubali katika hili, kama unajihisi wewe mweneywe kutoshiriki nadhani haitokuwa ngumu kutumia watu wako . Si ndio?”Aliongea na kumfanya Hamza macho yake kuchanua katika hali ya uovu.
“Simba unaenda mbali sasa , ile mara ya mwisho uliniomba teknolojia ya Barham na Baffold , kwahio yote ilikuwa ni kwa ajili ya kujiandaa na hili kusanyiko la wagawa maksi?”
“Haha.. nadhani unajua Tanzania bado ni nchi ndogo sana na mapungufu mengi kulinganisha na mataifa ya ulimwengu wa kwanza . Tunaweza kuimiliki Earth Axis lakini bado tupo dhaifu kuilinda na ndio maana tumekuomba vile. Ijapokuwa unaweza usijichukulie kama raia wa Tanzania , lakini wewe ni Mtanzania , au nakosea?”Aliongea na kumfanya Hamza kufikiria.
Muda ule alikumbuka Regina alikuwa pia na mpango wa kusafiri kwenda Ulaya mwezi ujao na kwasababu alihitaji kumsindikiza aliona sio mbaya kama atachukua muda wake kwenda kuhudhuria hilo kusanyiko.
Hamza aliona nchi ya Amerika haikuwa na utani kwenye kupigania maslahi yake na kama kweli wakichukua hatua watakaoathirika sio yeye bali wanawake waliokuwa karibu yake, ikiwemo biashara za Regina kwa ujumla.
“Basi kama ni hivyo utanitaarifu muda ukiwadia . Namaanisha nimekubali lakini sina uhakika nitakuwa salama..”Aliongea Hamza.
“Ili mradi ukijitahidi . Naamini hakutakuwa na tatizo kabisa . Hii ni msiheni ndogo sana ukilinganisha na misheni ulizofanya , ikiwemo ile ya Vita takatifu”Aliongea Afande Simba huku akiwa na tabasamu pana usoni na Hamza alipotaka kuongea Afande Simba aliingilia haraka.
“Kuhusu hili ombi letu usije ukasema lipo ndani ya mahitajio mawili mawili yaliobaki , hii ni ziada na usije kwenda kinyume na maneno yako”Aliongea na kumfanya Hamza kukuna kichwa na kujiambia hilo lizee kweli lina akili.
Muda huo Afande Himidu alirudi akiwa na wale wazee wafuasi wa Nyoka.
“Afande Simba , Bosi ! Kwanzia sasa hili swala limeisha . Mzee Sembe na wenzake hawana pingamizi tena”Aliongea Himidu.
“Oh! Mzee Sembe kweli umekubali hili lipite?”Aliuliza na Mzee Sembe na wenzake walimwangalai Hamza na macho ya heshima na wasiwasi kwa wakati mmoja.
“Bila shaka tumekubali yaishe lakini shukrani zetu zimwendee Mshauri mkuu kwa kuwa hiari kutuambia kuhusu Hamza … Kitendo cha kuwa maarufu kama alivyo Nyakasura nadhani ni swala la shukrani zetu kumuacha kwa ajili ya maslahi ya taifa . Lawama ni kwa Farook kwa kwenda kinyume na sheria na kusababisha kambi yetu kupata hasara kubwa”
Hamza mara baada ya kusikia maelezo hayo , palepale alimpiga Afande Himidu teke la makalio kwa kuwa mbeya.
“Himidu kwahio umewaambia kuhusu siri yangu sio?”
“Bosi sikuwa na namna ya kumaliza hili swala ndio maana . Lakini hata hivyo wameahidi hawatotoa taarifa ya chochote nilichowaambia . Lakini bosi wewe ni kama Kimulimuli gizani , huwezi kujificha kirahisi”Aliongea.
ITAENDELEA.
 
SHETANI RUDISHA NAFSI ZETU.

MTUNZI:SINGANOJR.

SEHEMU YA 166.
Kimulimuli Gizani.
Hamza alianza kumfukuzia Mzee Farook , huku akimpotezea Nyakasura na moto wake . Alijiambia hata kama akifa lazima amuue kwanza Master Farook.
Lakini hata hivyo kabla hata hajamfikia , Mzee Farook alitupiwa moto na Nyakasura kwa spidi ya juu kiasi kwamba ulitoboa tumbo lake na kilichoweza kusikika ni ‘puch’.
Mzee Farook aliishia kugeuza uso wake kumwangalia Nyakasura na alijikuta akitoa ukulele wa kutotaka kufa na palepale alidondoka chini na kuanza kuungua.
Mwili wake wote uliunguzwa na moto wa Nyakasura kiasi kwamba ni kama amemwagiwa petroli na ndani ya sekunde kadhaa aligeuka majivu.
“Nilikuambia usiondoke , ina maana hukuyachukulia maneno yangu kwa uzito . sasa ni zamu yako kuungua na wewe”Aliongea Nyakasura.
Hamza aliishia kuachama kiasi . Ingawa aliweza kuhisi kitu kikija kutoka nyuma yake , lakini hakuhisi hatari ikimaanisha yeye ndio hakulengwa, lakini alishangaa kuona Nyakasura ndio amemuua Mzee Farook.
Ilishangaza kwasababu Nyakasura ndie aliekuwa akimzuia kutokumuuwa mzee huyo lakini muda huo ni kama amebadilika na hakujali tena kuhusu sheria . Alichokuwa akitaka muda huo ni kupigana basi.
Kuwa na nguvu kubwa hutengeneza ukiburi na hilo ndio alionyesha Nyakasura kiumbe Foeniksi.
“Nyakasura kuna ulazima wa sisi kuendelea? Farook amekufa hivyo mimi naondoka”Aliongea Hamza huku akijiambia kuhusu Fabi hana haja ya kuwa na wasiwasi , kwasababu bila ya baba yake maana yake hakuwa na nguvu yoyote.
“Usijifanye sijui hujapigana na mimi ukiwa siriasi wakati mimi nikikuonyesha nia yangu ya dhati. Ukikimbia wewe sio mwanaume”Aliongea Nyakasura kwa kejeli huku akiinua kichwa chake , moto uliokuwa umezingira mwili wake ulikuwa ukitisha na haikueleweka alikuwa akiwezaje kuudhibiti.
Sehemu tu aliokuwa amekaa kila kitu kumzunguka kilikuwa kikiungua m alikuwa ni kama jua linalotembea , kama mfalme wa ndege wote.
Hamza alishindwa kujizuia na kuishia kutetemeka mwili mzima , hisia za kuwa na mwili kama wake mbele ya kiumbe huyo ilimfanya damu kuchemka na vinyweleo kusimama.
Mpaka hapo busara aliona ni kukimbia na ndio anaweza kupona katika hali hio. Aliona hakuwa na haja ya kuhatarisha uhai wake kudili na kiumbe ambae hakuwa binadamu , maana aliona ili mradi akiwa karibu na moto hawezi kufa.
Lakini licha ya hofu hio aliokuwa nayo , lakini ndani kabisa katika moyo wake asingeweza kukimbia , hadhi yake na utu wake kama mtaalamu wa mapigano ilikuwa imeguswa haswa . ile hali ya kutaka kuendelea kulinda hadhi yake hakutaka kuipoteza kwasababu tu ya miaka mitatu ya kuwa nje ya ulingo.
“Kwasababu umesema mwenyewe basi sina budi zaidi ya kupambana na wewe”Aliongea Hamza na palepale aliinama na kuangalia mwili wake. Nguo zake zote zilikuwa zimeungua na kubakia uchi lakini kwa Nyakasura hakuona tashwishwi ya aina yoyote . Alionekana alikuwa mzoefu wa kuona watu wakiwa uchi.
Ilikuwa ni bahati tu kwamba wao pekee ndio walikuwa juu ya mlima la sivyo ingekuwa kadhia ya mwanaume ambae yupo uchi anapambana na kiumbe mrembo.
Hamza aliishia kutingisha kichwa chake akipotezea mawazo hayo na kisha palepale alivuta pumzi nyingi na kuzishusha mara kadhaa na kadri alivyokuwa akifanya hivyo mpangilio wa pumzi yake ulianza kubadilika , mwanzoni alianza kupumua kwa haraka kama binadamu lakini muda huo alikuwa akitumia muda mrefu kupumua na kushusha pumzi.
Muda ule mwili wa Hamza misuli yake ilianza kutanuka kwa kasi na viungio vya mifupa katika mwili wake vilipiga kelele. Dakika ambayo Hamza aliyafumbua macho , yalikuwa yameingia ndani kwa kuwa siriasi na alipiga hatua moja na kukanyaga chini kwa nguvu.
Boom!
Kitendo cha kukanyaga chini kulitokea kishindo kizito na ardhi ilibonyea kwenda ndani na kutengeneza shimo.
Misuli yake ya kiuno ilionekana kuunganika moja kwa moja na mapaja yake , miguu na hata vidole na kumtengenezea muunganiko mkubwa wenye nguvu.Kila wakia(ounce) ya nguvu ya msuli wake ilikuwa imeungana pamoja na kutengeneza mkusanyiko wa nguvu ya juu.
Kuona vile Nyakasura macho yake yalisinyaa na alijikuta akitingisha kichwa huku akimwemwesa maneno.
“This is very interesting…”Aliongea.
Hamza hakuongea neno , kwa hatua moja alimsogelea Nyakasura bila ya kujali moto wake.
Kwa mbali ilikuwa ni kama vile jua halitaki kupatwa. Miale ya moto ya Nyakasura ilimfunika Hamza na kuunguza kila kitu . Lakini spidi ya Hamza ilikuwa sio kidogo , alikuwa kama mwanga na kumfanya Nyakasura kushindwa kuendana nae kutokana na miale yake ya moto ilitembea katika spidi ya mkondo wa hewa.
Hamza alikuwa akitumia uwezo wake wa kujongea kwa spidi kukwepa miale ya Nyakasura.
Nyakasura upande wake alionekana ni kama ashajua tatizo hilo na hakumfukuzia Hamza na badala yake alisimama katika eneo moja huku akisambaza miale pande zote.
“Ah!
Hamza alinguruma akiamua kuikaribisha baadhi ya miale ambayo aliona hawezi kuikwepa na muda huo huo alisogea kwa spidi kubwa kumshambulia Nyakasura na teke , akilenga maeneo dhaifu ya mwili wake.
Nyakasura mara baada ya kuona Hamza amefanikiwa kupita katika moto wake na sasa anamsogelea , alijikuta akishituka lakini hakutaka kusubiria kizembe.
“Mbawa mbayumbayu!”
Mara baada ya kuongea hivyo ghafla tu moto wake wote ulimfunika na kugeuka mbawa ambazo zilimpaisha kukwepeshwa na shambulizi la Hamza.
Hamza kuona hivyo alijikuta akishikwa na mshituko . Alijikuta akimwangalia Nyakasura akipaa kwenda angani na mbawa zake kwa spidi kubwa kiasi kwamba ndani ya sekunde tu alikuwa mita kadhaa mbali, na kumfanya aonekane kama malaika wa moto.
“Damn.. unaweza hata kupaa!!”
Hamza alijikuta akiamini uwezo wa damu ya kifoeniksi haukuwa wa kawaida kabisa . Ilikuwa kheri kama damu hio ingekuwa na nguvu pekee lakini ilikuwa na nguvu za kimitego nyingi za siri. Hamza yeye hakuwa na uwezo wa kupaa bali alikuwa na uwezo wa kuruka na kama Nyakasura anao uwezo wa kupaa watawezaje kuendelea kupigana.
Nyakasura akiwa hewani alikusanya donge kubwa la moto na mara baada ya kulichezesha kwa sekunde tu liligeuka na kuwa mkuki na kurushia sehemu alipo Hamza , mkuki huo kwa namna ulivyokuwa ukikata hewa ulikuwa ukitoa mlio kama wa ndege Mwewe , lakini sauti yenye kuumiza masikio.
Hamza mara baada ya kuona siraha hio hakuthubutu kabisa kuisogelea karibu na haraka sana alikimbia mbali.
Sekunde mluki ule wa moto ulivyochoma ardhi ulitengeneza wimbi kubwa la moto na kuyeyusha kila jiwe lililokuwa pembeni na kutengeneza shimo.
Nguvu hio ya uharibifu binadamu angeweza kuishuhudia angezimia hapo hapo. Lakini kwa Hamza hakuwa na muda wa kujali sana kuhusu maajabu hayo kwasababu Nyakasura alikuwa akimsogelea kwa kasi na mbawa zake za mbayumbayu.
Hamza aliamini kama akikutana moja kwa moja na nguvu hio ya mbawa inayomsogelea anaweza akawa katika hali mbaya. Kwa macho yake makali aliona kisima cha kuhifadhia maji nyuma ya nyumba za kambi hio zilizoharibika na bila ya kujiuliza mara mbilimbili alitimua mbio kukisogelea.
Nyakasura mara baada ya kuona Hamza anakimbia , alimfukuzia kwa nyuma kwa spidi kubwa huku akirefusha moto wake na kugeuza kuwa mkuki wa mita kadhaa.
Ile Nyakasura anataka kumkaribia Hamza kumchoma na ule mkuki mgongoni, Hamza aliwahi na kama mshale alitumbukia ndani ya kile kisima ‘chubwii’ na kula mbizi na kukoswa koswa na shambulizi.
“Unadhani utakuwa salama ukiingia kwenye maji?”Aliongea Nyakasura na palepale alinyoosha mkono wake na kushika ukuta wa kisima kile huku akisambaza moto mkali na ndani ya sekunde tu kisima kile mawe yake yalianza kuyeyuka huku maji yakianza kushika mvuke.
Muda huo huo Hamza alifyatuka kutoka kwenye kisima hicho kama Samaki na ile anafika nje alimtemea Nyakasura maji mengi kama Kiboko.
Hamza baada ya kufanya vile hakujua acheke ama alie, alidhania akimtemea maji Nyakasura angeuzima moto wake na kumfanya kuwa dhaifu lakini alijisumbua tu . Kwa alivyoona hata kama ingekuwa ni bahari pengine asingezimika.
Hamza palepale aliachana na mbinu ya kufikiria namna ya kuzima moto wake na badala yake aliona namna ya kushinda ni kupigana nae moja kwa moja na hapo ndipo vita ya mvutano ilipoanza.
Hamza alitumia uwezo wake wa kukimbia kumuacha mbali adui yake na wakati huo Nyakasura aliendelea kumfukuzia Hamza huku akimtupia moto na kukwepa mashambulizi yake ya kushitukiza.
Yalikuwa ni mapigano ya kwenda mbele na kurudi nyuma na hakuna alionekana kushinda ama kupoteza pambano.
Baada ya dakika kumi za mvutano , Hamza alikuwa na majeraha mengi ya moto katika mwili wake , huku upande wa Nyakasura akiwa amepigwa mara kadhaa na ilikuwa bahati hakupokea shambulizi la moja kwa moja.
Hamza ili kumshambulia Nyakasura ilibidi ajitoe muhanga wa kuunguzwa na moto lakini wakati huo huo akihakikisha shambulizi lake linamfikia kisawa sawa.
Hamza mara baada ya kutua chini baada ya kufanya shambulizi aliishia kuangalia mikono yake iliogeuka na kuwa mieusi kwa kuungua na alijikuta akipata msongo wa mawazo.
Nyakasura nguvu zilikuwa zimempugnua pia na alikuwa akihema kwa kuitafuta hewa , mbawa za moto alizokuwa nazo zilikuwa zimepotea pia.
“Nyakasura ni muda wa kuacha sasa , tukiendelea hivi tutakufa”Aliongea Hamza.
“Bado mshindi hajapatikana” Aliongea Nyakasura na palepale alivamia jengo la nyumba iliokuwa ikiwaka moto na kwenda kuoga moto.
Hamza mara baada ya kuona hivyo machozi yalitaka kumtoka . Alijiuliza huyu mwanamke anajaribu kufanya nini , wamepigana muda mchache tu lakini bado anataka kujirudisha katika hali yake ya kawaida.
“Hey! Kwa staili hio unadhani utachukua muda gani kumaliza kupigana?”Aliuliza Hamza na Nyakasura hakujali zaidi ya kuvuta pumzi ya moto na ndani ya dakika alitoka akiwa na ari mpya kwa ajili ya kuendelea kupigana.
“Usiwe na wasiwasi maana haitochukua muda mrefu nitakuwa nishakupiga”Aliongea Nyakasura akiwa katika hali ya kujiamini.
“Sidhani kama itawezekana ..”Aliongea Hamza.
“Nini! Usiniambie una mbinu ambayo hujaitumia bado?”Aliuliza Nyuakasura huku akionyesha ishara ya kutokuamini lakini bado aliamini kwa wakati mmoja.
Kwa mtazamo wake , mpaka Hamza kumlazimisha kuoga mara mbili katika moto haikuwa kawaida, ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na binadamu wa daraja la uwezo huo.
Hamza alifanya maamuzi katika moyo wake , uwezo wa kukimbia alikuwa nao , lakini hakutaka kufanya hivyo na njia pekee ya kushinda pambano hilo ni kutumia uwezo wake wa juu sana kumshikisha adabu vinginevyo licha ya kwamba alikuwa na mwili wa kuvumilia maumivu ya kuungua lakini isingekuwa vizuri kuendelea kuunguzwa.
“Ni mara yangu ya kwanza nakwenda kutumia hii mbinu ambayo nimeielewa kwa ufupi sana zidi yako kiumbe Phoenix ,. Sipo tayari kudhalilika nadhani pia hutojilaumu mwishoni”Aliongea Hamza.
Muda uleule mwili wake ulifunikwa na kivuli cha ajabn huku hewa kuzunguka ilianza kutingishika kama vile ni gesi inasambaa angani.
Hamza mwili wake ulianza kudunda kama vile misuli imegeuka na kuwa moyo, ilionekana ni dhahiri ni kama kuna kitu ambacho kipo ndani yake na kinataka kutoka.
Nyakasura alijikuta akikunja ndita . Alijikuta akihisi kuna kitu hakipo sawa kuhusu Hamza licha ya kuwa mbali,mapigo yake ya moyo yalibadilika.
Aliona Hamza ni kama alikuwa amefanana na anga linalomzunguka . Na sehemu aliosimama ni kama vile anga lake linadondoka chini.
“Decompose!”
Aliongea Hamza isieleweke anamaanisha nini na palepale alianza kutingishika kama vile anacheza kibwebwe huku akitamka maneno. Maneno ambayo alikuwa akitamka ni yale ambayo Yonesi alimpatia akimwambia kwamba aliokota maandishi yale jangwani katika misheni ya kijeshi.
Hamza hakuwahi kutumia maandiko yale tokea mara ya mwisho alivyojaribu kujifunza na kumuona mwanamke katika ndoto , sababu ya kuhisi muda huo ni wakati wa kutumia sio kwamba alikuwa na uhakika ila alipanga kujaribu akiwa katika hali ya juu sana ya uwezo wa mwili wake , kwani siku ile hisia alizopata ni kama akili yake ilitawaliwa na mdudu. Moja ya kanuni ya mafunzo ambayo yanajumlisha na nguvu ya kiroho , ili kupata majibu unayoyataka ni lazima kwanza consciosness yako iwe katika hali ya uamko(Active) ili kunyonya nguvu yoyote bila kuathiri nafsi yako. Mbinu hio wataalamu wa mafnnzo hayo wanaita Mgawanyiko wa nafsi na Roho (Soul and Spirit Disintergration).
Mbinu hio hata hivyo ilikuwa na hasara zake , kwasababu inatengeneza mlipuko wa nguvu ya ndani kutokana na kwamba nafsi na roho kiungo chake kikuu ni damu.
Hamza hakujali chochote, muda huo alitaka kuamsha uwezo wake wote wa damu kwa kuichanisha nafsi yake na damu ili kutengeneza mwili ulio huru. Mtego wa nguvu ya miili yetu upo katika nafsi zetu na roho , kuishinda nafsi maana yake ni kujiweka huru.
“Ah!”
Hamza alijikuta akipiga makelele huku akiangalia hewani , macho yake ni kama hayakuwa yake bali yameshikiliwa na kiumbe kingine na lile eneo alilokuwa amesimama lilianza kutitia na kufanya mawe kuporomoka.
Jambo lile lilimshangaza Nyakasura na alisogea mbali huku akijiuliza Hamza anafanya kitu gani. Licha ya kujiuiliza hivyo , ilikuwa ni wazi kabisa mbinu hio Hamza aliotumia imemuongezea nguvu zake maradufu.
Hamza mara baada ya kusimama juu wima , umbo lake ni kama vile lilikuwa limeongezeka maradufu , lakini haikuwa hivyo alikuwa kawaida lakini kivuli chake ndio kilimfanya kuonekana kama vile ameongezeka urefu na upana wa mwili. Ajabu ni kwamba yale majeraha yake yote yalipona mara moja.
Muda huo Hamza alikuwa kama sanamu la Shujaa wa Ugiriki ya kale na alihisi kabisa misuli yake ilikuwa na nguvu isiokuwa ya kawaida . Mwenyewe hakudhania mbinu hio ingemletea hali hio na kumtengenezea pia hali ya kupona.
Mara baada ya kuhisia joto la Nyakasura aliona halikuwa likiunguza kama ilivyokuwa mwanzo , cha kushangaza ni kwamba alijihisi kuwa mwepesi kama unyoya.
Palepale akili yake yote ilikuwa katika mwili wake na ile alivyokanyaga chini ni kama aliinuliwa na upepo na kusogea kwa spidi uelekeo wa Nyakasura alipo huku akiwa ametanguliza ngumi mbele na hakuhofia miale ya moto wake.
Nyakasura upande wake alikuwa amejiandaa pia kwa shambulizi hilo na palepale aliugeuza moto wake kuwa siraha na kushambulia ngumi ile ya Hamza , lakni ilivyogusana na ngumi ile ilisambaratisha na kumfanya ashikwe na mshituko mkubwa na kujiuliza amekuwa shetani wa aina gani. Mara baada ya kuona mkuki wake haukuwa na madhara kwa Hamza aliona akimbie kwa kurudi nyuma lakini muda ule bado ngumi nyingine ya Hamza ilikuwa ikimsogelea.
“Ngao!!”Aliita
Palepale mkono wake wa kushoto uliibuka na ngao ya moto wa Zambarau na kusambaa hewani kama sahani kubwa ya kumfunika mtu asionekane upande wa pili.
Boom!!
Ngumi ya Hamza ilienda kugongana na ile ngao na kutengeneza sauti kubwa yenye kishindo.
Lakini haikuwa mwisho . Hamza mabega yake . misuli ya mikono yake na vidole vilikuwa vikisambaza wimbi la nguvu kiasi kwamba ile ngumi ilimfanya Nyakasura kushindwa kuidhibiti na kufanya ngao itawanyike huku yeye mwenyewe mwili wake ukipepesuka na kumfanya aende kudondokea mwamba chini ya mlima.
Shambulizi la ngumi ambalo Nyakasura alipokea lilimretea majeraha makubwa sana. Pigo lile lilimfanya moto uliokuwa umemzingira mwili wake kupotea mara moja na nywele zake kurudi katika hali ya kawaida.
Nyakasura alijishika kifua huku viashiria vya kutoka damu vilionekana katika mdomo wake . Aliinua kichwa chake na kumwangalia Hamza katika hali ya mkanganyiko huku akijishangaa alikuwa amepata majeraha ya ndani na kujiuliza inawezekana vipi ilihali yeye sio binadamu.
“Wewe kiumbe .. nadhani mpaka sasa hakuna haja ya kuendelea kupigana”Sauti ya besi ilisikika kutoka juu
Nyakasura aliishia kung’ata meno yake kwa hasira na alipiga kibao ardhini kwa hasira na kusimama.
“Bado hujanishinda , pigo moja huwezi kusema shindano limeisha”Aliongea na palepale aliita moto na mbawa kwa mara nyingine na kupanda juu hewani.
Licha ya kwamba alikuwa ameumia , lakini haikutosha kumfanya aache kupambana . Alikuwa akipanga kupanda juu ya mlima ili kwenda kuoga katika moto kujiponyesha.
Hamza hakuwa mzembe , alikuwa akijua huyo msichana anataka kwenda kujirudisha upya katika moto na majivu. Kwasababu alishachoka kupambana nae kusikoisha , hakutaka kumpa nafasi hio. Hivyo alianza kumfukuzia huku akiwa ameshatengeneza ngumi yenye ujazo.
Aliamini ngumi hio ikipata , hata kama hatomuuwa lakini atahakikisha amemjeruhi kiasi cha kutoweza kupaa angani.
Hamza alikuwa ni kama Kombola namna alivyokuwa akimsogelea Nyakasura na ile anafikia miale ya moto hakujali na alipita kwa kasi kiasi cha kusababisha mlipuko mkubwa.
Nyakasura mara baada ya kuhisi mlipuko ule , palepale aligeuka na alijikuta akiwa katika hali ya mshituko kumuona Hamza akimkaribia.
Hamza hakutaka kupoteza muda , baada ya kumsogelea karibu aliiongezea ujazo wa kutosha ngumi yake akinuia kumaliza pambano hilo kwa ngumi moja tu kabla mwanamke huyo hajaingia katika lindi la moto na kujiponyesha.
Lakini sasa dakika hio anataka kushambulia sauti kama ya ngurumo ilisikika kutoka chini ya mlima . Ilionyesha ni dhahiri kuna mtu ambae ametumia nishati ya mbingu na ardhi kusafirisha sauti hio
“Hamza utamuuwa. Acha!!”
Hamza mara baada ya kusikia sauti hio imetoka kwa nani , palepale aliacha kumshambulia. Nyakasura alikuwa amefumba macho mara baada ya kuona hakuna namna ya kuwekepa shambulizi la Hamza na jasho lilimtoka lakini alishangaa baada ya kusikia sauti ya Hamza kuzuiwa kutokuendelea.
Dakika hio hio vivuli vya watu wawili vilitua katika mlima huo . Alikuwa ni Afande Simba na Afande Himidu.
Afande Simba mara baada ya kuona uharibifu uliotokea katika kambi hio na kuzunguka kilele hicho cha mlima aliishia kutingisha kichwa kwa masikitiko na mshangao kwa wakati mmoja.
“Nyakasura nimekutuma kwa ajili ya kuisadia kambi ya nyoka , lakini kwanini umeinguza ?”Aliuliza Afande Simba kwa sauti.
“Mimi nilisema nakuja tu kuangalia ila sikuahidi kama sitoiunguza na moto”Aliongea.
“Wewe…” Fande Simba alijikuta aking’ata meno kwa hasira , “Inaonekana nimekuharibu kwa hiki ulichokifanya , hivi unadhani wafuasi wake watakuchukuliaje? Na hii hasara uliosababisha unadhani nani atailipia? Ni hela za kodi za wananchi na unajua hilo”Aliongea.
“Ubaya ubwela, kama ni hela zipotee tu. Na usinizuie maana bado sijamaliza kupigana”Aliongea kwa kiburi.
“Kupigana! Kama nisingemzuia Hamza ungeweza kukwepa shambulizi lake?” Afande Simba alifoka na kumfanya Nyakasura kung’ata meno kwa hasira.
“Ningekubali anishambulie na kisha kujiponyesha na moto . Wewe jali mambo yako mimi nataka kuendelea kupigana”Aliongea kwa kiburi na kumfanya Afande Simba kushindwa kuongea na kutingisha tu kichwa na palepale aligeuza sura yake na kumwangalia Hamza aliekuwa na mwili uliotuna na misuli kuonekana nje na kumfanya kuoekana mgumu kama mti.Nguvu ya Hamza alioshuhudia ilimtisha mno.
Afande Himidu aliekuwa hapo alimwangalia bosi wake na kumwonyeshea kidole gumba cha kumkubali. Aliona fika bosi wake ambae ameachana na maswala ya kuvuna nishati bado hakuwa mdhaifu.
Mwanzoni alidhani kutokana na Hamza kupoteza uwezo wake wote basi atakuwa hayupo katika levo ileile kama Nyakasura lakini muda huo aliona alikuwa amekosea kuidharau mbinu binafsi ambayo Hamza alikuwa akijifunza.
Hamza aliona hana haja ya kuendelea kupigana tena , hivyo palepale aliachilia nguvu ile nafsi mgawanyo na kurudi katika mwonekano wa kawaida.
“Himidu hebu acha kuniangalia nikiwa uchi na fanya mpango nipate nguo za kuvaa”Aliongea Hamza .
“Hahaha.. sawa bosi , ngoja nimpigie mtu alete nguo haraka sana”Aliongea Himidu huku akiwa na furaha.
“Nani kakuambia tunaacha? Bado sijamalizana na wewe”Aliongea Nyakasura kwa hasira
Hamza aliishia kuona mwanamke huyo ni king’ang’anizi mno , kama wakiendelea kupigana itakuwa ni aidha amuue au auliwe,. Kitu ambacho hakuona kama kitakuwa na maana kutokana na kutokuwa na uadui kati yao.
“Nyaka ukiendelea hivi . nitawasiliana na baba yako kumwambia”Aliongea Afande Simba akionya.
“Wewe ni Simba mshenzi , Simba unaenuka , unaona ni vizuri hivi unavyonifanyia?”Aliongea huku akikanyaga miguu yake chini kwa hasira.
Hamza mara baada ya kuona hivyo alijikuta akifurahi , alijiambia kumbe Nyakasura anae baba ambae anaweza kumkontrol? Tukio hilo alifananisha na namna mwalimu anavyomtishia mwanafunzi kuita wazazi wake.
“Nipo tayari kutokuiambia familia yako juu ya kuunguza kambi ya Nyoka! Kama unataka wafahamu kila kitu ni kheri ukaishia hapa la sivyo utakosa uhuru wako”Aliongea na kumfanya Nyakasura kusaga meno yake kwa hasira huku akimwangalia Hamza.
“Mimi na wewe hatujamalizana , nitakuacha kwasababu ya Simba , ila usiombe tukutane tena!”Aliongea kwa kulalamika.
Hamza hakuwa na muda wa kuendelea kubishana na mwanamke huyo na aliishia kutingisha mabega yake kumpa ishara ya kumkaribisha muda wowote.
Haikuchukua muda mrefu Hamza aliletewa mavazi ya kuvaa na baada ya kuyachukua hatimae Himidu alimsogelea bosi wake.
“Bosi wewe ni hatari . Hii ni mara yangu ya kwanza kumuona Nyakasura kuwa katika hali ya kutaka kulia..”Aliongea Himidu kwa sauti ya chini lakini alisikiwa vizuri tu na Nyakasura na kumfanya azidi kupandwa na hasira.
“Himidu endelea kuropoka tu ukidhani siwezi kukuunguza na mtoto nikuue”Aliongea na Himidu alinywea huku akicheka chinichini.
“Hey! hebu acha kumtishia rafiki yangu na moto wako , kwanza nina njaa maana umenisumbua sana”Aliongea Hamza huku akishika tumbo lake.
“Bosi hio mbinu uliokuwa ukitumia mwisho mwisho , inaitwaje?”
“Unadhani naweza kukuambia kirahisi namna hio , Hio mbinu inaitwa Siri”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Himidu kukosa neno la kuongea. Hata hivyo alijua Hamza hawezi kumwambia.
Muda huo huo kundi la wazee wa kambi ya nyoka walipandisha mlima na kusogea wakiongozwa na Mjomba ambae jina lake ni Mzee Sembe.
Walisikitika sana kuona msingi wote wa kambi yao ulikuwa umeungua kwa moto na macho yao yote yalimwangalia mkuu wa majeshi wakimtaka achukue hatua.
“Mzee Farook yupo wapi ?”Aliuliza Afande Simba huku akimwangalia Hamza na Hamza baada ya kuulizwa hivyo alimnyooshea kidole Nyakasura.
“Ameshakufa.. kauliwa na huyo mrembo”
“Nini!?” Mkuu huyo ndita ilijikunja huku akimwangalia Nyakasura kwa mshangao ,”Kwanini umemuua mzee Farook ikiwa nimekutuma kuja kumsaidia?”





















SEHEMU YA 167.
Wafuasi wa Nyoka mara baada ya kusikia kufa kwa Mzee Farook kumesababishwa na Nyakasura walijikuta wakiwa katika hali ya kumshangaa. Walikuwa wakiokoa maisha yao muda ule na hawakuweza kuona tukio hilo.
“Alikataa kusikiliza nilichomwambia na kukimbia akijifanya anataka kuokoa maisha yake ilihali yalikuwa mkononi mwangu. Mtu kalegea legea mnafanya kiongozi, nimemuuwa mimi”Aliongea Nyakasura kwa kejeli akionyesha hajutii kabisa alichokifanya.
Afande Simba aliishia kuvuta pumzi na kuzishusha huku akimwangalia Mzee Sembe kwa masikitiko.
“Jeshi litasimamia ujenzi upya wa kambi ya nyoka , ni bahati tu mnahifadhi nyaraka zenu muhimu ndani ya pango , hivyo tofauti na hasara ya majengo hakuna hasara kubwa. Kuhusu suala la Farook kutuma wanafunzi wake kwenda kufanya vurugu na kuhatarisha usalama wa raia wa kawaida lilikuwa kosa kisheria hivyo tutaishia hapa”Aliongea
“Asante sana Simba! Ingawa kambi yetu ya nyoka sio tajiri kuzidi taifa lakini tuna kiasi cha kutosha kuijenga upya . Hela na utajiri ni kitu cha kupita ila tunajali sana hadhi na taswira ya kambi yetu. Hatuwezi kumuwajibisha Nyakasura lakini kuhusu huyu Hamza, je hana kosa?”Aliuliza Sembe, alikuwa tayari kumsamehe Nyakasura kutokana na kutokuwa kiumbe wa kawaida lakini kuhusu Hamza hakutaka lipite kirahisi kwa kuwadhalilisha.
Afande Simba alikuwa katika hali ya mkanganyiko , aliishia kumwangalia Hamza na kisha wazee hao wa kambi pamoja na wanafunzi wao wakiwa na hamu kusikiliza maamuzi yake. Baada ya kufikiria kidogo aligeuzia kichwa chake kwa Afande Himidu.
“Mshauri mkuu , unamjua Hamza vizuri . Unadhani tunapaswa kudili nae vipi?”Aliuliza na kumfanya Himidu kuanza kumtukana mkuu huyo ndani kwa ndani baada ya kuona anamtupia mpira . Ila hata hivyo hakuongea na badala yake alikunja mikono yake nyuma na kutembea mpaka mbele ya wazee wa kambi.
“Wazee kuna mambo ni vigumu kuyaongea mbele ya watu wengi. Kwanini tusiende sehemu tulivu na kuongea kidogo ?”Aliongea na Mzee Sembe na wenzake walitingisha kichwa na kukubali na walishuka kuelekea chini ya mlima.
Nyakasura aliishia kumwangalia Hamza kwa macho ya chuki na kisha alimpa ishara ya heshima Afande Simba.
“Mimi natangulia kuondoka . Wewe,nitakutafuta turudie upya”Aliongea akimwashiria Hamza na kisha palepale aliyeyuka na Hamza alipumua kwa ahueni na kisha alimsogelea Afande Simba.
“Simba katika vitu vitatu ambavyo ulihitaji kutoka kwangu vimebakia vitu viwili tu”Aliongea.
“Unasemaje?”, Afande Simba alishikwa na mshangao, “Kwanini?”
“Usiniambie unataka kuwa kinyume na maneno yako , Si ndio wewe ulieniambia nimuache na nikaacha. Unadhani Nyakasura amepona ponaje?”Aliongea Hamza huku akicheka kiuovu.
“Na hio inahesabika? Hivi unajua ungejiingiza katika matatizo ya namna gani kama nisingekuzuia na ukamjeruhi Nyakasura?”
“Mimi sijali kuhusu hilo , vyovvyote vile wewe ndio ulieniambia nimuache , Hivyo ni sawa na mimi kukubaliana na hitajio moja katika yale matatu . Wewe ni mkuu wa jeshi hivyo sidhani utaenda kinyume na maneno yako”Aliongea lakini mkuu huyo uso wake ulionyesha kutokuwa tayari kukubaliana nae. Lakini hata hivyo alikosa njia ya kukataa. Alijiambia akienda kuelezea mbele ya mkuu wake atasema Hamza alimfanyia hila..
“Sijawahi kudhania mtawala wa ulimwengu wa giza mwenye uwezo wa kutingisha ulimwengu anapenda michezo ya hila”Aliongea
“Hakuna cha hila hapo , najaribu kupata haki yangu , kuna tatizo kwani mtu kudai haki yake?”Aliuliza Hamza.
“Basi sawa , tuseme umeshinda katika hili, lakini kwasababu yako kambi ya nyoka imeingia hasara kubwa . Ni ngumu sana kwenda kuelezea kilichotokea hapa kwa viongozi wa kiserikali. Kama hutaki kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria ni vizuri ukionyesha uaminifu wako”
“Uaminifu? Ni uaminifu wa namna gani unahitaji kutoka kwangu ? Ni wafuasi wa Nyoka ndio walifika katika kampuni ya mke wangu na kufanya fujo na nimefika hapa kwa ajili ya kulipa kisasi kulingana na sheria ya ulimwengu wa mapigano . Kuna kosa gani hapo?”
“Ndani ya nchi yetu ya Tanzania kuna sheria moja na hakuna sheria za kimapigano zinazoongoza nchi. Kama unataka kuendelea kuishi kwa amani ndani ya nchi yetu unapaswa kutii sheria bila shuruti”Aliongea na Hamza hakutaka kumjibu na kutaka kujua ni ombi gani anahitaji kutoka kwake.
“Niambie unataka nini kutoka kwangu ili niishi kwa amni?” Aliuliza na kumfanya Afande Simba kutoa tabasamu.
“Mwezi ujao Ulaya kutakuwa na kusanyiko la SETH Great . Nadhani hujasau?”
“Unazungumzia Sytor rating Assembly?”Aliongea Hamza huku akihesabu siku kupitia vidole vyake , “Ni kweli aisee , kama usingenikumbusha ningeshasahau mimi , miaka mitano imepita tayari”.
Seth Association ni jumuiya ambayo inashirikiana na mataifa makubwa ulimwenguni katika kutoa maksi na kupembua mashirika na jamii za siri ulimwengoni kote . Kila baada ya miaka mitano huitishwa kusanyiko la siri ambalo huitwa SETH Great Assembly au maarufu kama Set Rating Assembly.
Sababu ya kusanyiko hilo ni kwa ajili ya kugawa maksi kimadaraja kwa makundi ambayo yamepanda na kushuka katika ulimwengu wa siri.
Ilikuwa ni kama sherehe za ugawaji tuzo kwa wahalifu, tofauti tu ni kwamba sherehe hizo hufanyika kwa siri sana japo zinahudhuriwa na viongozi wakubwa duniani na wanachama wa mashirika ya siri na yale ya giza kama Freemason , Illuminat na mengineyo , haikuwa hivyo tu hata baadhi ya vitengo vya siri vya kiserikali kutoka mataifa mbalimbali hushindanishwa na kukwapua tuzo mfano Malibu pia wanayo haki ya kushiriki wakitaka.
Dunia ina jamii nyingi za siri za milengo ya kulia na kushoto ambazo zinachipua na kupotea na ndio maana wakaweka kipimo cha kutambua jamii ambazo zimeimarika zaidi katika muda huo ili kutambuliwa dunani kote.
Haikujalisha kundi ama kitengo kilikuwa cha ulimwengu wa giza ama ulimwengu wa haki , walipaswa kuweka unafiki pembeni na kisha kufanyiwa evaluation na jumuiya hio ya watoa maksi. Kwa ufupi ni kwamba hata wale wahalifu wa daraja la kwanza Duniani hupewa tuzo na wakati wa kusanyiko hilo wanakuwa nje ya sheria ya taifa husika na badala yake wanakuwa chini ya Sheria ya Seth Association. Kwa mfano wewe ni Jambazi wa kimataifa na Ulaya inakutafuta na ukataka kuhudhuria kusanyiko utaruhusiwa kuhudhuria chini ya ulinzi wa sheria za Seth na baada ya kusanyiko kuisha unapewa muda wa kwenda mafichoni kama kawaida na sheria za ulimwengu wa haki zitaanza kukutafuta upya . Ndio kipindi ambacho majambazi na magaidi hupata fursa ya likizo bila ya hofu ya kukamatwa mpaka kusanyiko liishe.
“Kama unataka serikali isiendelee kufuatilia hili swala basi unapaswa kushiriki chini ya kitengo chetu cha Malibu”
“Afande Simba unatania au? Wewe unajua nishaachana na hayo mambo ya ulimwengu wa giza muda mrefu halafu bado unataka nikashiriki kama mwakilishi wa kitengo chenu cha Malibu?”
“Kwa nafasi yako katika ulimwengu wa siri hata jumuia ya watoa maksi wakisikia sidhani kama watakuwa na furaha . ila sisi kuhusu hilo hatujali maana lipo juu yako”Aliongea
“Kama nikishiriki nitakutana na watu ambao nimepotezana nao kitambo na maadui zangu pia na nikishiriki chini ya kitengo chako ni sawa na kuwatangazia naishi Tanzania , wewe unadhani nitapata amani?”
“Usipokubali pia huwezi kuwa na amani hapa nchini , Unadhani Amiri jeshi mkuu atakubali hivi hivi umemuua ndugu yake . Amini usiamini ndani ya saa moja tu amri ikitoka watu wote ambao una uhusiano nao ikiwemo mkeo watakuwa chini ya ulinzi”Aliongea.
“Afande Simba unanitishia?”
“Sikutishii nakuonyesha njia ya kupita . Haupo peke yako , hata kama isiwe ni kwa ajili yako , kumbuka kuhusu familia yako. Au nakosea?”Aliongea na kisha alitembea na kumshika Hamza bega.
“Kijana wewe ni hatari sana , una nguvu kiasi kwamba nakuonea wivu. Sidhani tokea kale mpaka sasa kuna binadamu ashafikia uwezo wako bila ya kuwa na nishati za mbingu na ardhi. Lakini kumbuka haijalishi mwanaume ana nguvu kiasi gani lazima awe na udhaifu wake . Wapendwa wako na ndugu zako ndio udhaifu ambao unauwa watu wengi wenye nguvu , Hivyo hata kama una nguvu unapaswa kuwa na watu katika mfumo kukulinda. Vinginevyo unadhani hawa wazee ni kipi wanajali , unadhani wanaogopa kwasababu hawawezi kupigana na wewe ana kwa ana . Kama madaraka huna basi kuwa na koneksheni na wenye madaraka . Vinginevyo maadui zako hawatakuangalia uimara wako ulipo bali wataangalia ni wapi udhaifu wako ulipo”Aliongea mkuu wa majeshi.
Hamza licha ya kwamba hakufurahiswa na maneno hayo , lakini vilevile ilikuwa ni kweli. Ijapokuwa alikuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi lakini wengi ni wengi ,wakiamua lao asingeweza kufanya chochote.
“Endelea..”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Simba kucheka.
“Nikiongelea koneksheni , unapaswa kujua kabisa inaweza kukusaidia kutatua matatizo yako mengi , lakini je unajua ni koneksheni gani ngumu mtu kuwa nayo?”Aliuliza.
“Usiniambie ni Kitengo cha Malibu?”
“Hapana! Ni kuwa na koneksheni na raia elfu arobaini wenye nguvu ambao wapo chini ya kamandi. Ili mradi upo ndani ya mipaka ya Tanzania , haijalishi upo angani , ardhini au baharini hakuna mahali ambapo jeshi letu halifiki”Aliongea na kumfanya Hamza aliekuwa katika hali ya umakini akili yake sasa kufanya kazi. Alimwangalia Afande Simba akiwa katika hali ya tabasamu ambalo sio tabasamu.
Aliona ndio maana maneno ya bwana huyo yalikuwa yakishangaza siku hio , kumbe zunguka yote anataka kumungiza jeshini?.
“Niseme ukweli , Simba uwezo wako wa kulobby ni mkubwa mno”Alitania Hamza na kumfanya Afande Simba kucheka.
“Viongozi wanakukubali sana , sizungumzii viongozi wa kisiasa namaanisha viongozi wa jeshi wa juu kabisa wanapagawa sana na mafanikio yako. Ili mradi ukisema ndio jeshi lipo tayari kukupatia cheo cha kuanzia cha Meja Jenerali na kama ukifanya vizuri haitokuwa ngumu kufikia cheo cha Luteni Jenerali ndani ya umri wa miaka therathini tu na kuvunja historia ya kuwa mkuu wa majeshi mwenye umri mdogo zaidi . Kubwa zaidi utakuwa mwenzetu sasa, ndani ya mipaka ya Tanzania hakuna ambae atathubutu kukugusa wewe wala watu wako wa karibu . Vinginevyo utakuwa ni mwenye kuhangaika tu na kulipa visasi” Mara baada ya kuongea hivyo Afande Simba alimwangalia Hamza kwa shauku.
“Vipi unaonaje kuhusu pendekezo langu?”
“Niseme ukweli maneno yako yamefanya damu yangu ichemke , kunipa cheo cha Meja Jenerali kama zawadi itamfanya mtu yoyote moyo kusukuma damu kwa shida .. lakini kwa heshima na taadhima nakataa”Aliongea Hamza.
“Kwanini?” Afande Simba alikunja ndita , “Au umeridhika na kuwa msaidizi ndani ya kampuni ya mke wako?"Aliuliza na Hamza alitingisha kichwa kukataa.
“Ulichopendekeza kinavutia , unanifanya niwe Jenerali na kisha jeshi linakuwa ndio koneksheni yangu . lakini kwa lugha nyepesi nikishakubali maana yake lazima pia nikitumikie cheo changu na kuhusu mimi nimechoka kupigana , ninachotaka ni maisha marahisi. Sitaki usumbufu labda tu nichokozwe. Hao mabosi nawashukuru kwa kunikubali . Lakini nimeishi maisha ya mbwa mwitu na kama nikiingia katika mfumo kuna kitu lazima kitatokea , tena kikubwa tu”Aliongea.
“Una uhakika huhitaji muda wa kufikiria kuhusu hili?”
“Tubadilishe tu masharti , sijioni nikikaa chini na kufikiria kuhusu hili”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Simba kuona utayari wa Hamza katika macho yake na aliishia kukubali kinyonge.
“Basi sawa , ila hata kama haupo tayari kujiunga na jeshi letu bado utapaswa kusafiri na timu yetu ya vikosi vya Malibu kwenda Ulaya . Bila hivyo awamu hii swala la kuharibu kambi ya Nyoka kuwajibika kutakuwa juu yako”
“Kwani kuna haja ya kushiriki katika hilo kusanyiko , kama mnahisi hamna nguvu ya kutosha sioni haja ya kushiriki”
“Upo sahihi hakuna faida ya sisi kushiriki ama kutokushiriki , lakini mwaka huu kwasababu ya kugundulika kwa Earth Axis kuwa chini ya jeshi letu . Ikitokea tumewekewa vikwazo na mataifa ya nje moja kwa moja lawama za wananchi zitaenda kwa serikali na kwa jeshi. Mpaka sasa Serikali ya Marekani kupitia viongozi wao wameshaanza kuiongelea vibaya nchi yetu na ni swala la muda tu kuchukua hatua kwa siri ama kwa njia ya wazi”
“Nyakasura pia atashiriki . Ijapokuwa anahesabika kuwa mtaalamu wa juu katika ulimwengu wa mapigano kama ilivyo lakini asili yake inaweza kuleta sintofahamu nje ya nchi na vilevile hata kama akishiriki uzoefu hana na isitoshe kuna wataalamu wengi ambao bado hajakutana nao . Kwenda kwetu kushiriki ni kwa ajili ya kukuza hadhi ya jeshi vinginevyo kusingekuwa na haja ya kushiriki na kuwapa kazi wanasiasa kutuliza hali , lakini kama mabeberu wataamua kutushambulia iwe moja kwa moja ama kwa njia isio ya moja kwa moja tutakuwa kichekesho kwa dunia kwa nchi ndogo kama yetu kujaribu kutunishiana misuli na taifa kubwa. Ndio maana tunachotaka ni kujijengea hadhi kwanza katika ulimwengu usionekana , ili kam wakitaka kuchukua hatua wajifikirie mara mbilimbili.”Aliongea kwa kirefu.
“Kule Dodoma nilikuambia utupatie teknolojia ya Barham na Baffold ila haukuwa tayari , basi kubali katika hili, kama unajihisi wewe mweneywe kutoshiriki nadhani haitokuwa ngumu kutumia watu wako . Si ndio?”Aliongea na kumfanya Hamza macho yake kuchanua katika hali ya uovu.
“Simba unaenda mbali sasa , ile mara ya mwisho uliniomba teknolojia ya Barham na Baffold , kwahio yote ilikuwa ni kwa ajili ya kujiandaa na hili kusanyiko la wagawa maksi?”
“Haha.. nadhani unajua Tanzania bado ni nchi ndogo sana na mapungufu mengi kulinganisha na mataifa ya ulimwengu wa kwanza . Tunaweza kuimiliki Earth Axis lakini bado tupo dhaifu kuilinda na ndio maana tumekuomba vile. Ijapokuwa unaweza usijichukulie kama raia wa Tanzania , lakini wewe ni Mtanzania , au nakosea?”Aliongea na kumfanya Hamza kufikiria.
Muda ule alikumbuka Regina alikuwa pia na mpango wa kusafiri kwenda Ulaya mwezi ujao na kwasababu alihitaji kumsindikiza aliona sio mbaya kama atachukua muda wake kwenda kuhudhuria hilo kusanyiko.
Hamza aliona nchi ya Amerika haikuwa na utani kwenye kupigania maslahi yake na kama kweli wakichukua hatua watakaoathirika sio yeye bali wanawake waliokuwa karibu yake, ikiwemo biashara za Regina kwa ujumla.
“Basi kama ni hivyo utanitaarifu muda ukiwadia . Namaanisha nimekubali lakini sina uhakika nitakuwa salama..”Aliongea Hamza.
“Ili mradi ukijitahidi . Naamini hakutakuwa na tatizo kabisa . Hii ni msiheni ndogo sana ukilinganisha na misheni ulizofanya , ikiwemo ile ya Vita takatifu”Aliongea Afande Simba huku akiwa na tabasamu pana usoni na Hamza alipotaka kuongea Afande Simba aliingilia haraka.
“Kuhusu hili ombi letu usije ukasema lipo ndani ya mahitajio mawili mawili yaliobaki , hii ni ziada na usije kwenda kinyume na maneno yako”Aliongea na kumfanya Hamza kukuna kichwa na kujiambia hilo lizee kweli lina akili.
Muda huo Afande Himidu alirudi akiwa na wale wazee wafuasi wa Nyoka.
“Afande Simba , Bosi ! Kwanzia sasa hili swala limeisha . Mzee Sembe na wenzake hawana pingamizi tena”Aliongea Himidu.
“Oh! Mzee Sembe kweli umekubali hili lipite?”Aliuliza na Mzee Sembe na wenzake walimwangalai Hamza na macho ya heshima na wasiwasi kwa wakati mmoja.
“Bila shaka tumekubali yaishe lakini shukrani zetu zimwendee Mshauri mkuu kwa kuwa hiari kutuambia kuhusu Hamza … Kitendo cha kuwa maarufu kama alivyo Nyakasura nadhani ni swala la shukrani zetu kumuacha kwa ajili ya maslahi ya taifa . Lawama ni kwa Farook kwa kwenda kinyume na sheria na kusababisha kambi yetu kupata hasara kubwa”
Hamza mara baada ya kusikia maelezo hayo , palepale alimpiga Afande Himidu teke la makalio kwa kuwa mbeya.
“Himidu kwahio umewaambia kuhusu siri yangu sio?”
“Bosi sikuwa na namna ya kumaliza hili swala ndio maana . Lakini hata hivyo wameahidi hawatotoa taarifa ya chochote nilichowaambia . Lakini bosi wewe ni kama Kimulimuli gizani , huwezi kujificha kirahisi”Aliongea.
ITAENDELEA.
Thanks
 
Back
Top Bottom